UFUFUO WA YESU - download.jw.orgdownload.jw.org/files/media_magazines/05/wp_SW_20130301.pdf ·...
Transcript of UFUFUO WA YESU - download.jw.orgdownload.jw.org/files/media_magazines/05/wp_SW_20130301.pdf ·...
34567MACHI 1 , 2013
UFUFUO WA
YESU
UNA UMUHIMU
GANI KWAKO?
Je, ungependa kupatahabari zaidi au kujifunzaBiblia nyumbani kwakobila malipo?
Tembelea www.jw.org /swau utume ombi lako ukitumiamojawapo ya anwani zilizohapa chini.
SOUTH AFRICA:Watch Tower Bible and Tract SocietyPrivate Bag X2067,Krugersdorp, 1740.
KENYA:International Bible Students AssociationPO BOX 21290,Nairobi 00505.
Ili upate orodha kamili ya anwani zetu ulimwe-nguni pote, tazamawww.jw.org /contact.
˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙ ˙
GAZETI HILI, Mnara wa Mlinzi,
linamheshimu Yehova Mungu,
ambaye ndiye Mtawala wa
ulimwengu. Linawafariji watu kwa
habari njema kwamba hivi karibuni
Ufalme wa Mungu ulio mbinguni,
utakomesha uovu wote na kuigeuza
dunia kuwa paradiso. Linawatia moyo
watu wamwamini Yesu Kristo, ambaye
alikufa ili tupate uzima wa milele na
ambaye sasa anatawala akiwa Mfalme
wa Ufalme wa Mungu. Gazeti hili
limekuwa likichapishwa tangu 1879
na si la kisiasa. Linashikamana na
Biblia ambayo ndiyo msingi wake.
The Watchtower (ISSN 0043-1087) is published
semimonthly by Watchtower Bible and Tract
Society of New York, Inc.; L. Weaver, Jr.,
President; G. F. Simonis, Secretary-Treasurer;
25 Columbia Heights, Brooklyn, NY 11201-2483,
U.S.A. Printed in the Republic of South Africa by
Watch Tower Bible and Tract Society, 1 Robert
Broom Drive East, Rangeview, Krugersdorp, 1739,
R.S.A. Periodicals Postage Paid at Brooklyn, NY,
and at additional mailing offices. � 2013 Watch
Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania.
Haki Zote Zimehifadhiwa
Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu
ya Biblia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa
kwa michango ya hiari. Isipokuwa iwe imeonye-
shwa vingine, Maandiko yamenukuliwa kutoka
katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.
Je, Wajua? 8
Wasomaji Wetu Wanauliza . . .
Je, Yesu Alimwahidi Yule Mtenda-Maovu Kwamba
Ataishi Mbinguni? 9
“Niliona, Lakini Sikuelewa” 10
Mkaribie Mungu
—“Ni Amri Gani Iliyo ya Kwanza Kati ya Zote?” 13
Wafundishe Watoto Wako
—Petro na Anania Walidanganya
—Tunajifunza Nini? 14
Majibu ya Maswali ya Biblia 16
34567Kila Toleo Linalochapishwa:44,978,000 KATIKA LUGHA 205 MARCH 1, 2013�����������������������������������������������������������������������������������������������������������
KICHWA KIKUU
�����������������������������������������������������������������������������������������������������������
PIA KATIKA TOLEO HILI
s SOMA HABARI ZAIDI KWENYE INTANETI � www.jw.org/sw
Vol. 134, No. 5SemimonthlySWAHILI
Ufufuo wa YesuJE, KWELI ULITUKIA? UKURASA WA 3
UFUFUO WA YESU HUMAANISHA UZIMA! 7
MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGIKUHUSU MASHAHIDI WA YEHOVA—Je,Nyinyi Ni Wakristo?
(Tafuta kwenye KUTUHUSU/MASWALI YANAYOULIZWA
MARA NYINGI)
r
PAKUA GAZETI HILI KATIKAMIUNDO MBALIMBALI
KWENYE INTANETI
(
(
HERODOTO, mwanahistoria Mgiriki aliyeishimiaka 2,500 iliyopita, alisimulia kuhusu Wa-
misri wa siku zake. Aliandika hivi: “Katika kara-mu ya matajiri, baada ya chakula cha jioni mwa-namume fulani hubeba jeneza lililo na sanamuya maiti, iliyochongwa na kupakwa rangi ili ifa-nane kabisa na maiti, yenye urefu wa mkonommoja au mwili. Anamwonyesha kila mtu ali-yeko akisema, ‘Kunyweni na msherehekee, kwamaana; mtakapokufa mtakuwa hivi.’ ”
Si Wamisri peke yao waliokuwa na maonikama hayo kuhusu uhai na kifo. Leo, msemo“Kuleni, mnywe, na msherehekee” ni wa ka-waida. Ikiwa kifo ni mwisho wa uhai, kwa niniusijifurahishe? Kwa nini ujitahidi kufanya yali-yo sawa? Ikiwa kifo ni mwisho wa mambo yote,kuishi kwa ajili ya sasa kunatosha. Mtume Pau-lo alizungumzia jambo hilo. Alifafanua mtazamowa watu wasioamini ufufuo akisema hivi: “Ikiwa
wafu hawatafufuliwa, ‘na tule na tunywe, kwamaana kesho tutakufa.’ ”—1 Wakorintho 15:32.
Bila shaka, Paulo mwenyewe hakuamini kwa-mba wafu watasahauliwa milele. Alisadiki wafuwataishi tena, wakiwa na tumaini la kuishi mi-lele. Usadikisho wake ulitegemea tukio kubwana muhimu, ukweli ambao aliamini haupingiki—ufufuo� wa Kristo Yesu. Kwa hakika, ufufuohuo ni tukio kubwa la kipekee ambalo liliimari-sha imani ya wanafunzi wa mapema.
Hata hivyo, ufufuo wa Yesu una umuhimugani kwetu? Kwa kweli, tunajuaje kwamba uli-tukia? Acheni tuone jinsi Paulo alivyozungumziajambo hilo alipowaandikia Wakristo walioishiKorintho.
� Katika Biblia, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “ufufuo” kiha-lisi humaanisha “kusimama tena.” Hilo linadokeza kwamba mtuhurudishiwa uhai, akiwa na sura ileile, utu, na kumbukumbulake.
KICHWA KIKUU
Ufufuo wa YesuJE, KWELI ULITUKIA?
MACHI 1, 2013 � 3
INGEKUWAJE KAMA KRISTO HAKUFUFULIWA?
Wakristo fulani wa jiji la kale la Korintho wali-tatanishwa na jambo hilo, na wengine hawakua-mini ufufuo hata kidogo. Katika barua yake yakwanza kwa Wakristo hao, Paulo aliorodheshamambo ambayo yangetokea ikiwa ufufuo hauku-wa halisi. Aliandika hivi: “Ikiwa, kwa kweli, ha-kuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa.Lakini ikiwa Kristo hakufufuliwa, hakika kuhu-biri kwetu ni bure, na imani yetu ni bure. Zai-di ya hayo, tunaonekana pia kuwa mashahidi wauwongo wa Mungu . . . Imani yenu ni bure; ni-nyi bado mko katika dhambi zenu. . . . Pia, walewaliolala usingizi katika kifo katika muunga-no na Kristo waliangamia.”—1 Wakorintho 15:13-18.
Paulo alianza kwa maneno ambayo hayawezikupingwa: Ikiwa wafu hawatafufuliwa, basi, Kri-sto, aliyekufa hakufufuliwa. Kama Kristo haku-fufuliwa ingekuwaje? Basi, kuhubiri habari nje-ma ingekuwa kazi bure na uwongo mkubwa.Zaidi ya yote, ufufuo wa Kristo ulikuwa sehemumuhimu ya imani ya Kikristo, na haungetengani-shwa na mafundisho ya msingi ya Biblia kuhusuutawala wa Mungu, jina lake, Ufalme wake, naukombozi wetu. Ikiwa ufufuo haukutukia, uju-mbe ambao Paulo na mitume wengine walita-ngaza ungekuwa bure kabisa, usio na thamaniyoyote.
Mambo mengine yangefuata. Ikiwa Kristo ha-kufufuliwa kutoka kwa wafu, imani ya Kikristoingekuwa bure, isiyo na thamani yoyote, na ina-yotegemea uwongo. Zaidi ya hayo, Paulo na we-ngine wangelikuwa wamesema uwongo si juu yaufufuo wa Yesu pekee bali pia kumhusu yuleambaye walisema alimfufua Yesu, yaani Yeho-
va Mungu. Zaidi ya hilo, dai la kwamba Kristo“alikufa kwa ajili ya dhambi zetu” lingekuwa lauwongo—kwa maana ikiwa Mkombozi mwenye-we hakukombolewa kutoka katika kifo, angewe-zaje kuwakomboa wengine? (1 Wakorintho 15:3)Hilo lingemaanisha kwamba Wakristo walioku-fa, kutia ndani waliouawa kwa sababu ya imaniyao, waliangamia wakiwa na tumaini la uwongokwamba watafufuliwa.
Paulo alihitimisha hivi: “Ikiwa katika maishahaya tu tumemtumaini Kristo, sisi ndio wa kusi-kitikiwa zaidi kati ya watu wote.” (1 Wakorintho15:19) Kama Wakristo wengine, Paulo alipata ha-sara, aliteswa, akavumilia matatizo, na kuuawakwa sababu aliamini ufufuo na yale ambayo ufu-fuo ungetimiza. Ingekuwa bure kabisa kama ku-singekuwa na ufufuo!
KWA NINI UNAPASWA KUAMINI UFUFUO?
Paulo hakufikiri kwamba aliamini uwongo.Alijua Yesu alifufuliwa kutoka kwa wafu, na ali-malizia uthibitisho wake kwa Wakorintho hivi,“kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetukulingana na Maandiko; na kwamba alizikwa,ndiyo, kwamba alifufuliwa siku ya tatu kulinga-na na Maandiko; na kwamba alimtokea Kefa,kisha wale kumi na wawili.”� Halafu akaonge-za hivi: “Baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya miatano kwa wakati mmoja, ambao walio wengi katiyao wapo mpaka sasa, lakini wengine wamelalausingizi katika kifo. Baadaye alimtokea Yakobo,kisha mitume wote; lakini mwisho kabisa alini-tokea mimi pia.”—1 Wakorintho15:3-8.� Usemi “wale kumi na wawili” unamaanisha “mitume,” inga-
wa walibaki 11 baada ya Yuda Iskariote kufa. Kwenye tukiomoja, 10 pekee waliwakilisha wale mitume 12, kwa kuwa Toma-si hakuwepo.—Yohana 20:24.
“Aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa wakati mmoja . . .
Baadaye alimtokea Yakobo, kisha mitume wote; lakini mwisho
kabisa alinitokea mimi pia.”—1 Wakorintho 15:6-8
4 � MNARA WA MLINZI
MACHI 1, 2013 � 5
Paulo alianza kwa maneno yenye usadikishokwamba Kristo alikufa, akazikwa, na kufufuliwakwa ajili ya dhambi zetu. Kwa nini Paulo alikuwana uhakika huo? Sababu moja ni kwamba watuwengi walijionea. Yesu aliyefufuliwa aliwatokeawatu mmoja mmoja (kutia ndani Paulo mwe-nyewe), vikundi vidogo, na hata umati wa watu500, ambao wengi wao hawakuamini waliposikiakwamba Yesu alikuwa amefufuliwa! (Luka 24:1-11) Wengi wa mashahidi hao walikuwa hai wa-kati wa Paulo na wangeweza kuulizwa ili kuthi-bitisha tukio hilo. (1 Wakorintho15:6) Ingekuwarahisi kumpuuza shahidi mmoja au wawili, laki-ni si uthibitisho wa watu 500 au zaidi.
Pia, kumbuka Paulo alitaja mara mbili kwa-mba kufa, kuzikwa, na kufufuliwa kwa Yesu ‘ku-lilingana na Maandiko.’ Matukio hayo yalithibi-tisha kwamba unabii ulio katika Maandiko yaKiebrania kuhusu Masihi ulikuwa wa kweli nabila shaka, Yesu ndiye Masihi aliyeahidiwa.
Licha ya uthibitisho wa mashahidi na Maandi-ko, kulikuwepo, na bado kuna watu wanaoshu-ku ikiwa Yesu alifufuliwa. Wengine wanasemamwili wake uliibiwa na wanafunzi wake ambaowalidai kwamba walishuhudia ufufuo. Hata hi-vyo, wanafunzi hawakuwa na nguvu wala uwezowa kuwashinda askari Waroma waliokuwa wa-nalinda kaburi. Wengine wanadai ufufuo uliku-wa jambo la kuwaziwa tu. Maoni hayo si ya kwe-li kwa sababu Yesu aliwatokea watu wengi kwanyakati tofauti. Pia, je, unaweza kuamini kwa-mba mtu wa kuwazia angepika na kuwapa wa-nafunzi samaki kama Yesu aliyefufuliwa alivyo-fanya huko Galilaya? (Yohana 21:9-14) Je, mtu wakuwaziwa anaweza kuwaomba watu wamguse?—Luka 24:36-39.
6 � MNARA WA MLINZI
Wengine wanasema kwamba ufufuo ni uwo-ngo uliotungwa na wanafunzi. Lakini wangepa-ta faida gani kwa kufanya hivyo? Kutoa ushahidikuhusu ufufuo kulifanya wanafunzi wadhihaki-we, wateswe na kuuawa. Kwa nini wahatarisheuhai kwa kuunga mkono uwongo? Zaidi ya hayo,kwanza walitoa ushahidi wao Yerusalemu, mbe-le ya wapinzani wao, ambao walikuwa tayari ku-tumia kisingizio chochote ili kuwashutumu.
Ufufuo ndilo jambo lililowapa wanafunzi uja-siri wa kutangaza juu ya Bwana wao licha ya ku-nyanyaswa vikali. Ukweli kuhusu ufufuo ukawasehemu muhimu ya imani ya Kikristo. Wakri-
sto wa mapema hawakuhatarisha uhai wao ilitu kutoa ushahidi kuhusu mwalimu mwenye he-kima aliyeuawa. Walihatarisha uhai wao ili ku-hubiri ufufuo wa Yesu kwa sababu ulithibiti-sha kwamba alikuwa Kristo, Mwana wa Mungu,mwenye nguvu, aliye hai ambaye aliwategemezana kuwaongoza. Ufufuo wake ulimaanisha kwa-mba wao pia wangefufuliwa kutoka kwa wafu.Kwa kweli, kama Yesu hakufufuliwa, kusinge-kuwa na Ukristo. Kama Yesu hakufufuliwa, hatahatungewahi kumsikia.
Hata hivyo, ufufuo wa Kristo una umuhimugani kwetu leo?
Ni nani watakaofufuliwa?“Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio
waadilifu.” (Matendo 24:15) Waadilifu watatia
ndani wanaume na wanawake waaminifu kama
vile Noa, Abrahamu, na Sara. Wasio waadilifu
watatia ndani wote ambao hawakufuata viwa-
ngo vya Mungu kwa sababu hawakupata fursa
ya kujifunza kuvihusu.
Wale watakaofufuliwa wataishi wapi?Baadhi yao watafufuliwa na kupewa uhai usio-
weza kufa wakiwa viumbe wa roho mbinguni ili
watawale na Kristo wakiwa wafalme na maku-
hani juu ya dunia. (Ufunuo 5:9, 10) Hata hivyo,
wengi watafufuliwa na kuishi duniani. Watafura-
hia uzima wa milele katika dunia paradiso.
—Luka 23:39-43.
Ufufuo utatukia lini?Wakati ujao, baada ya waovu kuondolewa du-
niani. Biblia inaonyesha kwamba wengi watafu-
fuliwa wakati wa utawala wa miaka elfu moja
wa Yesu, ambapo dunia itabadilishwa na kuwa
paradiso.—Ufunuo 20:6.
Je, desturi za Ista zinahusiana na ufufuo?Desturi za Ista zinazohusisha sungura, mayai
yenye rangi, mishumaa, maua, na pia jina lenye-
we Ista, zilitokana na dini za kipagani. Mambo
hayo yote hayahusiani na ufufuo wa Yesu,
ambao unadaiwa kuwakilishwa na Ista. Je,
kuna ubaya wowote? Ndiyo. Neno la Mungu lina-
tuamuru tujitenge na dini ya uwongo na ‘tumwa-
budu baba kwa roho na kweli.’—Yohana 4:23;
2 Wakorintho 6:17.
Ikiwa Yesu ni Mungu, kama dini fulanizinavyofundisha, ni nani aliyemfufua?Yesu si Mungu—ambaye jina lake ni Yeho-
va—bali ni Mwana wa Mungu. Yehova alimfufua
Yesu kutoka kwa wafu. (Waroma 10:9) Msomi
fulani wa Biblia anasema: “Haiwezekani kwa-
mba mtu yeyote—hata Kristo—angeweza kujifu-
fua.”�
� Ili upate majibu zaidi ya maswali haya, ona sura ya 7 na 8ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Ma-shahidi wa Yehova, au utembelee www.jw.org/sw.
MASWALI AMBAYO HUULIZWA MARA NYINGI
MACHI 1, 2013 � 7
UFUFUO wa Yesu sio tukio la zamani tu, lisilona umuhimu wowote kwetu leo. Mtume Pau-
lo alionyesha umuhimu wake alipoandika hivi:“Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matundaya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi kati-ka kifo. Kwa kuwa kifo ni kupitia mwanadamu,ufufuo wa wafu pia ni kupitia mwanadamu. Kwamaana kama vile katika Adamu wote wanakufa,vivyo hivyo pia katika Kristo wote watafanywakuwa hai.”—1 Wakorintho 15:20-22.
Yesu alifufuliwa Nisani 16, 33 W.K., tareheambayo Wayahudi walimtolea Yehova Mungu ma-tunda ya kwanza ya mazao yao katika patakatifu pahekalu huko Yerusalemu. Kwa kumwita Yesu ma-tunda ya kwanza, Paulo alimaanisha kwamba ku-ngekuwa na watu wengine ambao wangefufuliwa.
Maneno yanayofuata ya Paulo yanaeleza jamboambalo limewezekana kwa sababu ya ufufuowa Yesu. Paulo alisema: “Kwa kuwa kifo ni ku-pitia mwanadamu ufufuo wa wafu pia ni kupi-tia mwanadamu.” Sote tunakufa kwa sababu tuliri-thi dhambi na kutokamilika kutoka kwa Adamu.
Hata hivyo, kwa kutoa mwili wake mkamilifu wakibinadamu kuwa dhabihu, Yesu alifanya iwezeka-ne kwa wanadamu kukombolewa kutoka kwenyeutumwa wa dhambi na kifo kupitia ufufuo. Akihiti-misha hoja yake vizuri, Paulo aliandika hivi kwenyeWaroma 6:23: “Mshahara ambao dhambi hulipa nikifo, lakini zawadi ambayo Mungu hutoa ni uzimawa milele kupitia Kristo Yesu Bwana wetu.”
Yesu mwenyewe alifafanua umuhimu wa kifona ufufuo wake kwetu. Akizungumza kujihusualisema: “Mwana wa binadamu atainuliwa, ili kilamtu anayemwamini apate kuwa na uzima wa mile-le. Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu sanahivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pe-kee ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe baliawe na uzima wa milele.”—Yohana 3:14-16.
Wazia—uzima wa milele bila maumivu, kutese-ka, wala huzuni! (Ufunuo 21:3, 4) Tazamio zurikama nini! Msomi mmoja anasema hivi: “Inga-wa makaburi yanatukumbusha kuhusu ufupi wamaisha, ufufuo unatuhakikishia ufupi wa kifo.”Naam, ufufuo wa Yesu unamaanisha uzima! ˇ
Ufufuo wa Yesu HumaanishaUzima!
8 � MNARA WA MLINZI
Wayahudi walizika wafu muda mfupi baada ya kufa, kwa kawai-
da siku ileile. Kuna sababu mbili kwa nini walifanya hivyo. Kwa-
nza, maiti huoza haraka katika mazingira ya joto huko Mashari-
ki ya Kati. Pili, wakati huo, watu walifikiri kuacha maiti bila kuizika
ni kumkosea heshima mtu aliyekufa na familia yake.
Vitabu vya Injili na kitabu cha Matendo vina rekodi nne hivi za
mazishi yaliyofanyika siku ileile ambayo mtu alikufa. (Mathayo
27:57-60; Matendo 5:5-10; 7:60–8:2) Karne nyingi mapema, Ra-
heli mke mpendwa wa Yakobo alikufa familia yake ilipokuwa sa-
farini. Badala ya kupeleka mwili huo hadi mahali pa kuzikia pa
familia, Yakobo alimzika katika kaburi “njiani kuelekea . . . Be-
thlehemu.”—Mwanzo 35:19, 20, 27-29.
Masimulizi ya Biblia kuhusu mipango ya mazishi yanaonyesha
kwamba Wayahudi walitayarisha maiti kwa uangalifu sana kab-
la ya kuzika. Marafiki pamoja na watu wa familia waliosha maiti,
wakaipaka manukato na mafuta mazuri, na kuifunga kwa vita-
mbaa. (Yohana 19:39, 40; Matendo 9:36-41) Majirani na wengi-
ne walikuja ili kuomboleza na kufariji familia.—Marko 5:38, 39. ˇ
JE, WAJUA?
Wayahudi wa karne ya kwanza walitayarishajewafu kabla ya kuwazika?
Wayahudi wengi walizika wafu kwenye mapango au makaburi ya-
liyochongwa kwenye miamba laini inayopatikana katika sehemu
nyingi za Israeli. Kwa kufanya hivyo, walifuata mfano wa wazee wa
ukoo. Abrahamu, Sara, Isaka, Yakobo, na wengine walizikwa kwe-
nye pango la Makpela karibu na Hebroni.—Mwanzo 23:19; 25:
8, 9; 49:29-31; 50:13.
Yesu alizikwa katika kaburi lilichongwa kwenye mwamba. (Mar-
ko 15:46) Kwa kawaida makaburi kama hayo yalikuwa na mlango
mwembamba. Ndani kulikuwa na sehemu zilizochongwa kwenye
mwamba mfano wa rafu za vitabu, ambapo maiti ziliwekwa. Baa-
da ya mwili kuoza, mifupa iliyokauka ilikusanywa na kuwekwa kwe-
nye sanduku la mifupa, kama ilivyokuwa desturi wakati wa Yesu.
Hivyo, familia ilipata nafasi katika kaburi ya kuzika wafu wakati
ujao.
Siku ya Sabato Wayahudi hawakuruhusiwa na Sheria ya Musa
kufanya mipango ya mazishi. Kwa sababu Yesu alikufa saa tatu
hivi kabla ya Sabato kuanza, Yosefu wa Arimathea na wengine wa-
limzika Yesu bila kukamilisha matayarisho. (Luka 23:50-56) Hivyo,
baadhi ya rafiki za Yesu walienda kwenye kaburi lake baada ya Sa-
bato, ili kukamilisha matayarisho hayo.—Marko 16:1; Luka 24:1. ˇ
Je, Yesu alizikwa kulingana na desturi zaWayahudi?
Swali hilo huzuka kwa sababu Yesu alimwahidi
uhai katika Paradiso yule mhalifu aliyeuawa pa-
moja naye. Alisema hivi: “Kwa kweli mimi nakua-
mbia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”
(Luka 23:43) Ona kwamba Yesu hakutaja mahali
ambapo Paradiso ingekuwa. Hivyo basi, je, Yesu
alimaanisha kwamba yule mtenda-maovu ange-
kutana naye mbinguni?
Kwanza, acheni tuchunguze kama mtenda-
maovu huyo alistahili kuishi mbinguni. Wanada-
mu wenye tumaini la kimbingu wamebatizwa kati-
ka maji na kwa roho takatifu na hivyo ni wanafunzi
wa Yesu waliozaliwa kwa roho. (Yohana 3:3, 5) Ni
lazima pia wafuate viwango vya Mungu vya maa-
dili na kuonyesha sifa kama vile unyoofu, utimilifu,
na huruma. (1 Wakorintho 6:9-11) Pia, lazima wa-
baki washikamanifu kwa Mungu na Kristo mpa-
ka mwisho wa maisha yao duniani. (Luka 22:28-
30; 2 Timotheo 2:12) Wakitimiza matakwa hayo
tu ndipo wanaweza kuonyesha kwamba wanasta-
hili kufufuliwa na kupewa wajibu mkubwa unaowa-
subiri mbinguni, yaani, kutumika wakiwa makuha-
ni na wafalme pamoja na Kristo juu ya wanadamu
kwa miaka elfu.—Ufunuo 20:6.
Kinyume cha hilo, mhalifu aliyekuwa kando ya
Yesu aliishi na kufa akiwa mhalifu. (Luka 23:32,
39-41) Ni kweli, alionyesha heshima alipomwa-
mbia Yesu: “Unikumbuke utakapoingia katika
ufalme wako.” (Luka 23:42) Hata hivyo, hakuwa
amebatizwa, hakuwa mwanafunzi wa Yesu aliye-
zaliwa kwa roho, wala hakuwa ameweka rekodi
nzuri ya maadili na uaminifu. Je, inapatana na aki-
li kwa Yesu kumwahidi ufalme wa kimbingu pamo-
ja na wafuasi wake waaminifu, ambao wameonye-
sha utimilifu?—Waroma 2:6, 7.
Kwa mfano: Ikiwa mtu aliyekuibia pesa anakuo-
mba msamaha, unaweza kuamua kutomdai pesa
hizo. Lakini je, utamwamini asimamie biashara
yako au kutunza familia yako? Unaweza kuwa-
pa daraka hilo wale tu unaowaamini zaidi. Vivyo
hivyo, lazima wote wanaopewa tumaini la kuishi
mbinguni wathibitishe kabisa kwamba watatetea
viwango vya haki vya Mungu watakapotawala wa-
nadamu. (Ufunuo 2:10) Ingawa yule mtenda-mao-
vu alimsihi Yesu kwa unyoofu, hakuthibitisha ushi-
kamanifu wake.
Lakini je, Yesu hakumwambia yule mtenda-
maovu kwamba angekuwa naye mbinguni siku hi-
yohiyo? Haingewezekana kwa kuwa Yesu mwe-
nyewe hakuingia mbinguni siku hiyo. Badala yake
alikaa “katika moyo wa dunia,” yaani, kaburini
kwa siku tatu. (Mathayo 12:40; Marko 10:34)
Hata baada ya kufufuliwa, alikaa duniani siku 40
kabla ya kupaa mbinguni. (Matendo 1:3, 9) Hivyo,
yule mtenda-maovu hangekuwa na Yesu mbingu-
ni siku hiyo.
Hivyo basi, yule mtenda-maovu angeingia kati-
ka Paradiso gani? Baada ya kufufuliwa, ataishi ka-
tika dunia Paradiso ambayo itatawaliwa na Yesu.
(Matendo 24:15; Ufunuo 21:3, 4) Ili ujifunze me-
ngi kuhusu Paradiso hiyo na yale ambayo Mungu
anataka, zungumza na mmoja wa Mashahidi wa
Yehova. ˇ
WASOMAJI WETU WANAULIZA . . .
Je, Yesu alimwahidi yule mtenda-maovu kwambaataishi mbinguni?
10 � MNARA WA MLINZI
Nilipokuwa bado mchanga, wazazi wangu wali-talikiana, na mama akalazimika kutulea—mimi,kaka zangu wawili, na dada yangu mkubwa—aki-wa peke yake. Wakati huo, nchini Ufaransa wa-toto viziwi walifundishwa kwa njia tofauti na zasasa, na wakati mwingine njia zilizotumiwa zi-liwasababishia mateso mengi. Hata hivyo, tanguutotoni, nimekuwa na hali bora ambayo viziwi we-ngi hawana. Acheni niwasimulie.
Kwa muda fulani, walimu wengi waliaminikwamba watoto viziwi wanapaswa kufundishwakwa kutazama midomo ya mwalimu. Kwa kweli,nchini Ufaransa nilikolelewa, ilikuwa marufukukuzungumza kwa lugha ya ishara. Hata mikono yawatoto fulani viziwi ilifungwa mgongoni walipo-kuwa darasani.
Kwa miaka kadhaa utotoni, nilitumia muda fu-lani kila juma pamoja na mtaalamu wa matamshi.Nilishikwa taya au kichwa na nikaamuriwa kutoatena na tena sauti ambazo sikuzisikia. Sikuwezakuwasiliana na watoto wengine. Niliteseka sanakipindi hicho.
Kisha, nilipokuwa na umri wa miaka sita, nili-pelekwa kwenye shule maalumu ya bweni. Kwamara ya kwanza, nikakutana na watoto wengineviziwi. Huko pia, lugha ya ishara ilikuwa imepi-gwa marufuku. Tulipozungumza kwa ishara dara-sani, tuliadhibiwa kwa kugongwa kwenye vidoleau kuvutwa nywele. Hata hivyo, tuliwasiliana kisi-ri, tukitumia ishara tulizobuni. Mwishowe nilifau-lu kuwasiliana na watoto wengine. Ilikuwa miakaminne yenye furaha.
Hata hivyo, nilipokuwa na umri wa miakakumi, nilipelekwa kwenye shule ya watoto wanao-sikia. Nilivunjika moyo sana! Nilifikiri wale wato-to wote viziwi walikuwa wamekufa na kwamba nimimi tu niliyebaki duniani. Kufuatia ushauri wamadaktari, ambao waliogopa ningepoteza ustadiwa kutambua matamshi, familia yangu haikuwaimejifunza lugha ya ishara na sikuruhusiwa kushi-rikiana na watoto viziwi. Bado ninakumbuka nili-pomtembelea daktari fulani. Alikuwa na kitabucha lugha ya ishara kwenye dawati lake. Nilipoo-na picha zilizokuwa kwenye jalada, nilimwonye-
SIMULIZI LA MAISHA
“Niliona, LakiniSikuelewa”
LIMESIMULIWA NA OLIVIER HAMEL
Nilikuwa na umri wa miaka miwili mwaka wa 1975 mama ya-
ngu aliposhuku kwamba nilikuwa na tatizo. Mama alipokuwa
amenibeba mikononi, rafiki yake aliangusha kitu kizito sakafu-
ni, na kukatokea kishindo kikubwa. Mama alitambua kwamba
hata sikusogea. Nilipokuwa na umri wa miaka mitatu, bado si-
kuweza kuongea. Kisha familia yetu ikapokea habari za ku-
shtua, wataalamu walithibitisha kwamba nilikuwa kiziwi kabisa!Nilipokuwa na umri wamiaka mitano hivi
MACHI 1, 2013 � 11
sha kitabu hicho na kusema, “Ninakitaka!” Maramoja yule daktari akakificha.�
JINSI NILIVYOANZA KUJIFUNZA BIBLIA
Mama alijitahidi kutulea sisi watoto kulinga-na na kanuni za Kikristo. Alitupeleka kwenyemikutano ya Kutaniko la Mashahidi wa Yehovala Merignac, karibu na Bordeaux. Nikiwa mtoto,sikuelewa mengi mikutanoni. Hata hivyo, watumbalimbali waliketi karibu nami kwa zamu nakuandika mambo makuu yaliyosemwa. Niligu-swa moyo na upendo na hangaiko lao. Tukiwanyumbani, mama alinifundisha Biblia, lakini si-kuelewa kikamili mambo niliyofundishwa. Nilihi-si kama nabii Danieli, ambaye baada ya kupokeaunabii kutoka kwa malaika alisema: “Nikasikia,lakini sikuweza kuelewa.” (Danieli 12:8) Katikakisa changu “Niliona, lakini sikuelewa.”
Hata hivyo, pole kwa pole kweli za msingi zaBiblia zilitia mizizi moyoni mwangu. Nilithaminimambo niliyoelewa na nikajaribu kuyatumia mai-shani. Pia, nilijifunza kwa kutazama tabia za we-ngine. Kwa mfano, Biblia inatuhimiza tuonyeshesubira. (Yakobo 5:7, 8) Lakini sikuelewa subira ninini. Hata hivyo, kwa kuwatazama waabudu we-nzangu wakionyesha sifa hiyo, nilielewa maana yasubira. Kwa kweli, kutaniko la Kikristo limekuwamsaada mkubwa kwangu.
KUVUNJIKA SANA MOYO,KISHA MSISIMKO MKUBWA
Siku moja nilipokuwa tineja, niliwaona vijanafulani viziwi wakizungumza kwa ishara. Nilianzakushirikiana nao kisiri na nikaanza kujifunza Lu-gha ya Ishara ya Ufaransa. Niliendelea kuhudhu-ria mikutano ya Kikristo, ambako kijana fulaniShahidi anayeitwa Stephane alifanya urafiki nami.Alijitahidi sana kuwasiliana nami, na tukawa ma-rafiki wa karibu. Hata hivyo, muda mfupi baada-ye jambo baya lilitokea. Stephane alifungwa gere-
� Mwaka wa 1991, Serikali ya Ufaransa iliidhinisha rasmi ma-tumizi ya lugha ya ishara katika kuwaelimisha watoto viziwi.
zani kwa kukataa kujiunga na jeshi. Nilivunjikasana moyo! Stephane alipokuwa gerezani, nilita-mauka sana na nikaacha kuhudhuria mikutano.
Miezi kumi na moja baadaye, Stephane alia-chiliwa huru na akarudi nyumbani. Wazia nili-vyoshangaa Stephane alipoanza kuwasiliana namiakitumia lugha ya ishara. Sikuamini macho ya-ngu! Ni nini kilichotukia? Alipokuwa gerezaniStephane alijifunza Lugha ya Ishara ya Ufaransa.Nilitazama ishara za mikono na uso wa Stephane,na nikasisimuka nilipofikiria jinsi ambavyo ninge-faidika.
MWISHOWE NIKAZIELEWA KWELI ZA BIBLIA
Stephane alianza kunifundisha Biblia. Tanguwakati huo, nilianza kuunganisha kweli mbali-mbali za Biblia nilizokuwa nimejifunza. Nilipo-kuwa mtoto nilipenda kutazama picha marida-di kwenye machapisho yetuya Biblia, na kuwalingani-sha wahusika huku nikichu-nguza kwa makini kila kituili nikumbuke hadithi hizo.Nilijua kumhusu Abrahamu,“uzao” wake, na ule “umatimkubwa,” lakini ni waka-ti tu mambo hayo yalipofafa-nuliwa katika lugha ya isharandipo nilipoyaelewa kikami-li. (Mwanzo 22:15-18; Ufu-nuo 7:9) Ni wazi kwambanilikuwa nimeipata lugha ya-ngu, lugha iliyogusa moyowangu.
Sasa, kwa vile nililelewa mambo yaliyosemwamikutanoni, moyo wangu ulichochewa na nikata-mani kujifunza mengi. Kwa msaada wa Stepha-ne, niliendelea kuielewa Biblia, na kufikia mwa-ka wa 1992, nikajiweka wakfu kwa Yehova Munguna kubatizwa. Hata hivyo, licha ya maendeleo ni-liyofanya, nilikuwa mwenye haya kwa sababu si-kuweza kuwasiliana nilipokuwa mtoto.
St´ephane alinisaidia
kuielewa Biblia
12 � MNARA WA MLINZI
KUPAMBANA NA WOGA
Mwishowe, kikundi chetu kidogo cha viziwi ki-liunganishwa na kutaniko la Pessac, lililo kwe-nye kitongoji cha jiji la Bordeaux. Hilo lilinisaidiasana na nikaendelea kufanya maendeleo ya kiro-ho. Ingawa bado nilikuwa nikipambana na tati-zo la kuwasiliana, rafiki zangu wenye uwezo wakusikia walihakikisha kwamba nilielewa kila kitu.Wenzi wa ndoa Gilles na Elodie, walijitahidi sanakuwasiliana nami. Mara kwa mara, baada ya mi-kutano walinialika kula chakula au kunywa kaha-wa pamoja, na hivyo tukawa marafiki wakubwa.Inafurahisha sana kuwa miongoni mwa watu wa-naofuata njia za Mungu zenye upendo!
Huko ndiko nilikokutana na msichana mremboVanessa. Nilivutiwa na tabia yake ya kuwajaliwatu na mtazamo wa kupenda haki. Hakuona ka-mwe hali yangu ya kuwa kiziwi kama kizuizi, ba-dala yake, aliiona kuwa nafasi ya kujifunza mengi.Tulipendana, na tukaoana mwaka wa 2005. Inga-wa ni vigumu kwangu kuwasiliana vizuri, Vanessaamenisaidia kupambana na woga na kujieleza wa-ziwazi. Ninathamini sana msaada wake ninapo-shughulikia majukumu yangu.
ZAWADI NYINGINE KUTOKA KWA YEHOVA
Mwaka tulioona, nilialikwa kwenye ofisi ya tawiya Mashahidi wa Yehova ya Ufaransa huko Lou-viers kwa mwezi mmoja kwa ajili ya mazoezi yakutafsiri. Hivi karibuni, ofisi hiyo imekuwa nakazi nyingi ya kutayarisha DVD za machapishombalimbali katika Lugha ya Ishara ya Ufaransa.
Lakini kwa sababu kazi ni nyingi, watafsiri zaidiwalihitajika.
Mimi na Vanessa tuliliona kuwa pendeleo nazawadi kubwa kutoka kwa Yehova Mungu ku-tumika kwenye ofisi ya tawi. Hata hivyo, tuliku-wa na wasiwasi. Ingekuwaje kwa kikundi chetucha lugha ya ishara? Tungefanya nini na nyumbayetu? Je, Vanessa angepata kazi katika eneo hilo?Kwa njia ya ajabu, Yehova alisuluhisha kila tatizo.Kwa kweli nilihisi upendo wa Yehova kutuelekeana pia kuwaelekea viziwi.
KUTEGEMEZWA NA WATU WENYE UMOJA
Baada ya kufanya kazi ya kutafsiri, sasa ninae-lewa vizuri kazi inayohusika katika kuwasaidia vi-ziwi wamjue Mungu. Na inafurahisha kama ninikuona wafanyakazi wenzangu wakijitahidi ku-wasiliana nami! Ninaguswa moyo sana ninapoo-na wakijitahidi kuzungumza kwa ishara. Sijihisimpweke, hata kidogo. Matendo hayo yote ya upe-ndo ni wonyesho wa umoja usio na kifani miongo-ni mwa watu wa Yehova.—Zaburi 133:1.
Ninathamini kwamba kupitia kutaniko la Kikri-sto, sikuzote Yehova amehakikisha nimepata mtuwa kunisaidia. Pia, ninathamini sehemu ndogoambayo nimetimiza katika kuwasaidia viziwi we-nzangu kumjua Muumba wetu mpendwa na ku-mkaribia. Ninatazamia siku ambayo vizuizi vyotevya mawasiliano vitaondolewa na wanadamu wotekwa umoja watazungumza ile “lugha safi,” inayohu-siana na kujua ukweli kumhusu Yehova Mungu namakusudi yake.—Sefania 3:9. ˇ
Nikitoa hotuba inayotegemeaBiblia kwa kutumia Lugha
ya Ishara ya Ufaransa
Mke wangu, Vanessa, amenisaidia sana Nikifanya kazi katikaIdara ya Tafsiri
kwenye ofisi ya tawi
Mungu anataka tufanye nini? Je, kuna sheria nyi-
ngi sana ambazo tunapaswa kufuata? Hapana. Ku-
lingana na Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, yale
ambayo Mungu anataka tufanye yanaweza kufafa-
nuliwa kwa neno moja tu!—Soma Marko 12:28-31.Kwanza fikiria wakati ambapo Yesu aliyasema
maneno hayo. Alikuwa akifundisha hekaluni siku
ya Nisani 11, siku chache tu kabla ya kifo chake.
Adui zake walijaribu kumnasa kwa kumuuliza ma-
swali ya kumtega. Kila mara, aliwanyamazisha kwa
majibu yake. Kisha wakamuuliza Yesu hivi: “Ni amri
gani iliyo ya kwanza kati ya zote?”—Mstari wa 28.
Hilo lilikuwa swali gumu. Baadhi ya Wayahudi
walikuwa wamebishana kuhusu sheria iliyokuwa
muhimu kabisa kati ya sheria zaidi ya 600 zili-
zofanyiza Sheria ya Musa. Wengine waliona kwa-
mba sheria zote zilikuwa muhimu na kwamba lili-
kuwa kosa kuona sheria moja kuwa muhimu zaidi.
Yesu angejibuje?
Katika jibu lake, Yesu hakutaja amri moja bada-
la yake alitaja mbili. Kwanza alisema: “Nawe lazi-
ma umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako
wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote
na kwa nguvu zako zote.” (Mstari wa 30; Kumbuku-
mbu la Torati 6:5) Maneno “moyo,” “akili,” “nafsi,”
na “nguvu” yanakazia jambo moja.� Maana yake
ni: Tunapaswa kumpenda Yehova kikamili, na kwa
uwezo wetu wote. Kitabu kimoja cha marejezo ki-
nasema hivi: “Mungu anapaswa kupendwa kabi-
sa na kikamili.” Ikiwa unampenda Mungu, kila siku
utajitahidi uwezavyo kuishi katika njia ambayo ita-
mpendeza.—1 Yohana 5:3.
Pili, Yesu alisema: “Mpende jirani yako kama
wewe mwenyewe.” (Mstari wa 31; Mambo ya Wala-
� Katika Biblia neno “nafsi” hurejezea mtu kwa ujumla. Kwahiyo “nafsi” inaweza kutia ndani “moyo,” “akili,” na “nguvu.”
wi 19:18) Hatuwezi kumpenda Mungu na kumchu-kia jirani. Amri ya pili inatokana na ile ya kwanza.(1 Yohana 4:20, 21) Ikiwa tunawapenda maji-
rani kama tunavyojipenda, tutawatendea kwa njiaambayo tungependa watutendee. (Mathayo 7:12)Na hivyo, kuonyesha kwamba tunampenda Mungu
aliyetuumba sisi na pia majirani zetu, kwa mfanowake.—Mwanzo 1:26.
Amri ya kumpenda Mungu na jirani ni muhimu
kadiri gani? “Hakuna amri nyingine yoyote iliyo ku-bwa kuliko hizi,” akasema Yesu. (Mstari wa 31)
Katika simulizi linalofanana na hilo, Yesu alisema
kwamba amri nyingine zote hutegemea amri hizombili.—Mathayo 22:40.
Si vigumu kumpendeza Mungu. Mambo anayo-taka waabudu wake wafanye yanaweza kufafanuli-wa kwa neno moja tu: upendo. Sikuzote upendoumekuwa—na utaendelea kuwa—alama inayota-mbulisha ibada ya kweli. Lakini upendo hauhusishitu maneno na hisia; unapaswa kuonyeshwa kupi-tia matendo. (1 Yohana 3:18) Kwa nini usijifunze ji-nsi unavyoweza kusitawisha na kuonyesha upendowako kwa Yehova, Mungu ambaye “ni upendo”?—1 Yohana 4:8. ˇ
MKARIBIE MUNGU
“Ni Amri Gani Iliyo yaKwanza Kati ya Zote?”
Mambo ambayo Yehova anatakawaabudu wake wafanyeyanaweza kufafanuliwa kwa nenomoja tu: upendo
USOMAJI WA BIBLIA UNAOPENDEKEZWA
KWA MWEZI WA MACHI
Marko 9–Luka 6
Kama ujuavyo, uwongo ni jambo unalosema huku
ukijua si la kweli. Je, umewahi kudanganya?—�Hata baadhi ya watu wazima wanaompenda Mungu
wamewahi kudanganya. Huenda unajua mtu fulani
anayetajwa katika Biblia ambaye alidanganya. Anai-
twa Petro, mmoja wa mitume 12 wa Yesu. Acheni tu-
sikilize hadithi kuhusu kilichofanya adanganye.
Baada ya kukamatwa, Yesu anapelekwa nyumba-
ni kwa kuhani mkuu. Ni usiku wa manane. Petro
anaingia kwenye ua wa nyumba ya kuhani bila ku-
tambulika. Kupitia mwangaza wa moto, kijakazi wa
kuhani mkuu aliyemruhusu Petro aingie anamta-
mbua. “Wewe, pia, ulikuwa pamoja na Yesu,” ana-
sema. Kwa woga, Petro anakataa.
Biblia inasema baadaye “msichana mwingine ali-
mwona.” Akasema: “Mtu huyu alikuwa pamoja na
Yesu.” Tena, Petro anakataa. Baada ya muda mfupi,
watu wengine wanamjia Petro na kumwambia: “Ha-
kika wewe pia ni mmoja wao.”
Petro anazidi kuogopa. Hivyo, kwa mara ya tatu,
anadanganya, kwa kusema: “Simjui mtu huyo!” Jo-
goo anawika. Yesu anamtazama Petro, na Petro
anakumbuka kwamba saa kadhaa mapema, Yesu
alimwambia: “Kabla ya jogoo kuwika, utanikana
mara tatu.” Petro anaanza kulia kwa uchungu. Ana-
sikitika sana!
Je, unaweza kupatwa na jambo kama hilo?—Unapokuwa shuleni, unaweza kusikia wanafunzi
wakizungumza kuhusu Mashahidi wa Yehova. “Ha-
wapigii bendera saluti,” anasema mmoja wao. “Ha-
wapiganii nchi yao,” mwingine anaongezea. Huku
mwingine akidai: “Kwa kweli si Wakristo, kwa sa-
babu hawasherehekei Krismasi.” Kisha mmoja wao
anakuangalia na kusema, “Si wewe ni mmoja wa
Mashahidi wa Yehova?” Utasema nini?—
� Kama unasoma sehemu hii pamoja na mtoto, unapoona ki-stari kama hiki (—), tua na umtie mtoto moyo atoe maoni yake.
WAFUNDISHE WATOTO WAKO
Petro na AnaniaWalidanganyaTUNAJIFUNZA NINI?
14
Kabla jambo kama hilo halijatukia, unapaswa ku-
jitayarisha ili ujibu inavyofaa. Petro hakuwa tayari.
Aliposhinikizwa, alidanganya! Hata hivyo, alihuzuni-
shwa na yale aliyofanya, na Mungu akamsamehe.
Anania ni mwanafunzi mwingine wa Yesu, amba-
ye pia alidanganya. Lakini Mungu hakumsamehe
yeye wala Safira, mke wake. Alikuwa amekubalia-
na na mumewe kudanganya. Acheni tuone kwa nini
Mungu hakuwasamehe Anania na Safira.
Siku kumi baada ya Yesu kuwaacha mitume na
kurudi kwa Mungu mbinguni, watu 3,000 hivi wana-
batizwa huko Yerusalemu. Wengi wametoka mae-
neo ya mbali ili kuja kusherehekea Sherehe ya Pen-
tekoste, na baada ya kuwa wanafunzi wa Yesu,
wanataka kuendelea kukaa Yerusalemu ili wajifu-
nze mengi kuhusu imani yao mpya. Hivyo, baadhi ya
wanafunzi wa Yesu wanatumia pesa zao ili kuwatu-
nza.
Anania na mke wake wanauza mali fulani ili wa-
pate pesa za kuwasaidia watu waliotoka tu kubati-
zwa. Anania anapoleta pesa hizo kwa mitume, ana-
sema ni kiasi kamili cha pesa walizopata. Lakini
si kweli! Amejiwekea kiasi fulani cha pesa! Mu-
ngu anamwezesha Petro kutambua jambo hilo, hi-
vyo Petro anamwambia Anania: “Umedanganya, si
wanadamu, bali Mungu.” Papo hapo, Anania anaa-
nguka chini na kufa! Saa tatu hivi baadaye, mke
wake anaingia. Bila kujua kilichompata mumewe,
yeye pia anadanganya kisha anaanguka na kufa.
Hili ni onyo kali kwetu: Ni jambo muhimu kuse-
ma ukweli! Naam, sote tunapaswa kujifunza somo
hilo! Hata hivyo, tutakosea, hasa tunapokuwa wado-
go. Je, hufurahi kwamba Yehova anakupenda naatakusamehe kama alivyomsamehe Petro?—Laki-
ni kumbuka, tunapaswa kusema ukweli. Na kama
tutafanya kosa kubwa la kudanganya, tunapaswa
kuomba, ndiyo, kumsihi Mungu atusamehe. Bila
shaka, Petro alifanya hivyo, na alisamehewa. Tukiji-
tahidi kabisa kutodanganya tena, Mungu atatusa-
mehe pia! ˇ
SOMA KATIKA BIBLIAYAKO
Mathayo 26:69-75
Matendo 2:38-42;
4:32-37; 5:1-11
WHAT DOESTHE BIBLE
Really TEACH?
wp13 03/01-SW
Kwa nini Yesu anaitwaMwana wa Mungu?
Mungu hana mke ambaye walizaa naye watoto. Yeye
ndiye Muumba wa kila kitu. Wanadamu waliumbwa
wakiwa na uwezo wa kuiga sifa za Mungu. Hiyo ndiyo
sababu Adamu, mwanadamu wa kwanza kuumbwa
na Mungu, anaitwa “mwana wa Mungu.” Vivyo hi-
vyo, Yesu anaitwa “Mwana wa Mungu” kwa sababu
aliumbwa akiwa na sifa kama za Baba yake.—SomaLuka 3:38; Yohana 1:14, 49.
Yesu aliumbwa lini?Mungu alimuumba Yesu kabla ya kumuumba Ada-
mu. Kwanza, Mungu alimuumba Yesu kisha aka-
mtumia kufanya vitu vingine vyote, kutia ndani
malaika. Hiyo ndiyo sababu Biblia inamwita Yesu
“mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote” vya Mungu.
—Soma Wakolosai 1:15, 16.Kabla ya kuzaliwa huko Bethlehemu, Yesu aliishi
akiwa kiumbe wa roho mbinguni. Wakati ulipofika,
Mungu aliuhamisha uhai wa Yesu kutoka mbinguni
mpaka kwenye tumbo la uzazi la Maria ili azaliwe
akiwa mwanadamu.—Soma Luka 1:30-32; Yohana6:38; 8:23.
Kwa nini Mungu alitaka Yesu azaliwe duniani aki-
wa mwanadamu? Yesu alitimiza daraka gani mu-
himu? Unaweza kupata majibu ya maswali hayo
katika Biblia, na yatakusaidia sana kuelewa na ku-
thamini yale ambayo Mungu na Yesu wamekufanyia.
MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA
SOMA MAJIBU YA MASWALI ZAIDIYA BIBLIA KWENYE INTANETI
Yesu alikuwa kiumbe wa roho mbingunikabla ya kuzaliwa huko Bethlehemu
Kwa habari zaidi ona sura ya 4 yakitabu hiki, kilichochapishwa
na Mashahidi wa Yehova
sPakua gazeti hili namatoleo yaliyotanguliabila malipo
Makala na mazoezi kwaajili ya wazazi, vijana,na watoto
Biblia inapatikana kwenyeIntaneti katika lugha 50 hivi
no
mq
p