Sheria za maji media workshop 2010

23
Sheria za Maji Sheria na. 11 & 12 za Mwaka 2009 Warsha ya Waandishi wa Habari ARM Hotel – 8 – Novemba, 2010

description

Presentation on Tanzanian Water Legislation, shared with Daraja's media partners on the Maji Matone programme, November 8th 2010.

Transcript of Sheria za maji media workshop 2010

Page 1: Sheria za maji   media workshop 2010

Sheria za MajiSheria na. 11 & 12 za Mwaka 2009

Warsha ya Waandishi wa HabariARM Hotel – 8 – Novemba, 2010

Page 2: Sheria za maji   media workshop 2010

YaliyomoUtanguliziSheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira

Madhumuni Majukumu ya kitaasisi

Vyombo vya watumia maji Malengo Uanzishwaji Vyanzo vya mapato Taarifa

Page 3: Sheria za maji   media workshop 2010

1. UTANGULIZI Sekta ya Maji imegawanyika katika maeneo muhimu mawili

ambayo ni (i) rasilimali za maji na (ii) huduma za maji.

Sheria Mpya za Maji za 2009 zinasimamia maeneo hayo kama ifuatavyo:

(i). Rasilimali za maji Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji [The Water Resources Management Act] Na. 11 ya Mwaka 2009 inahusika na usimamizi wa rasilimali za maji - vyanzo vya maji juu na chini ya ardhi.

Imetungwa na Bunge tar 28/4/2009, imesainiwa na Mhe. Rais tar 12/5/2009 na kuanza kutumika rasmi tar 1/8/2009 baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali (GN 235 LA 10/7/2009). 3

Page 4: Sheria za maji   media workshop 2010

1. UTANGULIZI ...(ii). Huduma za maji:

- Sheria ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira [The Water Supply and Sanitation Act] Na. 12 ya Mwaka 2009 Inasimamia utoaji huduma za maji na usafi wa mazingira ktk mikoa yote TZ isipokuwa DSM na Pwani.Imetungwa na Bunge tar 28/4/2009, imesainiwa na Mhe. Rais tar 12/5/2009 na imeanza kutumika rasmi tar 1/8/2009 baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali (GN 234 la 10/7/2009).

- Sheria ya DAWASA inasimamia utoaji huduma za maji DSM na maeneo ya mkoa wa Pwani.Imetungwa 2001 na kuanza kutumika 2001

4

Page 5: Sheria za maji   media workshop 2010

1. UTANGULIZI ...Sheria za Maji zilizokuwa zinatumika kabla ya sheria mpya

za 2009 ni:-(i). Sheria ya Matumizi na Udhibiti wa Maji 1974

Ilikuwa inasimamia rasilimali za maji.

(ii). Sheria ya Miundombinu ya Maji 1949Ilikuwa inasimamia utoaji huduma za majisafi na majitaka.

5

Page 6: Sheria za maji   media workshop 2010

1. UTANGULIZI ...Sheria Mpya za Maji ziliandaliwa kwa kuzingatia matamko

yaliyomo kwenye Sera ya Taifa ya Maji ya 2002 na Mkakati wa kuendeleza Sekta ya Maji 2006-2015. Nyenzo hizi mbili zimeelezea malengo, mikakati na mifumo katika kusimamia sekta ya maji.

Lengo ni kuipa sera/mkakati nguvu za kisheria katika utekelezaji wake.

Sheria za Maji zinatekelezwa sambamba na sheria

nyingine za nchi (mf. Sheria za Mazingira, Ardhi, Misitu, LGAs, EWURA n.k). 6

Page 7: Sheria za maji   media workshop 2010

2. SHERIA YA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA NA. 11/2009

Imefuta Sheria ya Miundombinu ya Maji sura 272 (The Waterworks Act).

Inasimamia utoaji huduma za majisafi na usafi wa mazingira ktk mikoa yote isipokuwa DSM na Pwani ambako inatumika Sheria ya DAWASA.

Inahusika na uundaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira kwenye miji yote TZ, Vyombo vya Kijamii vinavyohusika na utoaji wa huduma za maji (Community Owned Water Supply Organisations - COWSOs) i.e Jumuiya za Watumiaji Maji n.k.

Imeainisha majukumu ya Waziri wa Maji, Waziri wa TAMISEMI, Sekretariati za Mikoa, Serikali za Mitaa, Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira na COWSOs.

Imeanzisha Mfuko wa Taifa wa Maji ambao utahusika katika uwekezaji kwenye vidakio vya maji.

7

Page 8: Sheria za maji   media workshop 2010

SHERIA YA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA...

MadhumuniKuhakikisha kuwa kila mtu anapata huduma ya maji na usafi wa

mazingira ya uhakika na endelevu kwa kuzingatia kanuni ambazo ni pamoja na:-

- Kujenga mazingira wezeshi na hamasa ktk kutoa huduma ya uhakika, endelevu na kwa bei nafuu.

- Kukasimu kazi za usimamizi wa utoaji huduma ktk ngazi stahili za chini kwa kuzingatia mfumo wa tawala za serikali za mitaa.

8

Page 9: Sheria za maji   media workshop 2010

SHERIA YA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA...

Madhumuni …- Kuweka utaratibu wa kuhakikisha kuwa jamii inamudu gharama za uendeshaji

na matengenezo ya miradi na kuchangia gharama za uwekezaji.

- Kuhamisha umiliki wa miradi ya maji vijijini kwenda kwa jamii husika na kuwawezesha kushiriki kikamilifu ktk usimamizi wa miradi.

- Uhamasishaji wa ushirika baina ya sekta ya umma na binafsi ktk utoaji huduma.

- Kuweka na kutekeleza viwango vya huduma ya maji na usafi wa mazingira.

9

Page 10: Sheria za maji   media workshop 2010

SHERIA YA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA...

Majukumu ya Taasisi zilizowekwa:1. Waziri wa Maji (k.5):

- Majukumu yake ni pamoja na kushughulikia utungwaji wa sera, mkakati na sheria zinazohusu utoaji wa huduma za maji; kutafuta fedha kwa ajili ya miradi mikubwa ya kitaifa.

2. Waziri wa TAMISEMI (k.6) - Majukumu yake ni pamoja na kuhakikisha LGAs zinatekeleza kazi zake zinazohusiana na sheria hii.

3. Sekretariati za Mikoa (k.7)

- Majukumu yake ni pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam kwa LGAs kuhusu masuala ya huduma za maji na usafi wa mazingira; kutathmini miradi ya LGAs na kutoa misaada ya kiufundi.

10

Page 11: Sheria za maji   media workshop 2010

SHERIA YA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA...

Majukumu ya Taasisi…4. Serikali za MitaaMajukumu yake ni pamoja na- kuratibu mahitaji ya bajeti za mamlaka za maji na kutoa fedha kwa mamlaka za

maji.

- Kuhamasisha uundwaji wa vyombo vya watumiaji maji na kusajili vyombo vya watumiaji maji.

- Kutatua migogoro ndani ya vyombo vya watumiaji maji.

- Kutunga sheria ndogo (by-laws) zinazohusu utoaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira ktk maeneo yao.

11

Page 12: Sheria za maji   media workshop 2010

SHERIA YA HUDUMA ZA MAJI NA USAFI WA MAZINGIRA...

5. Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira (WSSA)Majukumu yake ni pamoja na:- kutoa huduma za maji na usafi wa mazingira;

- Kushauri serikali kuhusu utayarishaji wa sera na viwango vya majisafi. 7. EWURA

Inadhibiti WSSA ktk utoaji wa huduma za maji na usafi wa mazingira (kutoa leseni, kupitisha bei za maji n.k)

6. Vyombo vya Watumiaji Maji

12

Page 13: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI

Kwa mujibu wa Sheria Mpya za Maji vyombo vya watumiaji ndiyo ngazi ya chini kabisa ambayo inahusisha watumiaji wenyewe.

Lengo ni kuhakikisha kuwa wananchi/watumiaji wanashiriki kikamilifu moja kwa moja katika kubuni, kusimamia na kuendesha miradi ya maji.

Vyombo vya watumiaji maji vipo katika mifumo mbalimbali na taratibu za uanzishwaji wake unategemea aina ya chombo na sheria inayohusika.

13

Page 14: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI...

Kwa mujibu wa Sheria Na. 12/2009 ..Kwa mujibu wa k.31 vyombo vya watumiaji maji (Community Owned Water

Supply Organisations – COWSOs) vinaundwa kwa makubaliano wengi kwenye jamii.

COWSOs vinaweza kuundwa katika mfumo wa:-a) Jumuiya ya Watumiaji Maji (Water Consumer Association)b) Udhamini (Water Trust)c) Chama cha ushirika (Cooperative Society)d) Shirika lisilo la kiserikali (Non Government Organisation)e) Kampuni (Company) au f) chombo kingine chochote kitakachoidhinishwa na Waziri wa Maji.

14

Page 15: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI...

Kwa mujibu wa Sheria Na. 12/2009 .. COWSO ni chombo cha kisheria chenye uwezo wa kushtaki na kushtakiwa [k. 31(3)] na

vina uwezo wa:-

kumiliki mali zinazohamishika na zisizo hamishika ikiwa ni pamoja miundombinu ya maji.

Kusimamia, kuendesha na kuiendeleza miundombinu, na kutoa maji safi na salama kwa wateja;

Kuwalipisha wateja maji waliyotumia;

Kuwasiliana na kushirikiana na mabaraza ya vijiji au taasisi inayohusika na ardhi ili kupanga na kudhibiti matumizi ya ardhi karibu na miundombinu ya maji.

Kuteua mtoa huduma (Service Provider) kwa makubaliano.

15

Page 16: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI...

Kwa mujibu wa Sheria Na. 12/2009 ..COWSO iliyopendekezwa inatakiwa iandae katiba na kuiwasilisha LGA kwaajili

ya kuidhinishwa. Inaweza kuomba LGA iwasaidie kuandaa katiba.

Taratibu za usajili zimefafanuliwa kwenye Kanuni GN 21 ya 22/01/2010.

Kutakuwa na Msajili (kutoka miongoni mwa watumishi wa LGA) wa COWSOs kwa kila LGA ambaye atateuliwa na Mkurugenzi wa Halmashauri husika.

Kuhusu COWSOs Msajili atahusika ktk kuidhinisha katiba; kusajili na kusimamisha au kufuta usajili; kuhifadhi kumbukumbu; kufanya uchunguzi wa uendeshaji wa COWSOs na kazi nyingine atakazoelekezwa na Mkurugenzi.

Msajili atasajili COWSO ndani ya siku 30 tangu apokee maombi

16

Page 17: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI...

Kwa mujibu wa Sheria Na. 12/2009 .. Maombi ya usajili yatawasilishwa na mmoja au zaidi ya wanachama waanzilishi na

yataambatishwa na katiba, muhtasari wa kikao cha wanachama, maelezo ya washika ofisi, anuani na mahali ilipo ofisi, ada ya usajili na maelezo mengine atakayohitaji Msajili [r.10(2)].

COWSOs zilizopo kabla ya sheria hii pia zinatakiwa kuomba usajili.

Baada ya usajili COWSO itawajibika na mradi wa maji husika [k. 34(2)].

Maamuzi ya Msajili yanaweza kufanyiwa mapitio na yeye mwenyewe au kwa kukata rufaa kwa Mkurugenzi

17

Page 18: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI...

Vyanzo vya mapato ya COWSO (k.36):-Malipo ya huduma kutoka kwa wateja

Michango kutoka kwa wanachama.

Michango, mikopo au misaada mingine yoyote ya kifedha kwa idhini ya Waziri mwenye dhamana ya TAMISEMI.

Kiasi chochote kitakachotengwa na Halmashauri.

Kiasi chochote cha fedha kitakachotolewa na Halmashauri husika kwa ajili ya kugharimia ujenzi wa miradi mipya, kukarabati na kupanua miradi iliyopo.

18

Page 19: Sheria za maji   media workshop 2010

VYOMBO VYA WATUMIAJI MAJI...Taarifa za COWSOsCOWSO iliyopata msaada wa fedha kutoka Halmashauri

inapaswa kuwasilisha kwa Halmashauri husika taarifa za utekelezaji zinazoonyesha mapato na matumizi na taarifa za ukaguzi [k.37A].

Taarifa za kazi za mwaka ambazo zitapatiwa wajumbe, Msajili, Mkurugenzi na wadau wengine [r.16].

Kuandaa tarifa za ukaguzi za kuziwasilisha kwa Msajili na Mkurugenzi [r.16].

19

Page 20: Sheria za maji   media workshop 2010

MAKOSA NA ADHABU

Sheria Mpya za Maji zimeainisha makosa ya jinai na adhabu ambazo zitatolewa kwa mtu atakayepatikana na hatia.

Sheria Na. 12/2009 - Makosa yanahusiana na uharibu wa miundombinu, uchafuzi wa

maji n.k- Adhabu ni kulipa faini na kifungo kulingana na ukubwa wa kosa.

Taratibu za kushughulikia makosa ya jina zimeelezwa kwenye Sheria ya mwenendo ya Makosa ya Jinai (Jeshi la Polisi, DPP wanahusishwa)

20

Page 21: Sheria za maji   media workshop 2010

HITIMISHOSheria za Maji ni mpya na zina malengo mazuri ambapo

zikitekelezwa vizuri zitasaidia kuimarisha sekta ya maji na hivyo kuwa na uhakika wa upatikanaji wa maji kwa afya na maendeleo ya jamii.

Ingawa kutojua sheria sio kinga, elimu kwa wadau ni muhimu hivyo sisi kama wadau tunapaswa kuendelea kutoa elimu hii kwa wananchi.

21

Page 22: Sheria za maji   media workshop 2010

quotes‘‘The Law is good, if a man use it lawfully’’

(1Timothy, 1:8)

“No man is above the law and no man is below it; nor do we ask any man’s permission when we ask him to obey it”.

(Theodore Roosevelt, 26th President of US)

“If he who breaks the law is not punished, he who obeys it is cheated.”

[Dr. Thomas Szasz, Prof. Syracuse University]

22

Page 23: Sheria za maji   media workshop 2010

aSaNtEnI

23