MwiliMmoja - norgeskristnerad.no · Nitaurudishaje ujasiri wangu ka-tika maamuzi yangu mwenyewe?...
Transcript of MwiliMmoja - norgeskristnerad.no · Nitaurudishaje ujasiri wangu ka-tika maamuzi yangu mwenyewe?...
UKIMWI na Jamii Inayoabudu
MwiliMmojaKITABU CHA 2
USHIRIKIANO WA MAKANISA YA NORDIC – FOCCISA
AFRIKA KUSINI ANGOLA BOTSWANA DENMARK FINLAND ICELAND LESOTHO MALAWI MSUMBIJI NAMIBIA NORWAY SWAZILAND SWEDEN TANZANIA ZAMBIA ZIMBABWE
UKIMWI NA Jamii inayoabudu
MwiliMmojaKITABU CHA 2
Mwili Mmoja Kitabu cha 1 kina makusanyo ya mitazamo
kuhusu changamoto, kwa ajili ya kanisa na unyanyapaa un-
aohusiana na UKIMWI.
Mwili Mmoja Kitabu cha 2 kimejikita katika maombi, utarati-
bu wa ibada, kuabudu na kujifunza Biblia, ikichanganyikana
na shuhuda binafsi kutoka kwa watu waishio na UKIMWI. Vi-
tabu vyote (cha Kwanza na cha Pili) vimetolewa katika lugha
za Kiingereza, Kireno, Kiswahili na Kinorwejiani.
Ushirikiano wa NORDIC FOCISSA ni uhusiano wa pamoja baina ya
mabaraza ya makanisa kumi na moja ya Kusini mwa Afrika na ma-
baraza ya makanisa ya nchi za Kaskazini mwa Ulaya.
Ushirikiano wa Makanisa Kusini mwa Afrika na Ulaya Kaskazini
(Nordic Foccisa) inato shukrani zake kwa NORAD na DANDA/ Dan-
Church Aid kwa uhisani wao kuusaidia Mradi huu.
MHARIRI Elizabeth Knox-Seith, DanChurchAid
MRATIBU Jan Bjarne Sødal, Baraza la Kikristo, Norway
BODI YA UHARIRI Precious Mwewa, Mwandishi wa Labari,
Zambia. Mch. Japhet Ndlovu Baraza
la Makanisa nchini, Zambia. Mch. Elias
Zacarias Massicame, Baraza la Makanisa,
Msumbiji. Jan Bjarne Sodal, Baraza la
Kikristo, Norway. Mch. Birthe Juel Chris-
tensen, DanChurchAid, Denmark.
MSHAURI WA NJE Gillian Paterson
WATAFSIRI George Mwita - CUAHA, Edwin Msiri - Tan-
zania Development Mates. Ivan Chetwynd
(Kiingereza na Kinorwejiani). Melodien na
Tony Winch (Kireno)
MPIGA PICHA Ulrik Jantzen, Das Büro, Copenhagen
WANAMITINDO Beauty Chandra na Preben Bakbo Sloth,
wanaharakati VVU+
MICHORO YA KITAALAMU Anne Mousten na Kit Harding
MPIGA CHAPA Jonsson Grafisk, Copenhagen
IMETOLEWA NA Ushirikiano wa Makanisa ya Kaskazini na
Kusini (NORDIC-FOCCISA)
ISBN 978-82-7941-031-7
© © Baraza la Kikristo, Norway, [email protected]
JINA LA AWALI LA KITABU One Body (Mwili Mmoja)Kitabu hiki si cha kuuza au kutumiwa kwa malengo ya kibiashara. Maandishi yanaweza kunukuliwa au
kurudufiwa, ili mradi upendeleo unatolewa kwa mwandishi na mtoaji wa kitabu hiki.
NAKALA ZA TOLEO LA KISWAHILI KITABU CHA KWANZA NA CHA KITABU PILI ZINAWEZA KUAGIZWA KUTOKA:
Jumuia ya Kikristo Tanzania Simu +255 262324445 email: [email protected]
Baraza la Kikristo Norway Simu +47 23081300 email: [email protected]
NAKALA ZA TOLEO LA KIINGEREZA ZINAWEZA KUAGIZWA TOKA:
Baraza la Kikristo Norway Simu +47 23081300 email: [email protected]
Baraza la Makanisa Zambia Simu 260-1-229551-224622 email: [email protected]
UTANGULIZI 1
Mwili Mmoja
USHIRIKIANO WA MAKANISA YA NORDIC – FOCCISA
UKIMWI NA Jamii inayoabudu
Mafunzo ya Biblia, Liturjià na Hadithi Binafsi Kutoka Kusini na Kaskazini
KITABU CHA 2
2 UTANGULIZI
UTANGULIZI
Kuabudu Katika Namna Tofauti
DENMARK Hali Halisi
DENMARK Yubile ya Maono kwa Kanisa
ZAMBIA Kuvunja Ukimya na Fedheha
NORWAY Unyanyapaa na Utu
NORWAY Mahali Salama kwa Mazungumzo
NORWAY Biblia Kitabu Kitakatifu
ZAMBIA Kujifunza Biblia
KANISA
ZAMBIA Kanisa Lenye Huruma
MSUMBIJI Kuwakumbatia Waliosahauliwa
DENMARK Kutengeneza Jumuia Mpya Zenye Tumaini
NORWAY Kuwa Mwili Mmoja
NORWAY Mwanamke Aliyekuwa Apigwe Mawe
DENMARK Pumziko Lenye Tumaini
UJINSIA WA BINADAMU
ZAMBIA Ubaba, Jinsia na Yesu
ZAMBIA Ujinsia – Kipawa na Wajibu
NORWAY Nani Anayediriki Kurusha Jiwe la Kwanza
DENMARK Maana, Kifo na Upotevu
SURA ZA MUNGU
DENMARK Imani
ZAMBIA Matendo ya Uponyaji ya Yesu
DENMARK Sura Nne za Mungu
ZAMBIA Mungu Anayesamehe
ZAMBIA Mungu wa Uumbaji
NORWAY Mwanamke Mlemavu
ZAMBIA Hakuna Hukumu
NORWAY Utaratibu wa Ibada Kwa Vituo
DENMARK Juu ya Ukaribu
DENMARK Mungu anayetugusa
DENMARK Kuwasha Mishumaa
DENMARK Sala Siku ya UKIMWI Duniani
3
5
6
10
12
14
16
18
21
22
24
26
29
30
33
34
36
40
43
44
46
48
49
50
52
54
58
60
62
64
UTANGULIZI 3
NA JAPHET NDLOVU, BARAZA LA MAKANISA LA ZAMBIA
JAN BJARNE SØDAL, JUMUIA YA KIKRISTO YA NORWAY
BIRTHE JUEL CHRISTENSEN, DANCHURCHAID – DENMARK
ELIAS MASSICAME, JUMUIA YA KIKRISTO YA MSUMBIJI
Tangu mwanzo Wakristo wengi wamechukulia kuabudu kama
tendo muhimu la utambulisho wao. Wanathiolojia wengi wa
Kikristo wamemfasili binadamu kama homo adoran: yaani ki-
umbe ambaye asili yake ni kuabudu. Hii ina maana kwamba
kumwabudu Mungu ndiyo kiini cha kuwa mwanadamu. Ni kati-
ka ibada zetu – roho za maisha yetu katika jumuia – tunapoweza
kuwasiliana na kumleta Mungu katika maisha binafsi.
Kama sehemu muhimu katika mradi wa pamoja juu ya
mtazamo wa kithiolojia kuhusu VVU na UKIMWI wa Jumuia
za Kikristo Kusini mwa Afrika na Nchi za Ulaya za Nordic –
FOCCISA – tumekuwa tukishughulikia masuala ya Liturjia na
kujifunza Biblia. Katika Biblia na kupitia mafunzo ya Biblia na
kwa kutengeneza majaribio kiliturujia, tumegundua vyanzo na
msukumo mpya. Hii inaonyesha uhitaji wa njia sahihi ambao
kwa pamoja unaleta neno la Mungu katika maisha yetu, katika
mtazamo wa VVU na UKIMWI na katika uhalisi wa changamoto
na mahitaji ambayo ugonjwa umeleta.
Liturjia ya kanisa imejengeka katika uzoefu wa jumuia fulani.
Kwa ujumla jumuia hizi zinaonyesha uzoefu tofauti na hali za
kimaisha – vijana na wazee, matajiri na masikini, wenye afya
na wagonjwa, wanaume na wanawake, wenye VVU na wasio na
VVU, familia na waseja, watu wanaoteseka kwa kukosa amani
na walio na amani, wale wenye furaha na wale wenye huzuni.
Liturjia ya kanisa inaonyesha ibada ya jumuia yote, kwa hiyo
kuabudu lazima kuwe ni kwa kubadilika ili kuweza kugusa
changamoto mbalimbali zinazowakabili wanadamu. Ni lazima
pia kuwe na majumuisho: ili kwamba kwa kuongea kuhusu au
kumwelezea Mungu, ni lazima tuelewe umuhimu wa kukwepa
unyanyapaa au hali za kutengana na lugha tunazotumia. Tume-
jaribu kuchunguza kanuni hizi katika liturjia na mafundisho
yetu ya Biblia, ili kufanya zikubalike kadiri inavyowezekana.
Tumefanya maamuzi yakini kutengeneza kitabu chenye
shuhuda binafsi kutoka kwa watu waishio na VVU na UKIMWI,
kutoka Kaskazini na Kusini mwa dunia. Shuhuda hizi zinaamsha
maswali muhimu juu ya kutambua, au kuelewa upya, imani
Kuabudu Katika
Namna Tofauti
4 UTANGULIZI
ya Ukristo. Matumaini yetu ni kwamba kitabu chote kitatoa
sehemu ya jibu – angalau uradhi wa kuanzisha kwa pamoja
Liturjia na mafunzo ya biblia, kama sehemu ya changamoto
ambayo makanisa yanapitia dunia nzima, katika nyakati hizi
za UKIMWI.
Ushirikiano Kati ya Kusini na Kaskazini
Mradi huu ulitengenezwa na Jumuia tano za nchi za Nor-
dic na nchi kumi na moja za Kusini mwa Afrika chini ya
kivuli cha ushirikiano wa Kikanisa (NORDIC-FOCCISA),
ulipewa msukumo na makanisa nchini Zambia, Msumbiji,
Norway na Denmark ikiwa na lengo la kukuza mtazamo
wa kithiolojia katika masuala yaliyosababishwa na maam-
bukizi ya VVU.
Katika kitabu hiki, utajua njia za kutumia nyakati za UKIM-
WI, Liturjia, mafunzo ya biblia, ibada au hali zozote. Njia hizi
ni pamoja na shuhuda binafsi, mafundisho ya biblia, liturjia,
mashairi na fikra mbalimbali. Hizi zimeandikwa au kuanda-
liwa na watu waishio na VVU au UKIMWI au wanaohusiana
nao kwa karibu na ambao wanatambua kuwa rasilimali zili-
zopo hazilingani na mahitaji ya makundi yao au makanisa
kwa wakati huu.
Kitabu hiki kimelengwa kwa watu katika jumuia za chini
(mitaa), katika kaskazini na kusini pia, walio na majukumu
ya kufundisha, kuhubiri, kuabudu na kazi nyingine za mi-
kusanyiko ya waumini. Uhitaji ni mkubwa, katika utoaji wa
elimu ya Biblia na liturjia kwa ajili ya matumizi katika wakati
wa VVU na UKIMWI. Hata hivyo, desturi zetu kiliturjia ziko to-
fauti sana, na hatujifanyi kuwa makusanyo yaliyomo katika
kitabu hiki yanatosha sana kuelezea mahitaji yote yaliyopo.
Badala yake mradi huu unaonyesha uzoefu wa Kikristo ulio
tofauti kiasili kuhusiana na VVU na UKIMWI.
Dhamira Tatu
Malengo, kama ilivyo katika kitabu cha kwanza katika mtiririko
huu, yapo katika dhamira tatu kama zilivyoainishwa na uzoefu
wa VVU.
1) Kujumuisha Kanisa
2) Kujamiiana
3) Mfano ( au sura ya) wa Mungu
Tulichokifanya ni kuleta pamoja viini vya dhamira yetu kwa
kutumia vipengele vya Biblia, na kujiuliza namna Liturjia au
elimu ya Biblia inavyoweza kuwa katika mtazamo wetu – kama
ilivyoonyeshwa katika kitabu cha kwanza – juu ya kujamiiana,
kanisa na mfano au sura ya Mungu. Kwa hiyo, maandiko,
yanatofautiana kutokana na hali halisi ya eneo yalipoandikwa.
Hatuonyeshi kuwa hizi ni njia pekee ambazo maandiko ya
Biblia yanaweza kutumika. Hii itatofautiana kutokana na hali
na mazingira ya wale wanaoyatumia. Malengo yamekuwa ni
kuwa makusanyo haya ya maandiko yaonyeshe umoja kadiri
ya namna tulivyoitwa: Hali ya kuwa katika namna tofauti ya
mwili mmoja wa Kristo tunaouita Kanisa.
Unaweza kutumia maandiko haya kadiri unavyotaka. Una-
karibishwa kuchagua, kuchukua au kubandika katika namna
unavyoona inafaa katika desturi na mazingira yako.
Tunatumaini kuwa maandiko haya yatahamasisha na kukuza
mitazamo zaidi, itakayosababisha kuanzisha kwa liturjia mpya
na elimu ya Biblia katika masuala yanayohusu VVU na UKIMWI.
Zaidi ya yote ni matumaini yetu kuwa utaratibu tulioutumia
katika kutoa maandishi haya, utapanda mbegu ndogo ambazo
zinaweza kusababisha kuanzishwa kwa mikusanyiko ya pamo-
ja makanisani, kidunia, kitaifa pamoja na kimitaa au kifamilia.
Kokote tunakotoka, vyovyote tulivyo, iwe tuna VVU au ha-
tuna, tunategemeana ili kuwa kama tulivyo kwa namna Mungu
alivyodhamiria tuwe – Mwili Mmoja katika Kristo.
UTANGULIZI
UTANGULIZI 5
Ninaogopa....
Ninajiogopa mimi mwenyewe, ninauogopa ugonjwa nilionao.-
Kwani itatokea lini, itatokea lini?
Kifo cha taratibu, au labda cha haraka na bila maumivu?
Watu...
Wale wasionionyesha upendo
Wale wasionipa ulinzi ninaohitaji.
Tatizo la kifedha...
Ambapo hakuna msaada unaoweza kuonekana
Hufanya maumivu kuwa makali zaidi.
Wote wananitazama na kutikisa vichwa vyao...
“Hata hivyo unaenda kufa”
“Hatujui mbele hali itakuwaje”
“Una bima ya maisha?”
“Sithubutu kukupenda, Je kama ukifa na kuniacha!”
“Je ukiniambukiza?”
Ninataka kujiua...
Nitafunga kamba kuzunguka shingo yangu
Nitajirusha
Nitameza vidonge,
lakini labda kesho,
katika makutano ya barabara
au ndege ya kijeshi kuangukia katika sebule yangu
Hapana....
Nimetahadharishwa.
Tahadhari ambayo watu wachache tu hupata.
Je inanifanya mimi kuwa wa pekee?
Kitu cha pekee?
Inanifanya niogope
- lakini pia mwenye furaha.
Imenifundisha kupenda maisha
Na kuyathamini
Badala ya kuishi tu.
Sasa nahitaji kuishi
Nahitaji kuujua upendo.
Nahitaji kujua usalama.
Niamini....
Nifanye msikivu
Sikiliza sauti yangu ya ndani.
Sauti.
Hufanya ninyenyue kichwa changu juu
Na kutabasamu juu ya hatima yangu.
Inanifanya niishi kwa matumaini
Na kuniambia ni vyema,
maisha yangu yatakuwa mafupi kuliko ya wengine
Lakini labda mazuri zaidi?
Ninatumaini....
DORTHE, AISHIE NA VVU, DENMARK
Hali Halisi - Nina VVU
6 UTANGULIZI
NA PREBEN BAKBO SLOTH
Ukiwa kijana unatakiwa kuangalia mbele, kutengeneza mipan-
go, kuwa na maono na kuota ndoto. Kuangalia mateso na kifo
cha awali kwa kawaida hatuvioanishi na ujana. Lakini kuwa na
VVU katika umri wa miaka 24 hubadilisha mtazamo wako. Kwa
kuongeza, katika maongezi yetu, daktari aliniambia nina kama
miaka mitano iliyosalia ya kuishi. Wakati ujao ukawa ni tishio,
kupanga kukawa hakuna maana, maono ikawa ni ukwepaji,
ndoto – kufikirika na matumaini ya uongo.
Kuadhiriwa na mtu ambaye hakujali kukuambia ukweli, iliku-
wa ni pigo langu kubwa kuwaamini watu wengine. Nitawezaje
kuwaamini wengine, wakati imani yangu imesalitiwa kabisa
kiasi cha kunipa virusi hatari? Nitaurudishaje ujasiri wangu ka-
tika maamuzi yangu mwenyewe? Nitaweza tena kujitegemea
na kujisimamia maisha yangu mwenyewe? Maswali haya yali-
sababisha kujidharau na hisia ya kutojijali na iliwavunja mioyo
watu wengine.
Wakati huo wafuasi wengine wa mrengo wa kulia wa ka-
nisa walikuwa wakihubiri kuwa VVU na UKIMWI ni adhabu
Ushuhuda Kutoka Kwa Mhanga
Wa Siku Nyingi
kutoka kwa Mungu juu ya maisha ya dhambi. Nikiwa nime-
pooza tayari na mshtuko wa kuhukumiwa kifo, haikuwa ra-
hisi kutoyaweka mahubiri yao moyoni, kupokea hukumu hii
ya Mungu mimi binafsi, kujitwika mabegani mwangu na ku-
jaribu kukubali namna hii ya hukumu takatifu ya ajabu. Na
ndivyo ilivyokuwa mimi, na alama ya kifo ya VVU juu yangu,
iliyobandikwa na hasira ya Mungu, katika hali ya mgogoro
(wa ugonjwa) unaoandamwa na aibu na kujihukumu, niliona
haiwezekani kutaka msaada kutoka kwa mtu mwingine. Si-
kudhubutu kumwendea yeyote kumshirikisha taabu zangu,
kwa sababu nilikwisha ridhia kuwa kila mtu hatonijali, kama
vile Mungu alivyokwisha fanya.
Huwezi kumdanganya Mungu, lakini watu unaweza kujaribu.
Matokeo yalikuwa ni kuishi miaka miwili na siri yangu moyoni.
Miaka miwili ya mateso kisaikolojia, kiroho na kimhemuko. Mia-
ka miwili ya kudanyanya, visingizio na kunyamaza. Miaka miwili
iliyonichukua mbali, mbali sana na marafiki na familia yangu,
kwenye baridi na giza la upweke. Nililikimbia kanisa ambamo
nilikuwa mshirika, kwa kuwa nilipambana na kutengwa.
Yubile ya Maono K
UTANGULIZI 7
UTANGULIZI
Mfano Mpya wa Mungu
Ilikuwa ni baada ya miaka miwili ya kwanza nilipothubutu ku-
tafuta msaada, kujihatarisha kwa kuwa wazi kuhusu hali yangu
kiafya, kujua kama VVU ni adhabu kutoka kwa Mungu na kufi-
kiria mimi kama mfano wa Mungu. Mungu aliongea nami pia,
kwa kutumia picha zilizoniambia kwa uwazi kuwa ninaweza
kutoka kanisani, lakini Mungu hataniruhusu niondoke. Nilipata
nyumba ya kiroho katika kusanyiko dogo mjini Copenhagen.
Hapa nilipewa hamasa, walinielewa, walinikubali na kunijali.
Nilikutana na watu wengine wenye UKIMWI, hali iliyoanzisha
mchakato wa uponyaji ambao haujamalizika mpaka leo, miaka
kumi na tano. Nilijua kuwa hakuna kitu, hata VVU na UKIMWI,
kinachoweza kunitenganisha na Upendo wa Mungu (Warumi
8:38). Katika mazingira ya kushirikishwa na kupendwa hisia ya
hukumu na aibu haraka ilitoweka.
Mahubiri kuhusu upendo wa Mungu usio na masharti na
ushirika unaojali uliumba sura mpya ya Mungu kwa ajili yangu.
Sura ambayo niliweza kujiona na kupata nguvu. Taratibu imani
yangu kwa watu wengine na kwangu ilianza kujengeka.
Mchakato kufikia kujiheshimu na ujasiri ndani yangu na kwa
wengine ulichukua miaka mingi na ulifanikishwa kwa uvumili-
vu, upendo na uelewa wa watu wote ndani na nje ya kanisa, na
uzoefu wa hali inayojirudia ya kutojisikia kuachwa na Mungu
Uzima Huuliza Maana
Maswali mengine mengi na matatizo yameacha makovu katika
miaka kumi na nane iliyopita. Woga wa kujisikia mdhaifu, woga
wa maumivu, woga wa kifo, hali ya kujisikia kukata tamaa na
kutokuwa wa maana baada ya kupoteza marafiki wengi na
kuachwa, kutoamini maisha ya mbele nk. Wakati mwingine
imekuwa ni vigumu kuwa na malengo hata ya muda mfupi,
bila kutaja kuwa na maana katika maisha katikati ya maumivu,
hasara na mateso. Ni katika miaka minne tu iliyopita nime-
tambua kuwa kama maisha na kifo yana maana, basi mateso
lazima yana maana pia. Bila kuamini katika maana, au uhiari
wa kutafuta maana, ningelikwisha kata tamaa, ningeona kila
kitu hakina maana na kumegeka kiroho na kiakili. Kwa hakika
ni uzima pekee ndio huuliza maana na ni lazima nijibu. Nijibu
kwa kutafuta na kupata maana, maana katika hatua tofauti ka-
tika maisha ziletazo majibu.
Kuzungumza na Mungu, maombi na kumtafakari, katika ku-
angalia maisha yangu ndani ya injili na kitabu cha Zaburi, kuku-
tanika na kuzungumza katika kanisa na kukutanika na wengine
walio na UKIMWI imekuwa ni vyombo vya Mungu katika mcha-
kato huu wa uponyaji.
Jumuia ya kanisa na kukutana na wakristo wengine imekuwa
ni msaada usio na kifani. Wamesaidia kujenga daraja kutoka
mauti hadi uzima, kutoka katika kuvunjika hadi kutovunjika na
kutoka kujichukia hadi upendo.
Kanisa lina UKIMWI
Mpambano wangu na kanisa na ujumbe wake, mara baada ya
kuambukizwa, ilikuwa ni kusikia ujumbe wa kuhukumiwa. La-
kini “ kuhukumu ni kuficha upendo wa Mungu”, kama mchun-
gaji Carina Wøhlk alivyosema wakati fulani katika siku ya
UKIMWI duniani. Ni kwa nini kanisa, au angalau sehemu yake,
ni msemaji wa hukumu? Ninaona mifano mingi ndani ya Biblia
kuwa umbo halisi la tabia ya Mungu juu ya wanyonge, walio ka-
tika hatari na waliotengwa ni kuwaingiza kundini, kuwapenda
na kuwajali. Na kama ulivyomtendea mmoja wa wanafamilia
yangu, umenitendea mimi – kwa mema au mabaya.
Kwa Paulo kulinganisha kanisa kama mwili katika akili, wakati
mwingine huwa ninaona kama baadhi ya wanathiolojia na wa-
tafsiri wa maandiko ni meno, nami ni sehemu ya ute ambao
mwili unataka kuutoa! Lakini wakati sehemu moja ya mwili
ina UKIMWI, mwili wote huumia, na kwa hiyo kanisa lote lina
UKIMWI. Kanisa ni lazima lionyeshe huruma kwa kujali, kama
linataka kuishi kufuatana na mtazamo wa Paulo. Kama halitaki
kufanya hivyo, basi lijiite kitu kingine, kwa sababu limekuwa
chanzo cha kuvunja moyo, kukatisha tamaa na mateso.
ubile ya Maono Kwa KanisaDENMARK
8 UTANGULIZI
Kukosa Makazi
Nimekuwa nikiwa na kanisa, Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Den-
mark, kama nyumba yangu ya pili. Kwa namna ile ile nilivyoifa-
hamu nyumba yangu mwenyewe, nilizoea maisha ya kanisani,
ibada na lugha zake na nilijisikia kuwa nyumbani. Lakini nili-
pogundua katika moja ya nyumba zangu siwezi kusema mau-
mivu na mateso yanayohusiana na kuishi na VVU, ghafla niliji-
sikia kutokuwa nyumbani katika nyumba yangu mwenyewe.
Wakati mwingine maumivu na mateso yamekuwa ni makali
kiasi kwamba nimelazimika kuzungumza na mtu yeyote, na
wakati imani ya ujasiri wangu inapokutana na ukimya na chu-
ki mbaya iliyofichika, najisikia kukosa makazi katika nyumba
yangu mwenyewe. Ningejigawa. Kama ningeweza kujigawa ili
kupata sehemu ya mwili wangu yenye afya, inayofanya vizuri,
inayoheshimika, basi ingekuwa ni maumivu kidogo kuiacha
nyumba na kubakia kama ulivyo na ukiwa na maumivu – lakini
usiye na makazi.
Kusikia wanafamilia yangu na washirika wa kanisa wakisema
wamejisikia kudhalilika kwa sababu yangu iliniongezea hali hii
ya kujisikia kutokuwa na makazi.
Kanisa linapowakataa watu wenye VVU kwa namna hii, wa-
natakiwa wawe na imani kubwa au uzoefu mkubwa wa dini
vinginevyo wanaweza kumwacha kumwamini Mungu. Lakini
si matokeo yanayojulikana kwa kanisa.
Kuwa Mtu Mkamilifu
ndani ya Nyumba ya Mungu
Mungu aliumba watu wakamilifu. Roho, nafsi na mwili. Na
kwa hiyo ndani ya nyumba ya Mungu mtu mkamilifu lazima
aangaliwe na pia kumjali. Kwa asili, hii inajumuisha ushauri wa
kichungaji, uongozi wa kiroho, maombi nk. – lakini kwa mtu
mwenye magonjwa yanayonyanyapaliwa kama VVU na UKIM-
WI, haitoshi kujua tu kuwa unaweza kwenda kanisani na mata-
tizo yako ya kiroho.
Kanisa ni lazima litoe taarifa za jumla na zisizo na mwisho
kuwa watu wenye VVU wanakaribishwa. VVU, UKIMWI, kuja-
miiana, unyanyapaa nk, ni lazima kila wakati kuwa kwenye
ajenda za kanisa – siyo tu kuihusianisha na Siku ya UKIMWI
Duniani.
Kwa bahati ninaona makanisa katika sehemu nyingine za du-
nia ambayo yanaishi nje ya maono yao ya Ufalme wa Mungu,
katika ibada zao na jumuia zao. Lakini kukiwa na watu millioni
arobaini duniani wenye VVU hili ni hitaji la muhimu. Katika hali
hii kanisa lazima lijitoe katika fikra zilizozoeleka na kupooza,
kunyanyasa na thiolojia ya matengano na mila iliyozoeleka.
Kama tawi la mwaka wa sherehe wa Agano la Kale – japo hili
linaweza kuwa halijawekwa katika vitendo – kanisa linaweza
kutangaza mwaka wa sherehe, wakati wa sherehe na mahali
pa sherehe.
Itaweza kuleta furaha na uhuru kutoka katika kujihukumu na
aibu – kwa kuonyesha kujali na kukubali watu walio na VVU.
Sherehe itahusisha maombi kwa ajili ya msamaha kwa miaka
mingi ya kuzembea kufanya hivi. Kutakuwa sherehe kwa ajili
ya jamuia ambayo kila mtu huchukuliwa kwa usawa: ambapo
busara, uzoefu na hekima ya watu wenye VVU inathaminiwa
na kutumiwa. Sherehe kwa ajili ya watu ambao wamewekwa
huru kutokana na mateso yaliyowafanya kupooza. Sherehe
kwa sababu tunaweza kuanza kuishi maisha yenye ubora.
Sherehe kwa kuiona heshima ya watu wenye VVU ikikua na
uwezo wao ukionekana kwa faida ya kila mtu.
Ujasiri
Wapi kanisa litapata ujasiri wa kufanya haya yote? Nadhani
inatubidi tuanze kuchunguza hisia zetu – na si hizia zetu za
mapenzi tu. Pia maumivu, huzuni, simanzi na hasira vinaweza
kuwa hali ya mabadiliko ya hali ya akili inayoweza kutuunga-
nisha na watu wengine na jamii zinazotuzunguka. Ni lazima
tuchunguze mahitaji ya watu wenye VVU, tusikilize maoni yao
na tutafute njia na namna ya kuyatatua.
Lazima tuombe kwa ajili ya ushujaa, kumtumaini Mungu na
sisi wenyewe pia, kwa ajili ya imani ambayo roho wa Mungu
atatupa ili kufanya maono ya sherehe ya kumbukumbu iti-
mie: chumba chenye wingi wa matarajio maishani na uhuru
na matumaini, pamoja na kuta zenye upendo, kujali, heshima
na imani.
Kama kazi yote ya kanisa inaweza kwa moyo wa uwazi na
kuaminiana, kama Kaka Roger wa Taizé alivyosema, basi watu
wenye VVU hawataogopa kuliendea kanisa.
UTANGULIZI 9
TumainiTuna tumaini la mbingu mpya na nchi mpya, ambamo amani inaishi, ambapo pumzi ya Mungu ndiyo uzima na hutengeneza up-
inde wa mvua wenye rangi na maumbo tofauti. Tuna tumaini la mbingu na nchi mpya, ambamo upendo unaishi, ambamo roho ya
Yesu Kristo itoayo uzima hukaa ndani ya watu na kati ya watu, ambamo mateso yameteswa, kifo kimekufa na kaburi li wazi kama
lilivyokuwa asubuhi ya Pasaka. Tuna tumaini la mbingu mpya na nchi mpya, ambamo furaha inaishi, ambamo Roho Mtakatifu wa
Mungu anaendelea kuumba upya ibada kwa wanadamu na tumaini lisilozuilika la maisha bila mipaka.
Amen.
Mwili wa UlimwenguLazima nitubu kwa sababu nadhani mara nyingi kanisa ni hodari kujiweka katika upande ambao unaegem-
ea mawazo ya umma – na kwa kufanya hivyo linapuuza wajibu wa asili lililokuwa nao kama taasisi na nguvu
kwa ajili ya mema. Wajibu wa kanisa ulikuwa ni kuwaendea watu na kuonyesha kuwa inawezekana kufikiri
tofauti. Kwamba kulikuwa na njia mbadala namna ya kuwaangalia watu, na mtazamo wa uhai.
Wewe ni Mkristo hasa, uliye na imani ya kutosha na ninajisikia mshirika halali wa kanisa, kama unaishi na
UKIMWI kama ambavyo unaweza kuwa na kansa au kifua kikuu au ugonjwa mwingine wowote. Ninaweza
kuelewa kuwa baadhi ya watu wanajisikia kuwa kanisa haliwakaribishi – na hilo linanitia huzuni, kwa saba-
bu kanisa limepuuza wajibu wake na kukwepa jukumu lake la asili la kuwa mahali pa kukutanika wanyonge
na waliokataliwa na jamii.
Kama kanisa linatakiwa kuwa la watu wote, lazima limjumuishe kila mmoja, hata wale wanaoishi na VVU
– na wanaweza kupatikana katika makundi yote ya jamii. Hakuna anayekwepa. Kanisa la pamoja linaweza
kukusanya kila mtu katika mbawa zake. Hii ni changamoto kubwa kwa kanisa wakati huu, kuonyesha kwa
mapana namna linavyoweza kuwafikia wengi. Kuonyesha kuwa siyo mahali pa kukutana kwa wanaojulika-
na na wanathiolojia. Kwamba ni mahali ambapo watu wanaweza kuja na kupata faraja, nguvu na ongezeko
wanalohitaji kuwawezesha kukua kiakili, kiroho na kimwili. Hii inajumuisha si kwa wagonjwa tu, bali pia
kwa walio karibu nao.
Tatizo la UKIMWI ni la kila mahali kwa watu wote. Hitaji hili la kibinadamu ndilo kanisa linatakiwa kuliti-
miza na hakuna shaka kwamba hamasa ipo kutokana na amri ya Yesu kuhusu upendo. Kuna nafasi kwa ajili
yetu sote ndani ya maneno hayo na haitakiwi kuhukumiana sisi kwa sisi.
USHUHUDA WA JESPER, ALIYEKUFA KWA UKIMWI, DENMARK
UTANGULIZI
10 UTANGULIZI
Kupima na Kuishi kwa Matumaini
NA JOY LUBINGA, MRATIBU WA DUARA ZA MATUMAINI
Siyo rahisi kukabiliana na ukweli kuwa karibuni au baadaye
nitakufa kwa sababu nimeathirika kwa ugonjwa usio na tiba.
Japokuwa siku moja nilikuwa na ujasiri na kwenda kupima na
nikaonekana nimeathiriwa na VVU.
Mimi ni mjane wa miaka 52 ninayeishi na VVU. Nilipima mwaka
2003. Nina watoto watano – wote wa kike- wana umri kati ya mi-
aka 3 hadi 13, na ninamwangalia mpwa wangu ambaye wazazi
wake walikufa kwa UKIMWI.
Mume wangu alichunguzwa na kuonekana ana kifua kikuu
mwaka 1998. Baadaye alionekana kuwa na homa ya uti wa
mgongo inayosababishwa na fangasi, na madaktari waliniambia
alikuwa na UKIMWI na angekufa wakati wowote au kuwa kichaa.
Habari hii ilinifanya nitetemeke sana kwa sababu nilihisi kuwa
ninaweza kuwa na VVU. Siku moja nilipokuwa nimerudi nyum-
bani kutoka kazini, ninakumbuka watoto wangu walivyoniam-
bia kuwa baba yao alikuwa hajaamka kutoka kitandani. Niliingia
na kumuuliza jinsi alivyokuwa akijisikia. Aliangalia pembeni.
Huu ulikuwa mwanzo wa ugonjwa wa muda mrefu, alikwenda
kila mara hospitali mpaka alipokufa tarehe 5 September 1998.
baada ya kuambiwa alikuwa na kifua kikuu, alipoteza tumaini na
alitumia dawa za kifua kikuu kwa muda mfupi. Ninahisi kuwa hii
ndiyo sababu iliyofanya afe mapema.
Tangu hapo maisha yangu yaliendelea kama kawaida. Niliishi
na watoto wangu, na kuwasaidia kwa mahitaji ya msingi ambayo
waliyahitaji kwa ajili ya shule. Haikuwa rahisi. Lakini nilijitahidi
kwa kiasi fulani. Wazo la kupima halikunijia kwa sababu sikuwa
na dalili za ugonjwa wowote.
Kupima na Kuonekana Nimeathirika
Mwaka 2003 kitu fulani kilinitokea nikiwa ofisini mwangu
kilichonisumbua kwa kuwa sikukubaliana nacho. Hii ilikuwa ni
mwanzo wa maumivu yasiyoisha ya kichwa, kukosa hamu ya
kula na kupoteza uzito. Si kuwa na furaha na nilipoteza uzito
ghafla. Nilionekana mbaya kwa sababu nilipata vipele miguuni
na usoni. Sikuweza kuvaa nguo fupi. Mpaka pale afya yangu
ilipoanza kuzorota ndipo nilipokumbuka madaktari walinia-
mbia mume wangu alikuwa na UKIMWI. Hili lilinifanya niende
kupima VVU.
Kuonekana nimeathirika halikuwa jambo la kushtusha kwan-
gu. Lakini lilikuwa ni pigo kubwa kwangu kukabiliana na uk-
weli kwamba sasa nilikuwa ninaishi na VVU. Kitu cha kwanza
nilichofikiria ilikuwa ni kifo, na ukweli kuwa ningeweza kuacha
watoto wangu wakiwa yatima. Wazo hili daima limeniletea hu-
zuni na mtu wa kwanza kumshirikisha habari hizi alikuwa ni
binti yangu mkubwa. Tulilia pamoja na alinipa maneno mengi
ya matumaini na kunitia moyo.
Baada ya hapo nilifanya vipimo vyote vya muhimu. Mwanzoni
kiwango changu cha chembechembe nyeupe za damu (CD4)
kilikuwa 314 ambacho hakikuwa kibaya kutokana na muundo
wa Zambia. Lakini kwa sababu ya wasiwasi mwingi, zilishuka
na kuwa 119 katika muda mfupi – ndani ya mwezi mmoja hivi.
Nilishauriwa kuanza matibabu ya kupunguza makali ya VVU na
kurefusha maisha. Kwa kuwa matibabu haya yalikuwa ghali,
niliamua kumshirikisha hali hii ngumu bosi wangu, Katibu Mkuu
wa Baraza la Makanisa la Zambia. Alinisaidia kupata dawa kupi-
tia ufadhili wa serikali. Kwa hakika nilisaidiwa. Nilipopimwa na
kuonekana na VVU nilikuwa na uzito kwa kilo 51, lakini sasa
nina uzito wa kilo 90. Na chembechembe nyeupe za damu
(CD4) zangu zimeongezeka na kuwa 470. Ninamwona daktari
kila mwezi kwa ajili ya uchunguzi na kujitunza mwenyewe kwa
sababu ninajua hali yangu.
Nimewashirikisha watu wengi hadithi yangu, si kwamba ni-
napenda kuwa na VVU au ninaifurahia hali hii - lakini nimeona ni
muhimu kuwatia nguvu wengine wanaojikuta katika hali kama
iliyonikuta. Nimenyanyapaliwa na kukataliwa katika maisha. La-
kini ninajua kwamba Mungu ananipenda. Ana nafasi ya mwisho
katika maisha yetu na hakika ameahidi kuungana nasi ili kuvunja
unyanyapaa, ukimya na fedheha ya VVU na UKIMWI.
Kuvunja Ukimya na FedhehaZAMBIA
UTANGULIZI 11
NA ACKIM SAKALA, MTENDAJI KATIKA DUARA ZA MATUMAINI, ZAMBIA
Nilianza kuugua mwaka 1998. Nilikuwa na maumivu makali
ya tumbo, madaktari hawakuweza kujua kilichokuwa kikisa-
babisha maumivu. Niliwekwa katika matibabu ya vidonda vya
tumbo japokuwa sikuwa navyo. Kabla ya hapo mwaka 1995 –
nilimpoteza rafiki wa karibu. Alikufa akiwa mwembamba sana
na dalili zote za UKIMWI. Baadaye, mwaka 1996 nilipoteza rafiki
mwingine katika namna hiyo hiyo.
Katikati ya mwaka 2003 nilionyesha dalili zote kama za rafiki
zangu waliokwisha fariki. Ni wakati huo nilipoamua kuchukua
hatua. Kati ya mwaka 1998 na 2002 nilishapoteza uzito kutoka
kilo 70 hadi kilo 41. Nilishapata malaria za mara kwa mara, ku-
toka jasho usiku na vipele – hizi ni baadhi ya dalili.
Upimaji
Ilikuwa ni June 2002 wakati nikiwa mjini nilipoona Kituo Kip-
ya cha Upimaji na Ushauri ambapo kitu fulani kiliingia akilini
mwangu. Niliamua kwenda kupima. Nilipitia katika ushauri,
upimaji na kuonekana nimeathiriwa na VVU.
Nikiwa nashuka ngazi baada ya kupima nilipata kwikwi iliyodu-
mu muda wa siku sita, usiku na mchana. Nilichunguzwa na nika-
onekana nilikuwa na kifua kikuu na nikaanza tiba ya kifua kikuu
kuanzia mwezi June 2002 mpaka Februari 2003. Nilishaongeze-
ka uzito hadi kilo 65. Mtu niliyekuwa nimemweleza hali yangu
baada ya kupima alikuwa ni mke wangu. Baadaye niliwaambia
dada na kaka zangu na rafiki wachache niliowaamini. Tangu ni-
lipopimwa nikawa mgonjwa sana. Mke wangu alizingatia katika
kunihudumia, lakini ninajua kwa hakika alikuwa akiogopa kuam-
bukizwa. Baada ya miezi sita alikwenda kupima VVU. Tangu hapo
amekuwa akienda kupima kila baada ya miezi mitatu. Bahati, kila
mara amekuwa anaonekana kutokuwa na VVU.
Kuishi Kwa Uwazi Kama Familia
Haijawa rahisi kuishi na virusi. Nilizaliwa June 24, 1961, katika
familia ya watoto tisa – wanne wa kiume na watano wa kike.
Baada ya kuoa tulipata watoto watano, watatu wa kike na wawili
wa kiume. Mkubwa kwa sasa ana miaka 16 na mdogo ana mi-
aka 4. Miaka miwili ya kwanza sikuwaambia watoto wangu
chochote, lakini baada ya kupata mazoezi kimatibabu mwaka
2004 niliamua kuwa wazi kuhusu hali yangu. Niliombwa kue-
leza kidogo kuhusu maisha yangu katika kituo cha televish-
eni cha taifa, na kabla ya hapo niliwapeleka binti zangu wawili
wakubwa katika ushauri. Hivi ndivyo hali yangu ilivyowekwa
wazi kwa watoto wangu. Ninaelewa haijawahi kuwa rahisi kwa
binti zangu walio shule za sekondari kuwa na baba aliye na
VVU – kama ambavyo haikuwa rahisi kazini kwangu na katika
jumuiya yangu. Lakini ilinilazimu kukumbana na unyanyapaa
na fedheha na kusaidia kuvunja ukimya kwa kuongea kuhusu
hali yangu kwa uwazi.
Matibabu
Nilianza kupata matibabu ya kurefusha maisha (ART) kwa sa-
babu nilipata kifua kikuu. Baada ya miezi minne niliambukiz-
wa homa ya uti wa mgongo. Miezi sita baadaye, nilipokwenda
kupimwa chembechembe nyeupe za damu (CD4) zilikuwa
chini hadi 270 lakini nilipokwenda kupima miezi sita baadaye
kipimo kilionyesha 324. Hivi karibuni nitakwenda kwa ajili ya
kipimo kingine, na ninatumaini zitakuwa zimeongezeka kwa
kuwa ninajisikia mwenye afya nzuri zaidi kuliko pale mwanzo.
Baada ya kuwa nje ya kazi kwa mwaka mmoja, nimerudi katika
kazi yangu ya ualimu na kama mwamuzi wa mpira wa miguu.
Tabia ya Maisha Yangu Leo
Kwa sasa ninaishi maisha yenye kujali. Ninaamini mimi ni uum-
bwaji wa Mungu na kwamba ninaishi kwa makusudi ya Mungu.
Ninaamini ninaweza kusaidia kuvunja ukimya ndani ya kanisa
na katika jumuiya kwa sababu ya nafasi yangu kama mwalimu
katika jamii.
Ninaweza kuongea kuhusu hali yangu ndani ya kanisa na katika
umma kupitia Duara za Tumaini, mtandao ulioundwa na Ba-
raza la Makanisa la Zambia. Kupitia Duara za Tumaini ninapata
masaada wenye thamani na mahitaji yangu binafsi yanatimiz-
wa. Sote tunajaribu kuvunja unyanyapaa na fedheha na kutiana
moyo kuwa wazi juu ya hali zetu ili kuwasaidia wengine.
Ujasiri wa Kuwa Wazi
Ni mtandao wa kusaidia watu waishio au walioathiriwa na VVU na
UKIMWI. Vikundi vya masaidiano vimeundwa katika jiji lote la Lusaka,
na kazi itatawanywa katika miji mingine ya Zambia pia. Kwa kawaida
vikundi hukutana katika makanisa na mikusanyiko ya kiroho, lakini
pia hata majumbani. Kazi hii ilianzishwa na Baraza la Makanisa la Zam-
bia. Joy Lubina ni mshauri wa saikolojia ya jamii na Ackim Sakala ni
mwalimu. Wote wawili wanajulikana vyema kati umma wa wazambia
kwa sababu wamekuwa na ujasiri wa kuwa wazi kuhusu hali zao. Kupi-
tia mikutano mingi katika mtandao wa kiimani wa makanisa na katika
mahojiano ya televisheni na redio pamoja na magazeti wanawashauri
na kuwatia moyo wengine kuvunja ukimya na unyanyapaa juu ya VVU/
UKIMWI.
Ushuhuda
Duara za Tumaini
12 UTANGULIZI
Katika kuitikia wito juu ya mtazamo wa kithiolojia kuhusu un-
yanyapaa unaohusiana na VVU na UKIMWI, Baraza la Kikristo la
Norway liliwaalika watu waishio na VVU kuhudhuria katika ma-
jadiliano. Waliungana na wafanyakazi kutoka katika makanisa,
seminari na taasisi zingine za Kikristo. Majadiliano yalifanyika
Aksept, katikati ya jiji la Oslo mahali lilipo kanisa la wale walio-
athirika kwa VVU na UKIMWI. Mikutano ya namna hii iliendelea
kwa miezi kadhaa, katika makundi madogo na makubwa. Mita-
zamo ifuatayo inafafanua mtiririko wa maongezi tuliyoshirik-
ishana Oslo na ni jaribio la kushirikishana yale yaliyojitokeza
katika majadiliano yetu. Yanaeleza uzoefu kuhusu unyanyapaa
na uhitaji wa kuelewa nini maana ya kuwa mwanadamu.
Mazingira ya Unyanyapaa
Nchini Norway, watu waishio na VVU wanakumbana na un-
yanyapaa kwa mapana sana. Japokuwa tabia za unyanyapaa
hazionyeshwi kwa maneno, ziko dhahiri kwa wale waishio na
VVU. Mtu mmoja alisema “watu wanakuchukulia tofauti: wa-
nakukwepa na wanakusengenya. Ujumbe hupokelewa vyema
kama vile ambavyo ungesemwa kutoka juu ya mapaa ya ny-
umba.” Hata katika taasisi za afya, “mahali ambapo tunatege-
mea kupata utaalamu na kupokelewa bila upendeleo,” kume-
kuwepo taarifa za mara kwa mara za wagonjwa wenye VVU
wanaoachwa katika foleni au kukataliwa huduma za upasuaji.
Kwa mujibu wa muathirika wa ubaguzi wa aina hii “inatokea,
kwa sababu macho, mioyo na fikra zao zimefungwa!”
Kwa mujibu wa watu waishio na VVU, uzoefu wa unyanya-
paa katika jamii mara nyingi umesababishwa na kujinyanya-
paa, ambako husababisha kufichika kwa hali zao kwa wengine.
Wakati mwingine woga huu wa kukataliwa hauwezi kuthibit-
ishwa na watu wengine wanaweza kuonyesha hisia zisizotara-
jiwa za upendo na kukubalika katika kueleza hali zao kuhusiana
virusi. Hata hivyo kinyume chake ni kweli. Mama mmoja akase-
ma anaogopa kusema na anajisikia hawezi kuwaambia rafiki
zake kuwa mwanae wa kiume ana VVU kwa sababu anaogopa
“kupoteza heshima yake.” Kuna woga wa kujihalalishia kuwa
watoto watanyanyapaliwa, au kwamba mtu atapoteza misaa-
da inayohitajika ya marafiki na familia yake.
Hivyo “ katika hali ya kutoaminika wapo wengi ambao hu-
jitenga, wakikaa nyumbani bila kutoka nje”: hali ya mahusiano
inayoweza kuwa useja wa kujitengenezea, inayoweza kusaba-
bisha kufadhaika na wakati mwingine kujiua.
Mawazo, Uzoefu na Mtazamo Juu ya
Watu Waishio au Walioathirika kwa VVU
Unyanyapaa na UtuNORWAY
Utambulisho na Lawama
Masuala ya utambulisho yanaoneka kuwa na utata hasa yan-
apohusu VVU. Hii kwa sehemu ni kwa sababu ya dalili za la-
wama zinazoambatana nayo. Kama mshiriki mmoja alivyose-
ma. “Ninaposema nina VVU, ninasikia sauti inayosema, ‘kwa
nini unavyo?’ Tofauti na kansa, VVU inaonyesha kuwa ni kitu
ulichojitakia.” Kwa kukumbana na mitazano hii, kuishi na VVU
kunaweza kumfanya mtu akaweka moyoni sura anayoumbiwa
na wengine, na kuigeuza kuwa ni sahihi juu yake mwenyewe.
Hivyo virusi kuwa kielelezo cha utambulisho wa mtu. “Kusema
kuwa mtu ana VVU ni kitu tofauti na kusema mtu anaishi na
VVU au ni VVU halisi, akasema mtu mmoja. “Ndiyo”, mwingine
akakubali: “Hiyo ni tofauti yenye maana sana kwa sababu ‘ni’
inahusika na utambulisho wa jumla wa mtu; ambapo kama
ukisema una virusi, inakuwa kitu tofauti na wewe, kitu ulicho-
nacho na siyo namna ulivyo. Hii ina maana kuwa haifungamani
na utambulisho wako.” “Ina maana kuwa” akasema mwingine,
“Lugha hiyo ni muhimu, pamoja na jinsi tunavyozungumza
kuhusu sisi wenyewe.”
Kutengwa
Kadiri mazungumzo yalivyoendelea, iliendelea kuonekana dha-
hiri kuwa uzoefu wa watu wenye VVU ulitoa mwanga katika mta-
zamo wetu na maana ya kuwa mwanadamu katika jamii yetu.
“Siwezi kumwambia yeyote nina VVU kwa sababu ninaogopa
watanihurumia” alisema mtu mmoja; watahusiana nami ka-
tika njia tofauti; watakuwa waangalifu kile wanachoniambia.”
“Ninajisikia mdogo sana.” Alisema mshiriki mwingine. “Kama
wangeweza kubaini kuwa mimi ni mtu halisi mwenye malengo
na mwenye rasilimali: lakini vyote wanavyoona ni virusi.” Wa-
shiriki walieleza juu ya ukuta wa kutofahamu wanaokumbana
nao kila wakati wanapojaribu kueleza kuwa hata wao ni wana-
damu wenye mahitaji ya kawaida ya kibinadamu. Washiriki wen-
gi walielezea hisia za kudharauliwa na kuhukumiwa.
Hii ni kwa sababu watu wanaangalia zaidi virusi (ambavyo ni
vya kibaolojia) na kutolea sababu zenye utashi (si za kibaiolo-
jia). Si kwamba watu wenye VVU ni watenda dhambi kidogo
kuliko wengine, lakini pia si watenda dhambi wakubwa kuliko
wengine. Uovu na ubaya vinaishi duniani, na sote tuna uovu
na ubaya. Hiki ndicho tulichonacho kimsingi, alisema mshiriki
mmoja. “Lakini tatizo ni kwamba kuna mfano au sura kamili-
fu ambayo watu hudhani ni lazima wafanane nayo,” alisema
UTANGULIZI 13
mshiriki mwingine; ‘ kutwisha mzigo wa ubaya kwa watu fulani
ni njia ya kulinda ‘sura kamilifu’ tunayopenda kuwa nayo juu
yetu wenyewe. Na ndipo sura hizi timilifu na maumbo zinaleta
ugumu kwetu sisi kujiona na kuwaona wengine kama tulivyo:
tunaumba makundi yasiyo sahihi na kupoteza mawasiliano
na maisha yetu wenyewe, kwa mwelekeo wetu wenyewe ku-
fanya yaliyo sahihi na mabaya.’ Kama suluhisho wale wanao-
taka kurejesha maadili katika jamii huanzisha visingizio vya
“kubeba dhambi”, kama ilikuwa; na kama ikitokea tusikatae
ukweli kuhusu jamii, tunakataa kitu cha muhimu kuhusu sisi
wenyewe kama wahusika.”
Mfumo Gonganishi
Makundi haya bandia huumba tofauti kati ya watu. “Lakini
tatizo ni, ‘alisema mshiriki mmoja’, pia yanasababisha tofauti
hata ndani ya watu. Hivyo mmoja anakwepa kujihusisha yeye
mwenyewe na watu wengine kama tulivyo (au walivyo). Am-
bapo mifumo gonganishi hutokea.: mtu anasema kitu hiki, na
mwindine anafanya au kuishi kwa namna tofauti. Jambo am-
balo ni unafiki. Watu wanaliona hili, na ndiyo sababu baadhi ya
watu wanaacha kwenda kanisani. Lakini ‘kuwa mwanadamu’ ina
maanisha ni kujifunza kuwa sisi wenyewe, si kuendana na sura
halisi ambayo hata hivyo ni bandia. Tusilazimishane kuwa kama
sisi wenyewe na tusihukumiane kwa sababu ya kuwa tofauti.”
Hivi ‘kuwa tofauti’ ina maana gani, basi? ‘Tofauti ina maanisha
kutoweka kwa wazi kutoka sura halisi ya kawaida tuliyonayo
wote, katika mazingira yetu ya ndani. Tukihusianisha sura hii
na mwanadamu halisi, hivyo tumeelemea katika kufanya hu-
kumu zisizo sahihi juu ya wale wasioikubali. Na tunajiweka
mbali nao. Lakini fulani ana mapungufu katika ubinadamu
kwa sababu tu ni wa tofauti.” Kuna utofauti mkubwa miongoni
mwetu, kwa namna ile ile kwamba kuna tofauti ndani ya kila
mtu na kila mmoja miongoni mwetu.
Hofu na Kukataa
Upinzani mwingi juu ya nini ni tofauti ni matokeo ya
hofu.”Lakini kila mtu anaogopa kitu fulani,” Alisema mtu
mmoja. “inahusiana na kuishi. Tunaogopa vitu vinavyotishia
maisha yetu. Na tunajitahidi kukiweka kando chochote ki-
nachotishia maisha yetu.” “Lakini woga mwigi unahusiana na
ujinga, na upendeleo,” alisema mwingine. “Sote tuna upen-
deleo na kukata tamaa. Lakini ni lazima nikubaliane na ukweli
huu na nifanye kitu fulani kuhusu hiki, kama kurekebisha mi-
tazamo yangu mibovu au kuchunguza mapendo yangu.”
Kwa uhakika ni kwamba kuhukumiana kwa sababu ya tofauti
zetu ni kukataa ukweli thabiti kuhusu hali za kibinadamu,
ambao ni kuwa sisi sote tu tofauti, lakini kwa namna fulani,
sisi sote ni sawa.
Biblia yenyewe imetumika mara nyingi kuridhia ubaguzi.
“Kwa mfano, ‘Wamebarikiwa walio maskini wa roho’ wakati
fulani imeonekana kama ujumbe unaoonea unaowaambia
maskini au watu wanaoteseka, ‘kwa kuwa unavyoteseka au
ukiwa maskini hapa duniani, basi utakwenda mbinguni utaka-
pokufa.’ Lakini pengine maana yake ni kwamba, kwa sababu
ya mateso yao, upendeleo maalum hutolewa kwa wale walio
katika mazingira magumu, wagonjwa au waliobaguliwa au
- kwa namna yetu – kuishi na VVU au UKIMWI.”Ni kama ma-
cho yao yamefunguliwa na kuona kitu cha muhimu.” ‘Mtu
hulazimishwa kujishughulisha yeye mwenyewe, kunyenyua
mawe mazito yeye mwenyewe, kama yalivyo na kutafuta
kilichojificha chini yake.”
Hivyo Agano Jipya limekuwa ni maandiko ya kinabii
na ukombozi, ikiongelea udhaifu wetu na uwezo wetu,
dhambi zetu na mazuri, kufanana kwetu na tofauti zetu: na
kusisitiza kuwa yote haya ni sehemu ya nini maana ya kuwa
mwanadamu.
UTANGULIZI
14 UTANGULIZI
Mahali Salama kwa MazungumzoUmuhimu wa kuwa na sehemu salama kwa mazungumzo mara
kwa mara umesisitizwa. Mjini Oslo, Aksept, kituo kwa ajili ya
yeyote aliyeathirika kwa VVU, mfululizo wa maongezi ulifanyi-
ka kati ya watu walioambukizwa VVU na walioathirika kwa VVU
na UKIMWI kwa namna moja au nyingine. Wazo na hamasa ya
kufanya aina hii ya mazungumzo ilitokana na mtaala wa ma-
fundisho kuhusu mbinu za Kujifunza Biblia iliyotengenezwa
katika kituo cha Ujamaa kilichopo Piertermartzburg, Afrika
ya Kusini. Mazungumzo yaliendelea kwa miezi kadhaa, katika
makundi madogo na makubwa. Kutokana na uzoefu katika
mazungumzo haya – yote hasi na chanya – tulifikia katika mi-
tazamo ya msingi na mashaka yaliyo muhimu ili kufanya maz-
ungumzo haya kuwezekana. Vipengele hivi vifuatavyo vimeo-
nyeshwa kwa mifano kwenye mikutano yetu Oslo.
1. Kuanza kwa Uzoefu
Katika mazungumzo yetu tulifikia katika uzoefu halisi wa maisha
ya watu waliotengwa na kunyanyapaliwa jinsi yalivyokuwa na
kipaumbele tangu tulipoanza. Lakini mara nyingi, wakati mta-
zamo wetu wa kualika jumuia katika mazungumzo ya aina hii
katika Kanisa na miradi ya kithiolojia, imekuwa ni rahisi kuweka
ajenda za mikutano ambazo hazikidhi uzoefu halisi na mahitaji
ya msingi ya washiriki. Katika kujaribu kulikwepa hili, tuliandaa
mkutano wa kwanza kwa misemo mitatu ya ufunguzi.
I. Unyanyapaa ni dhambi
II. kujamiiana ni kuzuri
III. Kanisa lina UKIMWI
Wanawake wawili wenye UKIMWI walitoa madokezo ya utan-
Baadhi ya Madokezo kwa Vitendo
Uzoefu kutoka kwenye kundi Lililopo Oslo
gulizi na waliulizwa kujibu maswali yafuatayo: “Unadhani ajenda
ya kanisa juu ya UKIMWI ni nini?” na “Nini iwe ajenda ya kanisa
kuhusu UKIMWI?”
2. Kutengeneza Nafasi Salama
Tulipokutana kwa mara ya kwanza, tulichelewa kuanza mku-
tano, ili kuona kama wengi wa wale waliokuwa wamesaini kuja
kama wangekuja. Wengi hawakuonekana. Kulikuwa hali ya
kusita. Tutakuta mtazamo gani kwenye kikundi? Washiriki wen-
gi walikuwa hawajamwambia yeyote kuwa walikuwa na VVU.
Lakini ilikuwa wazi walipojieleza wao wenyewe, waliokuwepo
pale kwa sababu ya kazi zao katika kanisa na waliokuwepo pale
kwa sababu VVU ilikuwa sehemu ya maisha yao wenyewe. Huu
ulikuwa mwanzo usio sawia, ingeweza kutisha kwa baadhi na
ilisisitiza umuhimu wa kuwa na nafasi salama.
3. Mahali
Sehemu ya mkutano wetu haikuwa isiyo eleweka. Majadiliano
yetu daima yalifanyika Aksept. Hili limekuwa ni muhimu katika
kutengeneza mfumo salama kadiri inavyowezekana kwa wale
waliosema juu ya uzoefu wao wenyewe katika kuishi na VVU.
4. Washiriki
Ili kuumba ujasiri mkuu kwa ajili ya kushirikishana uzoefu,
mkutano wa pili ulikuwa wa siri, hasa kwa watu waishio na
VVU. Baadaye tuliruhusu mazungumzo kwa washiriki wengi
zaidi, lakini pia tulikuwa na vikundi vidogo vya mazungumzo
ambapo watu wangelizungumza zaidi juu ya mawazo yao na
UTANGULIZI 15
Mahali Salama kwa Mazungumzouzoefu. Katika Pietermaritzburg zaidi wanafanya kazi katika
vikundi vidogo vya watu waishio katika mazingira magumu,
kwa sababu wamejijengea ujasiri binafsi wa kuongea.
5. Muwezeshaji
Wajibu wa muwezeshaji ni muhimu katika kuweka mazingira:
a) Kusimamia na kupangilia majadiliano
b) Kuhakikisha kuwa kila mtu anayetaka anapewa wasaa wa ku-
shirikisha
c) Kuhakikisha kuwa washiriki wanaruhusiwa kuvunja miiko
6. Kanuni za Msingi
Kanuni zilizo wazi ziliwekwa kwa ajili ya mazungumzo: ni
lazima usikilize, uhusudu na kuonyesha kuheshimu kili-
chosemwa, na siyo kushambulia au kuteketeza yale ambayo
wengine wameyasema. Inaweza kuchukua muda kwako
kutambua nini ni cha muhimu zaidi na kile unachodhani.
Hii hudhaniwa kabla kuwa unajua kuwa utakachosema haki-
takuwa kiini cha kukosoana.
7. Muda
Inachukua muda kutengeneza mahali salama. Na kundi imara
linalokutana mara nyingi daima litatengeneza ujasiri kuliko
kundi ambapo watu huja na kuondoka.
8. Mazingira ya Kukiri
Ya msingi na mara nyingi husahaulika! Lakini mawazo yetu, mi-
tazamo na kushirikishana uzoefu unatakiwa kuthibitishwa na
wengine, tunatakiwa kusikia kuwa yale tunayosema ni sawa au
mazuri au mengine sahihi.
9. Malumbano – Ushiriki Hai
Ukimya unaweza kuwa lugha ya uwezo. Ilitokea mmoja wa
washiriki katika mikutano yetu anayefanya kazi katika kanisa,
aliyekuwa kimya sana alipoulizwa na mmoja wa wanawake
waliokuwa wazi kuhusu maisha yake: “Unafikiri nini?” Jinsi
alivyojibu ilionyesha dhahiri kuwa alishangaa iwapo ukimya
ulikuwa unaficha aina fulani ya ukosoaji.
10. Mifumo ya Utawala
Katika mazingira kama ya VVU na UKIMWI kuna hatari ya kuwa
na ajenda ya siri. Mikutano na majadiliano inaweza isikidhi
matarajio. Uwepo wa mtu mwenye mamlaka katika jamii
au kanisa mara nyingi unaweza kuwafanya watu wengine
kuchukua tahadhali kuhusu yale wanayosema. Je ni salama
kutamka mambo ambayo kanisa mara nyingi linayahukumu
au kulikosoa kanisa kwa nguvu?
11. Kushirikishana
Taratibu, baada ya mikutano kadhaa, ujasiri ulianza kuimarika.
Tofauti miongoni mwetu zilikuwa ndogo na mazungumzo
yetu yakawa kwa undani zaidi. Tulishirikishana mawazo na
maswali, matukio katika maisha yetu, imani, kukata tamaa na
hatari. Kuwa na VVU au kutokuwa na VVU – kimsingi tulikuwa
watu tunaotafuta kitu kizuri kwa ajili ya maisha yetu na maku-
sanyiko yetu.
•KutokakwenyeMalengohadimaandiko
Katika aina hii ya kujifunza Biblia, hatuchagui maandiko yoyote, lakini yale tunayoona muhimu katika utaratibu wa
kushughulika na uzoefu wetu binafsi au masuala yanayohusiana.
•MamlakayaAndiko
Biblia mara nyingine imetumiwa kukandamiza au kuhalalisha ukandamizaji. Ile tu kuwa kitabu cha Kidini, ina
mamlaka kwa watu wengine kiasi kwamba wakati mwingine inawafanya watu kukaa kimya kuhusu maisha yao
binafsi. Hivyo inatakiwa kuelezwa na kutumiwa kwa uangalifu – uangalifu ulio na asili katika Injili yenyewe.
•MwenziwaTatukatikaMazungumzo
Andiko la Biblia linaweza kuwa na kazi ya kuwa mwenzi wa tatu katika mazungumzo wakati mnashirikishana.
Kila mmoja wa washiriki kwenye majadiliano alikuwa na hadithi yake na uzoefu. Ukweli unaweza kuoneka-
na kama upuuzi. Hadithi ya Biblia “kwa sehemu ya tatu” inaweza kuwa hadithi halisi ambayo inaweza kutoa
mwanga katika maisha yetu na kuleta matumaini, au kudhihirisha matumaini ambayo yapo tayari.
Kutengeneza nafasi kwa ajili ya Utaratibu wa Kujifunza Biblia
Watu wengi wamepata uzoefu hasi kwa namna ambavyo Biblia imekuwa ikitumika. Ni
kitabu kilichofungwa kwa baadhi yao. Lakini katika mazingira salama, maandiko ya
Biblia yanaweza kuanzishwa na kuonekana ya maana. Vipengele vya muhimu katika
njia tunazotumia ni:
NORWAY
16 UTANGULIZI
Hatua ya Kwanza Katika Maisha Yetu
Biblia ni kitabu kitakatifu kwa Wakristo wote. Ni muhimu
katika maisha ya binafsi ya Mkristo na katika kuielewa
jamii. Wengi wanaamini kuwa wale waliosoma Biblia wana
aina fulani ya kanuni inayofungua maandiko mbalimbali
na kwamba haijalishi namna wanavyoyaelewa maandiko.
Tunaelewa kuwa ufahamu wa kithiolojia ni muhimu ka-
tika kujifunza Biblia, lakini tunaamini pia kuwa uzoefu
wetu wa kila siku ni muhimu kwa kuelewa ujumbe uliomo
katika maandiko ya Biblia. Wakristo Amerika ya Kusini na
Afrika ya Kusini wametufumbua macho juu ya umuhimu
kwa watu wa kawaida katika kusoma Biblia. Kanuni ya
msingi ya kujifunza biblia ni kuiainisha Biblia na maisha
ya kila siku kwa kila mmoja wetu, kwa ushawishi kuwa
kuna uhusiano kati ya yale Biblia inasema na yale watu
wanakumbana nayo.
Utaratibu unaoelezewa hapa umesimamia katika tara-
tibu zinazotumika katika kituo cha Ujamaa kilichopo Pi-
etermaritzburg, Afrika ya Kusini. Vikundi vya kujifunza
Biblia huko vimepangwa kutokana na tofauti za watu,
pamoja na watu waishio na VVU na UKIMWI. Hawa wana-
jifunza Biblia kwa kufuata uzoefu wa watu wenye VVU.
Kwa njia hii maandiko ya Biblia yanatoa mtazamo mpya
na wa ndani. Tunaamini utaratibu wao wa kujifunza bib-
lia unaweza kutusaidia kuangalia kwa uwazi mahusiano
yaliyomo kati ya maandiko ya biblia na VVU na UKIMWI na
unyanyapaa.
Mafunzo ya Biblia Yanayomhusisha Mtu
Kama kiongozi wa kikundi cha kujifunza Biblia, jukumu lako
zaidi ni kama muwezeshaji na si mwalimu. Washiriki wasiele-
kezwe maana ya andiko. Wafike katika maana ya andiko kuto-
kana na mazingira yao. Baadhi ya watu hudhani wanajua zaidi
ya wengine! Na kuna wengine wasioamini kuwa tafsiri zao
wenyewe zina umuhimu wowote. Kwa mfano: “Wewe ni mc-
hungaji, huwezi kutueleza maana ya andiko hili?” Ni muhimu
kuwa uweke wazi kwa washiriki wote kuwa uzoefu wao ni
muhimu katika kuelewa andiko. Uchunguzi wa maandiko ya
Biblia si njia inayotakiwa kufuatwa kwa ubinafsi. Ni suala la
tabia katika kusoma Biblia. Kadiri unavyozoea na kuridhika
na utaratibu huu wa kujifunza Biblia, unaweza kujiweka huru
kutoka kwenye maswali. Uchunguzi wa maandiko ya biblia un-
aweza kuelezwa kama tabia nne unapojifunza maandiko:
1. Kusoma Biblia katika mtazamo wa mazingira ya wasomaji
wenyewe na changamoto zinazowakabili.
2. Kusoma Biblia pamoja na wengine.
3. Kusoma Biblia kwa ufasaha na kwa undani.
4. Kusoma Biblia ukiwa na wazo la kufanya siku ya kila mtu na
mabadiliko kijamii.
Tabia Nne za Msingi1. Soma Biblia katika
Mazingira ya Msomaji Mwenyewe
Utaratibu unaotumika hapa ni wa jumla na unaweza kutumi-
ka kwa mada yoyote inayokufurahisha. Tunashauri kuanza
majadiliano kwa maswali yanayosaidia kila mtu katika kundi
kushirikisha uzoefu ambao utaweza kukusaidia kuelewa
ujumbe wa maandiko ya biblia. Kuhusu VVU na UKIMWI
kama mada, kuna watu ambao hawajui ni kwa namna gani
ilivyo kuishi na VVU. Japokuwa unaweza ukawa huna VVU
wewe mwenyewe, tunaamini kuwa unao uzoefu ambao un-
aweza kuutumia.
2. Soma Maandiko Mkiwa Pamoja
Baada ya kushirikisha uzoefu unaohusiana na mada, someni
maandiko ya Biblia. Ni muhimu mkisoma kwa pamoja, kwa
sauti. Kusoma kwa pamoja kunakuwezesha kuielewa kama
kikundi.
Ni vyema kuchagua maandiko ambayo yanahusiana kwa
karibu na mada kadiri inavyowezekana. Inawezekana uka-
ona kuwa Biblia haijishughulishi na mwelekeo wa mada
Utaratibu katika
Kujifunza Biblia
Biblia Kitabu KitakatifuNORWAY
UTANGULIZI
UTANGULIZI 17
unayofikiria. Kwa mfano VVU havikuwapo nyakati za Biblia.
Lakini kunyanyapaliwa na kutengwa na kuuliza dhambi ya
nani imesababisha magonjwa ni mambo ambayo yaliku-
wapo.
3. Soma Maandiko
Kwa Umakini Na Kwa Kina
Baada ya kusoma maandiko pamoja, mnaweza kuuliza-
na maswali ambayo yatawasaidia kuingia katika andiko.
Mshiriki mmoja aandike maneno ya msingi katika karatasi
kubwa na kuzibandika katika ukuta. Kwa njia hii kila kitu kili-
chosemwa kitasikika na kuangaliwa kwa umakini.
Kwanza, baadhi ya maswali ya jumla:
• Maandikoyanahusunini?
• Makusudi na malengo yapi yameshughulikiwa katika
maandiko?
• Nini kilikustusha sana kuhusu maandiko haya? Halafu
chunguza maandiko kiundani:
• Naniwanahusikakatikahadithihii?
• Tunajifunzaninikuhusuwahusikakatikahadithihii?
Tumia muda katika maswali haya na ruhusu muda fulani kwa
ajili ya vitu fulani vilivyotajwa ili kuamsha mawazo mapya
kwa wengine. Unaweza kumuuliza mtu kueleza kwa undani
zaidi Kuhusu kile alichosema. Lakini usithubutu kusema si
sahihi. Kila mmoja wetu tunaangalia kwa miwani ambayo
maisha yetu na uzoefu vimetupa.
Wakati mwingine inaweza kusaidia ikiwa washiriki
wataachwa kujadili baadhi ya maswali katika jozi au kuy-
atafakari kila mmoja peke yake kwa kipindi kifupi kabla ya
kushirikisha majibu yao kwa kikundi chote.
Inaweza kuwa na msaada pia kwa kuangalia uhusiano kati
ya mtu katika maandiko, pia kijamii, kisiasa, kidini na kiu-
chumi
• Mahusianoyawatuuliowasomayanahusunini?
• Wanachukulianajewaokwawao?
• Jewanamahusianotimilifu?
Unapokuwa umeelewa yote haya unaweza kujaribu kudha-
ni ni nini mtu katika maandiko anafikiri kuhusu maisha na
kuhusu Mungu. Ikiwa unaangalia katika moja ya vitabu vya
injili. Unaweza pia kuangalia namna Yesu anavyomwelezea
Mungu katika maandiko katika maswali.
• NiniuelewakuhusuMungualionaomtu?
• Nininikiletachotumaininamwangakatikamaandiko?
Baada ya kuwa umeyachunguza maandiko ya Biblia kwa
umakini, ni muhimu
Ukiyageukia maisha yako na hali zako mwenyewe.
• Nani miongoni mwetu ana uzoefu unaoendana au ulio
sawa na mtu aliye katika maandiko?
• Tunahusianajesisikwasisikatikahalizanamnahii?
• Tuhusianevipisisikwasisi?
Unapoongea kuhusu hali za siku za leo, unaweza kukagun-
dua kuwa ni muhimu kurudi katika maandiko na kuangalia
yanasema nini. Hii inasaidia kufungua mazungumzo kati ya
maandiko na hali zetu wenyewe. Unaweza kupata ufafanuzi
katika uzoefu wako wewe mwenyewe ambao ghafla utaku-
saidia kuona mambo mapya katika maandiko na kitu fulani
kipya kuhusu wewe.
4. Soma Maandiko Ukiwa na
Matazamio ya Kubadilika
Usomaji wa Biblia haukomi mpaka pale unapoona kile unachowe-
za kufanya kuleta matumaini katika maandiko katika siku za leo.
• Tunawezakufanyaninikukomeshadhulumaleo?
• Tunawezaje kuboresha maisha kwa wale wasio tendewa
haki?
Wakati mwingine mabadiliko ya muhimu sana ni pale am-
bapo malengo yanaletwa na kujadiliwa. Nyakati nyingine in-
aweza isieleweke nini unachoweza kufanya. Lakini unaweza
kupiga hatua kidogo kuyaboresha maisha ya mtu fulani. Un-
aweza kufanya kitu kutengeneza hali ya uwazi kuhusu kitu
ambacho kimekuwa kigumu kukiongelea, pingana na tabia
zisizofaa, anzisha mradi au anza kuwa na mawasiliano na
watu unaojua wanapambana na maisha yao.
18 UTANGULIZI
Utaratibu wa VitendoZAMBIA
Kujifunza Biblia
Hatua zifuatazo zinaweza kufuatwa katika mifumo tofauti ya ku-
jifunza Biblia. Lakini mambo matatu mara nyingi ni ya muhimu:
1. Maisha ya Kiroho – Kukosekana hili husababisha kukosekana
kwa majadiliano kitaaluma.
2. Kutumia Akili – Kukosekana kwa nidhamu kiakili na kufikiri
kwa kina husababisha “mawazo mazuri” yasiyo na msingi, pia
mitazamo isiyo sawia.
3. Utashi – kukosekana kwa utashi wa kutii kunasababisha ku-
tojifunza kwa vitendo.
1. Soma Maandiko Kwa Uangalifu
Fanya uchunguzi wa awali. Soma kipengele mara kadhaa, iki-
wezekana katika tafsiri tofauti. Andika kila wazo litakalokujia.
Amua aina ya uandishi kama ni shairi, nathari, historia au hoja.
2. Kujifunza kwa Undani
Jaribu kuandika katika sentence moja kusudi la muhimu lili-
lomo katika fungu la maandiko.
3. Kugawanya Maandiko
Tafsiri za kisasa zimewekwa katika aya. Lakini inawezekana
kuzigawanya aya hizi
4. Miunganiko
Maandiko mengi yameunganika. Ni lazima tujaribu kuvumbua
maunganiko kati ya aya. Maneno “sasa basi” na “basi” ni mfano
wa hili: Warumi 6:1 na 8:1.
5. Vielelezo
Tunahitaji vielelezo kutusaidia katika mawazo yaliyofupishwa,
kama mifano ya Yesu na namna alivyotumia maneno kama
mwanga, chumvi nk.
6. Marudio
Mwalimu yeyote mzuri anajua thamani ya marudio. Zingatia
mlinganyo uliomo katika Zaburi: Ushairi katika Biblia ni wa mar-
udio; mwandishi anaeleza ukweli katika njia moja na pia ukweli
huo huo katika mfumo mwingine. Mfano Zaburi 42:1-2
7. Mhusika
Wakati mwingine tabia hutajwa ili kusisitizia pointi. Jaribu
kutafuta zaidi kuhusu mtu huyo. Tofauti inaweza kuonekana
miongoni mwa wahusika, kwa mfano Mafarisayo na watoza
ushuru, Luka 18:9-14.
8. Mtazamo Wetu Kwa Masuala Ya Kisasa
Iwapo tunaiamini Biblia mtazamo wetu utakuwa tofauti ku-
toka kwa ule wa wengine wengi. Kwa mfano hatutashawi-
shika na hali au mazingira. Tutaichukulia biblia kama ni
sahihi katika hali zetu za sasa. Masuala fulani yameshughu-
likiwa kwa uwazi. Matatizo mengine hayajashughulikiwa –
tunatakiwa kuanzisha utaratibu tofauti wa kujifunza juu ya
matatizo haya.
9. Kutafuta Kanuni
Kukuongoza kufikia Majibu
Kama wakristo ni lazima tuambatanishe maisha yetu
kwa Kristo, hivyo tutapata miongozo kwa masuala yenye
utashi kwa asili ya Mungu na kwa lipi Mungu amelidhi-
hirisha kuhusu makusudio yake kwa ajili yetu. Vipengele
vifuatavyo vinaweza kuunda mfumo ambao utatuwezesha
kufikia hitimisho kuhusu matatizo mengi yanaotokea siku
za leo:
Upendo wa Mungu – Kumbukumbu la Torati7:6-8 Warumi 5:6-11
Haki ya Mungu - Kumbukumbu la Torati32:4, Warumi 3:21-26
Utakatifu wa Mungu – Mathayo 5:48
Mungu ni Muumbaji – Mwanzo 1:2, Zaburi 8:5-8
Mungu ni Mtunzaji – Mathayo 6:25-33
Mungu ni Mkombozi – Waefeso 1:7
Mungu ni Hakimu – Mathayo 25:31 – 46
Sisi ni watumishi wa ulimwengu – Mwanzo 1:28-30
Tunategemeana sisi kwa sisi – Mwanzo 4:9-11, Walawi 19:18
10.Jinsi ya Kutumia Kanuni
Kwanza kusanya taarifa nyingi kadiri inavyowezekana
kuhusu tatizo la kushughulikia na amua kanuni ipi
ya biblia inahusika. Soma kwa uangalifu vifungu vya
maandiko vinavyoonekana kuoana. Tengeneza wasaa
kwa mazingira yanayobadilika tangu nyakati za Biblia.
Iwapo kanuni inaonekana yenye kukinzana, kwanza
angalia tafsiri yako. Kama bado kuna mikinzano amua
kanuni ipi ni ya juu. Kumbuka kutofautisha kwa uan-
galifu kati ya mawazo yako mwenyewe na mafundisho
ya Biblia.
UTANGULIZI 19
Kwa maana mwili si kiungo kimoja bali ni vingi.
Mguu ukisema kwa kuwa mimi si mkono, mimi si
wa mwili, je! Si wa mwili kwa sababu hiyo? Na sikio
likisema kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili,
je! Si la mwili kwa sababu hiyo? Kama mwili wote
ukiwa jicho ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio
ku wapi kunusa? Bali Mungu amevitia viungo kila
kimoja katika mwili kama alivyotaka. Lakini kama
vyote vingekuwa kiungo kimoja mwili ungekuwa
wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmo-
ja. Na jicho haliwezi kuuambia mkono , sina haja
na wewe, wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu
sina haja na ninyi. Bali zaidi sana vile viungo vya
mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahita-
jiwa zaidi. Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo
kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima
zaidi, na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uz-
iri zaidi sana. Kwa maana viungo vyetu vilivyo na
uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha
mwili, na kukipa heshima heshima zaidi kile kiungo
kilichopungukiwa, ili kusiwe faraka katika mwili,
bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. Na
kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia na-
cho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote
hufurahi pamoja nacho.
1KORINTHO 12:14-26
Mwili Mmoja
20 KANISA
KANISA 21
au walioathiriwa na VVU na UKIMWI. Kwa nyakati fulani, Sakra-
ment imekataliwa kwa watu waishio na VVU, ibada za mazishi
zimekataliwa kwa watu waliokufa kwa UKIMWI na hatujawafariji
wasio na matumaini. Tunakiri kuwa kanisa limekataa wakati li-
lipotakiwa kukumbatia na kuhukumu lilipotakiwa kuonyesha
upendo, huruma na uangalizi. Tunatubu dhambi hizi. Kwa hiyo
tunajiweka sisi wenyewe katika kukubali kwa uaminifu kuvunja
ukimya, kusema kwa uwazi na kwa ukweli kuhusu kujamihiana
VVU na UKIMWI. AMINA.
6. Kutangaza Msamaha na Neema
K: “Hili ni Agano nitakalo agana nao baada ya siku hizo, asema
Bwana: Nitaweka sheria zangu katika mioyo yao na kuziandika
katika akili zao, sitazikumbuka dhambi zao na matendo yao
maovu milele.” Waebrania 10:16-17.
7. Wimbo wa Kusifu na Shukrani
8. Ombi la Ufunguzi wa Neno la Mungu
K: Mungu baba yetu neno lako ni taa kwa miguu yetu, bila hiyo
tunapotoka. Fungua macho yetu na masikio yetu ili tuweze
kuona na kujua siri zilizofichwa katika neno lako. Baba, tu-
fundishe kupitia neno hili. Katika jina la Yesu Kristo tunaomba.
AMINA.
9. Kusoma Neno
1 Korintho 12:14 – 26
10. Mahubiri
• Huuniwitokwakanisadunianzimakukubalikuwajangala
VVU na UKIMWI ni kama lake;
• Kanisa lisikubali tu kuwa VVU vipo katikati yake, bali litoe
kwa ukamilifu na kukubali kwa uwazi na kuwajali kwa up-
endo walioathirika na kuathiriwa.
11. Maombi Baada ya Mahubiri
12. Wimbo wa Kufunga
13. Baraka
W: Mungu baba mwenye huruma na upendo atukuzwe milele
na milele kupitia Yesu Kristo Bwana wetu. AMINA.
ZAMBIA
Kanisa Lenya HurumaLiturjia
Katika kanisa la “Reformed” nchini Zambia mchungaji mmoja
ambaye ni mratibu wa VVU/UKIMWI, aliunda liturjia hii na kui-
tumia kwa baadhi ya vikundi vya watu waishio na VVU nchini
Zambia.
K = Kiongozi
W = Wote
1. Wito Kwa Ajili ya Kuabudu
K: Bwana apewe sifa! Asifiwe, O watumishi wa Bwana, Lisifiwe
jina la Bwana! Libarikiwe jina la Bwana kuanzia wakati huu na
milele.
Kaka na Dada katika Yesu Kristo: Tumekutanika leo mbele za
Mungu baba yetu mwenye huruma na upendo. Kwa hiyo kwa
mioyo ya unyenyekevu tumwabudu kwa maombi, nyimbo na
sifa. AMINA
2. Nyimbo za Sifa
3. Maombi ya Ufunguzi
W: Mpendwa Mungu, Tunalitukuza na kulisifu jina lako kwa
sababu ya upendo na ulinzi unaotupa kila siku katika maisha
yetu. Asante kwa upendo na ulinzi unaoendelea kutupa hata
leo.
Bwana tumekutanika kudai kupotea kwa asili ya kanisa lako
katika ulimwengu huu ulio katika maumivu kwa sababu ya
janga la VVU na UKIMWI.
Bwana kama kanisa tumekuwa kimya kwa masuala ya VVU na
UKIMWI na kwa kufanya hivyo tumejitenga na huduma yako
na watu wako walioathiriwa na ugonjwa huu. Tunaomba msa-
maha wako.
Bwana tunakuomba kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo
kubadili mafundisho yetu na matendo kwa kaka na dada zetu
walioathirika au kutoathirika kwa VVU. Tupe moyo usiohu-
kumu bali unaopenda na kujali. Katika jina la Yesu tunaomba.
AMINA.
4. Wimbo
5. Toba ya Pamoja
W: Tunakiri na kukubali kuwa sisi kwa namna fulani tu-
mechangia unyanyapaa na ubaguzi na kwamba makanisa yetu
hayajawa salama au mahali pa ukaribisho kwa watu waishio
KANISA
22 KANISA
Agano la Kale linatuambia kuwa watu waliokuwa na ukoma
na kifua kikuu walisahauliwa na kutengwa na jamii ambamo
waliishi (Walawi 13). Jamii kwa ujumla imerithi tabia hii ya ku-
nyanyapaa watu wanaoteswa na magonjwa yanayochukuliwa
kuwa sugu. Lakini Bwana ni ndiye mwangalizi wa majira yote
na sehemu kwa sababu anajua ali za watu wake katika magon-
jwa na afya njema.
Ni kwa sababu hii kanisa lazima lifanye kazi na watu walio-
athiriwa au kuathirika kwa VVU na UKIMWI ili kuwasaidia kuwa
na imani, kwa kuwa ni kwa imani milima huhamishwa, dhoruba
hupoozwa na miujiza kutendeka. Ni muhimu kuwakumbusha
wale wanaoteseka kuwa ni Mungu pekee ndiye anayeweza ku-
kubali hali zote za kibinadamu na kwa kufanya hivyo tutawasa-
dia kuponya hali zao za kiroho. (Waebrania 10:39). Kwa mtaza-
mo huu imani huja kama silaha muhimu, ambayo ni muhimu
na imara katika kuelewa changamoto ya VVU na UKIMWI. Biblia
inatueleza kuwa Ayubu aliteseka sana lakini uvumilivu wake
katika imani ulimfanya kumshinda mwovu.(Ayubu 1:14-21)
Katika maandiko, injili ya Yohana 8:1-11 inaelezea kisa kati
ya Yesu Kristo na mwanamke aliyezini. Ukweli kwamba Yesu
hakuruhusu mwanamke apigwe mawe ni ishara iliyo wazi ya
ulinzi na kuwaangalia watu waliokataliwa na jamii.
Mfano mwingine uliotolewa na Yesu Kristo unapatikana ka-
tika Injili ya Mtakatifu Mathayo 8:1-3. Hapa ni pale Yesu alion-
yesha upendo kwa kumgusa mtu mwenye ukoma, aliyekuwa
ametengwa kufuatana na sheria ya Musa.
Kwa kumgusa mwenye ukoma Yesu Kristo alionyesha up-
endo alionao kwa kila mtu bila ubaguzi na alivunja desturi za
kukataliwa na kubaguliwa kwa wanaoteseka kwa ukoma.
Tukiongelea kithiolojia, katika mfano huu Yesu Kristo ameo-
nyesha kuwa ugonjwa na udhaifu wa kibinadamu hauwakilishi
matakwa ya Mungu.
Katika baru yake kwa Warumi 3:10, Paulo anaonyesha ukweli
dhahiri kwa wakristo wote kwa kueleza, “ hakuna mtu liye safi.
Hata mmoja.” Kwa upande mwingine, Isaya 6:5 pia inaonge-
za, “Maana hata mimi ni mtu nisiye na midomo iliyo safi na
ninaishi kati ya watu wasio safi.” Kwa hiyo tendo la kusafisha
midomo hutokea kama ishara ya shukrani kwa Mungu. Ni kwa
neema yake tunachukuliwa kama wasafi. Hatuna haki ya kuwa-
cheka wengine. Hii ndiyo maana kuwanyooshea vidole watu
wenye VVU na UKIMWI si haki bila kujali namna au sababu ya
kuathirika kwao.
Mfano mwingine wa Yesu Kristo unapatikana katika Injili ya
Marko 10:46-52. Hapa kipofu Batimayo, mwana wa Timayo
aliyekuwa ametengwa na jamii yake katika mji wa Yeriko, baa-
da ya kusikia kuwa Yesu wa Nazareti alikuwa akipita, alianza
Mtazamo Wa Kibiblia:
Ugonjwa, Unyanyapaa Na Wajibu Wa Kanisa
Kuwakumbatia WaliosahaulikaMSUMBIJI
KANISA 23
kupiga kelele: “Yesu mwana wa Daudi Unihurumie!” Bila ku-
jali mwitikio wa wafuasi wa Yesu na umati wa watu uliokuwa
unamfuata, Yesu alisimama na kumwita Batimayo na kufanya
aone tena.
Leo hii, Batimayo anamwakilisha dada au kaka aishiye na VVU
na UKIMWI. Na kanisa na viongozi wake wameitwa kufungua
macho yao, kufikiri na kusikia sauti ya Batimayo, ambaye kati-
ka jamii ya leo ni watu waishio na VVU na UKIMWI, ambao wito
wao kwa matendo ni kwa kanisa na jamii kwa ujumla.
Upendo na huruma vinaonyesha huduma ya Yesu na anaku-
wa wa muhimu juu ya wote wale walioitwa kwa jina lake Kristo.
Kwa hiyo, kama wakristo tumeitwa kupenda na si kuhukumu.
Yesu mwenyewe alitupa mfano kwa namna alivyoonyesha up-
endo na huruma kwa wale waliokuwa wakiteseka nyakati zake.
Kwa yesu, Upendo lazima uonyeshwe katika “pendaneni ninyi
kwa ninyi kama unavyojipenda mwenyewe” na hurumia “ kwa
kusudio na kuteseka na mwingine”.
Ni wajibu wa kanisa kuwa karibu na watu waishio na VVU na
UKIMWI, ili weweze kuuona uso wa Mungu. Kanisa lina wajibu
wa kuwafanya watu waishio na VVU na UKIMWI kuelewa kuwa
Mungu anampenda kila mtu. Ndiyo maana alimtoa mwanaye
Yesu Kristo, ili kwamba wale wanaoamini kupitia yeye wasian-
gamizwe bali wawe na uzima wa milele.
KANISA
Kanisa limeitwa kuwa sauti ya kinabii na taasisi
inayoponya, kama sehemu ya safari ya kupiga
vita unyanyapaa na kubaguliwa. “Café Ecuméni-
co” ni jina lililotolewa kwa mradi unaoleta watu
wenye au walioathiriwa na VVU na UKIMWI, uon-
gozi wa kanisa, mtandao wa wachungaji walio
katika mapambano na VVU na UKIMWI na vyama
vya kijamii. Malengo yake makuu ikiwa ni kuli-
fanya kanisa kuwa wazi na sehemu salama kwa
mitazamo ya kawaida na mijadala juu ya VVU na
UKIMWI.
Mara moja kila mwezi, watu hukutana ku-
jadiliana masuala yanayohusu VVU na janga la
UKIMWI. Wanakutana chini ya mradi wa Kuzuia
na kuondoa VVU na UKIMWI, kwa ubia na Baraza
la Kikristo la Msumbiji, Mtandao wa Wachungaji
katika Kupambana na VVU/UKIMWI katika jiji na
jimbo la Maputo, chama cha watu waishio na VVU
na UKIMWI kilichopo katika eneo liitwalo ‘Caniço
Residential Area’ na World Relief.
Kwa sasa kuna zaidi ya wanachama 140 kati-
ka Chama cha watu waishio na VVU na UKIMWI
pale Polana Caniço Residential Area na kama 30
watumishi wa kanisa wanachama wa Mtandao
wa Wachungaji katika Kupambana na VVU na
UKIMWI. Wanahusika katika nafasi muhimu ka-
tika kuunda mtandao wa masaidiano. Baadhi ya
wachungaji wanatoka katika makanisa ambayo
si wanachama wa Baraza la Kikristo la Msumbiji,
inayoleta changamoto mpya katika “Café Ecu-
ménico’.
Mgahawa wa Kiekumenia
24 KANISA
NA CARINA WØHLK
Katika kipindi cha miaka michache, kusanyiko la watu wa-
chache ambao wanaishi au wameathirika kwa VVU na UKIMWI
limeundwa ndani ya kanisa la Roho Mtakatifu katika jiji la Co-
penhagen, ambako kuna kituo kinachojishughulisha na VVU
na UKIMWI. Uanzishwaji halisi wa kusanyiko ulitokea sambam-
ba na faragha kwa ajili ya watu wenye VVU na UKIMWI mwaka
1999. Kusanyiko limeongezeka haraka na kimya – pamoja na
kusanyiko la kuabudu na kusanyiko lingine maalum liabudulo
usiku.
Juhudi za kuanzisha kusanyiko la wenye VVU zilianzishwa na
watu wenye VVU wenyewe. Walisema wanahitaji kuabudu na
kukusanyika katika mazingira ya Kikristo. Ombi lao linaeleweka
ninapofikiria kuhusu upweke ambao mara nyingi ninauona ku-
husiana na huu ugonjwa hatari na unaounda desturi fulani. Ka-
tika ushauri wangu wa kichungaji, nimekutana na seti mbili za
matatizo yanayohusiana na upweke: hiari na usio wa hiari.
Upweke wa hiari unatokea kwa watu wenye VVU, kutokana
na matatizo mengi ya kijamii na viwewe vinavyohusiana na
ugonjwa walionao, wamechagua kujitenga na jamii. Wanata-
futa maisha yao ya pekeee na jamii zao bila mahusiano yoyote
ili kukwepa kupoteza mengi.
Upweke usio wa hiari ni tatizo la watu wenye VVU ambao wa-
mekataliwa na kutengwa na jamii kwa sababu ya kuwa na VVU.
Wamesukumwa mbali na hawajaribu kutafuta mahusiano na
jamii kwa kuogopa kulaumiwa na kutupwa.
Kuushinda Upweke
Katika Warumi 14:7-8 Paulo anaandika, “Hatuishi kwa ajili
Ushauri wa Kichungaji na Kazi za Kikanisa Miongoni
mwa Watu Waishio na VVU na UKIMWI
yetu wenyewe na hatufi kwa ajili yetu wenyewe. Kama tukiis-
hi, tunaishi kwa ajili ya Bwana na kama tukifa tunakufa kwa
ajili ya Bwana: Kwa hivyo sasa, iwapo tunaishi au kufa, sisi ni
wa Bwana.”
Maneno haya yanaweza kuongelea moja kwa moja juu ya
upweke ambao watu wengi wenye VVU wanauona – kama
ukumbusho kutoka kwenye injili kwamba hatujatengwa,
hata kama wakati fulani inaonekana hivyo.
Kwa jinsi ninavyoona, kanisa lina mchango kiasi fulani ku-
wezesha kuushinda upweke. Katika Ukristo, wanadamu
wote wameumbwa kwa sura ya Mungu na wana thamani in-
ayolingana.Tunaishi kwenye mwili mmoja. Mtiririko huu wa
mawazo una maana kuwa unaunganika na kutegemeana na
wanadamu wengine. Tunategemeana, ili maisha yaendelee.
Lakini kwa hakika kuna tabia, hata katika kanisa kuwa kudha-
ni baadhi ya watu ni bora zaidi kuliko wengine na hii ni tishio
kwa kanisa.
Mwaka mmoja uliopita, baada ya safari yangu Zambia amba-
po nilijionea kwa mara ya kwanza ukubwa wa janga, nilihubiri
katika Kanisa la Roho Mtakatifu. Katika mahubiri yangu nilitu-
mia usemi “kanisa lina UKIMWI” ili kuhamasisha mshikamano
na roho ya uwajibikaji kwa wakristo. Usemi huu ulionekana
ni wa makosa. Wasikilizaji walisikia kitu kimoja tu; kwamba
kanisa linaumwa na kwamba ugonjwa unahusiana na ngono.
Lakini msisitizo wangu ulikuwa na hakika ni kwamba VVU
na UKIMWI unatuhusu sisi sote. Janga la UKIMWI ni changa-
moto kwetu sisi sote. Kama wakristo ni lazima tuhusike na
maumivu ambayo kaka na dada zetu katika kristo wanapitia.
Lazima tuonyeshe huruma na kuwajibika kama tunataku ku-
towesha janga hili.
Kutengeneza Jumuia Mpya Zenye Tumaini
DENMARK
KANISA
KANISA 25
Iwapo tutakuwa pamoja, tunaweza kuuondoa ugonjwa na
chuki miongoni mwetu. Kanisa linatakiwa kujifungua kwa ajili
ya kusanyiko linaloweza kumkumbatia kila mmoja. Na katika
kusanyiko hili tunaweza kusababisha uwezekano wa kuwa
wazi, kama vile tulivyo.
Kuanzisha Mtandao wa Sharika
Kusanyiko la wenye VVU katika Kanisa la Roho Mtakatifu ni
mfano wa mtandao wa kijamii na kiroho kwa ajili ya watu wali-
oathirika kwa VVU na UKIMWI. Kwa kuanzia, mtandao ulikuwa
dhaifu na wa kificho. Huduma mara ya kwanza zilitolewa kwa
watu wenye VVU tu, kwa sababu wanachama wake hawakuta-
ka kujulikana. Kulikuwa hali ya kutengwa, lakini sababu iliku-
wa uzoefu uliokuwepo wa kuhukumiwa na Wakristo wenzao.
Kadiri muda ulivyokwenda, Wakristo wenye VVU wameweza
kuaminiana na kuwa wazi. Wameanza kujisikia huru na kuan-
za kuaminiana na kutegemeana kuhusuana
na wahudumu na kusanyiko lote ndani ya
kanisa.
Leo hii, ibada ni kwa wote walioathiriwa
na VVU/UKIMWI na si kwa wale walioam-
bukizwa tu. Hii ina maana kwamba wale
walioathiriwa, familia zao na marafiki, wa-
fiwa, walioajiliwa kati kazi inayohusiana na
masuala ya UKIMWI nao wanakaribishwa.
Kusanyiko la wenye UKIMWI halijafikia ki-
wango ambacho litaweza kugonga kengele
na kufungua milango wazi, lakini malengo
yamekuwa ni kuchangamana.
Mara nne kwa mwaka, Januari, Aprili, Julai na Oktoba, ibada
kwa wenye VVU huchukua sura ya Sakramenti takatifu ikifu-
atiwa na chakula cha pamoja. Ni muhimu kwamba mikusa-
nyiko hii iwavutie washiriki wengi – kwa kawaida zaidi ya 20.
Wanafanya aina mbili cha kusanyiko – mezani pa Bwana za
katika meza ya chakula.
Washiriki wanapata wasaa wa kuhusiana - na watu wengine
na Mungu. Alama ya muhimu kwa Ukristo, msalaba, unatuo-
nyesha umuhimu wa kutoka nje kwa ajili ya uzima.
Wanadamu wanahitaji msingi ulio imara na mahusiano ya
karibu. Hii inatumika si kwa wale wenye VVU, ambao wame-
poteza sana na mahusiano yaliyovunjika, kukataliwa sana,
ndiyo, pengine hata hisia za kuwa wamekataliwa na Mungu.
Ni matumaini yangu kuwa, kadiri muda unavyoenda, kuta-
kuwa na utashi mwingi kila mahali kuwakumbatia wale wais-
hio na VVU na UKIMWI. Tunahitaji Kusanyiko la Kikristo lililo-
wazi lenyewe.
26 KANISA
Katika mazungumzo Oslo, Noway, yaliyowahusisha watu
waishio au walioathirika kwa VVU, moja ya mambo ya muhimu
ilikuwa kwamba ‘sisi sote ni wabeba mazuri na maovu.’ Tu-
natengeneza makundi yasiyo sahihi na kutosema kweli
kuhusu sisi wenyewe ikiwa tunabebesha mizigo ya uovu watu
wengine. Japokuwa tu watu tofauti kama watu sote ni sehemu
ya mwili mmoja. Hii ni sehemu ya liturjia hii. Maneno ya utan-
gulizi na malalamiko ni nukuu za mazungumzo. Ni vyema ku-
wafanya watu tofauti wengine kusoma maandiko tofauti.
K = Kiongozi
M = Msomaji
W = Wote
1. Utangulizi
K: Unachomfanyia mwingine, unajifanyia mwenyewe na sisi
sote. Katika ufahamu wa ndani, sisi ni mtu mmoja. Mwili
mmoja. Tunapomharibu mtu mmoja, tunaharibu kitu fu-
lani ndani yetu pia na kama madhara kitu fulani katika ubi-
nadamu. Lakini hii haimanishi kuwa sisi wanadamu tunafa-
nana. Kunatofauti kubwa miongoni mwetu, katika njia sawa
kwamba tofauti ipo ndani ya kila mtu kati yetu.
2. Wimbo
3. Malalamiko
Wasomaji wawili kutoka nyuma ya madhabahu:
W: Lini, Ee Bwana Utanisahau milele?
M1: Ni kama vile watu wananikwepa, wananisengenya,
wananichukulia kama vile ni wa tofauti. Wanadhani nime-
haribikiwa. Nimetengwa.
M2: Sithubutu kumweleza mtu ye yote kuwa nina VVU, kwa
sababi sifahamu wengi watalipokeaje.
M1: Nimeumizwa na kuchoshwa kwa maswali mengi! Ni
hitaji la kibinadamu kuwa na mwandani; Nina mahitaji pia,
hamu ya kuwa na watoto, hamu ya kuwa na mume.
M2: Baadhi ya watu wanaona virusi pekee, hawanioni mimi!
M2: Ninaogopa sana kukataliwa au kuvunjwa moyo. Sid-
hubutu kuwa katika mapenzi.
M2: Kwa nini inaonekana kama vule Mungu anakasirika ni-
napojitahidi kufanya vizuri?
M1: Nimemtafuta Mungu anayenipenda, asiyenihukumu
na ambaye anaweza kunisaidia kukubali VVU na kuwa huru
kuokana na mashutumu. Sikumpata kanisani. Umekuwa ni
utafiti wa upweke.
W: Mpaka lini, Ee Bwana? Utanisahau milele?
4. Ukiri wa Pamoja Ulio Sahihi
Soma kutoka upande mmoja wa madhabahu:
M: Tunakiri kwamba sisi ni sehemu ya vyote alivyoumba
Mungu na aliviona kuwa ni “vizuri sana” kwamba sote tu-
nasehemu katika ya vizuri hivyo na ndani yetu uzuri unakaa.
Tunakiri kwamba mtu wentu wa ndani, na miili yetu pia, ma-
hitaji yetu na hamu yetu vyote ni sehemu ya sura ya Mungu
ndani yetu.
Tunakiri kuwa sote tuna thamani na kwamba tuna thamani kwa
sababu sote ni uumbaji wa Mungu, kwa sababu tupo na tunaishi
5. Kimya au Wimbo
6. Uthibitisho wa
Kushiriki Katika Uharibifu
Soma kutoka upande mwingine wa Madhabahu:
M: Tunakiri kushiriki katika kuunda makundi na kutenga baa-
dhi ya watu wakati tunawaingiza wengine.
NORWAY
Kuwa Mwili Mmoja
Liturjia
KANISA
KANISA 27
Tunakiri hisia zetu, kwamba tunaogopa yale yasiyozoeleka
na kwamba tumechangia tabia ya watu kujiona wametengwa,
wamenyamazishwa na kubaguliwa.
Tunakiri kuwa tumejihusisha zaidi na hadhi ya mtu na kuwa
tofauti zaidi kuhusu hali zao za ndani, umuhimu wao na ubi-
nadamu wao wa kawaida.
Tunakiri kuwa kuwa mara nyingine tunaona baadhi ya watu
au vikundi fulani vya watu kuwa ni waovu na kwamba hat-
uoni kuwa sisi ni sehemu ya uovu na wema.
Tunakiri kutotenda haki kuwa wenye nguvu, afya na mata-
jiri kati yetu wanapewa kipaumbele, wanahudumiwa vizuri
na kwa njia hiyo tunapata hata zaidi.
Tuangalia kwa huruma, tusamehe, tusafishe na tufanye wa-
takatifu.
7. Kimya au Wimbo
8. Ukiri kwa Usawa Wetu Kibinadamu
Soma kutokea katikati ya madhabahu
M: Tunakiri kuwa sehemu yetu ya ubinadamu imeumizwa
na kujeruhiwa, i uchi na kudhalilika.
Tunakiri kuwa tu sawa kibinadamu. Ambapo hakuna hata
mmoja aliye juu au chini ya wenzake, hakuna aliye mwema
au mbaya zaidi ya wengine. Tunakiri kuwa sisi ni tofauti,
aina na maumbile tofauti ambayo vyote ni sehemu ya ubi-
nadamu mmoja: kwamba sisi ni sehemu ya mwili mmoja,
kanisa moja – ambako wa mwisho ni wa kwanza na ambako
nguvu ni ya yule aliye mnyonge.
9. Ukiri Kwa Upendo wa Mungu
K. Unapendwa, zaidi ya unavyofahamu – unapendwa, umesa-
mehewa na kukombolewa.
10. Kusoma Maandiko
Luka 13:10-17
11. Ukiri wa Imani
W: Tunaamini katika Mungu aliye Upendo;: aliyetuumba kwa
upendo; anayeteseka tunapoteseka na aliye kazini duniani
kwa ajili ya mema.
Tunaamini katika Mungu ambaye hatumi magonjwa au
mateso mengine kama adhabu kwa dhambi.
Tunaamini katika Yesu Kristo, aliyejichukulia miili na damu
yetu; aliyetuonyesha namna Mungu alivyo; anayewaweka
watu juu ya sheria na kanuni; atusafishaye na kutuweka
huru kufuata njia ya upendo.
Tunaamini kuwa Yesu Kristo hawezi kumilikiwa au kutawa-
liwa na yeyote na kudhibitiwa na sheria na taratibu.
Tunaamini katika Roho Mtakatifu ambaye hatuondoi ka-
tika miili yetu au maisha ya duniani na ambaye hawafanyi
baadhi ya watu waumini wazuri kuliko wengine.
Tunaamini kuwa sote ni sehemu ya kanisa, na kwamba
sote ni jumuia inayong’ara, katika kanisa hili hakuna hata
mmoja ambaye kwa maana amewekwa nje, katika kanisa
hili watu hupata msaada kukubali na kujipenda wenyewe na
kupenda jirani zao.
Tunaamini katika kanisa ambalo halinyanyapai, halibagui,
halitengi au kumhukumu yeyote.
Tuamwamini Mungu. Msaada kwa kutoamini kwetu.
12. Kutafakari Maandiko
Hapa ni baadhi ya miongozo:
Katika Luka 13:10-17 tunakutana uso kwa uso na Mungu
ambaye anapinga mamlaka na kulegeza vifungo vya watu
waliofungwa. Ni Mungu ambaye si tu kwamba yuko kazini
nyakati za kazi kuanzia saa tatu hadi kumi na moja, ie ndani
28 KANISA
ya taratibu fulani, bali ni nguvu ambayo haifungwi au ku-
dhibitiwa. Mungu mwenyewe huvunja taratibu za maandiko
kwa sababu watu na huruma ni muhimu sana kuliko sheria.
Lengo la sheria ni muhimu sana kuliko utii kwa sheria fu-
lani. Asili ya Mungu ni Upendo na makusudi yake kutokana
na maneno yake na matendo ni kulegeza vifungo, kuwai-
nua waliokandamizwa na kuwaweka watu huru; Mungu
anaponya na kuokoa.
Kisa hiki na hadithi zingine kuhusu Yesu zinaweza kuku-
saidia kuondoa mitazamo ya Mungu inayomhusisha na
ukandamizaji, kulipiza visasi na kuadhibu, na badala yake
kuelekeza katika kiini hasa cha injili – Upendo wa Mungu
kwa ajili ya kila mtu.
Ukristo na injili vina umuhimu kiasi kwamba nyakati fulani
zinaonekana kuwa havijatumika ipasavyo. Vinaweza kuwa
vyombo vizuri vyema sana kwa maisha yetu: vinaweza ku-
tuweka huru na kutusafisha katika kila kitu ndani yetu na
mazingira yetu yanayo tukandamiza. Yanaendana na hali
ya kutokuwa mkamilifu kibinadamu, inayoumba hukumu
na fadhaa na ambayo huwashusha watu chini. Vina sisitiza
umuhimu wa kujipenda na kuwapenda majirani.
13. Maombi ya Mwombaji
• Munguwakilamwanadamu,tupeuwezonaujasiriku-
tambua na kukataa kila aina ya unyanyapaa, kutengwa
na kubaguliwa. Tusaidie kupinga upendeleo na tupe
uwezo wa kutambua uwepo wako ndani ya kila mtu.
Ndani ya mioyo yetu tunawaleta kwako wale ambao
tunawafahamu wanapitia hali ya kutengwa.
• Mungu wa Upendo, jifunue kwetu na tusaidie kush-
uhudia kwako kwa ukweli. Tuondoe na vishawishi ku-
tumia vibaya ili kuwaumiza wengine, au kuhudumiwa
badala ya kuhudumia Tusaidia kushirikiana upendo
ulioleta kwetu na kujitahidi kuondoa mitazamo mi-
bovu kuhusu wewe.
• Mungu, chanzo cha maisha na uzima, tusaidie kuic-
hunga miili yetu, maisha yetu na sisi wenyewe. Tupe
ujasiri na nguvu ya kupingana na dharau, ubaguzi
na ukatili kwa wanawake, na kukomesha udhalimu
unaotokea ndani na nje ya ndoa. Daima tusaidie ku-
waangalia watu wenye upungufu kuliko sisi na kuon-
gea kuhusu VVU kwa lungha zinazoonekana kuwa za
heshima, upendo, msamaha na urafiki.
• Mungu wa Utatu, zifanye sehemu zetu za kukutani-
ka mahali pa kujumuika wote, ambapo ujuzi wetu na
thamani ya kila mtu unathaminiwa. Tusaidie kuwa vile
ambavyo ndani yetu tayari tuko: wanachama wa mwili
mmoja. Tusaidie kumwona mtu kabla ya sheria, virusi
na ugonjwa. Tunaomba kwa ajili ya kanisa linaloweza
kufanya maisha kuwa mazuri na yanayowezekana kwa
ajili yetu sote, linaloweza kuwa mkondo wa nguvu
zako za uponyaji humu duniani.
14. Maombi ya Baraka na Kutawanyika
K: Bwana awabariki na kuwatunza.
Bwana awaangazie uso wake na awarehemu; Bwana awasame-
he na kuwapa amani yake.
Mwende kwa amani: kwa ujasiri na furaha; mkielewa kuwa
mnapendwa; daima mkielewa na kila mahali kwamba ninyi ni
mwili wa Kristo.
Mwende kwa amani na mmtumikie Bwana wa uzima.
KANISA 29
Mwanamke Aliyekuwa Apigwe MaweWakati tunatafakari juu ya kuhusishwa kwa kanisa inakuwa
muhimu Pia Kuangalia na kuchunguza sababu za msingi kwa
nini unyanyapaa na kubaguliwa kunachukua nafasi katika jamii
zetu na unajisikiaje ikiwa wewe ndiye unayenyanyapaliwa.
Funzo hili la Biblia pamoja na hadithi ya Zakayo katika Luke
19:2-10, inaweza kutusaidia kufanya hili
1. Soma Andiko Kimtazamo wa Hali
yako na Changamoto Zinazokukabili.
• Unawezakusemakuhusuwakati ambaoulitendewa isivyo
haki?
• Aukuhusuwakatiambaoulilaumiwakwasababuyajambo
ambalo hukutenda?
• Ulitakaninikifanyikaulipoonakuonewa?
2. Soma Andiko Pamoja
Soma hadithi ya mwanamke ambaye ilikuwa apigwe mawe,
Yohana 8:1-11, pamoja. Hili linaweza kuwa andiko lenye nguvu
sana, hasa awaliokandamizwa. Hisia kali zinaweza kuibuka un-
apofanyia kazi andiko hili.
3. Soma Andiko kwa Umakini na kwa Undani
Andika maneno ya muhimu kwenye ubao. Jiulize maswali ya
jumla kuhusu andiko kwanza.
• Andikolinahusunini?
• Ninikimekushtuakuhusuandikohili?
• Nivipiandikohililinahusiananakutendewaisivyohaki?
Halafu angalia kwa undani kwenye andiko:
• Tunamkutananikatikahadithi?
• Tunajifunzaninikuhusuwatukwenyeandiko?
Inaweza kusaidia pia kuangalia mahusiano ya watu katika
andiko, pia katika mtazamo wa kijamii, kisiasa, kidini na kiu-
chumi. Kwa mfano:
• Unadhaniwaandishiwalimtendeajemwanamke?
• UnadhanikwaniniwaandishiwalimletamwanamkekwaYesu?
• Unadhaniwaandishiwalimkamatamwanamkewapiwakati
akifanya uzinzi?
• UnadhaniKwaninihatusikii lolotekuhusumwanaumeali-
yekuwa akifanya naye uzinzi?
• Unadhani kwa nini hakuna amri inayosema mwanaume
apigwe mawe?
• NiniYesuanakifanyaanapokutananawaandishinamwan-
amke?
• Kwaniniwaandishiwanaondokabilakumpigamawemwa
namke?
• NiniYesuanadhihirishakuhusuMungu?
Baada ya kuwa umelichunguza andiko kwa uangalifu, ni
muhimu kuangalia maisha na hali yako mwenyewe.
• Unawezakujionakwenyeandiko?
• Unajionaukiwananani?
• Je,uliwahikupitiahalikamahiyo?
• Naniunadhanianapitiahalikamahiyoleo?
4. Soma Andiko Ukiwa na
Mtazamo wa Kufanya Mabadiliko
Kujifunza Biblia hakumaliziki mpaka unapokuwa umeona kile
unachoweza kufanya kuleta tumaini lililo kwenye andiko ka-
tika siku zetu za leo.
• Tunawezakufanyaninikuwazuiawatuhasawanawake,ka-
tika aina hii ya ukandamizaji?
• Tunawezaje kufanya maisha bora kwa watu wanaopitia
ukandamizaji huu?
NORWAY
Jamii ilikuwa inapanga kumhukumu mwanamke aliyekuwa amekutwa akifanya
mapenzi nje ya ndoa; mwanaume aliyekuwa naye ilikuwa asihukumiwe.
Walimleta kwa mwalimu aliyekuwa mjini wakati huo. Mwalimu hakupinga
mpango wao. Kwa urahisi alisema yeyote asiye na dhambi awe wa kwanza
kurusha jiwe. Mmoja baada ya mwingine, kuanzia mkubwa hadi mdogo,
waliondoka. Kwa hiyo jaribio la kugawa na kutenga lilitenguliwa, siyo kwa
muujiza, lakini kwa ufunuo wa msingi ambao wote tunashiriki. Kwa njia hii
sote ni mwili mmoja.
ANGALIA YOHANA 8:2-11
KANISA
Kujifunza Biblia Kuhusu Unyanyapaa
30 KANISA
NA CARINA WØHLK
Pumziko ama kurudi nyuma kunaweza kuelezewa kama mka-
kati wa kujitoa. Kijeshi neno hili halina maana ya kushindwa.
Inaweza kuonyesha haja ya kusimama na kufikiri juu ya hali
fulani iliyojitokeza.
Kuwa na mapumziko ni desturi ya muda mrefu ndani ya ka-
nisa. Neno pumziko ndani ya kanisa lina maana kuwa ni wakati
na mahali kwa ajili ya ukimya na kutafakari, Pumziko ni wasaa
wa kujitoa ili kupumzika na kukusanya nguvu.
Yesu Kristo mwenyewe anatupa uwezekano wa kuwa na
pumziko. Katika Marko 6:31 Yesu anawaambia wanafunzi
wake, “ Twendeni mahali pasipo na watu tukapumzike”. Yesu
mwenyewe anatafuta wasaa wa kutafakari - hebu fikiria busta-
ni ya Getsemane. Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na
hamu ya kuwa na mapumziko na nguvu na mtazamo ambao
vinaweza kuwapa watu wa dunia ya leo.
Tangu mwaka 1991 nimeshirikiana na rafiki kutoka Chama
cha Kitaifa cha Kilutheri cha UKIMWI katika kuwa na mapum-
ziko kwa ajili ya watu walioathiriwa kwa VVU na UKIMWI – hii
ni kusema kuwa wale walioambukizwa pamoja na ndugu na
jamaa wa wanaoishi na VVU au waliokufa kwa UKIMWI. Ma-
pumziko hufanyika katika kituo cha mapumziko kaika mazin-
gira muafaka.
Changamoto mojawapo inoyohusiana na mapumziko ime-
kuwa ni kutafuta uhusiano sahihi kati ya mazungumzo na
utulivu. Mapumziko ya kwanza yalifanzika katika ukimya, na
tulitumia sauti zetu pale tulipoomba na kuimba. Kwa baadhi
ya washiriki hii iliwasababishia wasiwasi. Mmoja wa washiriki
alijisikia kama vile akili imenyenyuliwa na hakujua namna ya
kuendana na hisia na mawazo ya wasiwasi yaliyomjaa.
Ukimya
Ilikuwa wazi kwangu kuwa watu wengi wenye VVU wanauhu-
sisha ukimya pamoja na kifo. Watu wanaoishi katika mazingira
ya kutengwa na upweke kwa sababu ya hali zao ki-VVU wana-
Kuonyesha Upendo na Uangalizi katika
Mazingira Muafaka Kiroho
hitaji kuongea na si kuwa kimya. Ni muhimu sana kushirikiana
na kukutana na wenye virusi. Kwa kuangalia hali zao wenyewe
kwa wengine, watu wenye VVU wanaweza kujifunza mikakati
mipya ya kuondoa ugonjwa.
Miaka ya hivi karibuni tumetengeneza uwiano kati ya maon-
gezi na ukimya katika njia maalum. Tumehakikisha kuwa tuna-
weza kutumia njia mbili zilizo zoeleka. Ya kwanza ni katika ma-
ongezi na nyingine ni kwa wale wanaohitaji ukimya na ambao
wanahitaji kuangalia zaidi mhitaji yao ya ndani. Kuongezea
kila mshiriki ana njia moja ambayo anaweza kuitumia kutafuta
amani na ukimya.
Tunawapa motisha washiriki kuwa wawe kimya katika kipindi
kuanzia kuanzia ibada ya jioni mpaka wakati wa kifungua ki-
nywa asubuhi inayofuata. Siku ya mwisho kabla ya ibada ya
kufunga tunakula kifungua kinywa kimya, tunawasiliana kwa
tabasamu, kukumbatiana na ishara.
Mbiu ya Pumziko
Mbiu ya mapumziko kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa
“Mwanga katika giza”, “Ujasiri kuishi”, “Wasiwasi au woga”,
“Ukaribu”, “Furaha ndani ya uzima” “Makosa na msamaha”, na
“Ifanyike”. Kila mwaka baada ya pumziko fomu maalumu ya
kutathmini hutumwa na tunawaomba washiriki kupendekeza
mbiu kwa ajili ya mwaka ujao. Kwa njia hii washiriki wenyewe
kwa hamasa wanaijaza na kuamua kuyaweka mambo ya mu-
himu katika form.
Pumziko lina mbiu maalum. Hufanyika mwishoni mwa wiki,
kuanzia ijumaa mchana mpaka jumatatu saa sita mchana.
Vifungu viwili vya maandiko katika Biblia vinavyohusiana na
mbiu ya mwaka huo huchaguliwa. Vifungu hivyo hujadiliwa,
kimoja Jumamosi na kingine Jumapili.
Pumziko hufungwa Jumatatu kwa ibada na sakramenti. Hu-
duma hii hukusanya mawazo na hisia kwa msisitizo na mazun-
gumzo kwa mbiu ya mwaka husika imetekelezwa.
Sakramenti na matumizi ya amani ki-liturjia katika ibada hu-
Pumziko Lenye TumainiDENMARK
KANISA
KANISA 31
sisitiza wajibu wa pumziko la kuumba kusanyiko. Washiriki
wanaweza kwenda njia tofauti wakijua kuwa hawajaachwa pe-
keyao. Mungu yuko pamoja nao – na kuna wengine wanaoshi-
riki uzoefu wao na kuusambaza nchi nzima.
Siku mbili nzima tunazozitumia kwenye pumziko zina vi-
pindi vitatu vya kuabudu katika muundo wake: maombi ya
asubuhi, tafakuri juu ya maandiko ya Musa na kusoma jioni.
Mambo haya matatu ndiyo ya lazima kufanyika kwa kila siku.
Kuwa pamoja katika pumziko, peke yake inatosha. Ni muhimu
kwamba mpango mzima usiwe wa kuchosha. Ni lazima kufikiri
hitaji la washiriki la kupumzika na mlo pamoja na dawa. Kwa
kuongeza ni lazima kuwe wasaa wa maongezi na matembezi.
Ibada yenye Msisimko
Kila mwaka kati ya watu 20 na 30 hushiriki katika pumziko –
Mashoga na wasio mashoga walio na VVU, familia, marafiki na
wale waliopoteza wapendwa wao kwa UKIMWI. Kwa ufupi Ma-
pumziko ni wasaa wa muhimu na ibada yenye msisimko wa
roho kwa wale wenye VVU na familia zao. Fomu nyingi za tath-
mini kwa miaka mingi zimethibitisha umuhimu wa mapum-
ziko, kiroho na kijamii.
Labda faida kubwa ya mapumziko haya ni kwamba zimetia
nguvu uanzishwaji wa jamii zinazomwabudu Mungu kwa ajili
ya watu waishio au walioathirika kwa UKIMWI. Baada ya pum-
ziko la kwanza, wazo lilitolewa la kuwa na huduma kwa washi-
riki. Kwa miaka jamii hii imeongezeka na ina watu 30.
Hamu inayojirudia mwaka baada ya mwaka kwa ajili ya ma-
pumziko na jamii ya wanaoabudu walioathirika kwa VVU na
UKIMWI inasisitiza namna ilivyo muhimu kwa kanisa kuwaku-
bali kundi hili la watu katika ibada zake. Kanisa la kikiristo ni
lazima lifike kwa wanyonge ili kuwavuta katika Upendo.
Sijawahi kudhani kuwa imani ni kuhusu kile una-
chofanya kanisani. Imani ni sehemu ya maisha
yako, maisha yako ya kila siku. Wala sijawahi ku-
fikiri kuwa unaweza kuwasiliana na Mungu kwa
kuomba kabla ya kwenda kulala au kuomba nee-
ma kabla ya kula. Maombi ni wasaa mzuri sana tu-
lionao katika kuwasiliana na Mungu kwa ukaribu,
na inaweza kutumiwa katika hali zote na nyakati
zote – mchana na usiku. Nafikiri inapendeza sana
kuomba kwa pamoja kanisani – kwa mfano kuse-
ma sala ya Bwana- lakini nafikiri ni muhimu kuwa
na mahusiano binafsi na Mungu.
Ninajisikia huzuni ninapoona watu wanaopayu-
ka kwa sauti zao kufanya maombi hapa na pale
au hebu tukae chini na tukunje mikono yetu na
ooh, ni kwa namna gani imani yetu ni kubwa au
sisi ni wakristo safi. Ni muhimu kukumbuka kuji-
tunza kila wakati, katika mazingira yoyote uliyo-
mo, katika maisha yako yote.
Sisemi kuwa maombi ni ya thamani au kwamba
hakuna nguvu ya kutosha kuwa katika uelewa
kuwa mtu fulani anaomba kwa ajili yako na
kwamba upo katika mawazo ya watu kwa nam-
na ya upendo. Nimeona matunda ya hili – lakini
kwa ajili ya mahusiano yako binafsi na Mungu, ni
muhimu usijifariji mwenyewe kuwa ni kitu una-
choweza kufanya unapopiga magoti pembezoni
mwa kitanda chako kabala hujazima taa.
Ni wasaa tulionao kila wakati na ni kitu ninach-
okiona kuwa cha thamani sana na muhimu pale
ninapoimba. Nafikiri ni katika kuimba nimekuwa
na ukaribu zaidi, ukaribu sana na Mungu. Nimejisi-
kia kuwa kuimba imekuwa ni njia yangu ya kuomba
– njia yangu ya kukiri imani yangu. Baadhi ya watu
huiita ushuhuda na wanaruhusiwa kufanya hivyo.
Imani haina kitucha kufanya juu ya ufafanuzi. Ima-
ni hakika ni kitu rahisi na kilicho kimya na kilmelala
pale kama uzi katika maisha yangu.
USHUHUDA WA JASPER, ALIYEKUFA KWA UKIMWI, DENMARK
Wimbo Ulio Kimya
32 UJINSIA WA BINADAMU
UJINSIA WA BINADAMU 33
Utangulizi
Kwa kirahisi tu, ngono ni tofauti ya kimaumbile baina ya wa-
nawake na wanaume. Inahusu ukweli kuwa tunazaliwa wa-
nawake ama wanaume. Kwa upande mwingine, ujinsia unahu-
su hisia za kijinsia, tabia zake na mahusiano yake. Ni uhusuano
baina ya wapenzi wawili ama wale wanaotarajia kuwa wapenzi.
Lakini katika jamii mbalimbali, suala la ujinsia linalolinganishwa
na dhambi limejengeka ndani ya maadili ya kiutamaduni.
Mtazamo wa Kibiblia
-Mwanamke aliyekamatwa akizini
katika hadithi hiyo tunaona jinsi dhambi ya kujamiiana ili-
vyosimikwa katika utamaduni na desturi za Kiebrania. Ma-
farisayo waliitunza sheria ya Musa, yaani torati. Walimleta
mwanamke waliyemkamata akizini ili kumjaribu yesu. Jibu
lake kwa maswali yao liliwapa changamoto kubwa washitaki
wake. Yesu akasema, yeyote kati yenu asiye na dhambi awe
wa kwanza kumtupia jiwe. Alimlinda yule mwanamke. Was-
hitaki wake waliondoka mmoja baada ya mwingine wakiwa
wamevunjika. Yesu akamwagiza yule mwanamke asifanye
dhambi tena naye akasamehewa.
• Jetunafanyajekwawalewanaoshutumiwaleo?
• Jetunawapachangamotoileilewaliopatawenzetu?
• Jetunasameheamabadotunabebamitazamoileile?
Tafakuri
• Tungependakujua kwanini yulemtualiyehusikana tukio
hilo hakuwa na wasi wasi wowote.
• Kwamawazoyetuwenyewedhambininini?
• Jewanawakewanaonekanakuwajibikazaidinadhambiza
kujamiiana kuliko wanaume?
• Je tunatambua kuwa ujinsia wa kibinadamu ni maadili ya
kiutamaduni yanayoamuliwa na desturi
• Je ujinsia ni kipawa toka kwa Mungu ama laana toka kwa
Shetani?
• Ujinsiaunafaidaganikwawanaumenawanawake?
Hitimisho
Hadithi kutoka Yohana 8:3-11 inazungumzia hadhi: “Musa al-
ituamuru tuwapige mawe wanawake wa jinsi hii.” Uanaume
na hali zinazofanana zimeshamiri katika kanisa leo. Dhambi
ya ujinsia imenyanyapaliwa kama DHAMBI ILE. Yesu aliwapa
changamoto wanaume wa Kiebrania katika jibu lililotolewa.
Yesu alifahamu shabaha yao katika kuwabagua wanawake.
Tunamsikia Yesu akisema:
• UjinsianikipawakutokaMungu–Mwanzo1:2728
• Ujinsiaunabebadarakafulani
• Unahitajikuwajibikakikamilifukwawatuwajinsiazote
• Zaidi ya yote unahitaji kupendana (Efe 5:2532; Col.
3:12-13)
Maadili ya kijamii na mafao yake yamejengwa katika mitaza-
mo iliyojengeka kwa wengi katika jamii ambazo kwa upande
mwingine zinaendeleza mifano ya watu kama wababe na
wenye nguvu, na wanawake ama wasichana kuonekana kama
wale wasio na nguvu, na hii inategemea majukumu ya kanisa
kuondosha udhalimu wa kijamii na ubaguzi wa kijinsia.
UJINSIA WA BINADAMU
Ubaba, Jinsia na Yesu
Kujifunza Biblia Juu ya Ujinsia wa Binadamu, Unyanyapaa na VVU
ZAMBIA
Nitatoa mkono wangu na mguu ili kuwa na kikundi cha Mduara wa Matu-
maini. Ninaweza kuwashirikisha watu hawa siri zangu za ndani kabisa na
bado wakanipenda. Nilipougua kwa mara ya kwanza ilikuwa ni kikundi
hiki kilichonipa nguvu ya kuendelea mbele. Katika kundi hilo tulionge-
lea juu ya maisha na pia tulipata mgeni aliyekuja kutufundisha juu ya
lishe, vipengele vya sheria, tiba mbadala na programu nyingi zingine. Ni-
lipomsikia mwezeshaji akielezea hadithi yake jinsi alivyogundua yuna
VVU, nilijiweka katika nafasi yake na kumwelewa. Hii ilinipa nguvu kuta-
mbua kuwa sikuwa peke yangu. Maisha yangu yaliokolewa kutokana na
hili. Ndiyo maana najua ni jinsi gani hili ni muhimu kwa watu wengine.
MJUMBE WA MDUARA WA MATUMAINI KITONGOJI CHA GARDEN
34 UJINSIA WA BINADAMU
Ujinsia - Kipawa na wajibuUtaratibu huu wa ibada uliandaliwa na kutumiwa na Duara
za Matumaini huko Busokolo mjini Lusaka, Zambia. Duara za
matumaini ni vikundi vya misaada kwaajili ya wanoishi na VVU
na UKIMWI.
K: Kiongozi
M: Msomaji
1. Msafara na nyimbo zikiimbwa.
2. Salamu na Ukaribisho wa Wageni
K: Ndugu kaka na dada zangu, tumekusanyika hapa leo kush-
erehekea uzuri wa uumbaji wake Mungu na huu ndio uzuri
wa ujinsia wetu. “Kwa hiyo Mungu aliumba wanadamu kwa
mfano wake.Kwa sura na mfano wake aliwaumba; mwanaume
na mwanamke aliwaumba….Kisha Mungu akaona kila kitu ali-
chokitenda kuwa ni chema.” Kwa hiyo, kwa maombi na sifa fikra
na matendo, tumwabudu Mungu wa milele. Amina
3. Somo la Ufunguzi
I Korintho 7:3-12
4. Wimbo wa Sifa
5. Maombi ya Kufungua
K: Mtakatifu Mungu uliye hai
Ambaye tumetokana na mkono wako wa kiufundi
Tunakushukuru kwa kipawa hiki cha ujinsia,
Tunakushukuru kwa kazi zako kuu,
Utuongoze ili tuweze kuikubali miili yetu
Na kwamba tuweze kuuelezea ujinsia wetu katika njia ya ku-
wajibika zaidi.
Tuongoze kukubali kuwa sisi ni hekalu la Roho Matakifu
Utusamehe tunapoupungukia na kuupunguzia makali uum-
baji wako
Utufundishe ili tusitumie vibaya uwezo wetu wa kuvutia ki-
mapenzi
Utupe ujasiri wa kupinga mifumo yote inayogeuza miili ya bi-
nadamu kwa biashara
Kwa Roho wako, utuwezeshe kufurahia ujinsia wetu
Tunaomba kwa Jina la Yesu Kristo
K: Sasa tuzingatie kwa muda kidogo na kuleta mbele ya mawa-
zo yetu mabaya ambayo tumeyatenda katia eneo la ujinsia.
6. Sala ya Toba
K: Katika nafasi zetu na katika majukumu kama watu binafsi
– baba, mama, walezi wa kiroho, viongozi wa vijana n.k. hatu-
jafikiria na kuyafanya yale yote tunayopaswa kuyafanya kuelezea
uzuri na fumbo la ngono, ujinsia na mahusiano mazuri. Kwa wingi
tumedumu katika mambo hasi yanayohusu ngono na hivyo kuu-
pagaisha ujinsia. Mungu tunaomba msamaha wako.
7. Wimbo
8. Masomo Mwanzo
1:27, 2:24
9. Mwongozo wa Mahubiri
a. Utangulizi
Wakati mamilioni ya watu wanaishi ama wameathiriwa kibin-
afsi na VVU na UKIMWI, ugonjwa huu ni mojawapo ya matatizo
makubwa sana katika zama zetu. Taasisi za kidini kwa ujumla na
makanisa yote kwa pamoja yana nafasi kubwa ya kupambana na
kuenea kwa ugonjwa huu kutoka mtu mmoja kwenda mwing-
ine. Mungu aliumba wanadamu wakiwa na hisia zenye nguvu
za ujinsia ambazo wanadamu wanaweza kuzitumia vizuri ama
vibaya. Hisia hizi zenye nguvu zinaweza kubebwa maishani na
kufanyiwa kazi kwa njia ya kuwajibika. Kazi moja ya kanisa ni ku-
zungumzia juu ya maadili na uwajibikaji na kusaidia kupunguza
mazingira hatarishi kupitia elimu. Ukristo umenyanyapaa ngono
na kuifanya dhambi juu ya dhambi zote na kumbe imani ya Kibib-
ZAMBIA
Utaratibu wa Ibada juu ya Ujinsia
UJINSIA WA BINADAMU
UJINSIA WA BINADAMU 35
lia inaielewa dhambi kuwa ni dhambi.
Tunaposherehekea ujinsia wetu, tunafanya yafuatayo:
• Tunakubali kwamba Mungu aliwaumba wanadamu wote –
waume kwa wake – katika sura ya Mungu, na kwa kufanya hivyo
alitupa kipawa cha kuthaminiwa, kufurahiwa na kuenziwa.
• Kuukubaliujinsiakamasehemumaalumyautambulishowetu
inadumisha ushirikiano baina ya watu na kuleta starehe.
• Tunakumbushwakuwapamojanauwezowakuboreshamap-
enzi na furaha katika uhusiano wa kibinadamu ujinsia un-
awaweka watu wazi baina yao wenyewe na pia mbele ya nguvu
za kijamii
b. Mafunzo yaliyotolewa
• Uumbaji wa wanadamu kama mwanaume na mwanamke
haukuwa wa kubahatisha;
• Kujamiiana katika ndoa ulikusudiwa na Mungu kutoa ma-
funzo ya kisaikolojia, kimwili, kihisia, na ukamilifu wa kijamii
na kiroho, zaidi ya kuzaa na kuongezeka tu.
• Ikiwa familia ya Kikristo haiwezi kutoa majibu kwa vijana
chipukizi, basi itawapoteza hao kwa watu wengine wataka-
oweza. Ikiwa kanisa litakaa kimya, nalo litawapoteza pia.
Ujinsia wa mwanadamu kwa hakika ni kipawa toka Mungu amabacho Kina-
paswa kufurahiwa na wapenzi wawili. Kipawa cha ujinsia kinaendelea ku-
wepo ndani tya watu wanaosihi na VVU na kinatakiwa kutumika na si kukan-
damiza. Ujinsia ni uumbaji wa ajabu wa Mungu, na unapaswa kufurahiwa na
wote wanaoshi na VVU na wale wasio navyo.
DUARA ZENYE A MATUMAINI
Ujinsia wa kibinadamu
10. Maombi
• OmbakwambaMunguatupehekimakufundishakuhusu
kile kilicho sawa na salama juu ya ngono, matendo ya ku-
jamiiana, na mahusiano kwa kuzingatia VVU na UKIMWI
• Kuwaombeawanawakenawatotowaliodhalilishwa
• Kutoa shukrani kwa ajili ya uongozi wa Mungu, ulin-
zi, na nia kwamba tuishi maisha yenye maendeleo na
manufaa.
11. Matoleo - Huku nyimbo ikiimbwa
12. Sala ya kuombea Matoleo
13. Baraka ya Kufunga
K: Bwana Mungu wa amani mwenyewe awatakase ninyi nyote
kikamilifu; na roho zenu nafsi na mwili zihifadhiwe bila lawa-
ma hata kuja kwake Bwana Yesu Kristo. Neema ya Bwana wetu
Yesu Kristo iwe pamoja nanyi Amina.
14. Wimbo wa Kutawanyika
36 UJINSIA WA BINADAMU
Nani Anayediriki Kurusha Jiwe la Kwanza?
Kutoka kujifunza Biblia Yoh 8:2-11
Kila mwaka ibada katika Siku ya UKIMWI duniani ndani ya Kanisa
Kuu la Kilutheri mjini Oslo Norway, hutayarishwa huko Aksept -
Kituo cha Kimisheni cha Kanisa Jijini Oslo kwa wote wale ambao
wameathiriwa na VVU. Mwaka 2002 mahubiri yaliandaliwa kwa
kushirikiana na wateja wa Aksept. Ifuatayo ni taarifa ya mchaka-
to na mahubiri yaliyotolewa katika ibada hiyo.
Unyanyapaa, ubaguzi, na ujinsia
Mchakato ulianza kwa wasaa wa kubungua bongo kutafuta
masomo na maandiko ambao ulionekana kuwa wa kufaa uli-
fanyika kwa wakati muafaka na ulioenda sambamba na wale
walioshiriki mijadala husika. Kumbukumbu toka katika mikutano
hiyo iliweka msingi wa kuandika mahubiri hayo. Shabaha ilikuwa
kuendesha mazungumzo baina ya wanadamu na Mungu - ma-
hubiri yanayosikiliza, yanayoelewa, yanayofariji na yanayoleta
changa moto. Mbinu iliyotumika inaweza kuwa msaada kwa ku-
pata mfano wa mahubiri na hata kuwa mahubiri yenyewe. Zaidi,
inatupatia undani wa kufikiri na hata kufanya mazungumzo kati
ya wale walioathirika kwa VVU, mchungaji na kifungu cha Biblia.
1. Kubungua bongo kwa mara ya kwanza:
Watu wanaoishi na VVU walioko Aksept walipata fursa ya kuku-
tana mara mbili kwa kazi ya kikundi na kusema kitu juu ya kile
wanachodhani kuwa ni muhimu kuelezea katika siku ya UKI
WI Duniani mwaka huu. Asubuhi ya kwanza ilikuwa pamoja na
“mjadala wa mwanzo juu ya maadili, dini, na falsafa kituoni.
Hizi ni baadhi ya kumbukumbu zilizonakiliwa daftarini
Matakwa na fikra juu ya ibada
• ujinsiaungekuwasomokuumwakahuu
• kanisalimehamishwambalisananaukwelilinapozungum-
zia ngono
• hatamsimamowetukuhusuujinsianimgumukuutekeleza
• ingelikuwasahihikuendeshaibadayamsetoyamadhehebu
yote ya kidini katika siku kama hii! VVU na UKIMWI umetu-
athiri sote.
Tunataka kusema nini kwa Mungu, Mahubiri yanaweza kuwa
kama mazungumzo kati ya Mungu na wanadamu
• hitajiladawayakuukomeshaUKIMWI
• kukubalikazaidikutokawatuwengi.NilazimaMunguafun-
gue macho ya watu
• hajayakupatamtuwakumpenda.WalewenyeVVUwanahi-
taji kupata nafasi ya kupenda.
• mzigomoyonikwawatotowanaozaliwanaVVU
• Kwaninimimi?nivigumukuikubalihadhiyamtu;kugha-
sighasi mtu humkasirisha!
• haja ya kumsaidia mhusika kurejea mahala pa kazi. Watu
bado wanakutana na ubaguzi
Wale wanaoishi na VVU hawaundi kikundi cha watu wenye
NORWAY
UJINSIA WA BINADAMU 37
ya UKIMWI Duniani yanaweza kufuata mwelekeo kwamba wale
wote wanaoishi na VVU si waaminifu kwa wake ama waume
zao. Hii yenyewe ni mtazamo wenye kunyanyapaa.
4. Mahusiano yanayowezekana
Kwa upande mwingine, kifungu kinachokoza vyama vingi. Ka-
tika mkutano wa pili, majuma mawili yaliyofuata, tafakuri ili-
fanywa kwa kifungu toka Yohana 8:2-11.
Mwanamke huyu alikuwa tayari amekwisha hukumiwa na
wale watu waliomleta kwa Yesu. Hao Mafarisayo na Waandi-
shi walikuwa na hatia gani? Je waliiona akisi yao wenyewe
ndani ya mwanamke yule? Lazima tujikague wenyewe kabla
ya kuhukumu wengine.
Waandishi na Mafarisayo walionyesha mtazamo hafifu kue-
lekea wanawake. Je mwanamke yule anajua nini kinachoende-
lea? Mwanaume naye, Je yuko wapi? Inawezekana hakufanya
kitu chochote kabisa. Alikuwa ni mwathirika tu katika jamii ili-
yomilikiwa na wanaume. Je mwanamke huyo alikuwa na VVU?
Je alikuwa ameshitakiwa kwa kumuambukiza mtu? je mwana-
mke alijiamulia mwenyewe kujihusisha na shughuli iliyokuwa
imetengwa kwa ajili ya wanaume? Je alikuwa akifanya biashara
ya ngono? Ama alikuwa mwanamke aliyempenda mwanaume
na akawa mwathirika wa ndoa ya nguvu. Kuna kila uwezekano
hapa. Kifungu hakituelezi chochote kuhusu mwanamke yule.
Naye hasemi chochote cha kujitetea.
Tunajifunza zaidi kuhusu wanaume waliompeleka kwa Yesu.
Walitaka kumtega mtego Yesu, ama kwa kumlazimisha aifuate
sheria na kanuni au kuthibitisha kuwa alikwisha jitenga na ka-
nuni, sheria na desturi za Kiyahudi. Wanathiolojia na watauwa
waliifahamu sheria, walikuwa mafundi katika hiyo. Kulingana
na sheria, mwanamke yule alipaswa kupigwa mawe! Nao wali-
kuwa tayari kufanya hivyo. Je walikuwa wamemwelewa vibaya
Yesu wakidhani kuwa yu upande wao?
Lakini wanaume hawa walikuwa na nini katika dhamiri zao?
Kwa nini walikuwa na hamaki sana? Je walikuwa kinyume na
wanawake walioendesha maisha yao wenyewe ya kujamii-
ana? Je walikuwa ni wandume waliokuwa wamefadhaishwa
na mambo? Je walikuwa wametimiza matendo mangapi ya
udhalilishaji wa ujinsia? Hatuelezwi chochote lakini tunaweza
kutumia dhana zetu....
Kifungu hiki kinaangaliwa kwa kuhusiana na VVU na kinan-
yanyapaa jinsi kilivyo: VVU havihitaji kuzungumziwa pamoja
na kutokuwa mwaminifu. Zaidi ya hayo ngono si pekee inay-
asilia moja ama kabila moja. wanawake na wanaume, vijana
kwa wazee, wenyeji wa Norway na wageni, mashoga na wasio
mashoga, n.k.
Katika Siku ya UKIMWI Duniani dhamira mbili kuu zilijitokeza:
). Unyanyapaa/ ubaguzi na
2.Ujinsia. Katika mkutano wa kwanza tulifanya kazi kutafuta
kifungu cha Biblia kitakachokuwa msingi wa kutafakari juu
ya maudhui haya mawili. Hivyo ilipendele zwa kufanya rejea
kwa Wasamaria - Wasamaria walikuwa kundi lililonyanyapaliwa
na kubaguliwa wakati wa Yesu. Lakini kuna rejea chache zina-
zohusika na ujinsia katika kifungu kile. Wimbo wa Sulemani
pia ulitajwa, lakini hautaji chochote juu ya unyanyapaaji. Ha-
timaye tuliishia na hadithi juu ya mwanamke aliyepatikana na
zinaa.
2. Yoh 8:2-11 Inasomwa
3. Mwanamke aliyepatikana na Zinaa
Hatukuwa tumeridhika na kifungu hiki pia, kwa sababu kiliun-
ganisha ujinsia na utendaji dhambi. Kifungu hicho pia kingewe-
za kuonekana kama kinanyanyapaa; kwa nini ni mwanamke
tu peke yake aliyekamatwa katika tendo hilo? Nini kilimtokea
mwanaume yule (lazima tudhanie kuwa kuna mwanaume ali-
yehusika)? Pia, mashirika na vyama katika siku kama hii, Siku
UJINSIA WA BINADAMU
Unyanyapaa awali ya yole, ni mfumo wa kulin-
da. Inaunganishwa na fikra kuwa kuna kitu am-
bacho hakipo sawasawa kinachotutisha. Mara
nyingi; kitu ambacho hatukijui ama cha kigeni.
Hofu yetu yaweza kuwa na sababu kamili ama
yaweza kuwa haina msingi wowote. Hata hivyo,
tumejitungia mawazo na mifano juu ya vile tu-
navyoviamini kuwa ni hatari. Haya ni mawazo
ambayo huenda hatuyaelewi vilivyo, kwani un-
yanyapaa hujenga mizizi yake katika fahamu
zetu zizlizolala –katika mitazamo na mawazo
tulio nayo, lakini tusiyoyazungumzia na hata
kuyakubalia. Ili tuweze kuhakiki sura hizi, tu-
nahitaji utashi na ujasiri wa kujaribu misima-
mo yetu dhidi ya ukweli, na kuzifanyia tathmini
ukizipima na mtazamo wetu juu ya ubinadamu
tunaodai kuwa nao. Lakini huu unaweza kuwa
mchakato wenye shida nyingi hivyo fursa zina-
zojitokeza zinahitaji kuimarishwa kwa maku-
sudi kabisa na nafasi salama zikipatikana
KUTOKA TAFAKURI ZA KITHIOLOJIA MJINI OSLO
38 UJINSIA WA BINADAMU
ngono. Wengi wanatazamia kukutana na mtazamo wa jinsi hii
hata katika sekta ya huduma ya afya. wapo wengi walio na VVU
ambao hawatadiriki kufanya ngono na wengine kwa sababu ya
kuogopa kuwaambukiza wengine, pia wanafikiri hawafai tena na
hakuna atakayetaka kufanya ngono na yule ambaye ana VVU.
Wengi wameeleza juu ya matukio yanayofanana kiasi fulani
na lile la mwanamke katika kifungu cha Biblia. Wengine wameji-
weka wazi kwenye vyombo vya habari kwa kuwa walijiachia we-
nyewe na kufanya ngono na mtu fulani, lakini tofauti na hadithi
hii leo watu wapo tayari kuliko kawaida kutupa mawe, hasa kwa
kuwatwika majukumu makubwa watu wanaoishi na VVU zaidi
ya wale wasio navyo. Je mawe haya hufananaje?
“Umepata kile unachokistahili.” “Usinikaribie!” Umeleta aibu
katika ukoo wako!” hii ni baadhi ya ya jinsi mawe hayo ‘yalivyo’,
na yanauma zaidi ya mawe halisi.
Sababu kubwa ya kuwanyanyapaa watu wanaoishi na VVU ni
kuwa VVU vimeunganishwa na mambo mengi ambayo yame-
kwisha kuhukumiwa kuwa ni dhambi katika utamaduni wetu:
ujinsia, ukahaba, matumizi ya madawa ya kulevya, ushoga,
uasherati, na kadhalika.
Watu wametupa mawe katika mazingira ya jinsi hiyo kwa karne
nyingi, ijapokuwa kuna hadithi kama ile ya Yohana Sura ya 8.
6. Wanadamu kama Viumbe wenye Ujinsia
Je tufanye nini ili tuondokane na hawa wenye uchu wa kuy-
atupa mawe yao? Tunawapata hao ndani yetu wenyewe, ikiwa
tutazichunguza nafsi zetu.
Huenda inasaidia kuzungumzia ujinsia katika njia iliyo wazi na
ya moja kwa moja kama inavyowezekana si tu kwa jinsi inavy-
opaswa kuwa ama jinsi gani mtu anavyotaka kuwa.
Ujinsia si kile kitu alicho nacho mtu: ni vile mtu alivyo. Ujinsia
ni jambo kubwa na gumu ikiwa pamoja na VVU ama bila VVU.
Ni vigumu mtu kuishi katika viwango vyake vya kimaadili. Ujinsi
unajumuisha yote mafanikio na mapungufu. Ni jambo la kimb-
ingu na pia linafadhaisha. Linaweza likawa na utata nje ama
ndani ya ndoa. Hakuna furaha itakayokuwa bora zaidi, hakuna
itakayokuwa wazi zaidi.
Ni vigumu kuzungumzia juu ya ujinsia wa mtu binafsi, yote
hasa kuhusu nyakati za furaha na zile nyakati ambazo mtu an-
gependa zisitokee. Inauma sana kujisaliti mwenyewe, kwa sa-
babu wapo watu wamesimama mstarini tayari kutupa mawe.
Wengi ambao wana VVU wanapitia ukweli kwamba virusi vy-
UJINSIA WA BINADAMU
oleta maambukizi ama kueneza ugonjwa. Lakini kila kitu ki-
nachohusika na ngono tayari kina hatia. Dhambi kwa hakika
inakuwa dhana potovu katika mantiki hii kwa sababu ngono
yenyewe si dhambi. Lakini ngono inapata ugumu tunapoingi-
za VVU. Ngono ilikuwa na ugumu hata kabla ya VVU watu wen-
gine wameacha kufanya ngono baada ya kupata VVU. Mwana-
mke katika kifungu hicho alihukumiwa na jamii yake yote, na
sisi pia tunahukumiwa na jamii yetu nzima. Mtu ameondolewa
haki yake ya kuishi kwa kuwa tu ana VVU. Watu wanasema
“wamepata kile walichokistahili”: “Ni hukumu ya Mungu”, bado
unasikia wachungaji na mashehe wakizungumza namna hiyo.
Mmoja katika kikundi alisikia kisa cha mwanamke aliyeuawa
kwa sababu ya uzushi usio na kweli!
Dhambi ni nini? Ni kwa jinsi gani tutauhudumia “Ujinsia ulio
mzuri”. Ni vibaya wakati wengine wanapoelezea na kuamua
dhambi ni kitu gani. Inapaswa kuwa jukumu la mtu binafsi,
kwa sababu kile ambacho wengine wanaamini kuwa si sawa
chaweza kuwa sawa kwa mwingine. Je vipi kuhusu wale am-
bao bado hawajaolewa? Lakini kutokuwa mwaminifu ni dham-
bi; kwani daima mtu mmoja huumia mwishoni.
Je ina maana gani kutupa mawe leo? Ni matendo ya huku-
mu, kujiweka juu ya wengine na kuwatenga wengine. Nchi 183
hazitoi vibali vya kuingia nchini kwa watu wenye VVU. Lakini
tumewahukumu pia wale waliotuambukiza? Je tumewatolea
taarifa? Ama sivyo? Ngono ni tukio ambalo wahusika wote
wawili wanawajibika wakati uhusiano ni wenye usawa. Itaku-
waje ikiwa utakamatwa katika hali ya kufanya ngono, na labda
ukimwambukiza mwingine na VVU “Kama ningejua nimem-
wambukiza mwingine nimpendaye - ningeweza kuimudu hali
hiyo.”
Je mwanamke alipokea jibu? Je amesaidiwa? Hata nami si-
kuhukumu! Haya ni maneno yenye maana sana. “Nenda na
usifanye dhambi tena.” Je hiyo ina maana hakuna ngono tena?
Ama ina maana: “Ondoka hapa na uishi maisha ya ‘kawaida’
kuanzia sasa? Ondoka na ujitunze mwenyewe; epuka ubaya,
usiruhusu mtu akudhuru tena.”
Je ni kipi kinacholeta mabadiliko katika mitazamo? Ufahamu,
ujuzi wa mtu binafsi:”Ingeweza kuwa mimi.”
5. Ubaguzi
Kuna mambo mengi ambayo tunaweza kuyatambua. Watu we-
nye VVU mara nyingi wanakutana na mtazamo huu: usifanye
UJINSIA WA BINADAMU 39
enyewe vimekuwa ni ishara ya usafi katika ujinsia; inafunua
dhana kwamba mtu husika hakuishi maisha yaliyonyooka.
Kana kwamba kila mtu huishi maisha hayo.
7. Unyanyapaa na Ubaguzi
Ni jambo la kuzingatia kwamba Kanisa ambalo limerithi ha-
dithi hii ya mwanamke aliyepatikana na kosa la zinaa halijawe-
za kuwaelimisha waumini wake na kubadili utamaduni wake
wa kuhukumu, angalau kuupunguza kidogo. Badala yake,
tunayo historia ya kanisa ambapo watupa mawe wamepewa
uhuru wa kufanya mambo yao watakavyo. Wakati umefika
ambapo tabia hii ya unyanyapaaji na ubaguzi itambulike kwa
jinsi ilivyo, yaani kama dhambi kinyume cha Mungu na injili.
Kama ujinsia ni zaidi ya kuzaa tu - na ndivyo ilivyo - basi lazima
uwe kitu ambacho kila mmoja ana haki nacho, si kwa wateule
wachache tu - bila kusahau umuhimu wa kuwajibika. Hapa
pawe mahala pa kuanzia kwa mazungumzo yote juu ya jinsi
tunavyoweza kuishi pamoja kama viumbe wenye ujinsia. Na
tutakaposhirikisha kila mmoja katika hili ndipo tutakapoweza
kuondoa mipaka ile ya ubaguzi tuliyojiwekea. Na inaenda bila
kusema kuwa hii lazima ijumuishe watu ambao wanaishi na
VVU.
Unyanyapaa upo wazi. Watu wanaoishi na VVU wamekata-
liwa vibali vya kuingia nchini katika nchi 183 za dunia, mad-
aktari wa meno wamekataa kuwatibu, marafiki wao wame-
wasuta hata wafanyakazi wenzao mahala pa kazi. Yote haya
yanajengeka na kuwa mitazamo kinyume cha ujinsia ambayo
yanalingana na kutupiwa mawe.
8. ”Hata mimi sikuhukumu!”
Hii ndiyo injili: “Hata mimi sikuhukumu.” Baada ya kulibaini
hili: kwamba hakuna mtu aliye bora kuliko wengine inapokuja
katika maisha ya ujinsia, nini hatua ya baadaye? Sisi tutaishije
pamoja katika katika maisha yetu ya ujinsia? Tutawezaje ku-
zuia kuumizana? Tutawezaje kumheshimu kila mmoja? Tut-
awezaje kuvumilia fumbuzi zingine, na kadhalika?
Yesu alimwambia yule mwanamke hatimaye kuwa - “usitende
dhambi tena.” - hii haina maana kufanya ngono siku zijazo.
Zaidi ni suala la kujiangalia mwenyewe kwa siku zijazo. Hii ni
changamoto! Hatutaukwepa mjadala juu ya haki na kile kisicho
haki. Lakini tunaepushwa na unafiki ambao watu wengine ni
bora kuliko wengine katika eneo hilo.
Je ina maana gani kuwa binadamu? Kuwa
na VVU ama kutokuwa navyo, maisha
yote na maisha ya kila mmoja ni maisha
yaliyo hatarini, kila maisha ni maisha
yaliyowazi. Ndani ya tofauti zote, kila
mtu yu tupu na katika maana halisi ya
neno, amejeruhiwa.
Tunakumbushwa juu ya hili kila mara.
Hata hivyo, tunajaribu kulikataa, na
kuliweka mbali, tunajaribu kujishawi-
shi wenyewe na wengine kwamba tuko
salama, wazima na sisi si wa kufa.
Ushirika wa kweli unawezekana tu pale
watu wanapokuja pamoja na kutambua
kuwa kila maisha yao binafsi yapo wazi
kwa jambo lolote - si kama ufahamu tu
lakini kama taarifa ya uwazi unaom-
kabili mtu yeyote kuweza kukutana na
jambo lolote yumkini hata kupata maje-
raha.
Kisha ipo nafasi ya kukutana baina
yetu, tupo katika ngazi moja na hivyo
tunaweza kuzungumza.
KUTOKA TAFAKURI ZA KITHIOLOJIA MJINI OSLO
40 UJINSIA WA BINADAMU
NA ELIZABETH KNOX-SEITH
Katika utamaduni wa magharibi, kifo huonekana kama tukio
la kushindwa – na kuwa mgonjwa, yaani kuwa katika hatari ya
kufa, kunakuwa kulingana na ufahamu wa ndani namna moja
isiyo ya kupendeza sana ya adhabu. Kwa kuwa tumejaribu sana
kutokomeza kifo kama sehemu mojawapo ya mzunguko wetu
wa maisha, hivyo kuwa mgonjwa, ambayo ni kama kuwa katika
mchakato wa kufa kunakuwa tishio katika utu wetu wa ndani.
Ni lazima tusife: chochote na kitokee sisi ni lazima tuishi –
milele ama kwa muda mrefu tunaoweza. Hili lenyewe hugeuza
ugonjwa kuwa tukio la kushindwa.
Ili tuweze kuelezea kuwa kifo ni sehemu asilia ya mzunguko
wa maisha yetu mara nyingi tumetafuta sababu binafsi za mtu
kuwa mgonjwa. Tunasema, ni mtu mwenyewe ndiye aliyeko-
sea, aliyeshindwa kimaadili. Mtu huyu amefuata tabia ambayo
ni sahihi na haki kama ataugua. Ugonjwa na kifo una maana nzi-
to sana katika utu wetu wa ndani kwani vyote vinaashiria kuwa
hatuna haki ya kuishi. Pale mateso yanapotufikia, yanatuambia
japo si moja kwa moja kuwa tumepoteza maana yetu kama wa-
nadamu, yaani haki yetu ya kuishi.
Kwa njia moja, namna hii ya kufikiri inafanya vitu kuwa rahisi
kwa wote wanaoishi na wote wenye afya. Wale wanaoumwa wa-
naweza, ikiwa tu watabadili mtindo wao wa kuishi na kuachilia
wanayoyaita kuwa ni “makosa”, matumaini ya kupata tena haki
yao ya kuishi na hivyo kupona kutoka ugonjwa walio nao – na
wale walio na afya njema wanaweza wakati ule ule kwa ushindi
kutangaza kuwa wale wanaoishi maisha yenye haki na sahihi
nao watapewa haki ya kuishi milele
Lakini ugonjwa kama UKIMWI unaumbua udhaifu ambao kila
mwanadamu na kila jamii hata ile iliyo duni kabisa inaupitia
wanapokaribiwa na ukweli kama vile kifo. Katika maudhui ya
kukata tamaa UKIMWI huchipua swali, kwa nini mimi? Kwa nini
mimi nifikiwe na haya? Kwa nini mimi nipoteze maisha? UKIMWI
umeweka wazi kuwa kifo kinaweza kuingia katika umri wowote
na kwamba tiba ya kisasa haithibitishi ongezeko la maisha ya
milele. Na kama swali halinihusu mimi, linaweza kumhusu kaka
yangu, dada yangu, rafiki yangu wa kike, rafiki yangu wa kiume,
mwanangu ama dada yangu, baba yangu ama mama yangu.
Ikiwa mtu fulani aliye karibu yetu akaangukia eneo la hatari basi
swali hilo huwa halisikiki tena katikati ya maumivu tulio nayo
Kweli zilizopo katika
sura nzima ya UKIMWI
Maana, Kifo na Upotevu
KUJAMIIANA
DENMARK
UJINSIA WA BINADAMU 41
– uwezekano wa kumpoteza huyo “fulani” unakuwa ndiyo kig-
ezo kitakachotawala juhudi za dhati za kutafuta maana halisi ya
mambo hayo yote.
Kuambiwa Ukweli
Taarifa ya kuambiwa kwamba una VVU huleta mshutuko kwa
karibu kila mtu kwani ni kama pigo kubwa ambalo hubadili
maisha yao kabisa. Kila mmoja ambaye amekwisha pima
VVU na UKMIWI anajua jinamizi ambalo mtu hupitia, hasa
pale mtu anaposubiri majibu yake. Hata mtu angejaribu ku-
jiandaa namna gani kupokea majibu hayo imekuwa vigumu
kujiandaa. Hata kwa wale wanaofikiri kwamba hatari ya kua-
mbukizwa ni ndogo kusubiri ni zoezi ambalo wangependa
kutokuwa nalo. Haishauriwi pia kuchukua vipimo ikiwa hauna
mtandao wenye nguvu unaokuzunguka. Kukabiliwa na hatari
ya kupata maambukizi ya VVU ni kukabiliwa na maswali ya
msingi mengine bado kufikiriwa, na kama utaachwa peke
yako ukiwa na matarajio mbalimbali na mashaka mengi ya-
nayohusika inaweza kukuletea madhara binafsi.
Shauku ya kuhukumu ni sehemu maarufu ya mfumo wa ki-
hisia kuhusu VVU na UKIMWI, yote kwa wote walioambukizwa
na kwa familia zao. Je majirani wasema nini ikiwa watagundua
ya kwamba mwanangu….? Je mama na baba yangu watase-
ma nini, ikiwa watafahamu kuwa nime….? Daima nimekuwa
binti mzuri …..Je watafikiri nini sasa….?
Picha zinacheza mbele ya macho ya akili zetu mara tu ma-
zungumzo yanapogeukia VVU na UKIWMI – na swali litaka-
oulizwa ambalo daima haliulizwi kwa sauti ni, Je ameam-
bukizwa namna gani?
Ngono bado ni eneo ambalo limezungukwa na fumbo, ma-
tarajio na hofu - na hakuna mipaka katika mawazo ambayo
hufufuliwa na hoja kama hii hasa pale mtu anapogundua
kuwa mtu aliye karibu nao ameambukizwa.
Maswali ya hatia siku zote hubakia nyuma tu – na hivyo
ni muhimu kumkamata ngombe dume katika pembe zake
na kusema hilo haliwezekani kutofautisha baina ya “hatia”
na “wahanga wa VVU’ wasio na hatia. Wote wamo katika
mtumbwi ule ule, bila kujali wameambukizwaje. Kwamba
mtu anaweza kuwa na uzoefu binafsi wa hatia na fedheha
unaohitaji kushughulikiwa, ni jambo lingine – lakini uzoefu
huo unaweza kuwa na ugumu pia, tena bila kuzingatia vi-
rusi vilipatikanaje. Mama atakayeruhusu mtoto wake apewe
damu kabla damu hiyo haijapimwa, anaweza kuwa na mzigo
mkubwa sana kuubeba wa hatia – na ni lazima asaidiwe kwa
namna ile ile ambayo yule aliyeambukizwa na mpenzi wake
wa kiume angehitaji kusaidiwa ili kushughulikia hasira anay-
oweza kuwa nayo dhidi ya mpenzi wake na nafsi yake. Ma-
tukio ya kujisikia hatia na kuona aibu mara nyingi ni matokeo
ya kutoikubali hasira. Huyo ni ngombe dume mwingine
anayepaswa kukamatwa pembe, na hiyo inahitaji juhudi za
kutosha –lakini huwa ni amani sana pale ngombe dume huyo
anapokuwa ameondoshwa njiani. Mafahali wanaweza kuon-
gozwa kwa kuzikamata pembe zao kwa wakati muafaka,
lakini hiyo ina maana ya kuwepo mapambano daima. Kama
wataruhusiwa kubaki hasara itakayopatikana itakuwa sawa
na ile katika duka la vyombo vya udongo.
Shauku kwamba watu wote wana uzoefu kutokana na
kuogopa yasiyojulikana, kifo na njia ile ambayo ugonjwa
husika utafuata, mara nyingi kwa muda mrefu. Kwa mtu
aliye na VVU, kisichojulikana hujulikana, ama kitajulikana
hatua moja baada ya nyingine na muda ukiendelea. Kwa ka-
waida wale ambao wapo karibu ya watu wenye VVU hujikuta
wakiwa na shauku kubwa kuliko hata wahanga wenyewe,
hasa kwa sababu wao wenyewe hawaupitii mchakato huo
na wanaweza kudhania tu jinsi gani yalivyo mateso hayo.
Hofu ya kitu gani kitatokea ni kubwa zaidi kuliko hofu aliyo
nayo mtu wakati jambo limekwisha tokea na linaendelea ku-
wepo – na kwamba watu wengi wanaoishi na VVU wanaweza
kusema sambamba kuwa ni nafuu wanapozifikia awamu
za ugonjwa waliougopa hapo awali. Hii haina maana kuwa
shauku inapotea- daima kuna kitu kipya kinachoweza kuto-
kea: awamu mpya za ugonjwa unaoambaa katika upeo wa
maisha halisi huku ukileta tishio japo kwa mbali.
Kuishi na VVU na UKIMWI ni tendo jepesi la kuweka uwiano
baina ya uwezo wa kuachilia mambo na uwezo wa kudhibiti
– si tu katika ujinsia bali katika maisha pia. Hili ni tendo la ku-
jenga uwiano ambalo linaboresha ufahamu wa mtu wa nini
maana ya kuwa binadamu.
Uzoefu wa upendo, kukubalika na msaada baina ya vikundi vya huduma
ambapo upendo wa Mungu hudhihirika inaweza kuwa nguvu kubwa ya
uponyaji. Uponyaji unalelewa pale makanisa yanaposhiriki maisha ya kila
siku mahali ambapo watu hujisikia salama kusimulia habari na shuhuda
zao. Kupitia ibada za kweli, makanisa husaidia watu kuingia eneo la upon-
yaji la Mungu. Makanisa yana huduma muhimu sana katika kuhimiza ma-
jadiliano na changanuo za habari, kusaidia kutambua matatizo na kuunga
mkono ushiriki kuelekea mabadiliko yenye maendeleo katika jumuia.
JAPHET NDHLOVU
´
42 SURA ZA MUNGU
SURA ZA MUNGU 43
Kuwa sehemu ya matumaini ya
Kiulimwengu katikati ya mateso
Hii ilikuja yenyewe tu. Nilijitenga mwenyewe katika nyumba
moja mikoani na nikaanza kipindi kirefu cha maombi. Nilitaka
kuomba - na maisha katika utu wangu wa ndani yakaanza,
kama inavyokuwa unapoanza kuomba. Huu ni ulimwengu
wa ndani ambao unaendelea kujifungua wenyewe na kuleta
hali ya ushirikiano. Nilishi katika hali yangu ya hofu ya kufa na
kupata maambukizi ya UKIMWI na pole pole nikaanza kugund-
ua kuwa haikuwa sababu yangu kupata ugonjwa huo. Haikuwa
sababu kwamba nilistahili adhabu. Nimeupata ugonjwa huu
kwa sababu zingine kabisa.
Hivyo nilipata nguvu mpya ya kisaikolojia na nafasi ya kuto-
sha pia. Niligundua kuwa nimeendelea kuwa na furaha zaidi?
Maombi yaliwezesha furaha ipatikane na niliweza kukusanya
nyenzo mbalimbali na nguvu ambazo ningetumia kwa muda
uliobaki.ilikuwa kama chemichemi ya furaha ilikuwa ikitiririka
ndani yangu. Sasa nilikuwa nimekutana na kitu kingine na kama
Mkristo ningeweza kusema kikawaida kabisa kuwa nimekutana
na Yesu Kristo ama Mtakatifu. Mungu alinigusa, aliugusa moyo
wangu, ….na aliufungua moyo wangu,ili kwamba niweze kusi-
kia furaha ya msingi katika kuwa hai, furaha ya kuwa mwanad-
amu na kuishi na wanadamu wengine. Hofu yangu ilipungua,
na sasa ikiwa nitakufa ama nitaugua kukawa na maana kidogo
sana. Hakunisumbua tena. Cha maana zaidi kikawa hali iliyopo
kwa sasa kwani nilikuwa nimekutana na ulimwengu wa ndani
uliokuwa umejaa na vingi sana, na hii ikanipa nguvu zaidi na
uwezo wa kuishi, kiasi kwamba mipango yangu kwa ajili ya
siku zijazo ikaanza tena kuwa na maana.
Imani yangu ya ndani kabisa ni kuwa, watu wote wana-
oteseka, watahusika na kubeba maumivu ya ulimwengu wote
– mateso ambayo Kristo aliyapitia, hasa alipoona dhambi zote
ulimwenguni katika historia yote – zote mara moja. Imani
yangu ni kuwa kila mwanadamu anayeteseka hushiriki katika
kubeba mateso haya ya pamoja, ambayo wanadamu wote wa-
nashirikiana. Kwangu mimi, hii ina maana kwamba katika sabu-
ri niliyo nayo na ugonjwa wangu ninashiriki katika mateso haya
ya kiulimwengu. Hivyo kwa njia moja ninayashiriki mateso ya
Kristo, hii inanipa nguvu na furaha kubwa.
USHUHUDA WA BJARNE, ALIYEKUFA KWA UKIMWI
ImaniNimekuwa muumini kwa muda mrefu kadiri ninavyokumbuka,
lakini kama vile ilivyo kwa watu wengi imani yangu imepitia awa-
mu mbalimbali na migogoro mbalimbali.
Kwa muda mrefu kabla sijaambukizwa na VVU, nilipitia kipindi
kizima cha kuchanganyikiwa kuhusu dini, na sikuwa na uzoefu
mwingi wa maisha ya kihisia. Baada ya kugundua kuwa nina VVU
kidogo ama zaidi nimerejea tena kule nilikoanzia. Nimewahi
kuwa na mashaka na mtazamo wangu wote juu ya Kristo, mta-
zamo wangu kama fikra niliyonayo. Lakini katika kipindi hicho
cha migogoro ya kimaisha ndipo nilipogundua ya kuwa nilikuwa
nina VVU. Tangu hapo nimerejea kwa namna fulani katika imani
niliyokuwa nayo wakati wa utoto. Ninakumbuka matukio kadhaa
nikingali mtoto, moja ni uhusiano wenye kina pamoja na Yesu.
Uhusiano wa jinsi hiyo umenipatia nguvu –na ni chanzo cha mai-
sha mapya ya kupumzika katika imani yangu.
Baada ya kugundua kuwa nina VVU, nilipitia vipindi kadhaa vya
mitafaruku ya kihisia. Mawazo juu ya dhambi na hatia moyoni,
kama inavyotokea kwa wengi wetu – kujisikia kwamba mimi ndiye
niliyeusababisha ugonjwa huu. Kisha fedheha iliyofuata baadaye
kama matokeo ya hali hiyo. Nilipambana na hali hiyo kwa mwaka
mmoja na vita hiyo ilinifanya nijione mtu wa kuogofya sana.
Nilikuwa nimejilaumu sana mwenyewe. Nilikuwa na hak-
imu ndani yangu, ambaye daima aliniambia nimejisababshia
mwenyewe ugonjwa ule. Kwa mwaka wote ule nilizidi kujisikia
fedheha, mwenye hatia na mwenye dhambi. Ingawa niliende-
lea, kupambana na hali zote hizo. Nilikosa baraka ya ushirika wa
Kikristo ambao ungenisaidia kushinda hatia, fedheha na dhambi
moyoni mwangu. Ina sumbua sana pindi unapogundua vema ya
kwamba una VVU kwani unaanza kupata dalili ndogo ndogo hapa
na pale, na hiyo hukuvunja pole pole.
Nilimaliza mapambano yangu ndani ya mwaka mmoja kwa
juhudi zangu mwenyewe. Yote kwa sababu nilikosa na mtu wa
kunisaidia kufanya hivyo.
Maombi
Maombi yamenisaidia katika vipndi vyote vya shida yangu.
Nilipogundua ya kuwa nina VVU, mchakato ulianza, na katika
hatua fulani niligundua kuwa yanipasa nianze kuomba tena.
SURA ZA MUNGU
DENMARK
44 SURA ZA MUNGU
NA JAPHET NDHLOVU
Matukio ya Kibiblia juu ya uponyaji alioufanya Yesu inajumuisha
maelezo ya kutosha juu ya watu walioponywa, na jinsi walivy-
oupokea uponyaji huo. Mwanamke yule asiyekuwa safi na
mwenye hali duni, mwenye ukoma aliyedhalilishwa na kudhi-
hakiwa, mtu yule aliyepooza na kutengwa, omba omba asi-
yeona – hawa wote walikutana na kukumbatiwa na upendo wa
ajabu toka kwa Mungu. Mara tu baada ya kujisikia kupendwa
na kukubalika, hali hii huwa tishio kwa wenye nguvu waliopo,
desturi, na watu ambao wamewapuuza, kuwakataa, na hata
kuwakandamiza.
Baada ya mahubiri ya Petro kwa watu zaidi ya wakati wa
Pentekoste mlemavu mmoja mwenye umri wa miaka 40 ali-
yelala langoni mwa Hekalu aliponywa. Naye Petro akatangaza
kuwa nguvu ya Yesu ya ufufuo ambayo ilifanya kazi kurejesha
mambo yote, ilimponya yule mlemavu na kwamba huyu Yesu
alipaswa kuabudiwa kama Bwana juu ya wote. Watawala we-
nye hofu wakawakamata Petro na Yohana. Walielewa kwamba
uponyaji huu si jambo jema la kawaida tu lililotendeka, bali
changamoto dhidi ya mamlaka yao, na wito mpya wa utii na
shambulio kwa mfumo uliopo.
Uzito aliokuwa nao Yesu alipokabiliana na magonjwa una-
tolewa kielelezo katika kisa cha uponyaji wa mtu aliyekuwa na
mkono uliolemaa (Mk 3:1-6). Uponyaji huu unapata umuhimu
katika siku ya Sabato, kwani katika fikra ya Kiebrania kutom-
ponya mtu yule kungemwacha katika hali inayokaribia kufa.
Mapambano dhidi ya ugonjwa ni mapambano ya kuwaokoa
wale ambao wameumizwa na nguvu ya mauti na hatari zake.
Kwa kuwa ugonjwa unapingamana na nguvu ya muumba ya
kuokoa, lazima urekebishwe na uumbaji kurejeshwa. Yesu ni
mkombozi ambaye rehema za Mungu zinapatikana. Kilicho
kipya katika huduma yake ni kwamba wenye kunufaika na hu-
ruma za Mungu si viongozi wa kidini na wasomi wa sheria lakini
ni wale wanaochukuliwa kama walio nje, masikini, walemavu,
wagonjwa, na wale waliofiwa. Yesu alijiweka huru kufikiwa na
kila mmoja aliyemhitaji, akipuuza mipaka iliyozoeleka na hivyo
kuwatambua rasmi wale waliotupwa na ulimwengu kwa saba-
bu moja hadi nyingine. Kwa utaratibu wa kudumu alikutana na
watu katika maeneo yao ya kuhitaji na kuyashughulikia mahi-
taji hayo. Yesu anaelezwa kama mpiganaji, ambaye mara kwa
mara kwa nguvu alizo nazo anapingana na mamlaka yale am-
bayo yamewaweka watu katika hali ya unyonge. Chochote kile
kilichowafunga watu lazima kikabiliwe na nguvu inayowezesha
hayo kuharibiwa. Kwa jinsi hiyo wagonjwa waliponywa, wale-
mavu wakapewa nguvu mpya ya utendaji na walionyanyaswa
kufunguliwa.
Wakati yesu alipowakaribisha wagonjwa na walemavu kwa
mikono meupe aliwasilisha mfano wenye nguvu kwa wafuasi
wake. Namna ambayo makanisa na washirika wake wanakabili-
ana na changamoto ya VVU na UKIMWI ni kielelezo cha kiwango
cha umakini walio nao katika kumfuata Yesu. Itikio lenye up-
endo na huruma - la mikono iliofunguliwa- linatakiwa toka
kwa watu wa Mungu. Ni daraka ambalo Yesu Kristo alilitoa, kwa
mfano maelezo juu ya Hukumu katika Matt 25:31-46. Zaidi,
itikio kama hilo ni ishara ya neema na upendo wa Mungu, si
katika maudhui ya UKIMWI tu bali kwa jumuia yote kwa ujumla.
Inatangaza kwa ajili ya wote kusikia na kuona kwamba utawala
wa Mungu unaanza kutambulika na kuanza kupata sura yake
duniani.
Kuwakubali katika upendo wale wanaoishi na VVU inatangaza
kuwa nguvu ya Mungu ya kuokoa inachukua hatamu dhidi ya
mauti na nguvu yake ya kuharibu. Huruma kwa hakika ndiyo
wito wa awali walio nao watu wa Mungu katika janga lililosaba-
bishwa na wimbi la VVU na UKIMWI.
Ni ufahamu gani wa undani ambao imani ya Kikristo inatupa-
tia katika hatua hii ya ukomavu wa kuwepo kwa UKIMWI. Baa-
dhi ya maandiko ya Agano Jipya yanaashiria kile tunachoamini
kuwa lazima kijumuishwe katika harakati kamilifu za Kikristo za
kupinga ukimya, fedheha, na unyanyapaa kwani haya yote ya-
nahusishwa na maambukizi ya VVU na UKIMWI, hatua ambayo
ni muhimu leo kama ilivyokuwa mara tu baada ya UKIMWI ku-
tambuliwa.
Matendo ya Uponyaji ya Yesu
tafakuri ya BibliaZAMBIA
SURA ZA MUNGU 45
Labda, hakuna ugonjwa ambao ulikuwa wa kutisha sana ka-
tika Palestina ya karne ya kwanza kama vile ukoma. Ukoma ulie-
nea polepole hadi kuufanya mwili uchukize na hivyo kunyang-
anywa umahiri wake. Kupata maambukizi hayo kulimaanisha
kutengwa ili kutogusana na mtu yeyote asiye na ukoma; ukoma
si tu haukuwa na tiba bali pia ulikuwa ni hatari.
Alipokutana na mwenye ukoma katika barabara kuu ya Gal-
ilaya, Yesu angeliweza kutamka neno la uponyaji kutokea
mbali, kama alivyofanya katika matukio mengine (k.m.Luka
7:1). Lakini Yesu alichagua kuunyosha mkono wake na kum-
gusa mwenye ukoma huku akimponya. Kwa kufanya hivyo,
Yesu alizipinga desturi za kijamii na pia kutoujali ukoma katika
hali yake halisi. Aliamua kuhatarisha afya yake na kibali chake
mbele ya jamii kwa kuweka mikono yake juu ya mtu aliyechoka
na maisha.
Kwa nini Yesu alitenda kwa namna hii isiyokubalika kiafya na
kijamii? Marko anatueleza ya kuwa Yesu alifanya hivyo kwa
sababu alisukumwa na huruma kwa tatizo la mwenye ukoma
yule.
Uponyaji wa mwenye ukoma yule haukuwa tendo lililojiten-
ga. Huruma iliambatana na maisha na huduma ya Yesu. Mara
kwa mara aliguswa na huruma alipoiona njaa, alipouona ujinga,
ugonjwa, na hata alipokiona kifo. Kwa hiyo Yesu alikamatwa
na huruma wakati alipowaona watu wa kawaida katika hali ya
kupoteza shabaha ya maisha na kuwa kama “kondoo wasio na
mchungaji” (Math 6:34), wagonjwa na wasioona wakiwa mion-
goni mwa makundi ya watu (Math 14:14; 20:34), na huzuni ya
wale waliopoteza wapendwa wao (Luka 7:13; Yohana 11:35).
Bila kubakia tu katika eneo la hisia, huruma ya Yesu ilijieleza
yenyewe katika utendaji wake ndani ya huduma yake. Kuto-
kana na huruma yake aliwafufua wafu (Yohana 11; Luka 7:14),
aliwafundisha watu wengi (Marko 6:34), na kuponya wagonjwa
(Math 14:14; 4:23; 9:23; 9:35; 19:2)
Katika kuwahudumia wenye shida Bwana Yesu hakuogopa
kugusana nao. Alikamata mikono ya wagonjwa (Marko 1:31;
Math 9:25) na wale waliofungwa na shetani (Marko 9:27). Vid-
ole vyake viliwagusa wasioona (Math 20:34; Yohana 9:6; Math
9:29), viziwi (Marko 7:33), na wasiosema (Marko 7:33). Cha
kushangaza kabisa zaidi ya yote, Yesu aliwagusa wenye ukoma
– wale waliotengwa wa enzi zake (Math 8:3; Marjo 1:41; Luka
5:12-13), na hivyo kuonyesha kina cha huruma yake.
Huruma ya Yesu haikuwa na mipaka, ilivuka rafiki zake wote
na hata kuwazunguka maadui zake. Akitarajia hatimaye ku-
kataliwa kwake katika taifa alilolipenda, Yesu aliulilia mji wa Ye-
rusalemu (Math 23:37). Wakati wa kukamatwa kwake alipenda
kumponya askari ambaye sikio lake lilikuwa limejeruhiwa ka-
tika purukushani iliyotokea (Luka 22:51). Yesu pia aliomba Baba
yake ajibu kwa rehema na msamaha kwa maaskari waliokuwa
wakimsulubisha (Luka 23:34). Kwa kufanya hivyo,Yesu aliishi
katika yale aliyofundisha, kwamba huruma zielekezwe kwa
mtu yeyote bila kubagua, kama mfano ule wa Baba wa mbin-
guni (Math 5:43-45). Kama mmoja wa wafuasi wake wa awali
alivyosema baada ya kuyatafakari maisha ya Yesu, “Kwani una-
ijua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo kwamba ingawa alikwa
tajiri lakini kwa ajili yetu akawa maskini ili kwamba kwa umas-
kini wake tuwe matajiri” (2 Kor 8:9).
Kulingana na Agano Jipya, Yesu si mfano mkubwa wa hu-
ruma peke yake. Muhimu zaidi, yeye anabeba moyo wa
huruma wa Mungu wa Biblia. Dhamira ya Mungu mwenye
huruma, inayoibuliwa kutokana na ufunuo wake mwe-
nyewe, inapatikana katikati ya imani ya jumuia ya Kiebra-
nia, baada ya kulifunua jina la kimungu kwa Musa mlimani
Sinai, Yahweh alijieleza mwenyewe kama “Mungu mwenye
neema na huruma, si mwepesi wa hasira, mwenye upendo
na mwaminifu” (Kut 34:6). Mungu huyu anawahurumia
watu katika taabu zao, si kwa sababu ya sifa zao za kibi-
nadamu ila kwa sababu ya upendo wa Mungu na rehema
zake nyingi. Tukumbuke kuwa Mungu ni mwenye neema
hata katikati ya dhambi na uasi wa kibinadamu. Mungu
hakika ni mwenye neema na rehema katika mazingira
haya ya UKIMWI. Huruma za Mungu zinatungoza kufikia
utendaji wa kimungu unaoonyeshwa Yatika Yesu Kristo.
SURA ZA MUNGU
46 SURA ZA MUNGU
Tokea tukio la kwanza la kujitokeza kwake, VVU na UKIMWI dai-
ma umetafsiriwa kama adhabu toka kwa Mungu. Watu wengi
wenye VVU wameikubali tafsiri hii, na hii huongeza mateso
juu ya mateso. Dhana kwamba VVU na UKIMWI ni adhabu toka
kwa Mungu inaashiria sura asilia ya Mungu kama nguvu inay-
oadhibu na kukaripia.
Katika mafunzo ya Biblia yanayofuata tutazingatia visa vinne
toka Agano Jipya vinavyotupatia mbadala wa sura ya Mungu
yenye upendo na maendeleo.
Msingi wa kawaida wa visa hivi vinne ni kuwa vina akisi sura
ya Mungu katika mwendo. Mungu husogea na huweza ku-
sogezwa. Mungu si mgumu na si aliye mbali. Hukutana nasi
hapa, na pale tulipo.
LUKA 15:11-32
Mfano wa Mwana Mpotevu
Mungu anayekimbia na kukutana nasi
Hadithi ya Mwana mpotevu inatuonyesha sura yenye nguvu
ya Mungu kupitia mtazamo na matendo ya Baba. Mungu ndiye
anayetukumbatia – kwa dhati na kwa ukarimu. Anakimbia ku-
tujia na kutuzungushia mikono yake, kama vile hadithi inavy-
osema hivyo ndivyo baba anavyofanya. Na kinachomhimiza
ni ile nguvu ya upendo aliyonayo. Mwana mpotevu ni kielel-
ezo cha wale wanadamu walioko chini udongoni na pia nje ya
ulingo. Hii inaweza kumtokea mtu yeyote. Na mambo men-
gi yanaweza kutufanya tuzame chini kwa kuvunjika moyo.
Maana inayotolewa na hadithi hii katika injili ni kuwa Mungu
hutupa uwezekano wa maisha mapya, yanayopewa kielelezo
na uzoefu tulioupata na undani wa kifahamu tulioupata katika
safari yetu kuelekea chini. Kipo kituo cha mageuzi katika kila
mgogoro wa kimaisha, na kwetu sisi pia hata pale tulipovuruga
fursa zilizojitokeza kwa ajili yetu, zaidi kwetu tena hata pale
tunapoona aibu juu ya maamuzi na makosa yetu.
Hadithi hii inatupa matumaini kwamba tunaweza kuendelea
kuishi maisha yetu pamoja na hayo yote yanayotupata – na
kwamba yupo Mungu na wapo wanadamu ambao wanasubiri
kutukaribisha jinsi tulivyo – bila kujali hali yetu ya kiafya na
VVU ama historia ya maisha yetu.
Maswali ya Kufikiria
• LiniMungualikujanakukutananawekatikaharakatizamai-
sha yako?
• Unawezakujifananishanananizaidimwanampotevuama
kaka yake mkubwa ambaye anadhani hakutendewa vizuri
na babaye?
• Nanikatiyaoyukombalikabisanababayao?
• Kunauhusianoganikatiya“msamaha”na“haki”?
LUKA 24: 13-35
Simulizi ya Safari kulekea Emmau
Mungu anayetembea kando yetu
Huzuni huleta ganzi katika fahamu zetu. Hivi ndivyo ilivyo-
tokea kwa wanafunzi baada ya Yesu kufa. Ni wagumu kusiki-
liza, akili zao zimepumbaa, wasioona vizuri na walioyumba
na kwenda mbali. Hawatambui kuwa Bwana aliyefufuka
anatembea kando yao.
Hadithi hii inaelezea sura ya Mungu aliyeshinda mateso ili
aweze kuchukuliana nasi katika huzuni yetu. Yeye anatem-
bea katika barabara mbaya pamoja nasi – bila kutuacha tu-
poteze lengo na mwamko. Hutubeza ili atuwezeshe kuona
mambo yote katika mtazamo mpya. Upendo wake wenye
nguvu unatufanya tuweze kuukabili ulimwengu unaotuzun-
guka – na kuendelea na maisha yetu. Anatutia moyo na ku-
tupa changamoto ya kuishi. Hukutana nasi kwa maneno na
kwa vitendo.
Sura hii ya Mungu imepewa maana yake na dhana ya Agano
La kale ya Mungu aliye Imanueli, yaani Mungu pamoja nasi.
Ndiyo. Mungu yu pamoja nasi, na amekuja na kukaa nasi. Yu
karibu – hata pale tunapotoa machozi ma kukasirika kwa ku-
toonekana kwake.
Maswali ya kufikiria
• Marangapi katikamaishayakoumejisikia kwambaulitele-
kezwa?
• Je inawezekana sura hii ya Mungu kuwa mfano mzuri
kwetu?
• JeinawezekanakweliMungualiyetembeakandokandoyetu
atatufundisha jinsi ya kutembea pamoja na wanadamu wen-
zetu wenye mahitaji?
• Je sura ya Mungu anayetembea pembeni mwetu inaleta
maana gani kwa wale wanaokufa na UKIMWI?.
• WanafunziwalimtambuaYesualipoumegamkatewakatiwa
Kujifunza Biblia
Sura Nne za MunguDENMARK
SURA ZA MUNGU
SURA ZA MUNGU 47
chakula cha jioni. Je sakramenti ya Chakula cha Bwana ina
maana gani kwa watu wenye huzuni?
YOHANA 13:1-17
Hadithi ya Yesu akiwaosha miguu wanafunzi wake
Mungu anayeinama chini kutugusa
Hadithi ya Yesu akiwaosha miguu wanafunzi wake inatupa
picha ya Mungu aliye tayari kupiga magoti ili aweze kutu-
karibia. Utayari huu unafunuliwa katika kufanyika kwake
mwili, ambapo Mungu Mwana anainama chini kutoka mbin-
guni hadi chini, na katika tukio hilo kabla tu ya matukio ya
Ijumaa Kuu na Pasaka, ambapo Yesu anainama kuwahudu-
mia wanafunzi wake. Kwa njia hii anaonyesha unyenyekevu
na utayari kwa kugusana nao.
Watu wengi wenye VVU ni wahanga wa chuki na hofu ya
kugusana kimwili. Wanajisikia kuwa ugonjwa wao unawal-
izimisha kwenda magotini na kwamba watu wengine wa-
nawadharau na kujitenga nao. Yesu akiwa tayari kunyoosha
mkono wake na kuwagusa na kuwainua walio wanyonge ni
mfano mzuri kwa Wakristo binafsi na hata kwa kanisa kwa
jumla.
Maswali ya Kufikiria
• Jeliniilikuwamarayamwishokwakokupigamagotiilikum-
fikia mtu mwingine?
• Je umewahi kuwa, ama unahisi kuwa umekuwa mwenye
hofu ya kuwagusa wengine?
• JeunafikirininijuuyasurayaMunguaikwachiniameinama
na kukushika miguu na mikono?
• JesurayaainahiyoyaMungu inamaanaganikwawenye
VVU na UKIMWI?
YOHANA 9:1KK
Uponyaji wa mtu aliyezaliwa akiwa asiyeona
Mungu anayejinyoosha kutufikia na kutuponya
Katika kisa hiki cha uponyaji, Yesu anaondoa muunganiko wow-
ote kati ya hatia na hatima. Kwa kufanya hivyo pia anaondoa sura
ya Mungu kama yule anayehukumu ama kuadhibu, yeye anayet-
upatia tunachokistahili. Badala yake, katika uponyaji peke yake,
anachora picha halisi ya Mungu anayetufikia kwa nia ya kutuka-
milisha
Wakati wanapokutana na yule asiyeona, wanafunzi wanakuwa
na tahadhari. Wanatafuta mtu wa kumtupia lawama. Watu wengi
wenye VVU wanakutana na hali ya jinsi hiyo yenye utata wa ki-
maadili hata pale wanapojifungua na kueleza hali ya ugonjwa
walio nao. Uonevu wa kawaida ni ule ambapo wale wenye VVU na
UKIMWI wametengeneza vitanda vyao, na sasa ni lazima wavila-
lie. Katika hadithi hii Yesu anaweka wazi kuwa hatupati kile tuna-
chokistahili. Hadithi hii ya Injili ni moja tu kati ya nyingi zilizomo
katika Agano Jipya kuhusu uponyaji. Watu ambao wanumwa sana
wanahitaji kupewa matumaini, lakini matumaini bandia yanaweza
kuleta maumivu makubwa. Hata hivyo hakuna uwezekano kwa
wale wenye UKIMWI kuponywa, lakini matumaini yanayoletwa
na Injili, ni sura na mfano wa Mungu mwenye upendo ambaye
anaweza kutupatanisha sisi katika ukweli wa ugonjwa na kutupa-
tia nguvu ya kuishi – bila kujali yote yaliyopo.
Maswali ya Kufikiria
• Jeunaamini kamakunauhusianobainayakile tunachoki-
fanya na kile kinachotutokea?
• Jewakatiwamiujizaumekwisha?
• Jeupatanishonaugonjwamkubwaunawezakuletaupon-
yaji wa kiroho?
48 SURA ZA MUNGU
Mungu Anayesamehe1. Utangulizi
Katika tamaduni nyingi za kiafrika, kama si zote uhusiano baina
ya mtoto na mzazi hauwezi kuvunjwa kirahisi na kitu chochote.
Hata dhambi na kifo haviwezi kusitisha uhusiano wa aina hiyo.
Tunapohusisha mambo haya na Mungu muumbaji wa vyote
wakiwemo wanadamu., tunagundua kuwa hakuna kinachowe-
za kututenga na upendo wa Mungu. Je VVU na UKIMWI vinaweza
kututenga na Mungu jinsi hiyo mwenye kusamehe.
2. Tafakuri
Katika kujifunza kwa upana kifungu hicho – ambacho kinawe-
za kusomwa mara nyingi kutoka tafsiri mbalimbali ili kuweza
kukielewa vizuri na kuukubali mfano huo – maswali yafuatayo
yanaweza kusaidia:
a. Maswali yanayohusu kifungu chenyewe:
• OnyeshajinsimfanohuuunavyojibuhojayaMafarisayoka-
tika Luka 15:2
• Baba, Mwana na Roho wanapenda kufanya nini na kuona
nini kinatendeka?
• Kamayulemtotoaliyemdogokatikakisachetuangejihukumu
mwenyewe. Je! Baba angeweza kumpokea tena nyumbani?
• Je mfano wa mwana mpotevu unatufundisha nini juu ya
uhusiano wetu na Mungu?
• JeMafarisayowalitarajikujifunzaninikutokananakisahiki
cha kusisimua.
b. Maswali yanayohusiana na VVU na UKIMWI:
• Jeunaonamwelekohuohuokatikajuhudizetuzakukabili
maambukizi ya VVU?
• Je kuna wakati ambapo tunawadharau wale wanaoishi na
VVU kama watoto ambao wamepotea?
• Je huenda tunawaangalia kama wenye dhambi waliopata
maambukizi ya virusi kwa kuendesha maisha ya kutojali
chochote
• Tutatambuajechanzochamaambukizinakwanininilazima
tufahamu, je si kwa sababu zile zile za kutoa lawama.
• Je Mungu anaangalia watu wanaoishi na VVU na UKIMWI
kama wakosaji ambao hawawezi kusamehewa?
c. Jinsi kifungu kinavyohusika na mazingira yetu:
• Jetunawezakuionatabiaaliyokuwanayokakamkub-
wa katika kisa chetu miongoni mwa jamii ya Kikristo
katika kuendekeza ukimya, fedheha, na unyanyapaa
unaohusishwa na maambukizi ya VVU?
• Hebu angalia herufi zilizotajwa katika kifungu na
somo gani linaweza kutolewa humo na kulitumia ka-
tika mapambano dhidi ya unyanyapaa unaombatana
na VVU.
• Tunapatakanunizipitokakatikavifungu?
• Jinsi gani Kanisa linaweza kuwa chemichemi ya up-
endo na ukarimu?
Mfano wa Mwana mpotevu
Kujifunza Biblia Luka 15:11-32
ZAMBIA
SURA ZA MUNGU 49
SURA ZA MUNGU
Katika semina ambayo iliendeshwa katika ukumbi wa Mt. Pau-
lo UCZ Kabwata mjadala ulifanyika ukijumuisha kundi la watu
walioishi na VVU. Wote hawa ni wanachama wa mtandao wa
kuhudumiana unaojulikana kama Mduara wenye Matumaini.
Ifuatayo ni kumbukumbu ya majibu yao juu ya vifungu kadhaa
vya Biblia.
LUKA 15:1-11
Kondoo aliyepotea na Sarafu iliyopotea
Kifungu kilisomwa na kundi lote kutoka tafsiri mbalimbali
za Biblia ili kupata maana halisi ya kifungu kile.
Baada ya kukisoma kifungu washiriki walipewa changamo-
to ni kwa jinsi gani watajisikia kama waishio na VVU endapo
kifungu kingesomwa mbele yao.
Yafuatayo ni majibu:
• Kujisikiamsamaha–Munguhusamehe
• Kujisikiaupendo–Mungunipendo
• Kujisikiakukaribishwa–Mungunimkarimu
•Kujisikiakuombasanabaadayakupitiamatatizo.Lazima
tukumbuke kuwa yupo Mungu mwenyezi wa kumpelekea
maombi yetu. Kifungu kinatupatia hisia za kuwa na uhakika
kiasi kwamba hata baada ya kupitia matatizo ama magumu
yupo Mungu wa kutusamehe daima tunapochukua hatua
zinazostahili.
Wengine walidhani ya kuwa kifungu kilileta hali ya kujisikia
kuhukumiwa tayari – mtu mmoja alisema: “ unapokisoma
kifungu hiki kwa mara ya kwanza utadhani sasa unahuku-
miwa hasa ikiwa umeishi maisha yasiyokuwa na tahadhari
tena yaliyohususisha ngono.”
Kundi lilithibitisha ya kwamba wamejifunza Mungu yupo
ili kusamehe na kuwasaidia kuanza maisha maisha mapya
ambapo hawataangalia jinsi walivyopata ugonjwa bali kuishi
maisha yasiyo na majuto.
MWANZO 27-28
Mungu anaumba Mwanadamu kwa sura yake
Kifungu kilisomwa kutoka tafsiri tofauti za Biblia ili kuielewa
kwa udani maana yake.
Baada ya kusoma kifungu hicho tena, washiriki waliulizwa
nini kilikuwa kinaendelea katika fikra zao walipokuwa wak-
isikiliza kifungu hicho. Yafuatayo ni majibu waliyotoa:
• Mungunimkuu
• Mungunimwenyezi
• MungunimuumbahatakamatunaVVU,nayeametubari-
ki
• Tumeumbwa kwa sura ya Mungu na hivyo tunafanana
na Mungu na yote tunayoyapitia tuyaache mikononi mwa
Mungu kwani yeye ni muumba wetu. Muumba huyu anajua
na kuvielwea virusi hivi sana.
-Tunapaswa kuwa na shukrani na daima kumwomba Mungu
na kuendelea kumshukuru kwa maisha yetu.
Jambo lingine waliloliona wanachama ni kuwa ikiwa Mungu
ni muumba wetu –kwa nini tupitie mateso mengi – kwa nini
tuwe na VVU? Kwa nini asiviondoe virusi toka kwetu?
Mungu wa Uumbaji ZAMBIA
Masomo mawili ya Biblia
Sikuwahi kabisa kupitia maisha yaliyokamilika kama
nilivyofanya baada ya kugundua ya kuwa nina VVU.
Ili kukutana na nafsi yako mwenyewe - ni vigumu, ni
kazi kubwa, kitu ambacho ungependa kukiepuka kama
ungeweza, na tunahitaji msaada wa kila moja wetu
katika safari yote. .
USHUHUDA WA RONNY, ALIYEKUFA KWA UKIMWI, DENMARK
50 SURA ZA MUNGU
Katika mijadala mjini Oslo, iliyowahusisha watu wanaoishi na
VVU ama kuathirika, kifungu hiki cha Biblia kikawa muhimu
sana kwa uelewa wetu juu ya kile kinachomaanisha kumwona
mtu kando yetu na kutopagawa na amri na taratibu za kisheria.
Miongozo ifuatayo inaweza kusaidia kujifunza kifungu hiki.
1. Soma kifungu kwa kuzingatia mazin-
gira yako mwenyewe na changamoto un-
azozikabili:
Kabla ya kusoma kifungu cha Biblia uulize maswali kadhaa juu
ya jinsi washiriki wanavyomchukulia Mungu kuwa ni nani na
jinsi gani mazingira tofauti ya maisha yanavyoweza kutupatia
sura tofauti ya Mungu. Kwa mfano:
• JeunawezakutuelezawakatiambapoulifikiriMunguame-
kuadhibu? Ulifanya nini?
• Je umewahi kujisikia ya kuwa Mungu anakupenda pale
tu unapokuwa unastahili hivyo ama kamaunazitii amri za
Mungu?
• Je pamewahi kuwepo mazingira ya aina nyingine ambapo
ulikosa uhakika wa upendo wa Mungu, ukifikiria kuwa Mungu
anaweza kuwa amekasirika kidogo ama mgumu kumwamini?
Turuhusu washiriki wafikirie juu ya jambo hili kwa muda kabla
hatujaanziasha mjadala wa vikundi. Ili kuweka mambo katika
wepesi wa kutokuwaogofya wengine unaweza kuanza kwa
kuwaeleza juu ya tukio ambalo unadhani huenda lilikuwa ad-
habu ya Mungu. Jaribu kuwasaidia watu kuelewa mifano na
sura tofauti tunayobeba pamoja nasi daima. Unaweza pia ku-
ziandika sura tofauti zilizotajwa katika karatasi pana ya ubaoni,
kwa mfano: Mungu anayekasirika; Mungu mwenye hali zina-
zobadilika; Mungu anayehukumu na kuendelea.
2. Kisome kifungu hicho kwa pamoja
Soma hadithi juu ya mwanamke mlemavu katika Luka 13:
10-17. kila mmoja asome sentensi ama andiko moja.
3. Kisome kifungu kwa ufasaha na kwa kirefu
Andika maneno ya msingi katika karatasi. Uliza maswali
ya jumla juu ya kifungu hiki.
• Kifunguhichokinahusunini?
• Ninikinakugusajuuyakifunguhiki?
• Dhamiraganizimokatikakifunguhiki?
Kisha angalia kwa makini katika kifungu:
• Unakutanananinikatikahadithi?
• Tunajifunzaninijuuyakifunguhiki
Inaweza pia kuwa na msaada mkubwa kuangalia mahu-
siano baina ya watu katika kifungu hicho, pia kutoka
katika mitazamo ya kijamii, kisiasa, na kiuchumi.
• Je viongozi wa sinagogi wanahusiana vipi na mateso
ya mwanamke?
• JeYesuanahusianavipinaviongoziwasinagogi?
• JeYesuanahusianavipinaSabato?
• Je viongozi wa sinagogi wanahusiana vipi na maisha
ya binadamu, hasa kulingana na alichosema Yesu?.
• Je watu tofauti waliokuwepo walisema nini mwisho-
ni?
• KunathiolojiaganiyaYesuyauelewawaMungukatika
kifungu?
• Unajisikiajekulinganishanakifungu?
Baada ya kufanya kazi kwa karibu pamoja na kifungu
hicho cha Biblia, ni vizuri kwamba myaangalie maisha
yenu na mazingira yenu.
• Jeunawezakuitambuahalialiyokuwanayoyulemwa-
namke?
• Je umewahi kukutana na matukio kama yale yaliom-
tokea yule mwanamke?
• Je kitu gani kingine unachodhani kinafanana na hali
aliyokuwa nayo yule mwanamke?
• JeUnahusianavipinanawenginewanaofanananaye
siku hizi
Mwanamke MlemavuNORWAY
Kujifunza Biblia kutoka Luka 13:10-17
SURA ZA MUNGU 51
4. Soma kifungu ukiwa
na wazo la kubadili mambo
Masomo ya Biblia yaliyowekwa katika mazingira ya ma-
hali hayamaliziki hadi utakapoona kile ambacho unaweza
kufanya kuleta upeo wa matumaini katika kifungu katika
siku zetu za leo.
• Nanianayefanyamawasilianohayoamawapitunapata
sura ya Mungu ambayo Yesu anaiwakilisha leo?
• Tutapambana namna gani dhidi ya sura zinazopoto
shwa za Mungu.
• Tutawezaje kueneza sura ya Mungu ambayo Yesu
ameleta?
• Tutafanyaje maisha kuwa bora kwa watu walio katika
hali kama ile aliyomo yule mwanamke?
Tafakuri
Mazungumzo mjini Oslo juu ya kifungu hiki yanaweza kupewa
muhtasari ufuatao;
Ukweli kwamba Yesu aliponya watu siku ya Sabato umekuwa
na maana kwa kuelewa moja ya sifa maalu sana za Mungu.
Hapa tunakutana na Mungu anayepinga mamlaka na kufun-
gua vifungo vya wale waliofungwa.
“Ni Mungu yule ambaye si tu anapatikana kwa shughuli kati
ya saa 3 asubuhi na saa 11 jioni, bali yeye ni nguvu isiyoweza
kuwekewa mipaka ya utendaji.”
Katika hadithi hii tunaona Mungu mwenyewe akivunja kanu-
ni za maandiko ”kwa sababu Mungu ameweka watu na huruma
juu ya sheria. Kile ambacho Yesu amekimaanisha ni kwamba
kusudi la sheria ni muhimu sana kuliko kufuata vipengele bi-
nafsi vya sheria yenye sura ya kutobatilika.” Au kama mshiriki
mmoja alivyosema , “Ni asili ya Mungu kupenda, na kusudi
la maneno na vitendo vyake ni kufungua vifungo vya watu,
kuwainua waliokandamizwa, kuweka huru waliofungwa, na
kuponya na kuokoa.”
SURA ZA MUNGU
52 SURA ZA MUNGU
SURA ZA MUNGU
Hakuna Hukumu ZAMBIA
Mungu ni muumbaji mwenye upendo wa kudumu. Mungu ni Mungu anayesa-
mehe. Ijapokuwa mtu anaweza kuwa na VVU, tunajua kwamba Mungu anatu-
penda na anatuhudumia. Kwa kuwa yeye ni muumba wetu tumekubali hali
zetu za kiafya na kuendelea kumtafuta katika maisha yetu yote. Si wale wa-
naoishi na VVU ama Mungu anayestahili kulaumiwa kwa ugonjwa huo kuto-
kea. Upendo wa Mungu na kazi zake zinaweza kuwa zimedhihirishwa kupitia
walio baina yetu wanaoteseka. Mungu ni Mungu mwenye upendo kwa sababu
tuliumbwa kwa mfano wake na kubarikiwa naye. DUARA ZA MATUMAINI, ZAMBIA
K - Kiongozi
W- Wote
1. Ukusanyaji wa watu
muziki ukichezwa
2. Wito wa kuabudu
K: Bwana anasema “Mimi ndiye nikuponyaye…uniangalie mimi
nawe utapona.”
Marafiki, tumekutana hapa mbele za Mungu mwenyezi, yeye
anayejali na mwenye huruma. Kwa hiyo kupitia maombi na sifa
na nyimbo tumwaabudu Mungu anayeishi milele na mwenye
upendo mwingi. Amen.
3. Nyimbo za Sifa
4. Sala ya kufungua
K: Baba, upendo wako unafanya kazi kupitia uumbaji wote.
Mwana wa Mungu, katika mfano wako tutafanywa wapya. Roho
mtakatifu, umeyagusa maisha yetu kwa matumaini. Pokea
ibada yetu, utuchukue tena tukutumikie mbele zako: utuweke
huru ili tukutukuze leo.
Bwana, katika uwepo wako tunakubali sehemu yetu katika
dunia ambayo imechoshwa na maumivu. Katika zama zetu hizi
tunakutana na maumivu kwa njia mbalimbali. Tunapokutana
leo, wengi wanateseka kwa sababu ya wimbi la VVU na UKIMWI.
Watu wanaoishi na VVU wananyanyapaliwa. Tunakuomba Bwa-
na kwamba utatutumia sisi kama vyombo ambavyo upendo
wako unaweza kutiririka kuwafikia kaka zetu na dada zetu wa-
naoishi na VVU.
Bwana mwenye rehema, pale ambapo tumewanyanyapaa
rafiki zetu na pia sisi kwa sisi, utusamehe na uhuishe upendo
wako ndani ya mioyo yetu ili kwamba tuweze kuonyesha kujali
na huruma kwa wale wanaoishi na VVU.
Utuongoze katika ibada hii. Tunaomba tukutane na ushirika
wa kweli baina yetu nawe na baina yetu sisi kwa sisi.
Utusikie katika Jina la Mwanao Bwana wetu Yesu Kristo. Amina.
5. Maombi ya Toba
K: Bwana mwenye neema, kwa toba yetu yote ya imani ambayo
hutoweka utendaji unapohitajika, tumekiri kuwa tunakupenda na
kwamba tunapendana sisi kwa sisi lakini bila shaka haikuwa hivyo.
W: Tusamehe tunaomba
K: Utusamehe kwa kutokutii kwetu
W: Tumeshiriki maonevu, ukatili, na unyanyapaa dhidi ya wale
miongoni mwetu wanaoishi na VVU, kwa hivyo kuwanyanganya
watu maisha yenye uzima tele na tumaini ulilotupa ndani ya Mwa-
nao Yesu Kristo.
K: Kama jumuia yenye imani kwa Mwanao, hatujawaonyesha kaka
zetu na dada zetu wema wako.
SURA ZA MUNGU 53
W: Uturehemu eeh Bwana
K: Kama Kanisa, hatujawa na upendo baina yetu kama vile Kristo
alivyotupenda: hatujasameheana kama tulivyosamehewa; hatu-
jajitolea kutumikia ulimwengu ulioharibika kwa upendo.
W: Tunakiri kuwa dhambi yetu kama kanisa katika jina la Bwana ali-
yejaa neema: Amina
6. Tamko la Msamaha
K: Marafiki, katika Yesu Kristo, hapa tuna uthibitisho wa upendo
wa ajabu wa Mungu. Ilikuwa wakati tukingali wenye dhambi
Yesu alikufa kwa ajili yetu. Pokea rehema za Mungu kwa Jina la
Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu.
W: Neema ya ajabu jinsi gani ilivyo tamu ile sauti iliyoniokoa
fukara kama mimi, nilikuwa nimepotea hapo awali lakini sasa
nimepatikana, nilikuwa nisiyeona lakini sasa ninaona
7. Maombi na ufahamu zaidi
K: Bwana mwenye neema, neno lako linatupatia uzima tele
katikati ya maumivu na mateso. Lnaleta matumaini wakati tu-
mekata tamaa. Naomba uturuhusu sisi kuisikia sauti yako leo
tunaposoma neno lako takatifu na tunaomba liponye kuvun-
jika kwetu moyo. Katika Jina la Yesu Kristo tunaomba. Amina!
8. Somo kutoka maandiko matakatifu
Yohana 8:1-11
9. Mwongozo wa Mahubiri
• walimuwasheriawalimletamwanamkenamtuanaweza
kushangaa yuko wapi mwanamume aliyekuwa akizini
naye. Sheria ya Musa ilihitaji kuuwawa kwa wote wawili na
si mwanamke peke yake [law 20:10, Kumb. 22:22]
• Waalimu washeria walitaka kumwaibisha yule mwanam-
kena kumnyanyapaa. Jambo ambalo ni baya sana kuli-
fanya. Wale walioambukizwa VVU hawapaswi kunyanya-
paliwa.
• Baadhiyetutunatendakanakwambahatujawahikufanya
dhambi siku za nyuma na kufikiri kuwa kaka zetu wanaoi-
shi na virusi wamefanya dhambi zaidi yetu. Sisi nasi ni
wenye dhambi pia.
• Yesu hakumhukumu lakini alionyesha huruma na kwa
neema kubwa alimwambia asitende dhambi tena.
10. Maombi
Kwa uchaguzi wako mwenyewe.
11. Nyimbo ya kufunga
12. Maombi ya Kufunga
W: Neema ya Bwana wetu Yesu, Upendo wa Mungu baba
na ushirika wa roho Mtakatifu, uwe nasi leo na siku zote.
Amina!
54 SURA ZA MUNGU
“Ndani yake tunaishi
tunatembea na kuwa na uzima”
Utaratibu wa Ibada Kwa VituoNORWAY
Ibada hii ni matokeo ya mazungumzo yaliyofanyika Oslo juu ya
unyanyapaa wa watu wanaoishi na VVU. Inatarajiwa kwamba
ibada yote itajumuisha mahubiri yatakayoelezea sura ya Mun-
gu na fikra juu ya ubinadamu.
Utangulizi wa Utaratibu
wa Ibada na maandalizi yake
Utaratibu wa Ibada sio mwongozo ulionyooka wa ibada. Wakati
mwingi wa ibada wale ambao watapenda wanaweza kutafuta
nafasi ya kwenda katika vituo mbalimbali katika chumba kile.
Vituo hivyo mbalimbali vinahusika na maisha ya binadamu na
kile kinachofanyika mbele za Mungu ambaye ametuumba,
ametukubali, na kutuweka huru.
Ibada hii kimsingi si ile ya kawaida, kwa hiyo ni muhimu
kwamba waabuduo waandaliwe mapema ili kwamba wawe
na mawazo ya kile ambacho watakishiriki. Maandalizi haya
yanaweza kufanyika katika vipindi vya mwanzo vya ibada,
vijalida vya kanisa na kadhalika. Hii ina maana ya kuwafanya
watu wasijisikie ya kutengwa ama kubaguliwa. Ni muhimu ku-
weka agenda kwa ibada ambayo inaelezea dhana iliyo nyuma
yake pamoja na maendeleo yake. Ibada hii ina mambo yanay-
ofanana na vituo asilia vya Msalaba.
Vituo vilivyotajwa hapa ni mapendekezo yetu. Vinapaswa
kuandaliwa kabla ya ibada. Kwa kuwa wanahitaji nafasi ya
kutosha unaweza kuongeza ama kupunguza idadi kulingana
na matakwa ya mahali mlipo na nafasi zilizopo. Katika maz-
ingira mengi, idadi ya vituo vilivyoorodheshwa inaweza isiwe
halisi. Kwa hiyo tunashauri ya kwamba ufanye uchaguzi. La-
kini kituo tulichokiita Mahali pa Ajabu lazima kiingizwe, ni
bora sana kwanza kutafuta namna asili za kuelezea jambo
zitakazotuwezesha kupata alama kwa vituo mbalimbali. Tu-
meandaa mapendekezo kadhaa ya rangi yatakayoweza kuju-
muishwa kwa kutundika vipandev ya nguo zilizofumwa uku-
tani ama kuzilaza chini. Pia inawezekana kuruhusu vipande
vyembamba vya nguo hizo vitoke katika vituo hadi Mahali pa
Ajabu. Kuwepo pia na Biblia iliyo wazi katika kila kituo, hasa
ikiwa imefunguliwa katika moja ya vifungu vya Biblia vilivyo-
pendekezwa. Kwa nyongeza kifungu kilicho kifupi kinaweza
kuandikwa katika karatasi na kuninginizwa juu ama kuwekwa
pembeni karibu na Biblia. Hii itasaidia kuona kituo kinamaan-
isha nini. Hatushauri watu kutumia vikaratasi vidogo vyenye
gundi. Muhimu sana: fanya mambo rahisi na yanayoweza
kutendeka. Haya tuliotoa ni ushauri tu, si mambo ya lazima:
mazingira ya mahali lazima yazingatiwe na hayo yataashiria
kile utakachopenda kujumuisha.
Pia tumeshauri mahali utakapoweka vituo hivyo mbalim-
bali katika chumba. Sehemu hizi pia zinategemea ucha-
guzi wako. Uwezekano mwingine ni kuendesha ibada hiyo
yote nje. Mlango wa kuingia “kanisani” unaweza kutumika
pia kama eneo la madhabahu. Lakini si wazo zuri kuwa na
vituo vingine ndani na vingine nje ya jengo. Hii itaweza
kutafsiriwa kana kwamba vituo vingine ni muhimu zaidi
ya vingine.
Shule ama jumba la parokia linaweza kutumika kama mahala
pa kuabudia. Maandalizi ya ibada yanaweza kuwa nafasi nzuri
ya kuendesha warsha inayowahusu vijana na watu wazima.
Muda unaweza kutumika kutafakari juu ya vituo na namna ya
kuvifikia, kushughulikia umoja wa ibada, kuandaa ramani na
kutengeneza vituo, na labda kutafuta njia mbadala ya kuvitolea
utambulisho. Unaweza, kwa mfano, kuambatanisha, uzoefu
binafsi na visa vingine katika baadhi ya vituo. Ni muhimu haya
nayo yawekwe kwa kifupi.
SURA ZA MUNGU
SURA ZA MUNGU 55
• Mahali pa manunguniko na malalamiko
Uchungu, mawe, giza na rangi zinazon’gaa. Karibu na mlango
wa kuingilia nyumba ya ibada. Zab 22:2
• Mahali pa mazungumzo
Uwezekano wa kutua mizigo; toba. Pamewekwa nyuma ya
eneo la kuabudia. Viti vimepangwa viwili Viwili. Meza zikiwa
na vikombe na chai ya moto. Mawe yakiwa na mishumaa inay-
owaka juu yake. Rangi ya kijani iliyoiva sana. Yohana 3: Niko-
demo alikuja usiku kwa Yesu ili kusema……
• Mahali pa Ushirika
Pamewekwa nyuma pembeni mwa chumba. Mshumaa un-
aowaka umewekwa katikati ambapo watu wanaweza kuketi
katika mduara wakizunguka mwanga. 1 Kor 12;12-26 (mst.
13);Filipi 2:1.
• Mahali pa kicheko na furaha
Ukiambata moja ya kuta za nje. Manjano, rangi nyingi nyingi,
pua nyekundu, ama mchoro wa msanii. Mwanzo 18:12; I Kor
1:27a..
• Mahali pa mwili na Ujinsia
kuchua miguu ama mikono. Rangi zinazovutia kiupendo-
pinki, maua, mitandio, shela iliyoandaliwa vizuri. Wimbo wa
Sulemani Wimb.4:1; Luka 7:38b
• Mahali pa thamani
Lulu, nyota, kibahri. Kutoka Isaya 45:3: “ Nitawapa ninyi hazina
gizani na katika utajiri wa maeneo ya maficho. Ili ujue kwamba
ni mimi Bwana ninayekuita kwa Jina lako”.
• Kijito cha maji
Ni kisima. Katika kituo cha ubatizo, ukiwa na mimea iliyohifa-
dhiwa katika chungu, na mti. Mkondo wa maji wa kumwagilia
maua; maji baridi ya kunywa; karai la kuoshea. Rangi ya kiba-
hari na kijani. Yohana 4:14; Ubatizo wa Yesu, Ufunuo 22:1 , 17;
Zab 42:1
• Mahali pa uwazi na maumivu
Katikati, kuelekea nyuma ya eneo la kuabudia. Kitambaa cha
kufumwa rangi nyekundu (damu ya mzee) Uwezekano wa ku-
soma shairi na vifungu vingine. Yeremia 30:17.
• Mahali pa Ajabu
Ni mahali pa mageuzi, hamasa ya maisha na nguvu. Katikati ya
sehemu ya kuabudu. Kuna mkate na divai. Rangi zote zaweza
kukusanywa hapa..
• Mahali pa maombezi na kuwasha mishumaa
Njiani kuelekea eneo la madhabahu. Fursa ya kuwasha mshu-
maa na kuandika sala za maombezi katika vijikaratasi. Chungu
ama chombo kinachofanana. Rangi ya matumaini. Filipi 4:6
• Mahali pa Mapumziko
Mbele ya madhbahu. Rangi nzito zenye joto, mito ya vitanda,
blanketi, magodoro. Math 11:28
• Mahali pa Mapambano
Nyuma ya madhabahu, ikiwezekana sambamba na ukuta
kuelekea madhbahuni. Mabango, karatasi ukutani za kuandi-
kia. Rangi za mapambano. Zambarau. Ephe 6:12
Vituo
56 SURA ZA MUNGU
1. Msafara
Wakati nyimbo inayostahili ikiimbwa. Washiriki wanabeba divai
na mkate [mmoja], maji kwa ajili ya vijito vya maji na mshumaa
kwa ajili ya kila kituo. Kila mtu mmoja awe na mshumaa mmo-
ja, unaobebwa katika mikono iliyofumbwa. Msafara utaelekea
madhbahuni.
2. Salamu pamoja na Neno fupi la Biblia
• Mdo17:2425;27b–28
• Watu walio na mishumaa wataenda kwenye maeneo yao
rasmi ama baada ya salamu au ama wakati wa utambul-
isho pale kila kituo kitakapokuwa kinatajwa. Tunapofanya
hivyo, vituo vilivyoko karibu vitajwe mwanzoni, ili kwamba
ushirika uone kwamba pale ndipo wabeba mshumaa wana-
pokwenda. Baada ya hapo vifuate vituo vilivyopo mwishoni
mwa eneo la kuabudia.
3. Wimbo
4. Utangulizi
Maneno ya ufunguzi na maelezo ya chumba. Andaa mazin-
gira ya kiusalama ukizingatia kile kitakachotokea. Mambo ya
kutaja:
• Hakiyakuwakitukizima
• “TazamaMtuyule”,wekanafasikwaajiliyamaishayoteam-
bayo yanasaidiwa na Mungu
• Vituovyotevinatajwa,amanamtufulanianayesimuliatukio
lililotokea linalomuunganisha na kituo kimojawapo kati ya
hivyo, ama kwa kuchukua baadhi ya mawazo kutoka katika
mahubiri yaliyoandikwa mwishoni mwa orodha hii ya ibada
ilyopendekezwa. Ikiwa wabeba mshumaa wameelekea kati-
ka vituo vyao, basi wasimame pale kituo chao kitakapotajwa
huku wakiendelea kubeba mshumaa wao.
• Waeleze watu kwamba wanaweza kuendelea kukaa kimya
katika maeneo yao, au kwenda hadi vituo vyo vyote wa-
navyohitaji. Hakuna sababu ya kwenda kwenye vituo vingi
iwezekanavyo. Ni vema kusiskiliza hisia zako.
• Tangaza kama ibada ya Ushirika Mtakatifu itakuwepo ama
karamu ya chakula chenye upendo ama kitu kingine cho-
chote kufuatia ziara hadi vituo hivyo.
• KilakituKIFANYIKEmachonipaMungu,katikanyumbayake
na kimwelekee Mungu anayetukubali na aliyetuumba jinsi
tulivyo.
• Sala ya kuhitimisha Utangulizi Asante sana, kwamba
tunaweza kuwa watu tuliokamilika nyumbani mwako: wewe
muumba wetu: wewe Yesu, ambaye unatukubali na uliyetu-
weka huru: wewe Roho Mtakatifu, unayetoa na kufanya
upya maisha ndani yetu.”
5. Toba ya Imani
Pendekezo Kanuni ya Nicea
6. Muziki
Muziki wa ala ama wenye kuongoza kutafakari
7. Ziara kutembelea Vituo
Angalau kwa nusu saa: ama tukiwa kimya na muziki wa mbali
ukichezwa, ama katika ukimya ikiwa hilo haliogopeshi. Ikiwa
ukimya utachaguliwa, inaweza kuwa vizuri zaidi kuvunja
ukimya mara mbili ama tatu kwa kutumia nyimbo za kuta-
fakari. Hii inajenga hisia za ushirikiano katika chumba kizima
wakati watu wakitembelea vituo kadhaa.
8. Ushirika Mtakatifu au Mlo wa Upendo
Wakati watu wametawanyika chumbani, ibada inaendelea. Watu
wanaweza kubakia pale walipo.
• WakatikunaUshirikaMtakatifu:msherehekeajianapigama-
goti karibu na mkate na divai katika mlolongo wa kati wa viti
karibu na Mahali pa Ajabu na unaweza kuanza moja kwa moja
na maneno maalum ya kuendesha ibada hiyo: Usiku ule ali-
posalitiwa….”
• KuonyeshanaIsharayaAmani:“Tusalimianenisotekatikaup-
endo wa Yesu/ “Amani ya Bwana wetu iwe pamoja nanyi.”
• UgawajiwamezayaBwanaunaanziaMahalipaAjabu.Wale
wanaopenda wanaweza kupokea Ushirika Mtakatifu. Mkate
ambao umebarikiwa [si kuwekwa wakfu] unaweza kugawan-
ywa kwa wale ambao hawatarajii kupokea Ushirika. Ugawaji
huo unaweza kufanyika kimya kimya ukiambatana na nyim-
bo za kutafakari.
9. Sala ya Bwana, Baraka ya kufunga na kutawanyika
Kila mmoja anakusanyika katika katika duara ndani ya du-
ara. Sala ya bwana inasemwa kwa pamoja, kisha Mchungaji
anatamka Baraka ya Kufunga Ibada
10. Wimbo wa kuongoza msafara wa kutoka
Utaratibu wa Ibada
SURA ZA MUNGU
“Ndani yeke tunaishi,
tunatembea na kuwa na huo uzima”
SURA ZA MUNGU 57
Tupo hapa. Tumekuja kusimama mbele za Bwana ndani ya
uwepo wake Yeye Aliye Mtakatifu. Tumeupa kisogo ulimwengu.
Ulimwengu ulio laini, mgumu, usio na haki, uliojaa anasa na
wenye kupendeza. Tumesimama hapa, tukiangalia kwa uhakika
nje. Lakini “Ulimwengu” haujatupa sisi visogo. Sie tungali tu-
meubeba pamoja nasi, na ndani yetu fadhaa na hasira bado
zinakoroga mambo chini chini. Kutaka na kushindwa bado zi-
nashindana baina yao ili kutupotosha tusitafute kukutana na
Yeye Aliye Mtakatifu. Inawezekana mwili wetu huu wa kibinada-
mu unaweza kukumbuka uzoefu wa usiku ule ingawa roho zetu
zina mwelekeo wa kulisahau hilo, ya kwamba kujivunia mambo
mazuri yaliyopita jana inahatarisha unyenyekevu ama kuleta
fedheha kwa wale wanaotishia heshima yetu binafsi.
Tunajaribu kuwa kamili na tunaamini kuwa hii ni sawa na
kusema tuwe kamili katika hali ile tunayopaswa kuwa nayo tun-
apomkaribia Mungu…ama je si hivi ndivyo inavyopaswa kuwa?
Je kuwa kamili si kukubali tofauti zilizopo za mema na mabaya?
Je si mtu binafsi kujipatia haki ya kuwa sehemu ya uumbaji na
pia kuwa sehemu ya ulimwengu unaoendelea kuhangaika?
Ni pale tu tunapolikubali hili na kupeleka Kanisani vyote vile tu-
livyo navyo kama wanadamu, ndipo tunapoweza kukutana na Yeye
Aliye Mtakatifu. Hapo tunatoa nafasi kwa neema, kukaribishwa
tena kwa Mungu na furaha. Kila kitu kinawezekana kwa Mungu.
Katika ibada hii tutaruhusiwa kuwa vile tulivyo, yaani bin-
adamu. Ndani ya kila mmoja wetu kuna vyumba vya kutosha,
na leo kuna vyumba vingi katika nyumba hii ya Bwana. Wakati
mwingine ni vile vyumba vyenye furaha na shukrani ndivyo
vinavyotawala nafasi zilizopo ndani yetu. Ikiwa hivyo ndivyo
ilivyo kwako leo basi mfuate mbeba mshumaa hadi sehemu
ya furaha na kicheko. Ikiwa kwa upande mwingine ikiwa hii ni
siku ambapo chumba cha aibu na hasira kinatawala, basi ufuate
mbeba mshumaa mwingine hadi sehemu ya malalamiko na
manunguniko. Ikiwa mwili wako utahama kati ya kuwa na haja
ya kuguswa na haja ya kupumzika, basi utembelee vituo vyote
kile cha mwili, ujinsia na uhisia – na mahali pa mapumziko. Ama
ikiwa upo katika kipindi cha maisha yako unapoona kuwa kila
kitu kimekauka ndani yako, kana kwamba unazunguka ovyo
katika uwanda ulio kame, hivyo basi ufuate mbeba mshumaa
hadi kisima chenye maji yenye uhai au usafiri hadi mahali pen-
gine panapofaa ambapo utaweza tena kuinuka katika umaarufu
wako. Ama uchukue njia itakayokutoa toka sehemu ya mazun-
gumzo, ambapo unaweza kujifungua na kujiachilia mwenyewe
kwa mambo yote yanayokuzuia usikutane na wengine, hadi se-
hemu ya ushirikiano ambapo utapokea nguvu kwa kutiwa moyo
na wenzako. Kutoka hapo unaweza kuendelea mbele zaidi, ama
kwa wengine katika sehemu ya maombezi yenye kuombeana
na uwashaji wa mishumaa, ama unaweza kujitupa mwenyewe
uwanjani kupigania maisha bora katika mahali panapohusika.
Mwisho, fuata barabara inayoongoza kutoka vituo vyote hadi
MAHALI PA AJABU ambapo tunainua mikono yetu kama vyombo
vitupu na kupokea mkate na divai, ujasiri wa kuishi na nguvu ya
kutoka na kwenda ulimwenguni – pamoja na Mungu.
Namna hii tunakuwa salama. Tukiwa ndani ya nyumba ya Mungu
tukionana ana kwa ana na yeye Aliye Mtakatifu, tunaweza kuwa
vile tulivyo. Kila kitu kinawezekana kufanyika - kwa Mungu.
Kaa kimya kwa muda na ujisikie kile unachokihitaji leo. Labda
inatosha kutembelea kituo kimoja – ama utapenda kukaa tu ka-
tika viti vya kanisani wakati wote? Chochote ambacho ni sahihi
kwako bado ni sahihi tu.
Katika nyumba ya Mungu tupo huru.
Ndani ya Nyumba ya Mungu tunaishi nakutembea na kupata
uhai wetu.
Mahubiri Yaliyopendekezwa
58 SURA ZA MUNGU
Kila mwaka wakati wa majira ya baridi, kipindi cha faragha huan-
daliwa kwa ajili ya watu wanaoishi na VVU na UKIMWI pamoja
na wapendwa wao. Watu huja pamoja kutafakari, kuomba,
kuzingatia na kusaidiana – kwa ukimya na pia kwa kushuhudi-
ana. Huu ni mfano wa utaratibu wa ibada ya pamoja:
1. Nyimbo
2. Sala ya Asubuhi
Tuombe,
Mungu Bwana wetu
Tunakushukuru kwa ukimya huu
Katika ulimwengu uliojaa kelele na purukushani.
Asante kwa sababu upo hapa
Bwana, uende pamoja nasi katika siku mpya iliyo mbele yetu.
Hatujui ikiwa siku hii itangaa na kupendeza
Ama itakuwa imezingwa zingwa na iliyo chungu.
Lakini tunaamini na kutumaini kuwa wewe ni Mungu wa upendo,
Kwamba utaenda pamoja nasi kila siku hadi mwisho wa nyakati,
Ndiyo,hadi ndani ya umilele usio na mwisho,
Kwamba unatupenda na kutusaidia bila kujali kinachotokea.
Utusaidie tuwe na muda mzuri wa maombi leo
Utujalie kuyasikia mapigo ya moyo wako. Amina!
3. Somo la Biblia
: LUKE 24:13-35
4. Kutafakari
Tunaweza kufuata njia nyingi katika maisha yetu. Tunaweza
kuchukua njia kuu ama zile za pembeni. Tunaweza kuchukua
njia za mkato ama kuchukua mizunguko. Tunaweza kupotea
na kukengeuka. Tunaweza kusimama katika njia panda na ku-
kosa fikra ya kuchagua mwelekeo wa kufuata.
Tunaweza kufuata njia nyingi katika maisha yetu. Kati ya hizo
zingine hutuongoza katika njia isiyo na mpenyo wa kutokea.
Nyingine hutufikisha pale tunapotaka kufika. Na kisha vipo vijia
ambavyo hatujawahi kukanyaga miguu yetu, njia ambazo haz-
ijapitiwa, maeneo yenye fursa ambazo bado kuvumbuliwa.
Hapo zamani palikuwepo mtu aliyefikia mwisho wa safari
yake – mbinguni. Pamoja na Bwana aliona maisha yake yak-
ipita. Alifurahi alipoona nyakati za kupendeza na alilia alipoo-
na nyakati za kusiskitisha. Lakini aligundua ya kwamba katika
nyakati zote njema, kulikuwa na fungu lingine la nyayo pem-
beni mwa zile zake, kana kwamba kulikuwa na mwingine. La-
kini katika nyakati mbaya kulikuwa na nyayo za miguu miwili
zikipasua njia katika safari ya maisha.
Yule mtu alimwangalia Bwana na kumwuliza kwa kumkaripia,
“kwa nini ulikuwa nami tu pale kila kitu kilipokuwa rahisi nami
nikiwa na furaha? Kwa nini hukutembea nami wakati mambo
yalipokuwa mabaya zaidi?” Bwana akaligusa shavu lake na-
kumwambia “ Mtoto wangu mpendwa, wakati maisha yako
yalipokuwa hayavumiliki tena sikutembea pembeni mwako
bali nilikubeba.
Tunaweza kufuata njia nyingi katika maisha. Lakini muhimu
zaidi ya njia tunazochukua ni watu wanaotembea pembeni
mwetu, wenzetu tulio nao katika safari yetu. Yesu Kristo si tu
kiongozi wetu bali yeye ni mwenzetu. Hatua kwa hatua anat-
uongoza na anatusaidia katika mizigo yetu pale inapotuele-
mea. Yeye atatutegemeza, na kutuinua na kutuweka mabegani
mwake na kutubeba ikiwa tutwekwa chini kwa lazima. Amina!
5. Nyimbo
6. Amani
Amani ya Mungu inapokelewakwa kukumbatiana katika up-
endo wa kindugu.
Mwongozo wa Ibada wakati wa Faragha
Sala ya Asubuhi
Juu ya UkaribuDENMARK
SURA ZA MUNGU 59
Sala ya Mchana
1. Nyimbo
2. Maombi
Kama ilivyo kwa wanafunzi wako njiani kwenda Emmaus.
Nasi daima tunashindwa kuona
Kwamba ni wewe Yesu, uliyejiunga nasi safarini. Lakini pale
macho yetu yanapofunguka
Tunagundua kuwa ilikuwa ni wewe uliyeongea nasi siku
zote
Hata kama wakati mwingine tulikugeuka na hatukusikia
neno lolote ulilosema.
Lakini hiki ni kielelezo cha imani tuliyonayo kwako: kwamba
tujaribu kupenda na kusamehe pamoja na wewe
Ijapokuwa tumekuwa na mashaka, kwa sababu ya imani
yetu, wewe Yesu umekuwepo hapa daima, upendo wako
ukiwaka kwa kina kirefu ndani ya mioyo yetu.
Shukrani zetu zimfikie Mungu!
Amina!
3. Kusoma na Kutafakari
Luka 24:13 –35 ikisomwa polepole.
4. Ukimya Mfupi
Washiriki wanachagua neno ama sentensi kutoka masomo,
inayosambazwa kama kitambaa kilichorembwa kwa rangi
mchanganyiko na kutandikwa kanisani sakafuni.
5. Ukimya
6. Nyimbo
7. Baraka ya Haruni
hii itasomwa wakati wote wameshikana mikono: Bwana tu-
bariki na ututunze. Bwana ifanye sura yako in’gae juu yetu
na uwe na neema juu yetu. Bwana ainue hari yake juu yetu
na atupatie amani! Amina!
SURA ZA MUNGU
Pale ulipoketi Ukiwa na magamba ya
fedheha na uchafu
Wa mikono yako iliyo tupu bali imejawa na
makovu
Juu ya nafsi yako tupu na yenye makovu
Unasimulia hadithi yako na unahesabu
hasara uliyopata
Yule mtu aliyekuacha ama mtoto ambaye
ilibidi umwache
Sumu iliyofurika ndani ya mwili wako
Mto uliojaa ambao hakuna anayeweza
kuuzuia
Ambao hautaki kukoma katika kunguruma
kwake
Huku ikizipiga na kuharibu kingo zako zote
laini
Unasema nataka kufa Mimi sisemi kitu
Nina nyoosha mkono wangu na kuushika
mkono wako ulio mgumu na usio na raha
Sala ya Mchana
Kukaa Kimya na Kusikiliza
60 SURA ZA MUNGU
NA CARINA WØHLK
Tumeogopa sana kugusana sisi kwa sisi. Ninyi mlio na VVU kwa
kiwango kikubwa mmekutana na hofu hii ya kutokuwa karibu
na wenzenu katika mwili na nafsi yako – vyote pale wale wa-
sioambukizwa wamejiweka mbali nawe katika wasiwasi wao na
kutokujua kwao, na wakati ambapo ninyi wenyewe mmewasu-
kuma wengine mbali nanyi kwa sababu mmekuwa na uoga wa
kupuuzwa na kukataliwa.
Tumeogopa sana kugusana sisi kwa sisi, kwa sababu kugu-
sana kimwili kunaanika udhaifu wetu na utofauti wetu. Hivyo
tunawapiga butwaa watu kwa mbali badala ya kuwaruhusu
watukaribie. Tunajiepusha kushirikiana na wengine. Mara
chache sana tumejitokeza mbele na kueleza habari zetu hu-
susan kuwa sisi ni akina nani. Hii inahitaji kujisikia kwa dhati
ndani yetu na ndani ya wengine pia, inahitaji ukaribu kwa Mun-
gu anayetukumbatia na na anayetupenda kupita mipaka yote
ya ufahamu.
Katika faragha hii tumeangalia asili na umuhimu wa ukaribu.
Mbali na pilika pilika za maisha ya kila siku tumezingatia maneno
na fikra. Tumezungumza lugha ya maombi na tumekutana kila
mmoja na mwenzake katika ukimya. Sasa tunataka kutembea
kidogo na wanafunzi katika barabara inayoelekea Emmaus –ili
tuweze kudaka na kuelewa vizuri ukaribu wa kimungu.
Hadithi ya Emmaus inatupeleka hadi wakati na mahali – mahali
penye utupu – baada ya jeuri ya msalaba wa Kalvari.wawili kati
ya wanafunzi wa Yesu, wawili kati ya marafiki wawili wapendwa,
wapo njiani kuelekea katika kijiji cha Emmaus. Walikuwa katika
hali ya masikitiko makubwa huku wakienda. Ingawa ilikuwa ikin-
gali ni mchana, wao bado walikuwa gizani kabisa. Hawakuweza
kuiona njia ya kuepuka maumivu yao. Kwa niniYesu, ambaye
alikuwa mwema sana, kuufikia mwisho mbaya wa aina hii? Je
hakuwa ameahidi ya kuwa atakuwepo pale kwa ajili yao? Na kisha
anaenda akiwa amewatelekeza bila kujali. Hawaelewi chochote –
yaani hata yote yale ambayo imemlazimu Yesu kutaabika kwayo.
Hawaoni maana yoyote katika kisirani hiki.
Wanafunzi wa Yesu wamepotea. Wajipoteza wenyewe katika
kujisikia kwao kupoteza. Wamempoteze mtu waliyempenda.na
pia wamepoteza imani yao katika maneno yake. Wasingeweza
Mahubiri katika Ibada ya Faragha
Luka 24:13-35
kuamini tena ya kwamba yeye alikuwa yule aliyesema kuwa
ndiye –mkombozi na Mwana wa Mungu matarajio yao yote na
matumaini waliyokuwa nayo yalitoweshwa.
Walimfuata mtu waliyeamini kuwa ni njia ya kwenda mbingu-
ni – na kwamba njia hiyo ghafla imebadilika na kufikia mwisho
wake. Wamechanganyikiwa na kukata tamaa. Wameondoka
Yerusalemu kwa huzuni na mshangao. Mino’ngono ilidai japo
kwa ukweli fulani kuwa kaburi la Yesu lilikuwa tupu. Lakini hiyo
ilionekana kuwa si kitu cha kuamini, kwani kilikuwa chema
sana kuwa cha kweli.
Ghafla, mtu wa tatu alifika katika eneo la tukio. Huyu alikuwa
ni Bwana aliyefufuka, Yesu Kristo. Tunalijua hilo. Lakini wa-
nafunzi hawakumtambua. Yote wanayoyaona ni mgeni tu.
Hawakukatishwa tamaa wanachokiona ni njonzi.
Mtu aliwauliza kwa nini wapo chini sana. Wanaonekana kana
kwamba wamepoteza rafiki yao wa karibu…wanafunzi wal-
imweleza nini kilitokea Yerusalemu siku chache zilizopita. Wa-
namweleza jinsi ndoto zao zote zilivyoharibika na kuanguka
na sasa zimelala chini ya msalaba.
Kwa uwezo mkubwa, yule mtu anawatafsiria unabii wa kale.
Anawaelezea jinsi ilivyoandikwa katika maandiko kuwa im-
empasa Mwana wa Mungu ateswe na kisha kuchukuliwa juu
katika utukufu. Anajaribu kuweka sawa maoni ya wanafunzi
juu yamambo yaliyotokea. Wanapokaribia kijiji walichokuwa
wakienda, yule mgeni alitangulia mbele kidogo kana kwamba
alikuwa akiendelea. Lakini wanafunzi, waliofurahia kuwa naye
na pia maneno yake yenye ufahamu, walimwomba akae na
kula pamoja nao. Wakati wa chakula, muujiza ulitokea. Mag-
amba yalidondoka kutoka katika macho ya wanafunzi.
Kwa muda mfupi tu wakati Yesu akiumega mkate, Karamu ya
Bwana ikawa imefanyiwa marejeo – lakini kwa namna nyingine.
Sasa imekuwa wazi kuwa yule anayetoa ndiye anayepewa.
Yesu Kristo amekufa na kufufuka. Mwili wake na damu yake
ni moja pamoja na mkate na divai.Ni katika ushirika huu wa
kila siku, na si barua isiyo na uhai inayowapa wanafunzi imani
katika ufufuo. Ni kule kuambatana, na si mazungumzo, kina-
chofungua akili zao. Wanafunzi wanamwona Yesu akiwa hai
katika mwili kule barabarani, lakini haiwaingii vizuri. Wanasi-
Mungu anayetugusaDENMARK
“Bwana, uwe pamoja nasi hapa,
karibu yetu wakati siku inapochomoza
na jua na mwanga wa nyota unapozizima
katika virindi vya giza la usiku.
Roho yako isituache kabisa hadi
utakapotupokea mbinguni”
Anima!
B.S. INGEMAN, NO. 366. KATIKA KITABU CHA NYIMBO CHA KIDENMARK CHA 1966
SURA ZA MUNGU 61
kia anapotafsiri maandiko. Lakini hawamsikilizi kwa makini. Si
kwamba wana mioyo migumu tu, bali wao ni wagumu kusikia
na wazito kujifunza.
Ni wakati ule tu wanapokuwa wanajiandaa kula, muda wana-
poketi pamoja na Yesu chakulani, ndipo wanapogundua nam-
na gani mateso na utukufu vinaelea katika hadithi hii .Ufunuo
ni kuwa na macho yako wazi.
Katika furaha ya kutambuliwa, Yesu anatoweka. Njia zao
lazima zipishane kwa sasa, lakini wanafunzi hawasumbuliwi
tena na wasiwasi wa kutenganishwa na Yesu. Wamemwona na
kugundua kuwa yeye ni nani. Wamemtambua na kumkubali
kuwa yeye ni Mwana wa Mungu. Na kwamba anawaweka huru
warudie maisha yao na uhusiano na watu wengine. Mitume
waliokuwa wamekufa ganzi sasa wamepata nguvu mpya na
kuwa watendaji.
Hali za kimaisha ambazo hazitabiriki pia hazibadiliki haraka,
lakini si ilivyo kwa imani ya wanafunzi. Hawana majuto tena.
Hawapotezi mwelekeo tena. Sasa wanaweza kuiona maana ya
kile kilichotokea.
Hadithi ya safari kuelekea Emmaus ni hadithi ya mchakato wa
huzuni. Wanafunzi wanaenda katika safari ya ndani na ile ya nje.
Wanasafiri kutoka mashaka na kukata tamaa hadi utendaji.
Tunapowapoteza wale tuliowazoea, wakati vitu vinapopo-
romoka badala ya kuendelea mbele, wakati mioyo yetu inapo-
vunjika na hakuna kitu cha kutushikilia, tunaelemewa na hisia
za kutokuwa na maana na kukata tamaa. Tunakuwa kama wale
wanafunzi wawili wakielekea Emmaus. Tunajiona wapweke
na tuliotelekezwa na Mungu, na ndipo tunaililia mbingu “kwa
nini?”
Lakini hata hivyo hatuwezi kuiona maana mahali pasipo na
maana, ingawa pia hatuwezi kujenga mshikamano pale palipo
na maanguko, hatukuachwa peke yetu. Ipo njia ya kushinda
mateso. Yesu Kristo atajiunga nasi katika njia hiyo – hata pale
tunapomwona kama mgeni tu.
Yeye atatutoa kutoka katika giza la mashaka na kukata tamaa.
Atatupa ufahamu wa ndani ili tuweze kuiona hali yetu waziwa-
zi. Atatumwagia upendo wake na kutujaza matumaini. Matu-
maini huleta nuru katika maisha. Matumaini huyaona maisha
yetu jinsi yalivyo – wakati huo huo ikiangalia mianya ya kuleta
mabadiliko.
Tunaogopa sana kugusana sisi kwa sisi. Lakini tunaye Mungu
anayetugusa kwa uzuri wake mkubwa sana wa milele. Tu-
naogopa sana kukaribiana. Lakini tunaye Mungu ambaye huta-
ka tugusane naye: Mungu ambaye – kwa maana halisi- huja
ndani ya ngozi yetu, kwa sababu anatupenda.
Tunaogopa sana kugusana sisi kwa sisi. Lakini katika maisha
yetu na uhusiano baina yetu, Mungu huja karibu – hata kama
hatutaki chochote kutoka kwake na kinachomhusu. Yeye huja
karibu kwa upendo unaovuka mipaka yetu na kutuelemea kwa
nguvu zake. Amina!
Mpendwa Mungu Baba,
Asante sana kwa kuwa leo tulikuwa hapa
pamoja nawe na kila mmoja wetu
katika faragha hii.
Tunaomba:
Uiweke mioyo yetu tayari kuupokea
upendo.
Uyaweke macho yetu wazi
Kupokea ufunuo wako
Tuimarishe katika imani
Kwa kuwa wewe ni Bwana
Juu ya uzima na mauti
Juu ya walio hai na walio wafu pia
Wewe ambaye u sala moja mbali,
Uwe karibu nasi daima!
Amina!
Na sasa tuombe kwa muda mfupi tukiwa kimya…
Sasa mnaweza kusimama, na pamoja na mitume tunajiombea
na kumwombea kila mmoja.
Neema ya Bwana wetu Yesu kristo, Upendo wa Mungu Baba, na
ushirika wa Roho Mtakatifu
Uwe pamoja nasi sote
Amina!
SURA ZA MINGU
62 SURA ZA MUNGU
Mungu, uliumba ulimwengu mmoja,usio na mipaka na migawanyiko.
Tunatubu hakika kwamba ni kwa sababu yetu ulimwengu umepasuka na kumeguka.
Tusaidie kurejesha umoja ulimwenguni,
Na utuunganishe katika mapambano ya kuwapatia watu wote wenye VVU fursa sawa na haki wanazopate watu wengine.
Mungu, tunaomba kwa ajili ya nchi zile ambazo mamlaka yamefumba macho yao na kutouoona ukweli unaodhihirishwa na VVU na UKIMWI.
Tupatie ujasiri wa kuziweka wazi, ili kwamba hakuna mwingine yeyote anayehitaji kutolewa kafara katika madhabahu ya kukataa.
Tunauwasha mshumaa kwa ajili ya umoja wa wanadamu wote.(Mshumaa unawashwa)
Mungu tupatie ujasiri ili tufanyie kazi umoja
Mungu wewe ambaye ni chanzo cha utu na heshima yetu.
Utuonyeshe wajibu tulionao kwa kila mmoja wetu.
Utusaidie kujenga ulimwengu ambapo hakuna atakayefaidika na mateso na huzuni ya watu wengine,
ulimwengu ambapo watafiti, wazalishaji wa madawa na sisi wenyewe tutakuwa makini kufahamu wajibu wetu wa kimaadili.
Mungu tunaoomba kwa ajili ya ulimwengu ambapo maisha ndio hoja kubwa –si takwimu na faida.
Tunawasha mshumaa kwa ajili ya vipaumbele sahihi katika jamii. (Mshumaa unawashwa)
Mungu utupatie ufahamu wa ndani kutendea kazi haki
Mungu, wewe uliyetuumba sawa bila kujali shughuli zetu za kutafuta maisha, ngazi za kijamii, utaifa ama mielekeo yetu ya ujinsia.
Utuunganishe dhidi ya mipaka yote ya kijamii tuliyoiweka.
Tunaomba kwa ajili ya waliojiajiri kutoa huduma ya ngono wanaonyonywa na kuishi chini ya ugumu wa kazi yao.
Tunaomba kwa ajili ya wale wote wanaopambana kwa ajili ya haki ya kujilinda wenyewe dhidi ya VVU.
Hao tunaomba wasikilizwe na kwamba wapate wasemaji wenye nguvu na ndugu halisi katika mapambano.
Tunawasha mshumaa kwa ajili ya dunia ambayo haitakuwa na sisi na wao.(Mshumaa Unawashwa).
Mungu tupatie mshikamano ili tuwe sauti kwa wasio na sauti.
Kuwasha Mishumaa
SURA ZA MUNGU 63
Mungu, unatuhudumia na umetuita tumtumikie kila mmoja bila kuhesabu gharama.
Imarisha mwelekeo wetu na utayari wetu kumhudumia kila mmoja wetu.
Tunaomba kwa ajili ya waajiriwa katika sekta za afya na za kijamii na kwa waliojitolea wanaofanya kazi miongoni mwa watu wanaoishi na VVU.
Wasaidie kujua kuwa wanakutumikia wewe, Oh Bwana Mungu, na uwape ustahimilivu.
Tunawaombea marafiki, jamaa na wapenzi wa wale ambao wana VVU, na wale waliofiwa kutokana na UKIMWI.
Tunawasha mshumaa kwa ajili ya faraja kwa wale wanaomboleza. (mshumaa unawashwa)
Mungu utupe moyo wa huruma wa kuwahudumia wale wanaoteseka.
Mungu, umetuumba sisi sote kwa mfano wako na umetufanya kuwa waumbaji wenza wa ulimwengu wenye haki.
Utusaidie katika mapambano dhidi ya ubaguzi, ujinga, na upumbavu,
ili kwamba muda mfupi ujao tuweze kuona milima na mabonde ya ulimwengu unaowapatia heshima inayostahili wote wanaoishi na VVU.
Mungu, uwakaribie wale ambao wamepoteza ajira zao, marafiki wao, familia na wapenzi wao kwa sababu ya hali yao ya VVU.
Tunawasha mshumaa huu kwa ajili ya ulimwengu tukiwa na heshima na taadhima kwa watu wote. (Mshumaa unawashwa)
Mungu utupatie dira tutakayowashirikisha
Wale waliopoteza matumaini yole.
Mungu ambaye unatujua na kuyasikia maumivu yetu:
Tunajua kwamba hakuna kitakacho tutenganisha na upendo wako.
Tunaomba kwa ajili ya watu wote walio na VVU na wote ambao wameathiriwa na UKIMWI.
Ambao wanaishi na shauku nyingi, wakiwa na majonzi na kujisikia kupotelewa.
Mungu uliyeumba watu wote katika mfano wako, utusaidie kuwapo pale walipo wenzetu wanaoteseka.
Tunawasha mshumaa kwa ajili ya dunia ambapo tunashirikiana mateso na kuchukuliana mizigo. (Mshumaa unawashwa)
Mungu tupe upendo wako wa ziada ili tuweze kuelewa kwa kina zaidi maumivu na mategemeo ambayo ni sehemu ya binadamu.
Kumpenda Mungu
Tumeshirikiana na wewe katika
maumivu yetu na kupoteza kwetu.
Wewe ni tumaini letu
Katika mateso yetu na kuhitaji kwetu
Tunaomba tupate amani katika kuamini
kwamba wewe ni mwenye uwezo
miongoni mwa walio wadhaifu.
Utuonyeshe basi kuwa nguvu
zako zinaweza kudhihirika katikati
ya udhaifu wetu usio na kifani
64 UTANGULIZI
BabaYetu Uliye Mbinguni
Katika siku hii ya UKIMWI Duniani
tunakuja kwako na kila kitu
kinacho tuponda ponda na kutusukuma
Tunaomba:
Uwe pamoja na wanao na binti
wala wote wanaoishi na VVU na UKIMWI.
Watoto wamekuwa yatima,
wanawake wamekuwa wajane.
Vizazi vinatoweka.
Mungu utupe nguvu ya kukabili
wimbi la UKIMWI katika
upana na ukubwa wake
Tuinue juu,
ili tuweze kwenda ulimwenguni
na kupambana dhidi ya UKIMWI
na ubaguzi wenye jeuri kubwa.
Tusaidie kukabiliana na kujitangazia haki kwetu
binafsi na mawazo yetu yasio sahihi kuhusu VVU
na wale walioambukizwa.
Fungua mioyo yetu kwa
ajili ya mabadiliko na upatanisho.
Katika wema wako Mungu
wape mapumziko wale
waliofariki kutokana na
kwa wale wanaoishi na na VVU
Hili tunaliomba katika
Jina la Yesu Kristo
Bwana wetu.
Sala Siku ya UKIMWI Duniani
Mwili Mmoja ilianzishwa kwa pamoja na Kikundi cha Kuweka
Mikakati kilichokutana Lusaka 2004.
Kutoka Zambia: Japhet Ndlovu, Joy Lubinga, Munalula
Akakulubelwa, Rose Malowa. Kutoka Msumbiji: Dinis Matso-
lo, Elias Massicame. Kutoka Norway: Jan Bjarne Sodal, Estrid
Hessellund, Steinar Eraker. Kutoka Denmark: Carina Wøhlk,
Birthe Juel Christensen. Kutoka EHAIA: Sue Parry
WALIOCHANGIA KITABU CHA 2
ZAMBIA
Mch. Japhet Ndhlovu, Katibu Mkuu wa wa Baraza la Makanisa
nchini Zambia. Akishirikiana na Duara za Tumaini. Joy Lubinga
Mshauri Nasaha Masuala ya Akili na Jamii, Duara za Tumaini.
Ackim Sakala. Mwalimu, Mwana harakati UKIMWI+. Duara
za Tumaini. Askofu Luckson Chibuye, Mch. Pearson Banda.
Mratibu VVU na UKIMWI kutoka Kanisa la Reformed, Zambia.
MSUMBIJI
Mch. Elias Zacarias Massicame, Mratibu wa Kitaifa wa VVU/
UKIMWI katika Baraza la Makanisa Msumbiji akishirikiana
na Mch. Dinis Matsolo, Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa
Msumbiji
DENMARK
Mch. Birthe Juel Christensen, Afisa Habari, DanChurch Aid.
Denmark. Mch. Carina Wøhlk, Chama cha Taifa cha UKIMWI
cha Kilutheri. Preben Bakbo Sloth, HIV+ activist. Elizabeth
Knox-Seith, Mwana Soshiolojia Mtamaduni
NORWAY
Jan Bjane Sodal, Mratibu wa Mradi wa VVU/UKIMWI wa
Baraza la Kikristo Norway akishirikiana na watu waishio
au walioathiriwa na VVU wanaokutana Aksept – Kituo cha
kanisa Mjini Oslo. Norway: Helge Fisknes, Oslo City Mis-
sion. Steinar Eraker, former pastor at Aksept, Mch. Elisabeth
Tveito, Mjumbe wa Bodi katika Baraza la UKIMWI Norway,
Mhariri-mwenza, na Estrid Hessellund, wa Toleo ‘Positive:
Branding, Sexuality, HIV and AIDS. Verbum, Norway, 2005
uk 16 na 29’
TUNASHUKURU KWA RUKHSA YENU YA KUTUMIA
YALIYOMO KTIKA TOLEO HILI LA SASA
MwiliMmoja