KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika...

17
KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA WATENDAJI WA TRENI ZA MWAKA 2019 MPANGILIO WA KANUNI Kanuni Jina SEHEMU YA KWANZA MAELEZO YA AWALI 1. Jina la Kanuni. 2. Matumizi ya Kanuni. 3. Tafsiri ya Kanuni. SEHEMU YA PILI UTHIBITISHAJI WA MADEREVA 4. Uthibitishaji wa Madereva. SEHEMU YA TATU UTARATIBU WA KUPATA VYETI 5. Maombi ya Cheti. 6. Utoaji wa Cheti. 7. Kamati ya Uthibitishaji. 8. Majukumu ya Kamati ya Uthibitishaji. SEHEMU YA NNE UTOAJI USIMAMISAJI NA UFUTAJI WA CHETI 9. Utoaji wa Cheti cha Umahiri wa Dereva. 10. Ada ya Maombi. 11. Kibali cha Kuvuka Mipaka. 12. Alama Jumuishi. 13. Kusimamisha au Kufuta Cheti. 14. Kuhuisha Cheti. 15. Kuhamisha Matumizi ya Cheti. SEHEMU YA TANO USAJILI WA WATENDAJI WA TRENI 16. Maombi ya Usajili. 17. Matakwa ya Usajili. 18. Utoaji wa Vitambulisho vya Usajili. 19. Kuhamisha Matumizi ya Kitambulisho. 20. Kupotea kwa Kitambulisho.

Transcript of KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika...

Page 1: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA WATENDAJI WA

TRENI ZA MWAKA 2019

MPANGILIO WA KANUNI

Kanuni Jina

SEHEMU YA KWANZA

MAELEZO YA AWALI

1. Jina la Kanuni.

2. Matumizi ya Kanuni.

3. Tafsiri ya Kanuni.

SEHEMU YA PILI

UTHIBITISHAJI WA MADEREVA

4. Uthibitishaji wa Madereva.

SEHEMU YA TATU

UTARATIBU WA KUPATA VYETI

5. Maombi ya Cheti.

6. Utoaji wa Cheti.

7. Kamati ya Uthibitishaji.

8. Majukumu ya Kamati ya Uthibitishaji.

SEHEMU YA NNE

UTOAJI USIMAMISAJI NA UFUTAJI WA CHETI

9. Utoaji wa Cheti cha Umahiri wa Dereva.

10. Ada ya Maombi.

11. Kibali cha Kuvuka Mipaka.

12. Alama Jumuishi.

13. Kusimamisha au Kufuta Cheti.

14. Kuhuisha Cheti.

15. Kuhamisha Matumizi ya Cheti.

SEHEMU YA TANO

USAJILI WA WATENDAJI WA TRENI

16. Maombi ya Usajili.

17. Matakwa ya Usajili.

18. Utoaji wa Vitambulisho vya Usajili.

19. Kuhamisha Matumizi ya Kitambulisho.

20. Kupotea kwa Kitambulisho.

Page 2: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

SEHEMU YA SITA

MASHARTI KWA WATENDAJI WA TRENI

21. Masharti kwa Madereva na Treni Gadi.

22. Katazo kwa Watendaji wa treni.

SEHEMU YA SABA

MAKOSA NA ADHABU

23. Makosa na adhabu

24. Uwezo wa kufifisha makosa

MAJEDWALI

Page 3: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

NOTISI YA SERIKALI………………imetolewa …………………

SHERIA YA UDHIBITI USAFIRI ARDHINI (SHERIA NA. 3

YA MWAKA 2019)

Kanuni

(Zimetengenezwa chini ya kifungu cha 45)

KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA WATENDAJI WA

TRENI ZA MWAKA 2019

Page 4: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

SEHEMU YA KWANZA MAELEZO YA AWALI

Jina la kanuni 1. Kanuni hizi zinaweza kutambuliwa kama Kanuni za Uthibitishaji wa Madereva wa

Treni na Usajili wa Watendaji wa Treni za Mwaka 2019 Matumizi ya Kanuni 2. Kanuni hizi zitatumika kudhibiti madereva na Watendaji wa treni

Tafsiri 3. Katika kanuni hizi, endapo matakwa hayatahitaji vinginevyo:-

Sheria Na. 3 ya mwaka 2019

“Sheria” inamaanisha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini;

Act No. 3 of 2019 “Mamlaka” inamaanisha Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Ardhini (LATRA) kama

ilivyoanzishwa kupitia kifungu cha 4 cha sheria “Cheti cha Umahiri” kinamaanisha kibali kilichotolewa na Mamlaka kwa Dereva wa treni

GN. No…… “cheti” inamaanisha cheti kinachotolewa kwa dereva wa treni;

“Kamati ya Uthibitishaji ” inamaanisha kamati yenye jukumu la kuthibitisha madereva wa sekta

inayodhibitiwa kupitia sehemu ya 7 ya kanuni hizi

“Watendaji” inamaanisha Dereva, Treni Gadi, Mtunza Behewa na Mkaguzi wa Tiketi;

Sheria Na. 3 ya Mwaka

2019

“Mkurugenzi Mkuu” inamaanisha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka chini ya kifungu cha 15 cha

sheria

“nyaraka” inamaanisha nyaraka yeyote iliyotolewa au kupokelewa na Mamlaka;

“Tabibu” inamaanisha Tabibu aliyesajiliwa na “Baraza la Matabibu la Tanganyika” au aliyethibitishwa na mamlaka kukagua madereva wa treni;

“Alama Jumuishi” inamaanisha mfumo wa kuratibu umahiri wa dereva ambapo alama

zitapunguzwa kulingana na makosa na endapo alama zitakuwa chini ya kiwango kilichowekwa

kikanuni Dereva atafutiwa usajili

Kifungu Na. 95 “Dawa za kulevya” inabeba maana kama ilivyofafanuliwa kwenye Sheria ya Kuzuia Usafirishaji

wa Dawa Haramu (Drugs and Prevention of Illicit Traffic in Drugs Act);

“Afisa wa Mamlaka” inamaanisha Mkurugenzi, Meneja au Afisa yeyote wa Mamlaka;

“Abiria” inamaanisha mtu yeyote anayesafiri kwenye treni na ana Tiketi halali ya kusafiria;

“rejista” inamaanisha mchanganuo wa taarifa za usajili wa Watendaji wa treni

“ratiba” inamaanisha nyaraka iliyotolewa na Mtoa Huduma za reli ikionyesha muda wa treni

kuanza safari na muda wa kufika kwenye vituo vilivyoainishwa;

“Dereva wa Treni” Mtu aliyethibitishwa na Mamlaka kuendesha treni;

“treni” inajumuisha kichwa cha treni, kichwa cha treni kinachopanga mabehewa, kichwa cha

treni na mabehewa au kiberenge kilichoruhusiwa kusafiri;

SEHEMU YA PILI

UTHIBITISHAJI WA MADEREVA Uthibitishaji Madereva

4-(1) Mtu yeyote hatoruhusiwa kuendesha treni pasipo kuwa amethibitishwa na Mamlaka.

(2) Dereva atakayeendesha treni na kuvuka mipaka ya Tanzania Bara atatakiwa kuhakikisha

ana vitu vifuatavyo -

(a) Cheti cha usajili kilichotolewa na Mamlaka kwa mujibu wa kanuni hizi; au (b) Cheti cha Usajili kilichotolewa na mamlaka husika kwenye nchi anakotoka.

Page 5: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

SEHEMU YA TATU UTARATIBU WA KUPATA VYETI Maombi ya Cheti 5.-(1) Mtu yeyote anayekusudia kupata usajili wa Mamlaka kuwa Dereva wa treni anatakiwa

kuwasilisha maombi kwa Mamlaka katika muundo ulioonyeshwa kwenye Jedwali la Kwanza

(2) Maombi yatakayotumwa kwa mujibu wa kanuni ya (1) yataambatana na:

(a) nakala iliyothibitishwa ya cheti cha kuzaliwa au nyaraka nyingine ; (b) nakala iliyothibitishwa ya cheti cha elimu ya sekondari; (c) nakala iliyothibitishwa ya cheti cha mafunzo ya awali ya udereva wa treni toka kwenye

chuo cha reli kinachotambuliwa na serikali; (c) uthibitisho toka kwa mwajiri juu ya utendaji kazi usiopungua miaka miwili kwenye

udereva wa treni; (e) uthibitisho wa malipo ya ada ya usajili kwa Mamlaka; (f) Ripoti ya afya ya hivi karibuni iliyotolewa na Tabibu.

(3) bila kuathiri masharti ya kanuni ya (1) dereva yeyote - (a) aliyemaliza mafunzo ya awali ya kuendesha treni; na (b) mwenye uzoefu wa kuendesha treni usiopungua miaka mitano Atawasilisha maombi yake kwa utaratibu maalum utakaowekwa na Mamlaka.

Utoaji wa Vyeti

6. - (1) Mamlaka baada ya kujiridhisha kwamba mwombaji amekidhi matakwa ya maombi ya vyeti, itatoa cheti kwa mwombaji.

(2) Cheti kitakachotolewa na mamlaka chini ya kanuni (1) kitabeba taarifa zifuatazo–

(a) Jina na Anwani ya dereva wa treni aliyethibitishwa; (b) Muda wa uhai wa cheti husika; na (c) Masharti ya cheti.

Kamati ya

Uthibitishaji 7. -(1) Mkurugenzi Mkuu atateua kamati ya Uthibitishaji itakayoundwa na wajumbe wafuatao-

(a) Afisa Mkaguzi wa reli; (b) Mkaguzi wa vichwa vya treni; na (c) Mwanasaikolojia au Tabibu. (2) Kamati hii itadumu kwa kipindi cha miaka mitatu na inaweza kuongezewa kipindi kingine

kimoja. (3) Mamlaka itaandaa mwongozo wa namna Kamati itakavyotekeleza majukumu yake kwa

mujibu wa kanuni hizi.

Majukumu ya Kamati

ya Uthibitishaji 8- (1) Majukumu ya Kamati yatakuwa kama ifuatavyo:

(a) Kuchambua maombi ya uthibitishaji wa madereva yaliyowasilishwa;

(b) Kuandaa taarifa ya uchambuzi wa maombi; na

(c) Kutekeleza majukumu mengine watakayopangiwa na Mkurugenzi Mkuu

SEHEMU YA NNE

UTOAJI USIMAMISAJI NA UFUTAJI WA CHETI Utoaji wa Cheti cha

Umahiri wa Dereva 9.-(1) Mamlaka baada ya kujiridhisha na uwasilishaji wa maombi kwa mujibu wa kanuni hizi,

itatoa cheti kwa ajili cha umahiri wa Dereva

(2) Kwa mujibu wa kanuni hizi Umahiri wa madereva utapimwa kulingana na:

(a) Utaratibu uliowekwa kwenye Jedwali la Pili la kanuni hizi; na

(b) Utakuwa na jumla ya alama jumuishi 100 kama inavyoonekana kwenye

Jedwali la Pili:

(3) Cheti cha Umahiri wa madereva kitatolewa kila baada ya miaka miwili

Page 6: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

Ada ya Maombi 10.- Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye

Jedwali la Tatu la kanuni hizi .

Kibali cha Kuvuka

Mipaka 11.-(1) bila kuathiri masharti ya kanuni ya 5, Mamlaka inaweza kutoa kibali kwa madereva

wanaoendesha treni kuvuka mipaka ya Tanzania bara kwa mujibu wa mikataba ya makubaliano

ya kimataifa.

(2) Dereva wa treni wa nje ya nchi anayekusudia kuingia ndani ya mipaka ya Tanzania

atawasilisha maoni yake kwa njia za kielekroniki kama inavyoonekana kwenye Jedwali la

Nne.

Alama Jumuishi 13.-(1) Dereva wa treni atawajibika kufuata utaratibu wa alama jumuishi kama ulivyowekwa

kwenye Jedwali la Tano.

(2) Mamlaka itarekodi alama jumuishi zilizopunguzwa kwa Dereva kutokana na

makosa mbalimbali kwa kipindi cha miaka miwili tangu kukabidhiwa cheti.

(3) alama zitakazopunguzwa kwenye cheti cha umahiri wa dereva zitakuwa kwenye muundo

ulioonyeshwa kwenye Jedwali la Tano:

Kusimamisha au

Kufuta Cheti 14.-(1) endapo dereva atakiuka kanuni hizi, Mamlaka inaweza kufuta au

kusimamisha matumizi ya cheti chake kama ilivyoainishwa kwenye Jedwali la Tano

(2) bila kuathiri masharti ya kanuni ndogo (1), mamlaka itatoa notisi ya siku

saba kueleza sababu za kufuta au kusimamisha matumizi ya cheti

(3) Endapo Mamlaka haitaridhika na maelezo ya dereva, inaweza kufuta au kusimamisha

matumizi ya cheti cha uthibitisho wa dereva;

(4) dereva wa treni aliyefutiwa au kusimamishiwa matumizi ya cheti atatakiwa:-

(a) endapo amesimamishiwa matumizi ya cheti, asiendeshe treni kwa kipindi chote

alichosimamishwa; na

(b) endapo amefutiwa cheti, atakoma kuendesha treni kuanzia tarehe ya kufutwa rasmi kwa

cheti husika na atatakiwa kukabidhi cheti hicho kwa mamlaka haraka iwezekanavyo

(5) Endapo mtu yeyote hatokubaliana na maamuzi ya Mamlaka anaweza kuomba marejeo ya

shauli lake kwa mujibu wa sheria ndani ya siku kumi na nne tangu maamuzi hayo kutolewa.

Kuhuisha Cheti 15.-(1) Dereva wa treni anayekusudia kuhuisha cheti chake cha umahiri anaweza

kuwasilisha maombi kwa mamlaka kufanya hivyo ndani ya siku sitini kabla ya cheti hicho kuisha

muda wake;

(2) Maombi ya kuhuisha cheti yafanyike kwa kuambatanisha vifuatavyo:

(a) Nakala ya cheti kinachoisha muda wake;

(b) Nakala ya uthibitisho wa malipo ya ada ya usajili kama ilivyoainishwa kwenye Jedwali la

Tatu; na

(c) Ripoti ya afya ya hivi karibuni kutoka kwa Tabibu.

Kuhamisha Matumizi

ya Cheti 16.- Cheti cha umahiri kinachotolewa kwa mujibu wa kanuni hizi hakiruhusiwi kuhamishiwa

matumizi kwa mtu mwingine.

SEHEMU YA TANO USAJILI WA WATENDAJI WA TRENI

Maombi ya Usajili 17.- Mtu yeyote anayekusudia kufanya kazi za utendaji ndani ya treni atawasilisha maombi kwa

Mamlaka kama ilivyoelekezwa kwenye Jedwali la Sita la kanuni hizi;

Viambatanisho vya Maombi ya Usajili

18.- Maombi ya usajili wa Watendaji wa treni yataambatana na vifuatavyo:-

(a) barua ya utambulisho toka kwa mwajiri;

Page 7: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

(b) ripoti ya afya ya hivi karibuni kutoka kwa Tabibu; na (c) Cheti cha mafunzo kwenye kazi anazofanya. Utoaji wa Vitambulisho vya Usajili

19.- Mamlaka inaweza -

(a) Endapo imejiridhisha kwamba mwombaji amekidhi masharti ya kanuni ya 18 , itatoa

cheti kama ilivyooneshwa kwenye Jedwali la Saba; au (b) kukataa kutoa usajili na kumfahamisha mwombaji sababu za kufanya hivyo. Kuhamisha Matumizi ya Kitambulisho

20- Kitambulisho cha Usajili kinachotolewa kwa mujibu wa kanuni hizi hakiruhusiwi

kuhamishiwa matumizi kwa mtu mwingine. Kupotea kwa

Kitambulisho 21. Endapo kitambulisho kilichotolewa kwa mujibu wa kanuni hizi kitapotea, kuibiwa au

kuharibika; Mamlaka baada ya kujiridhisha itatoa kwa Mhusika nakala nyingine ya

kitambulisho.

SEHEMU YA SITA

MASHARTI Masharti kwa

Madereva na

Treni Gadi

22.-(1) Dereva na treni gadi wanatakiwa kuhakikisha yafuatayo-

(a) Wanafuata matakwa ya ukomo wa mwendokasi uliowekwa; (b) Wanahakikisha Milango imefungwa kabla ya kuondoa treni ya abiria. (c) Wanafuata ratiba iliyopangwa;

Katazo kwa

Watendaji wa

treni

23.-(1) Watendaji wote wa treni wakiwa kwenye majukumu yao wanakatazwa kuzingatia

yafuatayo-

(d) Kutozidisha abiria au mizigo juu ya uwezo wa behewa; (e) Kujaza batli na kufuata ratiba iliyopangwa; (f) Kuvaa kitambulisho cha kazi; (g) Kuvaa sare za kazi; (h) Kutokuwa na ulevi au uraibu wa aina yeyote; (i) Kutii amri halali ya Afisa wa Mamlaka; (j) Kutotumia lugha ya matusi au yenye kudhalilisha mbele ya abiria.

SEHEMU YA SABA

MAKOSA NA ADHABU Makosa na adhabu 24.-(1) Mtu atakayekiuka masharti ya kanuni hizi atakuwa ametenda kosa na endapo atatiwa

hatiani atawajibika kulipa faini isiyopoungua elfu hamsini na isiyozidi laki 1 na atafungwa jela

kwa muda usiopungua mwezi mmoja na usiozidi mwaka mmoja au vyote kwa pamoja Uwezo wa kufifisha

makosa (2) Bila kuathiri matakwa ya kanuni hizi, mtu atakayefanya makosa kwa mujibu wa kanuni hizi,

mamlaka inaweza kabla ya kumfikisha mahakamani; kufifisha makosa husika na kumpa uwezo

mtuhumiwa kulipa faini kama ilivyoonyeshwa kwenye Jedwali la Nane la kanuni hizi

Mamlaka itaweza kufifisha makosa yaliyoanishwa chini ya kanuni hizi endapo Mhusika atakiri

kwa maandishi kwamba ametenda makosa hayo na ataomba mamlaka iyafifishe

(3) Endapo mamlaka itafifisha makosa chini ya kanuni hizi, utaratibu ulioelezwa kwenye kanuni

ndogo (1)

(a) Utawekwa kwenye maandishi na utaambatanishwa kwenye wasilisho la masharti na

nakala atapewa Mhusika endapo atahitaji

(b) Utaeleza aina ya kosa lililotendwa, kiasi cha pesa kinacholipwa kama faini na tarehe ya

kulipa pesa hiyo;

(c) Utakuwa wa Mwisho na hautakatiwa rufaa mahakamani;

(d) Utakuwa ni sawa na hukumu ya kimahakama;

(2) Endapo mtu yeyote hataridhishwa na maamuzi yaliyotolewa chini ya kanuni ndogo (1)

Page 8: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

anaweza ndani ya siku thelathini tangu kutolewa agizo hilo, kukataa rufaa dhidi ya

maamuzi hayo kwenye mahakama kuu kupitia masharti ya Sheria ya Mwenendo Wa

Makosa ya Jinai ya mwaka 1985 na mabadiliko yake yatatumika kwenye rufaa hiyo kana

kwamba ni uamuzi uliotolewa na mahakama ya wilaya yenye mamlka ya kufanya hivyo

(4)Kosa lolote lililofifishwa chini ya kanuni hizi halitakuwa na uhalali wa kupelekwa

mahakamani na endapo Mhusika atashitakiwa na kosa hilo hilo ufifishaji chini ya kanuni hizi

utatolewa kama ushahidi kuhusu shauli hilo.

Page 9: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

MAJEDWALI

Page 10: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

Jedwali la Kwanza

(Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 5(1))

TRAIN DRIVING CERTIFICATE APPLICATION FORM

(a) a certified copy of birth certificate or any relevant document for proof of birth;

(b) a certified copy for successful completion of at least secondary school education;

(c) a certified copy of a successful completion of basic

(d) training in locomotive driving from a recognized railway institute;

(e) proof of completion of at least two years practical and

(f) internship training in railway operation;

(g) proof of payment of certification fees; and

(h) a recent medical examination report from a medical practitioner

Passport size

photo

PART 1: Applicant’s Details

1.1. Surname:…………………………………………………………………………..

1.2. Name(s):………………………………………………………………………….

1.3. Sex:

Male: …………… Female:…………………….

Date of birth (DD-MM-YYYY):……………………………………...............................................

1.4. Place of birth: ………………………………………………………

1.5. Nationality: ………………………………………………………...

1.6. Language spoken………………………………………………………

1.7. Postal address………………………………………………….

1.8. Application for:

a. First issue: …………… b. Replacement:………………………….

c. Renewal: …………….

NIDA Identification Number:……………………………………………………………………………………

Date of first issue …………………………………

Expiry date:……………………………………………………..

PART 2: List of documents to be appended

Page 11: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

PART 3 Declaration

I hereby declare that to the best of my knowledge that all the information provided in this

application is true.

Applicant’s Signature …………………………….. Date………………………

Page 12: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

12

JEDWALI LA PILI

(Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 9 (2) (a))

Certificate of competence

The United Republic of Tanzania

Land Transport Regulatory Authority

(LATRA)

CERTIFIED TRAIN DRIVER

Passport size

photo

Drivers Name:: …………………………………….

Staff ID No. …………………………………

Department: …………………………….

CERTIFICATION:

The bearer of this card is a Certified Train Driver as per LATRA requirements.

Date of Issue ………………….. Signature

Expiry Date …………………. ……………………………..

Serial No. …………………………… Director General

Page 13: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

13

JEDWALI LA TATU

(Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 11)

Application Fee

S/N Particular Amount

1. Application Fee 60,000/-

2. Replacement Fee 80,000/

Note: These fee items are paid per the term of the certification

Page 14: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

14

JEDWALI LA NNE

(Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 12(2))

Application Form – Transit Permit for Train Driver

Part 1. Personal Details

1. First Name(s) …………………………………………..

2. Surname ………………………………………………..

3. Postal Address………………………………………….

Town/City………………………………………………

4. Nationality……………………………………………...

Place of Birth…………………………………………...

Date of birth Day………Month ………………Year…………………………..

5. Gender: Male Female

Part 2. Other Information

Telephone number……………………………………….…………………..

Email………………………………………………………………….………

Purpose of the visit……………………………………………………………

Destination ………………………………Country ………………………….

Duration of stay in days ……………………………………………………..

Entry date ………………………………Expected return date………………

Employer’s……………………………………………………………………….

Employer’s Contact Address…………………………Tel. No…………………………

Part 3. License Details

1. Driver’s Certificate number …………………………………………..……………

2. Issuing Authority……………………………………………………………………..

3. Date issued ……..…………………………………………..………………………..

4. Expiry date ……………………………………………………………………...

Part 4. Declaration

I hereby declare that to the best of my knowledge that all the information provided in this application

is true.

Applicant’s Signature …………………………….. Date……………………………

Passport size

photo

Page 15: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

15

JEDWALI LA TANO

( Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 13(1))

Demerit Points

1. In these Regulations, “Accumulated demerit points” means the total demerit points in

a driver’s record acquired as a result of offences committed within any period of two

years.

2. The authority shall take the following decision in relation to accumulated demerit

points:

(a) suspend for the period of three months Driver’s Certificate of competence of the

driver who’s accumulated demerit points are between forty and fifty points;

(b) suspend for the period of six months Driver’s Certificate of competence of the

driver who’s accumulated demerit points are between thirty and forty;

(c) revoke Driver’s Certificate of competence of the driver whose accumulated

demerit points are below thirty; and

(d) any driver whose Certificate of competence has been revoked, shall not be

allowed to apply for the same certificate within the period of two years.

3. A table indicating type of offences and number of points attached to each offence is

here under:

S/N

NATURE OF OFFENCE NUMBER OF

DEMERIT POINTS

1. Driving under the influence of alcohol or any other narcotic substances exceeding set limit. 20

2. Driving above sectional running speed 15

3. Failure to observe and obey safety signs and signals 15

4. Driving the train while passenger’s door is open 10

5. Improper filling of the logbook 10

6. Driving a train without a line clear ticket 10

7. Blocking or obstructing intentionally other traffic at level

crossings 10

8. Driving a train without carrying safety protective equipment 5

9. Driving a train without carrying a certificate of registration 5

Total Demerit Points 100

Page 16: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

16

JEDWALI LA SITA

(Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 17)

APPLICATION FORM FOR TRAIN CREW REGISTRATION

PART 1: Applicant’s Details Passport size

photo

1.9. Surname: …………………………………………….

1.10. Name(s):……………………………………….

1.11. Sex: Male: ………. Female:…………………..

1.12. Date of birth (DD-MM-YYYY):…………………………

1.13. Place of birth: …………………………………

1.14. Nationality: ……………………………….

1.15. Language spoken…………………………

Applicant Physical address …………………………………….

NIDA Identification Number:……………………….

Date of first issue (YYYY-MM-DD):………

Expiry date:………………………………….

PART 2: List of documents to be appended

(a) a letter from the employer; (b) a recent medical examination report from the medical practitioner; and (c) a certified copy of a certificate of attendance in a relevant field.

PART 3 Declaration

I hereby declare that to the best of my knowledge that all the information provided in this

application is true.

Applicant’s Signature …………………………….. Date……………………………

Page 17: KANUNI ZA UTHIBITISHAJI MADEREVA NA USAJILI WA ......Ada ya Maombi 10.-Malipo ya vyeti yatafanyika kwa kufuata mchanganuo uliowekwa kwenye Jedwali la Tatu la kanuni hizi . Kibali cha

JEDWALI LA SABA

(Limetengenezwa chini ya Kanuni ya 19)

Crew Registration Card

The United Republic of Tanzania

Land Transport Regulatory Authority

(LATRA)

REGISTERED TRAIN CREW

Staff Name: …………………………………….

Staff ID No. …………………………………

Department: …………………………….

CERTIFICATION:

The bearer of this card is a registered …………… as per LATRA requirements.

Date of Issue ………………….. Signature

Expiry Date …………………. ……………………………..

Serial No. …………………………… Director General

Dodoma, Isack A. Kamwelwe

…….., 2019 Minister for Works, Transport and Communications

Passport

size

photo