Fataawa Za Wanachuoni (17)

45
1 Fataawa Za Wanachuoni [17] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

description

1 .·«·-|· ;¸··· Fataawa Za Wanachuoni [17] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush © 2 Dibaji: Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo. Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta

Transcript of Fataawa Za Wanachuoni (17)

Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (17)

1

������� ���

Fataawa Za Wanachuoni

[17]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (17)

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (17)

3

Fataawa zilizomo ni hizi zifuatazo:

1. Mtume Hakufanya Da´wah Kwa Kutenga Siku Maalumu

2. Msingi Wa al-Ikhwaan al-Muslimuun Hauna Maana

3. Rabiy´ al-Madkhaliy Ni Salafiy

4. Shaykh al-Jaabiriy Kuhusu ´Abdul-Maalik Ramadhaaniy

5. Mfano Wa Khawaarij Wa leo

6. Kusoma Kwa Mtu Asiyefanya Tabdi´ Kwa ´Ar´uur, al-Ma´ribiy Na al-

Maghraawiy

7. ´Allaamah al-Fawzaan Anakanusha al-As'ilah al-´Iraaqiyyah Cha al-

Halabiy

8. Ibaadhi Na Mashia Ndio Vijukuu Vya Jahmiyyah

9. ´Allaamah Ahmad an-Najmiy Kuhusu Picha Na Mawaidha Ya Video

10. Salafiy Haina Maana Mtu Kalindwa Na Madhambi

11. Allaamah al-Fawzaan Akimradi al-Qaradhwaawiy Anaesema Uhuru

Ni Bora Kuliko Shari´ah

12. Allaamah Rabiy´ Kuhusu Muhammad Mukhtaar ash-Shanqiytwiy

13. Hizi Mbwa Zenye Fujo Haziwezi Kudhuru Salafiyyuun

14. Kumnasihi Mtawala Au Mtu Kwa Dhati Yake Kwenye Mimbari

15. Da´wah Haianzi Kwa Maonyo

16. Hukumu Ya Mwenye Kupinga Kuja Kwa Dajjaal?

17. Imaam Ibn Baaz Kuhusu Utiifu Kwa Mtawala Wa Kuwait

18. Ni Wajibu Kusambaza Radd Za Wanachuoni

19. Tunaonya Hizbiyyuun Kwa Maslahi Yao Wenyewe

20. Haya Hawayajui Wale Walioghafilika Kuhusu Hizbiyyuun

21. Ni Sharti Wakubaliane Wanachuoni Katika Kumjeruhi Mtu? (1)

22. Radd Kwa Dr. Zakir Naik Asemae Kuwa Manaswara Ni Ndugu Zetu

Kibinaadamu

23. Radd Ni Dawa

24. Mdogo Anaweza Kumpiga Radd Mkubwa?

25. Ni Sharti Wakubaliane Wanachuoni Katika Kumjeruhi Mtu? (2)

26. Mume Kumpa Talaka Mke Bila Ya Sababu

27. Ikiwa Ni Radd Ya Haki, Haijuzu Kwako Kuiacha

28. Shaykh as-Suhaymiy Kuhusu Facebook

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (17)

4

29. Mwanachuoni Tu Ndiye Awezae Kupiga Radd?

30. Shubuha Zinazotumiwa Na Wale Wanaopinga Radd

31. Allaamah an-Najmiy Kuhusu Yule Anaewatuhumu Maimamu

Watatu Kuwa Ni Murji-ah

32. Nasaha Ya Shaykh Fawzaan Kwa Dada Ambaye Anapata Tabu Kwa

Ajili Ya Dini Yake

33. Je Awwaam Ni Salafiyyuun?

34. Jabriyyah Na Jahmiyyah Ni Watu Wa Bid´ah Au Makafiri?

35. Awwaam Watahadharishwe Dhidi YaWatu Wa Bid´ah

36. Allaamah al-Fawzaan Kauli Ya as-Suwaydaan Kupingana Na Allaah

Na Mtume Wake

37. Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh Kuhusu Kauli Ya as-

Suwaydaan Uhuru Wa Dini

38. Haitoshi Kujiita Tu Salafiy

39. Nasaha Za al-´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy Kuhusu Baadhi Ya

Mashaykh

40. Ni Yapi Madhehebu Ya al-Ikhwaan al-Muslimuun?

41. Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy Kuhusiana Na Maandamano

42. Ipi Hukumu Ya Kuweka Camera Msikitini?

43. Masanduku Ya Swadaqah Msikitini

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (17)

5

Wanachuoni waliomo ni hawa wafuatao:

1. ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

2. Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy

3. Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

4. Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy

5. ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah Aal ash-Shaykh

6. Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy

7. Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

8. Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy

9. Zayd bin Haadiy al-Madkhaliy

10. Muhammad bin Swaalih al-Luhaydaan

11. Muhammad bin Haadiy al-Madkhaliy

12. Swaalih bin Sa´iyd as-Suhaymiy

13. Ubayd bin ´Abdillaah al-Jaabiriy

14. Muhammad bin ´Abdillaah al-Imaam:

15. Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Waswaabiy

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (17)

6

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1. Mtume Hakufanya Da´wah Kwa Kutenga Siku Maalumu

Swali:

Yapi maoni yako kuweka mpaka siku maalumu kufanya Khuruuj katika njia

ya Allaah na Jamaa´t-ut-Tabliygh?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) haikuthibiti kwake kwamba

aliamrisha hilo kabisa. Na Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walikuwa

ni watu wenye hima kwa kheri na watu wenye kujikurubisha kwa yale Allaah

Anayoyapenda. Haikupokelewa kutoka kwa mmoja katika yao (Radhiya

Allaahu ´anhum) kitu katika hayo. Na ikiwa tutashindwa kufanya baadhi ya

´amali, tuko na mizani kamili; Maneno ya Allaah na maneno ya Mtume wake

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hivyo basi, tukimbilie kujifunza Dini. Na

mmoja wetu akitaka kubobea katika kitu, basi anaweza kuhifadhi na

kufahamu Maneno ya Mola wa viumbe na maneno ya Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Kwa hakika atakaeruzukiwa kufahamu Kitabu cha Allaah

(Jalla wa ´Alaa) na Sunnah za Mtume wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

atakuwa ameruzukiwa kheri kubwa.

Chanzo:

http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=130109&st=40

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (17)

7

2. Msingi Wa al-Ikhwaan al-Muslimuun Hauna Maana

Swali:

Yapi maoni yako kwa mwenye kusema:

"Tushirikiane kwa yale tunayoafikiana, na tusameheana kwa yale

tunayokhitilafiana."

´Allaamah al-Luhaydaan:

Haya maneno hayana maana. Wala haifai kuyafanyia kazi.

Haya maneno, ina maana wanamaanisha kama kuna mtu ambaye anadai ni

Muislamu ilihali ni Mulhid (kafiri) na mwengine katika Ahl-us-Sunnah wako

na kituwanaafikiana cha maslahi na mji wao, washirikiane kafiri huyu na yule

mwengine. Ingelikuwa sawa kama ni kuhusiana na kuulinda mji na

wavamizi, ama baadhi ya Madu´aat wanaosema tushirikiane kwa yale

tunayoafikiana, na tusameheana kwa yale tunayokhitilafiana, hichi ni kitendo

ambacho si sahihi.

Chanzo:

http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=130109&st=20

3. Rabiy´ al-Madkhaliy Ni Salafiy

Swali:

Ipi rai yako kwa anayemponda Shaykh Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy?

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (17)

8

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Ni kosa hili. Ni kosa.

Swali:

Unasemaje kuhusiana na Shaykh?

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Mtu huyu namjua. Ni Salafiy.

Swali:

Ipi hukumu ya kueneza mikanda ambayo Serikali imekataza, mfano wa

mikanda ya baadhi ya Madu´aat ambao wamepigiwa marufuku?

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Haijuzu.

Swali:

Haijuzu?

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Ndio.

Chazo: http://youtu.be/c6vBiepR1Y0

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (17)

9

4. Shaykh al-Jaabiriy Kuhusu ´Abdul-Maalik Ramadhaaniy

Swali:

Kuna swali kuhusu Shaykh ´Abdul-Maalik Ramadhaaniy.

Shaykh Dr. ´Ubayd al-Jaabiriy:

´Abdul-Maalik Ramadhaaniy imekuwa siku hizi anachanga sana mambo na

anakosa nia. Hafai.

Swali:

[Swali haliko wazi]

Shaykh Dr. ´Ubayd al-Jaabiriy:

Hapana, hapana. Siwanasihi kushikamana naye. Ni katika wafuasi wa al-

Halabiy sasa.

Swali:

Vitabu vyake vya zamani vipo hapa Libya.

Shaykh Dr. ´Ubayd al-Jaabiriy:

Vitabu vya zamani mtu anaweza kuchukua elimu akastafidi kwavyo, na

khaswa vile ambavyo vina Radd dhidi ya Khawaarij. Ni vizuri. Kwa mfano

kitabu "Madaarik-un-Nadhwar". Ni kizuri.

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (17)

10

Swali:

Ana kitabu hata cha Hijaab...

Shaykh Dr. ´Ubayd al-Jaabiriy:

Hakuna neno kusoma vitabu vya zamani. Lakini mtu huyu kwa sasa,

amekuwa kama nimevyokwambia. Kuanzia miaka ya nyuma amekuwa hana

tena nia. Anasapoti maneno na sifa za al-Halabiy kwa The Amman Message

ambayo imejaa Kufuru.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127471

5. Mfano Wa Khawaarij Wa leo

Swali:

Mtu anaweza kusema ya kwambawanachama wa al-Qaa´idah ni Khawaarij?

Shaykh Dr. Muhammad bin ´Abdillaah al-Imaam:

Ndio. Ni Khawaarij. al-Ikhwaan al-Muslimuun ni Khawaarij. Hizb-ut-Tahriyr

ni Khawaarij. Suruuriyyah ni Khawaarij. Suruuriyyuun wamefanya uasi

Algeria na katika miji mingine.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=6785

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (17)

11

6. Kusoma Kwa Mtu Asiyefanya Tabdi´ Kwa ´Ar´uur, al-Ma´ribiy Na al-

Maghraawiy

Swali:

Inajuzu kuchukua elimu kwa mtu ambaye hambadi´ Ar´uur, Abul-Hasan al-

Ma´ribiy na al-Maghraawiy na anasema shirika la Ihyaa' at-Turaath ni Salafiy?

Hajasoma na wala hana Tazkiyyah kutoka kwa wanachuoni. Anachukua

elimu kwenye mikanda na vitabu vya Ibn Baaz, Al-Albaaniy na Ibn

´Uthaymiyn (Rahimahumu Allaah).

´Allaamah Yahyaa an-Najmiy:

Kwa hakika ni kwamba yule ambaye hawabadi´ watu hawa, yeye ni kama

wao. Kwa kuwa watu hawa ni watu wa Bid´ah. Na al-Maghraawiy imethibiti

kwake kuwa ni Takfiyriy

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=865

7. ´Allaamah al-Fawzaan Anakanusha al-As'ilah al-´Iraaqiyyah Cha al-

Halabiy

Swali:

Sisi tuko magharibini, tumepata kitabu chenu kwa jina la "al-As'ilah al-

´Iraaqiyyah"...

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (17)

12

´Allaamah al-Fawzaan:

Tumesema kwamba ni cha uongo. Nimekipiga Radd. Ni cha uongo, uongo,

uongo.

Chanzo: http://alfawzan.ws/sites/default/files/bryhari--1427-2-12.mp3

8. Ibaadhi Na Mashia Ndio Vijukuu Vya Jahmiyyah

Swali:

Ipi tofauti kati ya ´Aqiydah (Itikadi) ya Jahmiyyah na ya Ibaadhi? Je, ni

kikundi kimoja kwa jina jipya?

Shaykh Dr. Swaalih as-Suhaymiy:

Katika mlango wa Sifa za Allaah, ni takriban kundi moja. Wote wanakanusha

Sifa za Allaah (Jalla wa ´Alaa) na wanakanusha waumini kumuona Mola Wao

Aakhirah. Wanakubaliana (Ibaadhi) na Raafidhwah (Mashia) na Jahmiyyah

katika masuala mengi.

Lakini katika mlango wa Ijraa´, wanatofautiana na Jahmiyyah. Jahmiyyah

wakali wanaamini ya kwamba ´amali si katika Imani, na kutokana na hili

wanakufuru kwani ni Ijraa´ ya Kufru. Nayo ni kuamini ya kwamba ´amali si

katika Imani, na kwamba inatoka nje ya Imani. Bila ya shaka mwenye kuamini

hivyo amekufuru. Na Jahmiyyah ni katika mkumbo huu. Ama Ibaadhi wao ni

Khawaarij, wako kinyume chao (na hao Jahmiyyah) hata hivyo

wanakubaliana katika masuala mengi; kama kukanusha Sifa za Allaah

(Subhaanahu wa Ta´ala).

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (17)

13

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=nT5Yqm-DM4o

9. ´Allaamah Ahmad an-Najmiy Kuhusu Picha Na Mawaidha Ya Video

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Haijuzu kwa yeyote kunichukua picha (Video). Ni Haraam juu yenu. Haijuzu

kwa yeyote kunichukua picha, sitaki yeyote anichukuepicha.

Mwanafunzi wa Shaykh:

"Ni ndugu zetu wenye simu za Camera wamezifugua na kutaka kumchukua

picha (sasa Shaykh amewakataza), kwa kuwa Shaykh haonelei kujuzu kwa

hilo."

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=rZz8NsqYqAw

10. Salafiy Haina Maana Mtu Kalindwa Na Madhambi

Swali:

Ikiwa mtu ana Manhaj safi na anapenda Salafiyyuun, lakini ana madhambi

mengi. Je, anaweza kuitwa Salafiy?

´Allaamah al-Waswaabiy:

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (17)

14

Kinachoangaliwa ni ´Aqiydah na Manhaj. Salafiy haina maana mtu kalindwa

na madhambi. Lakini ikiwa ana ´Aqiydah sahihi na Manhaj sahihi, ni Salafiy

na Sunniy. Tunamuusia kuwa na msimamo na kuachana na maasi.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=3436

11. ´Allaamah al-Fawzaan Akimradi al-Qaradhwaawiy Anaesema Uhuru Ni

Bora Kuliko Shari´ah

Yuusuf al-Qaradhwaawiy:

"Kwa hakika, hakuna dawa kwa Ummah huu isipokuwa mpaka kwa Uhuru

(Demokrasia). Kama nilivyotangulia kusema katika baadhi ya barnamiji

zangu, mimi ninaipa kipaumbele Uhuru (Demokrasia) juu ya kutekeleza

Shari´ah ya Kiislamu. Haiwezekani kutekeleza Shari´ah ya Kiislamu na Uhuru

(Demokrasia) inakosekana."

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema ya kwamba Uhuru ni bora kuliko Shari´ah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mna shaka ya kwamba ni kafiri? Mwenye kusema ya kwamba Uhuru ni bora

kuliko Shari´ah, huyu ni kafiri ukafiri mbaya - A´udhubi Allaah.

Chanzo http://alfawzan.ws/sites/default/files/bryhari--1427-10-14.mp3

Tarehe: 1427-10-14/2006-11-06

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (17)

15

12. ´Allaamah Rabiy´ Kuhusu Muhammad Mukhtaar ash-Shanqiytwiy

Swali:

Ndugu mmoja ametupa mkanda wa Sharh ´Umdat-ul-Ahkaam cha Shaykh

Muhammad [al-Mukhtaar] ash-Shanqiytwiy na una mikanda 400. Tuache

ibaki Msikitini?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Mtu mtu huyu, mimi sijasoma Sharh hii. Sijui. Nimeambiwa kuwa mtu huyu

hawezi kupambanua baina ya Ahaadiyth Swahiyh na Dhaifu, na kwamba

anatangamana na Hizbiyuun na Sufiyyuun nawala hana mawasiliano na Ahl-

us-Sunnah. Ndio maana siwezi kuzitakasa wala kumtakasa mtu huyu. Kwa

kuwa sijazisoma. Nanyi hamna haja... Ni nani anaesambaza mikanda ya mtu

huyu? Sio Ahl-us-Sunnah wanaosambaza mikanda yake. Wanaozisambaza ni

Hizbiyyuun. Yeye mwenyewe hajionyeshi kuwa ana vikundi vikundi. Lakini

wakati unapoona watu hawa wamemzunguka na mikanda yake na

wanamchukulia kuwa Imaam wa Waislamu, ni dalili ionyeshayo kuwa mtu

huyu ni katika wao. Ni njia ya khatari inayowafanya vijana kuwa vikundi

vikundi. Mko na vitabu vya Salaf. Vinawatosheleza.Fiqh ya Salaf

inawatosheleza. Kwa kuwa hayo yatakuja kuwapeleka katika mambo

mengine.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=Pknjz6e_fEo

13. Hizi Mbwa Zenye Fujo Haziwezi Kudhuru Salafiyyuun

Swali:

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (17)

16

Siku zilizopita waliongea sana watu wapotofu maneno ambayo wanadai

wanaiweka Salafiyyah kwenye usawa. Unasema nini kuhusu hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Jambo hili ni kitu ambacho watu mfano wao; katika wanafiki na makafiri

walikuwa wakilifanya. Walikuwa wakitukana watu wa Dini. Wanawatukana

Waislamu wanaoshikama na Dini yao. Tokea zamani. Hakuna jipya.

Wanafuata njia ya watu hawa. Hawakudhuru Salafiyyah wala Salafiyyuun na

lolote. Wanajidhuru wenyewe. Salafiyyah ya kweli kweli - Alhamdulillaah -

iko thabiti juu ya Qur-aan na Sunnah. Haikudhurika na fujo za mbwa.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=133045

Tarehe: 1431-04-11/2010-03-27

14. Kumnasihi Mtawala Au Mtu Kwa Dhati Yake Kwenye Mimbari

Swali:

Je, ni katika nasaha kumpa mtawala na kuamrisha mema na kukataza maovu

kukataza maovu wanayoyafanya juu ya mimbari?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Sio katika nasaha kumkosoa mtu au mtawala kwenye mimbari. Nasaha

hutolewa kwa njia ambayo itanufaisha. Ama ikiwa makusudio ni kuleta

tashwishi na kueneza aibu na chuki, hii sio katika nasaha. Ikiwa mtu anaweza

kumnasihi mtawala kuacha yale anayoyaona ni maovu au kumfanya akataza

maovu, amuombee Allaah Amuafikishe kufanya hivyo, au amwambie

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (17)

17

anaedhania anaweza kumnasihi ya kwamba kuna kasoro kadha na kadha,

ikiwa anajua kwa yakini makosa hayo.

Chanzo:

http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=130109&st=20

15. Da´wah Haianzi Kwa Maonyo

Swali:

Vipi tutajumuisha kati ya kutotaha-dharisha wanaokhalifu na kuelezea Njia

iliyonyooka? Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa ni

mwenye kutoa bishara na mwenye kutahadharisha. Tukinyamazia

wanaokhalifu na wala hatubainishi...

´Allaamah al-Fawzaan:

Wewe kitu cha kwanza, wafunze njia sahihi. Watakuja kujua wanaokhalifu.

Ama kuanza tu kuwakataza na wao hawana msingi wala hawana elimu, hili

halina faida. Litakuja kupelekea kwenye chuki tu. Wafunze njia sahihi.

Wafanye waifahamu Dini ya Allaah. Halafu baada ya hilo, ima wao wenyewe

watakuja kujua ni nani anaekwenda kinyume au wewe uwatanabahishe ikiwa

hawajui. Lakini haifai kuanza wao na kuwatahadharisha dhidi ya fulani na

fulani wakati hawafahamu lolote.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=133027

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (17)

18

16. Hukumu Ya Mwenye Kupinga Kuja Kwa Dajjaal?

Swali:

Ipi hukumu kwa mwenye kupinga kuja kwa Dajjaal?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu ikiwa anajua dalili na akapinga, ni kafiri. Kwa kuwa kapinga kitu

ambacho ni Mutawaatir kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam). Ama ikiwa ni mjinga na wala hajui dalili, huyu abainishiwe.

Akiendelea kupinga baada ya kubainishiwa, anahukumiwa ukafiri. Kwa

kuwa anamkadhibisha Allaah na Mtume Wake (´alayhis-Salaam).

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=124546

17. Imaam Ibn Baaz Kuhusu Utiifu Kwa Mtawala Wa Kuwait

Swali:

Kiongozi wa Kuwait ni mtawala na ni lazima kumtii kwa yale yanayoruhusu

kwa vile hahukumu kwa kutumia Shari´ah?

Imaam Ibn Baaz:

Ndio, ni watawala, sawa wa Kuwait, Jordan au Syria. Ni watawala. Ni wajibu

kuwatii kwa yale yanayoruhusu kama alivyosema pia Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Ni wajibu kuwatii kwa yale yanayoruhusu na wala

hawatiiwi kwa yale ambayo ni maasi, si wao wala wengineo. Kwa mfano

wakisema kunyweni pombe, wasitiiwe. Chukueni Ribaa, wasiitiwe. Wakisema

zinini, wasitiiwe. Ama wakiamrisha kumtii Allaah na Mtume Wake au

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (17)

19

wakaamrisha kwa kitu kinachowanufaisha Waislamu na wala hakikhalifu

Shari´ah au sheria za barabarani ili kuepuka ajali, ni wajibu kuwatii.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=133070

18. Ni Wajibu Kusambaza Radd Za Wanachuoni

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa Radd hizi ni za kielimu na zimetoka kwa wanachuoni waaminifu na

zina faida kwa Waislamu na zina nasaha na muongozo, basi ni wajibu

kuzisambaza ili watu wanufaike kwazo, na kwa ajili ya kuwanasihi Waislamu

na kuondosha utata, kwa vijana na kwa wale wasiojua utata huu. Radd hizi

kutoka kwa wanachuoni na Baswiyrah, kuna faida kwa watu wote. Kuna

kuondosha utata. Ni nasaha kwa Waislamu. Yule mwenye kuzisambaza ana

ujira kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=133178

19. Tunaonya Hizbiyyuun Kwa Maslahi Yao Wenyewe

´Allaamah al-Waadi´iy:

Ama kuhusu Hizbiyyuun, Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Anasema kwenye

Kitabu Chake Kitukufu:

و�و وا ����س ����

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (17)

20

"Na semeni na watu kwa wema." (02:83)

Sisi tunaonya watu dhidi yao kwa ajili ya maslahi yao wenyewe. Na lazima

kuwepo kujeruhiwa na kusifiwa, Jarh wa Ta´diyl. Wanachuoni wanaojulikana

wamekubaliana kujeruhiwa na kusifiwa, Jarh wa Ta´diyl, na kuonya dhidi ya

Ahl-ul-Bid´ah. Wao wenyewe wanaonya dhidi yetu mchana na usiku. Sisi

tunaonya dhidi ya watu wa Bid´ah na tunalingania watu kwenye Sunnah ya

Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Chanzo: http://muqbel.net/sounds.php?sound_id=39

Tarehe: 1420-05-28/1999-09-09

20. Haya Hawayajui Wale Walioghafilika Kuhusu Hizbiyyuun

´Allaamah al-Waadi´iy:

Ndugu! Hatuna muda wa kujadili. Katika sisi kuko wenye kutaka kuhifadhi

Qur-aan. Wengine wanataka kuwa mabingwa wa lugha ya kiarabu. Wengine

wanataka kuwa mabingwa wa Sunnah na kupambanua Swahiyh, dhaifu na

yenye kasoro. Hatuna muda. Wakati Hizbiy anakujia anataka kujadiliana na

wewe, mwambie aende kwa mwenye shaka kama yeye, mimi niko thabiti

kwenye Dini yangu. Wao hawana mengine zaidi ya haya; mjidala na

kukamata wenye kughafilika. Kuna wenye kughafilika katika wao. Hatutaki

kuwa na wenye kughafilika katika Ahl-us-Sunnah. Hatujui wapi mpaka

unapokwenda - kwetu Ahl-us-Sunnah au Hizbiyyuun? Wanasema:

"Hawa wamaamini ya kwanba Allaah Kastawa juu ya ´Arshi Yake. Wanaamini ya

kwamba Allaah Ana macho mawili. Wanamaani ya kwamba Allaah Ana mikono

miwili."

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (17)

21

Masikini wewe! Unasahau ya kwamba wanaharibu Sunnah!

Masikini wewe! Unasahau ya kwamba wanajuzisha Demokrasia na uchaguzi

wa kikafiri!

Masikini wewe! Unasahau ya kwamba wako na al-Ikhwaan al-Muslimuun!

Masikini wewe! Unasahau ya kwamba wamechukua Msikiti wa ndugu zetu

Aden!

Masikini wewe! Unasahau ya kwamba wanakimbiza watu kuikimbia Sunnah

na Ahl-us-Sunnah!

Allaah Amrehemu Aliyesema:

"Ukimuona mtu anawaponda Ahl-ul-Hadiyth, basi jua ya kwamba ni mtu wa

Bid´ah."

Chanzo: http://muqbel.net/sounds.php?sound_id=39

Tarehe: 1420-05-28/1999-09-09

21. Ni Sharti Wakubaliane Wanachuoni Katika Kumjeruhi Mtu? (1)

Swali:

Kujeruhi (Jarh) kumeshurutishwa Ijmaa´?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hii ni kazi ya wanachuoni wa Hadiyth. Sio sharti iwe Ijmaa´ ya kwamba mtu

huyu kajeruhiwa. Bali mwenye kuthibitisha anatangulia kabla ya mwenye

kupinga. Mwenye kutakasa, huyu ndiye anayepinga; na yule mwenye

kujeruhi (Jarh), huyu ni mthibitishaji na ndiye mwenye kutangulia.

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (17)

22

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=JgxnJbCQGLc

22. Radd Kwa Dr. Zakir Naik Asemae Kuwa Manaswara Ni Ndugu Zetu

Kibinaadamu

Swali:

Mwenye kusema makafiri ni ndugu zetu wa kibinaadamu na si katika Dini. Je,

maneno yake haya ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haitoshi kiubinaadamu. Hakuna undugu wa ubinaadamu. Wala mtu hasemi

hivi kwa kutaka kuwapaka mafuta au hisia zao. Hapana! Mtu asisemi hivi.

Inatakiwa kusema wao ni maadui zetu wala mtu asisemi ni ndugu zetu wa

kibinaadamu. Bali mtu anatakiwa kusema ni maadui zetu. Ikiwa ni maadui

zetu katika Dini, udugu wa kibinaadamu utafidisha nini? Utafidisha nini?

Fir´awn alikuwa pia binaadamu. Au sio? Je alikuwa pia ndugu yetu?

Haitakikani kusema hivi.

Chanzo: http://alfawzan.ws/node/1875

Tarehe: 1431-04-14/2010-03-29

23. Radd Ni Dawa

Swali:

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (17)

23

Mi napenda Sunnah na nnachukia Bid´ah na ukhurafi. Lakini Shaykh

kuwapiga Radd Ahl-ul-Bid´ah na watu waliopinda, baadhi ya watu hawako

katika Manhaj Salaf, na wanapopigwa Radd kuna watu wanaosema haifai

kuzisambaza isipokuwa tu zisambazwe kwa wanafunzi. Tunaomba nasaha

kwa swali hili.

´Allaamah al-Fawzaan:

Kama amevyosema muulizaji, Ruduud hakuna budi lazima ziwe zimetoka

kwa wanachuoni ambao wanajua mambo ya Radd, wanajua kosa na

wanaweza kulirudi kwa dalili katika Qur-aan na Sunnah. Kusambaza Ruduud

hili ni jambo la wajibu kwa kuwa ni kuwafunza Waislamu. Ikiwa mtu kaeneza

Bid´ah yake na akaeneza kosa lake kwa watu, ni lazima kusambaza Ruduud

sahihi [... sauti imepotea... ] kwa ajili kuondosha madhara ya Bid´ah na kosa.

Hili ni lazima na ni dawa. Radd ikifichwa shari itaenea kwa watu, Bid´ah

kuzidi kuwa kubwa n,k. Ni lazima kusambaza Ruduud zilizo sahihi na si kila

Ruduud. Ruduud sahihi zilizotoka kwa wanachuoni ambao wanajua Bid´ah

na wanajua kosa na wanajua vipi watalirudi kwa Qur-aan na Sunnah.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=Tvpvs9oXl5s

24. Mdogo Anaweza Kumpiga Radd Mkubwa?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Sawa ikiwa ni mkubwa au mdogo, ikiwa atabainisha kwa elimu hakuna

ubaya, sawa ikiwa ni mdogo au mkubwa. Kinachotazamwa ni yule

aliyepigwa Radd. Inaweza kuwa ni mtu mpotevu anayepoteza Ummah,

akampiga Radd aliye mdogo kuliko yeye na wala hakuna ubaya kufanya

hivyo.

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (17)

24

Chanzo: http://youtu.be/tARw5OfeH8E

25. Ni Sharti Wakubaliane Wanachuoni Katika Kumjeruhi Mtu? (2)

Swali:

Je, ni sharti katika kuwajeruhi Ahl-ul-Bid´ah Ijmaa´a (wakubaliane

wanachuoni wote) wa zama hizo? Au anatosha mwanachuoni mmoja tu?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Huu ni mfumo wa ulegezaji mchafu. Ni zama zipi zilizoshurutisha Ijmaa´ hii?

Na dalili iko wapi ya sharti hii? Kila sharti isiyopo katika Kitabu cha Allaah

sharti hiyo ni batili. Anapomjeruhi Imaam Ahmad bin Hanbal, au Yahyaa bin

Ma´iyn, wakamjeruhi Mubtadi´ah, je ni lazima wakubaliane wanachuoni wa

Sunnah wote duniani kote ya kwamba mtu huyu ni Mubtadi´ah? Ataposema

Ahmad bin Hanbal huyu ni Mubtadi´ah watakiwa kupokea hivyo. Na hivyo,

ilikuwa anaposema fulani ni Mubtadi´ah, watu wote wanakubali hilo.

Mashahidi wawili wanapotoa ushahidi kwa Qadhi kuhusu fulani ya kwamba

amemuua fulani, je ni sharti iwe Ijmaa´ (wakubaliane na wengine) ya kwamba

kweli ameua? Bali ni wajibu kwa Haakim kutoa hukumu kwa Shari´ah ya

Allaah, ima atoe Diyah au Qiswaas. Ni wajibu ahukumu kwa Shari´ah ya

Allaah (´Azza wa Jalla). Imeshurutishwa Ijmaa´ kwa ushahidi wa mtu huyu?

Na hili ni jambo kubwa kuliko kuwabadi´ Mubtadi´ah. Hawa ndio walegezaji,

Ahl-ul-Baatwil na Madu´aat wa shari. Msisikilize porojo hizi. Anapomjeruhi

mwanachuoni mwaminifu mtu, ni lazima kukubali Jarh hii. Mwanachuoni

mwengine mwaminifu anapopinga hilo, hapo ndipo kunaangaliwa nini

kasema huyu na huyu, kunatazamwa Jarh hii na Ta´diyl hii. Ikiwa Jarh hii

imefafanulia na kuwekwa wazi, basi inatangulizwa juu ya Ta´diyl, hata ikiwa

wanachuoni waliomsifu mtu huyo ni wengi. Mwanachuoni mmoja ametoa

Jarh iliyofafanuliwa, wakasema kinyume chake wanachuoni ishirini mpaka

khamsini pasina dalili, hawana zaidi ya kumdhania vizuri na kuchukulia kwa

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (17)

25

uinje wanavyomuona, na huyo mwanachuoni mwengine ana dalili kwa

kumjeruhi mtu huyu kwa dalili, basi Jarh hii inatangulizwa. Kwa kuwa

aliejeruhi ana hoja na hoja ndio inayotangulia. Na wakati mwingine

inatangulizwa hoja hata kama wataikhalifu mamia au maelfu ya watu.

"Jamaa´ah ni ile iliyoko juu ya haki hata kama mtu atakuwa peke yake."

Lau mtu atakuwa juu ya Sunnah, wakamkhalifu watu wa vijiji viwili au vitatu

- Mubtadi´ah, haki iko na mtu huyo. Na kunatangulizwa hoja alizonazo na

haki juu ya yale ya batili waliyonayo hao wengine. Ni wajibu kuheshimia haki

na kuheshimia hoja na dalili.

�ل ھ��وا �رھ���م إن ���م ��د��ن

"Sema: "Leteni ushahidi wenu kama nyinyi ni wasema kweli." (02:111)

وإن �ط+ أ�(ر )ن '& ا%رض �#�"وك ن ���ل �

"Na ukiwatii wengi katika hawa waliomo duniani watakupoteza na Njia ya

Allaah." (06:116)

Wingi hauna maana yoyote ikiwa hauna hoja. Ikiwa watu wa duniani wote

wamekusanyika katika upotofu pasina hoja, isipokuwa watu wachache tu

waliko kwenye haki, wengi hao hawana maana na wingi wao. Hata kama ni

mtu mmoja au watu idadi ya watu wachache. Hishimieni haki, shikamaneni

nayo na kubalini haki ikiwa ina hoja.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=M7DcNcQMKDA

26. Mume Kumpa Talaka Mke Bila Ya Sababu

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (17)

26

Swali:

Anapata madhambi mume akimpa Talaka mke wake bila ya sababu?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ataangaliwa kwa nini kamtaliki. Ikiwa yuko na sababu, atapewa udhuru na

wala hana juu yake kitu. Na kama amemuonea bila ya sababu miongoni mwa

sababu, si mtu mwenye aibu wala tabia katika khulka yake, anapata

madhambi bila ya shaka. Kwa kuwa kamuonea na pengine hata hana familia,

akaja kuathirika kwa taabu. Hivyo, ni juu ya mtu kumcha Allaah. Maisha ya

ndoa yamefungamana baina ya muumini mwanaume na muumini

mwanamke. Mke wa mja hapa duniani ndio mke wake huko Peponi kwa

kiwango kikubwa cha uzuri na ukamilifu; mbora kuliko hata Huur al-´Iyn

kutokana na Swalah zake, kisimamo chake na Imani yake. Hivyo ni juu ya

muumini kuwa makini, Akimsahilishia Allaah kumpa mke katika watu wa

Tawhiyd, mwema na mwenye kufunga. Na akiwa na kitu kama kasoro,

akiweke sawa kwa kadiri na uwezo wake. Na hakuna mtu isipokuwa ana

makosa na hukosea. Mtu kuwa na subira ni katika tabia ya muumini.

Muulizaji:

Anauliza pia kuhusiana na Kauli ya Allaah:

م ا���دال ز ��ن زوج وآ���م إ�داھن� ��ط�را '4 23�ذوا )0� /�.�وإن أرد�" وج )�

"Na mkitaka kubadilisha mke mahali pa mke, na hali mmoja wao mmempa

chungu ya mali, basi msichukue katika hayo kitu chochote." (04:20)

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (17)

27

Ndio, akitaka (kubadili mke), iwe ni kwa sababu miongoni mwa sababu.

Haifai kwake (mume) kumbadili (kumtaliki) mke ambaye kamhudumia na

wakaishi naye, isipokuwa iwe kwa sababu inayomlazimu kwa hilo, hapo

atakuwa halaumiki.

Chanzo: http://youtu.be/7BKHeJNFkZI

27. Ikiwa Ni Radd Ya Haki, Haijuzu Kwako Kuiacha

Swali:

Nitapoona ya kuwa Radd itamghadhibisha na kumkasirikisha mtu fulani. Je,

kuna maslahi ya kuacha kumpiga Radd hata kama ni Radd ya haki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa ni Radd ya haki, haijuzu kwako kuiacha. Mwenye kukasirika kwa ajili

ya Radd ya haki, mtu huyu hana kheri yoyote. Wewe usijali kuridhika kwake

na kukasirika kwake. Bali unatakiwa kujali haki ya Allaah (Subhaanahu wa

Ta´ala). Ni lazima kwako kubainisha haki bila ya kuogopa lawama za wenye

kulaumu. Ikiwa kuna kheri yoyote, atafurahi kwa hili. Ama ikiwa hakuna

kheri yoyote, usimjali.

Chanzo: http://youtu.be/SnXLKAuNr-8

28. Shaykh as-Suhaymiy Kuhusu Facebook

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (17)

28

Shaykh Dr. as-Suhaymiy:

Mfano wa hayo makundi mengine ni la kisiasa, ambalo linalingania watu

kwenye maandamano. Na hiyo ni alama miongoni mwa alama za Khawaarij

Qudaamah, wao na wanaowasaidia wote, na wanaopita katika njia yao au

kuwanusuru kupitia Internet, sawa ikiwa ni (tovuti) iitwayo Facebook au

nyinginezo katika vifaa ambavyo vimekuwa ni sumu na maskani mwa watu

waasi na Ahl-ul-Bid´ah, vibaraka vya Mayahudi na Manaswara ambao

wamefanya ufisadi katika miji mingi. Hakika kuwasaidia ni katika

kusaidizana katika dhambi na uadui. Allaah (Ta´ala) Amesema:

=وى و; �8�و�وا �: ا9(م وا 8دوان �� �ر< وا و�8�و�وا �: ا

"Na saidianeni katika wema na uchaji Allaah. Wala msisaidiane katika dhambi

na uadui." (05:02)

Miongoni mwa hayo makundi maovu pia, ni yale makundi ambayo yanaona

lengo (nia) nzuri inamjuzishia mtu njia. Wanaruhusu mambo ya Haramu kwa

ajili ya kufikia mambo yao maovu.

29. Mwanachuoni Tu Ndiye Awezae Kupiga Radd?

Swali:

Upi usahihi wa maneno ya baadhi ya watu:

"Hapigwi Radd mwanachuoni isipokuwa tu na mwanachuoni mwenzake?"

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (17)

29

Maneno haya ni makosa. Ina maana anyamazie kosa ikiwa hakupatikana

mwanachuoni wa kubainisha haki, na ikawa mdogo huyu (anaepiga Radd)

ana hoja na dalili! Ni wajibu kwake kubainisha aliyo nayo (dalili na hoja).

Nukta muhimu ni kuwa mwanachuoni na mwanafunzi haongei isipokuwa

kwa elimu, na wala haingii katika jambo lolote isipokuwa kwa elimu.

��ر وا @ؤاد � )+ وا �� ل" أو ـ.ك ��ن 0� )�ؤو; و; �=ف )� �س ك �0 �م إن� ا

"Wala usiyafuate usiyo na ujuzi nayo. Hakika asikio, na macho, na moyo -

hivyo vyote vitaulizwa." (17:36)

Kusema mambo usiyoyajua sawa hata ikiwa ni mwanachuoni,

maneno hayo mbali na wala hayakubaliwi na ni Haraam; na yanaweza kufikia

katika daraja ya Shirki kubwa kwa Allaah (´Azza wa Jalla). Kama Alivyosema

Allaah (Tabaaraka wa Ta´ala):

م ر�<& ا @وا�ش )� ظDر )�D� و)� )� �ر� �H�ر ا �ق< وأن �/ر� �ل إ�� &H� وا�طن وا9(م وا

ل �0 ��ط��� وأن �=و وا �: م ��ز< �( 0 �ـ���0 )� ; 8��)ون ا �ـ�

“Sema: “Hakika Mola wangu Ameharamisha fawaahish (al-kabaair;

madhambi makubwa, ueasharati, zinaa, liwati, n.k.) yaliyodhihirika na yaliyo

ya siri, na dhambi (za kila aina), ukandamizaji bila ya haki, na

(Ameharamisha) kumshirikisha Allaah kwa chochote kile ambayo

Hakukiteremshia dalili, na kusema juu ya Allaah yale ambayo hamyajui.”

(07:33)

Ibn-ul-Qayyim anasema katika Tafsiyr yake kwamba "Hakika Allaah katika

Aayah hii Kafanya mambo hayo kuanzia madogo kwenda kwenye makubwa;

na kubwa ya madhambi hayo ni kusema juu ya Allaah pasina elimu. Kwa

kuwa inaingia katika Shirki, Kufuru, Bid´ah na inaingia katika maasi n.k.

Chanzo cha balaa zote ni mtu kusema juu ya Allaah pasina elimu, na kusema

kwa jila la Allaha na kwa jina la Dini Yake pasina elimu. Ikiwa kuna

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (17)

30

mwanafunzi ambaye ana elimu katika jambo fulani na ana dalili ya jambo hilo

- na wanachuoni hawakuongelea jambo hilo, anatakiwa aseme haki.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=c4K4aLHLKXY

30. Shubuha Zinazotumiwa Na Wale Wanaopinga Radd

´Allaamah al-Fawzaan:

Na kwa hili kuna UWAJIBU wa kumradi anaekwenda kinyume, kinyume na

wanavyoseme baadhi ya watu acheni Ruduud, waacheni watu kila mmoja na

abaki na maoni yake na heshima yake, uhuru wa maoni na maneno. Kwa haya

Ummah utaangamia, kwa haya Ummah utaangamia. Salaf

hawakuwanyamazia mfano wa watu kama hawa, bali waliwafedhehesha na

kuwapiga Radd, kwa kujua kwao khatari yao kwa Ummah.

Sisi hatuwezi kunyamaza kwa shari yao, ni lazima kwetu kubainisha yale

Aliyoyateremsha Allaah. La sivyo tutakuwa wenye kuficha, wale ambao

Allaah kasema kuwahusu:

�@ �� ف �D)� إن� ا و� ��ت أو ا �)ر 'K 4��ح �0� أن �ط� 0 ')ن M�� ا ع 2�را 'Pن� وا )روة )ن /�8.ر ا �ـ� و)ن �طو�0 /��ر ��م ا �ـ�

"Hakika wale ambao wanaficha yale Tuliyoyateremsha katika Hoja zilizo

wazi na Hidaaya baada ya kuwa Tumeyabainisha kwa watu katika Kitabu,

hao Anawalaani Allaah na wanalaaniwa na kila mwenye kulaani." (02:159)

Jambo hili haliishii kwa Mubtadi´ah, bali linawapata pia watu

wanaowanyamazia. Mwenye kuwanyamazia (watu wa Bid´ah) dhambi

inampata na adhabu. Kwa kuwa ni wajibu kubainisha, kuwawekea watu

wazi. Na hii ndio kazi ya Ruduud za kielimu. Ruduud za kielimu zilizoenea

Page 31: Fataawa Za Wanachuoni (17)

31

kwenye Maktabah za Waislamu, zote zinasafisha (upotofu) kwenda katika

Njia iliyonyooka na zinatahadharisha dhidi ya watu hawa. Tusipandikizwe

fikra hii; uhuru wa maoni, uhuru wa maneno, kuheshimia wengine na

mengineyo.

Sisi makusudio yetu sio kuwaingilia watu, makusudio yetu ni haki.

Makusudio yetu sio kuwajeruhi watu na kutoa aibu za watu, makusudio yetu

sisi ni kubainisha haki. Hii ni amaana Allaah Kawapa nayo wanachuoni.

Haijuzu kunyamazia watu mfano wa hawa.

Lakini kwa masikitiko makubwa, kunapotokea mtu akawapiga Radd mfano

wa watu kama hawa, wanasema "Wewe una pupa, wewe una hili na lile, huyu

hastahiki kupigwa Radd, ungemnyamazia jambo hili lisingejulikana." Na

mfano wa maneno hayo ya kutia wasiwasi. Huyu hawezi kusitisha

wanachuoni kubainisha kwa watu shari ya watu hawa Madu´aat wapotofu.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=aw1awpALjGo

31. ´Allaamah an-Najmiy Kuhusu Yule Anaewatuhumu Maimamu Watatu

Kuwa Ni Murji-ah

Swali:

Baadhi ya watu waliolelewa kwa vitabu vya Suruuriyyah na Hizbiyyah,

wanawatuhumu maimamu watatu - Ibn Baaz, Ibn ´Uthaymiyn na Al-Albaaniy

(Rahimahumu Allaah) - Irjaa´ kwa kuwa hawawakufurishi watawala.

Unasemaje kuhusu hili?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Huu ni ujinga na upotofu. Hawa watu wa Bid´ah kila siku wanajitokeza kwa

picha nyingine. Ikiwa Al-Albaaniy, Ibn Baaz na Ibn ´Uthaymiyn ambao ni

Page 32: Fataawa Za Wanachuoni (17)

32

wanachuoni wa Ummah, viongozi na wakubwa, ni Murji-ah - nani aliebaki?

Ni nani aliebaki? Kuna yeyote aliebaki? Hapakubaki hata mmoja. Huu ni

msiba, haya ni magonjwa. Ninavyoona kuhusu watu hawa ni kuwa,

anaeonekana na kauli kama hii, akamatwe, atiwe adabu na apigwe. Ikiwa

hakujirudi, pengine kunahitajika kutumiwa mfumo mwengine.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=132786

32. Nasaha Ya Shaykh Fawzaan Kwa Dada Ambaye Anapata Tabu Kwa

Ajili Ya Dini Yake

Swali:

Allaah (´Azza wa Jalla) Kaniongoza baada ya kusikilia muhadhara wa mmoja

katika wanachuoni kuhusu Aakhirah. Baada ya siku hii nilihisi utamu wa

Imani na tangu sasa naishi maisha mengine ya raha na mafanikio na raha na

watoto wangu. Nawafunza Kitabu cha Allaah na kuwaita kwa Allaah na

kumkumbuka Allaah katika hali zote.

Pia nilianza kuvaa mavazi ya Kiislamu ambayo yanaendana na mwanamke

wa Kiislamu. Lakini pamoja na uzito wote huu na njia hii mpya

nimeyochukua, familia yangu, ndugu zangu wote katika familia wananiona

kama mgonjwa na ni mwenye wasiwasi. Ndio maana nimemtumia swali

langu bwana muheshimiwa Shaykh Swaalih ili anifanye kubaki kwenye

thabati na msimamo.

´Allaamah al-Fawzaan:

Hii ni bishara ya kheri kwa mwana mke huyu ambaye aliathirika kwa

muhadhara mzuri. Allaah Amjaze alieutoa kheri. Namna hii yatakikana

muhadhara kuwa, iwe ni wenye kuibainisha Dini hii na kubainisha fadhila za

Page 33: Fataawa Za Wanachuoni (17)

33

Dini hii na kuvutia watu kwayo. Muhadhara usizungumzia mambo mengine,

kuingia kwenye siasa na mfano wa mambo kama hayo ambayo yanapoteza tu

muda wa watu na linawaathiri na wala hawastafidi kitu. Bali wanadhurika.

Namna hii unatakiwa kuwa mihadhara na khaswa khaswa kwenye Misikiti.

Khutbah za Ijumaa na mawaidha iwe namna hii. Ikumbushe Allaah (´Azza wa

Jalla), ikiwafunza watu wasioyajua katika mambo ya Dini yao.

Na wewe mwanamke uliposema ya kwamba umetubu kwa Allaah na ukawa

na msimamo katika Dini ya Allaah na ukashikamana na Hijaab, jua kuwa hili

ni kheri kwako na maisha yako ya sasa na si kama maisha yako ya kwanza.

Maisha ya uongofu na Imani. Ni juu yako kuwa na msimamo na kuendelea

kwa hili. Jizidishie Imani. Jizidishie kusikiliza mihadhara mizuri na Dhikr.

Usibabaishwe na watu hawa waharibifu ambao wanataka kukurudisha

nyuma na uache neema Aliyokupa nayo Allaah. Hawa ni katika Mashaytwaan

wa kibinaadamu ambao wanapoteza watu na wanawakimbiza katika kheri.

Ni juu yako kushikama imara na Dini yako na kuwa na subira kwa uliyomo.

Ni juu yako kujifunza elimu yenye manufaa ili iwe kutubu kwako na ´Ibaadah

zako zimejengeka juu ya Baswiyrah na juu ya elimu yenye manufaa.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=133391

33. Je Awwaam Ni Salafiyyuun?

Swali:

Je ´Awwaam Waislamu tunaweza kuwaita Salafiyyuun?

Shaykh Dr. Muhammad al-Madkhaliy:

Page 34: Fataawa Za Wanachuoni (17)

34

Hapana. Itategemea na hali zao na mji waliyomo. Mtu ataangalia mji

waliyomo. Ikiwa wengi wao ni hivi, basi ni ndiyo. Na ikiwa wengi wao wako

katika Bid´ah, hapana.

Chanzo:

http://ar.miraath.net/sites/default/files/fatawah/questions/q&a_Almadkli

_...

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=IfT1EJQybiY

34. Jabriyyah Na Jahmiyyah Ni Watu Wa Bid´ah Au Makafiri?

Swali:

Kumekuja maswali mengi yanauliza kuhusu Jabriyyah na Jahmiyyah ni watu

wa Bid´ah au ni makafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni watu wa Bid´ah. Ama makafiri ni kama nilivyowaambia, mwenye

kukusudia khaswa na analingania katika madhehebu yake potofu huyu ni

kafiri. Ama mfuata kichwa mchunga huyu hakufurishwi, lakini ni mpotofu na

abainishiwe haki.

Chanzo: http://alfawzan.ws/sites/default/files/tg--1431-11-04_0.mp3

Tarehe: 1431-11-04/2010-10-11

Page 35: Fataawa Za Wanachuoni (17)

35

35. ´Awwaam Watahadharishwe Dhidi YaWatu Wa Bid´ah

Swali:

Je ni katika misingi ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah kutahadharisha dhidi ya

Ahl-ul-Bid´ah?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ama kutahadharisha Ahl-ul-Bid´ah, atahadharishwe yule asiyejua njama zao.

Ama mwenye kuijua, hahitajii mwenye kumtahadharisha nazo. Na watu

wengi wanaweza kuwa hawajui hali za Ahl-ul-Bid´ah, na hawajui ahkaam za

mapenzi juu yao na chuki juu yao. Na Bid´ah chafu na zakikafiri zinaingia

katika kauli ya Allaah (Jalla wa ´Alaa):

0 ور�و ون )ن ��د� �� وا �وم ا2Rر �واد" �S�� ; K�د �و)� �ؤ)�ون

”Huwakuti watu wanao muamini Allaah na siku ya Mwisho kuwa

wanawapenda wanao mpinga Allaah na Mtume Wake.” (58:22)

Bid´ah za kikafiri ni kumpinga Allaah na Mtume Wake.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=129784

36. ´Allaamah al-Fawzaan Kauli Ya as-Suwaydaan Kupingana Na Allaah Na Mtume Wake

Twaariq as-Suwaydaan:

Page 36: Fataawa Za Wanachuoni (17)

36

"Nukta nyingine kuhusiana na uhuru, ni uhuru wa kutabiri. Ni katika haki za

watu kusema watakalo ilimradi tu hawajaharibu tabia kama kulingania katika

fikra mbali mbali, kuwa na kipingamizi kwa mji, mtawala hata Uislamu. Mimi

sina tatizo nalo. Hata kuwa na kipingamizi kwa Allaah (Ta´ala) na Mtume wa

Allaah."

Twaariq as-Suwaydaan:

"Ni katika haki ya mtu kuchagua Dini na pote apendalo. Akitaka kuwa Shia,

Sunniy, Durziy... Yuko na uhuru. Na ni haki ya kila mtu kuabudu Mungu

amchaguaye kwa njia aipendayo. Kanisa zisikatazwe. Hekalu zisikatazwe. Ni

katika haki za watu."

Twaariq as-Suwaydaan:

"Mimi hata hadd [adhabu] ya kuritadi sioni kama ni ya kidini. Naona ni kama

adhabu ya kisiasa tu."

Swali:

Kumedhihiri baadhi ya Madu´aat wasemao hadd ya kuritadi ni jambo la

kisiasa na si jambo la kisasa. Pia anasema kuwa inajuzu kuwa na kipingamizi

kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) bali hata kwa Allaah (´Azza

wa Jalla). Ipi hukumu ya kauli yake? Je ni kuritadi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Bila shaka. Hakuna kuritadi baada ya huku. Anayemfanyia mzaha Allaah,

Mtume Wake na Ahkaam za Kishari´ah. Hakuna baada ya kuritadi kama

huku. Hii ni aina mbaya ya kuritadi.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=129316

Page 37: Fataawa Za Wanachuoni (17)

37

37.´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh Kuhusu Kauli Ya as-Suwaydaan Uhuru Wa Dini

Swali:

Nimesikia baadhi ya Madu´aat wakisema inajuzu kuwa na kipingamizi kwa

Allaah, Uislamu na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Na anasema

tuache watu wachague Dini na waabudu wapendacho. Na anataka

waondoshe adhabu ya kuritadi na anataka kuachwe kujengwe kanisa katika

miji ya Waislamu. Ipi Radd yako shaykh?

´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh:

Sijui maneno haya wayasemayo wanayasema kwa akili na Dini au upumbavu

na maradhi ya nyoyo. Je, haya yanatokwa na mtu aliyekosa Imani au kwa mtu

asiyejua alisemalo? Vipi tuwe na kipingamizi kwa Allaah? Allaah (Jalla wa

´Alaa) Katuamrishakumtii na kumtii Mtume Wake:

�ول �D ا �ذ�ن آ)�وا أط�8وا � وأط�8وا ا ر� �� أ�"

”Enyi mlioamini! Mtiini Allaah, na mtiini Mtume.” (04:59)

�D ا �ذ�ن آ) �وا أط�8وا � ور�و 0 و; �و �وا 0� وأ��م ��)8ون �� أ�"

”Enyi mlioamini! Mtiini Allaahna Mtume wake, wala msijiepushe naye, nanyi

mnasikia.” (08:20)

)وك '�)� /Kر �D��م >��� : � �#�ت و���<)وا ����)�'4 ور�<ك ; �ؤ)�ون ��� �( >( �Kم �رD�@�دوا '& أK� ; �م)

Page 38: Fataawa Za Wanachuoni (17)

38

”La! Naapa kwa Mola wako! Hawataamini mpaka wakufanye wewe ndiye

muamuzi katika yale wanayokhitalifiana, kisha wasione uzito katika nyoyo

zao juu ya hukumu utayo toa, na wanyenykee kabisa.” (04:65)

Akiwa na kipingamizi kwa Allaah akikusudia kukataa maneno ya Allaah na

Sunnah ya Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kupa

kipaumbele rai na matamanio kabla ya Kitabu na Sunnah, ni upotofu na

inaweza kumfanya mtu akaritadi. Tunawajibika kuamini.

0 وا )ؤ)�ون �لU آ)ن ��S و)T.0�� و���0 ور�� >� �ول �)� أ�زل إ 0� )ن ر� ��0 آ)ن ا ر� ق ��ن أ�د )<ن ر" 0 ; �@ر< �� ��وإ �ك ا )��ر و�� وا �)8�� وأطV ��8@را�ك ر

”Mtume ameamini yaliyoteremshwa kwake kutoka kwa Mola Wake, na

Waumini vile vile. Wote wamemuamini Allaah, na Malaika Wake, na Vitabu

vyake na Mitume Wake. Hatutafautishi baina ya yeyote katika Mitume Wake,

na (Waumini) husema: “Tumesikia na tumetii. Tunakutaka maghfira Mola

Wetu! Na marejeo ni Kwako”.” (02:285)

Haya maneno yana uchafu kama kipingamizi kwa Allaah na Mtume Wake, au

uhuru wa Dini!! Dini zote zimefutwa baada ya Allaah Kumtuma Muhammad

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), Shari´ah yake imekhatimu Shari´ah zote

za kabla na kufuta Dini zingine zote. Ikawa ni wajibu kwa viumbe vyote

kumtii Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kufuata Sunnah

zake. Anasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Hatosikia yeyote kuhusu mimi si myahudi wala mnaswara kisha asiniamini

ila ataingia Motoni."

Kwa kuwa Muhammad ndiyo Mtume na Nabii wa mwisho. Tunaamini

Mitume wote waliotangulia na Risalah zao. Lakini ´amali na utekelezaji ni

kwa mujibu wa Shari´ah ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Page 39: Fataawa Za Wanachuoni (17)

39

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=129316

38. Haitoshi Kujiita Tu Salafiy

Swali:

Baadhi ya watu wanamkataza mwenye kusema (kujiita) "Sisi ni Salafiyyuun"

na "Athariyyuun". Je, kukataza huku kunafaa? Na je, inajuzu kujinasibisha na

Salafiyyah, Athariyyah na Jaamiyyah au ni pote katika vipote?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sijui Jaamiyyah. Hakuna kundi liitwalo Jaamiyyah. Hili ni jina lililozushwa.

Halina asili. Kila mwenye kuwakhalifu [Mubtadi´ah] kwa jambo,

wanamchukia na kumpanga majina. Achane mambo haya. Ama kujinasibisha

na Salafiyyah, ni jambo zuri. Lakini lazima uwatambue Salafiyyah ni watu

gani. Wafuate kwa wema. Lakini unatakiwa kutambua madhehebu ya Salaf ili

uweze kuwafuata. Wala hakuna haja ya kujiita "Salafiy" kwa kujisifu. Usifanye

hivyo. Shikama na waliokuwemo Salaf (Wema waliotangulia) na wala

usijitakase nafsi yako ewe ndugu.

Chanzo: Fadhl-ul-´Ilm wal-´Ulamaa'

Källa: http://alfawzan.ws/allmohadrat

39. Nasaha Za al-´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy Kuhusu Baadhi Ya Mashaykh

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Page 40: Fataawa Za Wanachuoni (17)

40

Na ukitatizika na kitu wasiliana na wanachuoni waheshimiwa. Kama Shaykh

Ibn Baaz, Kama Shaykh Al-Albaaniy, Kama Shaykh Swaalih bin Fawzaan,

Kama Shaykh Rabiy´. Na mfano wa hawa ndugu zetu waheshimiwa wasiliana

nao na ustafidi kwao. Baaraka Allaahu fiykum. Hii ndo nasaha yangu kwa

ndugu zangu Waislamu. Na ninamuomba Allaah Atuhifadhie dini yetu na

Atufishe sote Waislamu.

Chanzo: http://muqbel.org/sounds.php?sound_id=8

40. Ni Yapi Madhehebu Ya al-Ikhwaan al-Muslimuun?

Swali:

Baadhi ya ndugu huenda wanatumia kauli yako kuwa kijana wa ki-Afghaniy

ni Malaika, na wanadai kuwa unawafananisha waabudu makaburi na

makhurafi kama Malaika Watukufu. Tunaomba tanbihi ya hili?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

al-Ikhwaan al-Muslimuun ndio wanasema hivi na si mimi. Ni makhurafi.

Mimi niliona kwa macho yangu makaburi na mlolongo mkubwa. Niliona hili

kwa macho yangu. Na kulikuwa ujinga, ukhurafi na Bid´ah. al-Ikhwaan al-

Muslimuun hapa walikuwa na makhurafi, na wanakuwa baina ya Salafiyyah

na mapote yote. Na wanaharibu kwa ajili ya hili. al-Ikhwaan al-Muslimuun ni

watu waovu watu wa shari. Wao ni khatari kuliko hata makhurafi. Wao

madhehebu yao itategemea na madhehebu ya mji waliopo. Kuna mmoja

anasema:

"Ninashahidilia kuwa ´Aliy ndio mpenzi wa Allaah."

Anapokuja mtu wa Yemen, anasema:

"Njooni katika kheri za Yemen."

Page 41: Fataawa Za Wanachuoni (17)

41

Kunapokuja kundi la Salafiyyuun, wanasema:

"Njooni katika mafanikio."

Hapana ndo walivyo. Katika kila mji na kila kundi wanakuwa na Dini yao. Na

walipokuja katika mji huu [Saudia] hivyo wakawa hawana budi kuwa

Salafiyyuun. Tatizo Iran ndo ndugu zao. Na Mayahudi ni ndugu zao na

Manaswara ni ndugu zao. Wanasema hivi kweli. Bali kasema hivi al-Banna.

Muulizaji:

Alisema pia Suufiyyah ni Salafiyyah.

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Hapana! Alisema:

"Hakuna baina yetu sisi [Waislamu] na Mayahudi uadui wa kidini, bali Qur-

aan imetuamrisha kinyume chake. Na Uislamu ni Dini ya kibinaadamu. Na

Qur-aan imefanya baina yetu sisi na wao ushirikiano."

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Hii ni kufuru. Hii ni kufuru tunaomba kinga kwa Allaah. Anaikadhibisha

Qur-aan.

��د وا���� أ����ا � �,+&ن أ�& ا��(س '&اوة �"��� آ ��ا ا�

“Hakika utawakuta walioshadidi kuliko watu wote katika uadui kwa

walioamini ni Mayahudi na washirikina.” (05:82)

��د وا��0(رى أو��(ء� �( أ��( ا���� آ ��ا 3 2,1�وا ا�

Page 42: Fataawa Za Wanachuoni (17)

42

“Enyi mlioamini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristokuwa ni marafiki.”

(05:51)

Kisha huyu anasema eti ni ndugu zetu?

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=WPEJ_GRsQO0

41.´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy Kuhusiana Na Maandamano

Swali:

Wanajuzisha baadhi ya watu maandamano ya amani dhidi ya mtawala

ambaye kakufuru na wanatumia hoja kwa kusema wanachuoni wamejuzisha

hilo. Je kauli yao hii ni sahihi?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Wanachuoni wamejuzisha tu kufanya Khuruuj kwa mtawala ambaye ni kafiri

dalili ziko wazi kama lionekanavyo juwa. Mpaka muone ukafiri wa wazi

kabisa wenye dalili kwa Allaah. Na demokrasia inaharibu Uislamu na si

katika Uislamu. Na maandamano si katika Uislamu. Na Waislamu hawafai

kufanya matendo kama haya. Kinachohitajika ni subira wakati wa fitina na

dhuluma za mtawala. Mpaka hapo Allaah (Ta´ala) Atapoleta nusra. Na kuna

kitabu - makala nimeandika kuhusiana na hili, wape ndugu wakisome na

wajue hukumu za Kishari´ah kwa demokrasia hizi na haya maandamano.

Mtajua hilo kwa dalili. Na nimebainisha upotofu wa wanaosema kuwa ni

katika Uislamu na ni katika kuamrisha mema na kukataza maovu. Madai haya

ni batili na si katika Uislamu. Bali katika Uislamu ni subira - kama

alivyotueleza hilo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na nimetaja kwa

dalili katika makala hii na mstaftafidi kwa jibu hili.

Page 43: Fataawa Za Wanachuoni (17)

43

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=SI3eQTaASkg

42. Ipi Hukumu Ya Kuweka Camera Msikitini?

Swali:

Ipi hukumu ya kuweka camera Msikitini kwa ajili ya kuchunga amani?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Camera ni Haramu Msikitini na nje ya Msikiti, lakini kuiweka Msikiti ni

Haramu zaidi. Mwenye kutengeneza picha amelaaniwa, na watu wataokuwa

na adhabu kali siku ya Qiyaamah ni watengeneza picha. Na Malaika

hawaingii nyumba yenye mbwa au picha. Na Mtume kakazia sana suala hili la

picha zaidi kuliko suala la Ribaa na watu waasi na matamanio. Ni watu wenye

adhabu kali siku ya Qiyaamah, watengeneza picha. Haya ndo makemeo

waliompa Fir´awn

آل >�'�ن أ�& ا�;�اب و��م 92�م ا�7('6 أد5"�ا

“Na itapofika Saa ya Qiyaamah patasemwa: "Waingizeni watu wa Firauni

katika adhahabu kali kabisa!”." (40:46)

Watu wanachukulia sahali suala la picha, wanaweka kwenye magazeti,

camera daima - unawaona Haram [Makkah na Madiynah] wanarekodi watu.

Ni vifuata mchunga vya Mayahudi na Manaswara, ni vifuata kichwa

mchunga vya Mayahudi na Manaswara. Wamesahau Sunnah ya Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), na makemeo yake makali kuhusiana na

picha na yanayofanana na hayo. Mtume (swallaSAllaahu ´alayhi wa sallam)

Page 44: Fataawa Za Wanachuoni (17)

44

aliona Qaram - koti lililokuwa na picha, akakasirika sana na akaamrisha

walitoe (´alayhis-Salaam). Na picha leo kwenye magazeti na TV ni fitina

kubwa na ni jambo liko wazi kabisa. Na hili ndo alikataza Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam). Baraka Allaahu fiykum.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=Q2ndKI5bhDs

43. Masanduku Ya Swadaqah Msikitini

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Nani kaiweka Msikitini? Yapi makusudio yao kuweka sanduku hii [ndani ya

Msikiti]?

Muulizaji:

Ni kamati.

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Ni kamati?

Muulizaji:

Ni kamati ya Msikiti.

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Page 45: Fataawa Za Wanachuoni (17)

45

Je, huwa wakiweka sanduku Msikitini daima [kila siku] au ni siku ya Ijumaa

tu au lini?

Muulizaji:

Ni kila siku wanaweka Msikitini.

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Kila siku!?

´Allaamah Rabiy´ al-Madkhaliy:

Naona hii ni njia ya Hizbiyyuun, si katika njia ya Ahl-us-Sunnah. Asli ya

kuomba omba ni Haramu! Na haijuzu isipokuwa katika hali ya dharurah -

Baraka Allaahu fiykum. Asli ya kuomba omba ni Haramu! Na mwenye

kukithiri kuomba omba atakuja siku ya Qiyaamah akiwa hana kipande cha

uso. Mmefahamu? Na hii ni njia ya Hizbiyuun - Baraka Allaahu fiykum. Yule

mwenye kutaka [... sauti haisikiki vizuri... ] na kuswali mwache aweze

kufanya hivyo, ama kumuomba omba hapana!

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=h23UFp2SudA

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.