Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

37
1 Fataawa Za Wanachuoni ´Allaamah Swaalih bin Muhammad al-Luhaydaan [20] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

description

Fataawa Za Wanachuoni 20 - ´Allaamah al-Luhaydaan

Transcript of Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

1

������� ���

Fataawa Za Wanachuoni

´Allaamah Swaalih bin Muhammad al-Luhaydaan

[20]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

3

Fataawa zilizomo:

1. Nini Maana Ya ´Ilmaaniyyah?

2. ´Aaliym Ni Katika Majina Ya Allaah (´Azza wa Jalla)

3. Allaah (Ta´ala) Alipomuumba Aadam Alimuongelesha Lugha Ipi?

4. Mtume Na Maswahabah Hawakufanya Khuruuj Wafanyazo Jamaa´at-

ut-Tabligh

5. Kuswali Nyuma Ya Imamu Mshirikina

6. Ni Kina Nani Wahaabiyyah?

7. ´Allaamah al-Luhaydaan Kuhusu Sigara

8. ´Allaamah al-Luhaydaan Kuhusu Shaykh Al-Albaaniy (Rahimahu

Allaah)

9. Hakuna Mjinga Mkubwa Katika Dini Kama Huyu!

10. Ifanye Swalah Ni Jambo Muhimu Zaidi Maishani Mwako

11. Khitmah Ni Bid´ah

12. Da´wah Kuifanyia Biashara

13. Hukumu Ya Dhikr Ya Pamoja (Kikundi)

14. Haijuzu Kumpa Wasia Mwenye Kurithi

15. Uadilifu Kwa Mwenye Mke Zaidi Ya Mmoja

16. Hukumu Ya Kusema Allaah Akimponyesha Mgonjwa Wangu

Nitamshukuru

17. Mwenye Kusema Ya Kwamba Dunia Imeumbwa

Kwa Ajili Ya Muhammad

18. Kutibu Uchawi Kwa Kutumia Uchawi

19. Radd Kwa Mwenye Kupinga Kustaawa Kwa Allaah Juu Ya ´Arshi Yake

20. Tasbiyh Ni Bid´ah

21. Kuswali Swalah Ya Usiku Jamaa´ah Nyumbani

22. Anaeswali Faradhi Anaweza Kuswali Nyuma Ya Anaeswali Sunnah?

23. Kukithirisha ´Amali Njema Kunaweza Kufuta Dhambi Kubwa?

24. Maiti Husikia Du´aa Za Wanaomuombea?

25. Mwanafunzi Katika Nchi Ya Ugenini Kuoa Kwa Nia Ya Talaka

26. Ni Lazima ´Aqiyqah Ifanywe Katika Mji Mtu Anapoishi

27. Hukumu Ya Kujiita Majina Ya Makafiri

28. Kumfunza Mke Wa Kaka Na Mke Wa Mjomba

29. Kumsusa Mubtadi´

30. Kunyanyua Mikono Wakati Wa Du´aa Baada Ya Darsa

31. Kuongea Kwenye Simu Msikitini

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

4

32. Kupewa Udhuru Kwa Ujinga

33. Kurudi Katika Mji Wa Kikafiri Kuwatendea Wema Wazazi

34. Kuswali Janaza Ya Shahidi Iliopita Miaka Mingi

35. Kusema "Sayyidna" Katika Tashahhud

36. Kusoma Qur-aan Makaburini

37. Kumsomea Maiti Suurat Yaasiyn

38. Kukabiri Baada Ya Kila Swalah Siku Ya Idi

39. Kutokwa Na Upepo Katikati Ya Twawaaf

40. Kuuza Maji Ya Zamzam

41. Allaah Hatomwangalia Mwenye Kuburuta Nguo Yake Kwa Kiburi

42. Muislamu Kupewa Udhuru Katika ´Aqiydah

43. Msafiri Wa Kunuia Kukaa Zaidi Ya Siku 3 Haruhusiwi Kufupisha Wala

Kujumuisha Swalah

44. Muziki Na kuvaa Mavazi Mafupi

45. Vitu Vimtokavyo Mwanamke Baada Ya Kukoga Janaba

46. Kufanya Bid´ah Kwa Kutokujua Kisha Mtu Akatubia Baada Ya Kujua

47. Du´aa Ya Shaykh Kwa Asiyekuwa Na Uzazi

48. Nasaha Za Shaykh al-Luhaydaan Kwa Wanandoa

49. Swahiyh al-Bukhaariy Na Muslim Hamna Hadiyth Dhaifu

50. Nyimbo Na Muziki Ni Haramu

51. Wanaume Kupiga Dufu

52. Wanawake Kumswalia Maiti

53. Wapeni Watoto Majina Ya Salaf-us-Swaalih

54. Watu Wa Peponi Hawatotatizika Katika Kumuona Allaah (Ta´ala)

55. Mjinga Kumsimamishia Hoja

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

5

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1. Nini Maana Ya ´Ilmaaniyyah?

Swali:

Ni nini ´Ilmaaniyyah? Na je, ni katika makundi 72?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Watu wanaposema ´Ilmaaniyyah wanachokusudia ni kwamba kusiwepo Dini,

bali watu wote wawe ni kama kitu kimoja. Kwa mfano asli ya mtu ni

mwarabu, kusiwepo tofauti ya Mnaswara na asiyekuwa Mnaswara, au

mshirikina na asiyekuwa mshirikina. ´Ilmaaniyyah yaani mtu asiamini Dini

yoyote. Ni katika mambo machafu mno yaliyozushwa ambayo

yamewadanganya watu wengi, wakapoteza mambo mengi ya Dini yao, na

huenda hata baadhi yao au wengi wao wakapotea (kutoka) katika Dini yao.

2. ´Aaliym Ni Katika Majina Ya Allaah (´Azza wa Jalla)

Swali:

Je, ´Aaliym ni katika Majina ya Allaah (´Azza wa Jalla), mtu akaitwa "´Abdul-

´Aaliym"?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ndio. Allaah ni Muta´aaliy. Mtu aitwe ´Abdul-Muta´aaliy.

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

6

3. Allaah (Ta´ala) Alipomuumba Aadam Alimuongelesha Lugha Ipi?

Swali:

Wakati Allaah (Ta´ala) Alimuumba Aadam (´alayhis-Salaam), kwa lugha ipi

Alimuongelesha?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Sijui nini utafaidika (kwa kuuliza swali hili)? Alimuongelesha Allaah (Jalla wa

´Alaa) kwa alichomuelewa Aadam kutoka kwa Allaah (Jalla wa ´Alaa).

Yasemekana Allaah (Jalla wa ´Alaa) Alimuongelesha Aadam kwa lugha ya

kiarabu. Lakini hili linahitajia uthibitisho.

4. Mtume Na Maswahabah Hawakufanya Khuruuj Wafanyazo Jamaa´at-ut-

Tabligh

Swali:

Yapi maoni yako kuhusu kutoka na Jamaa´at-ut-Tabliygh?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Sionelei hivyo. Na hili ni kutokana na maneno ya Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam):

"Atakayezusha katika amri yetu hii lisilokuwemo litarudishwa."

Katika upokezi mwingine:

"Atakayefanya ´amali isiyokuwa humo amri yetu, atarudishiwa."

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

7

Maswahabah ambao ni watu wenye hima na wao ni katika karne bora katika

Ummah huu, je walikuwa wakifanya hivi? Je, walikuwa wakitoka siku yoyote,

au katika wiki, au katika mwezi, au siku arubaini, je walikuwa wakifanya yote

hayo? Au walikuwa wamepitwa na kheri au kughafilika? Hapana!Kwa hivyo,

ni juu ya Ummah zilizokuja nyuma wafuate yale waliyoyafuata watu wa

kwanza wa Ummah huu. Na Kasema Imaam Maalik bin Anas:

"Hautofaulu Ummah wa mwisho huu isipokuwa kwa yale waliyofaulu kwayo

wa kwanza wao."

Kwa kheri wako nayo, na wana baadhi ya mambo yanayokwenda kinyume,

lakini yatosheleza kuwa ni ´amali ambayo haikufanya Mtume wa Allaah

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Na wala hakuna dalili ya kwamba

alielekeza hilo. Kwa hivyo, vipi hizi karne bora zitaghafilika ambazo Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kazitolea ushahidi wa kwanba ni karne

bora. Kumepita karne ya kwanza, ya pili, ya tatu, maimamu wa nne na

wanafunzi wao na karne nyingi zimepita na hawakujua katika hayo lolote ila

si chini ya miaka mia ya nyuma tu. Tunamuomba Allaah Atusamehe sisi na

wao, lakini ni juu ya Muislamu kuangalia njia aipitayo kama inaafikiana na

Shari´ah kwa kuwa Dini yote imetimia tokea uhai wa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) na imekamilika. Na kutokana na hili ndio maana Mtume

alitahadharisha Bid´ah, akasema:

"Tahadharini na mambo ya kuzusha, kwa hakika kila kitakachozushwa ni

Bid´ah na kila Bid´ah ni upotevu."

Na katika upokezi mwingine

"... na kila upotevu ni Motoni."

Ukweli ni kwamba, si kila mwenye kutaka kheri huafikiwa kuipata kheri hiyo.

Lazima kwa mwenye kutaka kufanya kheri, awe na dalili ya kheri hiyo.

5. Kuswali Nyuma Ya Imamu Mshirikina

Swali:

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

8

Ipi hukumu ya kuswali nyuma ya Imamu ambaye anajifunza uchawi na

anahudhuria walima zinazofanywa kwenye makaburi na wanayaadhimisha?

Pamoja na kujua ya kwamba ni Msikiti mmoja katika mji...

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa mna uhakika ya kwamba anajifunza uchawi na kuufunza, hukumu ya

mtu huyu iko wazi katika Qur-aan Kariym kutokana na kisa cha Haruut na

Maaruut.

���ر � � �ن �� � � ��و� إ و�� � ����ن �ن أ�د ���

"Na (hao Malaika wawili) hawamfundishi yeyote mpaka wamueleze: “Hakika

sisi ni fitnah (mtihani), basi usikufuru (kufanya uchawi).” (02:102)

Kujifunza uchawi haijuzu. Wala sionelei akaachwa kuwa Imamu

anayewaongoza watu naye yuko na sifa kama hii. Na ikiwa anahudhuria

walima zinazofanywa kwenye makaburi, hili halijuzu. Kwa nini? Je, kichinjo

kinachinjwa kwa ajili ya aliye ndani ya kaburi? Bila shaka kitendo hichi ni

upotevu. Ikiwa kumechinjwa nyama kwa ajili ya maiti, hii ni Shirki kubwa.

´Allaamah al-Luhaydaan:

Bila ya shaka, kufanya Maulidi ni Bid´ah. Kwa hakika haya Maulidi

hayajulikani kuwepo kwake katika uhai wa Mtume Muhammad (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam), wala katika uhai wa Maswahabah (Radhiya

Allaahu ´anhum), wala katika uhai wa Taabi´iyn, wala katika uhai wa

maimamu wanne, wala uhai wa wanafunzi wao. Hayakujulikana katika

ulimwengu wa Uislamu kitu kinachoitwa Maulidi kabisa. Sehemu ya kwanza

yalipopatikana ni Misri, yalizusha na Faatwimiyyuun, dola iliyokuwa chafu

ya maovu; al-Baatwiniyyah. Na yalipoanza kusambaa, katika watu wa Ahl-us-

Sunnah mtu wa kwanza aliyeanza kuyasambaza ni mfalme aitwae Irbel Iraaq

kutokana na ujinga wake wa kuwaiga Manaswara ambao na wao

wanaadhimisha siku ya ´Iysa (´alayhis-Salaam). Wakakataza wanachuoni hilo.

Yakaendelea kukua mpaka yakaenea leo katika ulimwengu wa Uislamu.

Maulidi yanaingia katika maneno ya Mtume:

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

9

"... na tahadharini na mambo ya kuzua, kwa hakika kila kitakachozushwa ni

Bid´ah na kila Bid´ah ni upotevu."

Na yanaingia katika maneno ya Mtume:

"Atakayefanya ´amali isiyokuwa humo amri yetu, atarudishiwa."

Mtu asijikurubishe kwa kitu anachokizingatia kuwa ni utiifu na kujikurubisha

kwa Allaah isipokuwa kwa dalili. La sivyo atarudishiwa mwenyewe. Na

kuichukulia siku hii kama Idi, na pengine kukafanywa makubwa zaidi ya

yanayofanywa katika Idi. Mtume alipoenda Madiynah na walikuwa Answaar

na siku ambazo wanasherehekea, akawaambia:

"Allaah Amewapa badala ya sikukuu za Kijaahiliyyah, Amewapa Idi al-Fitwr

na Id-ul-Adhhaa."

6. Ni Kina Nani Wahaabiyyah?

Swali:

Ni kina nani Wahaabiyyah? Na yapi madhehebu yao?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Neno Wahaabiyyah lilizusha maadui wa Da´wah ya Salafiyyah ambayo

ilihuishwa katika karne ya kumi na mbili Najdiy na Shayk-ul-Islaam

Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab na akasaidiwa na Muhammad bin Su´uud.

Kukakusanyika elimu pamoja na mfalme na dola ikawa dola ya Tawhiyd

kutokana na fadhila za Allaah (Jalla wa ´Alaa) kisha kwa sababu ya Da´wah

hii. Wakafanya kampeni maadui wa haki na kuiita Da´wah hii na

wanayoinusuru "Wahaabiyyah". Vinginevyo ni kwamba Shaykh na wafuasi

wake wote wako katika madhehebu na yale aliyokuwemo Imaam Muhammad

bin Hanbal na wafuasi wake. Na kuhusu ´Aqiydah yuko juu ya yale

aliyokuwemo Salaf wa Ummah huu kama Imaam Ahmad na wafuasi wake,

Shaafi´iy, Maalik na wafuasi wao. Na katika Da´wah hii hakuna

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

10

(hawakuunda) mfumo maalum na madhehebu maalum, bali madhehebu yao

ni kufuata madhehebu ya Imaam Ahmad. Isitoshe, haya madhehebu sio

lazima kwa mtu ashikamane na madhehebu yoyote, kwa hakika wanachuoni

unakuta mmoja wao mwanzoni wake yuko katika madhehebu ya Imaam

fulani, kisha anahama kwenda katika madhehebu mengine. Na kutokana na

hili kuna wanachuoni wengi maarufu (ambao hawakuwa na madhehebu

yoyote), kama mfano wa Ibn Daqiyq al-´Iyd ambaye alikuwa ni maarufu

katika karne ya saba Hijriyyah (hakuwa na madhehebu yoyoye).

7. ´Allaamah al-Luhaydaan Kuhusu Sigara

Swali:

Ipi hukumu ya kuvuta sigara?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Bila ya shaka ni katika Haramu. Kwa hakika Allaah (Ta´ala) Kawahalalishia

waja wake vitu vizuri katika riziki, na Akawaharamishia vitu vibaya. Na

siamini ya kwamba kuna mtu wa akili - hata kama mtu huyo atakuwa anavuta

- anaweza kusema sigara ni katika vitu vizuri. Si katika vitu vizuri sawa kwa

harufu yake, uchafu wake katika mwili, kuharibu mali bila ya faida yoyote ya

mwili; siamini ya kwamba kuna mtu wa akili ambaye anaweza kusema sigara

ni katika vitu vizuri (vilivyohalalishwa na Allaah). Bali hili ni katika majaribio.

Bila ya shaka ni katika vilivyoharamishwa. Mtu anapoteza mali yake bure bila

ya faida, mtu anafanya nazo maasi na maasi hayaji kwa kheri. Ni wajibu wa

kila Muislamu kujiepusha na yanayomdhuru.

8. ´Allaamah al-Luhaydaan Kuhusu Shaykh Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah)

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

11

Swali:

Kumekithiri maneno kuhusu Shaykh wetu Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah)

kwamba ana Itikadi ya Irjaa´. Je, una maneno yoyote ya kutuwekea wazi

manzila ya mwanachuoni huyu mkubwa?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Jambo la kwanza ni kuwa mtu huyu kishafariki (Allaah Amrehemu). Watu

wanatakiwa wajiepushe kwa kuwaudhi waliohai na waliokufa, isipokuwa tu

kama kutakuwepo maslahi. Na mtu huyu ana juhudi ambazo zinatakiwa

kushukuriwa (Rahimahu Allaah). Na hakulindwa na madhambi. Waliolindwa

na madhambi ni Mitume peke yao. Wengine wote, yanachukuliwa maneno

yao (yakiafikiana na haki) na yanaachwa (yakienda kinyume na haki); kama

alivyosema Maalik bin Anas.

9. Hakuna Mjinga Mkubwa Katika Dini Kama Huyu!

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kujuzisha kujenga Misikiti kwenye makaburi, na

anamtuhumu mwenye kukhalifu kauli hii kuwa ni mjinga haelewi nususi za

Dini?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa huyu si mjinga, basi ntakuwa sijui mjinga wa nususi za Dini. Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliomba Allaah Asiifanye kaburi lake kuwa

sanamu linaloabudiwa, na akawalaani Mayahudi na Maswara kwa

waliyokuwa wakiyafanya - kuyaabudu makaburi ya Mitume na watu wao

wema. Kisha kunajitokeza mtu na kusema makatazo haya si sahihi?

Je, Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walikuwa wakijenga kwenye

makaburi? ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anhu) na wengi katika Maswahabah

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

12

waliobashiriwa kuingia Peponi Madiynah waliyabomoa (majumba)

yaliyokuwa yamejengwa kwenye makaburi. Na si hao tu bali Maswahabah

wengi walifanya hivyo. Na ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anhu) alipokalifishwa na

mtu Abu al-Hiyaaj al-Asadiy na kumwambia:

"Je nikutume kwa alichonituma Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam); usiiache kaburi hata moja iliyoinuliwa isipokuwa uiweke sawa (na

zingine), wala usiache picha (sanamu) isipokuwa uiteketeze."

Maneno mfano wa haya hakuna haja wa kuyapiga Radd, yaani huyu

anayesema ya kwamba watu hawa hawafahamu Dini - kwa haya

wanayoyakataza.

10. Ifanye Swalah Ni Jambo Muhimu Zaidi Maishani Mwako

Swali:

Nimepitwa na Swalah ya Dhuhr na ´Aswr. Je, niswali kwanza ´Aswr au

Dhuhr?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapana, anza kuswali Dhuhr. Lakini jitahidi usiwe ni mwenye kupitwa na

Swalah na badala yake kuswali kila Swalah kwa wakati wake. Lifanye jambo

la Swalah ni jambo muhimu zaidi kwako, huko ni kumuiga Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam). Kimbilia pia kuinufaisha nafsi yako.

11. Khitmah Ni Bid´ah

Swali:

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

13

Katika mji wetu baada ya kuzikwa maiti, linakusanyika kundi la wanafunzi

katika nyumba ya maiti na wanasoma Qur-aan kwa nia ya kumtumia maiti

thawabu. Ipi hukumu ya hilo?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Bila ya shaka, haya ni katika mambo yaliyozushwa. Mambo ya kuzushwa

yanatofautiana athari yake, kwa ujumla yote ni Bid´ah. Maswahabah (Radhiya

Allaahu ´anhum) walikuwa wakifiwa na watoto, baba, na mama zao na

hawakuwahi kukusanyika katika nyumba ya yeyote na kusoma Qur-aan.

Wala kumueka mtu mmoja aje kusoma Qur-aan nyumbani kwa kumnufaisha

maiti wao. Kila kilichozushwa katika kujikurubisha kwa Allaah (Jalla wa

´Alaa), kinaingia katika Hadiyth ya ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anha) iliopo

katika Swahiyhayn, pale (Mtume) alipotahadharisha mtu kufanya ´amali

katika Dini hii isiyokuwa ndani yake na amri ya Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Mizani imara ya matendo yetu, ni Hadiyth:

"Atakayefanya ´amali ambayo hamna humo amri (Dini) yetu atarudishiwa

mwenyewe."

Huu ndio mzani wa ´amali zetu. Na

Hadiyth:

"Hakika ya ´amali hulipwa kutegemea kwa nia."

Mi mizani ya ´amali za moyoni.

12. Da´wah Kuifanyia Biashara

Swali:

Ipi hukumu ya kuchukulia ujira; vitabu, makala, sahifu na magazeti vya

kidini?

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

14

´Allaamah al-Luhaydaan:

Inajuzu kwa mtu kuvichukulia vitu hivi ujira. Lakini kule kutoviuza kwake na

akawa Anatafuta ujira kutoka kwa Allaah (Jalla wa ´Alaa) hili ni bora zaidi.

Hivi ni vitu vya Kishari´ah vya kheri. Inatakikana kwa kitu mtu akiweza

avifanye kwa kutafuta Wajh wa Allaah, atosheke na fadhila atazopata kutoka

kwa Allaah nazo ni bora zaidi na wala havilingani baina ya ujira huu

Ataoupata kwa Allaah na baina ya atakayempa ujira ima wa kidini au

kidunia.

13. Hukumu Ya Dhikr Ya Pamoja (Kikundi)

Swali:

Ipi hukumu ya kufanya Dhikr ya pamoja (kikundi) kwa sauti moja?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Maswahabah walikuwa hawafanyi hivyo. Bali ilikuwa kila mmoja (Allaah

Amuwie radhi) anamuiga Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa

kufanya Adhkaar zilizowekwa. Hivyo jambo hili ni uzushi katika Dhikr.

14. Haijuzu Kumpa Wasia Mwenye Kurithi

Swali:

Je, inajuzu kwa mrithi kumuusia mmoja wa warithi? Je, wasia naweza kumpa

mmoja wa watoto wangu?

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

15

´Allaamah al-Luhaydaan:

"Hakuna wasia kwa mrithi, hakika Allaah Kampa kila mwenye haki haki

yake, hakuna wasia kwa mwenye kurithi."

Haijuzu kumpa wasia mmoja wa warithi kwa chochote; si mtoto wala

asiyekuwa mtoto.

15. Uadilifu Kwa Mwenye Mke Zaidi Ya Mmoja

Swali:

Kuwafanyia uadilifu wake ni katika makazi peke yake?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Anatakiwa kufanya uadilifu kwa (yote) ayawezayo katika haki za mke. Na

Allaah Anajua mwenye kuwa na uwezo na asiyekuwa na uwezo. Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kasema kwa yule mwenye mke zaidi ya

mmoja na asiwafanyie uadilifu atakuja siku ya Qiyaamah na bega lake

limepinda; yaani atakuwa ni mwenye fedheha mbele ya watu. Uadilifu ni

jambo kubwa. Watu wanapaswa kuwa waangalifu kwa hili katika mambo

yote; awe ni muadilifu kwa kuhukumu, awe ni muadilifu kwa anachowapa

watoto na wake zake.

16. Hukumu Ya Kusema Allaah Akimponyesha Mgonjwa Wangu

Nitamshukuru

Swali:

Mtu kusema:

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

16

"Allaah Akimponya mgonjwa wangu nitamshakuru Allaah."

Je, huku ni kuweka nadhiri?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Subhaana Allaah. Na ikiwa Hakumponya hatomshukuru Allaah? Hii ni

nadhiri dhalimu. Ana azima chafu. Kwa kuwa inavyofahamika ni kwamba

ikiwa mtu huyu Allaah Hakumponyesha mgonjwa wake hatomshukuru

Allaah. Huku ni kuweka nadhiri kwa shari. Sio nadhiri bali ni shari.

17. Mwenye Kusema Ya Kwamba Dunia Imeumbwa

Kwa Ajili Ya Muhammad

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema ya kwamba dunia imeumbwa kwa ajili ya

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

Allaah Anasema:

و�� )��ت ا"&ن� وا$ س إ�� "� !دون

"Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi." (51:56)

Kisha anasema huyu mjinga mpumbavu ya kwamba imeumbwa kwa ajili ya

Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ametakasika Allaah. Ni

ajabu ilioje ya maneno haya na uongo wake. Allaah Anasema:

و�� )��ت ا"&ن� وا$ س إ�� "� !دون

"Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi." (51:56)

Hakuumba (kitu) chochote kwa ajili ya mwengine.

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

17

18. Kutibu Uchawi Kwa Kutumia Uchawi

Swali:

Huyu anauliza hukumu ya kutibu uchawi kwa kutumia uchawi?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Allaah Hakufanya kwa Ummah wa Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) dawa ya Haramu kiasi ambacho kukawa hakuna dawa nyingine

isipokuwa kwa kutumia tu dawa hiyo ya Haramu... yaani yawezekana

ikaponyesha dawa hii ya Haramu, lakini kuna dawa zingine zisizo za

Haramu. Sahihi ni kwamba si Halali kujitibu kwa kutumia uchawi. Isitoshe, ni

nani aliyekwambia kuwa maradhi haya ni uchawi? Je, ni mchawi? Wao sio

wakweli. Je, ni yule ambaye anatumia majini? Wao pia sio wa kweli. Ni nani

ambaye ni muaminifu na ni muadilifu ambaye ametoa ushahidi kuwa huu ni

uchawi?

19. Radd Kwa Mwenye Kupinga Kustaawa Kwa Allaah Juu Ya ´Arshi Yake

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema Allaah Hayuko juu ya ´Arshi na wala

Hayuko kila mahala bali Allaah hana mahala? Ipi Radd kwa kauli hii?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa hana mahala, yuko wapi sasa? Asli ya maneno haya ni kwamba

anakanusha ya kuwa hakuna mungu kabisa. Bila ya shaka huyu ni upotevu

mkubwa. Allaah Anasema:

ن ,�� ا" رش ا*�وى ـ �� ا"ر�

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

18

"Ar-Rahmaan (Mwingi wa Rahmah) juu ya ‘Arsh Istawaa (Yuko juu kwa

namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah)." (20:05)

Kisha anasema huyu mjinga "hapana" si kweli. Au akajikalifisha nafsi yake

mwenyewe na (badala ya kusema Kastawaa juu ya ´Arshi Yake) yeye akasema

Katawala. Na je, kabla ya wakati huyo alikuwa Hajatawala juu ya ´Arshi? Mtu

husema "fulani katawala kitu filani" ikiwa kabla ya hapo hajatawala kwa kitu

hicho wala hana neno lolote juu yacho. Madhehebu ya Ahl-us-Sunnah wal-

Jamaa´ah katika Qadhiya hii ndio ya haki na nususi za kutegemewa kama

ilivyokuja kutoka kwa Allaah na kwa Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam). Hii ndio Manhaj ya watu wa haki.

20. Tasbiyh Ni Bid´ah

Swali:

Muulizaji anauliza hukumu ya Tasbiyh?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Tasbiyh sio katika Sunnah. Ataeichukulia kuwa ni Sunnah, basi (ajue kuwa) ni

Bid´ah. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akimsabihi Allaah

kwa vidole vya mikono yake. Na alipoambiwa ´Abdullaah bin Mas´uud ya

kwamba kuna watu wanaleta tasbihi kwa mawe, na walikuwa ni katika

wanafunzi wa ´Abdullaah bin Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anhu), na kwamba

wanakusanyika mahala. Watu katika wakati huo hawakuwa na Tasbiyh.

Akatoka (Ibn Mas´uud) na kukaa nao. Kulikuwa mmoja wao anayesema

"Semeni mia", basi wanamsabihi Allaah mara mia na wakiendelea kufanya

vivyo hivyo. Alipohakikisha hilo (Ibn Mas´uud), akawaambia "Je, nyinyi ni

waongofu zaidi kuliko Maswahabah wa Mtume Muhammad au mmetuletea

tu Bid´ah? Tendeni ´amali zenu zitahifadhiwa. Atawakataza na akachukulia

hilo ni katika Bid´ah. Wamesema hili wanachuoni walioandika vitabu kuhusu

Bid´ah na baadhi yao ni katika wanachuoni wa Maalikiyyah wa Indonesia.

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

19

21. Kuswali Swalah Ya Usiku Jamaa´ah Nyumbani

Swali:

Je, inajuzu kuswali Qiyaam-ul-Layl (Swalah ya usiku) nyumbani usiku?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ndio, inajuzu.

22. Anaeswali Faradhi Anaweza Kuswali Nyuma Ya Anaeswali Sunnah?

Swali:

Inajuzu kutofautiana nia ya maamuma na Imamu katika Swalah?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ndio, inajuzu. Inajuzu mwenye kuswali Swalah ya faradhi kuswali nyuma ya

mwenye kuswali Swalah ya Naafil (Sunnah), au kinyume chake. Na wala

hakuna neno kufanya hivyo In Shaa Allaah.

23. Kukithirisha ´Amali Njema Kunaweza Kufuta Dhambi Kubwa?

Swali:

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

20

Je, dhambi kubwa inaweza kufutwa kwa kufanya ´amali njema?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ndio linawezekana. Lakini elimu yake iko kwa Allaah, sisi hatuwezi kujua

hilo. Mtu akifanya ´amali nyingi na akatubia kwa Allaah (Jalla wa ´Alaa),

inakuwa ni Tawbah (katubia kwa Allaah) isipokuwa tu kama kuna haki ya

waja (umechukua), hili halikafiriwi kwa Tawbah. Tawbah inapokelewa kwa

yale ambayo ni baina yako wewe na Allaah (Jalla wa ´Alaa). Ama haki za

waja, ni lazima kuzirudisha. Isipokuwa tu kama mtu huyo atakusamehe, au

Akakuridhia Allah (Jalla wa ´Alaa).

24. Maiti Husikia Du´aa Za Wanaomuombea?

Swali:

Je, maiti husikia Du´aa za watu wanaowaombea walio hao?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ndio wanasikia. Kafiri anasikia yanayomuudhi na kumbughudhi, na

muumini anasikia yanayomfurahisha na kumridhisha. Lakini hawezi kujibu.

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) siku ya Badr alipowaita waliouawa

katika vita vya Badr. Akamwambia ´Umar "Vipi utawaita watu wasiosikia?"

Akasema "Wanasikia mnayowaambia, lakini hawawezi kujibia." Waumini

wanasikia Du´aa za waumini wanazowaombea, lakini hawawezi kujibia.

25. Mwanafunzi Katika Nchi Ya Ugenini Kuoa Kwa Nia Ya Talaka

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

21

Swali:

Mimi ni kijana naishi katika mji wa kikafiri kwa ajili ya masomo. Je, inajuzu

kwangu kuoa kwa nia ya Talaka kwa kujizuia na fitina?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Kuoa kwa ni ya Talaka kunakurubiana na Mut´ah ambayo ameiharamisha

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) iliyokuwa inaruhusiwa katika

Jaahiliyyah. Kisha ikaharamishwa kama lilivyothibiti hilo katika upokezi

mwingi wa Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) ´Aliy na wengine. Kuoa

kwa nia ya Talaka, mtu akanuia ni kwa Mut´ah tu na akawa na azima ya

kutokuwamke wake, hili ni katika mambo wamekhitilafiana wanachuoni. Na

bila ya shaka kauli ya sahihi ni kwamba ni Haramu. Ikiwa umelazimika kuoa,

oa na weka nia na uazimie kwamba ikiwa atakuwa mwema, atakuwa mke

wako; na ikiwa hakuwa mwema Allaah Kajaalia kwa yule mambo

yamemkuwia mazito ataliki. Lakini asioe kwa kunuia kutaliki. Jambo hili

linakwenda kinyume na misingi iliyowekwa ya ndoa na Allaah (Jalla wa

´Alaa) kwa watu.

26. Ni Lazima ´Aqiyqah Ifanywe Katika Mji Mtu Anapoishi

Swali:

Nimepata mtoto wa kiume na niko na pesa kidogo. Je, inajuzu kwangu

kumfanyia ´Aqiyqah katika mji wa Kiislamu usiyokuwa wangu ambapo

kunaruhusiwa kufanya ´Aqiyqah?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hakuna ubaya kufanya hivyo. Muhimu tu kufanywe ´Aqiyqah.

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

22

27. Hukumu Ya Kujiita Majina Ya Makafiri

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kujiita kwamajina ya baadhi ya makafiri?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Akiitwa kwa majina ya baadhi ya makafiri, dogo tuwezalo kusema ni kwamba

hii ni aina ya kujifananisha nao. Na Mtume Anasema:

"Mwenye kujifananisha na watu, basi yeye ni katika wao."

Tunamuomba Allaah Atukinge. Kipi kinachomkataza kuitwa majina ya

Kiislamu na waislamu. Na lau angeenda katika vitabu angepata majina mengi

sana. Hakuitwa majina ya baadhi ya makafiri isipokuwa ni kwa sababu

amevutika nao.

28. Kumfunza Mke Wa Kaka Na Mke Wa Mjomba

Swali:

Je, inajuzu kumfunza mke wa kaka au mke wa mjomba?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ama kubainisha tu kitu, hakuna ubaya kufanya hivyo. Ama kukaa pamoja

naye na kumfunza, kufanya darsa kabisa na pengine hata wakawa ni wao

peke yao hili halijuzu. Ama kule kumueleza tu Halali na Haramu, hakuna

ubaya kufanya hivyo.

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

23

29. Kumsusa Mubtadi´

Swali:

Ni ipi dhawabiti ya kumsusa Mubtadi´?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ukiweza kumnasihi na kumuelekeza na kumuonesha haki, fanya hivyo. Na

ikiwa hatokubali, achana naye.

30. Kunyanyua Mikono Wakati Wa Du´aa Baada Ya Darsa

Swali:

Je, inajuzu kwangu nitapokutana darsa Msikitini niombe baada ya darsa na

kunyanyua mikono yangu na wanyanyue wasikilizaji mikono yao?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hakuna ubaya kufanya hivyo. Kwa hakika kunyanyua mikono wakati wa

Du´aa, ni sababu ya kukubaliwa Du´aa kama ilivyo katika Hadiyt ilioko katika

Swahiyh. Na ninakumbuka ya kwamba as-Suyuutwi (Rahimahu Allaah)

kaandika Risaalah kuhusu kunyanyua mikono wakati wa Du´aa. Na anasema

Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah:

"Hakika ni katika Sunnah kunyanyua mikono wakati wa kuomba Du´aa."

Lakini kunyanyua mikono, isiwe ni kama wanavyofanya baadhi ya watu

wanapotoa Salaam wananyanyua mikono kuomba Du´aa moja kwa moja na

wamemaliza. Akitaka kuomba Du´aa hakuna ubaya akanyanyua mikono,

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

24

isipokuwa tu wakati wa Du´aa kuitikia "Aamiyn" katika Khutbah ya siku ya

Ijumaa. Inatakiwa kwa msikilizaji kutulia na kukaa kimya, hakuna neno

akaitikia Aamiyn kwa sauti ya chini asijishawishi mwenyewe na wenye

kuswali.

31. Kuongea Kwenye Simu Msikitini

Swali:

Ipi hukumu ya kuongea kwenye simu ndani ya Msikiti?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Kule kuongea tu hakuna ubaya, ikiwa sio maongezi mabaya. Kama jinsi

anavyoweza kuongea na mtu, inajuzu kwake kuongea na swahibu wake kwa

simu, bila ya kuwashawishi watu.

32. Kupewa Udhuru Kwa Ujinga

Swali:

Je, mtu anaweza kupewa udhuru katika mambo ya ´Aqiydah?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Shirki kubwa hapewi udhuru yeyote. Mwenye kumuabudu asiyekuwa Allaah

(Jalla wa ´Allaa), hakuna yeyote awezae kumpa udhuru na kusema ni mjinga.

Je, huyu anayemuabudu anaona kuwa anamiliki kunufaisha na kudhuru,

kupatikana kwa kitu na kukosena, kutajirisha na kufukarisha? Ama baki ya

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

25

´amali ambazo sio ´Ibaadah na sio Shirki, yule ambaye hajui uhakika wake na

kwa mtu kama yeye inawezekana kweli akawa hajui, Allaah Kasema:

! ث ر*ول � !�ن ��� �� � ذ � و�� �

"Na Hatukuwa Wenye kuadhibu (yeyote) mpaka Tupeleke Mjumbe

(kuwaonya)." (17:15)

Na ni lazima kumsimamishia hoja. Lakini asibaki mtu katika ujinga na

kusema mimi ni mwenye kupewa udhuru. Akafanya apendacho na kusema

mimi sijui kuwa ni Haramu, hapana! Ni lazima aulize na ajifunze. Ama

kuhusu Shirki:

3 � 2��ر أن 5�رك !3 و2��ر "ك "�ن �5�ء إن� ا"�ـ� �� دون ذ

"Hakika Allaah Haghufuri kushirikishwa; na Anaghufuria yasiyokuwa hayo

kwa Amtakae." (04:48)

Ni lazima kwa mja kujiepushe na kila kitachomuingiza Motoni. Moto wa

duniani ambao ni dhaifu mara mia kuliko Moto wa Aakhirah, yatosha kuwa

onyo, vipi kwa Moto wa Aakhirah?

33. Kurudi Katika Mji Wa Kikafiri Kuwatendea Wema Wazazi

Swali:

Je, inajuzu kwa aliyefanya Hijrah kurudi katika mji wa kikafiri ili kuwatendea

wema wazazi wake?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa kurudi kwake hawezi kudhihirisha Dini yake, haijuzu kwake kurudi.

Na ikiwa kurudi katika mji wake ataweza kuidhihirisha Dini yake na wala

haitomtatiza na wazazi wake ni Waislamu, arejee kwa kuwa kuwatendea

wema wazazi na kuwaangalia ni aina ya Jihaad.

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

26

34. Kuswali Janaza Ya Shahidi Iliopita Miaka Mingi

Swali:

Mimi naishi mji wa mbali, jeinajuzu kwangu kuswali Swalah ya Janaza

kuwaswalia mashahidi waliokufa katika vita ya Uhud?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapana waombee maghfirah. Swalah ya Janaza, haiswaliwi Janaza ambayo

imeshapita miaka 1.400 na zaidi ya miaka 20. Na hili halikufanywa na Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), wala Maswahahah wala Taabi´uun.

Isitoshe waliokufa katika Uhud, asli ni kwamba haswaliwi anaekufa katika

Jihaad.

35. Kusema "Sayyidna" Katika Tashahhud

Swali:

Kusema "Sayyidna Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)" katika

Tashahhud ndani ya Swalah inajuzu au hapana?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapana haijuzu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwafunza nini

watachosema Maswahabah katika Swalah zao na Tashahhud zao, walikuwa

wakisema:

"Allaahumma Swalli ´alaa Muhammad" kama ilivyo katika Hadiyth ya Ibn

Mas´uud. Hakukuthibiti neno "Sayyidna" (Bwana wetu). Bila shaka yeye ni

bwana wa wanaadamu wote. Lakini tukomeke katika ´Ibaadah zetu kwa yale

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

27

tuliyojifunza. Mtume alipoambiwa "Tufunze ni vipi tutakuswalia". Hakusema,

semeni "Allaahumma Swali ´alaa Sayyidna Muhammad." Kawafunza ni vipi

watamswalia na ndio Swalah bora kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam); Swalah hizo ambazo watu walijifunza kutoka kwake nazo

ni Hadiyth Swahiyh. Kwa hivyo, mtu asiseme katika Swalah yake "Ashhadu

anlaa ilaaha illa Allaah, wa ashhadu anna Sayyidna Muhammad RasuuluLlaah",

hapana akomeke na aliyosema Mtume wa Allaah. Mtume wa Allaah ni mjuzi

zaidi wa haki ya ´Ibaadah hii kuliko kiumbe mwengine yeyote.

36. Kusoma Qur-aan Makaburini

Swali:

Je, inajuzu kusoma Qur-aan kwenye kaburi? Kuna baadhi ya Mahanafiy

wanadai ya kwamba kuna Hadiyth 23 zinatoa dalili kujuzu kusoma Qur-aan

kaburi na kwamba ni Hadiyth Swahiyh.

´Allaamah al-Luhaydaan:

Haikuthibiti ya kwamba Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum)

walipokuwa wakienda makaburini walikuwa wakisoma Qur-aan. Na Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuamrisha kisomo [kwenye makaburi].

Na kusema kwake kwamba [kuna Hadiyth Swahiyh], lau angetutajia Hadiyth

moja tu katika Hadiyth hizi ilituiangalie ukweli wake.

37. Kumsomea Maiti Suurat Yaasiyn

Swali:

Ipi hukumu ya kusoma Suurat Yaasiyn kwenye kaburi?

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

28

´Allaamah al-Luhaydaan:

Haijuzu. Haijuzu kwa mtu kwenda makaburini ili kusoma Qur-aan huko.

Qur-aan inasomwa Misikitini na majumbani. Ama makaburini, lililothibiti ni

waliohai kuwatolea Salaam waliokufa:

"Assalaam ´alaykum daara qawmin mu-uminiyn."

Awaombee maghfirah, na wala asiwasomee Qur-aan.

38. Kukabiri Baada Ya Kila Swalah Siku Ya Idi

Swali:

Siku za ´Iyd-ul-Adwhaa tunakabiri kwa sauti baada ya kila Swalah. Je, hili

linajuzu?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Inajuzu. Watu walikuwa wakikabiri hata Mina, alikuwa ´Umar akikabiri na

watu nao wakikabiri na wakipandisha sauti. Lakini si kwa Takbiyra sauti ya

pamoja. Kila mmoja akabiri...

39. Kutokwa Na Upepo Katikati Ya Twawaaf

Swali:

Mwenye kufanya ´Umrah akitokwa na upepo katikati ya Twawaaf yake. Je,

atoke ili atawadhe kisha arudi au akamilishe atapomaliza?

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

29

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapana atoke. Mtume (´alayhis-Salaam) kasema kwamba kutufu katika

Ka´abah ni Swalah, na Swalah imeshurutishwa kuwa na Twahara. Anatakiwa

kutoka atawadhe kisha akirudi akamilishe pale alipokuwa ameishia.

40. Kuuza Maji Ya Zamzam

Swali:

Je, inajuzu kuuza maji ya zamzam?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Atakayechukua maji ya mzamzam, inakuwa ni yeye ndiye mwenye

kuyamiliki. Akitaka kuyauza inajuzu.

41. Allaah Hatomwangalia Mwenye Kuburuta Nguo Yake Kwa Kiburi

Swali:

Vipi kuvaa Isbaal?

´Allaamah al-Luhaydaan:

"Allaah Hatomwangalia mwenye kuburuta nguo yake kwa kiburi."

"Kilichoko chini ya kongo mbili za miguu ni Motoni."

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

30

Kunaingia humo kubuta nguo ikiwemo na suruwali. Nguo ya muumini

inapaswa kuwa katikati ya mguu, na wala hakuna ubaya ikiwa itafika mpaka

kwenye kongo mbili za miguu. Na kilichoko chini ya kongo mbili za miguu ni

Motoni. Na kumekuja Hadiyth nyingi kuhusiana na hili.

"Allaah Hatomwangalia mwenye kuburuta nguo yake kwa kiburi."

42. Muislamu Kupewa Udhuru Katika ´Aqiydah

Swali:

Baadhi ya Madu´aat katika nchi ya Urusi wanasema mwenye kuishi Urusi

wao wako na udhuru kwa ujinga katika ´Aqiydah. Vipi kuwaradi?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ujinga ambao hakukupatikana sababu ya kuuondoa, yawezekana ikawa ni

kweli. Lakini kumshirikisha Allaah, hakuna mtu yeyote anayepewa udhuru.

Kwa mfano mtu hawezi kuabudu sanamu na kaburi na kusema kuwa alikuwa

hajui kuwa haijuzu, kwa kuwa angelifirikia kwa akili yake ataona kuwa

anayemuabudu badala ya Allaah hamiliki si mauti, uhai wala ufufuo. Ama

mambo ambayo hayafikiwi isipokuwa mpaka kwa elimu na akakosa mtu

mwalimu wa kumfunza, kwa mfano kazaliwa katika mji wa kikafiri na wala

hakupata wa kumfunza Swalah, idadi yake, wakati wake; anasema kuwa ni

Muislamu lakini hakuna yeyote wa kumfunza, huyu anapewa udhuru kwa

hili lakini hapewi udhuru kwa kuabudu asiyekuwa Allaah.

43. Msafiri Wa Kunuia Kukaa Zaidi Ya Siku 3 Haruhusiwi Kufupisha Wala

Kujumuisha Swalah

Page 31: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

31

Swali:

Ikiwa mtu ni msafiri na akafika Madiynah anapoenda. Je, inajuzu kwake

kujumuisha Swalah muda ataokuwepo hapo?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa Madiynah anapokwenda hakunuia kubaki zaidi ya siku nne, bali kanuia

kukaa siku tatu na siku ya nne kurudi, kauli ya sahihi ni kwamba hairuhusiwi

kwake kujumuisha wala kufupisha. Kwa kuwa asli ya kubaki ni kwamba mtu

asifupishe Swalah wala kujumuisha na nyingine isipokuwa tu kwa haja.

Kinachoruhusiwa katika safari ni kufupisha Swalah, ama kujumuisha ni

ruhusa [dharurah] imewekwa kwa mwenye kuihitajia. Kauli ya jamhuri ya

wanachuon ni kwamba kuchukua ruhusa ya safari, haiwi kwa mtu ambaye

amenuia kukaa zaidi ya siku nne. Wamechukua kwa yale wayajuayo kwa

yakini kwamba Mtume alifasiri akafupisha na hilo ilikuwa ni wakati wa Hajj

peke yake, ama kabla ya hapo haijulikani kama alikuwa anajua lini safari yake

itaisha.

44. Muziki Na kuvaa Mavazi Mafupi

Swali:

Kumeenea kukithiri kwa muziki na [wanawake wanaovaa] mavazi mafupi

yanayokhalifu haya. Ipi nasaha kwa watu hawa?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Twatumai - In Shaa Allaah - hapa Msikitini hakuna mmoja katika watu hao.

Na tunamuomba Allaah Awaongoze.

Page 32: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

32

45. Vitu Vimtokavyo Mwanamke Baada Ya Kukoga Janaba

Swali:

Ipi hukumu ya kutokwa na "saail" (ni maji maji yanayotoka kwenye tupu ya

mwanamke) baada ya kukoga janaba na kuendelea kutoka huku hata wakati

wa kuswali faradhi?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa yataendelea kumtoka, hukumu yake ni kama hukumu ya mwenye

maradhi ya kutokwa hovyo na mkojo. Sio wajibu kukoga... Ikiwa yanaendelea

kumtoka, hukumu yake ni kama ya mwenye maradhi ya kutokwa hovyo na

mkojo. Atatawadha katika kila Swalah ya faradhi.

46. Kufanya Bid´ah Kwa Kutokujua Kisha Mtu Akatubia Baada Ya Kujua

Swali:

Je, husamehewa mwenye kufanya Bid´ah kwa kutokujua na alikuwa na nia

nzuri?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapana. Kwanza Bid´ah ni upotofu. Na Hadiyth:

"Na kila Bid´ah ni upotofu."

Katika lafdhi nyingine:

"Na kila upotofu ni Motoni."

Njia ya kuingia Motoni haiwi sababu ya kusamehewa, isipokuwa ikiwa njia

hii ya Motoni mtu alijirejea na ikawa mja huyu kila anapokumbuka

Page 33: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

33

alichokifanya anatubia upya na kuomba msamaha... Bid´ah mtu hasamehewi

kwayo. Lakini akijuta au akajua kisha akatubia, atasamehewa kwa Tawbah

yake.

47. Du´aa Ya Shaykh Kwa Asiyekuwa Na Uzazi

Swali:

Niombee kwa Allaah afya mimi sina uzazi?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Tunamuomba Allaah Akupe afya na Amponye kila mgonjwa katika

wagonjwa wa Waislamu. Awape afya nzuri kwenye miili yao na roho zao na

akili zao. Na Ummah wa Kiislamu aupe hali nzuri kwa sasa na katika

Mustaqbal.

48. Nasaha Za Shaykh al-Luhaydaan Kwa Wanandoa

Swali:

Mimi nataka kuoa, waniusia nini?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ninakuusia kumcha Allaah (Jalla wa ´Alaa) na kumshukuru kwa

Aliyokukadiria katika ndoa hii. Umhimize mke wako kuhifadhi Swalah tano

kwa wakati wake, kuwa na heshima na kujisitiri, kusaidiana na kuishi kwa

Page 34: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

34

wema. Ninamuomba Allaah Awape watoto wema na mapatano katika maisha

yenu ya ndoa, na afanye iwe hivyo kwa kila wanandoa.

49. Swahiyh al-Bukhaariy Na Muslim Hamna Hadiyth Dhaifu

Swali:

Je, katika Swahiyh al-Bukhaariy na Muslim kuna Hadiyth dhaifu?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapana. Swali hili halina maana. Wakusudia nini, wataka kusema kwamba

kuna mwanachuoni yeyote anayesema kwamba katika al-Bukhaariy kuna

Hadiyth dhaifu? Ummah mzima umekubaliana kwa Swahiyh al-Bukhaariy na

Muslim kuwa ni Hadiyth Swahiyh. Maswali kama haya hayana kheri.

50. Nyimbo Na Muziki Ni Haramu

Swali:

Ipi hukumu ya kusikiliza nyimbo na muziki?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Kusikiliza nyimbo zenye ala ya taarabu, bila ya shaka ni Haramu.

51. Wanaume Kupiga Dufu

Page 35: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

35

Swali:

Hukumu ya wanaume kupiga dufu?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Dufu kawaruhusu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati wa

harusi kwa wanawake. Wanaume wanatakiwa kujiepusha nayo.

52. Wanawake Kumswalia Maiti

Swali:

Ipi hukumu ya wanawake kumswalia maiti Jamaa´ah nyumbani?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Ikiwa maiti yuko katika nyumba ambapo kuna wanawake, na wakamswalia

[maiti] kabla hajatolewa nje kwenye Muswalla, hakuna ubaya kufanya hivyo.

53. Wapeni Watoto Majina Ya Salaf-us-Swaalih

Swali:

Nimeruzukiwa mtoto, unaninasihi nimwite vipi?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Page 36: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

36

Mpe jina mojawapo la wanawake wa Salaf-us-Swaalih (wema waliotangulia);

mwite Khadiyjah, Ruqayyah, Faatwimah, ´Aaishah, Zaynab. Majina ni mengi.

54. Watu Wa Peponi Hawatotatizika Katika Kumuona Allaah (Ta´ala)

Swali:

Je, watu wa Peponi wanatofautiana katika kumuona Allaah (´Azza wa Jalla)?

Kuna ambao watakuwa wakimuona kila siku, wengine kila baada ya siku

mbili, wengine kila wiki.

´Allaamah al-Luhaydaan:

Hapakuja kitu chochote kuhusiana na hayo katika Hadiyth. Lililothibiti ni

kwamba watamuona Allaah (Jalla wa ´Alaa), na kwamba hawatosongamana

katika kumuona, na hawatotatizika katika kumuona, na kwamba watamuona

kama wanavyoona mwezi mweupe usiku wa Badr.

55. Mjinga Kumsimamishia Hoja

Swali:

Vipi mtu atapata kumsimamishia hoja mjinga?

´Allaamah al-Luhaydaan:

Kwa kumsimamishia hoja.

Page 37: Fataawa Za Wanachuoni (20) - ´Allaamah al-Luhaydaan

37

Chanzo:

http://www.alharamain.gov.sa/index.cfm?do=cms.scholarsubject&schid=309

81&subjid=31339&audiotype=lectures&browseby=speaker

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.