ANNUUR 1173.pdf

20
ISSN 0856 - 3861 Na. 1173 JAMADIUL AKHER 1436, IJUMAA , APRILI 17-23, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/= Sauti ya Waislamu facebook: [email protected] AHLU SUNNA WAL JAMAA HAJJ AND UMRA TRUST Silaha Msikitini Kidatu, Morogoro: Balaa kubwa linakuja Iwapo busara zaidi haitatumika, SIO ile… Mihemko ya Wabunge wetu Dodoma Masheikh msanubiri, Anti Balaka, Seleka? ‘Jihad’ kuangamiza Waislam Somalia na siasa za Zanzibar Soma Uk. 10 MUFTI wa BAKWATA Sheikh Shaaban Simba (kulia) akiwa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa. Picha chini, Sheikh Mohamed Idd (kulia), kushoto Sheikh Mohamed Issa. MOJA ya picha zinazosambazwa mitandaoni zikionyesha wapiganaji 'Mujahidina' wakiwa na bendera ISIS. Mtume(saw) amesema, "Husamehewa mwenye kuhiji na anaowaombea". Hakuna katika ibada nyingine yoyote uhakika huu wa Muislamu kukubaliwa maombi yake na kupata fursa ya kuwaombea wengine, kisha kukubaliwa, ila katika Hijja! Muda unakwisha! Gharama zote kwa Hijja ni Dola 4,500. Umra ya Ramadhani ni Dola 2,300. Karibuni Ahlu Sunna Wal Jamaa kwa huduma nzuri na uongozi bora. Wasiliana nasi: Tanzania Bara: 0765462022;0782804480; 0717224437. (7) HIJJA NI FURSA YA KIPEKEE!

Transcript of ANNUUR 1173.pdf

Page 1: ANNUUR 1173.pdf

ISSN 0856 - 3861 Na. 1173 JAMADIUL AKHER 1436, IJUMAA , APRILI 17-23, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/=

Sauti ya Waislamufacebook: [email protected]

AHLU SUNNA WAL JAMAA HAJJ AND UMRA TRUST

Silaha Msikitini Kidatu, Morogoro:

Balaa kubwa linakujaIwapo busara zaidi haitatumika, SIO ile…Mihemko ya Wabunge wetu DodomaMasheikh msanubiri, Anti Balaka, Seleka?

‘Jihad’ kuangamiza Waislam Somalia na siasa za Zanzibar

Soma Uk. 10

MUFTI wa BAKWATA Sheikh Shaaban Simba (kulia) akiwa na Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa. Picha chini, Sheikh Mohamed Idd (kulia), kushoto Sheikh Mohamed Issa.

MOJA ya picha zinazosambazwa mitandaoni zikionyesha wapiganaji 'Mujahidina' wakiwa na bendera ISIS.

Mtume(saw) amesema, "Husamehewa mwenye kuhiji na anaowaombea". Hakuna katika ibada nyingine yoyote uhakika huu wa Muislamu kukubaliwa maombi yake na kupata fursa ya kuwaombea wengine, kisha kukubaliwa, ila katika Hijja! Muda unakwisha! Gharama zote kwa Hijja ni Dola 4,500. Umra ya Ramadhani ni Dola 2,300. Karibuni Ahlu Sunna Wal Jamaa kwa huduma nzuri na uongozi bora. Wasiliana nasi: Tanzania Bara: 0765462022;0782804480; 0717224437.

(7) HIJJA NI FURSA YA KIPEKEE!

Page 2: ANNUUR 1173.pdf

2 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786

Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: [email protected]

Ofisi zetu zipo: Manzese Tip TopUsangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam

Tahariri

Inaendelea Uk.3

Balaa kubwa linakujaTAARIFA za Kipolisi zinadai kuwa kuna silaha zimekamatwa ndani ya Msikiti, juzi. Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoani Morogoro , Leonard Paul , vi tu vilivyokamatwa katika Msikiti uliotajwa kuwa ni wa Suni, Kidatu wilayani Kilombero ni pamoja na milipuko 30, bisibisi, ‘majambia?’, misumeno, nyaya za umeme, bendera yenye Kalima ya Shahada na vitu vya kufunika nyuso (mask).

Taarifa zaidi zinasema k u w a m t u m m o j a aliyetajwa kwa jina la H a m a d M a k w e n d o ameuliwa na wananchi w a k i t o n g o j i c h a Nyandeo, baada ya kumjeruhi polisi kwa ‘jambia’. Yote haya ni kwa mujibu wa taarifa za polisi.

Kingine kilichodaiwa k u k u t w a k a t i k a Msikiti huo au tuseme walichokutwa nacho watu hao ni bendera nyeusi ikidaiwa kuwa kama ya Al-Shabaab.

U k i c h a n g a n y a kuwa waliokamatwa wot e n i Wais lamu, wal ipokamat iwa n i Msikitini ikijumuishwa na kukutwa na bendera hiyo ya ki-Al-Shabaab/IS, wala haitakuwa sahihi kuvilaumu vyombo vya habari vilivyosherehesha zaidi na kusema moja kwa moja kuwa ‘magaidi wakamatwa’ Msikitini. Hiyo ndiyo biashara ya sasa.

J a m b o h i l i s i s i tuta l i tazama kat ika sura mbili. Moja kama Waislamu na pili kama Wa t a n z a n i a . K i s h a tutahitimisha kwa kutoa ushauri wetu, nini cha kufanya.

Hivi sasa ‘Jihad Feki’, ikiwa kwa sura ya IS, Al-Shabaab, na kwa jina lolote utakaloita, iwe kule Libya, Syria, Iraq,

Somalia, imekuwa ni saratani yenye kutafuna Uislamu na Waislamu. Mzaha huo wa jihad na batili (pseudo-jihad) i n a u f a n ya U i s l a m u uonekane kama alama ya ukatili na kielelezo cha itikadi ya kishenzi na watu washenzi wasio na ustaarabu hata chembe. Matukio kama hili la juzi Garissa, vyovyote utakavyolitizama, iwe la kweli au ni usanii uliofanyika (staged/false flag terror attack), lakini athari iliyoachwa katika vichwa vya watu ni kuwa waliofanya hivyo ni magaidi wa Al-Shabaab, ni Mujahidina, ni Waislamu wa Somalia wanaotaka kusimamisha Dola ya Kiislamu. Sasa yale madai kwamba w a l i f a n y a h i v y o kulipiza kisasi kwa Kenya kupeleka jeshi Somalia, haifuti picha h i y o i n a y o j e n g wa . Hali ni hiyo hiyo kwa yanayodaiwa kufanywa na IS, Boko Haram na Al-Qaidah.

S a r a t a n i h i i inatutafuna kutokana na vita inayochukua ushuru wa roho za Waislamu kule Afghanistan, Libya, Syria , I raq, Yemen, Somalia n.k. Ushuru huu na umwagaji damu huu unatisha zaidi kwa sababu ni Waislamu kwa Waislamu wanashikiana bunduki na kulipuana h u k u k u n d i m o j a l ikiamini kuwa lipo katika Jihad. Lakini wote hawa ama wanauziwa au kupewa silaha na kafiri/beberu. Hakuna mmoja kati yao mwenye kiwanda cha kumfanya ajitegemee kwa silaha. Kafiri anatajirika na kukuza uchumi wake kwa kumwaga damu zenu wenyewe. Lakini k w a n a m n a h i y o , mnasambaratika kama nchi. Beberu na kafiri anawakal ia kirahis i anakomba rasilimali

zenu.K w a u p a n d e

m w i n g i n e , k a f i r i /mabeberu wanatumia Jihad hii feki, kusambaza k i t i s h o c h a u g a i d i ili kupata sababu ya kuwapiga Waislamu na kuzivuruga nchi nyingine wanazozilenga. Uchochoro wa kupitia ni kuwa na mawakala wa kutangaza Jihad hii feki iwe ya Syria, Libya, Iraq au Somalia. Hili wimbi tunaloshuhudia hivi sasa asili yake ni mkakati u l e u l e u l i o t u m i k a kupata Mujahidina wa kupigana kwa niaba ya mabeberu Afghanistan. M a w a k a l a h a w a wamekuwa wakipita kila mahali kuhimiza Jihad Somalia na Syria. Na kama Waislamu, lazima tukubali kuwa miongoni mwetu, wapo mawakala wanaofanya kazi hiyo ndio maana wanapatikana vijana wasio na hatia (innocent) k a m a M b e r e s e r o aliyekamatwa Kenya au akina Ummul Khair, w a n a j i k u t a k a t i k a matatizo, kwa ujinga tu na utoto wao.

Tu l i wa h i k u e l e z a katika gazeti hili juu y a K h a t i b m m o j a katika Msikiti mmoja wa Mikocheni , Dar es Salaam, aliyetumia K h u t b a ya I j u m a a kuelezea namna ya k u c h i n j a m a k a f i r i . Tuliwahi kueleza pia juu hotuba zinazotolewa katika baadhi ya Misikiti jijini Mwanza zikihimza Wais lamu kuwa na s i l a h a m a j u m b a n i m w a o . U k i w a n a mawakala kama hawa na wakaachwa wakakoroga bongo za Waislamu, leo yanapotajwa haya ya Kilombero, tayari unakuta kuna msingi wa kujenga hoja. Hata kama itakuja kudaiwa kuwa watu wale wa Kidatu walibambikiziwa silaha zile na bendera ile nyeusi, lakini kwa kauli hizi za mawakala wa mabeberu zilizoachwa zikaota mizizi katika baadhi ya Mis iki t i , utetezi unakuwa wenye kupwaya.

A m b a c h o s i s i tulitarajia ni kuwa baada ya kuibuka watu kama hawa, basi Masheikh wangechukua nafasi zao,

katika hafla za Maulid, Khutba za Ijumaa na Darsa za Misikitini, hafla za ndoa na hata katika maziko; jambo h i l i l i z u n g u m z w e , lifahamike. Lakini kwa bahati mbaya Masheikh wetu wamepiga kimyaa.

M t u u n a j i u l i z a , nini vipaumbele vya Masheikh wetu kama h i l i l a k u p o t o s h a Umma wa Waislamu na lenye kuleta madhara makubwa katika Dini na jamii, hawalioni! Ndio hapo tunauliza, je, wanasubiri yaibuke yale ya Anti-Balaka na Seleka kule Afrika ya Kati ndio waseme?

Tu n a u l i z a s w a l i h i l i , k w a s a b a b u ukifuatilia yanayotokea Kenya, huko ndiko tunakosukumiziwa na mabeberu. Kila likitokea shambulio la kigaidi, utasikia wakisema kuwa Wakristo walitengwa mbali na Waislamu, kisha Waislamu wakaachiwa Wakristo wakachinjwa au kupigwa r i sas i . Tunadhani nini sababu ya propaganda hiyo?

Hebu turejee zile hasira za Wabunge wetu katika ile semina ya Suala la Mahakama ya Kadhi kule Dodoma, lakini turejee tena ule upumbafu uliokuwa ukiendelea w a k u p a n d i k i z a chuki kuwa Waislamu wanachoma makanisa na kuuwa viongozi wa Kikristo. Sasa chukua upumbafu huo na chuki hizi zilizosheheni katika vifua vya miongoni mwetu, halafu jaaliya ya l i y o t o k e a K e n ya ingekuwa ni Tanzania hali ingekuwaje!

Kwa hiyo, ukilitizama K i i s l a m u a u k a m a Muislamu, utaona kuwa balaa ambalo huenda likatukumba, kwa kiasi kikubwa litaharakishwa na upumbafu unaotisha tul io nao miongoni mwetu. Leo pamoja na yanayotajwa kufanywa n a B o k o H a r a m , likiwemo lile la hivi karibuni la kuuwa zaidi ya Waislamu 2000 na kuchoma moto nyumba zao kule Baga, bado wapo miongoni mwetu wanaodai kuwa Boko Haram, ni mujahidina!

Hebu someni ujumbe huu ukiwa miongoni wa

jumbe zinazomiminika katika Chumba Chetu cha Habari:

“Ama kama nyinyi An nuur ni wa kweli na mko kwa ajili ya A l l a h , h a m k o k wa ajili ya twaghuti, wiki hii wakufurusheni na Masheikh waliokwenda mahakama ya twaghuti kuwashitaki murtadiina Bakwata, siyo muishie k u w a k u f u r i s h a mujahidina wa haki al-shabaab, Boko Haram, Al-Qaida, dawla islamiya (IS)

Huyo ni msomaji wetu 0716 67 5313. Hillary Clinton anasema wao ndio walioanzisha Al-Qaidah ili wawatumie kupigana na Mrusi , msomaji huyu anasema Al Qidah ni Mujahidina wa Haki. Boko Haram i n a u w a Wa i s l a m u Nigeria ya Kaskazini, msomaji huyu anasema B o k o H a r a m , n i mujahidina wa Haki. Unamsaidiaje mtu kama huyu!

Msomaji huyu katika ujumbe wake mwingine anasema kuwa na Redio/TV Imaan, gazeti Imaan, Mizani, Kisiwa, An nuur, ni ukafiri mtupu kwa sababu yanasajiliwa na twaghuti!

Kwa wiki hii, huyu ndiye msomaji wetu ambaye katuma ujumbe wa maneno mara nyingi kuliko msomaji yoyote kupitia namba yake hii ya Tigo. Kwa Sheria ya Tume ya Mawasiliano, huwezi kumiliki laini ya simu na kuitumia mpaka usajiliwe. Sasa unashindwa kujua, nini kinachowafanya TV Imaan wawe matwaghuti kwa kusajiliwa na Tume ya Mawasiliano lakini isiwe utwaghuti kuwa na laini ya Tigo iliyosajiliwa na Tume hiyo hiyo ya Mawasiliano au Idara nyingine yoyote ya serikali!

Sasa unatizama hali kama hii inayodhihirisha jinsi mtu alivyo mtupu katika Uislamu (Qur’an na Sunnah) na maarifa ya ujumla ya kujitambua anaishi wapi na aishi vipi kwa mwongozo huo huo wa Uislamu, lakini ashaj ipa Ukamanda wa Kuhimiza Jihad na

Page 3: ANNUUR 1173.pdf

3 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Habari

TAASISI za Kiislamu nchini zimepinga Bakwata kuwa mwakilishi wa Shule zinazomilikiwa na Taasisi za Kiislamu katika mchakato wa uandaaji wa muswada wa elimu wa mwaka 2015.

Msimamo huo umekuja kufuatia Shirikisho la Wamiliki na Mameneja wa Shule na Vyuo visivyo vya Serikali Tanzania (TAMONGSCO) kuitaka Bakwata, kuwa mwakilishi wa Shule za Kiislamu, katika kuuendea mchakato huo.

Wadau hao wa elimu kutoka pande zote za dini na Serikali, walikutana m w i s h o n i m wa w i k i iliyopita katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Shaban Robart, Jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kujadili sera mpya ya elimu ya mwaka 2014 sambamba na Muswada wa Sheria ya Elimu ya mwaka 2015.

Akipinga pendekezo la TAMONGSCO kwa Serikali (Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi) kuwa Bakwata ndiyo iwe msemaji na mwakilishi wa shule za Kiislamu, S h e i k h M o h a m m e d Issa, alisema Jumuiya za Kiislamu hazikubaliani na pendekezo hilo.

Shk. Issa, alisema zipo sababu nyingi za kupinga pendekezo hilo, moja wapo ni kwamba katika sekta ya elimu Bakwata, inamiliki S h u l e c h a c h e n c h i n i ukilinganisha na Taasisi nyingine za Kiislamu.

Hata hivyo, alisema kumekuwa na kasumba si kwa asasi zisizo za Serikali tu bali hata kwa Serikali yenyewe mara kwa mara kuifanya Bakwata kuwa ndio chombo cha Waislamu kinachotakiwa kuwawakilisha Waislamu nchini, ilihali kuna Taasisi za Kiislamu nyingi zenye hadhi sawa na Bakwata.

“Bakwata imesajiliwa chini ya RITA, kama ambavyo Taasisi nyingine za Kiislamu zilivyosajiliwa (RITA), kwa hiyo kisheria Taasisi zote hizo zina hadhi sawa. Na miongoni mwa hizo Taasisi kuna madhehebu tofauti tofauti hivyo sio sahihi kuifanya Taasisi hiyo pekee kuwa ndiyo ya Waislamu wote nchini.” Alisema Shkh. Issa.

S h k h . I s s a a l i s e m a wakati ikiwa hivyo kwa Waislamu, kulazimishwa Bakwata kuwa mwakilishi na msemaji wa Waislamu wote, hali ni tofauti kwa

BAKWATA yapingwaNa Bakari Mwakangwale

Wakristo ambao Serikali hai tambui Taas is i au dhehebu moja la Kikristo.

Shkh. Issa ambaye ni

kiongozi wa Taasisi ya Answar Sunnah Tanzania (BASUTA), alisema kwa Wakristo kuna Taasisi za

madhehebu mbalimbali kama vile Wakatoliki, Walutheri, Angalikana n a m e n g i n e m e n g i ,

lakini Serikali haiegemei katikaTaasisi ya dhehebu moja.

Hata h ivyo Kat ibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome, alitoa muongozo juu ya msimamo huo wa Taasisi za Ki is lamu kupinga kuwakilishwa na Bakwata, kwa kuwataka kulifikisha suala hilo Wizarani kwa maandishi.

Awali katika kikao hicho, Taasisi za Kiislamu ziliitaka Serikali kusimamia haki na usawa katika suala zima la usajili na ukaguzi wa Shule za Serikali na Shule binafsi, ili kuweka usawa na kupunguza ugumu katika uendeshaji wa shule binafsi.

M k u t a n o h u o u l i s h r i k i s h a w a d a u mbalimbali binafsi wa elimu nchini na Serikali, ambapo kwa upande wa Serikali, miongoni mwa waliohudhuria ni pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome na Kamishna wa Elimu, Profesa Eustella Bhalalusesa.

SHEIKH Mohamed Issa (kulia), Sheikh Rajab Katimba (katikati) na Sheikh Ally Bassaleh (kushoto).

Balaa kubwa linakujaInatoka Uk. 2kuwatia wengine katika ukafiri!

Ukiacha hilo, kama t u l i v y o t a n g u l i a kusema, tatizo jingine ni la viongozi wetu wa kidini wenye dhamana. Wamekuwa kuwepo kwao ni kama hawapo.

P a m o j a n a k a z i k u b wa ya k u d u m u wanayotakiwa kufanya Masheikh wetu na wajuzi wa Uislamu kuelimisha jamii ya Kiislamu, lakini kama dharura, kuna haja ya jambo hili la ‘Jihad bandia’ kufafanuliwa vizuri na j i n s i l i n a v y o t u m i k a kuwavuruga Waislamu na kuuchafua Uislamu.

Kwa upande mwingine, k a m a n c h i n a k a m a Watanzania, tutakuwa tumefanya kosa kubwa sana kama tutawatizama vijana hawa wanaodaiwa kukamatwa na silaha kuwa ni ‘magaidi’ kwa sura inayotangazwa ulimwenguni hivi sasa. Tukiwatizama hivyo, n a t u k i j i k u b a l i s h a k u w a n c h i n i t u n a watu wa namna hiyo, tu jue kinachofuat ia ni kuingizwa katika ‘Mchezo wa Kifimbo Cheza’ unaoendelea Kenya na Nigeria. Na tumetangulia kusema, tut izame zi le chuki

walizo nazo miongoni mwetu linapokuja suala la Uislamu na Ukristo katika nchi hii, halafu tujiulize, yakipangwa na yakafanyika ya Garissa, tutakuwa na kifua na mioyo ya Wakristo wa Kenya ambao kwa hakika ndio wanaoifanya Kenya mpaka sasa iwe salama kwa kiasi kilichopo hivi sasa?

T u w a t i z a m e wa t u h u m i wa h a wa huku tukirejea katika ukweli usio na shaka kuwa mitandao yote ya mujahidina, kuanzia Afghanistan, ilipewa mafunzo na fedha na mabeberu. Rejea kauli ya Hi l lary Cl inton: We Created Al-Qaida. Tutizame pia Operation Cyclone. Lakini tudurusu p ia ya le a l iyosema m wa n a h i s t o r i a wa U i n g e r e z a M a r k Curtis alivyoonyesha k i n a g a u b a g a katika kitabu chake maridhawa, "Mambo ya siri: Ushirikiano wa Uingereza na Uislamu-itikadi," kwamba serikali za kibeberu zinaendelea kuunga mkono kwa siri

makundi yenye uhusiano n a A l Q a e d a k w a sababu zile zile kama mwanzo - kukabiliana na ushawishi wa Russia, na sasa ule wa China ili kueneza nguvu za Marekani juu ya uchumi wa jumla wa kibepari duniani.

Tusisahau pia kuwa haya ya Waislamu kuwa na hizi zinazodaiwa kuwa s iasa kal i na mawazo haya ya kuwa na silaha misikitini, k a t i k a m a d r a s a , skuli na majumbani, z a k u w a a n g a m i z a wa n a o d a i wa k u wa makafiri, yanatokana na hawa hawa wanaojifanya viranja, wafadhili na wataalamu wetu katika kupambana na magaidi.

Kama alivyoandika Dr . N af ee z Ah me d (PhD) katika makala na uchambuzi wake “Islamic State is the cancer of modern capitalism: Islamic State; US foreign policy; funding”, nchini Afghanistan, USAID iliwekeza mamilioni ya d o l a k u wa p a t i a watoto wa shule "vitabu vi l ivyojaa picha za

ukatili na mafundisho ya kipiganaji ya Kiislamu". Theolojia inayohalalisha jihadi ya kuua ilisanifiwa kwa michoro ya bunduki, risasi, askari na mabomu ya kutegwa. "Vitabu hivyo vya kiada vilifikia hata kusifu thawabu ambazo watapata "waking 'oa macho ya adui Mrusi na kukata miguu yake."

Kirusi hicho ndicho kinatafuna vijana kama hao wa Kidatu mpaka leo. Ufumbuzi hapa sio kuwaadhibu waathirika wa kirusi hiki. Hawa ni wagonjwa wanahitaji tiba. Usalama wetu ni kutizama kinakotokea kirusi hiki na kukizuiya kuingia akilini na mioyoni mwa vijana wetu na watu wetu.

Tukizingatia ukweli huo, tutatambua kwamba sisi na vijana wetu hao, adui yetu ni mmoja. Imekuwa bahati mbaya tu wao wamekuwa wapumbafu wanatumiwa h u k u w a k i d h a n i wanapigania Dini.

Lakini na sisi kama t u t a w a t i z a m a k u w a h a w a n d i o m a a d u i zetu. Ni Al-Qaidah, Al-Shabaab au IS wa kwetu, tutakuwa wapumbafu pia, kama walivyogeuzwa k u w a w a p u m b a f u wa n a o p a m b a n a n a Boko Haram Nigeria na wanaopambana na Al-Shabaab Somalia.

Page 4: ANNUUR 1173.pdf

4 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

MT U M E ( S . A . W. ) a n a s e m a k u w a kila binaadamu ni

mwenye kukosea na bora ya wanaokosea ni wale wenye kutubia. Kwa kua kiongozi wetu S.A.W. haongei kwa mapenzi au uamuzi wake, bali anachosema ni kwa uongozi wake ALLAH SWT, basi ni wazi kwamba kila binadamu kati yetu atafanya kosa katika maisha yake. Makosa kwa ufupi yanakuja na kifurushi cha kuwa binadamu.

Kinachomfanya Muislamu asikate tamaa baada ya kufanya makosa, ni ahadi nyingi alizotoa Allah SWT kuhusiana na huruma yake kwetu sisi wakosaji. Anasema Allah SWT kwenye Surat al-Nisaa, “Hakika Allah hasamehe kushirikishwa lakini anasemehe lolote chini ya hapo kwa anaeamua kumsamehe”.

Pamoja na kuwa ahadi za Allah SWT za malipo mazito kwa wasiotubu zina vitisho vikubwa vya adhabu kali, lakini bado Waislamu tunaenedelea kufanya maasi na kuyarudiarudia kila mara na wengi wetu hatimaye tunaiacha dunia tukiwa kwenye hali hiyo. Hasara ilioje mwisho huo!!

K w e l i k u n a m a k o s a tunayofanya kwa bahati mbaya na kuna mengine tunafanya kwa kutokujua au kwa kutokua na uelewa wa amri za Allah SWT. Lakini maasi ninayoongelea mimi ni yale ambayo tunafanya hali ya kuwa tunajua vizuri kuwa tunavunja amri za ALLAH SWT.

Katika kujiuliza sababu za kumuasi Allah SWT wakati tukijua, hivi karibuni nimeona video moja kwenye mtandao ik imuongelea Muislamu mmoja ambaye nadhani kwa mavazi aliokua amevaa ima ni mtu wa India, Pakistan, Bangladesh au Afghanistan. Ndugu yetu huyu kapewa mtihani mkubwa na Allah SWT. Ni kilema ambaye hana mikono kuanzia kwenye mabega. Kila jambo analofanya la kimaisha anatumia miguu yake. Kupiga mswaki, kuoga, kusaidia wanae home works, kupika na mengine mengi. Anatumia miguu yake na jambo moja tu anaonekana akifanya kwa kutotumia miguu ni pindi anapotaka kufungua Qura’an kufanya tilaawah ndio anaonekana akitumia uso wake kufungua kurasa za kitabu kitukufu.

La kusisimua mwili na akili na hata moyo kama bado una chembechembe za imani, ni kwamba hamna swala inayompita na ibada zake nyingine anazingatia. Anatawadhwa kwa kutumia miguu na anarukuu na kusujudu bila kua na mikono. Naomba tuzingatie mtihani wa huyu mtu vizuri kabla hatujaendelea kusoma.

K a m a k i l e m a h u y u hapotezi ibada zake, kwa

Sababu kubwa ya kufanya maasi

nini sisi wazima tunadharau. Huyu Muislamu ni dalili tosha kuwa, ulemavu si sababu ya kuvunja amri za Allah SWT. Tunaweza kudai kuwa maradhi kuna wakati yanatuzuwia kuabudu, lakini pia kuna wagonjwa wengi wa maradhi tofauti ambao wanatimiza amri za Allah SWT. Kuna wagonja ambao wamo jela ndani ya ngozi zao; watu ambao miili yao imepooza kuanzia shingoni kwenda chini lakini bado wanaabudu kadri ya uwezo wao. Kwa hiyo maradhi, si sababu ya kumuasi mmiliki wa nguvu zote, Allah SWT.

Tunaweza kudai kuwa hali ngumu ya kiuchumi ( u m a s i k i n i ) , i n a w e z a kusabibisha mtu kuasi au kutozingatia ibada zake. L a k i n i w o t e t u n a j u a watu ambao umasikini hauwazuii kuabudu. Au tunaweza kusema, hal i nzuri ya kibiashara/uchumi ndio sababu ya baadhi ya Waislamu kutokuabudu ipaswavyo. Lakini vilevile wote tunajua kuwa kuna Waislamu matajiri wakubwa na ni watu wa mashughuli mengi lakini hawaachi ibada zao. Sasa kama ulema, maradhi, umasikini na hata utajiri si sababu ya kukiuka amri za Allah SWT, sisi tunaomuasi Mungu usiku mchana, sababu inakuwa ni nini hasa?

Allah SWT anaposema “hatujaumba majini na b i n a a d a m u i s i p o k u a waabudu”, tujue kuwa Allah SWT anayakusudia hayo. Hamna mchezo na wala hakutokuwa na mabadiliko katika ahadi alizotoa Allah SWT kwenye Kitabu chake kitukufu.

Wakati Allah SWT anasema kwamba hajaumba yote haya akifanya mchezo, maana yake

ni kwamba sisi tunafanya maasi mengi kwa upuuzi na mchezo. Tunaabudu kwa kusuasua na tunavunja sheria zake kwa sababu hatuzipi HARAM na HALAL uzito wake. Tunafanya mambo yaliyokatazwa kwa sababu hatuzingatii vizuri balaa lake na ghadhabu tunayomtia Allah SWT.

Kwa ufupi sababu kubwa ya Maasi ni kutokuzipa amri za Allah uzito wake. Wengi hatuko makini na Amri zake Allah Subhanahu Wataala. Lakini Allah kishatwambia kuwa Yeye yuko makini na kwamba “Waman yaamal mithqaal dharratin khairin ya r a h wa m a n ya a m a l mithqaal dharratin sharran yarah.”

Imani ya Muislamu ni kichwa cha Uislamu wake. Muislamu bila Imani ni kama mwili bila kichwa. S.A.W anasema kuwa kwenye mwili kuna nyama ambayo ikikaa sawa basi mwili mzima utakaa sawa na hio nyama ni moyo. Imani ya Muislamu inajaribiwa kwa njia tofauti za kidini na za kidunia. Muislamu anajaribiwa na Ibada kama kusali kwa wakati na kufunga Ramadhan na ibada nyingine nyingi . Lakini kwa kuwa Waislamu wengi tumekua tunaacha Ibada au hatuzifanyi kwa wakati wake na hata bila kujihisi kuwa tunakosea, katika makala hii ntaongelea vitu vya kidunia ambavyo vinajaribu na kutingisha Imani zetu kama Waislamu. MuislamU, mbali na mambo ya ibada, Imani yake inapata m a j a r i b u k wa m a m b o mawili makubwa: wakati wa matatizo na wakati milango ya neema imefunguliwa. Sababu wengi wetu sisi mtihani wetu ni ugumu wa maisha, ntaliongelea jambo

la kubwana na vipi linatutia kwenye mtihani.

Sio kitu cha kushangaza kumkuta Muislamu kabanwa kiasi kwamba anaongea peke yake. Binadamu akiwa kabanwa kiuchumi mawazo yake yanafikiria nani wa kumkopa au kumsaidia. Mjomba, kaka, rafiki na mara nyingi hata kufikiria vitu vya haramu kama mikopo ya riba au hata utapeli Allah apishe mbali.

Ikiwa ni maradhi mtu anawaza daktari mzuri wa kumsaidia au kusaidia mtu wake, au hospitali nzuri au hata wapiga ramli au wenye kudai kuweza kuwasiliana na Mwenyezi Mungu wal-iyaadhu bi l laah. Huyu Muislamu kama anakumbuka maneno machache tu ya Allah na kwa kuyazingatia kwa dhati kama vile “Anaemcha Allah atamjalia mlango wa kutokea” au “inna maa alusr yusran”, basi ndani ya muda mfupi anajikuta roho yake imetulia hata kabla ya tatizo kutatuka. Tatizo kubwa ni kwamba Imani haziko thaabit na tukikumbwa na majanga, ALLAH SWT anakua wa mwisho kabisa kumfikiria.

Muislamu wakati kabanwa anatak iwa kukumbuka kuwa kat ika nguzo za Imani, ni kukumbuka na kuzingatia kiundani kuwa kuna nguzo inayoongelea kuwa tunatakiwa kukubali kuwa mazuri na mabaya yote yonatoka kwa Allah au kwa ruhusa yake. Ni kweli tunatakiwa kutafuta kwa bidii ufumbuzi wa matatizo y a n a o t u k a b i l i , l a k i n i tunatakiwa kukumbuka daima kuwa binadamu wanaotusaidia kiuchumi kama ndugu na marafiki

a u k i m a t i b a b u k a m a madaktari, si wao ambao ndio wanamaliza matatizo yetu. Inabidi tukumbuke k u wa h a wa b i n a d a m u wanaosimama na sisi wakati wa shida, ni ZANA tu za ALLAH anazotumia kututoa kwenye matatizo yetu. Wao wenyewe wanamtegemea Allah kwa kila kitu kwani mbinu za binadamu yoyote zinategemea uamuzi wa Allah SWT. “Wama Tashaauun illa an yashaa Allah Rabbu Al-alameen”.

M f a n o w a k u f u a t a n i Nabi Ayyub ambae alinyanganywa mali yake yote na akapewa maradhi ya ajabu lakini katu hakumpa nafasi Iblis kumnyang’anya. Cha muhimu alichokua kabaki nacho, IMANI yake bi LLAAH. Hatuwezi kama waislamu kuyumbishwa na matatizo ya kidunia na kuanza kutapatapa kama myama aliekatwa kichwa halafu wakati huo huo tukadai kuwa tuna Imani na uwezo wa Allah SWT.

T u k i w a n a I m a n i dhaifu na Qudra za Allah t u t a k u w a k a m a w a l e Q u r a ’a n i n a wa o n g e l e a ndani ya ayah hii ya Surat al-Hujuraat ayah 14: “Mabedui wamesema tumeamini . Sema: Hamjaamini, lakini s e m e n i : Tu m e s i l i m u . Kwani Imani hai jaingia katika nyoyo zenu”. Imani ilokamilika haitetereki kwa lolote. Muislamu mwenye Imani thabiti hamna janga la kuitingisha Imani yake na hofu yake mpaka anaingizwa kaburini inakuwa ni ya kumuogopa na kumcha Allah na kuamini kikamilifu kuwa hamna linaloweza kumtokea zuri au baya bila Allah kuliruhusu. Na Muislamu likimtokea zuri anasema Al-hamdulillah na likimtokea baya anasema “Inna Lillah wa Inna Ilaihi rajioun”.

K u r i d h i k a n i k a t i k a misingi ya Imani. Kuna ayah ambayo inaonyesha kuwa shukurani ya dhati ni nzito kuliko aina nyingi za ibada. Anasema Allah: “Na mwenye kutaka malipo ya duniani tutampa; na mwenye kutaka malipo ya Akhera tutampa. N a t u t a wa l i p a w e n y e kushukuru”. Kana kwamba wanaoshukuru kwa dhati wana daraja tofauti kabisa na wengine.

Uchumi mbaya, maradhi, matatizo mengine, tafuta sababu za kuyatoka, lakini wakati huo wote unaosubiri faraja na mfunguko, kuwa na subira na uamini kuwa hamna binadamu ambaye Allah SWT hafatilii mambo yake. Allah SWT anasema “na hizo siku tunazigawanya baina ya watu”. Kama leo sio siku yako, kuwa na Imani ya dhati kuwa yako inakuja”.

(Makala na ZHK).

WAPIGANAJI WA IS

Page 5: ANNUUR 1173.pdf

5 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Habari za Kimataifa

M U F T I M k u u w a Syria, Sheikh Ahmad B a d r u d d i n H a s s u n , amesema kuwa mji wa Alepo ulioko Kaskazini mwa nchi hiyo unalipa gharama za kulinda heshima na izza yake na kwa sababu hiyo magaidi

Mufti asema Saudia, Qatar zinaua wananchi Wasyria

HUKU akisisitiza juu ya kuendelea kuzingirwa Ukanda wa Gaza huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu na utawala wa kizayuni wa Israel, Ban Ki-moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa njia pekee ya kumaliza mgogoro wa Waarabu na Israel ni kubuniwa kwa nchi huru na ya kidemokrasia ya Palestina.

Akizungumza hivi karibuni na Sheikh Abdallah bin Nassir A a l T h a n i , Wa z i r i Mkuu wa Qatar muda mfupi kabla ya kikao cha 13 cha Umoja wa Mataifa cha kuzuia uhalifu na kupatikana uadilifu wa kisheria huko mjini Doha, Ban K i - m o o n , a l i s e m a kuwa ana wasiwasi kutokana na kukwama k w a m w e n e n d o w a m a z u n g u m z o ya mapatano kati ya Wapalestina na utawala wa Israel.

Umoja wa Mataifa umekuwa na nafasi m u h i m u k a t i k a kukaliwa kwa mabavu ardhi za Wapalestina na dhulma yote ambayo i m e f a n y i w a t a i f a dhulumiwa la Palestina tangu mwanzoni mwa karne ya 20 hadi leo.

Kuwekwa Palestina chini ya himaya ya Uingereza kwa kipindi cha miaka 30 katika miongo ya mwanzoni mwa karne ya 20 na baadae kupi t i shwa azimio nambari 181 katika Baraza Kuu la

Udhaifu UN, kiburi cha Israel kikwazo cha Palestina huru

Umoja wa Mataifa , a z i m i o a m b a l o kivi tendo l i l i igawa Palestina katika sehemu mbili za Wapalestina na Wayahudi mwezi N o ve m b a 1 9 4 7 , n i m a t u k i o m a w i l i muhimu katika historia ya Palestina ambayo umoja huo ulikuwa na nafasi muhimu katika kuyabuni na kuyasimamia.

Hata hivyo inaelezwa k u wa m a t u k i o h a y o yalichangia kwa kiasi k i k u b w a k u k a l i w a kwa mabavu ardhi za Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel na kwa msingi huo, bila shaka Umoja wa Mataifa unabebeshwa lawama kwa kuchangia sehemu kubwa katika kuanza kwa mzozo wa Wapalestina na Wazayuni, mzozo ambao bado unaendelea hadi leo katika karne ya 21, ambapo hivi sasa Katibu Mkuu wake anataka uhitimishwe.

K wa m b a b a a d a ya kupasishwa azimio hilo, u t a wa l a h a r a m u wa Israel ulitangaza rasmi kubuniwa kwake katika ardhi za Wapalestina, l a k i n i Wa p a l e s t i n a w e n y e w e a m b a o n i wamiliki halisi wa ardhi hizo hawajaruhusiwa kubuni nchi huru hadi leo ambapo ni karibu miongo saba imepita tangu ardhi hizo zikaliwe kwa mabavu na Wazayuni.

Jambo la kushangaza hapa ni kuwa mazungumzo ya mapatano ya Waarabu na Israel yal i fanyika mwezi Oktoba 1991 kwa usimamizi wa Umoja wa Mataifa ambapo kwa msingi wa maazimio

nambari 242 na 338 ya Baraza la Usalama la umoja huo, jeshi la Israel lilitakiwa kuondoka kwenye ardhi za Wapalestina na kubuniwa nchi ya Palestina.

K w a m u j i b u w a m a a z i m i o h a y o yaliyopasishwa na Baraza la Usalama katika miaka ya 1967 na 1973 jeshi hilo lilitakiwa kuondoka katika ardhi za Palestina zilizotekwa na kukaliwa kwa mabavu na Israel katika Vita vya Mwezi Juni.

Lakini kwa masikitiko makubwa maazimio hayo kama yalivyo maazimio mengine ya Umoja wa Mataifa kuhusiana na Palestina, yalitupwa kwenye kapu la sahau na hivyo kuwapa watawala wa Israel uhuru kamili wa kutekeleza mauaji ya kutisha dhidi ya Wapalestina wasio na hatia pamoja na kupora ardhi zao bila kujali.

Mauaji pamoja na ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayunji katika ardhi zilizoporwa za Wapalestina umezuia kikamilifu kubuniwa k wa n c h i h u r u ya Wapalestina.

Inasikitisha kuona kwamba upuuzwaji wa maazimio ya Baraza la Usalama na utawala h a r a m u wa I s r a e l unafanyika kutokana na uzembe pamoja na ushirikiano wa moja kwa moja wa Umoja wa Mata i fa ambao unadhibitiwa na nchi za Magharibi zikiongozwa n a M a r e k a n i , n c h i ambazo ni waungaji mkono wakubwa wa utawala huo ghasibu.

wamekuwa wakiulenga mji huo kwa makombora yanayonunuliwa na nchi za Saudi Arabia na Qatar na kuingizwa nchini Syria kupitia Uturuki.

Sheikh Hassun alisisitiza k u w a u l i m w e n g u unapaswa kuelewa kuwa

damu inayomwagwa katika mji wa Aleppo gharama yake italipwa na nchi za Saudi Arabia, Qatar na Uturuki kwa sababu Wasyria hawatasahau jinai hizo.

Shambulizi lililofanywa na makundi ya ISIS tarehe

23 Machi dhidi ya mji huo wa Aleppo lilisababisha vi fo vya watu 23 na kujeruhi wengine 30.

W a t u w a S y r i a wa n a a m i n i k wa m b a wa p i g a n a j i wa I S I S wanaofanya mauaji ya k u t i s h a k wa k u t a k a

vichwa vya watu au kuwachoma moto wakiwa hai, wanasaidiwa kifedha na silaha na nchi za Saudi Arabia, Qatar, Uturuki, utawala wa Kizayuni wa Israel na nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani.

ASKARI wa Saudia Arabia wameuawa na wengine kadhaa kukamatwa mateka kat ika shambuliz i l a kul ip iza k isas i l i l i l o f a n y w a n a wapiganaji wa kabila la Takhya nchini Yemen.

Ripoti zinasema kuwa wanachama wa kabila la Takhya Jumapil i i l iyopita wal i fanya shambulizi la kuvizia dhidi ya kituo cha jeshi la al Minare, karibu na mpaka wa nchi hiyo na Yemen.

S h a m b u l i z i h i l o limefanyika ikiwa ni kul ipiza kisasi cha mauaji yanayoendelea kufanywa na majeshi ya Saudi Arabia dhidi ya watu wa kabila hilo.

I j u m a a i l i y o p i t a askari watatu wa Saudia waliuawa na wengine wawili kujeruhiwa na roketi lililorushwa na wapiganaji wa Huthi h u k o K u s i n i m wa mkoa wa Najran nchini Saudia.

VITA YEMEN NA SAUDIA:

Askari wa Saudi Arabia

waonja chungu

Bi. Hillary Rodham Clinton amejitosa tena katika siasa za kusaka Urais wa Marekani mwaka 2016, kwa ahadi kuwa atakuwa kinara wa Wamarekani wa kawaida katika taifa ambalo ukosefu wa usawa wa kipato unazidi kutanuka.

Tofauti na miaka nane iliyopita wakati alipogombea na kushindwa na Barack Obama, Clinton na historia yake binafasi hawakuwa fokasi ya ujumbe wake wa kwanza wa kampeni. Hakuzungumzia wakati wake katika Baraza la Seneti wala miaka yake minne kama waziri wa mambo ya kigeni, au uwezekano wake wa kuandika historia kama rais wa kwanza mwanamke kuiongoza Marekani.

Badala yake, video yake ni mkusanyiko wa wapigakura wanaozungumzia maisha ya o , m i p a n g o ya o n a matarajio yao ya baadae.

" W a m e r e k a n i wa m e p a m b a n a k u t o k a katika nyakati ngumu za k i u c h u m i , l a k i n i h a l i iliyopo bado inaendelea kuwanufaisha wale walioko juu. Wamarekani wa kawaida wanahitaji kinara, nami nahitaji kuwa kinara huyo," alisema Clinton mwoshoni mwa video ya tangazo lake.

Video hiyo ya Clinton pamoja na mtandao wake h a v i k u g u s i a m a s u a l a ya kisera. Lakini ujumbe huo ulinuiwa kuwavutia Wa l i b e r a l i w a c h a m a cha Democrats , ambao wanachukulia usawa wa kiuchumi kama suala la kipaumbele.

Clinton sasa anapanga kuelekea katika majimbo yenye maamuzi ya Iowa na New Hampshire, kuungana na wapiga kura. Clinton anatumai kuepusha makosa ya mwaka 2008, alipoingia katika kinyanganyiro hicho kama mgombea anayepewa nafas i kubwa za id i ya kushinda na kushangazwa na Obama katika jimbo la Iowa.

Clinton mwenye umri wa m i a k a 6 7 a n a i n g i a katika kinyanganyiro hicho akiwa na rekodi ndefu ya utumishi wa umma, historia itakayomsaidia lakini pia kumuumiza.

Nitagombea Urais -Clinton

Page 6: ANNUUR 1173.pdf

6 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

Inaendelea Uk.8

MWEZI Novemba m w a k a j a n a nikiwa katika

ziara ya kifamilia wilayani Bukoba mkoani Kagera, nilipata pia fursa ya kumtembelea nyumbani kwake raf ik i yangu wa karibu aliyekuwa akifundisha katika shule ya sekondari Nyanshenye iliopo eneo la Nyamkazi katika Manispaa ya mji wa Bukoba.

K a t i k a s i k u t a t u nilizokuwa na swahibu wangu huyo, tulizungumza na kujadiliana mintarafu m a s u a l a m b a l i m b a l i yakiwemo ya kisiasa, ya kiuchumi pamoja na ya kijamii yaliyokuwa yakiendelea kujiri katika ngazi ya kitaifa na ya kimataifa kwa wakati huo.

Nakumbuka ilikuwa ni siku ya pili baada ya utekelezaji wa ibada ya swala ya magharibi katika msikiti mmoja uliopo eneo la Kashai mjini humo tukiwa mimi, swahibu yangu huyo pamoja na m wa l i m u m w i n g i n e wa shule ya sekondari Kahororo, ambaye kwa bahati nzuri sote tulikuwa tukifahamiana naye, mimi binafsi nilifahamiana naye tangu alipokuwa akiishi jijini Mwanza kabla ya kuhamia kwake mjini Bukoba; na yule swahibu wangu alipata kusoma naye miaka michache iliyopita katika Chuo K i k u u k i m o j a w a p o miongoni mwa Vyuo Vikuu vilivyopo mkoani Morogoro. Kwa ufupi wa maneno, sote watatu tulikuwa tukifahamiana vizuri.

Kufahamiana kwetu huko kulitusukuma katika mazungumzo ya hapa na pale ya masuala kadha wa kadha jioni ile yakiwemo ya kitaifa na ya kimataifa. Mojawapo ya suala la kitaifa tuliloligusia katika mazungumzo yetu hayo ingawa kwa muhtasari lilikuwa ni suala la kadhia ya ufisadi wa akaunti ya Tegeta ESCROW kwa k u wa k i p i n d i h i c h o ndipo mjadala motomoto kuhusu suala hilo ulikuwa ukiendelea kushika kasi kule bungeni Dodoma; na kwa upande wa masuala ya kimataifa tuliyaelekeza mazungumzo yetu katika

Na Abuu Nyamkomogi

suala la uibukaj i wa kundi linalojiita Dola la Kiislaamu (IS) na athari zake kwa Uislamu na Waislamu pamoja na kutathmini mwenendo wa harakati zake iwapo zinaafikiana na Qur-an na Sunnah au la.

S u a l a h i l i l a p i l i l i l i t u c h u k u a m u d a mrefu zaidi kulijadili k u l i k o l i l e l a a wa l i kiasi ambacho tulifikia hatua ya kulihitimisha k w a k u k u b a l i a n a kutokukubaliana kwa salama na amani.

Hali hiyo ilitokana na tofauti za kimtazamo na za kiuelewa au /na za

kimafuhumu juu ya suala la kundi la IS na uendeshaji wa harakati zake. Mimi pamoja na yule mwalimu wa Kahororo tulivyokuwa tukilitazama na kulielewa au kulifahamu lile kundi la Dola la Kiislaamu sambamba na uendeshaji

wa harakati zake, ilikuwa ni tofauti na mtazamo na uelewa au/na mafuhumu y a y u l e s w a h i b u wangu. Kwa hiyo ndio tukaamua kukubaliana kutokukubaliana pasi na kukejeliana, kudhihakiana na wala kukufurishana.

Naam, toleo la gazeti la An nuur la juma lililopita l i l i k u wa n a h a b a r i -

makala au habari kuu katika ukurasa wake wa kwanza yenye anuwani i l iyosomeka 'Kwenda Kupigana Somalia ni Ukafiri ' i l iyoandikwa n a m w a n d i s h i aliyejitambulisha kwa jina la Mussa Ame. Makala

hii iliibua sintafahamu sambamba na mshangao pamoja na maswali ya kitaharuki, kwa baadhi ya Waislamu niliopata kufuatilia kwa karibu mazungumzo yao katika kundi moja la Watsap ambalo nami ni miongoni mwa wadau wake, dhidi ya gazeti hili na mhariri wake kwa upande mmoja;

na mwandishi wa makala husika kwa upande wa pili.

Nianze mjadala wa suala hili kwa kunukuu h a p a s e h e m u y a mazungumzo ya baadhi ya wanakundi kuhusiana na makala husika kwa ajili ya mjadala zaidi kama yalivyowasilishwa kundini na mwanakundi mmoja sambamba na mrejesho kutoka kwa baadhi ya wanakundi.

Mwasilishaji taarifa: Gazeti La Annur, Tanzania l a p o t e z a m u e l e k e o . Limetoa habari kuwa kwenda kupigana Somalia ni ukafiri. Kisha akatuma kundini nakala ya ukurasa wa kwanza wa gazeti la Annuur lenye habari-m a k a l a h u s i k a k wa ithibati zaidi halafu chini yake akaandika hivi: Hii ni nakala ya An-nuur iliyotoka jana tarehe 10 April 2015

Mchangiaji wa kwanza: Ninalo hapa yani hili gazeti si la Kiislaamu.

Mwasilishaji taarifa: Kinachoonekana zaidi ni umamluki ulioingia k w e n y e wa n a h a b a r i hawa dhidi ya Uislamu na Waislamu. Mtume (s.a.w) anasema "aljihadi maadhwi i laa yawmi l-qiyama" yaani jihadi itaendelea hadi siku ya qiyama.

Mchangiaji wa pili : Kabisa yani sijuwi niliiteje hili gazeti. Mwasilishaji taarifa: Sasa wao kama wanaona Somalia hakuna jihad, wanaweza kutueleza ni wapi jihadi IPO?

Mchangiaji wa tatu: Wanapenda ubwabwa na tende watu wa maulidi mtihani sana.

Mwasilishaji taarifa: Kinachosikitisha zaidi ni ujinga wa mhariri wake, anapoiweka habari hii tena front page ikionesha ni habari muhimu sana kuliko zingine. Akiendelea kulingania ujahili wake a n a s e m a S o m a l i a wanaopigana ni Waislamu wao kwa wao.

Mchangiaji wa nne: Wao wanapenda kukuna nazi hata kama ni wanaume wamezoea kushika dufu hawazi kubeba AK47.

Mchangiaji wa tano: Kafiri wa kwanza yeye na kwani yeye nani si nabii wala si Mtume mdomo

Tujifunze kujadiliana kwa nguvu ya hoja

MAAFA yanayosababishwa na mashambulizi ya Saudi Arabia nchini Yemen.

MAAFA yanayosababishwa na mashambulizi ya Saudi Arabia nchini Yemen.

Page 7: ANNUUR 1173.pdf

7 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

S H A M B U L I Z I l a karibuni la mauaji ya wanafunzi 148 wasio na hatia katika Chuo Kikuu cha Garissa, Kaskazini Mashariki mwa Kenya ni tukio ovu, la kutisha na kumuhuzunisha kila mtu. Kimsingi ni tukio la kulaaniwa lisilokuwa na uhalali kwa namna yoyote.

Hata hivyo, baada ya msiba wa tukio hilo, umakini na uadilifu u n a h i t a j i k a k a t i k a m a t e n d o , k a l a m u , matamshi na kauli zetu hususan kwa vyombo vya habari, wanafikra, wa s o m i n a wa t u jumla nk. Kukosekana umakini na uadilifu huo kutapelekea kuchochea msiba mkubwa zaidi wa kijamii na kisiasa kuliko huu wa sasa.

Vyombo vya habari hususan magazeti mbali m b a l i v i n a i o n e s h a qadhia hii ya mauwaji ya Garissa kana kwamba ni vita baina ya Waislamu na Wakiristo. Jambo hilo sio sawa wala sio uadilifu. Ajabu! vyombo hivyo hivyo vya habari vinaporipoti kuhusu mauwaji ya Israel kwa Waislamu wa Palestina huwa havitamki kuwa ni vita baina ya Waislamu na Mayahudi.

Tu k u m b u s h e t u , m a r a n y i n g i k a m a sio zote vyombo vya habari vinaporipoti m a t u k i o m a o v u y a n a y o n a s i b i s h w a na Waislamu hukosa uadilifu katika kuripoti kwao. Kana kwamba hadhira ya vyombo hivyo ni wasiokuwa Waislamu peke yao. W a k a t i m w i n g i tunashuhudia vyombo mbali mbali vya habari kwa maksudi hupotosha uhalisia wa matukio h a y o i l i k u wa t o s a z a i d i W a i s l a m u . Kwa upande wa pili, yanapoj i r i matukio a m b a y o Wa i s l a m u ndio wahanga wakuu, vyombo hivyo hivyo huwa kama havipo au huwa kimya cha mfu ! Kwa mfano, mauwaji ya halaiki ya Waislamu nchini Burma, mauwaji ya halaiki ya Waislamu nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati nk. Au walau vyombo h ivyo vya habari kutaja kwamba katika tukio la mauwaji haya ya Garisa, mtu wa

Umakini katika tukio la GarissaSi Vita baina ya Waislamu, Wakristo

Masoud Msellem

mwanzo kuuwawa ni Muislamu aliyekuwa mlinzi wa chuo hicho.

A i d h a , w a k a t i mwengine tunaona vyombo vya habari n a m n a q a d h i a z i n a z o w a h u s u Waislamu zinavyotiwa chumvi na kulazimisha kinyume na ukweli ulivyo. Mfano mzuri wa kar ibuni n i i l e Operesheni ya Amboni Tanga, licha ya Jeshi la Polisi kukanusha kwamba waliokabiliana na polisi katika mapango yale walikuwa wahalifu na sio magaidi, bado vyombo mbali mbali vya habari vilionekana kushabikia kwa nguvu k u b w a n a k u n a d i wimbo wa magaidi na Al-Shabab.

K w a u p a n d e mwengine, tukio au matukio maovu ya wasiokuwa Waislamu yanapor ipot iwa na vyombo hivyo hivyo h u r i p o t i w a k w a heshima na uadilifu. Lakini tukio hilo hilo

lau l ingekuwa kwa Muislamu, ingekuwa balaa kubwa . Fikiria suala la karibuni la wafuasi wa Mchungaji Josephat Gwajima na jaribio lililoripotiwa kuwa la kumtorosha mchungaji huyo. Lau ingelikuwa wafuasi hao wa Gwajima ni Waislamu, ingelikuwa t a r u m b e t a k u b wa ! U n g e o n a v i c h w a vya habari “magaidi wavamia hospitali na bastola….” nk. Au tukio la siku chache zilizopita la Pol is i wilaya ya Kisarawe kumshikilia Joseph Mumbi baada ya kumkuta na bastola na risasi 8 kwenye ibada ya Ijumaa Kuu katika Kanisa la Mt Stephano. Angekuwa huyo sio ‘ J o s e p h ’ m a g a z e t i yangesemaje?

Kimsingi mwenendo huu wa vyombo vya habari wakati mwengine vikiwemo vya umma kukosa uadi l i fu na umakini ni jambo la hatari sana ambalo

huchochea zaidi fikra hatari ya ubaguzi na udini ambayo itapelekea mahusiano mabaya zaidi ya kijamii.

W a n a c h o p a s w a kukijua na kutanabahi vyombo vya habari, mufakirina/wanafikra na kila mmoja wetu ni kuwa chanzo msingi cha matukio kama haya ya Garissa na mfano wake ni mfumo batil wa kibepari na madola yake hususan Marekani na Uingereza. Madola hayo yana hali tatu: Kwanza, yana ajenda y a k u t a p a t a p a y a kupambana na mfumo ulioko dhidi yake ambao bila ya shaka kwa sasa n i U i s l a m u p e k e e . Ndio maana wakabuni kauli mbiu ya uongo ya “Vita vya Ugaidi”. Pili, madola hayo yana shauku na ghera kubwa ya kuzowa rasilimali za nchi changa zikiwemo nchi zetu kwa gharama yoyote. Tatu, katika hili

suala la kujikusanyia maslahi na kuzowa rasilimali hizo, madola hayo huzozana wao kwa wao kutokana na uroho wao. Kila mmoja akitaka ajipatie fungu nono.

K i l a d o l a k a t i k a madola haya mawili, katika kufikia malengo yao ya kujiimarisha na kujihakikishia kupata fungu kubwa na nono zaidi, hutumia mbinu mbalimbali hata chafu na za kiharamia. Katika hali hiyo ndio nchi zetu hutoswa kuwa chambo cha balaa na misukosuko isiyokwisha. Kilichoko sio mapambano baina ya Uislamu na Ukiristo wala kinyume chake. Bali ni harakati za mfumo wa kibepari na madola yake kujimakinisha, kujitanua na kujizolea maslahi kwa namna na mbinu yoyote hata kama ni kuangamiza maisha na kuzuwa migongano ya kijamii.

Kwa hakika, nchi zetu na dunia kwa ujumla inahitaji mfumo mwengine mbadala ili kuzitoa katika vurugu na mabalaa kama haya.

(Kwa maoni:Mob: 0778 870609)

BAADHI ya wanafunzi 148 wa Chuo Kikuu cha Garissa, Kaskazini Mashariki mwa Kenya wanaodaiwa kuuawa hivi karibuni.

Page 8: ANNUUR 1173.pdf

8 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

Inatoka Uk. 6wake halipii kodi mwache ajifurahishe.

Mwasilishaji taarifa: B inafs i n i l ihudhur ia semina ya taasisi kongwe ya I P C i l i y o f a n y i k a wilaya ya Same mkoani Ki l imanjaro , i l ikuwa mwaka juzi Desemba, m h a r i r i w a A n n u r alianzisha mada kama hii lakini vijana tulimpinga sana hadi ikawa ni vurugu kubwa.

Mchangiaji wa sita: Kwanza mungemtia adabu hata mdomo mngeupasua.

Mwasilishaji taarifa: Mhariri huyu Siku zote ameonekana kuwa ni mpinzani mkubwa wa jihadi kwa maslahi yake binafsi.

Mchangiaji wa saba: Kwa nini alitoka mrembo hata kope zake hamkunyofoa ilitakiwa kwa uchache hata kofi angepigwa.

Mwasilishaji taarifa: Ustaadhi Ilunga aliwapoza vijana na kusema jihad IPO na yeyote mwenye uwezo ni rukhsa kwenda popote penye jihadi kupigana.

Mwasilishaji taarifa: Mhariri Aliwahi kusema kwenye naka la zake zilizopita kuwa kama mujahidina wapo kweli, basi waende Afrika ya Kati, na hii ilikuwa ni kejeli.

Mchangiaji wa tisa: Sana sasa kama aliona kuna umuhimu mbona yeye hakuenda.

U k i y a d u r u s u k w a makini mazungumzo hayo hapo juu, utabaini k u wa s i m wa s i l i s h a hoja wala wachangiaji wa l i y o t h ub ut u s i t u kuki j ad i l i , ba l i ha ta kukidodosa kiini cha hoja ya msingi iliyowasilishwa na Bw. Mussa Ame katika gazeti hili toleo la wiki jana.

N a o m b a i e l e w e k e v y e m a n a m a p e m a kwamba kusudio langu hapa si kutaka kuunga au kutounga mkono hoja ya Bw. Mussa Ame bali ni kutaka kuonesha jinsi wengi wetu tusivyokuwa na uwezo wa kukabiliana na hoja kwa hoja na badala yake kushughulika zaidi na mtoa hoja badala ya hoja na hata kwenda mbali zaidi ya hapo.

N i t a f a f a n u a z a i d i kipengele hicho mara tu baada ya kurejelea mfano

wa tukio lililowahi kutokea takriban miezi sita iliyopita unaolandana na mjadala wetu wa leo ili kuonesha namna wengi wetu tunavyokabiliwa na tatizo la kutokuwa na uwezo wa kukabiliana na hoja kinzani.

Mfano wenyewe ni ule uliowahi kubainishwa huko nyuma na mwandishi mkongwe na mwenye tajiriba ya muda mrefu katika tasnia ya uandishi wa habari Bw. Omar Msangi katika makala yake ya mwezi Novemba mwaka jana katika gazeti hili iliyobeba anuwani iliyosomeka : 'Volikano ya Jihadi yaelekea Makkah'.

Kwa muktadha wa ninachokusudia kukieleza na kwa faida ya wasomaji ambao hawakupata bahati au fursa ya kuusoma mukadima wake katika makala hiyo, nimwombe Bw. Msangi aniruhusu kunukuu kile alichoandika katika utangulizi wake ule kabla ya kuendelea na hoja

WAPIGANAJI wa ISIS

yangu katika makala yetu ya leo.

''Kiasi cha wiki moja i l iyopita mtu mmoja alinipigia simu akiniambia kuwa alitaka kukutana na mimi. Hata hivyo akasema, kwa vile alikuwa njiani akitokea Kampala, atanipigia atakapofika mwisho wa safari yake. Hakuwahi kunipigia, ila nikawa napokea ujumbe wa maneno kupitia simu ya mkononi. Zilikuwa meseji nyingi kiasi zikifuatana moja baada ya nyingine. Kutokana na wingi wake, sitaweza kuzinukuu zote, ila ningependa kunukuu mbili tu ambazo zilinifikia s i k u y a J u m a m o s i ilivyopita baina ya saa moja na saa tatu asubuhi. Ya kwanza inasema:

''Ewe jaahili murakkab! Ewe khinziir wa Kishia! Ewe mchumia tumbo unaejipendekeza kwa ser ikal i ! Unasema IS w a n a p e w a m s a a d a n a U S A - I s r a e l . Tumeshuhudia Mashia na USA kuwapiga IS,

mbona umeufyata hujatoa makala kuhusu hilo? Na Alhamdulillah haukupita muda hata wa miezi miwili wakafarakana! Unafiki wenu ukawa hadharani! Eti taifa la Kiislaam mnaungana na USA kuwapiga ndugu I s lam? Ungekuwa s i khinziir ingetosha aibu hiyo na usingerudia tena k u wa f a n y i a wa j i n g a ' ' k a d a b r a k a a d a b r a ' ' kupinga Jihadi! Lakini ndio hivyo, khinziir ni khinziir tu.” (0683-270987).

' ' K a b l a s i j a m a l i z a kusoma ujumbe huo, mara ikaingia meseji nyingine. Yenyewe inasema:

' 'Mlipoona (Mashia) Jeshi la Allah sw linakaribia kuondoa utawala wa k inaf iq ! Utawala wa watu wanaowakufurisha Maswahaba kiraamin wa Mtume s.a.w katika Iraq, mkaona bora muungane na USA kuwapondaponda sasa nyie na USA mna dini gani? Maana yake inaonekana mnafanana mpaka mkakubaliana

kumpiga adui yenu IS! Allahu Akbar! Ungekuwa si khinziir hili jambo limekuvua nguo kabisa lakini wapi bwana. Lini khinziir atakuwa bora? Dawa yako inaiva...subiri, subiri, subir, subiri'' (0683-270987).

Baada ya mfano huo hapo juu, sasa nirejee katika ufafanuzi wa kile kipengele nilichoahidi kwamba ningekitolea ufafanuzi kutokana na unyeti wake katika mjadala wetu huu wa leo.

A w a l i y a y o t e , m wa s i l i s h a j i t a a r i f a alianza kutoa taarifa yake kwa madai kwamba gazeti hili limepoteza mwelekeo, nukta ambayo nimeitumia makusudi kama anuwani kuu ya makala yangu ili kuvuta hisia za wasomaji na kuwajengea raghba ya kusoma makala hii na kuitafakari maudhui yake kadri ya upeo wao aliyowajaalia Allah (S.W.). Ila nilichoongeza mimi

Inaendelea Uk. 12

Tujifunze kujadiliana kwa nguvu ya hoja

Page 9: ANNUUR 1173.pdf

9 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015Makala

Inaendelea Uk. 17

NCHI ya Saudi Arabia na baadhi ya Mataifa ya Kiarabu Mashariki ya Kati ni moja ya nchi ambazo ni soko muhimu sana la silaha za Marekani na baadhi ya nchi za Ulaya. S o k o h i l i l i m e k u w a chanzo muhimu cha kukua uchumi wa Marekani , kiasi kwamba Washington imekuwa ikitumia kila mbinu inayowezekana k u h a k i k i s h a k wa m b a maslahi yake yanalindwa katika ukanda huo.

Hata hivyo, pamoja na kuwa soko muhimu la silaha kwa Marekani, wachunguzi w a m a m b o w a n a o n a kwamba kitendo chake cha kuingia kijeshi kupambana na vikundi vya wapiganaji wanaopinga serikali ya Yemen, kumefungua zaidi milango ya soko hilo la silaha kwa Marekani. Si silaha tu, Saudia ambayo inaonekana kuwa ni moja ya nchi za Kiarabu ambayo ni mshirika mkubwa wa Marekani, imekuwa kama kituo cha kusimamia maslahi ya Marekani katika nchi nyingine za ukanda huo na pia na chanzo cha pato la mafuta kwa Marekani.

K w a m u j i b u w a mtandao wa irib, mwaka 2013, Serikali za Marekani na Saudi Arabia zilisaini m a k u b a l i a n o a m b a p o Washington iliuuzia utawala wa kifalme wa Riyadh silaha za kivita na zana za kijeshi zenye thamani ya dola bilioni 30. Makubaliano hayo, yaliiruhusu Marekani kuiuzia Saudi Arabia ndege 84 za kivita aina ya F15 kwa thamani ya dola bilioni 30. Andrew Shapiro, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani wa masuala ya kisiasa na kijeshi alidai kuwa Washington ilisaini m a k u b a l i a n o h a y o ya kuiuzia Saudia silaha, ili kuiimarisha kijeshi nchi hiyo kwa ajili ya kukabiliana na mashambulio yanayoweza kuikabili. Takribani mwaka mmoja nyuma, Congress ya Marekani ilipitisha muswada wa makubaliano ya kuiuzia Saudi Arabia silaha zenye thamani ya dola bilioni 60. Mauzo hayo yalijumuisha ndege za kivita aina ya F15, helikopta za kijeshi, makombora, mitambo ya rada na darubini za kuona kizani.

Hata hivyo, ili kupata ridhaa ya Congress, serikali

Saudia soko muhimu la silaha za MarekaniVita Yemen kuongeza soko Na Shaban Rajab

ya Washington ilihakikisha kwanza kwamba si laha z i t a k a z o u z i wa S a u d i a hazi takuwa t ishio kwa utawala dhalimu wa Israel. Pamoja na kwamba Saudia inaonekana kama sahiba mkubwa wa Marekani, lakini Israel ndiye msimamizi mkubwa wa kiusalama wa maslahi ya Marekani ndani ya Mashariki ya Kati na wakati huo huo akiwa ndiye adui mkubwa wa nchi za Kiarabu katika ukanda huo.

Aidha gazeti la Financial Times l inalochapishwa nchini Uingereza lilibainisha katika ripoti yake kwamba, pamoja na faida za kifedha za Marekani kuiuzia silaha Saudia, lakini pia hofu juu ya Iran imekuwa chachu kwa Marekani kuziuzia silaha zaidi nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi, ambazo nazo hazi j iamini mbele ya j irani yao Iran. Bila shaka kukosekana imani huko kumechochewa na propaganda za kiuadui za Marekani dhidi ya Taifa hi lo la Kiis lamu tangu mapinduzi ya Kiislamu ya mwaka 1979. Ni ukweli ulio dhahiri kwamba Iran inachukuliwa kama mpingaji namba moja wa utawala wa kidhalimu wa Israel, ambayo ni kipenzi muhimu kwa nchi za Magharibi na Marekani.

Mara baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, nchi za Magharibi na hasa Marekani zimekuwa z ik iz ishawishi nchi za Kiarabu za eneo la Ghuba ya Uajemi kununua silaha

kwa wingi kwa kisingizio kwamba, zijiweke tayari kukabiliana na uchokozi wowote wa kijeshi unaoweza kufanywa na Jamhuri ya Kiis lamu ya Iran, hasa ikizingatiwa kwamba taifa hilo limepiga hatua kubwa ki jeshi na k i teknolo j ia katika ukanda huo. Zaidi ni kwamba madai hayo ya nchi za Magharibi yamekuwa yakitumika kukuza farka kati ya Mataifa ya Kiislamu katika ukanda huo kupitia fitna ya Ushia na Usunni. Kwa mujibu wa gazeti hilo, katika kipindi cha hiki nchi za Saudi Arabia, Umoja wa Falme za Kiarabu - Imarati, Kuwait na Oman zimepanga kununua silaha na zana za kijeshi za Marekani zenye thamani ya dola bilioni 123 ambao ni uuzaji na ununuzi mkubwa zaidi wa silaha kufanywa katika mazingira ya amani. Weledi wa mambo wanasema hatua ya utawala wa kifalme wa Saudia ya kununua silaha za Marekani zenye thamani ya dola bilioni 30, ina umuhimu mkubwa mno kwa uchumi ulioporomoka wa Wa s h i n g t o n , k i a s i kwamba wanayachukulia makubaliano ya ununuzi wa silaha hizo kama msamaria mwema na muokozi wa uchumi wa Marekani.

Kwa upande mwingine, nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi zinaona kuwa kununua silaha za gharama ya dola bilioni 123 kutoka Marekani , kutazisaidia pia nchi zao huko baadae kuandaa maelfu ya nafasi za

kazi kwa raia zake. Mbali na hayo, Washington

inaonekana kuwa na lengo jingine katika makubaliano ya kuuza silaha kwa nchi hizo, ambalo ni kuanzisha mfumo na muundo mpya wa usalama katika Mashariki ya Kati kwa ajili ya usafirishaji n i s h a t i h a s a m a f u t a kuelekea Magharibi. Kama inavyofahamika falsafa ya mashirikiano ya Marekani kwa nchi nyingine, haina adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu. Vile vile ni falsafa ya Marekani kwamba inathamini yule ambaye atainufaisha zaidi kuliko yule anayeweza kuitia hasara.

We l e d i wa s i a s a z a Magharibi wanaona kuwa Marekani ina malengo m e n g i n e n y u m a p a z i a inayoyafuatilia na pengine muhimu zaidi katika uuzaji na urundikaji wa silaha katika eneo la Mashariki ya Kati. Nayo ni wafarakanishe, uwagawe na daima uendelee kuwanyonya kirahisi.

Mwaka 2010 Taasisi ya Utafiti wa Kimataifa wa Amani ya Stockholm SIPRI imetangaza kuwa, Marekani ni mdhamini mkubwa wa silaha kwa nchi za Kiarabu zilizoko katika eneo la Ghuba ya Uajemi kati ya mwaka 2005 hadi 2009. Taarifa iliyotolewa na taasisi hiyo imeeleza kuwa, Marekani ina mauzo ya silaha ya asilimia 54 ya kwa nchi za eneo hili, huku ikifuatiwa na Ufaransa ambayo ina asilimia 21 katika eneo nyeti la Ghuba ya Uajemi.

Taas i s i h iyo i l i e l eza

kuwa, baada ya Marekani na Ufaransa, nchi nyingine zinazouza kiasi kikubwa silaha kwa nchi za Kiarabu za eneo la Ghuba ya Uajemi, ni Urusi , Uingereza na China. Hata hivyo inaelezwa kuwa, Saudi Arabia ndiyo inaongoza kwa kununua silaha kwa wingi katika eneo hilo kuanzia mwaka 1990 hadi 2009, ikifuatiwa na Umoja wa Falme za Kiarabu. Ukweli ni kuwa katika miaka ya hivi karibuni Saudi Arabia imenunua silaha za mabilioni ya dola bila hata ya kukabiliwa na tishio lolote la adui wa kigeni katika miongo mitano iliyopita. Mbali ya nchi hiyo, Qatar, UAE, Kuwait na Bahrain pia miaka mitatu iliyopita zilisaini makubaliano ya ki jeshi na Marekani, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni thelathini. Kwa kuzingatia hali hiyo tunaweza kusema kuwa viongozi wa nchi za Kiarabu kwa muda mrefu wamezigeuza nchi zao kuwa maghala ya silaha zinazonunuliwa kutoka nchi za Magharibi kwa kutegemea pato la mafuta, bila hata ya kuzitumia silaha hizo. Leo silaha hizo zinawaangamiza wao wenyewe.

Wakat i Marekani na wenzake wa Magharibi wakilenga soko la silaha na kupata mabilioni ya dola, wakati huo huo zimekuwa zikifanya kila linalowezekana kuzusha anga ya hofu na ukosefu wa amani, kwa kuituhumu Iran kuwa ni tishio katika eneo la Ghuba ya Uajemi, lengo kubwa zaidi likiwa ni kuuza silaha kwa nchi za Kiarabu.

Sasa silaha zilizokuwa z i k i l u n d i k w a g h a l a n i zimepata pa kuzitumia. Wanaouliwa si wengine bali ni jamii ya Waislamu k wa m a d h e h e b u ya o . W a l i o z i t e n g e n e z a wanaendelea kutengeneza fedha, wanaendelea kukoleza f a r k a . Wa s i o n a h a t i a wanapoteza maisha. Syria, Iraq, Yemen, Libya, Misri ni mfano mzuri. Kwa mfano usiku wa kuamkia April 4, yalifanyika mashambulizi ya anga dhidi ya ki j i j i kimoja kilicho karibu na mji mkuu wa Yemen, Sana'a, na kuangamiza familia moja ya watu tisa. Taarifa zinasema k u w a w a t u w e n g i n e w a t a n o w a l i j e r u h i w a katika mashambulizi hayo yaliyofanywa na muungano

GARI la kurushia makombora la Jeshi la Saudi Arabia.

Page 10: ANNUUR 1173.pdf

10 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

Inaendelea Uk. 11

BAADA ya kuandika makala iliyopita juu ya ukafiri wa kuuana

Waislamu kwa Waislamu, nilipokea simu nyingi sana zilogawika katika makundi matatu. Kundi moja walinilaumu sana na kuona nimefanya dhambi kubwa sana. Kundi la pili walipongeza. akini Kundi la tatu waliniomba nifafanue mada zaidi kwa vile kuna vipengele vingi nilivikiuka. Mada hii itafafanua baadhi tu ya vipengele na mada itaendelea mpaka pale wasomaji watakapoelewa lengo la mada hizi.

Kuhusu vita vya Somalia n a k i r i k w a m b a h a p o mwanzo wakati Wasomali walipokuwa wakipambana na Ethiopia walikuwa katika jihadi, na pia walipokuwa wakipambana na majeshi ya Marekani walikuwa katika jihadi. Sasa baada ya Mataifa hayo kuona kuwa hawawezi kuwashinda, wa k a t u m i a m b i n u ya kuwagawa Wasomali katika makundi yenye kupingana na wameliweza hilo. Sasa Wasomali wanapiganishwa

Haki za Waislamu na mipaka ya JihadNa Mussa Ame

wenyewe kwa wenyewe. Ni katika hali hii sasa, jukumu la Waislamu waliobakia ni kuwasuluhisha s iyo kuchochea vita kwa kusaidia Kundi lolote lile. Kwani Waislamu kupigana wao kwa wao ni kitendo cha kikafiri.

V i t a v y a S o m a l i a vinatumiwa sasa kama mradi wa Mataifa kujipatia fedha za kupigana na ugaidi. Kwa hivyo kuendelea kwa mzozo huo, ni faida ya makafiri si Uislamu. Nchi zinazoshiriki kulinda amani, hujivunia

mamilioni ya fedha ndiyo maana wao hupendelea mzozo usimalizike.

Ama kuhusu mapigano yanayotokea huko Syria, Yemen na Iraq pia ni vita vya wenyewe kwa wenyewe. Wanaouwa ni Waislamu na

wanaouliwa ni Waislamu na damu ya Muislamu ni takatifu sana ni haramu kuimwaga. Na vita hivi vinapangwa na makafiri kwa kuwashawishi Waislamu kupigana kwa visingizio mbali mbali, na Wislamu hukumbwa na jazba wakaingia vitani kumwaga damu za wasio na hatia.

Leo nimeombwa nifafafue haki za Muislamu, pia wasomaji wengine wanataka nielezee ni wakati gani huwa halali kumuua Muislamu, lakini naona mada hiyo akipenda Allah (SW) nitaitoa baadaye.

Allah (SW) anasema: “Na saidianeni katika wema na uchaungu, wala msisaidiane katika dhuma na uadui na mcheni Allah (SW) hakika Allah (SW) ni mkali wa kuadhibu.” (Maidah :2)

Katika kuifafanua aya h iyo , amesema Imamu Tabarany (1/227) kuwa amesema Mtume (SAW) “Atakayekwenda kumsaidia dhalimu na anajua kuwa ni dhalimu ametoka katika Uislamu.”

Mtu huyu hawi kafiri wa imani kwamba si Muislamu

‘Jihad’ kuangamiza Waislam Somalia na siasa za Zanzibar

Na Omar Msangi

NA K U M B U K A n i l i w a h i k u h u d h u r i a

Mkutano mmoja wa REDET Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ilikuwa ni katika kile kipindi cha Muwafaka wa Pili wa Zanzibar baada ya ule uliofuatia Uchaguzi Mkuu wa 1995. Katika Mkutano huo aliyekuwa Waziri Kiongozi, Shamsi Vuai Nahodha aliusifia sana ‘Muafaka’ huo akisema kuwa ni wa kupigiwa mfano kwa sababu umetokana na Watanzania wenyewe. Kwamba haukuwa sawa na ule wa awali uliovunjika uliokuwa umesimamiwa na akina Anyauko. Na akahitimisha kwa kusema kuwa huo ulikuwa ni ushahidi kuwa Waafrika/Watanzania, tunaweza

k u t a t u a m a t a t i z o y e t u w e n y e w e b i l a kusimamiwa na mtu kutoka nje.

Kwa bahati mbaya hata muafaka huo haukuzaa matunda yal iyokuwa yametarajiwa. Zanzibar iliendelea kuonja tamu ya siasa za chuki, uhasama, v i s a v ya J a n j a w e e d n a m e l o d y . W a t u wakaendelea kuuliwa, kupigwa, yakawepo madai ya kubakwa wanawake, kuporwa mapambo yao ya dhahabu na visa vya kila aina.

U k i l i t i z a m a j a m b o hili na yaliyokuja kujiri baadae, unakuta kwamba kumbe Zanzibar walikuwa wamejidanganya kwa kudhani kuwa wakikaa kama CCM (Bara na Vi s i wa n i ) , a u k a m a Watanzania, ni wamoja. Rais Mstaafu Amani Abeid Karume na Maalim Seif,

chini ya uongozi wa kamati ya Wazee na Kamati ya Maridhiano, walilitambua h i l o wa k a k a a k a m a Wazanzibari. Wakafikia ‘Muafaka’ ulioleta amani na utul ivu. Muafaka ulioleta Serikali ya Umoja wa Kitaifa i l iyofanya Zanzibar ipumue.

Ukitizama yaliyojiri katika Bunge Maalum la Katiba lililopita Dodoma, na kauli zinazoendelea hivi sasa kwa upande wa wanaoitwa CCM, Wahafidhina, Zanzibar inae lekea kumeguka w a r u d i k u l e k u l e w a l i k o k u w a . H a w a Wazanzibari wahafidhina, ni wazi kuwa nguvu yao kubwa ni kwa CCM (Bara) ambako ndio kwenye serikali. Hali iliyojitokeza Dodoma ikiendelea, ni wazi hii hali ya muafaka na maridhiano itakufa na

Dkt. Ali Mohamed SheinMAALIM Seif Sharif Hamad Inaendelea Uk. 11

Page 11: ANNUUR 1173.pdf

11 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 201511 AN-NUURMakala

Haki za Waislamu na mipaka ya JihadInatoka Uk. 10tena, ila ametenda vitendo vibaya kinyume na desturi ya Waislamu. Tuelewe utukufu wa Muislamu na ubaya wa kumuua Muislamu mmoja tu aliyetoa shahada. Allah (SW anasema: “Kwa sababu ya hayo tukawaandikia wana wa Israili kwamba atakayemwua mtu bila ya yeye kuua mtu, au kufanya fisadi katika nchi ni kama amewaua watu wote, na mwenye kumwacha mtu hai (kumsaidia kuishi) ni kama amewaacha hai watu wote. Na bila shaka Mitume wetu waliwafikia na hoja zilizo wazi, kisha wengi katika hao baada ya haya walikuwa waharibifu sana katika nchi.” (Maida:32).

Aya hiyo ameitafs ir i Ibnu Abbas (RA) kuwa atakayezuia watu na kuua watu wasio na hatia, huyu ni kama amewahuisha wale watu wote na atakayeua nafsi moja, ni kama ameuwa watu wote.

Said bn Jubayri (RA) amesema, atakayehalalisha damu ya Muislamu mmoja asiye na hatia ni kama amehalalisha damu ya

Waislmu wote duniani, na atakayeharamisha damu ya Muislamu mmoja ni kama ameharamisha damu ya watu wote. Na amesema Mujahid (RA) atakayemuua M i s l a m u m m o j a t u makusudi pasi na hatia malipo yake ni moto. Allah (SW) atamghadhibikia na atamlaani na atamtayarishia dhabu kali sana. Maneno hayo ya Mujahid (RA ), ni sawa na aya aya Suratulnisai 93 “Na mwenye kumuua Muislamu kwa kukusudia, malipo yake ni jahannam, humo atakaa milele, na Allah(SW) amemghadhibikia n a a m e m l a a n i n a amemwandal ia adhabu kubwa.”

Amesema Ibn Kathyr k a t i k a a ya h i y o k u n a makemeo makubwa sana kwa anayeua kwa makusudi kumuua Muislamu. Na wameona Maulamaa wengine k wa m b a a t a k a ye m u u a Muislamu kwa makusudi na akafa hakutubia, basi ataingia motoni milele, na kwa vile atakuwa amelaaniwa. Ni kutokana na uzito wa aya hizo, ninahisi iko haja ya kuzinduana kwa sababu kuna

watu hufikiria kuwa kumuua Muislamu ni jambo la mchezo. Akishakuwa hakubaliani na itikadi yako basi unaweza kumchinja kama kuku. Wako waliokuwa na fikra ya kwamba kusimamisha dola, kunahalalisha mauaji

ya Waislamu. Ni kutokana na uzito wa aya hizo, ninahisi iko haja ya kuzinduana kwa sababu kuna watu hufikiria kuwa kumuua Muislamu n i j a m b o l a m c h e z o akishakuwa hakubaliani na itikadi yako basi unaweza

kumchinja kama kuku. Wako waliokuwa na fikra ya kwamba kusimamisha dola a Kiislamu ni kwa mapambano ya silaha, lakini jee unapambana na nani na Muislamu mwenzako?

U i s l a m u u m e k a t a z a kus imamisha jambo la halali kwa kutumia njia za haramu. Damu ya Waislamu inayomwagwa Iraq, Syria, Yemen na Somalia inafaa tuiangalie kwa mtazamo mpana zaidi. Jee, mizozo hii ni lazima itatuliwe kwa mtutu wa bunduki? Hakuna suluhu katika mambo haya?

Kwa nini ni sisi Waislamu t u n a o u wa n a s a n a k i l a wakati. Iran ilipigana na I r a q n a wa l i o k u f a n i m a e l f u y a Wa i s l a m u , baadaye tena, Waislamu hao wakadanganywa kuwa wakimuua Sadam Hussein watakomboka, matokeo yake ni vita isiyo na mwisho mpaka leo. Waislamu wa Libya wakatumiwa tena na NATO wakihadaiwa kuwa watasimamisha Uislamu kwa kumuondoa Gaddafi, maelfu wakauawa, majengo yakabomolewa, mafuta yao

‘Jihad’ kuangamiza Waislam Somalia na siasa za Zanzibar

Inatoka Uk. 10yaliyojiri hivi karibuni katika msafara wa CUF wakitoka mkutanoni , ni kwamba ‘melody’ na Janjweed yaweza kurejea na Serikali ya Umoja wa Kitaifa itaporomoka.

Ikifikia hapo, CCM wahafidhina watapata nguvu kubwa kutoka Bara na pengine hata Jumuiya ya Kimataifa na watakuwa ndio wenye ser ikal i . Waliosalia watakuwa ‘Al Shabaab’. Wapizani wa wahafidhina.

Ukisimama upande wa hawa CCM na CUF wanaotaka maridhiano na serikali ya Umoja wa Wazanzibari, hawa w a h a f i d h i n a n a o wanapewa nguvu kubwa kutoka CCM, Bara na Jumuiya ya Kimataifa. N i W a z a n z i b a r i w a n a r a r u l i w a . Wanararuana wenyewe kwa wenyewe. Sera ya w a g a w e u w a t a w a l e inafanya kazi. Hakuna k i n a c h o e n d e l e a , s i katika elimu, uchumi wala huduma za kijamii. Zanzibar inabaki doro.

Kwa maana hii, CCM Bara au kundi lolote l i t a k a l o d a i k wa m b a linaisaidia Zanzibar kwa kuliunga mkono kundi

la Wahafidhina wasio taka Serikali ya Umoja, litakuwa linadanganya. H a l i w a t a k i i m e m a Zanzibar. Kwa upande mwingine, mtu yeyote wa nje, iwe ni CHADEMA, NCCR au taasisi nyingine yoyote, itakayosimama na Wazanzibari kupambana na CCM wahafidhina, hataweza kuondoa tatizo bali kutia petrol katika m o t o . I t a k u wa s a s a ushabiki wa kupingana tu mradi kupingana kama ilivyojitokeza pale Dodoma. Namna pekee ya kuwasaidia Wazanzibari, ni kuwasaidia waweze k u k a a p a m o j a k a m a Wazanzibari na kutambua a g e n d a z a o n i z i p i , salama yao kama nchi ipo wapi, fursa walizo n a z o , c h a n g a m o t o , n g u v u w a l i o n a y o , madhaifu yao, maadui na kila l inalowahusu kama Wazanzibari. Kama hilo likishindikana, kwa siasa hizi tulizoshuhudia

Dodoma, Mungu aepushie mbali, laweza kuishia katika kuraruana wenyewe kwa wenyewe.

Sasa jaalia muafaka huu wa kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa, uliwapeleka kuwa na Ser ikal i kama i le ya Umoja wa Mahakama za

Kiislamu Somalia. Baadae wengine wakarudi katika ‘melody’ wakiwa na CCM Bara na Jumuiya ya Kimataifa nyuma yao. Ikifikia mtafaruku wa kuvunjika serikali hiyo, mtu akitoka Bukoba, Kigoma, Mwanza akidai kuwa anakwenda Jihad Zanzibar kwa kusimama upande wa kundi moja la Wazanzibar, hakuna anachoweza kuwasaidia za id i ya kuwasa id ia kuuwana nwenyewe kwa wenyewe.

K i s i a s a h a p o inawezekana kulikuwa na matatizo ya namna mbili. Moja ni kuwa inawezekana h a t a k a t i k a k u we k a maafikiano yaliyozaa Serikali ya Umoja wa Kita i fa , pal ikuwa na ubinafsi. Watu walikuwa wakitizama mbele maslahi yao binafsi , sio nchi, na wananchi. Kama si hivyo, basi yalikuwa ni maafikiano ya viongozi wa juu tu, lakini makada

waliowazunguka (CCM), p e n g i n e n a s e h e m u ya wa n a n c h i ( C C M ) hawakuwa tayari.

Sasa suala hapo haliwi kushikiana mtutu, bali Da’wah/Elimu/Ufahamu. Hawa makada wafikie m a h a l i wa o n e k u wa masilahi ya Zanzibar na Wazanzibari, ni muhimu zaidi kuliko masilahi yao ndani ya CCM.

Toka imeporomoka serikali ya Siad Barre, Wasomali wamekuwa katika machafuko. Juhudi zote za kimataifa kuwaleta pamoja zilifeli mpaka i l ipoibuka Umoja wa Mahakama za Kiislamu. Mara baada ya nchi kutulia, mabeberu waliokuwa wakichochea mgogoro huo na ambao walikuwa hawataki Somalia iwe na amani, hilo likawa pigo kubwa kwao. Kwanza waliwachukua wale wale wababe wa Kivita, wakawa wanawasadia kupambana na Serikali ya Umoja wa Mahakama za Kiislamu. Mabeberu wasivyokuwa na haya wala kuona vibaya, eti hawa wababe wa kivita ndio wakapaewa hadhi na wadhifa kuwa wanapambana na magaidi. ‘Magaidi’ wenyewe, eti

RAIS wa sasa wa somalia Sheikh Mohamoud.

Inaendelea Uk. 13

Inaendelea Uk. 13

MMOJA wa wananchi wa Yemen.

Page 12: ANNUUR 1173.pdf

12 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 201512 MAKALA/MASHAIRI

Inatoka Uk. 8ni anuwani hii ndogo 'Tujifunze kujadiliana kwa nguvu ya hoja ' . Kimsingi, hili ndilo suala nililokusudia kulijadili katika makala hii kupitia mazungumzo yale ya kundini na mfano ule wa mashambulizi dhidi ya Bw. Omar Msangi nilioutoa hapo juu.

N i l i t a r a j i a mwasilishaji taarifa angejikita zaidi katika maudhui ya mada ya mjadala na kutupa hoja mbadala kutoka katika Qur-an na/au Sunnah kwa kuonyesha kuwa 'Kwenda Kupigana Somalia si Ukafiri' kama alivyofanya Bw. Mussa Ame katika makala yake yenye anuwani 'Kwenda Kupigana Somalia ni Ukafiri'.

B a d a l a y a k e akakimbilia kulijadili gazeti kwa kudai kuwa limepoteza mwelekeo. Bila kuathiri uhuru wake wa kutoa maoni, yumkini kwa maoni yake hilo ni sahihi, nami sina haja ya kuonesha upinzani wowote juu ya maoni yake kuhusu hilo, ninachokishadidia hapa ni kwamba mwasilishaji taarifa ameshindwa kukabiliana na maudhui ya mada ya msingi kwa nguvu ya hoja na badala yake analishutumu gazeti lililotumika kama nyenzo ya kuwasilisha m a k a l a i l e k w a wasomaji; hali ni hiyo hiyo kwa mchangiaji wa kwanza na wa pili.

Hoja ya kujadiliwa h a p o h a i k u p a s w a kuwa gazeti, kwani lenyewe limetumika kama nyenzo tu ya kuwasilishia maudhui kilichopaswa kujadiliwa ni hoja ya Bw. Mussa Ame.

Hilo linanikumbusha i l e k a d h i a y a k u s h u p a l i w a n a hatimaye kufungiwa kwa Redio Iman na Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano baada ya kushindwa kuzikabili h o j a z i l i z o k u w a zikirushwa hewani kupitia chombo hicho cha habari.

Katika sehemu ya pili, mwasilisha hoja a m e s h u g h u l i k a n a wanahabari badala ya kushughulika na habari iliyowasilishwa na mwandishi , h i i ni sawa na kusema a m e s h u g h u l i s h w a zaidi na mwandishi wa habari-makala ile kuliko maudhui ya makala husika.

Vilevile, Kwa kuwa mwandishi ameonesha kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah kuwa kinachojiri Somalia si j ihadi, kwa hiyo mwasilishaji wa taarifa alipaswa kutoa dalili mbadala kutoka katika Qur-an na/au Sunnah z e n y e k u o n y e s h a kwamba kinachojiri Somalia ni jihadi badala ya kutaka aonyeshwe mahali j ihadi ilipo, kwani suala hilo si lenye kuhusiana na maudhui ya mada ya msingi ya mwandishi.

Mchangiaji wa tatu na wa nne, wao wameishia k u t o a k e j e l i k w a mwandishi badala ya kushughulika na hoja yake.

K a t i k a s e h e m u ya tatu, mwasilishaji taarifa anaonekana k u v u k a m p a k a n a kumshambulia moja kwa moja mhariri wa gazeti hili badala ya kushughulika na hoja ya mwandishi wa makala i le kwa kuonyesha kuwa 'wanaopigana Somalia si Waislamu kwa Waislamu' kama alivyobainisha yeye katika makala yake kuwa 'wanaopigana Somalia ni Waislamu kwa Waislamu'.

Mchangiaji wa tano ameishia kumkufurisha mwandishi wa makala badala ya kujibu hoja zake kwa nguvu ya hoja mbadala.

K a t i k a s e h e m u ya nne, mwasilishaji taarifa anadai kwamba yeye na vijana wengine walimpinga mhariri alipoleta mada kama hiyo katika semina kule Kirinjiko Same. Japo hakubainisha kama

walitumia nguvu ya hoja au hoja ya nguvu, yumkini walitumia hoja ya nguvu ndio maana pakatokea vurugu kama anavyodai !

Yote kwa yote hata kama walitumia nguvu ya hoja kufanikisha mapambano yao dhidi ya mhariri mwenyewe au hoja zake; kwanini basi leo anashindwa kukabiliana na hoja ya mwandishi na badala yake anaendelea na mashambulizi yake dhid i ya mhar i r i ambaye k ims ing i hahusiki moja kwa moja ka t ika ho ja iliyotolewa na Bw. Mussa Ame.

M c h a n g i a j i w a sita, wa saba na wa nane, wao wameishia kushadidia kutoa kipigo dhidi ya mhariri kule Kirinjiko huku wakiiacha hoja ya msingi ya mwandishi ikielea hewani pasi na kuikabili kwa nguvu ya hoja mbadala.

Mwasilishaji taarifa na mchangiaji wa tisa wanaonekana w a k i h i t i m i s h a mazungumzo kwa kuzidi kupambana kwa hoja ya nguvu na mhariri badala ya k u s h u g h u l i k a na hoja ya msingi ya mwandishi kwa nguvu ya hoja.

K wa m u k t a d h a huu, ndio maana naona kuna ulazima n a u m u h i m u wa kujifunza kujadiliana kwa nguvu ya hoja na si hoja ya nguvu. Haya shime ndugu zangu, tuanze sasa kujifunza hili kupitia kisa cha Nabii Ibrahimu (a.s.) na Mfalme Namrudha (2:258).

( M w a n d i s h i w a makala hii ni msomaji wa muda mrefu wa gazeti la AN-NUUR a n a y e i s h i j i j i n i Mwanza).

SIASA NA DINI1. Hebu niulize swali, mnipe jibu watunziShida imenikabili , kwenu naomba ujuziNielewe tafaswili , linitoke bumbuwaziHivi siasa na dini , zatofautishwa wapi

2. Siasa ni ya awali ,dunia imebariziMitindo ya serikali , hasa zama zetu hiziViongozi mbalimbali, wanatupa shinikiziHivi siasa na dini, zatofautishwa wapi

3. Dini yaja namba mbili, nayo inatupa kaziTumekuwa madhalili, kwa nini hatujifunziTumetupilia mbali, twafuata mageuziHivi siasa na dini, zatofautishwa wapi

4. Siasa za viririrni, sasa zimeshika kaziNi mashuhuri nchini, kila kona ziko waziZinatufundisha nini, na tufanye upembuziHivi siasa na dini, zatofautishwa wapi

5. Maimamu membarini, hawajachoka kuaziMashekhe madarasani, watafuta wanafunziMbona hatuonekani, kiwapi kipingamiziHivi siasa na dini, zatofautishwa wapi

6. Malenga wa redioni, naomba ufafanuziNanyi wa magazetini, mlango wenu uwaziKwetu siasa na dini, uko wapi ubaguziHivi siasa na dini, zatofautishwa wapi

7. Tamati natumaini, majibu kwenu wapenziIfanyeni tathmini, msione upuuziLa faida tubaini, litufae kwa MwenyeziHivi siasa na dini, zatofautishwa wapi

Mtunzi ni:-Zainab MtimaMbweni, Zanzibar0717 165 602

Tujifunze kujadiliana kwa nguvu ya hoja

Adayo hupendeleya, wa dinenu wapinzani,Mazuri kuyazuiya, yenu pasi hata soni,Kukuswibuni mabaya, wao ndilo hutamani,UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

Daima huwatakiya, yale yanokudhuruni,Ya shururi huridhiya, ninyi yanokufikeni,Ya khairati udhiya, yenu kwao ng'amueni,UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

Gaidhi i dhahiriya, kutoka mwao vinywani,Vyanda wanawaumiya, kwa indazo mitimani,Waloficha batiniya, kungaye i kwa MANANI,UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

Si kwamba nawazuliya, ishanena QUR-ANI,SURA ya TATU rejeya, si nyingine IMRANI,AYA nawakashifiya, hayo zenye kubaini,UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahahiriya.

MIATU wa THAMANIYA, ASHARA kwa tamakuni,Soma thuma endeleya, hadi MIA ISHIRINI,Humo utajioneya, yote kwa wake ndani,UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

ALLAH alotuambiya, si dhahania yakini,Wenyewe mwashuhudiya, yawahusu wao nini!MAHKAMA kugomeya, ya KADHI mahakamani?UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

Na hofu wamewatiya, viongozi wa nchini,Si kwa hoja usuliya, kwa pogo yao mizani,Lengo walokusudiya, lipate kuyumkini,UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

Nudhumu namaliziya, kwa nyote kukuombeni,Kujifunza kuteteya, kwa pamoja yenu dini,'Wenzenu' huwa pamoya, kwa yao hamuwaoni?UKWELI wa QUR-ANI, si kombo u dhahiriya.

ABUU NYAMKOMOGI-MWANZA.

NONGWA YA MAHKAMA YA KADHI

Page 13: ANNUUR 1173.pdf

13 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

Haki za Waislamu na mipaka ya JihadInatoka Uk. 11yakaibiwa na mpaka leo hakuna Uislamu uliosimama ila ni vita vinavyoendelea. Mabeberu na NATO yao wanavuna na kukomba mafuta bila ya udhibiti kutoka serikalini kama ilivyokuwa wakati wa Gaddafi. Hivi hatuna akili sisi? Hatuyaoni haya?

Syria kunatokea umwagaji mkubwa wa damu, Somalia m i a k a k a d h a a ya v i t a visivyokwisha, tumebakia kumtaka Muhali Mungu kwa kunyanyua mikono kuomba Allahuma nsuru Mujahidina fii Suria wa Somalia, wa Iraq, wakati tumekuwa kama vikaragosi wa mabeberu tunaotumiwa b i l a k u t u m i a a k i l i . Afghanistan hatukujifunza, Iraq hatukujifunza, Libya hatukujifunza, sasa tupo na IS, Al Shabaab, sisi watu gani? Haya tumeanzishiwa tena Yemen. Sasa kwa Yemen, ni upande upi upo katika Jihad? Saudi Arabia na washirika wake au Wahoudh na wananchi wa Yemen kwa ujumla!

Waislamu walipouliwa J a m h u r i ya A f r i k a ya K a t i h a k u n a h a r a k a t i iliyohamasisha kupeleka

wapiganaji kwa sababu m a b e b e r u w a l i k u w a hawakulitaka hilo kwa hiyo hawakuleta mawakala wao huku kuhamasisha Jihad. Au wale waliokuwa wakiuliwa Afrika ya Kati hawakuwa Waislamu? Tena kama ni Jihad ingekuwa ile maana kule ilikuwa wazi-Wakristo huku Waislamu kule. Mbona hilo hatukuona likishabikiwa kama hili la Somalia na Syria inaloratibiwa na Wamarekani na Mayahudi?

Wakati Waislamu wa Bosnia wal ipouliwa na

kunajisiwa nchi za Kiislamu z i l i n y a m a z a k i m y a , hakuna nchi ya Kiislamu iliyopeleka jeshi. Wapalestina wanapouliwa na Waizraeli hakuna umoja wa nchi za Kiarabu wala harakati ya ukombozi inayopeleka jeshi na kuhimiza watu kwenda huko kuwasaidia ndugu zetu Wapalestina bali hufunga mipaka yao mpaka misaada wanayoletewa Wapalestina na mashirika ya makafiri isiwafike. Lakini leo Umoja huo huo wa nchi za Kiarabu/Kiislamu zipo na Marekani/

MOJA ya Ndege za kivita za Saudi Arabia zinazotumika kuishambulia Yemen.

Israel kuipiga Syria, Iraq, Yemen na Somalia! Hatuoni? Hatujiulizi? Hatuna akili?

M t u m e ( S A W ) a l i t a h a d h a r i s h a s a n a kuhusu haki za Waislamu. Amesimulia Abuu Hurayra (RA) amesema Mtume(SAW) “ m s i h u s u d i a n e w a l a m s i z i d i s h i a n e n i b e i minadani, msibughudhiane, msihamane, wala asinunue mtu juu ya bei ya mwenzake. Kuweni waja wa Allah (SW) mlio ndugu. Muislamu ni ni ndugu wa Muislamu mwenziwe, asimdhulumu

a z i m d h a l i l i s h e w a l a asimdogoshe. Uchamungu u p o h a p a , a k a a s h i r i a moyoni mwake mara tatu, Muislamu kwa Muislamu mwenzake ni haramu damu yake (asiimwage), mali yake (asiichukue kwa dhulma) na heshima yake (asiivunje)”. (SM2564).

Usama bni Zayd (RA) alipigana na kafiri katika vita. Yule kafiri alipoona anashindwa alitoa shahada, lakini baadaye alipigana tena upande uleule wa makafiri. Usama bin Zayd (RA) akakutana naye tena wakapigana, na yule kafiri akatoa shahada tena, na mara ya tatu wakapambana mpaka akampiga mkononi, mara ya tatu wakapambana na akatoa shahada tena mara ya tatu, mara hii Usama bin Zayd (RA), alimuua yule Muislamu kwa sababu kwanza alikuwa a n a f a n ya m a s i h a r a ya kusilimu. Alimpiga Usama (RA) upanga. Habari hii alipoisikia Mtume (SAW) alikasirika na alimgomba Usama (RA) na alimuuliza jee ulimuua mtu baada ya kutoa shahada na alimlipia jizya, fidia. Katika riwaya nyengine alimuuliza Usama,

Inaendelea Uk. 16

‘Jihad’ kuangamiza Waislam Somalia na siasa za Zanzibar

Inatoka Uk. 11

ni Serikali iliyotokana na wananchi wenyewe wa Somalia baada ya Jumuiya ya Kimataifa kushindwa kuleta amani Somalia kama miafaka i l i y o s h i r i k i s h a wa t u kutoka nje ya Zanzibar ilivyokwama.

Wa l i p o f e l i . N d i o w a k a v a m i a k i j e s h i . Wakaitumia Ethiopia ikavamia ikaangusha Serikali ya Umoja wa Mahakama za Kiislamu. L i l i p o t o k e a h i l o , Wasomali wakagawika kama ambavyo hivi sasa Wazanzibari wanataka kugawika kuondoa Sera ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Kundi likaenda Nairobi kuunda Serikali inayotakiwa na mabeberu na kundi likabaki Somalia na kuibuka Al-Shabaab.

Hawa waliounda Serikali ya Mpito, walikuwa wale wale waliokuwa viongozi wa Serikali ya Umoja wa Mahakama za Kiislamu. Na hawa Al-Shabaab, vile vile ni katika waliokuwa k a t i k a U m o j a w a Mahakama za Kiislamu. Ukichukulia mahesabu mepesi kuwa hawa walio serikalini wameritadi, ni

wanafiki, ni makafiri, hapo ndio tunapokosea. Wale bado ni Wasomali, kama ambavyo Al-Shabaab ni

Wasomali. Wakipigana n i W a s o m a l i k w a Wasomali wanaopigana. N i W a z a n z i b a r i ,

wahafidhina wasiotaka Serikali ya Umoja wa Kitaifa, wanaopigana na wanaotaka maridhiano.

M s h i n d i k a t i k a v i t a hiyo nani? Hakuna na k u t a k u w a h a k u n a wakiendelea hivyo. Kile alichoeleza Mzee Nassoro Moyo kilichofanyika kabla na baada ya uchaguzi mkuu Zanzibar, ndicho p e k e e c h a k u w a p a Wazanzibari ushindi na ndicho pekee cha kuwapa ushindi Wasomali, kama u t a z u n g u m z a k w a mtizamo wa kisiasa au kidini. Na ndio Uislamu na Qur’an inavyoagiza, mnapogombana ndugu, W a z a n z i b a r i k w a Wazanzibari, Wasomali kwa Wasomali, Waislamu kwa Waislamu, haijalishi kama kundi moja litawaita wengine wanafiki au makafiri, bado sumu ya kutengana, kufarakana na kugombana wenyewe kwa wenyewe itawatafuna. Na maadui wataingia kusaidia pande zote mzidi kutafunana. Al-Shabaab hawana kiwanda cha silaha. Kinachowafanya wasipungukiwe na silaha ni nini?

Wiki iliyopita niligusia na kutoa ushahidi kuwa silaha zinazotolewa na Umoja wa Mataifa pamoja na zile zinazotolewa na

BAADHI ya wananchi wa Somalia walioathiriwa na vita vinavyoendelea nchini humo. Inaendelea Uk. 16

Page 14: ANNUUR 1173.pdf

14 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

Na Ben Rijal

Na Ben Rijal

Mchango wa Waislmau katika maendeleo ya Dunia

ABUU Mussa Jabir Ibn Hayyan ni katika ya wasomi waliokuja kupata msukusuko wa kufungwa kifungo cha nyumbani na babake naye kuuliwa na watawala. Kati ya wasomi wa siku hizo waliokumbana na mateso kutokana na viongozi huwezi kusoma bila ya kutajwa Jabir Ibn Hayyan.

J a b i r I b n H a y y a n katika midani za Ulaya anajulikana kwa jina la Geber, amezaliwa katika mji wa Tus uliopo Iran katika mwaka wa 721 na wengine husema kuwa amezaliwa mwaka wa 722. Uasili wake haufahamiki wengine wanafahamisha kuwa ni Mfursi na wengine wanatueleza kuwa ni Mwarabu mwenye asili ya Yemen.

Baba yake Hayyan al Azdi alikuwa ni mfamasia mjuzi wa uchanganyishaji wa madawa na muungaji m k o n o m k u b wa wa uongozi wa Banu Abass dhidi ya uongozi wa Banu Umayya wakati akiishi katika mji wa Tus nchini Iran. Kutokna na misimamo yake hio, alikamatwa na kuuliwa tukio hi lo l ikai fanya familia yake kuhama Tus na kuhamia Yemen na hapa ndipo utatanishi unapokuja juu ya asili ya Jabir bin Hayyan wengine husema ni Muarabu na wengine husema kuwa ni Mfursi.

Baada ya kukaa Yemen na familia yake, msomi huyu alirudi Kufa na akasoma kwa Imam Jafer al Sadiq na alipomaliza masomo yake akawa anafanya kazi ya utabibu wakati wa zama za Khalifa Harun al Rashid. Katika kuwa karibu na wakubwa sio mara zote mtu hubakia katika hali ya kukubalika

Abu Mussa Jabir bin Hayyan

Mchoro unaomuonyesha J a b i r n a v y o m b o alivyokuwa akivitumia

Leo Ijumaa Tarehe 27 Jumada-at-Thania 1436 AH yaani mfungo Tisa, tarehe April 17, 2015.

Tutaangalia kuandama kwa mwezi wa Rajabu tarehe April 19, 2015.

Tutaangalia kuandama kwa mwezi wa Shabana tarehe May 18, 2015.

Tutaangalia kuandama k w a m w e z i w a Ramadhani tarehe June 17, 2015.

Kutoka leo I jumaa tarehe 17 April hadi kufika Ramadhani tumebakisha siku 61.

Fatilia kuandama kwa MweziM w e z i u t a z a l i w a

ta rehe 16 June 2015 saa 11:05 za jioni, Juni 16 hautoonekna mwezi popote pale Duniani na tarehe 17 utaonekana kwa taklifu katika maeneo ya Kusini-Mashariki ya Asia, Kaskazini mwa Afrika, Australia na Indonesia lakini utaonekana kwa urahisi katika maeneo ya Afrika Mashariki na sehemu mbalimbali za Bara la Afrika. Ramadhani Mosi itakuwa tarehe 18 Juni, 2015.

Abu Mussa Jabir bin Hayyan-(7)moja kwa moja kwani alipofariki Khalifa Harun al Rashid katika mwaka wa 815, Jabir bin Hayyan alikamatwa na kutumia maisha yake yote yaliobaki kuwa katika kifungo cha nyumbani ikimaanisha kuwa hakuwa na ruksa ya kutoka nje ya nyumbani kwake.

Somo la Kemia likiwa na mchanganyiko wa mambo ya kiroho (alchamey) ndio alipozama sana na alikuwa mcha Mungu na kila akikaa alikuwa akifanya tafiti alizokuwa anaziunganisha na imani yake ya dini kwani aliathirika sana na mwalimu wake Imam Jafar al-Sadiq.

Kila somo huwa na muanzi l ishi wake na kuelezewa kuwa fulani ni baba wa somo hilo (father of …) Jabir Ibn Hayyan husemwa kuwa yeye ndio baba wa somo la Kemia kutokanana kazi zake nyingi alizozifanza na kugundua mambo mbalimbali katika uga wa kemia. Mbali na somo la kemia Jabir Ibn Hayyan alizama katika somo la nyota, ufamasia, udaktari, f a l s a f a n a u h a n d i s i . I n a f a h a m i k a k u w a utaalamu wake wa somo la kemia ndio uliokuja k u w a p a m w o n g o z o Priestly na Lavoisier katika karne ya 18 kwenye uwanja wa kemia.

J a b i r I b n H a y y a n aliweza kugundua aina ya vitu 19 katika uwanja wa kemia na kwa kisasa vitu hivyo vimepewa jina la “element”.

J a b i r I b n H a y y a n anae lezewa kama n i mtu mmoja wa mwanzo a l i o a n z a k u f a n y a majaribio katika somo la kemia, akifanya majaribio ya kugeuza aina moja ya kiungo cha maji maji na kukileta katika aina nyengine. Aidha alikuwa akifanya majaribio ya kuangalia aina ya vitu vinavyokuwa vigumu kisha vikawa kidogokidogo vinabadilika na kuwa na umaji maji. Katika majaribio hayo aliweza kugundua aina ya tindikali ijulikanayo kwa jina la acetic acid na kuweza kufahamu kuwa siki nayo ina maumbile ya tindikali, akenda mbali zaidi pale alipoweza kuitengeneza t indikal i i ju l ikanayo kama hydrochloric acid, akaja kugundua tindi kali

ijulikanayo ‘regia” yenye uwezo wa kuyayusha d h a h a b u , a k a i p a t a tindi kali ya citric acid kutokana na ndimu na jamii ya miti hiyo kama machungwa na kugundua aina ya tindikali ya tartaric acid inayopatikana na mabaki yaliotengenezewa pombe ya wine. Kazi hizi alizozifanya zilikubalika na kuelezewa kuwa ni

mafanikio makubwa ya somo la kemia zaidi ya miaka alfu iliopita.

J a b i r I b n H a y y a n alivigawa vitu katika m a k u n d i m a t a t u a l i p o k u wa a n a f a n ya m a j a r i b i o . K u n d i l a kwanza akaliita kundi la spiriti ambalo vitu vyake ukivipasha moto hupotea kwa mvuke ikijumuisha s u l f u r , a m m o n i u m chloride na kundi la pili akalita la metali ikiwemo shaba, dhahabu, vyuma na fedha na kundi la mwisho ni vitu ambavyo havimo katika kundi la vyuma na dhahabu mfano wa jabali, mkaa n.k. Mgao huu ndio ukaja kutumiwa katika mgao wa vitu vya metali na visio vya metali.

Kuzama kwake katika sayans i na u juz i wa k e m i a k u l i m s u k u m a kuchanganya na masuala ya k i r o h o . A l i k u wa a k i p e n d a k u f a n y a majaribio ya kila aina. Aliweza kutengeneza aina ya karatasi ambayo ukiichoma kwa kibiriti haiwaki. Na akatengeneza a ina ya wino ambao unaweza kusoma ndani ya giza. Katika vyombo alivyokuwa akivitumia katika majaribio ni aina ya chombo kijulikancho “retort”, pipette ya kuvutia vitu vya maji kujuwa k i wa n g o u k i t a k a c h o kuchanganya na kichupa kidogo cha kuchanganyia v i tu ( tes t tube) v i tu ambavyo vinatumika hadi sasa katika maabara yote duniani.

J a b i r I b n H a y y a n alimtangulia Muingereza ambaye naye alikuwa gwiji wa somo la kemia na John Dalton ambaye a n a z u n g u m z wa k wa mapana na marefu na Jabir

Ibn Hayyan kwa upande wake anazungumzwa kwenye historia tu.

Nyingi ya kazi kazi zake takriban akiziandika kwa njia ya alama na ilikuwa sio rahisi kuzifahamu ndipo j ina lake Jabir likafananishwa na kazi zake na kui twa kwa Kizungu “gibberish”

Alikwenda mbali katika kuvijua vitu na uasili wake na hapa akavigawa vitu kutokana na ujoto wake, ubaridi wake, ukavu wake pamoja na hali ya unyevu. Akaona moto kuwa una sifa ya moto na ukavu, dunia na udongo ukiwa upo katika hali ya ubaridi na joto wakati maji yakiwa katika hali ya ubaridi na unyevu na hewa kuwa ina joto na unyevu.

J a b i r I b n H a y y a n i n a e l e z e w a k u w a al iandika vi tabu 112 kwa kumtunuku Khalifa Harun al-Rashid pamoja na kutengeneza Jadwedi ya Emerald. Kati ya vitabu hivyo, vitabu 70 ambavyo vingi yake vilitafsiriwa katika lugha ya Latino, moja ya kitabu hicho ni Kitan al-Zuhra mambo ya kupiga bao na kuagua. Kitab al-Ahjar hichi sio kinazungumzia juu ya mawe ila kilikwenda mbali sana kuyasarfi mambo ya kiroho.

Kazi za Jabir Ibn Hayyan z i l i zo fanyiwa ta f s i r i katika karne ya 20 kwa Kiiengereza ni pamoja na The Arabic Works of Jabir ibn Hayyan kimetafsiriwa na Richard Russel in 1678. New York, E. P. Dutton (1928); vilevile na Paris, P. Geuther. Tafsiri nyengine ya kazi yake ni Syed Nomanul Haq, Names, Natures and Things : The Alchemists Jabir ibn Hayyan and his Kitab al-Ahjar (Book of Stones), [Boston Studies in the Philosophy of Science p. 158] (Dordrecht: Kluwer Academic Publishers, 1994). Kuna na kazi nyengine iliyotafsiriwa juu ya alchemy ikiwa: * Donald R. Hill, 'The Literature of Arabic Alchemy' in Religion: Learning and Science in the Abbasid Period, ed. by M.J .L. Young, J.D. Latham and R.B. Serjeant (Cambridge University Press, 1990) pp. 328-341, esp. pp 333-5. Katika kazi ya karibuni kabisa ni hii: * William Newman, New Light on the Identity of Geber, Sudhoffs Archiv, 1985, Vol.69, pp. 76-90.

Page 15: ANNUUR 1173.pdf

15 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

UWANJA WA VIJANA-JIONGEZEE MAARIFA

CHEMSHA BONGO

MAJIBUCHEMSHA BONGO NO: 1Weka duara kwenye jawabu ilio sawa, jawabu kamili

wiki ijayo.1. Surah ilikyokuwa refu ina aya ngapi? Baqara Aya

2862. Surah gani imeanza bila ya tamko Bismilahi

Rahman Rahim.3. Surah za Makka ni ……..854. Surah za Madinah ………….295. Wakusanyaji hadithi wawili mashhuri ni: Bukhari

na Muslim, 6. M t u m e S AW a l i k u wa n a u m r i g a n i

alipoteremshiwa Wahyi na Jibril? Miaka 407. Mke wa mwanzo wa Bwana Mtume SAW ni Bibi

Khadija8. Hijra ya mwanzo Waislamu walikwenda wapi?

Ethopia9. Safari ya Mtume SAW kutoka Duniani kwenda

Mbinguni inaitwa: Miraj10. Mtume SAW alifwatana na nani alipohama

Makka kwenda Madinah? Syd Abubakar

:25, Surah Al-Baqara: 74, Surah Al-Baqara: 249, Surah Al-Baqara: 266, Surah Al-Imran: 15, Surah Al-Imran: 136, Surah Al-Imran: 195, Surah Al-Imran: 198, Surah An-Nisaa’: 13, Surah An-Nisaa’: 57, Surah An-Nisaa’: 122, Surah Al-Maaida: 12, Surah Al-Maaida: 85, Surah Al-Maaida: 119, Surah Al-Anaam: 6, Surah Al-Aaraf: 43, Surah At-Tawba: 72, Surah At-Tawba: 89, Surah At-Tawba: 100, . Surah Yunus: 9, Surah Ar-Raa‘d: 3, Surah Ar-Raa‘d: 17, Surah Ar-Raa‘d: 35, Surah Ibrahim: 23, Surah Ibrahim: 32, Surah An-Nahl: 15, Surah An-Nahl: 31, Surah Al-Israa’: 90, Surah Al-Israa’: 91, Surah Al-Kahf: 31, Surah Al-Kahf: 33, Surah Ta Ha: 76, Surah Al-Hajj: 14, Surah Al-Hajj: 23, Surah Al-Furqan: 10, Surah An-Naml: 61, Surah Al-A‘Ankabut: 58, Surah Az-Zumar: 20, Surah Az-Zukhruf: 51, Surah Muhammad: 12, Surah Muhammad: 15, Surah Al-Fath: 4, Surah Al-Fath: 5, . Surah Al-Fath: 17, Surah Al-Qamar: 54, Surah Al-Hadid: 12, Surah Al-Mujadala: 22, Surah As-Saff : 12, Surah At-Taghabun: 9, Surah At-Talaq: 11, Surah At-Tahrim: 8, Surah Al-Buruj: 11, Surah Al-Bayyina: 8.

T u k i a n g a l i a k u n a aya nyingi katika Qur’an zinazoelezea juu ya maji iwe ya bahari, mito, mvua katika Surah mbalimbali.

Sehemu ya kiwililiwili c h e t u h u c h u k u a e n e o kubwa la maji iwe mate, damu na sehemu ambazo zinajiunga. Asilimia 75 ya kiwiliwili cha mwanadamu kimetengenezwa na maji na maji husaidia kuratibu hali ya joto kwenye kiwiliwili kwa kutokwa na jasho. Maji ni sehemu muhimu sana kwa maisha ya mwanadamu, atapokosa mtu maji kunywa kwa siku chache mtu huyo atapoteza maisha.

Kilimo chetu kinategemea maji zaidi na bila ya maji miti itatoweka na maisha kumalizika. Sayari yetu hii inakalika na kuendelea kuwa na viumbe mbalimbali kutokana na kuwepo kwa maji. Uislamu umezungumzia kwa mapana suala la maji na namna ya kuyahifadhi. Misiki t i mingi duniani imejengwa kwenye maeneo ambayo hupatikana kwa maji kirahisi. Qur’an inaeleza katika Suratul Anbiyaa:

“Je! Hao walio kufuru h a w a k u o n a k w a m b a mbingu na ardhi zilikuwa z i m e a m b a t a n a , k i s h a S i s i t u k a z i b a b a n d u a ? Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini?” (21:30).

Qur’an inatueleza kuwa maisha yanategemea maji na viumbe vyote vilivyohai

Uislamu, maji na mazingiraNa Ben Rijal

Maji kwenye maporomoko

vimeumbwa kutokana na maji. “Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini? (21:30).”

U n a p a t a u z i n g a t i i f u mkubwa unaposoma aya hizi kuona kuwa Mtume SAW katufahamisha zadi ya miaka 1400 kupitia Qur’an juu ya somo la uhai (Biology) kuwa viumbe vyote vimeumbwa kutokana na maji na viumbe hao hutegemea maji kwa maisha yao.

Katika Suratul An Naml tunaelezwa juu ya maji yanavyopatikana.

“AU NANI yule aliye ziumba mbingu na ardhi, na akakuteremshieni maji kutoka mbinguni, na kwa hayo tukaziotesha bustani zenye kupendeza? Nyinyi hamna uwezo wa kuiotesha miti yake. Je! Yupo Mungu p a m o j a n a M w e n y e z i Mungu? Bali hao ni watu walio potoka.” (27:60)

Hakika maji ni tunzo kwa mwanadamu kutoka kwa Mola wetu na tunatakiwa tusiyachafue. Maji siku zote hutakiwa yawe hayana rangi, harufu na ladha iliokuwa mbaya na hayatakiwi kuwa na nyongeza za kemikali katika kuyatumia kufanyia ibada iwe kutia udhu au kukoga janaba na nifasi.

Bahati mbaya duniani kote hivi sasa maji ambayo ni tunzo tuliotunikiwa na Mola wetu yanachafuliwa pakubwa na kupelekea matumizi makubwa ya maji ya chupa yakiwa ndio maji yalio safi na salama. Huko nyuma hakukuwa na mtindo wa kunywa maji ya chupa na haya maji ya chupa yanachangia kwa upande mwengine matatizo ya mazingira hasa kwa nchi zinazoendelea kutokana na kushindwa kuzirejeza (recycling) na matokeo yake kuzagaa kila mwahali.

Mito, maziwa na bahari zote z imechaful iwa na uchafu, maradhi kama ya kichocho na tai fodi

yanachangiwa kutokana na maj i machafu. Maj i yaliotuwama kuyachafua ni hatari sana kwa afya zetu, zaidi ya miaka 1,400 Mtume SAW amekataza kunywa au kukoga katika maji yalio machafu na akakataza kwenda haja ndogo na kubwa karibu na vianzo vya maji. Aidha kakataza kutupa uchafu katika maji yaliotuwama.

Katika Suratul Al-Arraf, Quran inasisitiza pakubwa juu ya uhifadhi kwa kusema “wala msifanye uharibifu katika nchi.” Hii ni uhifadhi wa mtizamo wa Mazingira.

Na kwa watu wa Madyana t u l i m t u m a n d u g u ya o Shua'ib. Akasema:

“ E n y i wa t u wa n g u ! M u a b u d u n i M we n ye z i Mungu. Hamna mungu mwengine isipo kuwa Yeye. Imekwisha kufikieni hoja wazi kutoka kwa Mola Mlezi wenu. Basi timizeni sawasawa vipimo na mizani, wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye uharibifu katika nchi, baada ya kuwa imekwisha tengenea. Hivi ndivyo bora kwenu ikiwa nyinyi ni Waumini.” (7:85)

Juu ya uf i sadi Mola anatufahamisha kuwa wale wenye kufisidi basi yeye Mola hapendi ufisadi uwe kwa mimea au viumbe. Hii ndio ile dhana nzima ya uhifadhi na maendeleo endelevu.

“Na anapo tawala hufanya juhudi katika nchi kwa kufisidi humo na kuteketeza mimea na v iumbe. Na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi.” (2:20)

Uislamu umejengeka zadi katika uhifadhi na Waislamu wanatakiwa kujifunza zaidi kuelewa mchango wao katika kuiweka dunia katika utulivu wa kimaumbile na utulivu wa imani.

Makala ijayo nitaangalia juu ya maj i na dunia tulionayo.

KATIKA makala mbili nitayazungumzia aina ya maji yaliotajwa katika Qur’an na makala ya pili itakuwa ni Maji na Mazingira.

Qur’an ni kitabu cha uwongofu kwa Waislamu na walimwengu kimeweka wazi suala zima la maisha na maumbile. Imefika wataalamu wengine wamefika kuwa na Maabara ya kufanya utafiti juu ya aya zilizokuwemo kat ika Qu’ran ( I s lamic laboratory) na kuweza kuzifanyia chambuzi za kila aina pamoja na kuzifanyia

kazi. Aya zielezao juu ya

maji ni: 47:15, 56:31, 56:68, 77:27 na 88:17 aidha aya 25:53, 27:61, 35:12, 55:19 na 55:21 zina maelezo ya bahari zinapoungana, aya zinazoelezea juu ya mvua 2:163, 2:265, 6:99, 7:57, 8:11, 10:24, 13:17, 14:32, 15:22, 16:65, 18:45, 20:53, 22:5, 22:63, 23:18, 24:43, 25:48, 27:60, 29:63, 30:24, 30:48, 31:10, 31:34, 32:27, 35:27, 39:21, 40:13, 41:39, 42:28, 42:33, 43:11, 45:5, 46:24, 50:9, 56:69, 57:20, 78:14, 80:25

Aya zinazoelezea juu ya Mito ni: Surah Al-Baqara

Page 16: ANNUUR 1173.pdf

16 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

Haki za Waislamu na mipaka ya JihadInatoka Uk. 13utaifanyaje Laailaha illa Llahu itakapokujia akhera.

(Nimefupisha maneno ya kisa halisi). Muttafaq .(Riyadh Salihyn mlango wa 49 hadithi ya 3-5)

Fikiria wewe mwenyewe jinsi tunavyoyachukulia mambo kirahisi, kwa kutaka kuwahukumu watu, lakini Mtume (SAW) hakuwa hivi tulivyo sisi. Akikosea Muislamu jambo dogo, tayari kafiri auliwe, wakati undani wake hatuujui wala hatutakiwi kuwahukumu watu ila tuwachukulie kwa dhahiri tu.

Vita vina taratibu zake na miiko yake. Jee vita hivi vya sasa ambavyo vinapiganwa kwa kisingizio cha kuleta dola za Kiislamu kweli vinafuata taratibu za Jihadi?

Amesimulia Abdillahi bn Umar (RA) amesema a l i k u t w a m w a n a m k e ameuawa katika vita, Mtume (SAW) akakataza kuuliwa wa n a wa k e n a wa t o t o .(SM1744 SB3014).

Amesema Imam Nawawy katika sherhe ya hadithi hii “Wamekubaliana Maulamaa wote kuifanyia kazi hadithi hii kwa kuharamisha kuuliwa wanawake na watoto (wa makafiri) ikiwa hawapigani.” (Sherhe ya Imama Nawawy

ya sahihi Muslim).Sasa wewe unaambiwa

Al Shabaab wameingia Garissa wameuwa watoto wa shule 150, unasema hiyo ni Jihad! Wameingia Wetgate Shopping Mall, Nairobi, wameuwa wanawake na watoto, unasema hiyo ni Jihad. Unaweza kusema kuwa wamesingiziwa. Ukisema hivyo, lazima ukubali kuwa jina hilo Al-Shabaab hivi sasa linatumika kama jinamizi la kuupiga vita Uislamu. Kwa hiyo wewe kushabikia Jihad ya Al Shabaab ni kutilia nguvu propaganda hiyo.

Hawa waliokatazwa kuuliwa katika Hadithi tuliyoinukuu, ni watoto na wanawake wa makafiri. Jee, vita hivi vya harakati za ukombozi hawauawi wanawake na watoto wa Kiislamu? Linapopigwa bomu Somalia kuwalenga askari wa Somalia (Waislamu) wakiwa mitaani, litachagua wanawake wapita njia na watoto? Kama wanauawa, basi harakati hizi zina kasoro katika aqida zake na pia zinakosa fiqhi sahihi ya jihadi badala yake zinatawaliwa na hamasa na katika hali hii inaupelekea kufikiri kwamba huenda wasioutakia mema Uislamu wameziteka harakati

hizi kwa faida yao na kwa hivyo tuzitizame harakati hizi kwa macho ya tahadhari badala ya kuzikumbatia na kuzishabikia.

Hoja kubwa inayotolewa kuhalalisha mapambano ya kumwaga damu ni kwamba wasiohukumu kwa kitabu cha

Allah (SW) ni makafiri. Kwa hivyo ni halali kupambana nao hata ukiwaua. Katika hoja hii nasema hivi kila aya imetafsiriwa na Masahaba kwa hivyo si vizuri mtu kutafsiri apendavyo.

Nitafafanua kwa kirefu hoja hii Inshaallah toleo lijalo

‘Jihad’ kuangamiza Waislam Somalia na siasa za Zanzibar

Inatoka Uk. 13Marekani, ndio hizo hizo wanazotumia Al-Shabaab. Kwa maana kuwa mchezo unaofanyika hivi sasa ni kuwapa silaha wote wawili wamalizane wenyewe kwa wenyewe.

Huko nyuma tuliwahi pia kueleza kuwa wapo makamanda wa AMISOM na wa Jeshi la Uganda ambao walikamatwa kwa kuwauzia Al-Shabaab silaha. Japo habari hiyo inapozwa na kufanywa kuwa ni ufisadi tu na njaa ya askari hao, lakini ukweli ni kuwa X anayewapa silaha Serikali ya Somalia, ndiye huyo huyo anayewapa Al-Shabaab.

Huko nyuma ilikuwa Al-Shabaab ikipata misaada pengine kupitia nchi ya tatu ya Kiislamu kama labda Qatar/Saudi Arabia. Kwa hiyo wenyewe wanadhani wanapata msaada kutoka k wa r a f i k i M u i s l a m u . Lakini kwa siasa za Qatar, Saudia Arabia na j ins i zinavyotumiwa na mabeberu katika suala la Palestina, Syria, zilivyotumika kuipiga Afghanistan, Iraq na Libya, ni mambo ambayo tulitakiwa t u t a f a k a r i k w a k i n a . Tizama leo zinavyotumika k u w a s a m b a r a t i s h a

Wayemen! Utasema Saudia, Qatar na Misri zinapigana Jihad, Yemen?

Kuna mambo mawili ya kutizama katika siasa za Somalia. Wale walioungana w a k a u n d a U m o j a w a Mahakama za Kiislamu, awali walikuwa katika makundi mbalimbali yaliyokuwa yakipingana. Inawezekana katika kuungana kule, kuna waliokuwa na nia thabiti ya kutaka Uislamu na kuna waliokuwa na nia ya kupata maslahi binafsi. Na ndio maana wakakimbilia Nairobi kuunda serikali uhamishoni baada ya kuona watapata nguvu ya Marekani na wababe wengine.

Ukiitizama Somalia ilivyo, Al-Shabaab walioshika silaha ni sehemu ndogo sana ya wananchi. Wapo Waislamu wengi ambao hawakubaliani na sera za Al-Shabaab walio katika makundi ya Twarika m b a l i m b a l i . N a h a wa ndio wenye watu wengi

zaidi. Ni kama unavyoona leo hapa kwetu . Watu wataona katika TV watu sehemu mbalimbali duniani wanaswali, lakini watasubiri swala waliyotangaziwa na Sheikh Alhad au Mufti wa Bakwata. Sasa ukisema kuwa namna ya kuwafanya hawa wafuate Kitabu na Sunna, na waswali unayoita wewe Idd ya Kimataifa, ni kuwashikia AK-47, utauwa Waislamu wangapi mpaka hilo litimie? Lazima ukubali kuwa hapo kuna tatizo la ujinga wa muda mrefu na ukosefu wa elimu. Na ujinga hauondolewi kwa mtutu wa bunduki, wala mabadiliko ya kijamii na kiimani hayaji kwa kufumba na kufumbua kwamba unashika silaha ghafla Jihad imewafanya Waislamu safi wa kuhukumu kwa Kitabu na Sunnah.

Huwezi kuwaita wale wazee na vijana wa Kisomali walio katika twarika za Ahlu Sunna Wal Jamaa, kuwa

sio Waislamu na kwamba namna ya kuwaelimesha wakubali Dola ya Kiislamu ni kuwaletea ‘Al-Shabaab’ kutoka Zanzibar au Tanga.

Ukisema kuwa Somalia kuna ‘Civil War’, maana yake ni kuwa Wasomali waliopo serikalini si watu kutoka Kenya au Uganda na Burundi. Ni Wasomali. Al-Shabaab, si Mujahidina kutoka Arusha wala Mwanza. Ni Wasomali. Wanapigana na kuuwana Wa s o m a l i . S a s a k a m a wewe utamuita mwingine Al-Shabaab mujahidina na mwingine umkufurishe, bado atabaki kuwa Msomali na bado atakuwa Muislamu. Ni Wasomali wanauwana wenyewe kwa wenyewe. Ni Waislamu wanauwana wenyewe kwa wenyewe, kama ambavyo wanaouwana Syria, Iraq, Libya na Yemen, ni Waislamu kwa Waislamu. Ni Waarabu kwa Waarabu.

K a t i k a s u a l a l a Mahakama ya Kadhi juzi

Bungeni, wale CCM wote Bara Wakristo waliokuwa na CCM Zanzibar na CC Waislamu Bara, katika suala la Katiba Inayopendekezwa, waliwatema CCM wenzao Waislamu. Wakaungana na Wakristo NCCR, Wakristo CUF, Wakristo CHADEMA na wengine kupinga. Katika suala hili walisimama kama Wabunge Wakristo, sio CCM au Wapinzani. Wakafanikiwa kuzuiya mpango wa serikali kuleta Muswada wa Sheria ya Mahakama ya Kadhi.

Kama lipo la kuwasaidia Wazanzibari, ni kuwasaidia wajitambue kuwa wao ni Wazanzibari kabla ya kuwa CCM na CUF. Kama lipo la kuwasaidia Wasomali, ni kuwafanya wajitambue kuwa wao ni Waislamu ni Wasomali. Wajue kuwa Mabeberu wanaoisaidia serikali kibaraka, sio kwamba wanawapenda Wasomali hao waliopo serikalini. Mabeberu hao ni maadui wa Wasomali wote, wanaotaka Dola ya Kiislamu na wasiotaka.

Sasa wewe ukimuona M s o m a l i m w e n z a k o , Muislamu mwenzako kuwa ni adui yako, ni ujinga tu ambao utazidi kumpa nguvu adui yenu awabamize kwa k u t u m i a m i k o n o ye n u wenyewe.

kwa kuonesha tafsiri ya aya hii sababu ya kuteremsha na maoni ya Maulamaa katika hukmu ya viongozi Wislamu wasioongoza kwa Sheria za Kiislamu.

Wabillahi tawfiiq.(Itaendelea toleo lijalo

Inshaallah kwa yale masuala ambayo bado sijayajibu.

WAPIGANAJI wa Al-Shabaab wa Somalia.

Page 17: ANNUUR 1173.pdf

17 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

MAKALA

Saudia soko muhimu la silaha za MarekaniInatoka Uk. 9wa majeshi ya nchi za Kiarabu, unaoongozwa na Saudi Arabia.

Wakazi wa kijiji hicho cha Okash, kilicho karibu na kambi ya jeshi la anga ya Jabal Shouaib, walinukuliwa wakisema familia iliyouawa ilikuwa na wanaume wawili, mwanamke mmoja , na watoto sita. Shirika la habari la Yemen la Sabaa, limetuma picha za familia hiyo kwenye mtandao wake. Bila shaka h a o w o t e n a we n g i n e wanaoendela kupoteza maisha ni Waislamu. Kisa ni tofauti tu ya kimadhehebu, tena inayochochewa na makafir kwa maslahi yao.

Kwa ujumla tunachoweza k u s e m a n i k w a m b a kinachodhidiri hivi sasa katika mzozo wa Yemen hata Syr ia na I raq , n i m a t u m i z i m a z u r i y a mkakati wa kufarakanisha ndugu na anayefarakanisha akizidi kuweka mazingira ya kuneemeka kiuchumi huku waliofarakanishwa wakijiangamiza wenyewe. F a r a k a y a U s h i a n a Usunni iliyopenyenyezwa inawatafuna Waarabu na Waislamu kwa ujumla. Saudi Arabia inaongoza Kundi la mataifa yenye Waislamu

wengi wa Sunni katika eneo hilo la Mashariki ya Kati katika mapambano na makundi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia yanayosaka mabadiliko ya kiutawala katika nchi zao au kupinga himaya ya Kisuni katika nchi zao.

Hilo limesababisha kile kinachoonekana kuwa ni vita vya kimadhehebu. Hivi sasa tunashuhudia raia wa Yemen ambao wengi ni Shia, wakiunda kikundi cha wanamgambo wa Huthi,

ambao ni wapiganaji wa Kiislamu wa dhehebu la Shia, kuukabili utawala wa Rais Hadi, ambaye wananchi hao hawamtaki walkiamini kuwa ni kibaraka wa Saudi Arabia (Sunni) na mataifa ya magharibi yanayounga mkono Sunni. Hivi sasa Rais Had, yupo mafichoni Saudia akipata hifadhi ya nchi hiyo. Nayo Saudia inapambana kumrejesha swahiba wao, ambaye anasimamia maslahi yao. Yemen ni ta i fa la Kiarabu lililopo jirani na

Saudi Arabia, taifa hili lina Waislamu wengi wa dhehebu ya Shia, tofauti na Saudi Arabia ambayo ina Wais lamu wengi wa dhehebu la Sunni. Umekuwa ni msimamo wa Saudi Arabia pale, ilipoahidi kuwa itaendelea kufanya mashambulizi makali dhidi ya raia wa Yemen mpaka wasalimu a m r i n a k u m k u b a l i R a i s H a d i , a m b a y e raia hao hawamtaki na ameshakimbia nchi.

Lakini kwa Saudia kuendelea kuua Waislamu wa Yemen kwa kutumia hazina yake ya silaha k u t o k a M a r e k a n i , n i wa z i k wa m b a n i kicheko kwa Marekani ambayo itajihakikishia kuongezewa kandarasi ya kuuza silaha zaidi kwa Taifa hilo. Hii ni kutokana na ukweli kwamba tayari kuna mahali pa kuzitumia s i l a h a h i z o h i v y o mahitaji yake yatazidi kuongoezeka.

Katika mashambulizi h a y a S a u d i A r a b i a inaungwa mkono na Israel na Marekani. Bila shaka ile falsafa ya Marekani ya wagawe, watawale ufaidikie kiuchukumi, i m e c h u k u a n a f a s i yake. Kwa kuwa silaha zilizokuwa zimerundikwa kwa muda mrefu sasa zimepata matumizi, bila shaka watumiaji watumia fursa iliyojitokeza kuagiza zaidi ili hazina isipungue. Na ni wakati huo ambapo soko la silaha za Marekani linapanuka zaidi.

Kwa mtindo huu kwanini Waarabu, ambao ni ndugu wa Kiislamu wasiendelee kufarakanishwa hadi pale watakapotahayari?

H A I N A m a s h a k a yoyote kuwa vyakula na vinywaji vinavyotokana na nafaka vinanoga! Au unasemaje kuhusu wali mweupe, pilau, b i r i a n i ? N a b a d o hapo hujagusia chips, chapati , kitumbua, andazi, na bajia! Mhh kule kuna soda, juisi, ice cream, pipi n.k. We wacha tu!

Mpaka siku mbili tatu zilizopita sikuwa na shaka yoyote ile kuhusu ubaya wa kubugia kwa wingi vyakula vya nafaka. Tukumbuke kwamba sukari, - yule adui namba moja wa afya, chimbuko lake ni nafaka! Nilijua, na naamini wengi wetu tunajua, kuwa sukari ni miongoni mwa vyakula vikuu vinavyosababisha mfuro (inflammation) na kwamba mfuro ni moja ya vyanzo vikuu vya maradhi ya kimfumo ndani ya mwili.

N i l i j u a k u w a chimbuko la nafaka kusababisha mfuro ni

Tunajimaliza wenyewe kwa ulaji huuNa Juma Kilaghai

sukari aina ya fructose ambayo au tayari ipo, au inakuwa ni moja ya mazao wakati nafaka inapochakatwa ndani ya miili yetu. Watafiti w a n a s e m a k u w a Fructose huchochea seli za mwili kuchoma nishati (ATP) iliyohifadhiwa humo kwa kas i ya kutisha na matokeo yake seli husika hukumbwa na 'shock'! Shock hii hupelekea vinasaba (DNA) katika hizi seli kusambaratika! Watafiti hawa wanaongeza kuwa DNA iliyosambaratika hujiunda katika kemikali zinazojulikana kama purines, ambazo nazo huishia kujiunda kuwa tindilkali ya urea, yaani uric acid! Tindikali ya urea husababisha seli za mwili kukumbwa na mfuro, huharibu mifupa laini inayounganisha v iungo vya mwi l i , husababisha mishipa ya damu kukumbwa

na mkakamo (haikubali k u p a n u k a w a l a kus inyaa) , k i tendo ambacho huleta maradhi ya mfumo wa mzunguko wa damu, nakadhalika.

K w a u p a n d e mwingine nilijua kuwa glucose (sukari ingine inayopat ikana kwa wingi kwenye nafaka na sukari ya mezani) inaweza kuleta shida kwenye ini, inaweza ikasababisha unene u l i o p e a , i n a w e z a kuchochea kisukari cha ukubwani, na pia kuwa ni chakula kikuu cha seli za saratani. Kitu ambacho sikukijua ni kwamba glucose pia ni chanzo kikubwa sana cha mfuro ndani ya mwili!

Kwa mujibu wa tafiti, Uchakataji wa glucose huzal isha kemikal i inayoitwa malonyl-c o A . M a l o n y l - c o A

hupunguza kwa kiasi kikubwa uwezo wa mitochondria (viwanda vya kuzalisha nishati vilivyomo ndani ya seli) kudhibiti chembe c h e m b e z i l i z o b e b a u m e m e h a s i ( h i g h e n e r g y e l e c t r o n s ) zinazotumika wakati wa uzalishaji wa nishati inayotwa Adenosine Tri-phosphate (ATP), ambayo ni kwa ajili ya matumizi ya baadaye mwil in i . Hiz i h igh e n e r g y e l e c t r o n s husababisha kuzaliwa kwa kiwango kikubwa cha chembe zilizobeba u m e m e c h a n y a zinazoitwa free radicals. Chembe hizi zina uwezo wa kubadilisha umbo na utendaji kazi wa vinasaba kwenye seli (DNA mutations) na kuharibu vimeng’enya mbalimbali ndani ya mwili!

Tafiti zimebaini kuwa

baadhi yetu miili yetu huchakata wanga bila madhara ukilinganisha na wengine. Watu wa aina hii husemekana w a n a m i f u m o y a u jenzi na uvunj i fu wa kemikali ambayo inaendana na vyakula vya wanga/nafaka au C A R B O H Y D R AT E TYPE kwa kitaalamu. Njia pekee ya kujua kama wewe ni miongoni mwa waliomo katika kundi hili au siyo ni kwa njia ya kipimo cha kutambua mfumo wako wa ujenzi na uvunjifu wa kemikali mwilini (metabolic typing test). Huko nyuma tuliwahi kukiweka kipimo hiki katika ukurasa wetu wa FB na kuwakaribisha wadau wajisaidie nacho. Hivi sasa kipimo hiki kiko katika mfumo wa kijitabu na unaweza kukipata katika ofisi z a H e r b a l I m p a c t z i l i z o k o m t a a w a Mosque, Kitumbini, D a r e s S a l a a m . (Kwa maelezo zaidi 0754281131/0715281131)

MSURURU wa vifaru vya jeshi la Saudi Arabia.

Page 18: ANNUUR 1173.pdf

18 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala

KU N A b a a d h i y a m i s e m o y a K i s w a h i l i

unapoisikia ikisemwa au unapoisoma, kuna wakati unaweza maneno yake ukayapita tu na wala usiuone umuhimu au tafsri ya msemo huo mpaka likupatapo. Kwa mfano kuna msemo usemao “ Majuto ni m j u k u u , M s i b a wa kujitakia huambiwi pole. Usipo sikiza la mkuu huvunjika guu”, na kadhalika.

Katika misemo hi i ambayo nilo iaynisha nataka niutumie huu “ Msiba wa kujitakia h u a m b i w i p o l e ” kuhusiana na kadhia hii ya kura ya maoni ya katiba, ambapo Mheshimiwa Spika Ameir Kificho pale alipotumia mamlaka ya k e ya k u m k u b a l i Mwanasheria Mkuu mteule Said Hassan Said alipowasilisha sheria ya kura ya maoni barazani kwa njia ya maandiko. M h e s h i m i wa S p i k a Kificho alitumia mamlaka yake hayo kwa kukataa upande wa upinzani pale ulipowasilisha hoja ya kwamba Baraza la Wakilishi haliwezi kutumika kuridhia sheria ambayo jambo lenyewe si la muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika, kufanya hivyo ni kinyume kabisa kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar na hili Mheshimwa Kificho alikuwa analijuwa fika. Lakini afanyeje, na tayari Mheshimiwa Kificho maji alikuwa ameshayavuliya nguo. Tayari alikuwa ameshayavul ia nguo tokea pale alipokuwa D o d o m a . H i v y o asingeweza tena kuwa kama ng’ombe kuutowa u l i m i wa k e k we n ye mdomo kuupeleka puani na baadaye kuurejesha mdomoni, kwa sababu hii siyo tabia ya muungwana na uungwana hasa wa Kizanzibari. .

Kukubalika kupigiwa kura ya maoni kwa katiba hii kwa wajumbe wa Baraza la Wakilishi upande wa chama tawala kulitarajiwa na wengi; kul i tara j iwa na hata wasio kuwa wanachama wa chama tawala kwa sababu ishara za matokeo

Msiba wa kujitakiNa Juma A. Simba

haya yalianzia Dodoma ambako kwa wakati huu maamuzi yote ya Zanzibar kupitia chama tawala ndiko yanako amuliwa wakibakia viongozi wa chama tawala Zanzibar, kushangiria kwa kupiga makofi, wingi wa vigelegele, shangwe na nderemo kwa vibakwizo, Mapinduzi Daima huku baadhi yao ati wakiomba wapewe pole.Katika hili la kujitakia msiba wenyewe Chama cha Mapinduzi hivi sasa, viongozi wake wanapita kila pahala, mbali na karibu Unguja na Pemba kuipigia debe katiba hii kupigiwa kura ya NDIO.

Katika kampeni yake ina jar ibu kuipamba katiba hii iwezavyo na kuvifafanuwa baadhi ya vifungu kwa ukengeza wa kuonesha uzuri wa katiba hii ilivyo nzuri, lakini cha kuvunda hakifukiliziki kwa udi wachilia mbali ubani. Miongoni mwa sifa zipambazwo ambazo hazipambiki ni pamoja na Rais wa Zanzibar kuwa Makamo wa Rais wa Muungano ambapo kiukweli atabakia kuwa tu na jina la Makamo wa Rais lakini hata zidi. Kwani hata itokeapo Rais wa Muungano atakapo kuwa hayupo nchini hatokuwa na mamlaka ya kukaimu; hatokuwa na mamlaka ya hata Zanzibar anayoiongoza kuiamuilia kujiunga na tasisi ya hapo Kenya wachilia mbali nchi za nje. Ruhusa ya kufanya hivyo mpaka

kibali kitoke Dodoma. Mfano isadifu kuwepo hayo mafuta Zanzibar au madini mengine ye yote yale yenye thamani, basi suala la uchimbaji wa madini hayo mpaka ruhusa itoke Dodoma,. ambapo masuala kama h a y a n a m e n g i n e o chama cha upinzani CUF katika kupigania kwake mamalaka kamili ndio inayoyataka yasiwe A b a d a n k u a m u l i wa kwake ni kwa kuomba ruhusa kutoka serikali ya Muungano, ba l i yaamuliwe Mbweni. Kwa sababu Chama cha Mapinduzi kinajuwa fika kwamba juu kampeni zake zote kwa hapa Zanzibar hakikuweza kufanikiwa kuwashawishi Wa z a n z i b a r w a l i o wengi juu ya kuikubalai katiba ya serikali mbili, pia kushindwa kupata asilimia mbili ya tatu hata Dodoma kwenyewe, pia hai jaj ipa matumaini kwamba hata kwenye visanduku vya kura itaweza kufanikiwa kwa hapa Zanzibar.

Hivyo kwa kutumia sect: 34 sheria ya kura ya maoni Chama cha Mapinduzi kimeona ili kiweze kushinda katika hili la kupiga kura ya maoni ni kuhalalisha k u p i g a k u r a k w a kutumiwa vitambulisho v ya M t a z a n i a , k wa k u w a o r o d h e s h a Wa t a n g a n y i k a w o t e waliopo Zanzibar kupiga kura kama ni Wazanzibari na sio tena Watanganyika, na Wazanzibari walioko

Tanganyika kupiga kura kama Wanzibari mradi tu katiba ipite. Utaratibu huu mpya wa kura ya maoni ni kuhakikisha tu katiba hii ima fa ima, vyo vyote viwavyo, lazima

Wazanzibari waikubali. Lakini mtu anaweza kujiuliza, jee kura hizi za Wazanzibari walioko Tanganyika tunaweza kusadikishaje kwamba idadi ya kura zitazopigwa ili kuchanganywa na za hapa Zanzibar wapiga kura wake kweli ni Wazanzibar? Jee kuna t a k w i m u ye y o t e ya mwaka wo wote inyo onyesha Tanganyika kuna Wazanzibari Wangapi?

Wanzibari wengi hakika wamekuwa wakijiuliza wenzetu ambao wana lazimisha kwa nguvu zote katiba hii lazima ipite ni kwa uzuri gani hasa uliomo ndani ya katiba hii? Jee wanachokiona kweli ni uzuri tu uliojaa katiba hii, hamna ubaya na baadye kuupima uzuri na ubaya? Jee pale mnapopaza sauti zenu juu kusifu Mapinduzi D a i m a , m n a k u s u d i a mapinduzi gani hasa, ya kuomba ruhusa kutoka Tanganyika kutuchagulia hata rais wa Zanzibar awe nani? Kwa sababu wanao ikataa katiba hii ni kwamba wanataka masuala ya Zanzibar wajiamulie wenyewena y a l e M u u n g a n o tuamuwe kwa pamoja ili kuondowa ule mfumo mithili y ukuloni mambo leo. Haya sio kabisa yaliyo kuwa madhumuni

y a M a p i n d u z i . Hatukupinduwa kwa sababu tu ya kutawaliwa na watawala wa kigeni au rangi, ili kukarabisha utawala wa Waafrika wenzetu ati tu kwa sababu wao ni weusi. Katiba hii ambayo hivi sasa imeshikiwa bango kupigiwa kura tarehe 30 Aprili, ilivyotengenezwa ni kutunyanganya kabisa umiliki wetu mamlaka yetu, mwishowe Zanzibar ye t u . H i i n i k a t i b a ambayo lengo lake hasa ni kututowa kikaangoni kututumbukiza katika moto.

Mwezi wa Aprili huu tunao uanza umetengwa kwa ajili ya kampeni rasmi ingawa rasha rasha za kampeni tayari tumesha zishuhudia. Inawezekana katika mwezi wa Aprili katika kampeni wananchi wakatiwa khofu na vitisho ikiwa ni njia moja ya aina ya kampeni, lakini aina yeyote ya vitisho tusifike pahala kujitafutiya msiba wenyewe. Wananchi w a n a p o p i g a k u r a kuwachaguwa viongozi wao, huwataka walio w a c h a g u w a w a w e ni watu waaminifu, waadilifu, wakweli, na wawe wanayawakilisha ya l e m a t a k wa ya wananchi wale walio wengi, hasa inapo jitokeza kuwa kinacho wakilishwa kina faida na manufaa kwa jamii yote. Uhuru wa mwanadamu yeyote y u l e u n a b o r a h a t a ukaandamana na shida na madhila. Hakuna utumwa uungwanawala mzuri.

Wazanzibar ni watu tulio zaliwa huru kama walivyo Tanganyika, Muungano usiwe chanzo cha kuujutia. Katiba hii ambayo chama tawala mnaipigia debe ya serikali mbili haitotufaidisha, tusiwasihi Wazanzibari Wachilia mbali kutaka kuwalazimisha kuipigia kura. Muelewe fika wale ambao maamuzi yenu yatabakia kung’ang’ania kuipigia kura katiba hii ya serikalimbili, ipo siku maamuzi yenu ya ta tughar imu sote , ikitokea sio sisi watoto wetu au vijukuu vyetu, hivyo tujiepusheni na msiba huu wa kujitakia kwa sababu hakutokuja kuwepo wa kutupa pole.

SPIKA wa Muda wa Bunge Maalum la Katiba,Mhe. Pandu Kificho akiingia bungeni mjini Dodoma kuliendesha bunge hilo.

Page 19: ANNUUR 1173.pdf

19 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Makala ya Mtangazaji

MOSCOW, (WAFA) – President Mahmoud Abbas Tuesday slammed Israel’s longstanding policy of deception, saying that it would no longer fool anybody.

Speaking at the Peoples’ Friendship University of Russia, which conferred u p o n h i m h o n o r a r y doctorate degree, Abbas stated that the world is still witnessing Israel’s aggression and racism against the Palestinian people and that Israel is still acting as a rogue; p lac ing i t se l f above international law and continuing its occupation of Palestinian territories.

He added that Israel

Abbas: Israeli Prolonged Policy of Misleading, Deluding Fools Nobodyis still maintaining its long-standing policy of conducting a meaningless v i c i o u s c i r c l e o f negotiations in an effort to shirk the prerequisites of just and comprehensive peace, gain time and impose a fait accompli to make it impossible to establish the future Palestinian state.

We aspire to witness peace reigning in the region, so that all future g e n e r a t i o n s i n o u r homeland as well as neighboring countries, including Israel, enjoy its fruits; a regional peace under which all live in security, safety, stability and good-neighborliness,

stated Abbas.Abbas made these

remarks during his latest official visit to Russia, during which Russia’s leader Vladimir Putin met with him on Monday in his Novo-Ogaryovo residence outside Moscow.

The current state of Israeli-Palestine relations as well as armed conflicts in the Middle East was at the top of the talks agenda. “Now as the situation grows more difficult in the region, of course, it is very important to hold consultations on the full range of issues. I mean of course, primarily the Israeli-Palestinian issue but not only that, I would

like to discuss with you the situation in Syria, Iraq and now in Yemen,” said Putin addressing Abbas at the start of the meeting.

Put in sa id , ' I t ’ s a pleasure to note that r e l a t i o n s b e t w e e n Palestine and Russia have been growing steadily and are constantly, step-by-step, becoming stronger.” He added, 'And now, when the situation in the region has become more complicated, of course, it is particularly important to consult with you on all the issues at hand.'

Abbas stated, 'I want to note that we highly appreciate the cooperation with your country and the

efforts of Russia to solve the Palestinian problem with regaining of the peace in our lands.'

He added, 'There are many problems in our region with which Russia has to work with and I must admit that Russia's efforts are successful.'

The two presidents also held talks over trade and the economic situation between both countries, with Putin stating 'I am glad to note that re lat ions between Palestine and Russia were developing and s t rengthen ing constantly.'

N A B L U S ( M a ' a n ) - - Israeli forces detained 31 Palestinians across Nablus overnight including 20 Hamas affiliates and several former prisoners.Palestinian security sources told Ma'an that more than 50 Israeli military vehicles raided Nablus around 2:00 a.m. Wednesday without informing the Palestinian Authority until already having entered the city.

Local sources added that Israeli forces raided the Balata refugee camp, al-Namsawi area, the Asira Street, the Old City and other neighborhoods across the city.

Witnesses also told Ma'an that dozens of Israeli soldiers raided the home of Abdullah al-Aker, 32, searching the house for three hours and confiscating 40 thousand shekels ($10,078), computers and mobiles.

T h e f o l l o w i n g we r e identified among those d e t a i n e d We d n e s d a y : Said Dweikat, Nidal Abu Rmeileh, Wajih Abu Eida, Abdullah al-Aker, Hussam al-Bustami, journalist Amin Abu Wardeh, Omar Abd al-Wahhab, Amjad Abu Ghosh, Muhammad Sawalmeh, Zahi Abu Eida, Samih Eleiwi, Youssef Marshud, Abu Hamzeh al-Jurf, Ziad Mreish, Amjad Zamel, Sami al-Assi, Anan Futouh, Saad Khudrieh, Mona Abu Bakr al-Sayeh, Ahmad Sawalha, Omar Abd al-Wahhab,

Omar Issa Atallah, Abu Hamzeh al-Jurf, Ghassan

Israeli forces detain 31 across Nablus in mass raid

Abu al-Baraa, Fares and Ghanem Sawalmeh, Sheikh Bassem Abu Juneid and Jasser Abu Hamada.

Most of the detainees are former prisoners.

The reported lack of communication by Israeli forces to Palestinian security p r i o r t o We d n e s d a y ' s raid marks a violation of internationally recognized policy regarding Palestinian autonomy in the occupied West Bank.

Israeli entrance into Area A -- the approximately 20 percent of the West Bank technica l ly under fu l l Palestinian control as a result of the Oslo Accords -- must be taken in only coordination with the PA.

Incidents of illegal Israeli incursion occur on a routine basis, with Israeli forces carrying out an average of 75 raids a week on occupied West Bank Palest inian neighborhoods and villages according to Hebrew and English news site Haaretz.

Israeli security forces have detained over 40 Palestinians in the last week across the occupied West Bank and East Jerusalem for "illegal activity."

The majority of Palestinian political organizations are considered illegal by Israel, including those that make up the PLO, and affiliation with such parties is often used as grounds for imprisonment, accord ing to Pr i soner Support and Human Rights Association Addameer.

G A Z A , ( WA FA) – A Palestinian youth Tuesday succumbed to wounds he sustained during the 2014 Israeli summer aggression on the Gaza Strip, whereas another was slightly injured in a building collapse, a c c o r d i n g t o m e d i c a l sources.

WAFA correspondent reported that Eliwa Nidal Eliwa, 22, was critically injured during the summer aggression on the strip, yet his medical condition did not improve. He was pronounced dead Tuesday after succumbing to his wounds.

During the summer Israeli aggression on Gaza last July and August, more than 2,190 Palestinians were killed and more than 10,000 others injured by Israel’s deadly

Gaza Man Dies of Wounds Sustained during Israeli Aggression

airstrikes and arti l lery attacks.

The Palestinian Authority became a member at the ICC on the 1st of April to investigate crimes allegedly committed during the Israeli aggression on the Gaza Strip during the summer of 2014, a step pursued by President Mahmoud Abbas following the United Nations failure to approve a draft resolution calling for the end of occupation and establishment of a Palestinian state within three years.

Meanwhile, a Palestinian resident was walking past a five-storey building, which was severally damaged d u r i n g t h e s u m m e r aggression, in Dir al-Balah area in central Gaza, when it collapsed to the ground, leaving him with l ight injuries.

During the Israeli summer aggression on the Strip, thousands of homes were destroyed and around 170,000 Palestinians were consequently left homeless.

Gaza still suffers from the repercussions of the Israeli aggression which took place in the summer of 2014; the infrastructure along with thousands of homes were completely destroyed, displacing thousands of families who up until the moment live in caravans on the rubble of their homes.

M e a n w h i l e , t h e U N News Center stated that, “United Nations agencies and offices were alarmed over the limited progress in rebuilding the lives of those affected by last summer's fighting between Israeli forces and Palestinian armed groups in the Gaza Strip.”

Page 20: ANNUUR 1173.pdf

20 AN-NUURJAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 201520 MAKALA AN-NUUR

20 JAMAADIUL AKHER 1436, IJUMAA APRILI 17-23, 2015

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

Tanzania Muslim Hajj Trust, uandikishaji unaendelea, gharama za Hijja ni US Dollar 4400, tarehe za Safari ni: 11 na 13 Septemba, kurudi 7 Oktoba, 2015.

Wahi kujiandikisha sasaKwa mawasiliano:+255 2221815770786 3838200713 764636

Safari ya Hijja Hijiria 1436

+255 222 1823700754 261910; 0717 0000650784 272723website-www.hajjtrust.or.tz

Baadhi ya viongozi wa Baraza la Wanawake wa Kiislamu Tanzania wamemtembelea Sheikh Ponda Issa Ponda katika gereza la Morogoro mwishoni mwa wiki iliyopita.

V i o n g o z i h a o wamefanya ziara gerezani hapo na kuonana na Sheikh h u y o a n a e s h i k i l i wa gerezani hapo.

V i o n g o z i h a o w a l i o w a w a k i l i s h a k i n a m a m a w e n z a o wakiongozwa na Ukhti Mayasa Sadallah ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa Baraza la wanawake wa Kiislamu Tanzania akiwa amefuatana na Amira wa Baraza hilo Wilaya ya Ilala, Ukht Hindu Abdallah.

Akiongea na mwandishi wa habari hizi Ukhti Mayasa baada ya ziara hiyo anasema anashukuru sana kwa mapokezi na ukarimu kutoka kwa

Akina mama wa Kiislamu wamtembelea Sheikh PondaNa Azza Ally Ahmed viongozi wa gereza hilo.

“Tulipofika tulikuta t a y a r i k u n a w a t u wameshakuja kumuona Sheikh hivyo zimebaki nafasi za watu wawili ambao ndio wanaoleta chakula baada ya kujieleza kuwa tumekuja kumuona S h e i k h P O N D A n a tunatokea Dar es Salaam, askari alituandika majina na kusema nyie ingieni na hao pia wanaotakiwa kuleta chakula wataingia hamna shida kwa kweli tulisikia faraja sana.” Alisema Mayasa.

“Alichousia na kusisitiza Sheikh ni kuwa Waislamu kudumisha mshikamano pamoja na kuendeleza Dini ya Allah bila kuchoka kufanya daawa.”

Al iongeza Mayasa akisema huo ulikuwa ndio ujumbe na nasaha za Sheikh Ponda kwa Waislamu.

Akielezea ukht Mayasa kuhusu afya ya Sheikh anasema anaonekana ni mwenye afya njema hana tatizo lolote.

Mimi ni Binti wa Kiislamu HAMIDA RASHIDI. Pia ni yatima, ambaye ninasoma Chuo cha Ualimu Ununio (Ununio Teacher’s College) mwaka wa pili.

Nimesimamishwa masomo kwa kutolipa ada na kushindwa kuendelea na masomo. Mpaka sasa nipo nyumbani. Mlezi aliyekuwa ananilipia ada ameshindwa kufanya hivyo kutokana na hali yake kuwa mbaya kiuchumi.

Naomba kila atakae guswa na habari hii anisaidie kwa kile atakacho jaaliwa na Muumba wake kwani kutoa ni moyo. Toa kile alicho kuruzuku Allah (S.w) hakika hutopoteza utayakuta malipo yako mbele ya muumba wako.

Kiasi cha ada ambayo nadaiwa ni Shilingi laki Nane (800,000). Unaweza ukatuma kwa namba ya mlezi wangu Yassin M. Mwagamile 0783 723312 au unaweza wasiliana na uongozi wa chuo 0715 822332, 0687 505 292 au unaweza lipia Benki ya KCB Account Namba 3300627761 kwa jina la Ununio Teachers' College kwa jina la Mwanachuo HAMIDA RASHIDI. Ukituma kwa akaunti ya chuo ni vyema ukatujulisha kwa namba ya mlezi wangu.

MSAADA WA KULIPIWA ADAWeka duara kwenye jawabu ilio sawa, jawabu kamili wiki ijayo. 1. Sura za Makiya ni ………………………2. Sura Madaniya ni ……………………..3. Anaitwa nani aliotafsiri Tafsiri ya Quran kwa jina la al-Tabari katika mwaka

wa 310 AH?4. Mtume SAW alipewa Utume akiwa na umri wa miaka mingapi?5. Ujumbe, Wahyi wa mwanzo aliteremshiwa Mtume SAW akiwa yupo wapi?6. Vita vya pili Waislamu walivyopigana baada vya Badr vinaitwaje?7. Mtume SAW alikufa akiwa na umri gani?8. Taja jina la Mtume alioishi wakati mmoja na Mtume Mussa………………9. Wataje watoto wawili wa Mtume Ibrahim …………………… na …………………..10. Bibi Aisha alikufa akiwa na umri wa miaka mingapi?

Unajua Kuwa Qu’ran ndio kitabu kinachosomwa zaidi kila siku duniani? Kuwa majina mengine ya Quran ni Al-Furqaan, Al-Kitaab, Al-Zikr, Al-Noor,

Al-Huda. Mtume Mussa ametajwa katika Qu’ran mara 136 katika Sura mbalimbali? Quran ina Surah 114. Suratul Naml ni Sura pekee Bismilalhi imetajwa mara 2. Mtume amepokea wahyi kwa kipindi cha miaka 13 na kati ya hayo miaka

10 peke yake amepokea wahyi akiwa Madinah. Kuwa jina la Bibi Maryam ni jina la mwanamke lilotajwa kwa jina. Kuwa Quran ni kitabu pekee kilichohifadhiwa kwa ghibu na watu wengi

duniani hakuna kitabu chochote ambacho watu wamekihifadhi kwa ghibu zaidi ya Qur’an.

Kuwa mwanadamu huvuta pumzi kwa kutumia gesi ya Oxygen na kutoa Carbon dioxide wakati miti huvuta pumzi kwa kutumia gesi ya Carbon dioxide na kutoa Oxygen.

Kuwa jangwa la Sahara ni kubwa kuliko yote duniani.

CHEMSHA BONGO NO:2