Maelezo ya msingi kuhusu Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai · Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na...

16
Maelezo ya msingi kuhusu Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai Utayarishaji na matumizi Mwandishi: Janet Maro Wachoraji: Godwin Chipenya na Emmanuel Grieshaber Toleo la kwanza Mei 2011

Transcript of Maelezo ya msingi kuhusu Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai · Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na...

Maelezo ya msingi kuhusu Mboji/Mbolea

Vunde/Mbolea Hai

Utayarishaji na matumizi

Mwandishi: Janet Maro

Wachoraji: Godwin Chipenya na Emmanuel Grieshaber

Toleo la kwanza

Mei 2011

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 2

Yaliyomo

1. Namna ya kutayarisha Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai....................................................... 3

1.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji ................................................................................ 3

1.2 Mfano wa vitu ambavyo vyaweza kutumiwa kutengeneza mboji ....................................... 5

2. Namna ya kutengeneza mboji ya mimea .................................................................................. 6

2.1 Hatua ............................................................................................................................................ 6

2.2 Zingatia ........................................................................................................................................ 7

3. Wadudu wenye manufaa na mazingira yanayohitajika kwenye Biwi.................................... 8

3.1 Wadudu ambao husaidia kufanya biwi kuoza ....................................................................... 8

3.2 Mazingira yanayohitajika kwenye biwi .................................................................................... 9

4. Matunzo ya Biwi .......................................................................................................................... 10

4.1 Maji ............................................................................................................................................. 10

4.2 Kupindua/kugeuza ................................................................................................................... 11

5. Muda wa kukomaa na matumizi ya mboji ............................................................................... 13

5.1 Muda wa kukomaa ................................................................................................................... 13

5.2 Matumizi ya mboji .................................................................................................................... 13

6. Faida za Mboji/Mbolea Vunde .................................................................................................. 14

Vitabu vya Kurejelea ............................................................................................................................. 16

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 3

1. Namna ya kutayarisha Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai

Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo

imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama

majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku

ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya

hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri.

Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye

udongo ili kuinua mazao ya shamba.

Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani

bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda

mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili

kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni

yanatumika katika kutengenezea mboji.

Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji

huchemka hata kiasi cha kuua magonjwa ya mimea na mbegu za magugu.

Majani makavu ya ndizi ni mazuri kwa kutunza vifaa vya mbolea na kuweka ukavu. Hali hii

huwa huzuia kupotea kwa maji kabla ya kujenga lundo la mboji na wakati mbolea inapokuwa

inaiva.

1.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji

Sehemu za mimea ambazo zimenyunyiziwa dawa ya kuwaua wadudu (viuatilifu) na

kwekwe juzijuzi (Pesticide/herbicides).

Vipande vya nyama kwa sababu vinavutia panya na wadudu wengine.

Sehemu nyingi za Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku))

ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu

kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa

huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya

hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 4

Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye

udongo ili kuinua mazao ya shamba.

Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani

bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda

mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili

kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni

yanatumika katika kutengenezea mboji.

Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani.

Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.

Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu.

Magugu ambayo yanarudiarudia kila mwaka. Magugu kama hayo huuliwa kwa kuanikwa

kwenye jua kali ili yakauke baadaye huchomwa ili yasienee na jivu lake laweza

kuongezwa kwenye lundo la mbolea.

Vitu visivyo kua na uhai kama plastiki na chuma.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 5

1.2 Mfano wa vitu ambavyo vyaweza kutumiwa kutengeneza mboji

VIFAA MAANDALIZI MUHIMU KUFAHAMU TAHADHARI

Nyumbani

Maganda ya

matunda

Huoza haraka

Jivu la kuni Kuna madini ya Potassium

(K) na chokaa (Lime)

Tumia kiwango

kidogo

Takataka za

kufagia

Viwango na ubora tofauti

Shambani

Mabaki ya mimea

baada ya kuvuna

Katakata vitu

vigumu. Kama ni

vikavu nyunyuzia

maji

Vitu vigumu huoza

pole pole

Usitumie vile

vilivyowekwa

dawa juzijuzi

Majani makavu/

yaliokauka

Kama ni makavu

fanya kama hapo juu

Mimea/majani ya

kijani au mabichi

Katakata kama ni

kubwa

Jamii ya kunde

hupendekezwa

Magugu Katakata kama ni

kubwa

Usitumie mizizi

ya magugu ama

mbegu za magugu

Asili

Samadi Ina rotuba nzuri sana

Mkojo Vigumu kukusanya

hupatikana kwenye

zizi la ng’ombe

Nyunyuzia kwenye

biwi/lundo la mbolea.

Hufanya mbolea kuoza

haraka

Tumia viwango

vidogo

Udongo Tumia udongo

kama sentimita 10

kutoka tabaka la juu

ya shamba

Hutumika kufunika

Biwi/lundo la mbolea

Magugu ya

baharini (Mwani)

Yafaa yakaushwe na

hutumiwa na majani

yaliyo kauka

yana madini muhimu

kwa wingi

Samadi kutoka kwa mifugo na mabaki ya mimea ni nzuri sana katika kutengeneza mbolea hai.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 6

2. Namna ya kutengeneza mboji ya mimea

Kusanya vitu na vifaa vinavyohitajika katika utengenezaji wa mboji ambayo ni;

Majani mengi mabichi/kijani na makavu. Majani jamii ya mikunde ni mazuri sana kwani

hutengeneza kirutubishi cha naitrojeni (N) kwa wingi.

Mabua ya mahindi au vitawi vya miti

Udongo wa kawaida wa juu

Samadi, mbolea yoyote ya wanyama au mboji ya zamani

Majivu au vumbi la mkaa

Maji

2.1 Hatua

1) Chagua sehemu karibu na eneo ambalo mboji itaenda kutumika na ambapo kuna hifadhi ya

kutosha kukinga dhidi ya upepo, jua na mvua.

2) Katakata majani yawe madogo madogo ili yaweze kuoza haraka. Tengeneza msingi kama mita

sita (6) urefu na upana wake mita 2 kwa kutumia majani magumu kama matawi/vijiti. Hii

itahakikisha maji yanatiririka na hewa ina zunguka vizuri. Hakikisha kuna nafasi ya kutosha

kufanyia kazi kwenye biwi bila kulikanyaga.

3) Weka sentimita 10 ya majani ambayo hayaozi haraka kwa mfano mabua vya mahindi au

mimea mibichi/kijani.

4) Weka sentimita 10 ya vifaa ambavyo huoza haraka kwa mfano maganda ya mboga na

matunda.

5) Weka sentimita 2 ya samadi (mbolea-hai ya wanyama), mabaki ya mbolea ya zamani kama

yaweza kupatikana.

6) Weka udongo wa juu sentimita 10 kutoka kwenye shamba ambalo hulimwa.

7) Majivu na mkojo vyaweza kunyunyuziwa juu ili kufanya biwi/lundo kuoza haraka.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 7

Kukatakata majani

8) Nyunyizia maji kwenye biwi mpaka lilowe.

9) Rudia mpangilio huu kuanzia namba nne (4) mpaka lundo lifike mita moja (1.m) hadi moja na

nusu (1.5m) kwenda juu isipokuwa vijiti/matawi ya kwanza.

2.2 Zingatia

Biwi/lundo cha mboji kinatakiwa kifunukwe ili kupunguza/kuzuia mvuke ama mvua

nyingi ambayo hubeba rotuba kutoka kwenye mbolea. Weka gunia, nyasi ama matawi ya

ndizi yaliyokauka.

Kila tabaka/kunjo/safu yafaa kupangwa kuanzia kwenye ukingo ili lundo la mbolea

lisiporomoke.

Namna nyigine ya kuzuia lundo kuporomoka ni kwa kuweka vipande vya mbao kando ya

biwi. Wavu wa nyuzi za chuma utafanya biwi kukauka.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 8

Katika sehemu zenye ukavu mwingi. Mianzi iliyo na mashimo husaidia kufanya hewa

kuingia na kuzunguka kwa urahisi.

3. Wadudu wenye manufaa na mazingira yanayohitajika kwenye Biwi

3.1 Wadudu ambao husaidia kufanya biwi kuoza

Viumbe wengi wanaohusika na kazi hii ya kuoza ni wadogo hawaonekani kwa macho

matupu. Ila viumbe hawa huhitaji maji, hewa na vipande/sehemu ya viumbe wengine ambazo

kwao ni chakula. Viumbe hawa hula vipande hivyo na hutoa hewa ya carbon dioxide, maji na

joto.

Kuna hatua tatu kubwa wakati biwi linapooza; hatua ya kupanda joto, hatua ya kupoa/kuwa

baridi na hatua ya kukomaa.

Wakati ya hatua ya kupanda joto, joto hufikia kiwango cha juu sana katikati mwa biwi.

Uzuri wa joto hili ni kwamba magonjwa yaliyokuwa kwenye viungo vya biwi na mbegu za

magugu huchomwa hadi kufa.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 9

Hatua ya pili ya kuwa baridi; uyoga (fungi) huwa na faida nyingi kwa sababu kazi yake ni

kuzisaga nyuzi ngumu ambazo zimo kwenye viungo vya mimea au majani.

Kwenye hatua ya tatu, ‘hatua ya kukomaa’ viumbe wakubwa kama mchwa na

nyungunyungu husaidia kusaga na kuchanganya mbolea.

Hali ya anga ikiwa na joto jingi viumbe hawa hufanya kazi haraka kuliko wakati ambapo hali

ya anga ni baridi. Aina ya viungo vilivyotumika kujenga/kukuza biwi na ukali/uchungu (pH)

wa udongo pia huathiri kiwango cha mbolea kuoza.

3.2 Mazingira yanayohitajika kwenye biwi

Biwi huhitaji vitu vitatu: hewa, maji na joto.

Hewa

Viumbe wadogo kwenye biwi huhitaji hewa ili waweze kuishi. Hewa ya carbon dioxide

(CO2) ambayo imetolewa na wadudu hawa huhitaji kutolewa nje. Ikiwa hewa safi

itakosekana, viumbe wengine wasiohitajika huingia na kutoa harufu mbaya na pia kufanya

mbolea isioze haraka.

Maji

Kazi ya viumbe wadogo huwa polepole ikiwa biwi ni kavu. Aidha ikiwa biwi litalowa maji

basi viumbe wadogo watakufa na kufanya biwi kuwa na uchachu badala ya kutengeneza

mbolea. Hivyo basi kukagua kiwango halisi cha maji huhitaji ujuzi fulani.

Joto

Biwi hutoa joto wakati linaoza. Lundo likiwa na joto jingi viumbe wadogo hutoka, kisha

huweza kurudi pindi linapopoa.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 10

4. Matunzo ya Biwi

Ili kupata mbolea nzuri, biwi linapojengwa yafaa lishughulikiwe kwa utaratibu. Biwi hilo

litahitaji maji, kupinduliwa, joto na muda unaofaa wa kukomaa.

4.1 Maji

Wakati wa kiangazi biwi/lundo la mboji huhitaji kumwagiliwa maji kila wiki. Maji katika

lundo la mbolea hupimwa kwa kuweka fungu dogo la nyasi na kulitoa baada ya dakika tano.

Nyasi isipoonyesha majimaji au unyevu itabidi maji yamwagwe kwenye lundo hilo.

Kuna njia kadha za kuzuia mvuke kuinuka kutoka kwenye biwi, hali kadhalika kiwango cha

maji yanayomwagiliwa:

Funika lundo kwa majani ya ndizi ama nyasi.

Funika lundo kwa udongo.

Lundo lisigeuzwegeuzwe

Biwi likilowa maji itabidi kifunuliwe na kuachwa kikauke kwenye jua kabla ya kujengwa

tena.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 11

4.2 Kupindua/kugeuza

Katika muda wa wiki tatu (3) baada ya kujenga/kukuza biwi/lundo ukubwa wake utakuwa

umepungua sana. Kupindua biwi uhakikishe ya kwamba majani yaliyo kando yameoza pia

hewa safi imerejeshwa. Kupindua biwi huchanganya majani yaliyotengenezwa na kukijenga

upya. Majani yalivyo kando huwekwa katikati, ikiwa kuna ukavu, maji mengi na

majani/viungo vikavu huongezwa. Kupindua kunatikiwa kufanyike kila baada ya wiki tatu.

Hali ya joto na kiwango cha maji yafaa kupimwa siku chache baada ya kupinduliwa.

Kupinduliwa kwa mara ya tatu kutahitajika ikiwa viungo havitakuwa vimeoza kikamilifu.

Muda wa kugeuza mboji baada ya kuitengeneza

Mbolea yaweza kutengenezwa bila kupinduliwa ila viungo vilivyo kando havitaoza. Mbegu

za magugu na viungo na magonjwa ya mimea hayatakufa. Viungo vilivyobaki hutengwa na

kutumiwa kwenye biwi lingine. Japokuwa kugeuza hakuna lazima, kunapendekezwa ili

kupata mbolea nzuri.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 12

4.3 Kiwango cha Joto

Kupima kiwango cha joto kwenye biwi kunahitaji kijiti kirefu kichomwe ndani ya lundo siku

kumi (10) baada ya kujengwa. Kijiti yafaa kionyeshe joto la kutosha kinapoguswa kwa

mkono, la sivyo kuoza bado hakujaanza kufanyika. Katika hali kama hii, maji ama hewa

itahitajika kwenye biwi na biwi kuachwa kwa muda. Ikiwa biwi lina joto jingi, biwi linaoza

basi viumbe hai wanaweza kufa. Katika hali hii, hewa na maji itabidi kuongezwa ili kufanya

biwi lipoe. Kiasi cha joto yafaa kupimwa mara kwa mara kwa kutumia kijiti.

Joto linalotakiwa ili mboji iweze kuiva

Chini ya 57C

Joto hili linaweza kuivisha mboji lakini haliwezi kuua mbegu za magugu na magonjwa.

57-71C

Joto muafaka kwaajili ya kuivisha mbojj na kuua mbegu za magugu na magonjwa. Katika

kiwango hiki cha joto, mbegu zote na vijimelea vyote vya magonjwa vilivyoko kwenye

mchanganyiko wa mboji hufa na hivyo kutokuwepo pale mboji inapokuwa imeiva.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 13

Zaidi ya 71C

Joto hili ni kali sana na huweza kusababisha madhara mengineyo kama vile kuzalishwa kwa

gesi zenye madhara pia wadudu wenye manufaa ambao husaidia mboji kuiva huweza

kukimbia.

Muhimu kuhakikisha kuwa joto halizidi sana ili kuweza kuwa na mboji nzuri yenye

virutubisho.

5. Muda wa kukomaa na matumizi ya mboji

5.1 Muda wa kukomaa

Lundo la mbolea yafaa liachwe likomae baada ya joto kupoa. Mbolea yaweza kutumiwa mara

tu viungo vya kwanza vinapokosa ama vinapopoteza utambusho, na rangi yake ikageuka

kuwa nyeusi na harufu ikawa ya kuvutia.

Hata wakati huu mbolea yahitaji kufunikwa ili isilowe kwa maji ya mvua ama kukauka kwa

ajili ya jua bali ibakie na unyevunyevu. Mboji ikikawia muda mrefu kabla ya kutumiwa,

hupoteza rotuba na wanyama wadogo huifanya makazi yao.

5.2 Matumizi ya mboji

Umuhimu mkuu wa mboji ni kuongeza mazao ya shamba kwa kusaidia udongo kushikilia

maji kwa muda mrefu na kufanya udongo kuwa na afya bora. Pia mbolea hufanya udongo

kushikamana hivyo hupunguza mmomonyoko wa udongo.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 14

6. Faida za Mboji/Mbolea Vunde

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 15

Mbolea hutumiwa mara nyingi kwenye shamba lililoko karibu nyumbani na mbali na

nyumba. Wakati shamba huandaliwa kwa kupanda mbegu, mbolea huchanganywa kwenye

udongo wa juu. Mbolea haifai kuwekwa ndani ya udongo kiasi cha kwamba mizizi ya mimea

haitaifikia. Njia bora ni kuweka mbolea kidogo kwenye shimo ambamo mmea utapandwa.

Kwenye sehemu za ukame, mitaro huchimbwa kisha mbolea ikawekwa ambamo maji

hukusanyika na kutumiwa na mimea.

Hupunguza magonjwa na wadudu waharibifu wa mimea yalioko udongoni hivyo basi mimea

huwa na nguvu, afya na hustahimili magonjwa na wadudu waharibifu.

Mbolea za kemikali japo hutoa rutuba kwa mimea, hazitengenezi mpangilio au hali ya

udongo. Pia ni ghali na huongeza mazao kwa muda mfupi tu. Mboji huwa haibebwi na maji

ya mvua kama ilivyo mbolea za kemikali ama za viwandani na faida yake hudumu kwa muda

mrefu.

Mimea ambayo hupandwa kwa kutumia mbolea za kemikali huvutia wadudu, kwa sababu

rangi yake humetameta na matawi yake ni mwororo mno.

Mbolea vunde pia yaweza kutumiwa ili kufunika udongo usipoteze maji mengi. Mbolea

ambayo haiko tayari hasa kutumika kwa kazi kama hii iwekwe udongoni ili iendelee kuoza na

kuchanganyika kwenye udongo. Mbolea inapotumika kwa kuzuia maji kwenye udongo, yafaa

ifunikwe kwa majani madogo (matandazo). Hii itazuia mbolea isipoteze rotuba kwa sababu ya

joto jingi na miale ya jua.

Mboji pia hutumika kukuza miche na hata kwa kuwalisha samaki.

Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea hai

Kilimo Endelevu Tanzania (SAT) na Swisscontact 16

Vitabu vya Kurejelea

Baadhi ya maelezo na michoro iliyomo humu imenakiliwa na kutafsiriwa

kutoka;

Henry Doubleday Research Association – HDRA (2005). “Composting in the

Tropics”. United Kingdom.

Kenya Institute of Organic Farming –KIOF (1994). “Field Notes on Organic

Farming”. Edited by Njoroge, J. P.O. Box 34972, Nairobi, Kenya.