Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah · Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma mwenye kurehemu....

76
1438 Masomo katika umuhimu wa Tawheed. Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah > Kiswahili - Swahili -سواحيلية ال< Mtunzi: Imamu Sheikh Saleh bin Fauzan Al-Fawzan. Mfasiri: Yasini Twaha Hassani. Abubakari Shabani Rukonkwa. Kimerejewa na: Yunus Kanuni Ngenda

Transcript of Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah · Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma mwenye kurehemu....

  • 1438

    Masomo katika umuhimu wa

    Tawheed. Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah

    > Kiswahili - Swahili -السواحيلية <

    Mtunzi:

    Imamu Sheikh Saleh bin Fauzan Al-Fawzan.

    Mfasiri:

    Yasini Twaha Hassani.

    Abubakari Shabani Rukonkwa.

    Kimerejewa na:

    Yunus Kanuni Ngenda

  • 1

    خمترص كتاب األصول اثلالثة

    صالح بن فوزان الفوزان فضيلة الشيخ: ل

    :ترمجة

    ياسني طه حسن

    أبوبكر شعبان ركونكوا.

    :راجعة م

    يونس كنون نغندا

  • 2

    MASOMO KATIKA UMUHIMU WA

    TAWHIID

    Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah

    Utangulizi:

    Kaanza kwa kusema Bismi llahi Rrahmani Rrahim; Kwajina la

    Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehma mwenye kurehemu.

    Ameanza Mwenyezi Mungu Amrehemu risala hii kwa jina la

    Mwenyezi Mungu mwingi wa rehma mwenye kurehemu, kwa kufuata

    kitabu cha Mwenyezi Mungu mshindi na mtukufu, kwa sababu macho

    yako yakiangalia ndani ya msahafu na kabla ya kila sura kuna (Bismi

    llahi Rrahmani Rrahim).

    Kuanzia neno hili katika risala na katika vitabu nikufuata kitabu

    cha Mwenyezi Mungu mshindi na mtukufu, vilevile nabii Muhammad

    (s.a.w) Alikua -ana mwambia muandishi- a'ndike mwanzo wa kila

    barua wakati anapo watumia viongozi na maraisi na waliyoko mbali

    ana walingania katika Uislamu, anaanza kuandika:

    Kwajina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma mwenye

    kurehemu.

    Na alikua Mtume (s.a.w) anaanza mazungumzo yake na maneno yake

    kwa: Bismi llahi Rrahmani Rrahim, yaonyesha kuanza kwa Bismi

    llahi Rrahmani Rrahim ni sunna ya Mtume (s.a.w), vilevile Nabii

    Sulaiman (s.a.w) alipo muandikia Malkia -Mfalme wa saba' Yemen-

    ameanza kuandika kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma

    mwenye kuruhemu: (Malkia akasema: Enyi wahishimiwa! Hakika

    nimeletewa barua tukufu* Imetoka kwa Sulaiman nayo ni:

    Kwajina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma Mwenye kurehemu*

    Msinifanyie jeuri, na fikeni kwangu nanyi mmekwisha kuwa wenye

    kusalimu amri).

    (An-Naml: 29-31).

    Inatakiwakuanza na jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma

    Mwenye kurehemu, katika kila jambo lenye umuhimu, na katika kila

    kitabu chenye umuhimu na thamani, na katika kila risala.

  • 3

    Kwa sababu hii wale ambao hawaanzi kwenye vitabu vyao na risala

    zao kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma Mwenye

    kurehemu, hao wameacha sunna ya Mtume na kuto kufuata kitabu cha

    Mwenyezi Mungu Mshindi na mtukufu, huenda kwa sababu hiyo

    vitabu vyao na risala zao hazina baraka na ndani yake hakuna faida;

    kwa sababu ikiwa hakuna jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehma

    Mwenye kurehemu huondolewa faida.

    Risala ya kwanza Maswala manne ambayo yameambatana na Surati

    Al-Asr,

    ILIMU Tambua Mwenyezi Mungu akurehemu.

    Hili ni neno linalo ashiria umuhimu wa mada, anapo sema: Tambua:

    lina maana ya kwamba atakacho kwambia nimuhimu sana.

    MWENYEZI MUNGU AKUREHEMU: Hii ni dua kwa mtafutaji wa Ilimu, anawaombea watafutaji wa elimu

    Mwenyezi Mungu awarehemu, na awape rehma zake, maneno haya

    ndani yake kuna upole kutoka kwa mwalimu kwenda kwa

    mwanafunzi, na kwamba yeye anaanza kwa maneno mazuri na dua

    njema, mpaka awaathiri kwa maneno hayo na wamuelekee mwalimu

    wao.

    Lakini mwalimu akianza maneno kwa ukali na maneno yasio faa

    jambo hili lina wakimbiza -wanafunzi-, wajibu wa mwalimu na wale

    wanao lingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, na nijuu ya yule anae

    amrisha mema na kukataza mabaya kuwa mpole kwa yule anae ongea

    nae, kwa kumuombea dua na kumsifu kwa maneno laini, kwani hili

    lapelekea kukubali.

    Lakini mtu mwenye kiburi mjeuri, yeye ana maneno maalumu,

    Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

    (Wala msijadiliane na watu wa kitabu ila kwa njia iliyo nzuri kabisa,

    isipo kuwa wale walio dhulumu miongoni mwao. Na semeni:

    Tumeyaamini yaliyoteremshwa kwetu na yaliyoteremshwa kwenu. Na

    Mungu wetu na Mungu wenu ni Mmoja. Na sisi ni wenye kusilimu

    kwake).

    (Al-Ankabut: 46).

  • 4

    Wake walio dhulumu nafsi zao miongoni mwa walio pewa kitabu,

    wakafanya ujeuri na kiburi, hao hawalinganiwi kwa upole, wao

    hulinganiwa kwa ukali. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

    (Ewe Nabii! Pambana na makafiri na wanaafiki, na wakazanie. Na

    makaazi yao ni Jahannamu, na huo ndio mwisho mbaya).

    (At-Tawba: 73).

    Wanaafiki hawajadiliwi kwa silaha, lakini hujadiliwa kwa hoja na

    maneno makali, nakuwatahadharisha watu wasiwe karibu nao, na

    Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na uwaambie maneno ya

    kuathiri na kuingia katika nafsi zao).

    (An-Nisaa: 63).

    Hao wana maneno yao maalumu; kwa sababu wao ni wapingaji

    wenye viburi, wala

    hawataki haki bali wanataka kuwapoteza watu, hao huambiwa kwa

    wanayo stahiki.

    NILAZIMA JUU YETU KUJIFUNDISHA MAMBO MANNE.

    Jambo hili sio hiyari, wala sio lenye kupendeza -ukitaka unafanya

    hukutaka unaacha- isipo kua ni lazima hasa.

    Tutapo acha kujifundisha mambo haya kwa hakika tuna pata

    madhambi, kwa sababu jambo hili ni lazima, hakusema: ni hiyari

    kwetu au yapendeza kwetu, lakini kasema: ni lazima kwetu, na jambo

    lazima maana yake: mwenye kuliacha hupata dhambi, na kwa sababu

    elimu haipatikani isipo kuwa kwa kujifundisha, na kujifundisha kuna

    hitaji umuhimu na juhudi na muda, na kuna hitaji ufahamu na

    kuhudhurisha moyo, huku ndiko kujifundisha.

    Mwenyezi Mungu Anasema katika Suratul Asr: kwa jina la Mwenyezi

    Mungu Mwingi wa rehma mwenye kurehemu (Naapa kwa Zama!*

    Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara* Isipokuwa

    wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na

    wakausiana kusubiri).

    (Al-Asr: 1-3).

  • 5

    MAS'ALA MANNE: yaani upekuzi, yameitwa mas'ala; kwa kuwa mambo hayo nilazima

    kuulizwa na kutiliwa umuhimu.

    JAMBO LA KWANZA: ILIMU. Ilimu: makusudio ya ilimu hapa ni elimu ya kisheria; kwa sababu

    ndio ambayo ni lazima kujifundisha, na mas'ala haya ni lazima

    kujifundisha kwa kila Muislam, mwanamume au mwanamke, alie

    huru au mtumwa, tajiri au maskini, mfalme au raiya. Kila Muislam ni

    lazima kwake kujifundisha mas'ala haya manne.

    Na hili ndio linaloitwa na wanachuoni Ulazima waki pekee, ndio

    ambao ni lazima kwa kila mmoja katika Waislam, swala tano kwa

    wanamume na wanawake, na swala ya jamaa misikitini kwa

    wanamume. Jambo hili ni lazima kwa kila Muislam kujifundisha, kwa

    sababu hiyo alisema: ni lazima juu yetu, na hakusema: ni lazima kwa

    baadhi yetu, ila kasema: ni lazima juu yetu, yaani sisi Waislam, hii

    nikatika elimu ambayo ni lazima kwa kila mtu; kwa sababu elimu zipo

    namna mbili: Jambo la kwanza ambayo ni lazima kwa kila mtu

    kujifundisha, hakuna udhuru kwa asiye jifundisha, nayo niile ambayo

    haisimami dini bila yenyewe, mfano nguzo za Uislamtano ambazo ni:

    A.Shahada mbili,

    B.kusimamisha Swala,

    C.kutoa Zaka,

    D.kufunga Mwezi mtukufu wa Ramadhani,

    E. Kuhiji nyumba ya Mwenyezi Mungu,

    Haifai kwa Muislam kuto jua mambo haya ni lazima kujifundisha.

    Kwa sababu kujifundisha maana ya Shahada mbili ndiko kujifundisha

    Tauhidi, anajifundisha Muislam tauhidi ili aifanyie kazi, na

    ajifundishe yanayo kwenda kinyume na tauhidi ili ajiepushe nayo,

    haya ndio mafungamano ya Shahada mbili, vilevile ajifundishe nguzo

    za swala na sharti zake, na yalio yalazima ndani ya swala, na sunna za

    swala.

    Vilevile ajifundishe hukumu za zaka, na ajifundishe hukumu za funga,

    na ajifundishe hukumu za hija, anapotaka kuhiji ni lazima ajifundishe

  • 6

    hukumu za hija na hukumu za umra, ili atekeleze ibada hizi katika njia

    ilio amrishwa.

    Na kipengele hiki hakuna udhuru kwa yeyote kuto kijua, nacho

    kinaitwa ulazima wa kila Muislam.

    Sehemu ya pili katika vigawanyo vya elimu: nayo ni tofauti na elimu

    ya kisheria ambayo umma unaihitaji kwa ujumla wake, nasio kila mtu

    huihitaji, mfano hukumu za kuuza na kununua na hukumu za

    muamala, na hukumu za kutoa wakfu,na mirathi na usia, na hukumu

    za kuoa, na hukumu za makosa ya jinai, mambo haya nilazima kwa

    umma; lakini sio lazima kwa kila mtu kujifundisha, isipokuwa watapo

    jifundisha wenye kutosheleza na malengo yakatimia miongoni mwa

    wanachuoni yatosha; jambo hili linaitwa: faradhi kifaya, wakifanya

    baadhi ya watu madhambi huondoka kwa wengine, na watapo liacha

    wote basi hupata dhambi wote.

    Ilimu ya lazima ndio ambayo ataulizwa mja siku ya kiyama, kwa nini

    hukujifundisha? Kwa nini hukuuliza? Ilimu ambayo ataisema pindi

    atapo wekwa ndani ya kaburi: Mola wangu ni Mwenyezi Mungu, na

    Uislam ndio dini yangu, na nabii wangu ni Muhammad (s.a.w) jambo

    hili laokoa, ataambiwa: umejifundisha wapi? Atasema: nimesoma

    kitabu cha Mwenyezi Mungu na nikajifundisha.

    Ama Yule alie jitenga mbali na elimu hiyo kwa hakika atapo ulizwa

    katika kaburi lake atasema: hahahaha sijuwi niliwasikia watu

    wakisema jambo Fulani nami nikalisema.

    Mtu kama huyu atawashiwa moto ndani ya kaburi lake -Allah

    atunusuru- na kaburi litambana hadi mbavu zake hupishana, na kaburi

    lake huwa ni shimo miongoni mwa mashimo ya moto wa Jahannam;

    kwa sababu yeye hakutaka kujifundisha wala kusoma, ataambiwa:

    (Hukutaka kujifundisha wala kusoma).

    Kapokea hadithi hii Imam Bukhari kwa ufupi kwa hadithi ya Anas

    (1338) na kaipokea pia Imam Muslim kwa ufupi hadithi ya Anas (r.a)

    (2870).

    Na kaipokea Abuudaud kwa hadithi ya Bara' bin A'zib (r.a) kwa urefu

    (4752).

  • 7

    Yeye hakujifundisha, wala hakuwafuata wanachuoni, bali yeye

    kapoteza uhai wake, huyu ndio ambae atakua sehemu mbaya -Allah

    atunusuru.

    ILIMU: Hii ndio ilimu ya kisheria, kinacho takiwa kwa ujumla wetu

    na mmoja mmoja nako nikumjua Mwenyezi Mungu kwa Majina yake

    na Sifa zake, na kujua haki zake juu yetu, nayo ni Kumuabudu yeye

    peke yake hana mshirika katika u'ngu wake, jambo la kwanza

    kulitambua mwanadamu ni kumjua Mola wake Mtukufu, na namna ya

    kumuabudu.

    NA KUMJUA MWENYEZI MUNGU, NA KUMJUA MTUME

    WAKE.

    KUMJUA MWENYEZI MUNGU: Vipi mja atamjua Mola wake? Atamjua kwa alama zake na viumbe

    wake, miongoni mwa alama za kumjua kwake: usiku na mchana, na

    katika viumbe vyake: jua na mwezi, kama tunavyo bainisha hapa kwa

    matakwa ya Allah.

    Hujulikana Mwenyezi Mungu kwa alama zake za kidunia na Aya zake

    za qur-ani. Anapo soma qur-ani, humtambua Mwenyezi Mungu

    Mtukufu kwamba yeye ndio ambae kaumba mbingu na ardhi, naye

    Mwenyezi Mungu ndie ambae kavifanya kuwa vyepesi vilivyoko

    mbinguni na ardhini, naye Mwenyezi Mungu ndie ambae Ana huisha

    na kufisha, naye nimuweza juu ya kila kitu, naye ni Mwingi wa rehma

    mwenye kurehemu, Qur-ani ina mtambulisha Mwenyezi Mungu

    Mtukufu, naye Mwenyezi Mungu ndie ambae Ametune'mesha ne'ma

    zote, naye Mwenyezi Mungu ndie Alie tuumba na kuturuzuku, utapo

    soma qur-ani utamjua Mola wako Mshindi na Mtukufu kwa Majina

    yake na Sifa zake na vitendo vyake.

    Na utakapo angalia katika hii dunia utamtambua Mola wako Mtukufu

    kama yeye ndie alie umba, na akafanya wepesi katika huu ulimwengu

    na akaupitisha kwa hikma yake na kwa Ujuzi wake, Hii ndio Elimu ya

    kumjua Mwenyezi Mungu Mtukufu.

    NA KUMJUA MTUME WAKE: Yeye ni Muhammad (s.a.w) kwa sababu yeye ni Mwenye kufikisha

    niaba ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na yeye niwakati baina yetu na

  • 8

    Mwenyezi Mungu Mtukufu katika kufikisha ujumbe, hapana budi

    kumjua, unafahamu yeye ni nani? Unafahamu ukoo wake?

    na ujuwe mji wake, na ujuwe aliyo kuja nayo (s.a.w) unafahamu

    namana Wahyi ulivyo anza kushuka? Na namna alivyo simama katika

    kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu katika mji wa

    Makkah na Madina, unajua hestoria ya mjumbe wa Mwenyezi Mungu

    (s.a.w) japo kwa ufupi?.

    Mtume (s.a.w) yeye ni Muhammad bin Abdullah bin Abdul muttwalib

    bin Hashim bin Abdi manafi mpaka mwisha wa nasabu ya mtume

    mtukufu ambayo inaishia kwa NaBii Ibrahim (s.a.w), na unajua

    namna alivyo ishi kabla ya utume, na namna alivyo jiwa na wah'yi

    kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na nini alicho fanya (s.a.w)

    baada ya kupewa utume, utayajua yote hayo kwa kusoma hestoria

    yake (s.a.w). na haifai kwa Muislam kutomjua mtume (s.a.w) vipi

    unamfuata mtu hali yakua humjuwi?! Haiingii akilini.

    NA KUIJUA DINI YA KIISLAM. Kuijua dini ya kiislam: ambayo ndio dini ya huyu Mtume (s.a.w) bali

    ndio dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ambae kawaamrisha kwa dini

    hiyo waja wake, naye ndio ambae amekuamrisha kuifuata, na wewe

    watakiwa kuifuata, hapana budi kuijua hii dini, na Uislam ndio dini ya

    Mitume wete. Mitume wete dini yao Uislam kwa maana ya ujumla,

    yeyote alie mfuta Mtume miongoni mwa Mitume huyo ni Muislam

    mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu mwenye kumfuata yeye,

    mwenye kumpwekesha yeye.

    Huu ndio Uislam kwa maana ya ujumla, hakika ni dini ya Mitume

    wote, Uislam nao ni kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu kwa

    tauhidi, na kumfuata yeye kwa kutii, na kujiepusha na ushirikina na

    watu wake.

    Ama Uislam kwa maana yake halisi niule ambao amemtuma nao

    Mwenyezi Mungu Mtume wake Muhammad (s.a.w) kwa sababu

    baada ya kutumwa Mtume (s.a.w) hakuna dini isipokuwa dini yake

    (s.a.w), na Uislam umehusishwa katika kumfuata yeye (s.a.w)

    haiwezekani Yahudi akasema: Mimi ni Muislam, au Naswara aseme:

    Mimi Muislam baada ya kutumwa Mtume (s.a.w) haliyakua hamfuati,

    Uislam baada ya kutumwa Mtume (s.a.w) ni kumfuata, Amesema

    Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda

  • 9

    Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu

    atakupendeni.

    )Al-Imran: 31).

    Huu ndio Uislam kwa maana ya ujumla na kwa maana yake halisi.

    KWA DALILI. Kwa dalili: sio kwa kuiga lakini kwa dalili katika Qur-ani na Sunna,

    hii ndio elimu.

    Amesema Ibnul-QaYyim katika kitabu chake Al-kafiyatu shafiya:

    Ilimu kasema Mwenyezi Mungu kasema Mtume wake kasema

    Swahaba hao ndiyo wajuzi Siyo elimu inayo sababisha tofauti za

    kijinga kati ya Mtume na maoni ya Fulani, hii ndio elimu.

    Elimu ni ile elimu ya kitabu(Quraan) na sunna, na kuhusu maneno ya

    wanachuoni yenyewe husherehesha na kuweka wazi zaidi maneno ya

    Mwenyezi Mungu na maneno ya Mtume wake (s.a.w)

    Na kwa hakika ndani ya maneno hayo au baadhi yake huwa kuna

    makosa.

    KUIFANYIA KAZI ELIMU JAMBO LA PILI: KUIFANYIA KAZI. Kuifanyia kazi, maana yake: kwa elimu kwa sababu mwanadamu

    anafundisha na ana jifundisha hapana budi kuifanyia kazi elimu yake,

    elimu bila matendo itakua ni hatari kwa mwenye nayo, haiwi elimu

    yenye manufaa ila kwa matendo, ama Yule alie jifundisha na

    hakuifanyia kazi elimu yake huyo kakasirikiwa; kwa sababu yeye

    kaijuwa haki na akaiacha kwa elimu.

    Mtunzi anasema: (Na Mwanachuoni hakuifanyia kazi elimu yake

    Ataadhibiwa kabla ya wenye kuabudia Masanamu).

    Na jambo hili limetajwa kwenye hadithi tukufu: (Mtu wa mwanzo

    kuingizwa katika moto siku ya kiyama, Mwanachuoni ambae

    hakuifanyia kazi elimu yake(.

    Kapokea hadithi hii Imam Tirmidhi (2382).

    nayo ni hadithi ndefu ndani yake: (Hao wenye sifa tatu ndio wa

    mwanzo kabisa kuingizwa katika moto siku ya kiyama), hadithi ya

    Abaa huraira (r.a).

  • 10

    Elimu imeambatanishwa na vitendo, na vitendo ndio matunda ya

    elimu, elimu bila vitendo ni kama mtu bila matunda, hauna faida

    ndani yake, na elimu imeletwa ili ifanyiwe kazi.

    Kama yalivyo matendo yasio kua na elimu inakua ni msiba na

    upotevu kwa mtendaji.

    Ikiwa mwanadamu anafanya matendo bila elimu kwa hakika matendo

    yake yana kuwa ni msiba na tabu kwa mtendaji, Amesema Mtume wa

    Mwenyezi Mungu (s.a.w):

    (Yeyote atakae fanya Amali hakuna Amri yetu yatakuwa ni yenye

    kurejeshwa).

    Kapokea hadithi hii Imam Bukhari kabla ya hadithi (7350), na Muslim

    (18/1718), hadithi ya Bibi Aisha (r.a), na kapokea Bukhari (2697) na

    Muslim (17/1718) kutoka kwa Bibi Aisha (r.a) Amesema: Amesema

    Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w): (Yeyote atakae zua katika dini

    yetu hii jambo lisilo kuwemo atarejeshewa).

    Na kwa sababu hii tuna soma katika suratul Fatiha katika kila raka:

    (Tuongoze njia iliyo nyooka* Njia ya wale ambao uliyo waneemesha,

    siyo ya wale waliyo kasirikiwa na wala waliyo potea).

    (Al-Fatiha: 6-7).

    Akataja Mwenyezi Mungu wale ambao wanafanya bila elimu walio

    potea, na wale ambao wanafahamu na hawayafanyii kazi

    wamekasirikiwa, tuzindukane na jambo hili kwa sababu ni muhimu

    sana.

    KULINGANIA KATIKA ILIMU. JAMBO LA TATU: KUILINGANIA KWAKE. Kuilingania katika njia ya Mwenyezi Mungu: maana yake: haitoshi

    kujifundisha mwanadamu na akafanya pekeyake, wala asilinganii

    katika njia ya Mwenyezi Mungu Mshindi na Mtukufu, hapana budi

    awalinganie wengine, ili ainufaishe nafsi yake na nafsi za wengine, na

    kwa sababu elimu hii ni amana, sio milki yako ukawa unailimbikiza tu

    na una wanyima watu, na watu wana shida nayo, ilio wajibu kwako

    kufikisha na kubainisha na kuwalingania watu katika kheri, hapana

    budi kuifikisha na kuibainisha kwa watu.

    Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na pindi Mwenyezi Mungu

    alipo funga ahadi na walio pewa Kitabu kuwa: Lazima

  • 11

    mtawabainishia watu, wala hamtokificha). (Al-'Imran: 187). Ahadi hii

    kaichukua Mwenyezi Mungu kwa Wanachuoni wawabainishie watu

    yale walio fundishwa na Mwenyezi Mungu ili waeneze kheri, na

    wawatowe watu katika gize kuwaweka katika nuru, Hii ndio kazi ya

    Mitume (s.a.w) na wafuasi wao, Amesema Mwenyezi Mungu

    Mtukufu: (Sema: Hii ndiyo njia yangu ninalingania kwa Mwenyezi

    Mungu kwa ilimu mimi na wanao nifuata.

    Na ametakasika Mwenyezi Mungu! Wala mimi si katika washirikina).

    (Yusuf: 108).

    Hii ndiyo njia ya Mtume (s.a.w) na nhia ya wafuasi wake, ilimu na

    matendo na kulingania kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, yeyote asie

    lingania haliyakuwa anao uwezo wa kulingania na ilimu anayo

    akaificha, kwa hakika atafungwa kamba za moto mdomoni mwake

    siku ya kiyama kama ilivyo katika hadithi. Kaipokea Abuu daudi

    (3658), na Tirmidhi (2649), na Ibnu Maja (261) na (266) hadithi ya

    Abaa huraira (r.a) Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu

    (s.a.w): (Yeyote atakae ulizwa katika mambo ya ilimu akaficha,

    atafungwa kamba na Mwenyezi Mungu za moto mdomoni mwake

    siku ya kiyama). Na Ibnu Maja (265) kwa hadithi ya Abii Saidi l-

    khudri (r.a) Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu

    (s.a.w): (Yeyote atakae ficha Elimu katiaka Elimu anazo wanufaisha

    Mwenyezi Mungu watu, mambo ya dini, Allah atamfunga siku ya

    kiyama kamba za moto mdomoni mwake).

    KUFANYA SUBRA JUU YA MAUDHI YANAYO PATIKANA NDANI YAKE.

    JAMBO LA NNE: KUFANYA SUBRA JUU YA MAUDHI YANAYO PATIKANA NDANI YAKE.

    Subra juu ya maudhi yanayo patikana ndani yake:

    kama inavyo julikana yeyote ane walingalia watu aka waamrisha

    mema na aka kataza mabaya, kwa hakika atafikwa na maudhi kwa

    watu waovu; kwa sababu watu wengu hawapendi kheri, bali hupenda

    matamaniyo na haramu na matakwa ya nafsi yaliyo mabaya,

    anapokuja mwenye kuwalingania kwa Mwenyezi Mungu, na kukemea

    matamanio yao, hapana budi.

  • 12

    Miongoni mwao kufanya vibaya ima kwa maneno au kauli,

    Ni lazima juu ya mwenye kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu

    na kutaka radhi za Mwenyezi Mungu asubiri maudhi, na aendelee

    katika kulingania, na kiigizo chake ni Mitume (s.a.w) na mbora wao

    na wa mwisho wao Muhammad (s.a.w).

    Yamemfika mangapi kutoka kwa watu? Na maudhi mangapia

    kayapata kwa maneno na vitendo? Walisema: mchawi, muongo,

    wakasema: mwandawazimu. Wakasema dhidi yake maneno ambayo

    ameyataja Mwenyezi Mungu Mtukufu ndani ya Qur-ani,

    wakamfanyia maudhi, kapigwa mawe mpaka miguu yake ikatoa damu

    (s.a.w) wakati alipo walingania katika njia ya Mwenyezi Mungu,

    kawekewa utumbo wa ngamia juu ya mgongo wake akiwa ana sujudu

    mbele ya Alkaaba, kaahidiwa kuuliwa katishwa, katika vita vya Uhudi

    ali dhuriwa yeye na maswahaba zake (s.a.w),

    kavunjwa memo yake manne ya mbele, kapasuliwa kichwani mwake

    (s.a.w) kasukumwa ndani ya shimo, haliyakuwa ni nabii wa

    Mwenyezi Mungu, madhara yote haya kayapata katika kulingania

    kwaajili ya Mwenyezi Mungu, lakini yeye kasubiri kavumilia

    haliyakua ndio mbora wa viumbe wote (s.a.w), hapana budi kwa Yule

    anae fanya kazi ya kulingania kufikwa na maudhi kiasi cha imani yake

    na dawa wake; pamoja na yote hayo yatakiwa asubiri, akiwa yupo

    katika haki, asubiri avumilie, yupo katika njia ya Mwenyezi Mungu na

    maudhi yanayo mfika yatakuwa katika mizani yake mema mbele ya

    Mwenyezi Mungu Mtukufu.

    Mambo haya ma nne nilazima tujifundishe kwa urefu,

    Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Naapa kwa Zama!).

    (Al-Asr1).

    Ameapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa zama na wakati nao ni

    kiumbe, na Mwenyezi Mungu Mtukufu anaapa kwa anacho kitaka

    miongoni mwa viumbe, na kiumbe haapi isipokuwa kwa jina la

    Mwenyezi Mungu, Na Mwenyezi Mungu haapi isipokuwa kwa kitu

    chenye umuhimu, na ndani yake kuna alama miongoni mwa alama

    zake, Utakasifu niwake na ametukuka, ndani ya zama kuna

    mazingatio na umuhimu, na kwa sababu hiyo Ameapa Mwenyezi

    Mungu kwa muda wa Laasiri, na kwa usiku unapo funika na akaapa

    kwa mchana. Ama kiumbe haifai kuapa isipokua kwa jina la

    Mwenyezi Mungu, na haifai kwetu kuapa kwa asie kua Mwenyezi

  • 13

    Mungu, Amesema Mtume (s.a.w): (Yeyote atakae apa kwa asiye kua

    Mwenyezi Mungu kwa hakika amekufuru au ameshirikisha). Kapokea

    hadithi hii Imam Abuu daudi (3251), na Tirmidhi (1535) kwa hadithi

    ya Ibni Omar (r.a).

    Na Akasema: (Yeyote anae taka kuapa Aape kwa jina la Mwenyezi

    Mungu au akae kimya).

    Kapokea hadithi hii Imam Bukhari (6108), na Muslim (1646) kwa

    hadithi ya Ibni Omar (r.a).

    NI LIPI JIBU LA KIAPO? Ni kauli yake: (Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika

    hasara).

    (Al-Asr: 2).

    Mwanaadamu Binaadamu woote hakuvuliwa hata mmoja siyo

    wafalme wala maraisi, wala matajiri, wala

    Mafakiri, wala walio huru, wala watumwa, wala wanamume wala

    wanawake, kila binaadamu yupo katika Hasara, maana yake: katika

    hasara na maangamio ikiwa wataupoteza huu muda ulio wa thamani,

    wakautumia katika kumuasi Mwenyezi Mungu, na katika yanayo

    wadhuru.

    Wanaadamu weete wamo ndani ya hasara na maangamio isipokuwa

    atakae sifika na sifa nne nazo: Ilimu, na Matendo, na kulingania katika

    njia ya Mwenyezi Mungu, na kufanya subra juu ya maudhi.

    Yeyote atakae sifika na sifa hizi nne ameokoka katika hii hasara. Wala

    haiwezekani kumuamini Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa Ilimu,

    Ambayo ndio kumjuwa Mwenyezi Mungu.

    (Na wakatenda mema). (Al-Asr: 3).

    Maana yake: wamefanya matendo yalio mazuri katika mambo ya

    lazima na yasio yalazima, wakatumia muda wao kwa matendo mema

    kwa yale yanayo wanufaisha katika dini yao na dunia yao.

    Hata matendo ya kidunia ndani yake kuna ujira ikiwa utakusudia

    katika hayo matendo kuwa ni sababu ya kufanya twaa, itakuwaje

    matendo kwaajili ya akhera, lamsingi jitahidi usipoteze muda utumie

    katika mambo yanayo kunufaisha na yanayo kufiidisha.

    )Na wakausiana kwa haki). (Al-Asr: 3).

    Wameamrisha mema, na Wamekataza mabaya, na Wakalingania

    katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Na Wakafundisha Ilimu

    yenye manufaa, na Wakazagaza Ilimu na kheri kwa watu.

    Wakawa walinganiaji katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

  • 14

    )Na wakausiana kusubiri). (Al-Asr: 3).

    Walifanya subra kwa yale walio yapata,

    Na Subra katiak lugha ya kiarabu: kuziwia, lakini makusudio hapa:

    kuiziwia nafsi katika kumcha Mwenyezi Mungu.

    Nazo zipo aina tatu:

    1. Kufanya subra katika kumtii Mwenyezi Mungu.

    2.Kufanya subra kwa yale aliyo kataza Mwenyezi Mungu.

    3.Kufanya subra juu ya makadara ya Mwenyezi Mungu.

    1.Subra katika kumtii Mwenyezi Mungu, kwa sababu nafsi inapenda

    uvivu na inapenda raha, hapana budi kuizoweza binaadam nafsi juu ya

    kutii na kusali na kufunga na kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi

    Mungu japokuwa mambo haya nafsi haiyapendi, anaiziwiya katika

    utiifi wa Mwenyezi Mungu.

    2.Kufanya subra kwa yale aliyo kataza Mwenyezi Mungu.

    Nafsi inataka mambo ya haramu, na mambo ya matamanio, inaelekea

    huko na kuvutiwa sana, hapana budi aifunge na kuiziweya katika

    mambo ya haramu, jambo hili lahitaji subra, na siyo jambo rahisi

    kuizuiya nafsi katika mambo ya matamanio ya haramu, ambae hana

    subra kwa hakika nafsi yake itamshinda na itamvuta kwenye haramu.

    3.Kufanya subra juu ya makadara ya Mwenyezi Mungu yenye kuu

    miza.

    Matatizo yanayo mpata mwanaadamu kwa kufiliwa na mtu wake wa

    karibu, au kupoteza mali, au maradhi yanayo mpata mwanaadamu,

    hapana budi afanye subra juu ya hukumu na makadara ya Mwenyezi

    Mungu, asikate tamaa wala kuchukia, bali auziwiye ulimi na kuto

    omboleza na kutokata tamaa, na aiziwiye nafsi kutokata tamaa, na

    aziwiye viungo na kuto jipiga makofi na kuchana nguo kwa hasira, Hii

    ndiyo subira wakati wa matatizo.

    Kuhusu maasi asifanyi subra juu yake bali atubiye kwa Mwenyezi

    Mungu na ayakimbiye; lakini wakati wa mitihani ambayo hukuingia

    ndani yake, bali nikutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu

    amekukadiria juu yako na kukupa mtihani au adhabu kwako kutokana

    na madhambi uliyo yafanya, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu

    Mtukufu:

  • 15

    (Na misiba inayo kupateni ni kwa sababu ya vitendo vya mikono

    yenu. Naye anasamehe mengi). (Ash-Shura: 30).

    Utapofika msiba kwa Muislam katika nafsi yake au mali zake au

    watoto zake au ndugu wa karibu au yeyote kati ya ndugu zake

    Waislam ni juu lako kufanya subra na kutegemea malipo kwa

    Mwenyezi Mungu.

    Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

    (Wale ambao ukiwasibu msiba husema: Hakika sisi ni wa Mwenyezi

    Mungu, na kwake Yeye hakika tutarejea * Hao juu yao zitakuwa

    Baraka zitokazo kwa Mola wao Mlezi na rehema. Nao ndio wenye

    kuongoka).

    (Al-Baqara: 156-157).

    Hii ndio subra, na mfano wake kufanya subra juu ya maudhi unayo

    yapata katika kulingania neno la Mwenyezi Mungu Mtukufu hayo

    nikatika matatizo, nilazima ufanye subra kwa hayo unayo yapata

    katika njia ya kheri, Nawala usiachi kufanya kheri; kwa sababu baadhi

    ya watu wanataka kufanya kheri lakini akikutana na jambo linalo

    chukiza anasema: sio lazima juu yangu kuiweka nafsi yangu kwenye

    mambo kama haya, kisha anaacha kufundisha ikiwa ni mwalimu,

    anaacha kulingania katika njia ya Mwenyezi Mungu, anaacha kuongea

    ikiwa ni khatwibu wa muskiti, anaacha kusalisha muskitini, anaacha

    kuamrisha mema na kukataza mabaya, Huyu hakusubiri kwa aliyo

    yapata miongoni mwa maudhi.

    Amesema Imam Shaafy (r.a): "Laiti Mwenyezi Mungu asinge teremsha dalili kwa waja wake ila surahii ingeliwatosha".

    Kwa hakika kanukuu Imam Shafy: yeye ni Muhammad ibni Idrisa

    Ashaafy nasabu kwa babu yake wa nne jinalake shafy, nae ni

    mkuraishi, katika familia ya mutw-labi, kafariki mwaka (204) h.j.r.

    naye ni mmoja kati ya Maimamu wa nne, na akasema maneno haya

    kwa sababu Mwenyezi Mungu kabainisha kwanye sura hii sababu za

    kupotea na sababu za kuongoka

    .

    Kuhusu sababu za kuongoka: Asifike mwanaadamu na hizi sifa nne:

    Ilimu, na Matendo, na Kulingania, nakufanya subra juu ya maudhi

    yanayo tokea katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, ikasimama

    hoja kutoka mwa Mwenyezi Mungu juu ya waja wake kwa sura hii,

  • 16

    Hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu ana waambia: Hakika mimi Allah

    nime kubainishieni sababu za kuokoka katika sura hii fupi sana.

    Na Qur-ani yate pamoja na Sunna vime fafanuwa zaidi mambo haya

    ma nne, lakini sura hii imebainisha sababu za kuongoka kwa ujumla,

    ikasimama hoja kwa viumbe, na zikabaki dalili ndani ya qur-ani na

    sunna ziki fafanuwa zaidi na kuweka wazi mambo haya ma nne, na

    wala sio makusudio ya Imam Shafy kwamba sura hii yawatosha watu,

    kama asingeliteremsha Mwenyezi Mungu sura tofauti na hii, lakini

    hoja imesimama juu yao; kwa sababu Mwenyezi Mungu kisha

    bainisha ndani yake sababu za kuokoka na sababu za uongofu,

    asitokei yeyote siku ya kiyama akasema:

    Mimi sijuwi sababu za uongofu wala sijuwi sababu za kupotea naye

    akisoma sura hii fupi sana.

    NA AKASEMA IMAMU BUKHARI (r.a): MLANGO UNAO ELEZEA ILIMU KABLA

    YA KAULI NA MATENDO.

    Na dalili: (Basi jua ya kwamba hakuna Mungu anayefaa kuabudiwa

    kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na omba maghufira kwa

    dhambi zako na za Waumini wanaume na Waumini wanawake).

    (Muhammad: 19).

    Akaanza Ilimu kabla ya kauli na matendo.

    Bukhari: yeye ni Muhammad bin Ismail bin Imrahim Al-Bukhary,

    kanasibishwa na Bukhara mji uliyoko Mashariki, ni Imam wa Hadithi

    bingwa wa kuhifadhi (r.a), mtunzi wa (Swahihi) kitabu ambacho kina

    usahihi baada ya kitabu cha Mwenyezi Mungu.

    Ilimu kabla ya kauli na matendo; kwa sababu matendo hayanufaishi

    isipokuwa yakijengewa juu ya ilimu, lakini matendo yaliyo jengeka

    juu kutenda.

    Na dalili: kuhusu kichwa cha habari kauli yake Mwenyezi Mungu

    Mtukufu: (Basi jua ya kwamba hakuna Mungu anayefaa kuabudiwa

    kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na omba maghufira kwa

    dhambi zako). (Muhammad: 19).

    Hakika kaanza na Ilimu, Na kauli ya ujinga kwa hakika

    hayamnufaishi mwenye nayo bali ni hasara kwake na upotovu juu

    yake siku ya kiyama, hapana budi atangulize kujifundisha kabla ya

    yake Tukufu: (Na omba maghufira) hii ndio Amali, Akaanza

    Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Elimu kabla ya amali; kwa sababu

    matendo yakiwa niya kijinga hakika hayamnufaishi mwenye nayo,

  • 17

    Aanze mwanaadamu na Elimu kwanza kisha afanye yale aliyo

    jifundisha, huu ndio msingi wa dini ya uislam.

    Utangulizi:

    Kila sifa kamilifu niza Mwenyezi Mungu muumba wa vitu vyote sala na

    amani ziwe juu ya kipenzi cha Allah mtume wetu Muhammad (s.a.w) ambae

    ametuwa akiwa nirehma kwa walimwengu wote akiwa nimwenye kubashiri

    pepo na kukhpfisha moto, na ziwe juu ya maswahaba zake wote waongofu na

    wote watakao fuata muongozo wake mpaka siku ya qiyama.

    Kitabu hiki ni muendelezo wa sehemu ya kwanza ya kitabu kilicho

    tangulia tukiwa tunaendelea kunufaika na maneno alio andika imamu Imamu

    Sheikh Saleh bin Fauzan Al-Fawzan. Mwenyezi Mungu amhifadhi.

    RISALA YA TATU MAMBO MATATU NI LAZIMA MUISLAM

    AJIFUNDISHE NA AYAFANYIE KAZI .

    Tambua Mwenyezi Mungu akurehemu ya kwamba nilazima juu ya kila

    Muislam wa Kiume na Wakike kujifundisha mambo haya matatu na kuyafanyia

    kazi.

    TAMBUA: ni neno ambalo huletwa kwaajili ya umuhimu wa kinacho elezwa

    baadae, na maana yake: jifundishe na ufahamu na uwe na yakini.

    MWENYEZI MUNGU AKUREHEMU: Hii ni dua kwako ya rehma, na

    hili pia limekwisha tangulia kwamba mwalimu yatakiwa awe mpole kwa

    mwanafunzi, na amuombee dua na kumuhimiza, kwa sababu haya nikatika njia

    bora za kufundisha, na wala haifai kwake kumkabili kwa ukali na uzito na

    chuki, kwa sababu haya nanapelekea achulie Elimu, pia yaonyesha nasaha ya

    mwanachuoni, na kwamba yeye anachotaka ni nasaha na kuelekeza na usawa.

    NI LAZIMA: Yaonyesha kwamba jambo hili siyo hiyari, anaetaka

    anafanya na asietaka anaacha, bali ulazima hapa ni katika namna ya mkazo

    kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na siyo ulazima kutoka kwa

    mwanachuoni, bali ni kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa yale aliyo

    yateremsha katika Kitabu na Sunna, katika kuwalazimisha waja kwa mambo

    haya.

  • 18

    NI LAZIMA JUU YA KILA MUISLAM WAKIUME NA WAKIKE,

    Maana yake: ni lazima juu yakila mwanamume na mwanamke miongoni mwa

    Waislam sawasawa wakiwa huru au watumwa au wanaume au wanawake, kwa

    sababu mwanamke hushirikiana na mwanaume kwenye mambo ya lazima mengi

    sana, isipokuwa yale yanayo wahusu wanaume pekeyao kwa dalili inayo

    wahusu wao tu, mfano: ulazima wa swala za jamaa misikitini, swala za ijumaa,

    na mfano wa kuzuru makaburi mambo haya ni haswa kwa wanaume, na mfano

    wa kupigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, sababu jambo hili ni

    maalumu kwa wanaume.

    MAMBO MATATU :

    Kujifundisha maana yake hapa: kupata elimu kutoka kwa wanachuoni na

    kuhifadhi na kufahamu na kudiriki mambo sawasawa, hii ndiyo elimu, nawala

    siyo makusudio kujisomea tu ovyo au kutwalii tu.

    Na haifai kujifundisha kwenye vitabu kama hali ya zama tulizo nazo, kwa

    sababu kujifundisha kwa kutumia vitabu ni hatari sana, hupatikana madhara

    makubwa, na kufundishana -kwanjia hiyo ya vitabu- kuna dhuru zaidi kuliko

    mjinga; kwa sababu mjinga anatambuwa kama yeye ni mjinga na husimama

    kwenye kiwango chake, lakini mwenye kujifundisha hujiona ya kwamba ni

    mjuzi, ana halalisha aliyo ya haramisha Mwenyezi Mungu, na ana haramisha

    aliyo ya halalisha Mwenyezi Mungu, na anaongea na husema juu ya Mwenyezi

    Mungu bila ya elimu, ni mambo hatari sana.

    Elimu haichukuliwi kutoka kwenye vitabu moja kwa moja, isipokuwa

    vitabu ni nyenzo tu, lakini uhakika wa elimu huchukuliwa kutoka kwa

    wanachuoni ambao wapo katika njia ya wema walio tangulia vizazi kwa vizazi,

    na vitabu ni nyenzo za kutafutia elimu.

    KUAMINI YA KWAMBA:

    A.MWENYEZI MUNGU AMETUUMBA.

    B. ANATURUZUKU.

    C. HAKUTUACHA BURE .

    Mwenyezi Mungu ametuumba na kuturuzuku na hajatuacha bure.

  • 19

    1:kwamba Mwenyezi Mungu ametuumba, maana yake: Ametuweka baada ya

    kuto kuwepo, sisi kabla yakutuumba hatukuwa chochote, kama alivyo sema

    Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hakika ulimpitia binaadamu kipindi katika zama

    ambacho kwamba hakuwa kitu kinachoweza kutajwa). (Al-Insaan: 1).

    Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Akasema: Ndio hivyo hivyo amesema

    Mola wako: Haya ni rahisi kwangu. Na hakika Mimi nilikwisha kukuumba

    wewe zamani na hali hukuwa kitu).

    (Maryam: 9) .

    Alikuwa binaadamu kabla ya kuumbwa si chochote, ambae kamuweka na

    kumuumba ni Mwenyezi Mungu Mtukufu, amesema Mwenyezi Mungu

    Mtukufu: (Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao

    ndio waumbaji?). (Tuur: 35).

    2:Na kuturuzuku: Tulipokuwa niwenye kuhitajia rizki chakula kinywaji

    mavazi nyumba vipando na mazuri, alitambua Mwenyezi Mungu Mtukufu shida

    zetu akawepesisha vilivyoko mbinguni na aridhini vyote kwa masilahi yetu

    kwaajili tubakie kwenye uhai, na kwaajili ya kuvitumia ili tufanye lengo la

    kuumbwa kwetu, nalo ni Ibada ya Mwenyezi Mungu Mtukufu.

    3:Na hakutuacha bure: ni kitu kilicho achwa ambacho hakina faida yoyote,

    Mwenyezi Mungu ametuumba na kuturuzuku kwa hikma, hakutuumba kwa

    mchezo wala bure, amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Je! Mlidhani ya

    kwamba tuli kuumbeni bure na yakwamba nyinyi kwetu hamtarejeshwa?). (Al-

    Muuminuun: 115).

    Na akasema Mwenyez Mungu Mtukufu: (Ati anadhani mwanadamu kuwa

    ataachwa bure?* Kwani hakuwa yeye ni tone ya manii lilio shushwa?* Kisha

    akawa pande la damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza

    vilivyo). (Al-Qiyamah: 36-38).

    Na akasema: (Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yao bure.

    Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utakao

    wapata). (Swaad: 27 (.

    Mwenyezi Mungu ametuumba na katuumbia hizi rizki na yanayo

    wezekana kwa hikma kubwa na lengo nzuri, nalo ni kumuabudu Mwenyezi

    Mungu Mtukufu, na wala hakutuumba kama wanyama ambao wameumbwa kwa

    maslahi ya viumbe kisha vinakufa na kuondoka; kwa sababu havija kalifishwa

    wala kuamrishwa wala kukatazwa, kwa hakika Ametuumba kwaajili ya ibada

    yake, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Nami sikuwaumba majini

    na watu ila waniabudu Mimi* Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe*

    Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu,

    Madhubuti). (Adh-Dhaariyaat: 56-58).

  • 20

    Wala hakutuumba kwaajili ya maisha ya dunia tu, ili tuishi ndani yake,

    tukeshe tucheze, na tule na tunywe, tujitanue ndani yake kisha pisiwe na

    chochote, na kwa hakika maisha ni shamba, na sokoni ni nyumba ya akhera,

    tunajiandaa kwa matendo mema, kisha tunakufa na tunaelekea huko, kisha

    tunafufuliwa, kisha tuna hesabiwa na tunalipwa kwa matendo yetu.

    Haya ndio makusudio ya kuumbwa majini na watu, na ushahidi wa hayo

    ni mwingi sana wakuonyesha kufufuliwa na malipo na hesabu, na akili

    inaonyesha hili, kwa sababu haiwezekani kwa hikma ya Mwenyezi Mungu

    Mtukufu kuumba kiumbe waajabu, na akaufanya huu ulimwengu kwaajili ya

    binadamu kisha awaache wafe waondoke bila faida. Huu ni mchezo, hapana

    budi kujulikana majibu ya matendo katika nyumba ya akhera.

    Kwa hili kuna baadhi ya watu wanao maliza umri wao katika Ibada ya

    Mwenyezi Mungu na katika kumtii yeye, hali ya kuwa yupo katika ufakiri na

    shida, na huenda akawa ni mwenye kudhulumiwa kubanwa kuonewa na wala

    asilipiwe katika hii dunia, na kinyume chake, unakuta mwengine kafiri

    hamuamini Mungu na ni muovu lakini amekunjuliwa ana furaha katika hii

    dunia, ana neemeka amepewa anayo yataka, anafanya aliyo haramisha

    Mwenyezi Mungu, anawadhulumu waja anawafanyia vibaya, anakula mali zao,

    anaua bila haki, anawasaliti watu anajinyanyuwa kisha anakufa katika hali hiyo,

    hakupata chochote katika adhabu.

    Je! Yafaa kwa uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu na hekima zake

    amuache huyu mtiifu bila malipo?, na amuwache huyu kafiri bila kumlipa?,

    jambo hili halifai kutokana na Uadilifu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu,

    Kwa sababu hiyo kajaaliya nyumba ya akhera aliye fanya wema kulipwa

    kwa wema wake, na aliye fanya mabaya kwa mabaya yake, patadhihirika

    matunda ya matendo.

    Dunia ni nyumba ya matendo, lakini akhera yao ni nyumba ya malipo,

    ima pepo au moto, na hakutuacha bure kama wanavyo dhani wasio muamini

    Mwenyezi Mungu na wanao amini uhai wa dunia bila akhera, amesema

    Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na walisema: Hapana isipokuwa huu uhai wetu

    wa duniani tunakufa na tunaishi, na hapana kinacho tuhiliki isipokuwa zama.

    Lakini wao hawana ilimu ya hayo, isipokuwa wao wanadhani tu). (Al-Jaathiyah:

    24) .

    Haya ndio maneno ya wasio muamini Mwenyezi Mungu ambao

    hawaamini kufufuliwa.

    Na kwa hakika Mwenyezi Mungu kawakanusha Akasema: (Kwani

    tutawafanya Waislamu mfano wa wakosefu?* Mna nini? Mnahukumu vipi?).

    (Al-Qalam: 35-36).

    Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Je! Wanadhani wanao tenda

    maovu kuwa tutawafanya kama walio amini, na wakatenda mema, sawa sawa

  • 21

    uhai wao na kufa kwao? Ni hukumu mbaya wanayo ihukumu!). (Al-Jaathiyah:

    21) .

    Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Ama! Tuwajaalie walio amini na

    wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika ardhi? Au tuwajaalie

    wachamungu kama waovu?). (Swaad: 28).

    Hili haliwezekani na wala haliwi.

    BALI KATUTUMIA MITUME .

    Ilivyokuwa Ibada haifai tuichukue kutoka kwa Fulani na Fulani tutakao

    waona wazuri, au kumuiga Fulani na Fulani katika wanadamu, katutumia

    Mwenyezi Mungu Mitume watubainishie Namna tutakavyo muabudu; kwa

    sababu Ibada ni kitu rasmi, na haifai kumuabudu Mwenyezi Mungu kwa

    chochote isipokuwa kwa aliyo amrisha.

    Ibada ni kitu rasmi juu ya yale walio kujanayo Mitume (s.a.w), na hekima ya

    kutumwa Mitume ili wawabainishie watu namna watakavyo muabudu Mungu

    wao, na wawakataze shirki na kumkufuru Mwenyezi Mungu Mtukufu.

    Hii ndiyo kazi ya Mitume (s.a.w), kwa sababu hii anasema Mtume (s.a.w):

    (Yeyote atakae zuwa katika dini yetu mambo ambayo hayapo atarejeshwa

    mwenyewe) .

    Kapokea hadithi hii Imam Bukhari kabla ya hadithi (7350), na Muslim

    (18/1718), hadithi ya Bibi Aisha (r.a (.

    Ibada ni kitu rasmi, na bida'a ni yenye kurejeshwa, na mambo yasio faa ni yenye

    kurejeshwa, na kufuata kama kipofu imekatazwa. Ibada hazichukuliwi

    isipokuwa katika sheria alio kujanayo Mtume (s.a.w).

    BALI KATUTUMIA MTUME :

    Nae ni Muhammad (s.a.w) mwisho wa manabii, amemtuma ili atubainishie

    kwa nini Ametuumba? Na atubainishie namna ya kumuabudu Mwenyezi Mungu

    Mtukufu, na atukataze ushirikina na ukafiri na maasi, hii ndio kazi ya Mtume

    (s.a.w) na amefikisha kwa uwazi, na akatekeleza amana, na akaunasihi Umma

    (s.a.w), na akabainisha na akaweka wazi, na akatuacha katika njia nyeupe usiku

    wake ni kama mchana wake, yeyeto atakae kwenda kinyume ataangamia, kama

    ilivyo katika maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Leo

    nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na

    nimekupendeleeni Uislamu uwe ndiyo Dini).

    (Al-Maaida: 3).

  • 22

    YEYOTE ATAKAE MTII ATAINGIA PEPONI, NA YEYOTE ATAKAE

    MUASI ATAINGIA MOTONI.

    Atakae mtii, maana yake: kwa yale aliyo amrisha ataingia Peponi, na atakae

    muasi, maana yake: kwa yale aliyo kataza ataingia Motoni.

    Ukweli wa haya ni mwingi ndani ya Qur-ani, kama alivyo sema Mwenyezi

    Mungu Mtukufu: (Mwenye kumti'i Mtume basi kwa hakika ndio amemti'i

    Mwenyezi Mungu). (An-Nisaa: 80).

    Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na mkimtii yeye mtaongoka). (An-

    Nuur: 54).

    Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na mtiini Mtume, ili mpate

    kurehemewa). (An-Nuur: 56).

    Yeyote atakae mtii ataongoka na ataingia Peponi, na yeyote atakae muasi

    atapotea na ataingia Motoni, amesema Mtume (s.a.w): (Nyoote mtaingia Peponi

    isipokuwa Yule atakaekataa, wakasema: ni nani atakae kataa ewe Mtume?

    Akasema: Yeyote atakae nitii Mimi ataingia Peponi na yeyote atakae niasi Mimi

    huyo ndiyo alie kata(.

    Kapokea hadithi hii Imam Bukhari (7280). hadithi ya Abaa huraira (r.a).

    Kauli yake Mtume (s.a.w): ATAKAE KATAA, maana yake: Amekataa kuingia

    Peponi. Na akasema Mtume (s.a.w): (Hato nisikia mimi yahudi au mkristo kisha

    hakuamini yale niliyo kujanayo isipokuwa ataingia Motoni) .

    Kapokea hadithi hii Imam Muslim (153), hadithi ya Abaa huraira (r.a) .

    Yeyote atakae mtii ataingia peponi na yeyote atakae muasi ataingia motoni,

    na hii ndio tofauti kati ya muislamu na kafiri.

    Na dalili kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Hakika Sisi tumemtuma

    kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni*

    Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamkamata mkamato wa mateso).

    (Al-Muzammil: 15-16) .

    Na dalili, maana yake: juu ya kutumwa Mitume kauli yake Mwenyezi Mungu

    Mtukufu: (Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu kama

    tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni* Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi

    tukamkamata mkamato wa mateso).

    Na maana ya: Tumemtuma: tumemtumia na tumemfunulia.

    KWENU: Enyi makundi aina mbili majini na watu, ni maneno kwa watu wote;

    kwa sababu ujumbe wa Nabii Huyu unaenea watu wote hadi kusimama kiyama .

    MTUME: ndie Muhammad (s.a.w).

  • 23

    SHAHIDI JUU YENU: maana yake: mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu siku

    ya kiyama kama yeye kakufikishieni ujumbe wa Mwenyezi Mungu na hoja

    ikasimama juu yenu, kama alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Mitume

    hao ni wabashiriaji na waonyaji, ili watu wasiwe na hoja juu ya Mwenyezi

    Mungu baada ya kuletewa Mitume. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu,

    Mwenye hikima) . (An-Nisaa: 165).

    Asitokee yeyote siku ya kiyama akasema: mimi sijui kama nimeumbwa kwaajili

    ya Ibada, mimi sijui yepi ni lazima kwangu, na sijui yepi ni haramu kwangu,

    haiwezekani akasema haya, kwa sababu Mitume (s.a.w) wamekwisha

    wafikishia, na huu Umma wa Muhammad (s.a.w) utashuhudiya juu yao, kama

    alivyo sema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (Na vivyo hivyo tumekufanyeni muwe

    Umma wa wastani, ili muwe mashahidi juu ya watu, na Mtume awe ni shahidi

    juu yenu). (Al-Baqara: 143) .

    Umma huu utakuwa ni shahidi juu ya nyumati zilizo tanguliya siku ya kiyama

    kwamaba Mitume wao wamewafikishia ujumbe wa Mwenyezi Mungu, kwa yale

    walio yakuta ndani ya kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu, kwa sababu

    Mwenyezi Mungu katusimulia habari za nyumati zilizo tanguliya na Mitume na

    walio yasema kwa nyumati zao .

    Yote hayo tumeyajua kupitia kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu kitabu

    ambacho Hautakifikia upotovu mbele yake wala nyuma yake, kimeteremshwa

    na mwenye hikima, msifiwa.

    NA ATAKUWA MTUME: Nae ni Muhammad (s.a.w), atakuwa ni shahidi juu

    yenu Ummati Muhammad, atashuhudia juu yenu mbele ya Mwenyezi Mungu

    kwamba yeye amesimamisha juu yenu hoja, na akafikisha kwenu Ujumbe, na

    akakupeni nasaha kwaajili Mwenyezi Mungu, hapatakuwa na hoja kwa yeyote

    siku ya kiyama kwa kusema: sikufikiwa na chochote, sikufikiwa na muonyaji,

    hadi makafiri Watakiri wakati watakapo tupwa motoni, amesema Mwenyezi

    Mungu Mtukufu: (Kila mara likitupiwa kundi humo walinzi wake huwauliza:

    Kwani hakukujieni mwonyaji? Watasema: Kwani! Ametuijia mwonyaji, lakini

    tulimkadhibisha, na tukasema: Mwenyezi Mungu hakuteremsha chochote.

    Nyinyi hamumo isipokuwa katika upotovu mkubwa!). (Al-Mulk: 8-9) .

    Wanasema kwa Mitume: Nyinyi mpo katika upotovu, wao wanawakadhibisha

    Mitume na kuwafanya ni wapotovu .

    Hii ndio hikima ya kutumwa Mitume; kwaajili ya kusimamisha hoja kwa waja,

    na muongozo kwa yule anaetakiwa na Mwenyezi Mungu uongofu, Mwenyezi

    Mungu huwaongoza waja wake awatakao kupitia mitume, na husimamisha hoja

    juu ya wenye kupinga na kukanusha na kukufuru.

    KAMA TULIVYO MTUMA MTUME KWA FIRAUNI: Mtume: ni Nabii

    Mussa (s.a.w), na Firauni ndie mfalme jeuri wa Misri, ambae alidai Uungu, na

    Firauni: ni jina la kubandikwa kila anae tawala Misri huitwa Firauni. Makusudio

    hapa ni Firauni alie dai Uungu: (Akasema: Mimi ndiye Mola wenu mkuu

    kabisa). (An-Naziat: 24) .

  • 24

    LAKINI FIRAUNI ALIMUASI HUYO MTUME: Huyo ni Nabii Mussa (s.a.w),

    alipingwa na Firauni kama alivyo simulia Mwenyezi Mungu katika kitabu chake

    yaliyo tokea kati ya Nabii Mussa na Firauni, na alipo fikia Firauni na watu

    wake .

    BASI TUKAMKAMATA, Maana yake: Tulimkamata Firauni kwa adhabu,

    nayo: hakika Mwenyezi Mungu alimzamisha yeye na watu wake ndani ya bahari

    kisha akawaingiza motoni: (Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa

    wakaingizwa Motoni). (Nuuh: 25).

    Akawa katika moto katika barzakhi (Kaburini), Amesema Mwenyezi Mungu

    mtukufu :

    )Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni). (Suuratul Ghaafir 46.(

    Adhabu hii itakuwa kaburini kabla ya akhera,wataonyeshwa motoni asubuhi na

    jioni,yaani kuchomwa namoto mpaka kitakapo simama kiyama,na huu

    niushahidi tosha wakuthibitisha kuwepo kwa adhabu kaburini,Allah atukinge,

    Allah anasema:

    (Na itapo fika Saa ya Kiyama patasemwa: Waingizeni watu wa Firauni katika

    adhabu kali kabisa!) (Suuratul Ghaafir 46).

    ADHABU TATU ZA WATU WA FIRAUN:

    1-Hakika mwenyezi mungu aliwazamisha na kuwapoteza kwamuda mmoja.

    2-Hakika wao wana adhibiwa Katika makaburi yao mpaka kitakapo simama

    kiyama.

    3-Watakapo fufuliwa siku yakiyama wataingia katika adhabu kali,Allah

    atukinge.

    Vilevile yeyote atakae muasi mtume (s.a.w) hakika mafikio yake yatakua katika

    adhabu kali kuliko Firauni, kwasababu mtume Muhamad (s.a.w) ni mtume bora

    kuliko mitume walio pita, atakae muasi adhabu yake inakuwa kubwa zaidi.

    Mwenyezi mungu anasema kuhusu firauna: (basi tukamshika mshiko wa

    mateso).

    Yaani kwa ukali na nguvu bila ulaini ndani yake.

    Anasema Mwenyezi Mungu katika surati Hudi:{Na ndio kama hivyo ndivyo

    inavyo kuwa Mola wako Mlezi anapo ikamata miji inapo kuwa imedhulumu.

    Hakika mkamato wake ni mchungu na mkali.}

    ( Hudi 102).

    Aya hii ni ushahidi tosha juu ya neema ya Mwenyezi mungu juu yetu kwa

    kumtuma mtume Muhamad (s.a.w) kwetu na hakika lengo la kumtuma ni

    kutubainishia njia sahihi ya kufanya ibada, yoyote atakae mtii ataingia peponi,

    na yoyote atakae muasi ataingia motoni, kama alivyo ingia firauni na watu wake

  • 25

    motoni, pindi walipo muasi Nabii Mussa (a.s), vilevile maadui wa mitume wote

    hii ndio njia yao.

    Mwenyezi Mungu mtukufu haridhii kushirikishwa nayoyote katika ibada.

    MAS’ALA YA PILI:

    Hakika Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa na yoyote katika ibada.

    Haya mas’ala yanaambatana na mas’ala ya kwanza, kwa kuwa ya kwanza:

    Yanabainisha uwajibu wa kumuabudu Mwenyezimungu na kumfuata mtume

    (s.a.w), na ndio maana ya shahada mbili, shahada ya (Lailaha ila Allah

    Muhamadu rasulu Allah).

    Na mas’ala yapili: Nikwamba ibada inapo changanyika na ushirikina

    haikubaliwi, kwasababu ni lazima iwe ibada kwaajili ya Mwenyezi Mungu

    mshindi mtukufu.

    Yoyote atakae muabudu Mwenyezi Mungu akamshirikisha na kitu kingine ibada

    yake inakuwa batili, kuwepo ibada hiyo na kuto kuwepo ni sawa, kwasababu

    ibada haifai bila ikhlas na kumpwekesha Mwenyezi Mungu, pindi zitakapo

    changanyika na ushirikina zitaharibika, kama alivyosema Mwenyezi Mungu

    mtukufu:{ Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa walio kuwa kabla yako:

    Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na

    lazima utakuwa miongoni mwa wenye kukhasiri{.(Azzumar 65).

    Na amesema Mwenyezi Mungu mtukufu:

    }Na lau wangeli mshirikisha yangeli waharibikia waliyo kuwa

    wakiyatenda}(An'aam-88).

    Ibada haiwezi kuitwa ibada ila ikiwa ni kwalengo la kumpwekesha Mwenyezi

    Mungu (tauhiidi), kama ilivyo swala haiwezi kuitwa swala mpaka uiswali ukiwa

    msafi (twahara.(

    Ikichanganywa swala na kinacho tengua udhu basi kinaiharibu swala na

    kuibatilisha, ndio maana unakuta Mwenyezi Mungu anakusanya katika aya

    nyingi baina ya kuamrisha watu wafanye ibada na anawakataza shirki.

    Alisema Mwenyezi Mungu:{Muabuduni Mwenyezi Mungu wala

    msimshirikishe na chochote {.(An-Nisaai-36).

    Alisema Mwenyezi Mungu {Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu

    Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na

    watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti}. (Al-bayyinah 5).

    Na alisema Mwenyezi Mungu:{Na hatukumtuma kabla yako Mtume yeyote ila

    tulimfunulia ya kwamba hapana mungu isipo kuwa Mimi. Basi niabuduni Mimi

    tu}. (Anbiyaa 25).

    Mwenyezi Mungu kusema:{hapana mungu isipo kuwa Mimi.}

  • 26

    Kunamambo mawili:

    1- kukanusha ushirikina.

    2-kuthibitisha ibada kwa Mwenyezi Mungu mtukufu pekeyake.

    Na alisema Mwenyezi Mungu mtukufu:{Na Mola wako Mlezi ameamrisha

    kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu}. (Sura Al Israai23)

    {Na kwa hakika kwa kila umma tuliutumia Mtume kwamba: Muabuduni

    Mwenyezi Mungu, na muepukeni Shetani.} (An Nahl 36) .

    Amekutanisha baina ya kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na kujiepusha

    na ibada za matwaghuti (Mashetani).

    Kwasababu ibada ya Mwenyezi Mungu haiwi ibada ila ikiwa ni pamoja na

    kujiepusha na matwaghuti, nao ni kufanya ushirikina.

    Anasema Mwenyezi Mungu mtukufu:{Basi anaye mkataa Shet'ani na

    akamuamini Mwenyezi Mungu bila ya shaka amekamata kishikio madhubuti,

    kisicho vunjika. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.}

    (Al-Baqara256).

    Kumuamini Mwenyezi Mungu peke yake haitoshi mpaka uyakufuru mashetani,

    na kama siyo hivyo hakika washirikina wanamuamini Mwenyezi Mungu pamoja

    na kuwa wanamshirikisha.

    Anasema Mwenyezi Mungu mtukufu:

    {Na wengi katika wao hawamuamini Mwenyezi Mungu pasina kuwa ni

    washirikina}(yusuf 106).

    Amebainisha Mwenyezi Mungu kwamba washirikina wanamuamini Mwenyezi

    Mmungu, lakini imani yao wanaiharibu kwa kumshirikisha Mwenyezi Mmungu

    katika ibada zao.

    Hii ndiyo maana ya kusema: yeyote mwenye kumuabudu Mwenyezi Mungu na

    akamtii Mtume (s.a.w) hakika mtu huyo hawezi kumshirikisha Mwenyezi

    Mmungu na chochote, kwasababu Mwenyezi Mungu haridhii ashirikishwe na

    chochote katika viumbe vyake.

    Kutoka kwa abuu huraira (r.a) alisema: alisema Mtume (s.a.w) katika yale anayo

    yapokea kutoka kwa Mola wake mshindi mwenye nguvu: (Alisema Mwenyezi

    Mungu mtukufu: Mimi ndio tajiri wa washirika kwa ushirikina wanao ufanya,

    mwenye kufanya ibada yoyote akamshirikisha katika ibada hiyo asiyekuwa

    mimi basi nitamuacha na ushirikina wake). Amepokea hadithi hii imamu

    Muslim (2985).

    Kuna watu wanaswali na wanashahidilia kuwa hapana Mola apasae kuabudiwa

    kwa kahi ila Mwenyezi Mungu, na Muhamad (s.a.w) ni mjumbe wa Mwenyezi

    Mungu, na wanakithirisha kusema hivyo, na wanafunga na wanahiji, lakini

    wanayaomba makaburi, na wamuabudu Imamu Hassan na Husein, na

    Albadawiy, na Fulani na Fulani,

  • 27

    Na wanaomba nusura kwa watu walio kufa, hao ndio ibada zao nibatili,

    kwasababu wao wanamshirikisha Mwenyezi Mungu mshindi mwenye nguvu,

    wanachanganya ibada na ushirikina, basi ibada zao ni batili, na nizenye

    kuporomoka, mpaka watakapo mpwekesha Mwenyezi Mungu mshindi mwenye

    nguvu, na wamtakasie utii Mwenyezi Mungu na waache kuabudu kisichokuwa

    Mwenyezi Mmungu.

    Na kama siyo hivyo hawatakuwa na chochote, basi ni wajibu kuzinduka kwa

    hilo, kwasababu Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa na chochote katika

    ibada yake kwa vyovyote atakavyo kua.

    Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa na yeyote atakavyo kua, ili asiseme

    yeyote: mimi nachukua kwa watu wema, na watu wazuri uombezi, mimi

    siabudu masanamu wala mizimu kama ilivyokua enzi za ujinga, mimi

    nawafanya hawa ni waombezi wangu na siwaabudu.

    Tunamuambia kuwa: hayo ni maneno ya watu wa zama za ujinga waliwafanya

    waombezi wao kwa Mwenyezi Mungu kwasababu ni watu wema, na ni mawalii

    katika mawalii wa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu haridhii hayo.

    Sio kwa malaika alie karibu na Mwenyezi Mungu wala Mtume aliye tumwa na

    Mwenyezi Mungu.

    Malaika aliye karibu na Mwenyezi Mungu ni malaika bora, kama jibrilu amani

    ziwe juu yake, na malaika wanao ibeba arshi ya Mwenyezi Mungu, na malaika

    walio karibu nao, na malaika walio karibu na Mwenyezi Mungu mtukufu.

    Pamoja na ukaribu na Mwenyezi Mungu na ukaribu wa waja wa Mwenyezi

    Mungu, na daraja kwa Mwenyezi Mungu, laiti angemshirikisha pamoja na asiye

    kuwa Mwenyezi Mungu pamoja na Mwenyezi Mungu katika ibada hakika

    Mwenyezi Mungu haridhii kushirikishwa pamoja nae malaika alie karibu na

    Mwenyezi Mungu, wala Nabii aliye tumwa, kama Muhamad (s.a.w).

    Na Nabii Issa na Nuhu na Ibrahim ambao ni Mitume walio pewa sheria, au

    walio tumwa kwa watu wote, au walio thibiti katika utume wao.

    Mwenyezi Mungu haridhii ashirikishwe na yoyote, hata kama atakua ni mbora

    wa malaika, au ni mbora wa watu.

    Yeye Mwenyezi Mungu haridhii ashirikishwe na yoyote katika malaika, au

    katika mitume, itakuaje kwa viumbe wasio kuwa mitume na malaika miongoni

    mwa watu wema na mawalii walio wema!

    Basi wasio kuwa malaika na mitume ndio kabisa, hawezi Mwenyezi Mungu

    kumridhia kwa kumshirikisha pamoja nae kitu kingine, katika ibada.

    Na haya ni majibu ya wale ambao wanao dai kwamba wao wanawafanya wale

    wema walio pita na mawalii uombezi kwa Mwenyezi Mungu ili awakurubishe

    hao kwa Mwenyezi Mungu, kama walivyo sema:{Sisi hatuwaabudu ila wapate

    kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu} (Azzumar3).

  • 28

    Na kama siyo hivyo hakika wao wanaitakidi kwamba hao hawaumbi wala

    hawatoi rizki na hawamiliki kifo wala uhai wala kufufuka, bali makusudio yao

    ni kupata mtu wa katikati ili awaombee kwa Mwenyezi Mungu mshindi

    mwenye nguvu, kwasababu hiyo waliwafanyia ibada kwa lengo la kujikurubisha

    kwao, walichinja kwaajili ya makaburi, na wakatoa nadhiri kwa ajili ya ibada,

    na wakaomba nusra na kuwaita walio kufa .

    Na ushahidi ni kauli ya Mwenyezi Mungu mtukufu:{Na hakika misikiti ni ya

    Mwenyezi Mungu, basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu}

    (Al-Jinn18(.

    Mwenyezi Mungu haridhii kushirikiana na yeyote atakavyo kua, na haya

    yametajwa wazi katika Qur'an, na Sunna za Mtume Muhamad (s.a.w), lakini

    yeyote ambae hakuwa na akili wala mazingatio, na kuacha kufuaata mtu kipofu,

    na kuleta sababu ambazo ni batili, na azinduke na nafsi yake.

    Na ushahidi kua Mwnyezi Mungu haridhii kushirikishwa na yeyote, ni kauli ya

    Mwenyezi Mungu mtukufu: {Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu, basi

    msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi Mungu} (Al-Jinn18(

    Misikiti ni nyumba za Mwenyezi Mungu, na ni sehemu zilizo andaliwa kwa ajili

    ya swala, nazo ni sehemu zinazo pendwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu, nazo ni

    nyumba ameidhinisha Mwenyezi Mungu zinyanyuliwe na litaje jina la

    Mwenyezi Mungu, na inapaswa iwe misikiti hii ni sehemu ya ibada ya

    Mwenyezi Mungu pekeyake, na kisitokee chochote katika misikiti ambacho ni

    cha kumshirikisha Mwenyezi Mungu, yasiwekwe ndani yake makaburi,

    kwasababu mtume (s.a.w) amemlaani mwenye kufanya kitendo hicho, na

    akaeleza kuwa kufanya hivyo ni kitendo cha mayahudi, na manaswara, na

    akatukataza kufanya hivyo mwisho wa uhai wake akiwa katika wakati wa

    kutolewa roho yake akisema: kutoka kwa Jundabi bin Abdillah albajaliy (r.a)

    alisema: alisema Mtume (s.a.w): "Fahamuni hakika walio kuwa kabla yenu

    walikua wakiyafanya makaburi ndio misikiti basi fahamuni msilifanye kaburi

    langu kua msikiti hakika mimi nawakataza hilo" Imepokelewa na Muslim (532(

    alikuwa akiyasema haya akiwa katika wakati wa kutolewa roho yake.

    Na kutoka kwa Aisha (r.a) alisema: alikuwa akisema Mtume (s.a.w) "Laana za

    Mwenyezi Mungu ziwe juu ya mayahudi na manaswara waliyafanya makaburi

    ya mitume wao kuwa ni misikiti" Ameipokea na Bukhari (435,436) na

    Muslim(531).

    Misikiti inatakiwa itwaharishwe kutokana na athari za ushirikina na mizimu, na

    yasisimamiwe makaburi kwa kuyatukuza, au kuyajengea, bali misikiti ifanywe

    ni sehemu za ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake, isimamishwe ndani yake

    swala, na litajwe jina la Mwenyezi Mungu ndani yake, na kisomwe ndani yake

    kitabu cha Mwenyezi Mungu, na ziwekwe ndani yake darsa mbalimbali zenye

    manufaa, na watu wakae itikafu kwaajili ya kufanya ibada, huu ndio wadhfa wa

    misikiti.

  • 29

    Ama kusimamishwa msikitini mizimu inayo abudiwa kinyume cha Mwenyezi

    Mungu, basi hiyo sio misikiti, na kufanya hivyo ni ushirikina hata kama wenye

    misikiti hiyo wataiita kua ni misikiti, kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema:

    {Na hakika misikiti ni ya Mwenyezi Mungu.{…

    Yaani misikiti siyo ya kisichokua Mwenyezi Mungu, na kwakuwa misikiti ni

    sehemu ya mkusanyiko wa watu, basi inatakiwa iwe ni sehemu twahara

    kutokana na ushirikina, na uzushi, na mambo yasiyo kubalika kisheria,

    kwasababu watu wanapata elimu na wanafanya ibada katika misikiti, pindi

    watakapo kuta katika misikiti ushirikina au mambo yasio faa kisheria huenda

    wakaathirika nayo au wakayachukua na kuyatangaza duniani kote, Kwahiyo ni

    wajibu iwe misikiti ni yenye kutwaharishwa kutokana na ushirikina.

    Na miongoni mwa misikiti mitukufu kulio yote ni msikiti mtukufu wa Makkah,

    kama alivyo amrisha Mwenyezi Mungu alie tukuka alie wa juu utwaharishwe,

    alisema Mwenyezi Mungu mtukufu:

    }Na pale tulipo muweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukamwambia:

    Usinishirikishe na chochote; na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya wanao

    izunguka kwa kut'ufu, na wanao kaa hapo kwa ibada, na wanao rukuu, na wanao

    sujudu} (Hajj 26(.

    Mwenyezi Mungu aliutwaharisha kutokana na nini? aliutwaharisha kutokana na

    ushirikina na uzushi na mambo yasiyo kubalika katika dini kama alivyo

    utwaharisha kutokana na na najsi au uchafu wa takataka.

    Msiombe enyi watu pamoja na Mwenyezi Mungu yeyote, msiombe nusra kwa

    yoyote pamoja na Mwenyezi Mungu, kama vile kusema: ewe Mwenyezi

    Mungu, ewe Muhammad, ewe Mwenyezi Mungu, ewe Abdul Qaadir,

    au kusema: ewe Abdul Qaadir, ewe Muhamad, au mfano wa hayo, hakika

    Mwenyezi Mungu haridhii hayo na hayakubali.

    Hakuna yeyote anae toka katika hukumu hiyo hakuna malaika alie karibu na

    Mwenyezi Mungu, wala mtume alie tumwa na Mwenyezi Mungu, wala sanamu

    au mzimu, wala kaburi la shekh, au walii, wala aliye kufa, vyovyote atakavyo

    kuwa.

    Qauli ya Mwenyezi Mungu {…basi msimuabudu yeyote pamoja na Mwenyezi

    Mungu} (Al-Jinn18).

    Inakusanya wote wenye kuombwa kinyume cha Mwenyezi Mungu, na Aya hii

    imeonyesha kuwa ibada haikupi manufaa mpaka uifanye ukiwa na Tauhiidi, na

    kwa hakika ukiichanganya na ushirikina basi inabatilika, na inakua ni mzigo

    kwa mfanyaji, kisha akasema Mwenyezi Mungu: {Nahakika misikiti ninyumba

    za Mwenyezi Mungu...} ni wajibu ijengwe misikiti kwa nia ilio takasika kwa

    ajili ya Mwenyezi Mungu, na siyo kwa ajili ya kujionyesha, au kutaka asikike,

    au kwasababu ubaki utajo wake baada ya kufa kama wanavyo sema, au uwe

    msikiti ni athari za kiislam, kujenga msikiti kwa sababu ya mambo hayo haifai.

  • 30

    Misikiti inajengwa kwasababu ya kufanya ibada, na kwa nia ya kufanya ibada,

    na iwe nia imetakasika kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mwenye nguvu alie

    tukuka, na misikiti inajengwa kwa lengo la kuchuma thawabu, na haijengwi

    kwasababu ya kuchuma haramu, kwasababu misikiti ni ya Mwenyezi Mungu,

    Kutoka kwa Abii Hurayra (r.a) alisema: alisema Mtume (s.a.w): "Na hakika

    Mwenyezi Mungu hapokei ila kitu kizuri" Imepokelewa na Muslim (1015).

    Na misikiti inajengwa kwa pesa ya halali, na iwe niya ya kujenga hiyo misikiti

    ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu mwenye nguvu aliye tukuka, hataki ingwe

    kwa sifa za watu au kubakia utajo wa mtu, au kujionyesha au kutaka asikike,

    hakika kujenga msikiti ni ibada na ibada ni wajibu iwe kwaajili ya Mwenyezi

    Mungu mshindi na mtukufu.

    Ndugu katika imani hii nisehemu ya pili katika kitabu hiki cha Masomo katika

    umuhimu wa Tawhiid .(2) Muhtasari wa kitabu cha Al-Usulu AL-Thalathah cha

    Imamu Fawzani Allah amuhifadhi tuwe pamoja katika sehemu ya tatu Allah

    akiipenda .

  • 31

    WALAA NA BARAA.

    3.Mwenye kumtii Mtume (s.a.w) na akampwekesha Mwenyezi

    Mungu,haifai kwake kuwapenda wale wenye kumfanyia uadui

    Mwenyezi Mungu na mtume wake hata kama watakuwa niwatu

    wakaribu zaidi.

    Haifai kwa mwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu kumpenda

    mwenye kumfanyia uadui Mwenyezi Mungu na mtume wake

    hatakama atakuwa nimtu wakaribu zaidi.

    Haya maswala ya walaa na baraa(kupenda kwa ajili ya Mwenyezi

    Mungu na kuchukia kwajili ya Mwenyezi Mungu) Nikatika maswala

    ya tauhiidi,pia nikatika haki ya tauhidi kuwapenda mawalii wa

    Mwenyezi Mungu,na kuwachukia maadui wa Mwenyezi Mungu.

    Muislam anawapenda wapenzi wa Mwenyezi Mungu,yaani hatakiwi

    kupenda ila vipenzi vya Mwenyezi Mungu,na awanusuru muislam

    anatakiwa awe karibu na waislam wapendane,kama alivyo sema

    Mwenyezi Mungu:{….Na jamaa wa nasaba wanastahikiana wenyewe

    kwa wenyewe zaidi katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu…. }(Al

    Anfaal 75) hayawi mapenzi baina ya muislam na kafiri,bali yanakuwa

    baina ya waislam,kama alivyo sema Mwenyezi Mungu:{….wala

    Mwenyezi Mungu hatawapa makafiri njia ya kuwashinda Waumini

    }.(An-Nisaa 141).

    Hivyo ndivyo inavyo paswa kwa waumini watambulike kwa

    makafiri,haifai kwa yoyote mwenye kumpwekesha Mwenyezi

    Mungu,na akamtii mtume (s.a.w)kuwapenda wenye kumfanyia uadui

    Mwenyezi Mungu.

    Na kufanya uaduia maana yake:nimtu kua katika upande na

    Mwenyezi Mungu mtukufu na mtume wake kua upande

    mwingine,(yaani wako tofauti).

  • 32

    Maana ya kusema (Hatakama nindugu wakaribu):

    Yaani katika upande wa nasabu,pindi atakapo kua nindugu yako

    wakaribu nimwenye kumfanyia uadui Mwenyezi Mungu na mtume

    wake(s.a.w)niwajibu juu yako kumfanyia uadui na kukata undugu nae.

    Na yoyote atakae kua kipenzi wa Mwenyezi Mungu na mtume wake

    (s.a.w) niwajibu juu yako kumpenda na umfanye kuwa rafiki yako

    hatakama nimtu wako wambali katika nasabu,hatakama atakuwa

    nimuejemi(Mtu asie kuwa wa rangi yako au lugha yako) au

    mweusi,au mweupe,au mwekundu, niwajibu kwako kumfanya rafiki

    na kumpenda, akiwa niwakutoka katika mji wako au niwakutoka

    mashariki ya mbali,au magharibi yambali,alisema Mwenyezi Mungu

    mtukufu:{ Na Waumini wanaume na Waumini wanawake wao kwa

    wao ni marafiki walinzi…}(Tawba71)

    Yaani baina ya waumini kuna mapenzi na kunusuriana na

    kusaidiana,na baina yao kuna kuzoweana baina ya waislam.

    Na ushahidi nikaulia ya Mwenyezi Mungu:{Huwakuti watu wanao

    muamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho kuwa wanawapenda

    wanao mpinga Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hata wakiwa ni

    baba zao, au watoto wao, au ndugu zao, au jamaa zao. Hao ameandika

    katika nyoyo zao Imani, na amewapa nguvu kwa Roho itokayo kwake.

    Na atawaingiza katika Mabustani yapitayo mito kati yake. Humo

    watakaa daima. Mwenyezi Mungu awe radhi nao, na wao wawe radhi

    naye. Hao ndio Hizbullahi, Kundi la Mwenyezi Mungu. Hakika Kundi

    la Mwenyezi Mungu ndilo lenye kufanikiwa}.(AlMujaadalah 22)

    Maneno hayo ameelezwa mtume (s.a.w) kwamba hayatokei hayo wala

    hayapo kamwe kwamba awe mtu nimwenye kumuamini Mwenyezi

    Mungu na mtume wake akawa anawapenda makafiri,ikiwa

    atawapenda basi huyo hawi nimuumini hatakama anadai kua yeye ni

    muumini.

    Alisema ibn Qayyim Allah amrehemu:

    Unawapenda maadui wa kipenzi na unadai Kumpenda!

    Haiwezekani kupatikana mapenzi.

  • 33

    Kisha unawafanyia uadui nakuwapiga vita wapenzi wake!

    Yakowapi mapenzi ewe ndugu wa Shetani!

    Hilo haliwezekani kamwe kuwapenda makafiri,kasha anasema:mimi

    nampenda Mwenyezi Mungu na mtume wake (s.a.w) kwakauli yake

    Mwenyezi Mungu: {Enyi mlio amini! Msiwafanye adui zangu na adui

    zenu kuwa marafiki mkiwapa mapenzi,…}( Al Mumtah'inah1) mpaka

    alipo sema Mwenyezi Mungu:

    {Hakika nyinyi mna mfano mzuri kwenu kwa Ibrahim na wale walio

    kuwa pamoja naye, walipo waambia watu wao: Hakika sisi

    tumejitenga nanyi na hayo mnayo yaabudu badala ya Mwenyezi

    Mungu. Tunakukataeni; na umekwisha dhihiri uadui na chuki baina

    yetu na nyinyi mpaka mtakapo muamini Mwenyezi Mungu peke

    yake…}(Al Mumtah'inah 4).

    Na amesema Mwenyezi Mungu:{Wala haikuwa Ibrahim kumtakia

    msamaha baba yake ila kwa sababu wa ahadi aliyo fanya naye. Lakini

    ilipo mbainikia kwamba yeye ni adui ya Mwenyezi Mungu,

    alijiepusha naye. Hakika Ibrahim alikuwa mwingi wa kuomba,

    mnyenyekevu, mvumilivu}

    (Tawba114).

    Hii ndio dini ya nabii Ibrahim alimkana baba yake na ndie mtu

    wakaribu wakati alipo baini kua niaduwi wa Mwenyezi Mungu.

    Na aya zimeonyesha pia kua kuwapenda makafiri kunapingana na

    imani ya kumuamini Mwenyezi Mungu nasiku ya Qiyama,ima katika

    asili ya imani au ukamilifu wake,lakini ikiwa kuwapenda kwao

    nipamoja na kuwaunga mkono katika midhehebu yao au mwenendo

    wao na ukafiri wao basi huko nikutoka katika uislam.

    Na ama ikiwa nikuwapenda bila ya kuwanusuru hii inazingatiwa kua

    niyenye kupunguza imani,na niuovu ambao una dhofisha imani.

    Na kauli ya Mwenyezi Mungu :{hao}inakusudia wale ambao wanao

    wanajitenga mbali na mapenzi ya kuwapenda wale wenye kumfanyia

    uadui Mwenyezi Mungu na mtume wake.

  • 34

    Na maana ya kauli ya Mwenyezi Mungu:{ Hao ameandika katika

    nyoyo zao Imani }

    Yaani amethibitisha Mwenyezi Mungu katika nyoyo zao na

    akazamisha katika nyoyo zao imani.

    Na ndio Mwenyezi Mungu akasema{na amewapa nguvu kwa Roho

    itokayo kwake. Na atawaingiza katika Mabustani yapitayo mito kati

    yake}.

    Alisema Mwenyezi Mungu mtukufu{Sema: Ameiteremsha hii Roho

    takatifu kutokana na Mola wako Mlezi kwa haki, ili awathibitishe

    wale walio amini, na kuwa ni uwongofu, na ni bishara kwa

    Waislamu}(An Nahl102)

    Na alisema Mwenyezi Mungu:

    {Ameuteremsha Roho muaminifu, } (Shu'araa193).

    Na amewapa nguvu kwa Roho itokayo kwake,yaani aliwapa nguvu

    kutoka kwa Mwenyezi Mungu mtukufu,na nguvu ya imani katika

    dunia,na akhera atawaingiza peponi pepo ambayo ina miti ilio shikana

    na mito na majumba mazuri.

    Na amesema Mwenyezi Mungu katika kuisifu pepo:{Na atawaingiza

    katika Mabustani yapitayo mito kati yake…}na wataishi humo bila

    kutolewa,alisema Mwenyezi Mungu mtukufu{ Watadumu humo;

    hawatataka kuondoka}(kahf 108. )

    Hawata ogopa kifo wala yoyote atakae kuja kuwatowa peponi,au

    kuwafukuza mfano wa yaliomo duniani,anaweza kua mtu duniani

    katika majumba mazuri lakini hawezi kusalimika na umauti ukamtowa

    katika majumba hayo,na pia hasalimiki na maadui kumvamia na

    kumtoa,mwanadamu daima katika dunia nimwenye kuogopa.

    Kauli ya Mwenyezi Mungu:{Mwenyezi Mungu awe radhi nao, na

    wao wawe radhi naye…}walipo wachukiza ndugu zao makafiri na

    wakawafanyia uadui aliwapa Mwenyezi Mungu ridhaa kutoka kwake

    Mwenyezi Mungu mtukufu malipo yao,hakika wao walipewa badala

    ya ya yale maudhi ya ndugu zao makafiri walipewa ridhaa ya

  • 35

    Mwenyezi Mungu mtukufu aliwaridhia Mwenyezi Mungu na wao

    wakaridhika.

    Kauli ya Mwenyezi Mungu{hao ndio kundi la Mwenyezi Mungu

    }yaani ndio jamaa wa Mwenyezi Mungu ama makafiri nikundi la

    shetani amesema Mwenyezi Mungu {hao ndio kundi la

    shetani}(almujaadala 19) .

    yaani ndio jamaa wa shetani na ndio wanao mnusuru shetani,

    Na ama waumini ndio wanao mnusuru Mwenyezi Mungu mtukufu.

    Maswala haya yana ambatanana kuwafanyia uadui makafiri na kuto

    kuwapenda,na haipelekei kwamba tukate uhusiyano na makafiri katika

    mambo yenye manufaa ya kidunia bali kuna mambo ambayo yanayo

    toka katika hukumu hii:

    1.Pamoja na kuwachukia na kuwafanyia uadui niwajibu kwetu

    kuwalingania wamfuate Mwenyezi Mungu mtukufu,niwajibu

    tuwalinganie waingie ndani ya uislam na tusiwaache tukasema:

    Hao nimaaduwi wa Mwenyezi Mungu na nimaadui zetu na inapaswa

    kwetu tuwalinganie wamfuate Mwenyezi Mungu huwenda Mwenyezi

    Mungu akawaongoza.

    2.Hakuna pingamizi kufanya mkataba na makafiri ikiwa waislam

    watahitaji hilo,kwakuwa waislam hawawezi kuwapiga vita,na

    inahofiwa kwa waislam shari zao.

    3.Hakuna pingamizi kuwalipa kwa wema wao kwa waislam,hakuma

    kiziwizi kuwalipa kwa wema walio ufanya,amesema Mwenyezi

    Mungu mtukufu:

    {Mwenyezi Mungu hakukatazini kuwafanyia wema na uadilifu wale

    ambao hawakukupigeni vita, wala hawakukutoeni makwenu. Hakika

    Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao uadilifu}.(Al Mumtah'inah

    8).

    4.Mzazi akiwa nikafiri inapasa kwa mtoto wake muislam amfanyie

    wema,lakini asimtii katika ukafiri kwa kauli ya Mwenyezi Mungu

    mtukufu:

  • 36

    {Na tumemuusia mtu kwa wazazi wake wawili. Mama yake

    ameichukua mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na

    kumwachisha ziwa baada ya miaka miwili. (Tumemuusia): Nishukuru

    Mimi na wazazi wako. Ni kwangu Mimi ndiyo marudio(14).

    Na pindi wakikushikilia kunishirikisha na ambayo huna ilimu nayo,

    basi usiwat'ii. Lakini kaa nao kwa wema duniani, nawe ishike njia ya

    anaye elekea kwangu. Kisha marejeo yenu ni kwangu Mimi, na Mimi

    nitakuambieni mliyo kuwa mkiyatenda}( Luqman14-15)

    Mzazi ana haki akiwa kafiri, lakini usimpende mapenzi ya moyoni,

    bali unamfanyia wema kama ujira wa kukulea nakwasababu yeye

    nimzazi,na ana haki kwako umfanyie wema.

    5.Kubadilishana biashara pamoja na makafiri na kununua kwao, na

    kununua mahitaji kwao na kuchukua bidhaa na silaha utoka kwa

    makafiri kwa kulipia pesa hilo halina tatizo,na alikuwa Mtume (s.a.w)

    ana alifanya kazi na makafiri,na alifanya kazi mtume (s.a.w)na watu

    wa khaybar nao ni Mayahudi alifanya nao kazi ya walime shamba

    kwa makubaliyano ya kile kitakacho vunwa kutoka shambani,kufanya

    hivyo sio kuwapenda makafiri,bali nikubadilishana masilahi.

    Niwajibu tufahamu mambo haya,na hayaingii katika kuwapenda

    makafiri na hayakukatazwa.

    Hakuna makatazo ya haya kwasababu mambo hayo niyakidunia

    na maslahi hayana maana ya mapenzi moyoni,lazima tutofautishe

    baina ya maslahi na kupenda,kwasababu kuna baadhi ya watu

    wakisikia dalili za kuwafanyia uaduwi makafiri na kuto kuwapenda

    huwenda wakafahamu kua hawafanyi nao kazi za kidunia,na

    hawafanyi mawasiliano na makafiri,na wanaelewa kua nikukata

    mafungamano nao moja kwa moja,

    Hapana!kuwapenda makafiri na kuwafanyia uadui kumewekewa

    mipaka kwa hukumu na mipaka na masharti zinazo julikana kwa wana

    wachuoni ilio chukuliwa kutoka katika Quraan na sunna za mtume

    (s.a.w).

    6.Mwenyezi Mungu Alihalalisha kuoa wanawake wa kiyahudi na

    kinaswara kwa sharti wawe niwenye kujihifadhi na kujiweka mbali na

  • 37

    zinaa katika heshima zao,na akahalalisha Mwenyezi Mungu kula

    wanyama walio chinjwa na mayahudi na manaswara.

    7.Hakuna ubaya kuitikia wito wao na kula chakula cha halali kama

    alivyo fanya mtume (s.a.w).

    8.Kuwafanyia wema majirani ambao nimakafiri kwasababu wana haki

    ya ujirani.

    9.Haifai kuwadhulumu makafiri alisema Mwenyezi Mungu

    mtukufu:{…Wala kuchukiana na watu kusikupelekeeni kutofanya

    uadilifu. Fanyeni uadilifu. Hivyo ndio kuwa karibu mno na

    uchamngu…}(Al-Maida8).

    Fahamu Mwenyezi Mungu akuongoze kwa kumtii

    Maneno haya nikama mwanzo wa ujumbe watatu kwasababu zimepita

    jumbe mbili:

    -Ujumbe wakwanza: Nimaswala manne ambayo yalikusanya suratu

    Al Asri,

    -Ujumbe wapili: Nimaswala ya matatu ambayo yamepita.

    -Ujumbe watatu: Ndio hii,na utakuja ujumbe wa Nne nao una

    maswala ma Nne.

    Kaanza mtunzi wa kitabu kwa kusema :(Mwenyezi Mungu

    akuongoze) hii ni dua ya shekh Allah amrehemu kwa kila atakae soma

    ujumbe huu kwa lengo la kuufahamu na kutafuta elimu kwa kusoma

    ujumbe huu,kwamba Mwenyezi Mungu amuongoze,

    Na muongozo ni Mwenyezi Mungu kukuongoza kupita njia ya sawa

    na kukupa taufiiqi ya kupata elimu yenye manfaa,na kufanya matendo

    mema,na uongofu nikinyume cha upotovu,

    Amesema Mwenyezi Mungu mtukufu:{Kwani Uwongofu umekwisha

    pambanuka na upotofu}( Al-Baqara 256)

    Na amesema Mwenyezi Mungu mtukufu:{Na wao wakiona kila Ishara

    hawaiamini. Wakiiona njia ya uwongofu hawaishiki kuwa ndiyo njia;

  • 38

    lakini wakiiona njia ya upotofu wanaishika kuwa ndiyo njia}.( Al-

    A'raaf)

    Na uongofu katika aya makusudio yake nidini ya uislam,na upotovu

    unakusudiwa dini ya Abuu Jahli,(Allah amlani).

    Hakika muislam pindi anapo ongozwa na Mwenyezi Mungu akawa

    nimenye kumtii basi atakuwa nimwenye kufanikiwa katika duniani na

    akhera,na kutii nikutekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu

    nakujiepusha makatazo yake,huko ndio kumtii Mwenyezi Mungu,

    Mwanadamu anatakiwa umtii Mwenyezi Mungu katika maamrsho

    yake uyafanye,na katika makatazo yake ujiepushe kuyafanya

    kwakutekeleza amri za Mwenyezi Mungu,na kutarajia malipo yake

    Mwenyezi Mungu mshindi mtukufu na utarajie thawabu zake,na

    uogope adhabu zake,yoyote atakae pewa taufiiqi ya kumtii Mwenyezi

    Munguna akaongozwa kuwa nimwenye umtii Mwenyezi Mungu

    hakika atakuwa nimwenye mafanikio duniani na akhera.

    UJUMBE WA TATU

    UISLAM NDIO DINI YA NABII IBRAHIM.

    Nini maana ya Uhanafiyyah:

    Uhanafiya ambao muislam anatakiwa ajifundishe na aujue nikwamab

    uhanafiyyah:Nidini ambayo alikuwa nayo Nabii Ibrahim (s.a.w).

    Nayo nidini ambayo inapingana na ushirikina na inaamrisha

    wanadamu woote washikamane na Tauhiid(kumpwekesha Mwenyezi

    Mungu mmoja bila kumshirikisha na chochote).

    Na nabii Ibrahim (s.a.w) alikuwa mwenye Uhanafiyyah na ni

    Muislam,

    Uhanafiya wa nabii Ibrahimu maana yake alikuwa nimwenye kupinga

    ushirikina, na nimwenye kumpwekesha Mwenyezi

    Mungu(Tauhidi),na nimwenye kufanya ibada zake zoote kwajili ya

    Mwenyezi Mungu,alisema Mwenyezi Mungu mtukufu:{. Hakika

    Ibrahim alikuwa mfano mwema, mnyenyekevu kwa

  • 39

    MwenyeziMungu, mwongofu, wala hakuwa miongoni mwa

    washirikina}( An Nahl 120).

    Uhanafiyyah nikatika sifa za nabii Ibrahim (s.a.w) ambayo maana

    yake nikupuuziya na kupiga vita ushirikina na nimwenye kuelekea

    moja kwamoja kwenye Tauhidi.

    Alielekea kwenye Tauhidi katika mambo yake yote nakuwa na ikhlasi

    katika mambo yake yote,amesema MwenyeziMungu mtukufu:{ Kisha

    tukakufunulia ya kwamba ufuate mila ya Ibrahim, mwongofu,wala

    hakuwa miongoni mwa washirikina}(An Nahl 123).

    Na amesema Mwenyezi Mungu mrukufu:

    { Ibrahim hakuwa Yahudi wala Mkristo, lakini alikuwa mwongofu

    Muislamu, wala hakuwa katika washirikina}

    (Al 'Imran67)

    Hizi nisifa kubwa za nabii Ibrahim(s.a.w) ambazo miongoni mwazo ni

    Alhanafiyyah nakwamba dini yake ni Alhanafiya nayo nidini ilio

    takasika kwaajili ya Mwenyezi Mungu mshindi mwenye nguvu,dini

    ambayo haina ushirikina ndani yake,na ameamrisha Mwenyezi Mungu

    Mtukufu mtume wake Muhammad (s.a.w)aifate dini ya nabii Ibrahim

    kwa kusema:{Kisha tukakufunulia ya kwamba ufuate mila ya Ibrahim,

    mwongofu,wala hakuwa miongoni mwa washirikina}.(An Nahl 123.)

    Na tukaamrishwa pia tufuate dini ya nabii Ibrahim (s.a.w)

    kwakusema:{Yeye amekuteueni. Wala hakuweka juu yenu mambo

    mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim. Yeye

    (Mwenyezi Mungu) alikuiteni Waislamu }(Hajj78).

    Nayo ndio dini ya mitume wote.

    Lakini kwakuwa nabii Ibrahim (s.a.w) nimbora wa mitume baada ya

    Muhammad(s.a.w)alikutana katika njia ya kulingania kwenye

    Tauhiidi(kumpwekesha Mwenyezi Mungu peke yake bila

    kumshirikisha na chochote) na adhabu na mitihani ambayo hakuna

    mtume alie kutana nayo akasubiri,

  • 40

    Nakwakua nabii Ibrahim(s.a.w) ndio baba wa mitume,hakika mitume

    walio kuja baada yake woote nikatika kizazi chake(s.a.w) basi uislam

    ndio dini ya mitume wote,na uislam(Alhanafiyyah) nikulingania watu

    wampwekeshe Mwenyezi Mungu mmoja na wasimshirikishe na

    chochote,hii ndio dini ya manabii wote,lakini zama ilipo kua kwa

    nabii Ibrahim msimamo kwa dini hii basi alinasibishwa kwake na

    mitume walio kuja baada yake,na mitume wote baada yake

    Walikuwa kwenye dini ya nabii Ibrahim,nayo nidini ya kumpwekesha

    Mwenyezi Mungu mmoja bila kumshirikisha na chochote na

    kumtakasia utii Mwenyezi Mungu mtukufu(yaani ibada zako zote

    ziwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu).

    Niipi dini hii ambayo ameamrishwa mtume Muhamad (s.a.w)kuifuata

    na tume amrishwa na sisi uifuata?

    Niwajibu juu yetu kuijiwa,kwasababu muislam niwajibu kwake

    kuyajuwa yale aliyo muamrisha Mwenyezi Mungu ili kuyatekeleza,na

    haitoshi kujinasibisha na uislam bila kuufahamu uislam wake,na

    hajuwi mambo ambayo yanatengua uislam,na nizipi sheria za uislam,

    na hukumu za uislam, na haitoshi kujinasibisha na dini ya nabii

    Ibrahim(s.a.w) ilihali hauijuwi,na utakapo ulizwa kuhusu dini ya nabii

    Ibrahim(s.a.w) unasema: sijuwi, kuwa hivyo kwa muislam haifai,

    niwajibu uijuwe dini yako vizuri ili uifuate ukiwa unaijuwa na ili

    usiache chochote ila umekitekeleza.

    NIWAJIBU KWA MWANADAMU AMUABUDU MWENYEZI

    MUNGU PEKE YAKE NA AFANYE IBADA ZOTE KWAAJILI

    YA MWENYEZI MUNGU.

    Dini ya nabii Ibrahim(s.a.w),inafundisha kumuabudu Mwenyezi

    Mungu mmoja na kufanya ibada zote kwa ajili ya Mwenyezi

    Mungu,nakumtakasia dini.

    Kufanya hivyo kunatakiwa mambo mawili:

    1.Kufanya Ibada.

    2.Kuwa na Ikhlasi (kufanya ibada zote kwa ajili ya Mwenyezi

    Mungu).

  • 41

    Atakae muabudu Mwenyezi Mungu na hakuwa na ikhlasi haitakuwa

    amefanya ibada yoyote, mwenye kumuabudu Mwenyezi Mungu

    ,akafunga na akahiji,na akaswali au kufanya umra,na akatoa sadaka,na

    akatoa zaka,na akafanya ibada nyingi lakini hakuzifanya kwa ajili ya

    Mwenyezi Mungu mtukufu katika ibada zake,ima kwasababu ya

    kujionyesha(Riyaa) au kwa kutaka sifa,au amechanganya ibada yake

    na chochote katika mambo ya ushirikina,kama kuomba kisichokua

    Mwenyezi Mungu,au kuomba nusra kwa asie kua Mwenyezi

    Mungu,au kuchinja kwa asie kua Mwenyezi Mungu,hakika mtu wa

    namna hiyo hatakuwa amefanya ibada kwa ajili ya Mwenyezi

    Mungu,bali atakuwa ni Mshirikina,na hatakuwa katika dini ya nabii

    Ibrahim(s.a.w).

    Wengi miongoni mwa wanao jinasibisha kwenye uislam katika zama

    zetu wana angukia katika shirki kubwa kwa sababu ya kuomba asie

    kuwa Mwenyezi Mungu,nakuabudu makaburi nakuchinja kwenye

    makaburi,na kuyatolea nadhiri makaburi,na kutufu kwenye makaburi

    na kutabaruku (kutaka baraka) kwenye makaburi,nakuomba nusra kwa

    watu waio kufa namengineyo,nawao wanasema niwaislam.

    Hao hawakujuwa dini yao au waliijuwa wakapinga wakiwa wanajuwa

    na hali hii ndio mbaya zaidi Mwenyezi Mungu atukinge.

    Dini ya nabii Ibrahim (s.a.w) haikubali ushirikina kwa namna yoyote

    itakavyo kuwa na atakae changanya ibada yake na ushirikina basi

    hatakuwa katika dini ya nabii Ibrahim (s.a.w),hatakama atajinasibisha

    na dini hiyo,na akadai kuwa ni muislam,jambo la wajibu nikuijua dini

    ya nabii Ibrahim (s.a.w) na kuifanyia kazi na ujilazimishe nayo kwa

    kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake na kumtakasia ibada bila ya

    kumshirikisha.

    Isiwe katika ibada zako chochote katika ushirikina sawa ikiwa nishirki

    ndogo au shirki kubwa.

    Hii ndio dini ya nabii I brahim (s.a.w) ilio takasika na shirki na

    kuupiga vita ushirikina kwa aina zake zote na ikahimiza watu

    washikamane na Tauhiidi kwa ujumla wake nakuwataka watu wote

    wamuabudu Mwenyezi Mungu mmoja na kumtakasia ibada.

    Na kwasababu hiyo ameamrisha Mwenyezi Mungu watu wote na

    aliwaumba kwasababu ya ibada.

  • 42

    Katia maneno kuna ishara ya kua mwanadamu anatakiwa amuabudu

    Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia dini,yani afanye ibada kwa ajili ya

    Mwenyezi Mungu,ameamrisha Mwenyezi Mungu watu

    wote,kawaamrisha watu wajinsia zote ,watu wote tangu kwa Adamu

    mpaka kwa binadamu wamwisho katika dunia hii,wote Mwenyezi

    Mungu kawa amrisha Mwenyezi Mungu wamuabudu yeye na

    wamtakasie ibada, anasema Mwenyezi Mungu mtukufu:{ Enyi watu!

    muabuduni Mola wenu mlezi aliye kuumbeni nyinyi na wale wa kabla

    yenu, ili mpate kuokoka{.

    Mwenyezi Mungu) ambaye amekufanyieni hii ardhi kuwa kama

    tandiko, na mbingu kama paa, na akateremsha maji kutoka mbinguni,

    na kwayo akatoa matunda yawe riziki zenu. Basi msimfanyizie

    Mwenyezi Mungu washirika, na hali nyinyi mnajua}.(Al Baqaraa21-

    22)

    Hakika Mwenyezi Mungu hana mfano,na hana anae fanana nae, wala

    wala anae lingana nae, nahaya nimakatazo ya shirki kubwa na shirki

    ndogo.

    Ameamrisha Mwenyezi Mungu watu wote wakwanza wao na

    wamwisho wao.

    Na Mwenyezi Mungu kawaumba kwasababu ya ibada wamuabudu

    yeye peke yake bila kumshirikisha, na wanadamu wameumbwa

    kwasababu ya ibada,kama alivyo sema Mwenyezi Mungu

    :{Nasikuumba majini wala watu ila kwasababu waniabudu}(Al

    dhariyati 56).

    na wameamrishwa hivyo katika k kauli yake Mwenyezi Mungu

    mtukufu:{Enyi watu mlio amini muabuduni mola wenu ambae ale

    kuumbeni}(Al Baqara 21).

    Hii ndio maana ya kusema (Kakuumbeni Mwenyezi Mungu

    kwasababu ya ibada na akawaamrisha waitekeleze ibada),

    Imekusanya kauli hii mambo mawili:

    1.Mwenyezi Mungu amewamrisha waja wake wafanye ibada.

    2. Mwenyezi Mungu amewaumba waja wake kwasababu ya ibada,

  • 43

    Kama alivyo sema Mwenyezi mungu:{Sikuwaumba majini na

    wanadamu ila waniabudu}kauli ya Mwenyezi mungu{sikuwaumba

    majini na watu} Mwenyezi mungu ndie muumbaji yeye ndie alie

    umba vitu vyote na kayika hivyo aliumba majini na watu na akawapa

    akili na akawalazimisha wamuabudu yeye peke yake wasimshirikishe

    na lolote na akatowa amri maalumu kwa majini na watu wamuabudu

    yeye Mwenyezi mungu peke yake,kwasababu Mwenyezi mungu

    amewapa akili na akawapa maarifa yakupambanua kitu chenya

    madhara na chenye manufaa,na ja jambo lahaki na labatili,na akaumba

    mambo mengi kwa maslahi ya majini na watu na manufaa yao.

    Na amefanya vikutumikieni vilivyomo anasema Mwenyezi mungu:{

    mbinguni na vilivyomo katika ardhi, vyote vimetoka kwake. Hakika

    }(Al jathiya13) katika hayo zimo Ishara kwa watu wanao fikiri

    Vyote vimewekwa kwa ajili ya mwanadamu ili avitumie kuweza

    kufikia lengo la kuletwa hapa duniani ambalo ni Ibada.

    Anasema Mwenyezi mungu {Sikuwaumba