Fataawa Za Wanachuoni (31)

36
1 علماء ال فتاوىFataawa Za Wanachuoni [31] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

description

Fataawa Za Wanachuoni (31)

Transcript of Fataawa Za Wanachuoni (31)

Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (31)

1

فتاوى العلماءFataawa Za Wanachuoni

[31]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (31)

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (31)

3

Fataawa zilizomo:

1) Kukufurisha Na Kubadiy´ Ni Kazi Ya Wanachuoni

2) Kuhiji Kwanza Au Kufanya Hijrah?

3) Tuko Ufaransa Na Hatuna Wanachuoni, Twaomba Nasaha Zenu

4) Tofauti Ya Wanawake Wa Leo Na Maswahabah Wa Kike

5) Swali Kuhusiana Na Sijda Ya Kusahau

6) Je, Salafiyyuun Wanafarakanisha Waislamu?

7) Nasaha Ya Shaykh Rabiy´ Kuhusiana Na Mashaykh Wawili

8) Nasaha Kwa Watafutaji Elimu (Wanafunzi)

9) Mwanamke Kupanda Gari Ya Mwanaume Na Mke Wake Bila Ya Mahram

10) Ibara "Lau Bila Ya Allaah Kisha Wanachuoni"

11) Hukumu Ya Raafidhwah (Mashia) Wote Ni Moja

12) Hukumu Ya Kusikiliza Mawaidha Ya Watu Wa Bid´ah Kama ´Aa´idh al-Qarniy

13) Hukumu Ya Kufuturu Kabla Ya Kuzama Jua

14) Da´wah Na Acha Kuingilia Makundi Potofu

15) ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Bia Isiyokuwa Na Pombe

16) Shaykh Mahiyr Qahtwaaniy Kuhusu Kumsikiliza Khaalid ar-Raashid

17) Hukumu Ya Wanawake Kuzuru Makaburi -2-

18) Tofauti Ya Hadiyth al-Qudsiy Na Hadiyth Za Mtume Za Qur-aan

19) Mke Wangu Anasema Uongo Sana

20) Kujifunza Mwenyewe - Maradhi Khatari Ya leo Je, Katika Zama Hizi Kuna

Maulamaa Wa al-Jarh Wa Ta´adiyl?

21) Je, Katika Zama Hizi Kuna Maulamaa Wa al-Jarh Wa Ta´adiyl?

22) Haijuzu Kwa Mwanamke Kuvaa Suruwali Yoyote Kwa Hali Yoyote

23) Shaykh Yahyaa al-Hajuuriy Kuhusu al-Halabiy

24) Wale Wasiopenda Kuzungumziwe Manhaj Ahl-is-Sunnah wal Jamaa´ah

25) Mwanamke Kuvaa Punjabi Yenye Suruwali

26) Lipi La Kufanya Unapojiwa Na Mawazo Mabaya?

27) Kufunga Siku Ya Maulidi Ya Mtume (´alayhis-Salaam)

28) Ipi Hukumu Ya Kutawadha Bafuni?

29) Hukumu Ya Kulala Kwa Tumbo (Kifudifudi)

30) Hadiyth Dhaifu Ya Mu´aadh (Radhiya Allaahu ´anhu)

31) Anampiga Binti Yake Kwa Kumtomsikiliza Yeye Na Mama Yake

32) ´Allaamah ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad Kuhusu Anashiyd

33) Usufi Si Katika Uislamu

34) Radd Kwa Jabriyyah Na Qadariyyah

35) Muislamu Aliyeacha Swalah Ni Kafiri Na Lazima Auawe

36) Lini Kuhukumu Kinyume Na Aliyoteremsha Allaah Mtu Anakuwa Kafiri?

37) Kitabu Na Sunnah Vinatangulizwa Kabla Ya Ijmaa´

38) Imaam Abu Haniyfah, Imaam Wetu, Kiigizo Chetu

39) Kumtolea Mtu Swadaqah Kwa Kuswali Naye Baada Ya Swalah Ya ´Aswr Na Fajr

40) Ipi Bora Kwa Wanawake Kuswali Jamaa´ah Au Kila Mtu Kivyake?

41) Inajuzu Kumhukumu Mtu Moja Kwa Moja Kuwa Ni Mnafiki?

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (31)

4

42) Hukumu Ya Kufanya Mazoezi Katika Ukumbi Za Muziki

43) Anashiyd (Qaswiydah) Ni Haramu

44) Mume Na Mke Wanadanganya Serikali Wameachana Ili Wapate Pesa Zaidi

45) Msikiti Unaokhatimu Qur-aan Na Usiyokhatimu, Wapi Nifanya I´tikaaf?

Wanachuoni waliomo:

1) Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

2) Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

3) ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy

4) ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

5) ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh

6) ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy

7) ´Allaamah Zayd bin Haadiy al-Madkhaliy

8) Shaykh Muhammad bin Haadiy al-Madkhaliy

9) ´Allaamah Swaalih Aal ash-Shaykh

10) Shaykh Ahmad bin ´Umar Bazmuul

11) Shaykh Abu ´Abdul-Haliym ´Abdul-Haadiy

12) Shaykh Yahyaa al-Hajuuriy

13) Shaykh Mahiyr al-Qahtwaaniy

14) ´Allaamah ´Abdir-Rahmaan al-Baraak

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (31)

5

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1) Kukufurisha Na Kubadiy´ Ni Kazi Ya Wanachuoni

Swali:

Ni haki ya Muislamu kumkufurisha [Takfiyr] au Tabdiy´ kwa kila ambaye

atatumbukia katika kufuru au Bid´ah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Msukumo wa kuwahukumu watu na Takfiyr na Tabdiy´, hili halijuzu

isipokuwa kwa wanachuoni, ambao wanajua mipaka ya kufuru, Bid´ah,

kuritadi na sababu zake wanazijua wanachuoni. Hili ni jambo khaswa kwa

wanachuoni. Haijuzu kwa yeyote kumhukumu mwenzake kwa Bid´ah,

kufuru, Shirki naye hajui sharti za Takfiyr, Tabdiy´ na madhambi. Mtu

auhifadhi ulimi wake. Kuna khatari akamwambia mtu ambaye siye, kwamba

ni kafiri, mtu wa Bid´ah, mpotofu, fasiki. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) anasema:

"Atakayemwambia ndugu yake "wewe kafiri!" naye si hivyo, maneno yake

yatarejea kwake".

Maneno yake yatarejea kwakwe mwenyewe, A´udhubi Allaah. Ni juu ya

Muislamu kuhifadhi ulimi wake na asiuache ukawa huru katika masuala

kama haya. Ni jambo khatari. Yanahitaji mtu kwanza asome na ajue masharti

ya Takfiyr, Tabdiy´, Tafsiyq na si kuongea tu kwa ujinga, hisia, hamasa au

ushujaa. Anaweza kutumbikia katika makosa na maneno yake yakamrejea

mwenyewe. Masuala haya ni khatari sana. Na haya maneno ambayo ulisema

katika kukufurisha watu, Tabdiy´ au Tafsiyq hayaachwi hivi hivi. Ikiwa

wanastahiki hayo, yanaenda kwao. Na kama hawayastahiki yanakurejelea

wewe. Ni juu yako kuuhifadhi ulimi wako katika masuala haya.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127359

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (31)

6

2) Kuhiji Kwanza Au Kufanya Hijrah?

Swali:

Mimi nina mali inayotosha kwa Hajj tu, na mimi naishi katika mji wa kikafiri,

lipi aula zaidi kwangu Hajj au kufanya Hijrah kwa kuzingatia ya kwamba

mali hii haitoshi kufanya Hijrah?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Ikiwa mali hii haikutoshi kufanya Hijrah na wewe unataka kutanguliza

kwanza kufanya Hajj, hakuna ubaya kutanguliza kwanza Hajj. Kwa kuwa

Hijrah inahitajia kwako kujikalifisha na safari, kuandaa nyumba ambapo

utaishi na mfano wa hayo, uzito utakuwa mwingi. Ikiwa hali ni kama hivyo,

ni juu yako kwanza kutanguliza kufanya Hajj. Lakini kadiri utavyoweza

katika siku za mbele ni wajibu kwako kuhama, kwa kuwa kufanya Hijrah ni

wajibu.

Chanzo: http://youtu.be/LNQ1ozM7OUo

3) Tuko Ufaransa Na Hatuna Wanachuoni, Twaomba Nasaha Zenu

Swali:

Mi naishi Ufaransa, kwa ukosefu wetu wa wanachuoni twatafuta elimu

kupitia vitabu kama cha Tawhiyd cha Shaykh Ibn ´Abdil-Wahhaab, kitabu

Sharh al-Mumtiy´ cha Ibn ´Uthaymiyn na visivyokuwa hivyo kama (vitabu)

vya Ibn Baaz, al-Albaaniy, al-Fawzaan, ´Abdu-´Aziyz Aal ash-Shaykh na mimi

huwa nikirejea kwa wanachuoni ninapokuwa na swali na masuala ya utata,

ipi nasaha yako kwetu?

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (31)

7

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Endelea kutafuta kwako [elimu], na tunawaombea kwaAllaah mafanikio.

Chanzo: http://youtu.be/DAlq8d8YNek

4) Tofauti Ya Wanawake Wa Leo Na Maswahabah Wa Kike

Swali:

Siku hizi twasikia sana kwamba mke si lazima kumhudumia mume wake

kama vile kupika na kufua nguo. Tunaomba kutoka kwako ufafanuzi

kuhusiana na suala hili.

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwanamke leo kaendelea na wala hamhudumii mume wake. Leo wakati una

haja ashughulikie moja katika haja zako, hayupo nyumbani. Mume anakuja na

kukaa nyumbani na kusubiri, mke haji ila mpaka ifike mwisho wa usiku.

Wanawake wa leo wamekuwa waasi. Ni katika Sunnah wanawake

kumhudumia mume wake. Maswahabah wa kike (Radhiya Allaahu

´anhunna) walikuwa wakiwahudumia waume zao; walikuwa wakipika,

wakiangalia mambo ya nyumbani. Isitoshe ni Maswahabah wa kike,

wanawake bora katika Ummah. Fatmah bint Muhammad (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) na (Radhiya Allaahu ´anha) alikuwa akibeba maji kwenye

mgongo wake mpaka kamba ikaacha alama kwenye mgongo wake.

Alimuomba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ampe mtumishi

akakataa, akakataa kumpa mtumishi. Akamuamrisha atafute msaada kwa

Dhikr na Istighfaar, naye ni binti wa Muhammad (´alayhis-Salaam).

Chanzo: http://youtu.be/J49hX6Z6HrI

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (31)

8

5) Swali Kuhusiana Na Sijda Ya Kusahau

Swali:

Je ni juu ya maamuma kuleta Sijda ya kusahau wakiswahili Jamaa´ah na

Imamu?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Hapana; akisahau mwenyewe hana juu yake [Sijda] ya kusahau [kama si

jambo la wajibu], wala Imamu. Lakini akisahau Imamu, ni juu ya Imamu na

walionyuma yake.

Chanzo: http://youtu.be/Njq6BZYbkck

6) Je, Salafiyyuun Wanafarakanisha Waislamu?

Swali:

Je ni sahihi wanayoyasema baadhi yao kwamba kuwakosoa watu wa Bid´ah

katika Suufiyyah au wengineo ndio katika sababu za kufarakanisha watu na

kufarakanisha Ummah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio tunataka kufarakanisha watu wa Bid´ah na washirikina na waabudu

makaburi. Sisi hatutaki wakusanyike na sisi. Hatuwezi kuwa pamoja ila na

watu wa Tawhiyd. Hili ndilo tunalotaka, mfarakano huu ni wakukusudia.

Allaah Kafarakanisha baina ya waumini na makafiri.

يستوون ل فاسقا كان كمن مؤمنا كان أفمن

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (31)

9

“Ati aliye Muumini atakuwa sawa na aliye mpotovu? Hawawi sawa.” (32:18)

كالفجار المتقين نجعل أم الرض في كالمفسدين الصالحات وعملوا آمنوا الذين نجعل أم

“Je! Tuwafanye walioamini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu

katika nchi? Au tuwafanye wacha Mungu kama waovu?” (38:28)

Sisi tunakusudia hili, tunakusudia kutenganisha baina ya yule asiyekubali

haki atutenge na tujiweke mbali naye, mtengo wa wazi kabisa.

Chanzo: http://youtu.be/SUWfE7z5lmo

7) Nasaha Ya Shaykh Rabiy´ Kuhusiana Na Mashaykh Wawili

Shaykh Ahmad al-Bazmuul:

Mimi nanawanasihi na kuinasihi nafsi yangu mwenyewe kwa nasaha za

Shaykh Rabiy´, nayo ni qadhiya ya Shaykh ´Ubayd al-Jaabiriy na Yahyaa al-

Hajuuriy. Ninawanasihi kwa aliyoniusia Shaykh Rabiy´ na kuwausia vijana

wa Salafiyiyn, waache kuongelea masuala haya. Kuacha kuongelea masuala

haya. Shaykh ´Ubayd ni mwanachuoni, muheshimiwa na ni maarufu kwa

elimu yake na Manhaj yake. Hali kadhalika Shaykh Yahyaa al-Hajuuriy ni

maarufu pia kwa elimu yake, heshima yake na ni katika wanafunzi wa Shaykh

Muqbil (bin Haadiy al-Waadi´iy). Na mzozano baina yao si tofauti ambazo

zinamuingiza mmoja wao katika Tabdiy´ au Tadhwliyl (upotofu). Bali ni

tofauti ambayo, yawezekana wameyaingilia watu waovu na kusababisha

matatizo na mfano wa hayo. Tunataraji kwa Allaah (´Azza wa Jalla) na

tunamuomba Allaah Atengeneze baina yao na Azikutanishe nyoyo zao. Na

tunataraji kwa vijana wote wa Salafiyiyn waache kuingia katika mambo

haya... kuingia katika masuala haya yatawaathiri. Na ninawanasihi kwa

nasaha za Shaykh Rabiy´ kuacha mambo haya. Na bila shaka Shaykh ´Ubayd

al-Jaabiriy manzilah yake yajulikana, na kusifiwa na baadhi ya watu kwa

majina mabaya haifai... Haifai, Shaykh ´Ubayd ni maarufu Allaah Amhifadhi.

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (31)

10

Chanzo: http://youtu.be/1JefmMwXklM

8) Nasaha Kwa Watafutaji Elimu (Wanafunzi)

Swali:

Ipi nasaha zako kwa watafutaji elimu (wanafunzi) wanaoanza?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Nasaha zangu kwao wakimbilie kutafuta elimu na wachukue [elimu] kama

Alivoamrisha Allaah, nako ni dalili kutoka katika Kitabu, Sunnah, kauli za

Salaf (Rahihamu Allaah).

Chanzo: http://youtu.be/IC-S42xXMK8

9) Mwanamke Kupanda Gari Ya Mwanaume Na Mke Wake Bila Ya

Mahram

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kupanda gari bila ya Mahram wake na ni safiri

[huku akiwa pamoja na] mwanaume ajinabi na mke wake akihitaji hilo kwa

kuzingatia ya kuwa ni waaminifu, na jua kuwa amejisitiri uso wake?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Kujuzisha mwanamke kupanda gari na [mwanaume] mwaminifu ikiwa

atakuwa pamoja na mke wake hili ndilo wanalosema na kulikariri

wanachuoni na Shaykh Muhammad bin Ibraahiym Muftiy aliyetangulia na

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (31)

11

kusema kuwa kila mtu anapaswa kuwa na mume wake, na ni wajibu awe

mume.

Chanzo: http://youtu.be/Qq9RWXVDEWI

10) Ibara "Lau Bila Ya Allaah Kisha Wanachuoni"

Swali:

Ibara hii, lau bila ya Allaah kisha wanachuoni tungelikuwa watu wapotofu, je

kusema hivi ni katika matamshi ya kishari´ah au ni katika matamshi ya

kishirki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Lau bila ya Allaah kisha Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam),

wanachuoni kuna uwezekano sehemu zote mbili: Kuna wanachuoni ambao

wako katika uongofu na kheri, na kuna wenye wako katika upotofu. Si

wanachuoni wote. Lakini ni Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

ndiye kalindwa na madhambi tu.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127660

11) Hukumu Ya Raafidhwah (Mashia) Wote Ni Moja

Swali:

Ipi hukumu ya watu ´Awwaam wa Raafidhwah? Je, hukumu yao ni kama

hukumu ya maulamaa wao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (31)

12

Enyi ndugu acheni maneno haya, Raafidhwah hukumu yao ni moja, hukumu

yao ni moja. Wote wanasikilzia Qur-aan, wote wanasoma bali wengi wao

wanahifadhi Qur-aan, hoja imekwishawasimamia. Wacheni falsafa hii na fikra

ambayo imeenea kwa vijana na wanafunzi, acheni hili. Aliyefikiwa na Qur-

aan hoja imekwishasimama kwake.

بلغ ومن به لنذركم القرآن هذا إلي وأوحي

"Na nimefunuliwa Qur-aan hii ili kwayo nikuonyeni nyinyi na kila

inayomfikia." (06:19)

Mpaka siku ya Qiyaamah.

Chanzo: http://aloloom.net/show_fatawa.php?id=247

12) Hukumu Ya Kusikiliza Mawaidha Ya Watu Wa Bid´ah Kama ´Aa´idh

al-Qarniy

Swali:

Je inajuzu kwetu kusema mtu fulani si Salafiy ikiwa ´Aqiydah yake ni

Salafiyyah lakini anasikiliza mikanda kwa mfano ya ´Aa´idh al-Qarniy?

´Allaamah Ahmad an-Najmiy:

Ikiwa huyu anayesikiliza mikanda ya ´Aa´idh al-Qarniy na hajanasihiwa na

yeyote na yeye hajui na anadhani kuwa ´Aa´idh al-Qarniy ni Salafiy, katika

hali hii atanasihiwa. Ikiwa atakataa kunasihiwa na akaendelea katika alioemo,

Hivyo ataambiwa ni mmoja katika Hizbiyyuun.

Chanzo: http://youtu.be/spapJXJpyKc

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (31)

13

13) Hukumu Ya Kufuturu Kabla Ya Kuzama Jua

Swali:

Tulikuwa katika Swawm ya Ramadhaan, akaadhini muadhini kabla ya

kuzama jua kwa makosa sisi tukafuturu, lipi la wajibu kwetu?

´Allaamah Yahyaa al-Hajuuriy:

Ni wajibu kwenu kulipa siku hio kutokana na kauli sahihi, kwa kauli ya

Allaah (´Azza wa Jalla):

وا ثم يام أتم الليل إلى الص

"Kisha timizeni Swawm mpaka usiku." (02:187)

Na atakayefuturu kabla ya kutimia Swawm ni wajibu kwake kurudi siku hio.

Chanzo: http://www.sh-yahia.net/show_sound_1431.html

14) Da´wah Na Acha Kuingilia Makundi Potofu

Swali:

Ipi rai yako kwa anaesema: "Ni juu ya mwanachuoni kufunza Manhaj Salaf-

us-Swaalih bila ya kuingilia makundi potofu na watu wa Manhaj potofu? Je

hili silinaingia katika msemeo wa ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhu):

"(Uislamu) utameguliwa seheumu kwa sehemu."

´Allaamah Swaalih ´ Aal ash-Shaykh:

Jibu ni kuwa, maneno haya si sahihi bali ni makosa. Kwa kuwa kuwapiga

Radd wanaokhalifu katika Dini ya Kiislamu ni katika misingi ya Dini hii. Kwa

kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye wa kwanza kuwaradi

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (31)

14

wanaomkhalifu Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Kuwapiga Radd wanaokhalifu ni katika mambo makubwa.

Anasema Shaykh-ul-Islaam:

"Na ni katika aina kubwa ya Jihaad." Na hili ni sahihi.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=126696

15) ´Allaamah al-Fawzaan Kuhusu Bia Isiyokuwa Na Pombe

Swali:

Kinywaji kinachoitwa "Beer/Bia" ambacho kipo katika baadhi ya maduka. Je

hichi kinywaji huchukuliwa ni katika alcohol (pombe) au inajuzu kukinywa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikijulikana kuwa kina alcohol kisinywe, ama ikujulikana kuwa hakina alcohol

asili itakuwa ni Halali.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=126775

16) Shaykh Mahiyr Qahtwaaniy Kuhusu Kumsikiliza Khaalid ar-

Raashid

Shaykh Mahiyr al-Qahtwaaniy:

Ama Daa´iy aitwae Khaalid ar-Raashid hatujui kuwa yuko katika Da´wah ya

Salafiyyah, khaswa (kama inavyojulikana) yuko na mikanda ambayo

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (31)

15

inahamasisha kumfanyia uasi mtawala na Jihaad za Bid´ah kama

nilivyowaambia. Siwanasihi kusikiliza mikanda yake.

Chanzo: http://youtu.be/hdzzU79RlV0

17) Hukumu Ya Wanawake Kuzuru Makaburi -2-

Swali:

Dada huyu anauliza kuhusiana na kuzuru kaburi la baba yangu na

kumuombea Du´aa. Sisi katika ada yetu ni kwenda kuzuru kaburi lake na

kumuombea Du´aa na kuweka baadhi ya miti katika kaburi lake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yote haya hayajuzu. Kwanza mwanamke kuzuru makaburi haijuzu. Kwa

kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwalaani wanawake wenye

kuzuru makaburi, wanayachukuliwa kuwa ni Misikiti na sehemu zao za

mwanga. Mwanamke hazuru makaburi. Hali kadhali kuweka (kupanda) mti

kwenye kaburi haijuzu. Kwa kuwa hii ni Bid´ah na ni njia katika Shirki.

Chanzo: http://youtu.be/B3Lw-SQ2Sbs

18) Tofauti Ya Hadiyth al-Qudsiy Na Hadiyth Za Mtume Za Qur-aan

Swali:

Ipi tofauti kati ya Hadiyth al-Qudsiy na Hadiyth za Mtume, na ipi tofauti kati

ya Qur-aan na Hadiyth al-Qudsiy?

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (31)

16

´Allaamah al-Fawzaan:

Hadiyth al-Qudsiy ni aliyoipokea Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

kutoka kwa Mola Wake kwa lafdhi na maana yake. Ama Hadiyth ya Mtume

ni aliyoisema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na maana yake

inamrudilia Allaah (´Azza wa Jalla). Tofauti kati ya Hadiyth al-Qudsiy na

Qur-aan, vyote viwili ni Maneno ya Allaah (´Azza wa Jalla). Lakini Qur-aan ni

Mutawaatir, Hadiyth al-Qudsiy inaweza kuwa si Mutawaatir, inaweza kuwa

Ahaad, dhaifu, hasan. Hadiyth al-Qudsiy inaweza kukumbwa na yanayoweza

kuikumba Hadiyth ambayo sio Qudsiy kwa kukataliwa mapokezi yake. Ama

Qur-aan yenyewe ni Mutawaatir kwa Ijmaa´ ya Waislamu. Hili ni jambo la

kwanza. Jambo lingine ni kuwa Qur-aan mtu anafanya nayo ´Ibaadah kwa

kisomo chake, kwa Swalah na mengineyo tofauti na Hadiyth al-Qudsiy

hakufanywi ´Ibaadah kwa kisomo chake.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2514

19) Mke Wangu Anasema Uongo Sana

Swali:

Mke wangu anasema uongo sana mbele yangu na mbele ya watoto wake na

familia yake, na anasema kuwa hawezi kuacha hilo. Una ninasihi nini Shaykh?

´Allaamah ´Abdul-´Aziyz Aal ash-Shaykh:

Mbainishie jarima ya kusema uongo, na hadhi ya uongo, na kuwa ni katika

tabia ya wanafiki na kuwa ni katika yanayopugunza uaminifu kwa

mwanamke au mwanamume. Usikae kimya kwa uongo wake, na usikubali

kitu kwake mpaka akubali kosa lake ajikerebishe na atubie kwa Allaah kwa

aliyofanya.

Chanzo: http://youtu.be/vkg2dX2mC8U

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (31)

17

20) Kujifunza Mwenyewe - Maradhi Khatari Ya leo

Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab kasema:

"34- Usiamini Dini yako katika vitabu na wale wanaojinasibisha kwa elimu."

´Allaamah al-Fawzaan:

Usiamini vitabu moja kwa moja. usiviamini. Kwa kuwa kuna haki na batili.

Usiviamini vitabu. Bali rejea kwa maulamaa (wanachuon) waliobobea katika

elimu. Usichukue elimu yako tu katika vitabu, au ukasoma kwenye vitabu

vyenyewe. Baadhi ya watu wanahifadhi mujaladi na maandishi, lakini

hawafahamu yaliyomo ndani yake na wala hawajui maana yake. Kwa kuwa

hawakusoma kwa maulamaa ambao wanasherehesha na wanabainisha

muradi wake. Wanaweza kufahamu ufahamu ambao ni wakimakosa. Hili ni

khatari! Usiamini hivi vitabu. Vitabu ni njia tu katika elimu. Usiviamini katika

kujifunza kwako. Si vitabu vyote vinakuwa sahihi. Hata kama kitabu ni sahihi

ufahamu wako una mpaka. Fahamu inatofautiana hata kama kitabu kitakuwa

sahihi. Je Khawaarij hawakupotea nao ni walikuwa ni wenye kuhifadhi Qur-

aan na wanasimama na kuisoma usiku katika Tahajjud wakiswali? Lakini

wamepotea. Allaah Atulinde. Kwa kuwa hawafahamu maana ya Qur-aan na

hawakuchukua elimu kwa maulamaa. Walijitenga na Maswahabah na

wakatosheka na kusoma Qur-aan na ufahamu wao kivyao. Ndo maana

wamepatwa na yaliyowapata. Na haya maradhi ya leo ni khatari. Mtu

kudhani kuwa anajua ni maradhi khatari, nako ni kuchukua elimu kwenye

vitabu au kwa watu wasiofahamu kwa wale wanaodhani kuwa wanajua na

wanaoanza. Hii ni khatari kwa mtu mwenyewe na ni khatari kwa Ummah.

Kwa kuwa atatoka aanze kutoa Fatwa, aanze kufasiri Qur-aan au afasiri

Sunnah apoteze watu.

Chanzo: http://alfawzan.ws/node/12520

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (31)

18

21) Je, Katika Zama Hizi Kuna Maulamaa Wa al-Jarh Wa Ta´adiyl?

Muulizaji:

Assalaam ´alaykum warahmtullaahi wa Barakatuh

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Wa ´alaykum-us-Salaam warahmtullaahi wa Barakatuh

Muulizaji:

Hayaak Allaah Shaykh, vipi hali yako?

´Allaamah an-Najmiy:

Mzima.

Muulizaji:

Nina swali Shaykh naweza kuuliza?

´Allaamah an-Najmiy:

Ndio.

Muulizaji:

Je, kuna maulamaa wa al-Jarh wa Ta´adiyl katika zama hizi?

´Allaamah an-Najmiy:

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (31)

19

Maulamaa wa al-Jarh wa Ta´adiyl wanakuwepo katika kila zama.

Muulizaji:

Na ni kina nani Shaykh?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Maulamaa wa al-Jarh wa Ta´adiyl wanakuwepo

katika kila zama.

Muulizaji:

Na ni kina nani katika zama hizi?

´Allaamah an-Najmiy:

Wapo, kama Shaykh Rabiy´ (al-Madkhaliy), Muhammad bin Haadiy (al-

Madkhaliy), (Swaalih) as-Suhaymiy na kadhalika.

Chanzo: http://youtu.be/1XmZLDbg2WI

22) Haijuzu Kwa Mwanamke Kuvaa Suruwali Yoyote Kwa Hali Yoyote

Swali:

Ipi hukumu ya kuvaa suruwali ya “jeans” na kanzu juu yake? Je, ni katika

mavazi ya makafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (31)

20

Kila ambacho hakisitiri na kina fitina haijuzu kukivaa, na suruwali ina fitina.

Kwa kuwa inabainisha viungo vya mwili wa mwanamke na maumbile ya

mwanamke, akamfitinisha yule anayemwangalia. Haijuzu kwa mwanamke

kuvaa suruwali kwa hali yoyote, kama kweli anamuogopa na kumcha Allaah.

Na haijuzu kuziuza kwa wanawake na thamani yake ni Haramu, haijuzu

kuziuza kwa wanawake. Kwa masikitiko makubwa leo sehemu za mavazi

hukuti mavazi ya Kishari´ah, bali unakuta mavazi ya kimagharibi na mavazi

yasiyositiri. Wanaziuza na wanakula thamani yake na wanakuwa tajiri kwazo.

Chanzo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=127853

23) Shaykh Yahyaa al-Hajuuriy Kuhusu al-Halabiy

Shaykh Yahyaa al-Hajuuriy:

Kuna makala ya Radd kwa ´Aliy al-Halabiy imesambazwa, hakuna ubaya

ndugu waiuze (Dammaaj) kutokana na tunavyomjua. Ndugu walinipa na

kunambia niangalie kama inaweza kuuzwa hapa. Hakuna ubaya (iuzwe).

(makala hio) ina (kauli ya al-Halabiy) kuhisiana na uchaguzi (katika ubunge),

na sisi yeyote anayehamasisha uchaguzi tunaona kuwa hakuna ubaya

kubainisha (kwa watu) makosa yake katika hilo. ´Aliy al-Halabiy bado

hajaachana na Abul-Hasan, aliachana nae au bado yuko nae?

Bado yuko nae! Bado hajaachana na ´Adnaan ´Ar´uur, hajaachana na al-

Maghrawiy, na hajaachana na Usaamah al-Quusiy, na hajaachana na Ihyaa at-

Turaath. Anasema "Bado huwa ninawazuru na tunanasihiana... " Anasema

kwa mfano "Siwezi kuwaficha ukarimu nilionao kwao... " na kadhalika. Huyu

ndiye (al-Halabiy)! ´Aliy al-Habaliy ni Mu´mayyi´ (mpaka mafuta) enyi

ndugu. Da´wah yake ni Da´wah ya Tam´yi´!

Chanzo: http://youtu.be/h4zEtZ6mlkc

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (31)

21

24) Wale Wasiopenda Kuzungumziwe Manhaj Ahl-is-Sunnah wal

Jamaa´ah

Swali:

Kuna kundi la vijana katika mji wetu, hawapendi kuzungumziwe Manhaj

kabisa wala hawachanganyiki na vijana walioko katika haki katu, bali

nikakundi kamejitenga Ipi hukumu ya kushirikiana nao?

´Allaamah Muhammad al-Madkhaliy:

Ikiwa hizi ndo sifa zao tahadhari nao. Hakika yule ambaye hataki kuongelewe

Manhaj ya haki - Manhaj Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, kushikamana nayo na

kutahadharisha na yanayoikhalifu huyu ni mtu wa shari. Usiwe pamoja nae.

Chanzo: http://www.youtube.com/mirathiyamitume

25) Mwanamke Kuvaa Punjabi Yenye Suruwali

Swali:

Baada ya kuangalia mavazi yaliyopo madukani na tukapata zinazositiri,

tukapata vazi linaloitwa "punjabi". Nayo ni kanzu ya wasaa inayofunika hadi

nusu ya magoti. Chini ya hio mtu huvaa suruwali ndefu na ya wasaa...

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni suruwali?

Muulizaji:

Ndio.

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (31)

22

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, haiwezekani. Suruwali haiwezekani.

Chanzo: http://youtu.be/rKR8UyI_8AM

26) Lipi La Kufanya Unapojiwa Na Mawazo Mabaya?

Swali:

Mawazo yangu mara nyingi yanakuja katika mambo yanayomchukiza Allaah,

na mimi daima huwa nikijiepusha na mawazo haya na kusema kuwa

yanatoka kwa Shaytwaan. Je, mtu atahesabiwa kwayo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hatohesabiwa kwayo:

"Ummah wangu umesamehewa kwa makosa yao na kwa kusahau, na

yanayohadithia nafsi zao maadamu tu hawajayatamka au kuyafanya".

Kule kuchukia kuyazungumzia na kuyasema, hii ni alama ya Imani. Ni juu

yako kutafuta kinga kwa Allaah kutokana na Shaytwaan aliyelaaniwa, na ni

juu yako kutupa mawazo hayo na kuepuka maingiliano yake.

Chanzo: http://youtu.be/waGR7ndX3IY

27) Kufunga Siku Ya Maulidi Ya Mtume (´alayhis-Salaam)

Swali:

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (31)

23

Inajuzu kufunga siku ya kuzaliwa kwa Mtume (maulidi)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana, ni Swawm ambayo haikuweka Allaah wala Mtume Wake na wala

haikuwekwa kwetu kufunga. Naam, siku ya Jumatatu unafunga, hapana ya

tarehe 12 Rabiy´ al-Awwal - unafunga Jumatatu kwa kila wiki, hii ni Sunnah.

Ama tarehe 12 ya Rabiy´ al-Awwal ikikutana na siku ya Jumatatu

unasherehekea [na kufunga] kwa kuwa imeangukia siku ya Maulidi, hapana

haijuzu hili.

Chanzo: http://youtu.be/AZNuq_-Nm7w

28) Ipi Hukumu Ya Kutawadha Bafuni?

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kutawadha bafuni, na je inajuzu Wudhuu wake?

Imaam Ibn Baaz:

Hakuna ubaya. Akitawadha bafuni, hakuna ubaya. Aseme kabla ya

kutawadha "Bismillaah" na atawadhe. Kwa kuwa [kusema] Bismillaah ni

wajibu kwa baadhi ya wanachuoni, na ni jambo la kusisitizwa kwa [kauli] ya

wengi. Aiseme, na ni karaha kuiacha, kwa kuwa kilicho cha karaha kinaachwa

wakati wa haja. Mtu kaamrishwa kusema Jina la Allaah mwanzo wa kutia

Wudhuu, hivyo atasema Jina la Allaah na kukamilisha Wudhuu wake. Ama

Du´aa baada ya Wudhuu inakuwa baada ya kutoka bafuni. Akimaliza anatoka

na kuomba Du´aa ya baada ya Wudhuu nje ya bafu. Lakini ikiwa bafuni ni

sehemu tu ya Wudhuu na hakuna sehemu ya kujisaidia wala kukojoa bali ni

sehemu tu ya Wudhuu, hakuna ubaya kusema jina la Allaah kwa kuwa si

sehemu ya kujisaidia.

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (31)

24

Chanzo: http://youtu.be/ImTC_0ASc6Y

29) Hukumu Ya Kulala Kwa Tumbo (Kifudifudi)

Swali:

Nimeambiwa kuwa kulala kwa tumbo ni Haramu, je hili ni sahihi? Na ikiwa

ni sahihi, nifanye nini kwa kuwa siwezi kulala vizuri ila mpaka nilale kwa hali

hii?

Imaam Ibn Baaz:

Imepokelewa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwamba

alimuona mmoja katika baadhi ya Maswahabah wake akilala kwa tumbo lake

akamtikisa kwa mguu wake na kumwambia:

"Hakika ni njia ambayo inamchukiza Allaah."

Katika Riwaayah nyingine:a

"Hakika ndo jinsi watu wa motoni wanavyolala."

Kwa hiyo ni makruhu kulala hivyo, inatakiwa kuacha isipokuwa kama

kutakuwa dharurah, kama kwa maumivu ambayo mtu anayapata ikamfanya

mtu alale hivi. La sivyo inatakiwa kuacha, dogo tunaloweza kusema ni

makruhu. Kwa kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Hakika ni njia ambayo inamchukiza Allaah."

Inatakiwa kuacha, dogo tuwezalo kusema ni kuwa ni makruhu kufanya

hivyo, kwa kuwa dhahiri ya Hadiyth inaharamisha. Inatakiwa kwa muumini

mwanaume na mwanamke kuacha kulala kwa njia hii, isipokuwa tu kwa

dharurah isiyowezekana.

Chanzo: http://youtu.be/RyV-HT6GiJA

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (31)

25

30) Hadiyth Dhaifu Ya Mu´aadh (Radhiya Allaahu ´anhu)

Shaykh Dr. Abu ´Abdul-Haliym ´Abdul-Haadiy:

Kwa kuwa kuna baadhi ya Hadiyth ambazo Ummah wamezikubali, ila

hazikuthibiti kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), kama Hadityh

mashhuri wakati Mtume alipomtume Mu´aadh (Radhiya Allaahu ´anhu)

kwenda Yemen. Akamwambia utahukumu Kwa nini? Akasema "Kwa Kitabu

cha Allaah." Akamuuliza "Ikiwa hukupata katika Kitabu cha Allaah?”

Akasema "Kwa Sunnah za Mtume wa Allaah." Akamuuliza “Ikiwa hukupata

katika Sunnah za Mtume wa Allaah?” Akasema "Ntajitahidi kwa rai yangu."

Hadiyth hii enyi waja wa Allaah, haikuthibiti kwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) hata kama Ummah wameikubali. Ni wajibu kutanabahi

jambo hili.

Chanzo:

http://www.assalafia.com/modules.php?name=tapes&dcategory=%C7%E1%

E3%E4%E5%CC

31) Anampiga Binti Yake Kwa Kumtomsikiliza Yeye Na Mama Yake

Swali:

Ninapotaka kumpiga binti yangu kwa tatizo baina yake yeye na dada yake au

vurugu zake nyumbani au kutosikiliza maneno ya mama yake au maneno

yangu na kadhalika; ninapompiga huogopa na husema: "Babangu mpenzi

Allaah Akuhifadhi, ninamuomba Allaah Akuingize Peponi." Naingiwa na

wasiwasi kwa Du´aa hii khaswa ninapoendelea kumpiga na ninajiambia

nafsini: "Sema, ewe Allaah Niingize Peponi ilihali na mimi niko nampiga."

´Allaamah ´Abdir-Rahmaan al-Baraak:

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (31)

26

Kwa nini unampiga? Kwa nini? Usimpige! Kwa nini umpige?!

Muulizaji:

Kwa kumuasi mama yake au baba yake.

´Allaamah ´Abdir-Rahmaan al-Baraak:

Hapana, hapana usimpige. Muadhibu kwa maneno. Kumpiga si njia nzuri.

Mpige kwa kukiuka haki ya Allaah, kwa kukiuka haki ya Allaah. Kwa mfano

haswali na kishafikisha miaka kumi, muadhibu kipigo cha kumuweka adabu.

(Kumpiga kwako) ni kosa. Kuna baadhi ya watu wanachupa mipaka. Hata

kuna baadhi ya watu wanawaadhibu watoto wao kwa moto! Huu ni ujinga.

Kumuweka mtoto adabu si kumtesa! Kuwa mwenye kurehemu utarehemewa

nawe. Usimpige binti yako. Muadhibu kwa [maneno]. (Kama kusema) huoni

aibu, huoni aibu, hili si sawa, unafanya nini hivyo?

Chanzo: http://youtu.be/rEq0EZMTMEg

32) ´Allaamah ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad Kuhusu Anashiyd

´Allaamah ´Abdul-Muhsin al-´Abbaad:

Mtu anatakiwa kuchunga wakati wake katika yatayomfaa duniani na

Aakhirah, ajishughulishe na kusoma Qur-aan, kusoma vitabu vyenye

manufaa, mashairi mazuri ambayo yanashaji´isha katika tabia nzuri na katika

adabu nzuri. Ama hizi Anashiyd ambazo zimezuka katika masiku haya

yamwisho na ambazo zinawashughulisha kila siku wengi na wanazisambaza,

haitakiwi kujishughulisha nazo na wala haitakiwi kuzisikiliza.

Chanzo: http://youtu.be/ouMuOfE0CHM

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (31)

27

33) Usufi Si Katika Uislamu

Swali:

Ipi hukumu ya Usufi katika Uislamu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Katika Uislamu hakuna usufi, hili ni Bid´ah. Usufi ni Bid´ah na si katika

Uislamu. Ni wajibu wa aliyetumbukia humo atubie kwa Allaah (´Azza wa

Jalla) na arejee katika Sunnah na katika waliyokuwemo Salaf-us-Swaalih

katika kuwa na msimamo katika Dini ya Allaah na kumuiga Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) na Makhalifah wake waongofu. Hii ndio Manhaj

sahihi. Kasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Na Ummah wangu utagawanyika katika makundi 73, yote yataingia motoni

ila moja tu. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wakauliza: "Ni lipi hilo

Mtume wa Allah? Akasema: "Ni wale watakaokuwa katika mfano wa yale

niliyomo leo na Maswahabah wangu."

Hakuna kusalimika wala kuokoka isipokuwa [kwa kushikamana] na mfumo

wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah wake. Na

usufi si katika mfumo wa Mtume (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam) na si

katika mfumo wa Maswahabah wake, na si katika mfumo wa karne bora bali

ni kundi limezushwa katika Uislamu, na lina upotofu mwingi. Na wakati

mwingine kunakuwa na makaburi na kumshirikisha Allaah (´Azza wa Jalla)

na kuwaamini maiti (wafu). Inakuwa ni usufi na Shirki pia.

Chanzo: http://youtu.be/4SUw8OSMKVo

34) Radd Kwa Jabriyyah Na Qadariyyah

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (31)

28

Shaykh Dr. Abu ´Abdul-Haliym ´Abdul-Haadiy:

Na kawaradi Allaah (Jalla wa ´Alaa) makundi mawili kwa kauli Yake (Jalla wa

´Alaa):

البصير السميع وهو شيء كمثله ليس

"Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona."

(42:11)

Anawaradi Mushabbihah (wale wanaozifananisha Sifa za Allaah za viumbe

Vyake) kwa kauli Yake Allaah:

شيء كمثله ليس

"Hapana kitu kama mfano wake." (42:11)

Hapa anawaradi mushabbihah. Na kauli Yake Allaah:

البصير السميع وهو

"Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona." (42:11)

Hapa Anawaradi Mu´attwilah (wale wanaokanusha Sifa za Allaah). Watu wa

haki (Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah) ndio wanathibitisha Sifa za Allaah (Jalla

wa ´Alaa) uthibitisho usiokuwa na mfano, na hawazifananishi na sifa za

viumbe kwa kutegemea Kauli ya Allaah (Jalla wa ´Alaa):

البصير السميع وهو شيء كمثله ليس

“Hapana kitu kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona.”

(42:11)

Wao wako kati kwa kati, katika mlango vitendo vya Allaah baina ya Jabriyyah

na al-Qadariyyah. Jabriyyah wamechupa mipaka katika Qadar, wakapinga

matendo ya waja na wakasema:

"Binaadamu kafungwa katika matendo yake, hana khiyari wala matakwa."

Ni mwenye kuzini na wakati huohuo si yeye mwenye kuzini, anaiba na si

yeye mwenye kuiba, wananasibisha kuwa matendo haya ni majawaliwa, na

[wanasema] kwa uhakika mtendaji ni Allaah (´Azza wa ´Alaa). Na haya ni

madhehebu batili, madhehebu ya Jabriyyah, na ndio madhehebu ya Jahmiy

bin Safwaan.

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (31)

29

Chanzo:

http://www.assalafia.com/modules.php?name=tapes&dcategory=%C7%E1%

E3%E4%E5%CC

35) Muislamu Aliyeacha Swalah Ni Kafiri Na Lazima Auawe

Swali:

Nina jamaa asiyeswali, nimemnasihi hakukubali. Nikamweleza msimamizi

wake na akasema anasikia uogo asije kuhamishwa. Akanambia nimsisitize

aswali na kwamba kumtisha kufukuzwa. Akanikasirikia sana. Je, kitendo

changu hiki ni kosa? Na lipi la wajibu katika hali kama hii?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yule asiyeswali sio Muislamu. Kutokana na kauli ya Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Kasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Baina ya mja na kufuru na Shirki ni kuacha Swalah."

"Ahadi iliyopo baina yetu sisi na wao [makafiri] ni Swalah, atakayeiacha

amekufuru."

Na dalili za kwenye Kitabu (Qur-aan) na Sunnah zinamkufurisha aliyeacha

Swalah ni nyingi. Wala haitoshi mtu kama huyu kuhamishwa tu kazini, bali ni

wajibu kuachishwa kazi kabisa. Bali ni wajibu auawe ikiwa hatotubia kwa

Allaah na kuhifadhi Swalah; ataambiwa aleta Tawbah ikiwa hakufanya hivyo

auawe. Na ulivofanya kwake huo ndo wajibu kwako; kumnasihi,

kumkumbusha Allaah. Na ikiwa hatokubali na akaendelea kuacha Swalah, ni

wajibu (kiongozi) kumuua. Wala haitoshi tu kumhamisha kazini, bali kitendo

tu cha kumuajiri ni kosa. Haijuzu kumuweka mtu kama huyu kafiri sehemu

za Waislamu, kwa kuwa anakuwa kiigizo [kibaya] kwa wengine.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=K2Ax448_J30

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (31)

30

36) Lini Kuhukumu Kinyume Na Aliyoteremsha Allaah Mtu Anakuwa

Kafiri?

Shaykh Dr. Abu ´Abdul-Haliym ´Abdul-Haadiy:

Wale wanaowakufurisha watawala wa kiislamu, na wanawakufurisha wale

ambao hawahukumu kwa yale Aliyoteremsha Allaah (Jalla wa ´Alaa), hata

hivyo masuala haya yanahitajia ufafanuzi. Kuhusiana na kuhukumu kwa yale

Aliyoteremsha Allaah (Jalla wa ´Alaa). Hakimu anaweza kuwa kafiri - ukafiri

wa kumtoa katika Uislamu akihukumu kinyume na aliyoteremsha Allaah

huku akiitakidi kuhukumu kinyume na Aliyoteremsha Allaah ni bora zaidi

kuliko kuhukumu kwa Aliyoteremsha Allaah (Jalla wa ´Alaa). Huyu ni kafiri!

Atakayehukumu kinyume na Aliyoteremsha Allaah huku akiitakidi kuwa

[hukumu hio] iko sawa na hukumu ya Allaah huyu ni kafiri! Na

atakayehukumu kinyume na Aliyoteremsha Allaah huku akiamini kuwa

inajuzu kuhukumu kinyume na Aliyoteremsha Allaah, huyu pia ni kafiri

kufuru kubwa! Ama akihukumu kinyume na Aliyoteremsha Allaah huku

akiamini kuhukumu kwa Aliyoteremsha Allaah ndio bora zaidi na iliyo

kamili, lakini kwa [kupewa] rushwa, kupenda cheo au kutaka kufikia jambo

fulani la kidunia, akahukumu naye ni mwenye kuitakidi kuwa ni dhalimu na

ni muasi kwa hali hii hatoki katika Uislamu na kufuru yake ni kufuru ndogo

kama alivosema Ibnu ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kwa kauli ya

Allaah:

“Na wasiohukumu kwa Aliyoteremsha Allaah, basi hao ndio makafiri.”

(05:44)

Akasema ni kufuru ndogo. Khawaarij wanamwita mtu huyu kafiri, na

wanahalalisha damu yake na mali. Hivyo ndo maana walimkufurisha ´Aliy,

Mu´aawiyah na Maswahabah wao na wakahalalisha yanayohalalishwa kwa

makafiri. Ama Mu´tazilah wanasema mwenye kufanya dhambi kubwa

anatoka katika Imani (Uislamu) na wala haingii katika kufuru, mtu huyo yuko

katika manziylah mbili - mtu hawezi kusema ni kafiri wala kusema ni

muumini. Hii ni katika misingi ya Mu´tazilah. Wana misingi mingine

kuhusiana na Tawhiyd, makusudio ya Tawhiyd kwao ni kupinga [kuzikataa]

Sifa [za Allaah]. Hivyo akiongelea mtu kuhusu Tawhiyd ni juu yake

Page 31: Fataawa Za Wanachuoni (31)

31

kubainisha uhakika wa Tawhiyd ambayo waliomo. Kuna ambao wanasema

Tawhiyd maana yake ni al-Haakimiyyah - maaya ya laa ilaaha illa Allaah

maana yake ni al-Haakimiyyah. Na hii ndio Itikadi ya al-Ikhwaan al-

Muflisiyn.

Chanzo:

http://www.assalafia.com/modules.php?name=tapes&dcategory=%C7%E1%

E3%E4%E5%CC

37) Kitabu Na Sunnah Vinatangulizwa Kabla Ya Ijmaa´

Swali:

Wakati fulani kunasemwa katika masuala "Dalili ya hili ni Ijmaa´, Kitabu na

Sunnah. Kwa nini kunatangulizwa Ijmaa´? Je, Ijmaa´ ina nguvu zaidi kuliko

Kitabu na Sunnah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana hili ni kosa. Dalili ya hilo ni Kitabu na Sunnah na Ijmaa´. Hakuna

yeyote awezae kutanguliza Ijmaa´ kabla ya Kitabu na Sunnah.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2513

38) Imaam Abu Haniyfah, Imaam Wetu, Kiigizo Chetu

Swali:

Tulikusikia wakati wa darsa ukisema:

"Abu Haniyfah (Rahimahu Allaah)"; Ulimrehemu...

Page 32: Fataawa Za Wanachuoni (31)

32

´Allaamah al-Fawzaan:

Rahmah kunjufu! Namuomba Allaah Amrehemu Rahmah kunjufu na

Amsamehe. Ni Imaam wetu na kiigizo chetu bora. Afurahi mwenye kufurahi

na achukie mwenye kuchukia.

Chanzo: http://youtu.be/A7KDMfJCXGY

39) Kumtolea Mtu Swadaqah Kwa Kuswali Naye Baada Ya Swalah Ya

´Aswr Na Fajr

Swali:

Aliingia mtu Msikitini baada ya Swalah ya ´Aswr nami nimekaa, akanambia

nitolee Swadaqah na uswali na mimi. Nikakumbuka kuwa ni wakati wa

makatazo [kuswali], lakini nikaswali naye. Ipi hukumu ya kitendo hiki? Na je

vipi ikiwa ni baada ya Swalah ya alfajiri?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Hukumu ni ya kitendo hiki ni thawabu na ni sahihi, sawa ni baada ya Swalah

ya alfajiri au baada ya Swalah ya alasiri. Swadaqah yake ni sahihi na wewe ni

mwenye ujira.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action?s_menu=23&idFatwa=2547

40) Ipi Bora Kwa Wanawake Kuswali Jamaa´ah Au Kila Mtu Kivyake?

Swali:

Page 33: Fataawa Za Wanachuoni (31)

33

Muulizaji kutoka Sweden, je inajuzu kwa wanawake kuswali Jamaa´ah? Na

lipi bora kwao kuswali Jamaa´ah au mmoja mmoja?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Ndio waswali Jamaa´ah wakiweza hilo na waongozwe na msomi mjuzi wao

na asimame katikati yao. Kuswali Jamaa´ah katika hali zote ni bora kuliko kila

mmoja kuswali kivyake.

Chanzo: http://youtu.be/eV8zv4vsxpM

41) Inajuzu Kumhukumu Mtu Moja Kwa Moja Kuwa Ni Mnafiki?

Swali:

Muuliza kutoka Ufaransa, je atayedhihiri kuwa na alama za unafiki

atahukumiwa kuwa ni mnafiki?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Atahukumiwa kwa matendo yake kama walivyokuwa wakifanya Salaf-us-

Swaalih. Walikuwa wakisema atayefanya kadha, atakuwa kadha.

Atakayefanya ukafiri kakufuru, atakayefanya unafiki amenafaka. Inakuwa

atakayefanya kadha katumbukia katika unafiki, na mtu hasemi moja kwa

moja wewe ni mnafiki. Kwa kuwa usulubu huu si usulubu sahihi. Da´wah

inatakiwa iwe kwa hekima na mawaidha mazuri.

Chanzo: http://youtu.be/Ubv_ks-MbHA

Page 34: Fataawa Za Wanachuoni (31)

34

42) Hukumu Ya Kufanya Mazoezi Katika Ukumbi Za Muziki

Swali:

Muulizaji kutoka Ubelgiji, mama yangu kafikwa na maradhi ya mafuta

yaitwayo "sumna", na alienda kwa daktari akamwambia ana umuhimu

mkubwa wa kufanya mazoezi, na ukumbi zote za mazoezi zina muziki.

Afanye nini?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Anaweza kufanya mazoezi nyumbani kwake, na haijuzu kwake ikiwa kweli ni

Muislamu mwanamke kwenda katika manyumba ya muziki na yaliyomo

katika ufisadi. Tahadhari! Anaweza kufanya mazoezi nyumbani kwake, au

akatoka yeye na Mahram wake mahala pazuri na akafanya mazoezi; kama ya

kutembea, kufanya harakati n.k. na akafikia lengo lake katika hayo. Na

ajiepushe na ukumbi za muziki na nyinginezo.

Chanzo: http://youtu.be/dX-_xi66OqQ

43) Anashiyd (Qaswiydah) Ni Haramu

Swali:

Ipi hukumu ya kusikiliza Anashiyd ambazo zinahalalishwa na baadhi ya

wanachuoni na baadhi ya wengine wanaziharamisha? Na ikiwa ni Haramu

vipi vikwazo vyakuharamisha?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Bila shaka Anashiyd sio katika ´Ibaadah mpaka mtu apewe ujira kwayo

mwenye kuziimba na msikilizaji, na si katika uongofu wa Salaf na

litalokwenda kinyume na hili ni batili. Kuna baadhi ya wanachuoni

wameandika kuhusiana na Anashiyd na kubainisha ubatili wake khaswa

Page 35: Fataawa Za Wanachuoni (31)

35

katika zama hizi za mwisho kumekuwa Anashiyd za nyimbo na zimeathiri

sana kuliko Qur-aan na khaswa vijana. Ni wajibu kujiepusha nazo, na ibara

mbaya wamezipa ni pale wasemapo "Anshiyd za Kiislamu", sio za Kiislamu

kwa hali yoyote. Ni Haramu bila shaka.

Chanzo: http://youtu.be/nbfiRXqzx9o

44) Mume Na Mke Wanadanganya Serikali Wameachana Ili Wapate Pesa

Zaidi

Swali:

Muulizaji kutoka Sweden, lau ikiwa mtu ataidanganya serikali na kuwaambia

kuwa amempa Talaka mke wake kwa kuwa watampa mwanamke yule

aliyetalikiwa mali, na isitoshe akapiga saini kwa hilo. Je, kitendo hiki kinajuzu,

na je Talaka imepita?

´Allaamah Zayd al-Madkhaliy:

Atachukuliwa kuwa ni muongo na uongo ni jarima munkari hata kama

itakuwa ni kwa kafiri. Watu wawe na tahadhari kwa kufikia mali kwa njia

chafu kama hii ya uongo.

Chanzo: http://youtu.be/90Ui0scVyEo

45) Msikiti Unaokhatimu Qur-aan Na Usiyokhatimu, Wapi Nifanya

I´tikaaf?

Swali:

Page 36: Fataawa Za Wanachuoni (31)

36

Ipi bora zaidi kwa mwenye kukaa I´tikaaf, afanye I´tikaaf katika Msikiti wake

ambapo wanasoma nusu juzu katika Kitabu cha Allaah au atoke aende katika

Msikiti ambapo wanakhatimu Qur-aan?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni mwenye khiyari kuchagua kufanya I´tikaaf katika Msikiti wowote ambapo

anaona ni bora kwake, achague Msikiti ambao anaona ni bora kwake katika

mji wake.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/node/2655

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad , na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.