Haliuzwi - Johns Hopkins Center for Communication Programsccp.jhu.edu/documents/Si Mchezo 67 Jul-Aug...

32
ISSN: 0856-8995 Usije mjini Jipange kwanza Usije mjini jipange kwanza Haliuzwi KATUNI

Transcript of Haliuzwi - Johns Hopkins Center for Communication Programsccp.jhu.edu/documents/Si Mchezo 67 Jul-Aug...

ISSN

: 08

56-8

995 Usije mjini

Jipange kwanzaUsije mjini jipange kwanza

Haliuzwi

KATUNI

2 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Si Mchezo! Huzalishwa na kusambazwa.

Si Mchezo! husambazwa.

Lilikozalishwa toleo hili.

Kuja mjini bila mpango ni kujidhalilisha na pia unakuwa mzigo kwa

wengine. Tuliza akili na anza kuangalia fursa zilizoko huko kijijini kwako kisha zifanyie

kazi. Omba ushauri kwa wataalamu ikibidi

Maisha ni kama mchezo wa kuigiza kwani kila

wakati unatakiwa ubuni kitu kipya na kukiendeleza. Lengo lako litatimia kama

utakuwa mbunifu wa kuboresha yale uliyolenga

kuyatimiza.

3

TAHARIRIJiji la Dar es Salaam hupokea vijana zaidi ya laki moja kila mwaka ambao

huja ‘kusaka’ maisha. Wengine kabla ya kuingia mjini husikia kwenye

nyimbo ujumbe ‘usije mjini’. Huenda hofu inatanda katika nafsi zao na

kukosa malengo. Wengine huishia mikononi mwa mgambo wa jiji! Sawa

basi peruzi kitu kipya kilichopikwa katika jiji la Bongo kisha tujadili

mustakabali wa maisha yetu vijana.

Majuka

YALIYOMO

4 Stori Yangu: Usije mjini, jipange kwanza

6 Mambo Mapya:Unaishi vipi Dar?

8 Hadithi ya Picha: Mjini mipango

12 Je, Wajua: Jiangalie, utapotea jombaa

14 Sauti yangu

16 Burudani: Karibu Dar

18 Ruka Juu: Joseph nd’o jembe!

20 Nguvu za mwanamume: Ngono na mapenzi

21 Nguvu za mwanamke: Kweli, inawezekana

22 Cheza salama: Kona ya mtaa

24 Katuni: Jilinde...

27 Ukweli wa mambo: Sema hapana, mlinde mwenzako

28 Sema Tenda:Tusilalamike, tuchakarike

30 Ushauri

Mkurugenzi MtendajiDr. Minou Fuglesang

Mkurugenzi wa HabariAmabilis Batamula

Meneja MachapishoJiang Alipo

Mhariri Mkuu Majuka Ololkeri

WaandishiRaphael NyoniGaure MdeeBetty LidukeJosephat Mwambula

WashauriTimu ya Femina HIP

Meneja UhusianoLilian Nsemwa

Katuni na UsanifuBabaTau, Inc.

Mpiga Chapa Jamana Printers Ltd

Usambazaji EAM Logistic LtdFemina HIP na Washirika

Si Mchezo! limefanyika kwa hisani kubwa ya Serikali za Sweden (Sida), Denmark (DANIDA), HIVOS, RFSU, TWAWEZA na JHU-CCP/TCCP

Yaliyomo humu ndani ni jukumu la Femina HIP na hayawakilishi maoni au mitazamo ya wafadhili.

Wasiliana nasi kwa:S.L.P. 2065, Dar es SalaamSimu: (22) 212 8265, 2126851/2 Fax: (22) 2110842email: [email protected] Mchezo! huchapishwa na Femina HIP.Sms: Andika SM acha nafasi andika maoni yako kisha tuma kwenda 15665

Ukiingia kichwa kichwa mjini uta-

potea! Shauri yako.

Mmh kweli, tupeane michongo lakini

4 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Kusaka maisha kunahitaji utulivu wa akili na

kugundua fursa zinazokuzunguka vinginevyo

utajikuta upo kwenye wakati mgumu. Wengine

wana bahati zao lakini kama wahenga walivyosema,

“Bahati ya mwenzio, usiilalie mlango wazi”.

Naitwa Hamad Masoud (27), nilizaliwa Urambo,

Tabora. Nilipozaliwa tu, baba na mama

wakatengana. Mama alishindwa kunisomesha.

Nilipofikisha miaka 12 nilianza kusaka pesa ili

kumsaidia mama kutunza familia. Nilipata ajira

ya kuuza maandazi nikiwa nalipwa 2,000/= kwa

mwezi. Nilijifunza kutengeneza maandazi pia.

Baada ya miaka miwili, binamu yangu anayeishi

Tabora mjini aliniita nikafanye kazi ya kuuza

mitumba. Nilifika na kuanza kazi hiyo kwa ujira wa

1,000/= kwa siku. Pesa hiyo ndiyo chakula, malazi

na mavazi. Nilifanya kwa miaka mitatu lakini

nikaona hainilipi kulingana na gharama za maisha

ya mjini. Wakati huo nilikuwa nikisikia kwamba Dar

es Salaam panalipa. Sikuwa na nauli lakini nilisafiri

hadi Dar kwa treni kwa kumkwepa mkaguzi wa

behewa ili nisikamatwe mpaka nikafika. Mfukoni

nilikuwa na 500/= tu ambayo nilinunulia mihogo.

Nilifika stendi ya Mnazi Mmoja na kupanda basi

liendalo Tabata. Lilikuwa basi linalonadiwa na

wapiga debe nikajua watu wote wanakwenda

huko. Niliposhuka Tabata sikuwa na ndugu wala

rafiki wa kufikia kwake. Njaa iliuma na sikuwa

hata na senti mfukoni. Nilimuona dada aliyekuwa

dukani. Nilimfuata kumwomba msaada na baada

ya mahojiano na kumweleza ukweli alinipa kazi

ya kuuza maji. Nilipeleka mapato jioni. Malipo

yangu kwa mwezi yalikuwa 30,000/= Baada

ya miaka mitatu nilishindwana na bosi wangu

nikaacha kazi na kurudi Tabora. Maisha hayakuwa

kama nilivyotarajia.

Pamoja na kurudi Tabora, ‘ramani pia haikusoma’.

Rafiki yangu tuliyekuwa tukiuza naye mitumba

alinishauri nirudi Dar kwa dada yake ambaye

angeweza kunipatia kazi. Niliona kuna neema

inakuja mbele baada ya kukatiwa tiketi ya safari

ya Dar. Nilipofika Dar, kazi niliyopewa kwa miezi

mitatu ya mwanzo ilikuwa ni kufua na kuosha

vyombo huku nikisubiri kazi niliyoahidiwa.

Baadaye nilipewa 10,000/= kama mtaji wa biashara

ya maji ya paketi huku kila siku jioni nikitakiwa

Hamad akiwa katika moja ya mishemishe zake huko

Magomeni, Dar es Salaam

STORI YANGU

Usije mjini, jipange kwanza

5JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

kurudisha faida ya 25,000/=. Nilifanya kwa uvumilivu kwa muda

wa miaka miwili nikiamini ipo siku nitapewa mtaji wangu.

Kuna kipindi sikuwa na maelewano mazuri na yule dada. Niliugua

sana na baada ya matibabu na kupona, mume wa yule dada

alinihamishia kwa mke wake mwingine Magomeni. Kazi zilikuwa

zile zile ila penyewe ujira ulikuwa mkubwa hadi nikaweza kupanga

chumba cha 6,000/= kwa mwezi. Baadaye kidogo tajiri alibadili

biashara hivyo ‘nikapigwa chini’.

Maisha yakabadilika. Sikuwa na chanzo cha pesa tena. Nililala

popote kwa kushindwa kulipia kodi ya chumba. Nilikuwa navaa

nguo zangu zote tano nilizokuwa nazo. Safi ndiyo iliyotangulia

kwa juu na chafu kwa ndani.

Mwaka 2008, nilianza kazi ya kupiga debe katika vituo vya

daladala, kazi ambayo naifanya hadi sasa. Kazi hii ni ngumu sana

kwani unaishi katikati ya watu wenye dhiki na wenye mitindo

ya maisha yenye changamoto kama kutumia dawa za kulevya,

wizi na pombe. Ushauri wangu kwa vijana wenzangu ni kwamba

usije mjini kabla hujajipanga kwani utaweza ukajutia uamuzi

wako. Nina mchumba ambaye naishi naye na wote tunaishi kwa

kuaminiana na kujihadhari kwani tunajua kuwa maambukizi ya

VVU yapo.

Hamad akiwa na

mchumba wake

Fatuma Ally (24)

mitaa ya Magomeni,

jijini Dar.

6 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

MAMBO MAPYA

Unaishi vipi Dar?

Asubuhi na jioni utaona kila mtu ‘bize’ akiwahi mishemishe zake na wengine wakirudisha

‘majeshi’. Kutokana na tatizo la ajira, wachache wamebahatika kupata ajira maofisini tofauti

na mawazo ya wengi. Labda nikuulize, hivi umeshawahi kujiuliza waliobaki huwa wanaishia

wapi? Au maisha yao wanayaendesha vipi? Hebu chekecha akili halafu upate picha ya changa-

moto ya ajira iliyopo Bongo Dar es salaam.

Matunda kwa afya

Wakati unajenga

afya, wao wanain-

giza mkwanja, ‘fea’

kabisa yaani. Ukiwaona

mtaani unaweza

kuwadharau, lakini

wengi wao wanamudu

kulipa kodi za nyumba

na kusomesha watoto

wao kutokana biashara

ya matunda.

Kujituma ndiyo mpango mzima

Baadaye ukimkuta

jamaa kanyuka pamba

za ‘ukweenh’, unaweza

kufikiri kuwa ndiye

yule mshikaji uliyeku-

tana naye kitaa anauza

maji?

Mmachinga amka!

Wewe mmachinga ni mjasiriamali unayechipukia, hivi unafahamu

kwamba kuna Vibindo? Ni jumuiya ambayo inasaidia na kuende-

leza biashara ndogondogo kwa kuwasaidia wajasiriamali wadogo

kuanzisha kuimarisha na kukuza biashara.

Ndiyo! Kama una biashara yako na hujui jinsi ya kuisajili, kiroho safi

tu wanakuelekeza mchakato mzima. Usifanye biashara yako kienye-

ji. Kama vipi wapigie 022 2152359/ 0784 546 122 kwa maelezo zaidi.

7JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

Poza koo japo kidogo!

Unatoka zako nyumbani kuwahi shu-

ghuli zako, jua kali unajipa moyo uta-

pata sehemu ya kupumzika, upo kwenye

foleni, koo linakereketa. Ukitupa macho

dirishani unakutana na jamaa anaku-

chombeza kwa maji baridiii!

Usafi siyo wa mwili tu

Watu wengi wanakumbuka

kusafisha miili yao lakini

wanasahau kutunza mazin-

gira. Usifanye mchezo kuli-

tunza jiji na barabara zake!

Ili lionekane safi inabidi

baadhi ya watu waonekane

kivingine kabisa.

8 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Maisha ni kutafuta na sio kutafutiana, na

kila mmoja inabidi achakarike ki mpango

wake. ‘Ntoke vipi’ ndio swali ambalo kila

mtu anajiuliza kichwani. Nchumali kafikiria

akaona hapana, siwezi kutoka nikiwa hapa

hapa kijijini labda niende mjini. Twende

naye huko mjini...

9JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

10 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

11JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

12 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

JE, WAJUA?

KumbukaFanya kazi kwa bidii, jitume, maisha popote,mjini au kijijini.

Jiangalie, utapotea jombaa!

Ukweli ni huu

Fursa zilizoko vijijini hazina tofauti kubwa

na zile ambazo tunazikimbilia mjini.

Wakati mwingine, kijijini ndiyo mwake

zaidi kwani kuna ardhi kubwa ya kulima na

kufanyia vitu vingi ilimradi tuchangamshe

akili zetu kubuni kitu cha kufanya.

Bora uende mjini ukiwa na michongo

yako mizuri kijijini, kuliko kwenda kuhaha

ukaishia mikononi mwa mgambo wa jiji,

utajuta!

Jibebe

Hata kama ukipata mwenyeji

akakupa hifadhi, haimaanishi

huyo atakuwa mlezi wako ndani

ya jiji, inabidi ujue utakula wapi

na utaishi vipi. Jipange!

Zingatia haya

kwenda MJINI

unapoishi na uzitumie.

na manufaa kwako.

Eti kuzaliwa mjini ‘Form Six’ kuishi

mjini chuo kikuu! Unaacha

mipango yako ya maana ili uwahi

fasta ‘chuo kikuu.’ kakudanganya

nani?

Kuishi mjini kunahitaji ujipange na

siyo kuishi kwa kutegemea misemo

ya kale. Si wote unaowaona wako

mjini mambo yamewanyookea, la

hasha! Wengine wamepigika kweli

lakini hawataki tu kukubali matokeo

na kwenda kujipanga upya kijijini

kuliko kuishia kuhaha bila ‘ramani’

13JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

MAMA MISITU AD

14 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Wewe pia unaweza kulonga na vijana wenzako. Tuandike maoni, ushauri,

vichekesho,maswali nk, weka anuani yako na tuma ukiambatanisha na picha yako kwa Mhariri, Jarida la

Si Mchezo!, S.L.P Dar es Salaam.

[email protected] tumbukiza katika boksi la

Si Mchezo! kama lipo katika eneo unaloishi.

SAUTI YANGU Kama una chochote unachotaka kusema tuandikie ili upate fursa ya kuwaelimisha wengine

Maoni yaliyotolewa katika ukurasa huu

ni ya wasomaji, si lazima yalingane na

msimamo wa Femina.

Si Mchezo!Femina HIPSLP 2065,

DSM

Tujiheshimu kwanza

Wasichana kuvaa nguo nusu utupu

mnajidhalilisha. Siyo kujidhalilisha

tu, mnatudhalilisha hata sisi wen-

gine mbele ya wazazi wetu na jamii

kwa ujumla. Mila na desturi zetu

haziruhusu kuvaa nguo nusu utupu

ila tunafanya kuiga nchi za wen-

zetu. Tubadilike tuache tabia hiyo

na tuendeleze utamaduni wetu

ili kuokoa kizazi

kijacho.

Khadija Omary,

Dar es salaam.

Mabasi ya wanafunzi ni muhimu

Kwa mtazamo wangu naona wanafunzi hasa wanaosoma mbali na shule wanapata tabu ya usafi ri hapa Dar. Tatizo hili linawa-fanya wachelewe kufi ka shule na kukosa baadhi ya vipindi darasani. Naishauri serikali ifanye jitihada za kutafuta njia mbadala kama kutoa mabasi maalumu kwa ajili yao ili kuwa chachu ya mafanikio yao ya kielimu na katika jamii.Othman Juma,Dar es salaam.

Kamari zinaharibu vijana

Kero yangu kubwa ni kwa vijana kujihusisha na mchezo

wa kamari. Vijana wengi waliopo mitaani na hata wa-

nafunzi shuleni, hucheza mchezo wa ‘kubeti’ ambao un-

awapotezea muda mwingi na kujikuta hawafanyi shughuli

za kujiingizia kipato au kusoma. Naiomba serikali kupitia

wizara inayohusika na mambo ya vijana,

wazazi, walezi na wadau wote wa vijana

waliangalie suala hili na kuchukua hatua

haraka iwezekanavyo.

Ally A. Dauka,

Dar es salaam

Dawa za kulevya ni noma

Inasikitisha vijana wengi wa-

napotea kwa kujiingiza katika

suala la utumiaji wa dawa za

kulevya.Tunapaswa kujua

kwamba vijana ndiyo nguzo

kubwa ya taifa letu. Tuepukane

na tabia hizo hatarishi zinazot-

ufanya tupoteze

malengo yetu.

Mary R.

Mwandu,

Dar es salaam.

15JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

“Inatosha,” anasema Shukama mume wa mama wa nyumbani aitwaye Ndope kwa miaka 10 sasa. Shukama anadhani anampenda mke wake ambaye ni mjamzito, lakini kanasa kwenye mtandao wa mapenzi. Ana wapenzi wengine wa nje (nyumba ndogo). Siku ya siku, mambo yakawa si mambo, kama anavyosimulia mwenyewe:

“Juzi nilipokea ujumbe mfupi kwenye simu

yangu, mmoja kati ya wapenzi wangu

Anita alikuwa ananiulizia kuhusu kodi ya

pango na ujumbe mwingine kutoka kwa

mpenzi wangu Zawadi aliyekuwa anataka

hela kwa ajili ya kulipia karo ya shule ya

mdogo wake. Mezani nyumbani kwangu

kulikuwa kuna karatasi yenye ujumbe

kutoka shuleni kwa mwanangu wa kiume

ukinitaka kulipa karo ya shule ndani ya

siku mbili la sivyo mwanangu

atafukuzwa shule.

Jana niliamua kumsindikiza mke

wangu kliniki, baada ya kutafakari ombi

Rajafa. Kliniki tulielezwa mengi kuhusu

elimu ya afya kwa mama mjamzito na

mtoto aliye tumboni, umuhimu wa kuzuia

maambukizi ya VVU kutoka kwa mama

tumboni,

pamoja. zinazochangia

ya VVU, ikiwemo kuwa na uhusiano wa kingono na wanawake zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Mafunzo haya ya kliniki na zile kasheshe zingine za ada na pango, zilinifanya nitafakari kwa kina juu ya tabia zangu na

mtandao wa ngono.

Hii ni moja ya stori tulizowahi

kusikia mara nyingi kutoka kwa

kwenye mitandao ya kingono.

Wakati mwingine hawatambui

hatari iliyopo kwenye mitandao ya

aina hiyo ni ya kweli, mpaka

kitokee kitu cha kutisha. Sikiliza

stori hii:

ya sekondari na kwa sasa amejiunga na masomo ya chuo kikuu kitivo cha

kingono na Sikioni ambaye ni mwanachuo mwenzake wa mwaka wa kwanza.

Mbali na kuwa na uhusiano ya kingono na Sikioni, pia ana uhusiano ya kingono na Mzikombo ambaye ni mfanyabiashara maarufu. Matokeo ya mtihani wa muhula wa kwanza wa masomo yameonyesha kuwa

inamlazimu kurudia masomo matatu.

Kiboboko na kumshawishi wafanye ngono kwa masharti ya kupewa alama

kwa masomo mawili yaliyobaki.

kuwa yuko peke yake katika uhusiano ya kingono na wanaume wake. Kwa kuwa

alikuwa mzuri na mwenye akili hakuona sababu itakayomfanya mwanamume wake awe na mwanamke mwingine.

Alipatwa na mshangao siku alipomtembelea Mzikombo nyumbani kwake na kumkuta anafanya ngono na mwanafunzi mwingine aitwaye Jusiku.

Kitendo hiki kilipiga kengele akilini

kwa kina kuhusu hali ya afya yake. Akaamua kutembelea kituo cha afya ili kupata uhakika wa aina ya majanga aliyojitumbukiza. Aliamua kupima VVU na hakuwa na maambukizi.Alishangaa kwa kuwa alikuwa kwenye mtandao wa ngono na bado amefani-kiwa kuwa salama. Alijua siyo kila mtu

mwenye hiyo bahati. Akaamua kuach-ana na mitandao ya ngono. Bila shaka kuna faida nyingi za kujitoa kwenye mitandao ya ngono zikiwemo kuepuka hatari ya kupata maambukiziya VVU, kumlinda mwenza wako dhidi ya maambukizi ya VVU, kuepuka gharama zisizo za lazima za kuhudumia wana- wake wengi kwa wakati mmoja katika kukidhi mahitaji yao ya maisha, kuleta furaha na maelewano mazuri na mwenza wako nyumbani. Kwa mantiki hii, tujiangalie kwa kinasisi wenyewe, tujitathimini na kupima faida dhidi ya hasara na kusema...

KWA NINI WATU WANAACHANA NA MITANDAO YA KIMAPENZITAHARIRI AWAMU YA PILI

Pia nilijifunza tabia hatarishi

mtu kupata maambukizi

wangu mpendwa na mtoto tunayemtarajia na kisha kuamua INATOSHA. Hapana tena

lake na ushauri wa rafiki yangu.

Uhandisi. Sotafia ana uhusiano wa

kwenda kwa mtoto aliye ushauri

na kupima

Sotafia alibahatika kufaulu mitihani yake

16 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Utangulizi

Dada tuma eeh! Ngoja kwanza,Producer mbeziYo ha haaaa 0444

Ubeti wa 1Picha linaanza kama muvi ya Solomoni, Gafl a vumbi linazidi wajanja wanavaa miwani, Hii ndio dar karibu ili usijisikie nyumbani,Hapo Ubungo usinunue simu utauziwa sabuni, Panda daladala tukutane buguruni, kuna watu wanapiga ndole utadhania majiniGizani usiku utaona rangi zote za bikini, wanauza mwili ili wanunue wali maini, usicheke broo! Kwa sababu mi sio Mr. Bean,chunga wallet hapa kuna wizi wa mfu-koni, haukawii kushuka kwenye gari hauna phone, kuwa makini uvukapo huku gari hazipigi honi,dala dala zinaa,Bajaj zinakesha macho, Kama huamini ngoja siku ije uamini we Tomaso, Wasio na kazi wanashindia stori za freemason,Wajanja wamepanga sinza, Kino na Tabata, Mchana wanazibua vyoo usiku wanakula bata, Usikojoe ovyo bro! Mgambo watakukamata,Hii ndio dar, mbona unadata kabla hata hujapata starter?

Kiitikio x 2Mmh bata ni daily, daily’Karibu bushman kaa chini tukupashe habari Shangaa mataa Dar ugongwe na gari (Dar es salaam ya sasa)

Ubeti wa piliKaribu sana kwenye hili jiji la joto, Uswahilini chumba kimoja baba mama na watoto, Si ulisikiaga ma-bomu ya gongo la mboto?Yalifanya rafi ki yangu wa damu akafi a

Ghetto,Yaliacha kovu kubwa kama la mba-gala, Dar es salaam watu wengi tu hawanaga pa kulala,Kama unataka mirungi twen’ zetu mitaa ya ilala, Magomeni, mi ujanja wangu wote niliitwa fala,Watu wanaingiza pesa wakiwa wamelala, Watu wengi toka waje ha-wajawahi kurudi kwao,Sababu hawana nauli japo wamemisi ndugu zao, Kuhusu kushinda na njaa hapa ndo zao, Wauza sura wanaishi kwa kuuza mademu zao,Mama anauza bangi, Baba amekata ringi anashinda anacheza bao,Wake zao wanazini kulisha watoto wao, Vijana wao wanatembeza karan-ga, wanatembeza maji,wanatembeza vocha,Jioni wanakabidhi hesabu kwa bosi wao,

Hii ndio dar, ukipenda unaweza kuiita bongo, Machizi wakikosa hela ya bia wanakula gongo,See, haiwi siri uswahilini ukipata mchongo, Wapangaji watakuandama bro mpaka utahama,Ni majungu mixer wanga, utaenda tu kwa mganga, Utapo lala Ghetto kwako kasha ukamwagiwa mchanga

Kiitikio x 2Mmh bata ni daily, daily’Karibu bushman kaa chini tukupashe habari Shangaa mataa Dar ugongwe na gari (Dar es salaam ya sasa)

Ubeti wa tatuDar es salaam ingekuwa nchi, huku Rais angekuwa LowasaHuku watu washashtukia kuna mchezokwenye siasa,Usione watu wamependeza, wengine hawana hata mia,

BURUDANI

Wimbo: Karibu DarWasanii: Kala Jeremiah akimshirikisha Ben Paul

17JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

Hapa mboga ni maharage, nyanya chungu na bamia,Brother man anatembea toka keko kwa miguu, Anakwenda mlimani city kununua mkate tu,(Are you on the facebook?) Ndo mas-wali ya maduu,Ukitaka demu wa peke yako kata mgomba lala juu,Ukimwita demu wako bar wanakuja crew, Utachunwa mpaka ubaki na raba ubaki miguu juu,Hapa bomba halijatoa maji mwezi mzima,Hii ni uswahilini tu na sio kwa jiji zima, Twende Mbezi au Masaki yanatoka mwaka mzima,Katiza Kwa Mtogole uporwe simu mchana,Siku hizi mwanaume anavaa suruali ya kubanaa, Siku hizi dada’ko anakalio za kichina, ukimtafuta humpatiAmeshakuwa wa kimjinimjini

!!! !Nimetoka wapi?DOGO: Baba kwani mimi

nimetoka wapi?

BABA: Dah! mwanangu mbona

unaniuliza swali gumu hivyo?

Hebu kaa hapo nikuhadithie.

Nilikutana na mama yako

kituo cha basi siku moja wakati

anatoka kazini mvua kubwa

ikaanza ikatulazimu tuchelewe

sana kupanda basi, hivyo tu-

kazoeana sana. Baada ya kama

miezi mitatu tukaona ni vyema

tuoane, tukawaeleza wazazi

wetu wakatukubalia, harusi

ikafanyika, tena kubwa sana,

tukaanza kuishi pamoja na kwa

kifupi ndiyo wewe ukapatikana.

Ukikua kidogo utanielewa nina

maana gani

DOGO: Haya, ila mwalimu

atanipiga nisipomwambia ke-

sho, katuambia wote tuwaulize

wazazi wetu tumetoka wapi.

Mwalimu wetu kasema yeye

ametoka Bukoba.

Ndani ya DaladalaDaladala lilipofi ka Manzese konda

akauliza;

KONDA: kuna mtu anashuka?

MREMBO: Tumeyaacha nyumbani,

hapa tuna mitandio tu!! Kufi ka

Ubungo Maziwa, yule dada aliyele-

ta nyodo akataka kushuka

MREMBO: Konda nashuka maziwa

KONDA: Kayanunulie SIDIRIA

yasishuke

Roboti laumbua!Baba mmoja alinunua roboti maal-

umu kwa lengo la kudhibiti tabia ya

uongo katika familia yake. Kwamba

mtu akisema tu uongo basi roboti

linamtandika vibao dakika hiyo hiyo.

Siku moja baba akamuuliza mwa-

nae: “Mage umekuwa wa ngapi

kwenye mtihani?” Mtoto akajibu:

“Wa kwanza!” Bila kuchelewa roboti

likampiga kibao. Baba akaanza kuji-

nadi: “Enzi zangu mimi kila mtihani

nilikuwa nashika namba moja!” Saa

hiyohiyo roboti likamnasa kibao.

Mtoto alipoanza tu kucheka, mara

mama akatokea na kumfokea: “Un-

acheka nini sasa, hujui kama huyo ni

baba yako?” Bila kuchelewa roboti,

likamtandika kibao na yule mama!

Duh...

18 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

RUKA JUU

Joseph nd’o jembe!

Baada ya wiki 13 za kutifua ardhi, kujifunza na

kushindana, hatimaye mshindi wa msimu wa

pili wa shindano la Ruka Juu amepatikana! Joseph

Kizito, 28, kutoka Nkasi, Rukwa, ndiye mkali!

Joseph, amejinyakulia kitita cha shilingi milioni

tano, “Sikuwahi kufikiria kwamba mimi na

kilimo changu ningeweza kupata hadhi hii

au fursa ya namna hii. Kupitia Ruka Juu, watu

sasa wananifahamu na wanakuja kwangu kwa

ushauri,” anaeleza Joseph.

Joseph ni nani?

“Watu waliomzunguka walimfahamu kama

mkulima wa nyanya ambaye aliwahi kuvamiwa na

wezi, wakampora fedha, lakini hiyo haikumkatisha

tamaa ya kulima,” anasema Amabilis Batamula,

mtangazaji wa Ruka Juu ambaye aliwatembelea

washiriki wote sita katika mashamba yao wakati

wa shindano. “Sasa atafahamika kama Mshindi

wa Ruka Juu.”

Ushindi haukuwa rahisi

Joseph, anasema kuwa kushiriki shindano la Ruka Juu

haikuwa kazi ndogo, hasa lilipokuja suala la kusaka

kura. Anaeleza jinsi alivyolazimika kuwa ‘mwanasiasa’

kwa muda wote wa shindano! Alipita nyumba hadi

nyumba wilayani Nkasi, akibisha hodi, kujitambulisha

na kuomba kupigiwa kura “Nakumbuka namna

nilivyokuwa nikiwashawishi watu kwamba ushindi

huu usingekuwa wangu peke yangu, bali wa wana-

Nkasi wote na wilaya yetu na hata utaonyesha juhudi

zetu katika kilimo.”

Joseph, mwenye mke na watoto wanne,

anasema “Mke wangu hakuwa akiunga

mkono uamuzi wangu wa kushiriki Ruka

Juu na alikuwa na uhakika kwamba

sitoshinda. Alianza kubadili mawazo yake

alipoanza kuona alama zangu kwenye

TV wiki chache baadaye na baada ya

ushindi alinipigia simu kunifahamisha jinsi

alivyosherehekea pamoja na wananchi

wa Nkasi na walikuwa wakinisubiri kwa

hamu.”

19JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

Juhudi binafsi ni muhimu.

Naweza kumsaidia mtu

yeyote atakayehitaji msaada

wangu na nimekuwa nikifanya

hivyo hata kabla ya Ruka Juu.

Mkulima ‘Mpya!’

“Nimejifunza mengi wakati wote wa shindano.

Nahitaji mbinu bora za kupata masoko, sitolima bila

kuwa na uhakika wa soko. Nitamtumia bibi shamba

na bwana shamba zaidi kuanzia sasa,” anasema.

Amejifunza umuhimu wa kuchukua mkopo benki,

“kuwa katika shindano si tu kwamba kumewawezesha

watu kuamini kwamba mimi ni mkulima mzuri,

bali pia ni mwaminifu. Meneja wa Benki ya NMB

alinipigia simu na kuniomba nionane naye mapema

iwezekanavyo kwa ajili ya mkopo.”

Hongera!

Joseph pamoja na washiriki wengine wote wa Ruka Juu; Aziza, Tatu, Mustafa, Yusta na Lawriani. Nyote mlifanya vizuri na kwa hakika mifano yenu imebadili mitazamo ya jamii juu ya kilimo.

20 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

NGUVU ZA MWANAMUME

Ngono na mapenzi

Kumekuwa na mitazamo

mbalimbali katika jamii

ambapo inaonekana hakuna

mapenzi bila ngono. Hii

inatokana na watu kuwa na

mazoea kwamba urafiki kati

ya msichana na mvulana basi

kuna viashiria vya ngono.

Mapenzi yanaweza kujengeka

Unapomuona mtu kwa mara ya kwanza

Baada ya kupendezwa na tabia au muonekano

wa mhusika

Pia yanaweza kufifia pale unapogundua

upungufu wa mhusika

Ngono je?

na ya kiume (Japo kumekuwa na mwingiliano

wa tofauti na iliyozoeleka kunakohusisha

jinsia moja)

puchu

Msukumo unaotoka katika jamii hufanya wengi

kujiingiza katika ngono japo bado hawapo tayari

kimapenzi.

KumbukaMapenzi siyo lazima yahusishe ngono. Inawezekana pakawepo mapenzi ya dhati na yasihusishe ngono.

Mapenzi ni nini?

Mapenzi ni hisia ya upendo kwa mtu

fulani au kitu fulani. Mfano utasikia

mtu akisema, “Napenda sana mpira

wa miguu” tunapozungumzia

suala la mapenzi katika uhusiano

limegawanyika katika sehemu mbili

Mapenzi yanayohusisha hisia

za mwanamume kwenda kwa

mwanamke au mwanamke

kwenda kwa mwanamume

Mapenzi baina ya wazazi,

watoto, ndugu na marafiki.

Mapenzi ni hisia zenye msisimko wa

pendo la dhati zinazotoka moyoni

kwa mtu kwenda kwa mwingine

21JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

NGUVU ZA MWANAMKE

Kweli, inawezekana!

Wape laivu

Kama upo katika mtandao

wa uhusiano na unataka

kuukatilia mbali, waambie

kuwa haupo tayari kuen-

delea katika uhusiano hayo

kwa sababu:

kwa dhati

kulinda afya yako na ya

mwenza wako

matumizi yasiyokuwa

na lazima

-

awishi uwe na wenzi

wengi ‘wapotezee’

Vuta picha, upo nyumbani umetulia na barafu wa moyo wako mkitaniana na kufurahi

pamoja. Simu yako ipo mezani lakini moyoni huna amani hata chembe. Kila mara mwenza

wako akitaka kuishika unatoa sababu zisizoeleweka, moyoni unajua kabisa kuwa simu yako ni

“weka mbali na mpenzi”.

KumbukaMawasiliano ndiyo msingi wa mapenzi, tengeneza mawasiliano mazuri na mwenza wako na kuvunja mtandao wa ngono.

Unaweza kuepuka hili

Mweleze mwenza wako kama ulishawahi kuwa na

uhusiano

Tumia muda mwingi na mpenzi wako baada ya shughuli

zako za kila siku

Tuma ujumbe mwingi wa kimahaba kwa simu

mnapokuwa mbali.

KUWA MUWAZI kwa mwenza wako, kama hakuridhishi

mweleze, muongeze ‘mautundu’

Kaa na mwenzi wako mpange kwa pamoja bajeti yenu ya

mapato na matumizi.

22 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Kona ya mtaa

Niaje mwana? Maisha ya mtaa yanasemaje? ‘Sista’

siyo kwamba nakupotezea! Nilikuwa namaliza

kusalimiana na mshkaji, halafu nije kwako, si unajua raha

ya mbio ni kumaliza! Mambo vipi? Joto la Dar linasemaje?

Umekwishaanza kuzoea mazingira au yanakuelemea? Poa

tulia basi nikupe mkanda wa jinsi picha linavyokwenda.

Tuliza boli

Usibabaike na kila unayemuona

ukamuamini, ukampa moyo wako na

mapenzi motomoto, utajikuta kaburini.

Hapa hapendwi mtu linapendwa

pochi! Kumbuka kupanga bajeti katika

mapato, matumizi na kutunza pesa.

Ukiendekeza washkaji na kula bata

utakuwa jalala la dhiki.

Kuna wazee ambao ni sukari za vijana,

chunga sana hawana maana zaidi ya

kutaka kuuchezea utu wako.

CHEZASALAMA

23JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

Gogozembe aka kijiwe

Hapa ndiyo tunapokutana na kush-

irikishana stori zote za kitaa, kupeana

dili na michongo mbalimbali. Uki-

zubaa unaweza ukakuta jioni im-

eingia na huna kitu mfukoni wakati

mwenye kijiwe chake biashara inaen-

delea kama kawa na jioni anahesabu

‘mpunga’ wake . Inawezekana ikawa

ni saluni au kwa yule fundi viatu au

wa baiskeli pale kwenye mti wenye

kivuli murua.

Hapa hapa

dawa za kulevya wakakushawishi. Jiepushe nao.

yao wanakutafutia mabuzi. Watenge kabla

hawajakutenda.

kuiga tabia zao chafu. Kubali kuwa mshamba.

kama umekuja Dar kutafuta maisha au kufa.

Kumbuka

Kuna malengo ambayo umejiwekea wakati unakuja mjini kutafuta maisha, yazingatie hayo mengine yaache siyo yako.

24 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Mich

oro:

bab

atau

car

toon

s 201

3 Wenye nazo

wanavyokaba

hadi kuwaweka

wengine katika

mazingira hatarishi.

Ni Jukumu lako

kuchagua mbivu

na mbichi! Fuatilia

mchezo huu…

JIlinde...

KATUNI

25JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

26 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Haya yaliyomkuta binti huyu yanahitaji kufikiri na kuchukua uamuzi ambao haukudhuru wala kumdhuru mwingine. Tuombe ushauri tunapokutana na magumu yanayotushinda

27JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

Jambo lililotokea katika katuni stori hii linatokea sana katika

maeneo mengi yenye huduma za kijamii kama vile nyumba

za kulala wageni. Kuna njia kadhaa za kukabiliana nalo kama

vile;

kinachokukabili

limevuka mipaka kama kulazimishwa kufanya kitu

usichokitaka

mwili wako

Toa taarifa kwa vyombo vya dola ili kumnasa huyo

anayejihusisha na kuwauza wasichana kwa wateja wake.

UKWELI WA MAMBO

Sema hapana, mlinde mwenzako…

Ni dhahiri kabisa kwamba

udhalilishaji wa wanawake

hapa Tanzania bado ni tatizo

kubwa. Sehemu nyingi hasa

zenye biashara ya pombe (bar),

matendo hayo huonekana hata

mchana kweupeee. Wadada

wanaohudumia wateja usiku

na mchana wameelezea kero

zao na kusema hawana jinsi.

Kumbuka

Mabadiliko chanya huanza na wewe! Ukisema hapana na kuonyesha mfano, wengi watakuiga na kuchukua hatua kisha kujikomboa huku tukitoa elimu kwa wale wachache wanaotumia madaraka yao kinyume na taratibu za ajira.

Usikubali kuburuzwa

Mwenye uamuzi wa kutumia

mwili wako vibaya au vizuri

ni wewe.

bosi kwani unahatarisha

maisha yako kwa kupata

mimba zisizotarajiwa

na magonjwa ya ngono

ikiwemo VVU

kwa kujiendeleza

katika kupata taarifa

sahihi na kupata ujuzi

utaokujengea uwezo

wa kusema hapana kwa

matendo kama hayo.

Jiamini.

28 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

SEMA, TENDA

Mara nyingi, asilimia kubwa ya vijana wakikaa kijiweni, mbali

na stori zote, huishia kukandia baadhi ya mambo ambayo

yamekaa vibaya katika mtaa wao au karibu na eneo wanaloishi

wakisahau wao pia ni sehemu ya hilo tatizo kwa kuendelea

kuliruhusu liwepo katika jamii yao. Hii ni tofauti kwa ‘wana’

wa Tandale. Tandale Youth Centre wanapokutana, wanakuwa

na mtazamo chanya juu ya maendeleo ya kata yao ya Tandale.

Tusilalamike, tuchakarike!

Tandale Youth Centre ni nani?

Wao wanajitambulisha kama wanaharakati kutoka Kata

ya Tandale. “Harakati zetu zinahusisha vijana kutoka mitaa

sita. Vijana hawa ni wale wali o mashuleni na nje ya shule.

Wasichana kwa wavulana, alimradi tu wawe na ‘mzuka’ wa

kuleta maendeleo katika kata yetu” anaeleza Hassan Pukey

ambaye ni mratibu wa matukio katika kikundi hicho.

Uelimishaji rika

Vijana hawa wanatoa elimu katika maeneo makuu

mawili

Elimu ya afya

Utambuzi na tiba ya magonjwa ya ngono

Uzazi wa mpango

Kushawishi vijana kwenda kupima VVU kwa

hiyari.

Uraia

Wajibu na haki za msingi kwenye shule za msingi,

nyumba kwa nyumba, Camps za vijana, mata-

masha. Kwa wale ambao katikati ya wiki hawana

muda wa kupata elimu wamewatengea darasa lao

siku ya jumapili. Yote haya yanafanyika ndani ya

kata yao.

Malengo

Kuhusisha vijana kwa kuwa-

jengea uwezo wa kutambua

fursa za uchumi na kuzitumia

Kuhakikisha kila mwana

Tandale ana elimu ya afya ya

uzazi

Kutengeneza mtandao wa

vijana wa Tandale

Kutumia vipaji vya vijana

kama ajira.

Kupambana na maambukizi

mapya ya VVU

Kufungua Saccos ya vijana.

29JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!

Mafanikio

jamii

Tandale katika shughuli mbal-

imbali.

Changamoto zinazowakabili

vipeperushi n.k

kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kijamii

kutokana na changamoto za kimaisha

30 Si Mchezo! JULAI-AGOSTI 2013

Betty Liduke ni rafiki mkubwa

wa vijana, hata wewe unaweza

kulonga naye. Ni msambazaji

mkubwa wa Jarida la Si

Mchezo! Mkoani Njombe. Ni

mshauri nasaha na ni Mratibu

wa Kitengo cha Udhibiti

Ukimwi katika Kampuni ya

TANWAT, Njombe.

Mwandikie kupitia

Jarida la Si Mchezo!

Si Mchezo!

S. L. P. 2065

Dar es Salaam

SMs; Andika SM acha nafasi, andika maoni yako kisha tuma kwenda namba 15665

na utuambie kama ungependa

uchapishwe.

USHAURI

Swali

Dada yangu inabidi umwambie mume

wako asiogope kumwambia kaka yake

juu ya uwepo wake na jinsi anavyowa-

bana. Kama haitawezekana waite wazazi

wa pande zote mbili ili kutatua tatizo

hilo lakini dada usiache

ndoa yako

Geradi G.Nyamoga,

Dar es salaam.

Unatakiwa ujadiliane na mumeo ili

muone jinsi gani mtatatua hilo tatizo.

Kama itashindikana mtafute mshenga

wenu ili awaeleze wazee.

Usichukue uamuzi wa ha-

sira na usiwe na haraka.

Farida M.Membe,

Dar es salaam.

Mpe shemeji yako mwongozo wa

ndoa jinsi unavyotaka kwa kum-

shirikisha na mumeo. Mweleze

utaratibu wa ndoa, hali yenu ya

maisha na jinsi mnavyoshindwa

kuifurahia ndoa yenu. Arudi

nyumbani au aangalie utaratibu

mwingine wakati akitafuta kazi.

Maulid

Mziwanda,

Dar es salaam.

Mimi nina shida, naomba ushauri kwa wenzangu. Mimi ni msichana wa miaka 30, nimeolewa.

Nampenda na namheshimu mume wangu. Tatizo ni kaka yake. Amekuja mjini mwaka mmoja

uliopita kutafuta kazi na hadi leo anasema hajapata. Tunaishi kwenye chumba kimoja na sebule na tunaishi naye

kwa mwaka mzima sasa. Kusema kweli nimechoka. Nahitaji kufurahia ndoa yangu. Anatubana na nakosa uhuru na

faragha. Mume wangu naona anashindwa kumwambia kaka yake aondoke japo anajua sifurahii tena uwepo wake.

Nimeamua nifungashe vilivyo vyangu niondoke au yeye aondoke. Tafadhali naomba ushauri

Msomaji wa Si Mchezo!

Dada vumilia usiondoke kwani

ukiondoka shemeji yako na ndugu

wa mwanamume watajisikia vibaya.

Mshauri mumeo aendelee kumtafu-

tia kaka yake kazi ili aweze kujitege-

mea. Hiyo ni moja ya changamoto za

maisha ya ndoa.

Zawadi Khamis,

Dar es salaam.

Mimi nina mke na mtoto mmoja ambaye nilizaa na mwanamke mwingine ni-

kiwa Ifakara. Nikimshauri mke wangu kwamba nikamchukue mtoto Ifakara ha-

taki, anasema nikienda sitarudi. Nifanyeje ili nimpate mwanangu?

Baba .K. Mmulunga

Newala

Nakupongeza kwa kuuliza swali zuri. Kuishi ni kujifunza na kuwa

kwenye ndoa kunahitaji kuvumilia na kushirikishana katika kila

jambo, kufunga mizigo kuondoka siyo suluhu. Kaa jadiliana na

mumeo pamoja na huyo kaka wa mume wako mwelezeni hali

halisi mliyonayo na baada ya hapo chukueni uamuzi ulio sahihi

utakaojenga nyumba yenu.

SWALI LA TOLEO LIJALO

31JULAI-AGOSTI 2013 Si Mchezo!