Kodi ya mimba, nani alipe

32

description

a cartoon booklet written by Churchill Shakim and Richard Mabala of a story about how lack of protection can infringe the right of education to female adolescents. There is more to be done by the community if we all feel the burden the same way and start taking action.

Transcript of Kodi ya mimba, nani alipe

Page 1: Kodi ya mimba, nani alipe
Page 2: Kodi ya mimba, nani alipe

Kijitabu hiki kimetayarishwa na watendaji wa Tamasha kwa kushirikiana na Twaweza

Waandishi: Richard Mabala na Winston Churchill Shauri

Mchoraji: Daniel Mzena

Wahariri: Rakesh Rajani, Evarist Kamwaga, Joseph Ngwegwe na Justice Rutenge

Usanifu:Winston Churchill Shauri

©Tamasha/Twaweza 2011

Barua:S.L.P. 15044, Arusha, TanzaniaSimu: +255 719 751 928 +255 787 220 233

Barua pepe: [email protected] [email protected]

Tovuti: www.tamashavijana.org

Unaruhusiwa kunakili sehemu yoyote ya kijitabu hiki kwa sababu zisizo za kibiashara tu.Unachotakiwa kufanya ni kunakili chanzo cha sehemu uliyonakilia na kutuma nakala mbili kwa Tamasha.

Page 3: Kodi ya mimba, nani alipe

i

Utangulizi

Ndugu wasomaji,

Hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya aliwaagiza madiwani kutunga sheria ndogo za kuwakamata wanafunzi wa kike wanaopata mimba. "Wakilala ndani watawataja waliowapa mimba ndipo sheria za nchi zitafuatwa”

Aliendelea:"Mpango wa kuwakamata waliowapa mimba wanafunzi hautoshi kukomesha tatizo hili, sasa tuwakamate na ninyi wenye mimba, labda tumwache aliyebakwa tu, lakini wengine mmepata kwa hiari yenu na hakuna sababu ya kutowachukulia hatua".Kauli kama hizo zimetolewa na viongozi mbalimbali maana idadi ya wanaopata mimba inatisha. Kwa mujibu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika kipindi cha 2004-8, wasichana 28,590 wakiwepo 11,599 wa sekondari na 16,991 wa msingi walikatishwa masomo kwa sababu ya kupata mimba. Kutokana na ongezeko la shule za sekondari, yawezekana idadi inazidi kuongezeka.

Ni rahisi kuwalaumu wasichana wenyewe bila kuangalia mazingira yanayowasababishia kupata mimba. Katika utafiti wa kitaifa kuhusu ukatili dhidi ya watoto, iligundulika kwamba karibu theluthi ya wasichana wamenyanyaswa kijinsia. Kati yao, 5% wamelazimishwa kufanya ngono wakati ni watoto. Robo walisema kwamba walipofanya ngono mara ya kwanza, ama walidanganywa ama walishinikizwa ama walilazimishwa.

Hali hii inaonyesha kuna ulinzi dhaifu wa wasichana. Wao bado ni watoto, miili yao na akili zao hazijapevuka. Wengi sana wanadanganywa na wanaume wanaowazidi umri na mbinu.

Tufanye nini kukomesha hali hii?

Richard MabalaMkurugenzi, Tamasha

Page 4: Kodi ya mimba, nani alipe

ii

Wahusika Mjasiriamali, mchambuzi wa mambo na mkereketwa wa maendeleo

Bonge:

Bibiye:

Mwelimishaji rika, mchambuzi na mwanaharakati

Mwenyekiti:

Kiongozi anayesikiliza na kuheshimu vijana. Mpenda maendeleo lakini anaamini zaidi msaada kutoka nje kuliko nguvu ya wananchi

Mtendaji:

Mchapakazi lakini mrasimu. Hapendi vijana na azma yao ya kuchukua hatua wenyewe

Msichana aliyebakwa

Rehema:

Page 5: Kodi ya mimba, nani alipe

1

Page 6: Kodi ya mimba, nani alipe

2

Page 7: Kodi ya mimba, nani alipe

3

Page 8: Kodi ya mimba, nani alipe

4

Page 9: Kodi ya mimba, nani alipe

5

Page 10: Kodi ya mimba, nani alipe

6

Page 11: Kodi ya mimba, nani alipe

7

Page 12: Kodi ya mimba, nani alipe

8

Page 13: Kodi ya mimba, nani alipe

9

Page 14: Kodi ya mimba, nani alipe

10

Page 15: Kodi ya mimba, nani alipe

11

Page 16: Kodi ya mimba, nani alipe

12

Page 17: Kodi ya mimba, nani alipe

13

Page 18: Kodi ya mimba, nani alipe

14

Page 19: Kodi ya mimba, nani alipe

15

Page 20: Kodi ya mimba, nani alipe

16

Page 21: Kodi ya mimba, nani alipe

17

Page 22: Kodi ya mimba, nani alipe

18

Page 23: Kodi ya mimba, nani alipe

19

Page 24: Kodi ya mimba, nani alipe

20

Page 25: Kodi ya mimba, nani alipe

21

Page 26: Kodi ya mimba, nani alipe

22

Page 27: Kodi ya mimba, nani alipe

23

Page 28: Kodi ya mimba, nani alipe

24

Page 29: Kodi ya mimba, nani alipe

25

Page 30: Kodi ya mimba, nani alipe

26

Je wajua?

Unyanyasaji kijinsia wa mtoto unamwathiri kimwili, kimaadili, 1. kihisia na kiakili kwa maisha yake yote. Anaweza kujiona duni, asijijali na kujipeleka kwenye vitendo hatarishi. Kwa mujibu wa sheria, kufanya ngono na msichana chini ya miaka 2. 18 inahesabiwa kuwa kosa la ubakaji. Hii ni kwa sababu bado hajakua vya kutosha kiakili na kimwili.Licha ya sheria kali, ubakaji unazidi kushamiri, hasa kwa kuwa 3. wabakaji huchukuliwa hatua mara chache.Katika utafiti uliosimamiwa na Serikali4.

a. Ubakaji hutokea zaidi saa za mchana b. Majirani na wageni walitambulika kuwa wabakaji zaidi c. Vijana wa kiume nao wanalazimishwa d. Nusu ya wasichana na theluthi mbili ya wavulana hawakumwambia mtu baada ya kunyanyaswa kijinsia e. 80% ya wasichana na 90% ya wavulana hawakutafuta huduma baada ya kunyanyaswa. f. Watoto walionyanyaswa kijinsia wako hatarini zaidi kuambukizwa UKIMWI kwa sababu ya kufanya ngono isiyo salama1.

Katika utafiti wa TAMASHA:5. a. Wasichana walisema wanatongozwa angalau mara kumi kwa siku. b. Wasichana hawajaandaliwa kuhimili shinikizo kama hizo nyumbani wala shuleni. c. Wilaya ambapo wasichana wengi zaidi wanapanga chumba ili waende sekondari ndiyo wilaya ambapo kuna mimba nyingi zaidi.

Tukumbuke kwamba leo ni msichana yule, kesho ni mtoto wangu.6.

1 Takwimu zote zinatokana na Violence Against Children in Tanzania (URT, 2011)

Page 31: Kodi ya mimba, nani alipe

27

Msomaji: Serikali yako inataka kukusikia! Shiriki kwa kutuma maoni yako. Mawazo yako yanaweza kuboresha huduma kwa jamii na utawala bora. Pia, hii itakuza ushirikiano kati ya wananchi na Serikali. Maoni yako yanaweza kuhusiana na chochote ulichopata katika kitabu hiki. Kigezo cha kupata washindi ni ubunifu au wazo jipya.

Zawadi: Kila baada ya miezi mitatu kwa mwaka 2012, maoni ya wanafunzi yatakayotumwa kupitia shule zao yatashindanishwa. Maoni kumi bora yatachaguliwa na yatachapishwa kwenye vitabu pamoja na tovuti. Kila shule itakayoshinda itapata kompyuta ndogo mbili (laptops).

Mwisho wa maoni yako weka taarifa zako:

a) Tareheb) Majina kamili, umri wako na jina la shule/taasisic) Jinsia - Mwanaume/Mwanamked) Anuani (SLP) kamili, makazi (Kata, Wilaya, na Mkoa)e) Simu yako na/au Barua pepe (kama unayo)

Unangoja nini! Shiriki basi kwa njia zifutatazo.

Tuma kwa:

Fikiria. Paza Sauti. Twaweza!

ShindanoToa maoni, shiriki na jishindie kompyuta!

Barua OGP Ikulu,S.L.P 9120 Dar es Salaam

Barua pepe [email protected] au [email protected]

Tovuti: www.wananchi.go.tz

Page 32: Kodi ya mimba, nani alipe

Kwanza, ni vizuri kufahamu hali halisi ya jamii yetu. Wasichana wanaweza kufanya utafiti kwa wasichana wenzao ili kupata picha kamili na pia wasichana wenyewe wanaona hatua gani zichukuliwe.

Katika jamii nyingine, viongozi wakishirikiana na vijana:

Wanadhibiti ushiriki wa watoto katika maeneo hatari kama • vile disko na video au ngoma za usiku wa manane.Wanafanya mipango ya kuwalinda wasichana hasa katika • maeneo kama vile kwenda kisimani, kutafuta kuni au shambani.Wanawashirikisha vijana kuwalinda vijana wenzao.• Wanachukua hatua dhidi ya wanaoonekana wananyasaji. •

Tufanye

nini?