KANUNI MPYA 2007A

131
1 KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977 (SURA YA 2) ________ KANUNI ________ [Zimetungwa chini ya Ibara ya 89] _______ KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE, TOLEO LA 2007 _______ SEHEMU YA KWANZA UTANGULIZI 1-. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007. 2-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba, Kanuni hizi zitatumika kwa mambo yote yanayohusu utaratibu wa uendeshaji wa Shughuli za Bunge. (2) Iwapo jambo au shughuli yoyote haikuwekewa masharti katika Kanuni hizi, Spika ataamua utaratibu wa kufuata katika jambo au shughuli hiyo, kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturi za uendeshaji bora wa Shughuli za Bunge na uamuzi huo utaingizwa katika Kitabu cha Maamuzi ili kuongoza mwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa Shughuli za Bunge. 3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo yatahitaji vinginevyo:- “Akidi” ni idadi ya Wabunge inayoruhusu kufanya maamuzi ya Bunge kwa mujibu wa Kanuni za 77, 78 na 79 za Kanuni hizi; “Bendera” ni Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ina rangi ya bluu iliyoiva iliyo katika umbo la mstatili na yenye umbo dogo la bendera ya Taifa ndani yake katika Matumizi Jina Tafsiri

Transcript of KANUNI MPYA 2007A

1

KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YAMWAKA 1977

(SURA YA 2)________

KANUNI________

[Zimetungwa chini ya Ibara ya 89]_______

KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE, TOLEO LA 2007_______

SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI

1-. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2007.

2-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba, Kanuni hizi zitatumika kwamambo yote yanayohusu utaratibu wa uendeshaji wa Shughuli zaBunge. (2) Iwapo jambo au shughuli yoyote haikuwekewa masharti katikaKanuni hizi, Spika ataamua utaratibu wa kufuata katika jambo aushughuli hiyo, kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuninyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamojana mila na desturi za uendeshaji bora wa Shughuli za Bunge nauamuzi huo utaingizwa katika Kitabu cha Maamuzi ili kuongozamwenendo wa baadaye wa uendeshaji wa Shughuli za Bunge.

3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa kama maelezo yatahitajivinginevyo:-

“Akidi” ni idadi ya Wabunge inayoruhusu kufanya maamuzi yaBunge kwa mujibu wa Kanuni za 77, 78 na 79 za Kanuni hizi; “Bendera” ni Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muunganowa Tanzania ambayo ina rangi ya bluu iliyoiva iliyo katika umbo lamstatili na yenye umbo dogo la bendera ya Taifa ndani yake katika

Matumizi

Jina

Tafsiri

2

pembe juu ya upande wa kushoto na Siwa, chini kukiwa na utepewenye maneno “Bunge la Tanzania”; “Bunge” ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzanialililoanzishwa kwa mujibu wa Ibara ya 62 ya Katiba; “Bunge Jipya” ni Mkutano wa Kwanza wa Bunge ulioitishwa naRais kwa mujibu wa Ibara ya 90(1) baada ya kutangazwa matokeoya Uchaguzi Mkuu; “Chama” ni Chama cha Siasa chenye uwakilishi Bungeni; “Gazeti” ni Gazeti la Serikali ya Jamhuri ya Muungano; “Hoja ya Kamati” ni hoja iliyokubaliwa na Kamati ya Bunge baadaya majadiliano ya Kamati husika; “Hoja ya Mbunge” ni hoja inayotolewa na Mbunge asiyekuwaWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali; “Jamhuri ya Muungano” ni eneo lote lililokuwa ndani ya Mipakaya Jamhuri ya Tanganyika na eneo lote lililokuwa ndani ya Mipakaya Jamhuri ya Zanzibar kabla ya tarehe 26 Aprili, 1964; “Kamati” ni Kamati yoyote ya Bunge iliyoundwa kwa mujibu waKanuni hizi; “Kamati ya Bunge Zima” ni Kikao cha Wabunge wote wanapokaakama Kamati wakati wa:-

(a) kupitisha Muswada wa Sheria;(b) kujadili taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi

kuhusu mashtaka dhidi ya Rais au Makamu waRais;

(c) kujadili hoja ya kutokuwa na imani na WaziriMkuu; au

(d) kujadili hoja ya kumwondoa madarakani Spikaau Naibu Spika.

“Kamati ya Matumizi” ni kikao cha Wabunge wote wanapokaakama Kamati kushughulikia Makadirio ya Matumizi ya Fedha zaSerikali; “Kamati ya Mipango” ni kikao cha Wabunge wote wanapokaakama Kamati katika Mkutano wa mwezi Februari ili kujadili nakushauri kuhusu mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwakutekelezwa na Serikali katika mwaka wa fedha unaofuata; “Katiba” ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977; “Katibu” ni Katibu wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 87 yaKatiba na inajumuisha pia mtumishi mwingine yeyote wa Bungealiyeidhinishwa kutekeleza kazi yoyote ya Katibu; “Kikao cha Bunge” ni kikao cha siku moja kinachoanza kwakusomwa Dua na kumalizika kwa kuahirisha Bunge hadi sikuitakayotajwa;

Sura ya 2,Toleo la2002

3

“Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni” ni Mbungealiyeteuliwa au kuchaguliwa na Wabunge wanaounda Kambi Rasmiya Upinzani ili kuwa Kiongozi wa Kambi hiyo na inajumuisha NaibuKiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni; “Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni”ni Waziri Mkuu kamailivyoainishwa katika Ibara ya 52(2) ya Katiba; “Kitabu cha Maamuzi” ni kumbukumbu ya maamuzi mbalimbaliya Spika kuhusu suala lolote la utaratibu Bungeni; “Madaraka ya Bunge” ni haki na madaraka ya Bunge kamayalivyofafanuliwa katika Ibara ya 100 ya Katiba na katika Sheria yaKinga, Madaraka na Haki za Bunge; “Maisha ya Bunge” ni muda wote unaoanzia tarehe ambapoBunge Jipya limeitishwa na Rais kukutana kwa mara ya kwanzabaada ya Uchaguzi Mkuu na kuishia tarehe ya kuvunjwa kwa Bungekama ilivyoelekezwa na Ibara ya 65 ya Katiba; “Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu waIbara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri yaMuungano; “Mkutano wa Bunge” ni mfululizo wa vikao vya Bunge, kuanziakikao cha kwanza hadi cha mwisho; “Mgeni” maana yake ni mtu yeyote ambaye si Rais, Mbunge,Katibu au mtumishi yeyote na ambaye hatekelezi kazi rasmizinazohusu Bunge; “Mpambe wa Bunge” ni mtumishi wa Ofisi ya Bungeanayetekeleza majukumu yaliyoainishwa katika Kanuni ya 20 yaKanuni hizi; “Mwenyekiti” ni Mbunge aliyechaguliwa kuongoza Shughuli zaBunge na pia lina maana ya Spika, Naibu Spika au Mbunge mwingineanapokuwa anaongoza Kamati ya Bunge Zima, Kamati ya Matumiziau Kamati ya Mipango na vilevile inajumuisha Mbunge yeyoteanayeongoza Kamati ya Kudumu, Kamati Ndogo ya Kamati yaKudumu, Kamati Teule au Mkutano wa Uchaguzi wa Spika; “Naibu Spika” ni Mbunge aliyetajwa kuwa Naibu Spika wa Bungekwa mujibu wa Ibara ya 85 ya Katiba na kuchaguliwa kwa mujibuwa Kanuni ya 10 ya Kanuni hizi; “Naibu Waziri” ni Mbunge aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu waIbara ya 55(2) na (3) ya Katiba; “Orodha ya Shughuli” ni karatasi mahususi zinazooneshampangilio wa Shughuli za Bunge katika kila kikao cha Bunge; “Rais” ni mtu aliyechaguliwa kushika Kiti cha Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, kama ilivyoelekezwa katika Ibara ya 33 yaKatiba; “Shughuli za Serikali” ni shughuli zinazowasilishwa Bungeni naWaziri au na Mwanasheria Mkuu wa Serikali;

Sura ya296,Toleola 2002

4

“Siwa” ni rungu la dhahabu linalotumika kama kielelezo chamamlaka ya Bunge ambalo hubebwa na Mpambe wa Bungeakimtangulia Spika wakati wa kuingia na kutoka kwenye Ukumbiwa Bunge kabla na baada ya kikao cha Bunge; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 84 yaKatiba na kuchaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 9 ya Kanuni hizi; “Taarifa Rasmi” ni taarifa za majadiliano ya Bunge zilizotajwakatika Kanuni hizi; “Tume ya Huduma za Bunge” ni Tume iliyoanzishwa kwa mujibuwa kifungu cha 5 cha Sheria ya Tume ya Huduma za Bunge, Sura ya115, Toleo la 2002; “Waziri” ni Mbunge aliyeteuliwa na Rais kwa mujibu wa Ibara ya55 ya Katiba; “Wimbo wa Taifa” ni Wimbo wa Taifa wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania.

SEHEMU YA PILI

UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA BUNGE

Uongozi wa Bunge

4. Spika atachaguliwa na Wabunge kwa mujibu wa Kanuni ya 9 nakushika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba na Kanuni hizi.

5.-(1) Katika kutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika Ibaraya 84 ya Katiba, Spika ataongozwa na Kanuni hizi na pale ambapoKanuni hazikutoa mwongozo, basi Spika atafanya kazi kwakuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo,maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturiza Mabunge mengine yenye utaratibu wa kibunge unaofanana nautaratibu wa Bunge la Tanzania.

(2) Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, naMbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifuSpika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.

(3) Spika anaweza kumtaka Mbunge yeyote anayekiuka Kanunihizi kujirekebisha mara moja.

(4) Mbunge yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa Spikaanaweza kuwasilisha sababu za kutokuridhika kwake kwa Katibuwa Bunge ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.

Spika

Mamlaka ya Spika

5

(5) Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni za Bungena kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na Kamati hiyo.

(6) Spika au Naibu Spika hatakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuniza Bunge inapokaa kujadili uamuzi unaolalamikiwa, bali wajumbewatachagua Mwenyekiti wa muda kwa asilimia 50 ya kura za siri.

(7) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, wakatiwowote ambapo Spika hayupo Bungeni au kwa sababu nyingineyoyote hawezi kutekeleza madaraka au majukumu ya Spika, basimadaraka au majukumu ya Spika yatatekelezwa na Naibu Spika.

6.-(1) Naibu Spika aliyetajwa katika Ibara ya 85(1) ya Katiba,atachaguliwa kwa mujibu wa Kanuni ya 10 kutoka miongoni mwaWabunge na kushika madaraka yake kwa mujibu wa masharti yaKatiba na Kanuni hizi.

(2) Naibu Spika atakuwa msaidizi wa Spika katika kuliongoza Bungena atatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Kanuni hizi.

(3) Spika anaweza wakati wowote bila kutoa taarifa rasmi kwaBunge kumtaka Naibu Spika au Mwenyekiti kuongoza Shughuli zaBunge.

(4) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, wakatiwowote ambapo Spika na Naibu Spika wote hawapo Bungeni aukwa sababu nyingine yoyote, hawawezi kutekeleza madaraka aumajukumu yao, basi madaraka au majukumu hayo yatatekelezwana Mwenyekiti wa Bunge.

(5) Naibu Spika anaweza wakati wowote, bila kutoa taarifa rasmikwa Bunge, kumtaka Mwenyekiti wa Bunge kuongoza Shughuli zaBunge.

7.-(1) Kutakuwa na Wenyeviti watatu wa Bunge ambaowatachaguliwa na Wabunge kutoka miongoni mwao kwakuzingatia jinsia na pande za Muungano.

(2) Kamati ya Uongozi itapendekeza majina ya Wabunge sitaambayo yatawasilishwa Bungeni ili kupigiwa kura.

(3) Wenyeviti wa Bunge wanaweza kuongoza shughuli za Bungekwa utaratibu na maelekezo ya Spika au Naibu Spika kwa mujibuwa Kanuni hizi.

MajukumuyaWenyeviti wa Bunge

Majukumuya NaibuSpika

6

(4) Endapo Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge wotehawapo, Wabunge watamchagua mmoja wa Wenyeviti waKamati za Kudumu za Bunge kuendesha Shughuli za Bungekufuatana na utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi.

8. Kwa kuzingatia matakwa na masharti yaliyowekwa na kiapocha kazi zake na kwa madhumuni ya utoaji wa maamuzi nauendeshaji wa Shughuli za Bunge kwa haki na bila upendeleo, Spika:-

(a) Ataendesha shughuli za Bunge na kutoamaamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki walaupendeleo wowote, kwa kuongozwa na Katiba,Sheria za nchi, Kanuni hizi, Kanuni nyinginezilizopo, maamuzi ya maspika wa Bungewaliotangulia na pia kwa kuzingatia uzoefupamoja na mila na desturi za mabunge mengineyanayofuata utaratibu wa kibungeunaofanana na unaofuatwa na Bunge la Tanzania;

(b) Hatafungwa na msimamo utakaowekwa aumakubaliano yatakayofikiwa na Kamati yoyoteya Chama cha Siasa kinachowakilishwa Bungeni.

Uchaguzi wa Viongozi wa Bunge

9.-(1) Kutakuwa na Uchaguzi wa Spika utakaofanyika kwa mujibuwa masharti ya Ibara ya 84 (1) ya Katiba pamoja na Kanuni hizi.

(2) Kila Chama cha Siasa kitakuwa na haki ya kupendekeza jinamoja la Mbunge wa Chama hicho ambaye atakuwa mgombea wanafasi ya Spika, kwa mujibu wa Katiba.

(3) Majina ya wagombea wasio Wabunge yatawasilishwa navyama husika kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi siku tano kabla yauchaguzi.

(4) Baada ya kupokea majina hayo, Tume itayachambua na kishaitawasilisha majina ya wagombea wenye sifa kwa Katibu siku mbilikabla ya uchaguzi.

(5) Endapo wamependekezwa wagombea wawili au zaidi,uchaguzi utafanyika kwa kufuata utaratibu ulioainishwa katika fasilizinazofuata za Kanuni hii.

Uadilifu kwa Kiongozi wa Bunge

Uchaguzi wa Spika

7

(6) Mgombea yeyote anaweza kumtaarifu Katibu kwa maandishikwamba anajitoa kugombea, kabla ya shughuli za kupiga kurakuanza Bungeni, na Katibu atalifuta jina la mgombea huyo katikakaratasi za kura.

(7) Mwanzoni mwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza waBunge Jipya, mara baada ya Katibu kusoma Tangazo la Rais naKikao kujigeuza kuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Spika, Katibuatamwomba Mbunge asiye mgombea wa nafasi ya Spika kutokamiongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa Wabunge kwamfululizo kwa muda mrefu, awe Mwenyekiti wa Mkutano huo waUchaguzi.

(8) Kabla ya kikao cha Bunge cha kumchagua Spika kuanza, Katibuataandaa karatasi za kura zitakazoonesha majina ya wagombeawote waliopendekezwa na wakati wa kupiga kura atatoa karatasimoja tu ya kura kwa kila Mbunge.

(9) Mbunge ambaye kabla ya shughuli za uchaguzi kumalizikaatakosea katika kuweka alama kwenye karatasi ya kura ataruhusiwakumrudishia Katibu karatasi hiyo, na papo hapo Katibu ataifuta nakuiharibu kisha kumpa Mbunge huyo karatasi nyingine.

(10) Kila Mbunge atapiga kura ya siri kwa kuweka katika karatasiya kura alama ya “V” katika mraba pembeni mwa jina la Mgombeaanayemtaka awe Spika, na ataitumbukiza karatasi hiyo katikasanduku la kura.

(11) Baada ya Katibu kuridhika kwamba Wabunge wote waliomoBungeni wamepiga kura na kutumbukiza karatasi zao za kurakwenye masanduku ya kura, masanduku yote yatakusanywa nakuwekwa mahali panapoonekana na baada ya hapo masandukuhayo ya kura yatapelekwa kwenye chumba maalumu na kura hizozitahesabiwa chini ya usimamizi wa wawakilishi walioteuliwa nawagombea, mmoja mmoja kwa kila mgombea.

(12) Endapo zoezi hili la uchaguzi litaendeshwa kwa mfumo waelektroniki wa upigaji kura basi upigaji na uhesabuji kura utakuwawa papo kwa papo na matokeo yake yatakuwa halali.

(13) Mgombea atakuwa amechaguliwa kuwa Spika kama atapatazaidi ya nusu ya kura za Wabunge wote na iwapo hakutakuwa namgombea aliyepata zaidi ya nusu ya kura hizo, uchaguzi utarudiwalakini ni wagombea wawili tu waliopata kura nyingi zaidi ndio

8

watakaopigiwa kura, na katika hatua hiyo, mgombea atakayepatakura nyingi zaidi atatangazwa kuwa mshindi.

(14) Endapo wagombea wawili au zaidi watapata kura sawa katikanafasi ya mwanzo, basi wagombea hao tu ndiyo watakaopigiwakura na mgombea atakayepata kura nyingi zaidi atakuwa ndiyemshindi.

(15) Iwapo wagombea wawili au zaidi watapata kura sawa katikanafasi ya pili na yule wa kwanza hajapata zaidi ya nusu ya kurazilizopigwa, basi wagombea hao wawili pamoja na yule wa kwanzandio watakaopigiwa kura na mgombea atakayepata kura nyingizaidi atakuwa ndiye mshindi.

(16) Endapo awamu ya pili ya upigaji kura itashindwa kumpatamshindi, basi Mwenyekiti atapiga kura yake ya uamuzi ili mshindiapatikane.

(17) Endapo kutakuwa na mgombea mmoja tu basi mgombea huyoatapigiwa kura ya “Ndiyo” au “Hapana” na atatangazwa kuwaamechaguliwa kuwa Spika iwapo atapata kura za “Ndiyo” za idadiya zaidi ya nusu ya kura za Wabunge wote.

(18) Mara baada ya mshindi kupatikana, Katibu atamtangaza Spikaaliyechaguliwa na Spika huyo Mteule ataapa viapo vilivyowekwakwa mujibu wa Sheria na Kanuni hizi.

(19) Muda wa Spika Mteule kuapishwa utakapowadia, Mwenyekitiatamwita Spika Mteule ajongee mbele ya Bunge ili aape viapovinavyohusika.

(20) Mtu au Mbunge yeyote aliyechaguliwa kuwa Spika, kabla yakushika madaraka yake, ataapa mbele ya Bunge Kiapo cha Utii naKiapo cha Spika vitakavyokuwa na maneno yafuatayo:

Kiapo cha Utii:

“Mimi, …………..….. naapa kwamba, nitakuwa mwaminifu kwaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wanguwote na kwamba, nitaihifadhi, nitailinda na kuitetea Katiba yaTanzania kwa mujibu wa Sheria iliyowekwa. Ewe Mwenyezi Mungu,nisaidie.”

9

Kiapo cha Spika:

“Mimi, …………., naapa kwamba, nitaitumikia vyema na kwamoyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangukama Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheo hichonitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuni zaBunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano na kwavyovyote vile sitatoa siri za Bunge. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”

(21) Wakati wa kuapa, Spika anayeamini kuwa kuna Mungu,atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifukinachotambuliwa na imani ya dini yake.

(22) Iwapo Spika haamini kuwa kuna Mungu, basi hatashika Bibliaau Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno “EweMwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkono wakewa kuume juu.

10.-(1) Kutakuwa na uchaguzi wa Naibu Spika wa Bunge katikanyakati zilizowekwa na Ibara ya 86(1) ya Katiba na utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi.

(2) Uchaguzi wa Naibu Spika utafanyika katika Mkutano wa Kwanzawa Bunge jipya, au mapema iwezekanavyo baada ya wakati huoau katika kikao cha kwanza cha Bunge mara baada ya nafasi yaNaibu Spika kuwa wazi, au mapema iwezekanavyo baada ya kikaohicho.

(3) Uchaguzi wa Naibu Spika utaendeshwa kwa utaratibu ule uleunaotumika kumchagua Spika, isipokuwa kwamba, Mbunge hawezikushiriki katika uchaguzi wa Naibu Spika iwapo hajaapa Kiapo chaUaminifu.

(4) Mbunge yeyote atakayechaguliwa kuwa Naibu Spika, kabla yakushika madaraka yake, ataapishwa na Spika Kiapo cha NaibuSpika ambacho kitakuwa na maneno yafuatayo:-

“Mimi, …………., naapa kwamba, nitaitumikia vema na kwamoyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangukama Naibu Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheohicho nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuniza Bunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano nakwa vyovyote vile sitatoa siri za Bunge. “Ewe Mwenyezi Mungunisaidie.”

UchaguziwaNaibu Spika

10

(5) Wakati wa kuapa, Naibu Spika anayeamini kuwa kuna Mungu,atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifukinachotambuliwa na imani yake ya dini.

(6) Iwapo Naibu Spika haamini kuwa kuna Mungu, hatashika Bibliaau Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno“EweMwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkono wakewa kuume juu.

11.-(1) Uchaguzi wa Wenyeviti wa Bunge utafanyika kwa kuzingatiajinsia na pande za Muungano na kwa kufuata utaratibu kwamba:-

(a) karatasi ya kura itakuwa na majina ya Wabungesita ambao wamependekezwa na Kamati yaUongozi kupigiwa kura kutoka miongoni mwaWenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati zaKudumu za Bunge;

(b) kila Mbunge atapiga kura kwa kuchagua majinamatatu katika orodha hiyo; na

(c) wagombea watatu watakaopata kura nyingizaidi kuliko wenzao ndio watakuwawamechaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge.

(2) Wenyeviti wa Bunge waliochaguliwa kwa mujibu wa mashartiya fasili ya (1) ya Kanuni hii watashika madaraka yao kwa mudaambao wataendelea kuwa Wenyeviti au Makamu Wenyeviti waKamati zao za Kudumu za Bunge mpaka mwisho wa Mkutanounaofuata mara baada ya Mkutano wa Kumi wa Bunge (ambaondio hukamilisha nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge) utakaofanyikabaada ya kuchaguliwa kwao, lakini wanaweza kuchaguliwa tenakuwa Wenyeviti wa Bunge katika kipindi cha pili kilichobaki chamaisha ya Bunge la kipindi kinachohusika iwapo watachaguliwatena kuwa Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge.

12. Uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katika vyombo vingineambavyo kwa mujibu wa Sheria zilizounda vyombo hivyovinatakiwa viwe na wawakilishi wa Bunge na uchaguzi wakuwachagua Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki utafanywakwa kuzingatia, kwa kadri iwezekanavyo, uwiano wa idadi yaWabunge wa Vyama mbalimbali vya Siasa vinavyowakilishwaBungeni, uwakilishi wa jinsia na uwakilishi wa pande zote mbili zaMuungano.

UchaguziwaWabungewanao-kwendakwenyevyombovinginevyauwakilishi

UchaguziwaWenyeviti wa Bunge

11

13. Endapo Waziri Mkuu ambaye ndiye Kiongozi wa Shughuli zaSerikali Bungeni hatakuwepo Bungeni kwa kipindi kinachozidi sikumoja, basi atamteua Waziri mwingine kuwa Kiongozi wa muda waShughuli za Serikali Bungeni.

14.-(1) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atachaguliwachini ya utaratibu ulioainishwa kwenye fasil i za Kanuni hiizinazofuata.

(2) Wabunge wote wa Upinzani wanaweza kuunda Kambi Rasmiya Upinzani iwapo idadi yao itakuwa si chini ya asilimia kumi nambili na nusu ya Wabunge wote.

(3) Chama cha Upinzani hakitakuwa na haki ya kuchaguaKiongozi wa Upinzani Bungeni, isipokuwa tu kama kina idadi yaWabunge wasiopungua asilimia kumi na mbili na nusu ya Wabungewote.

(4) Endapo kutakuwa na Vyama vya Upinzani zaidi ya kimojaambavyo kila kimoja kina Wabunge asilimia kumi na mbili na nusuau zaidi, basi Chama chenye idadi kubwa zaidi ya Wabunge kulikovingine ndicho kitakuwa na haki ya kuchagua Kiongozi wa KambiRasmi ya Upinzani Bungeni, lakini, ikiwa kutakuwa na vyama viwiliau zaidi vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidi ya asilimiakumi na mbili na nusu, Wabunge wa vyama vinavyohusikawatachagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni chini ya utaratibuwatakaokubaliana wenyewe.

15.-(1) Chama chenye haki ya kumchagua Kiongozi wa Kambi Rasmiya Upinzani Bungeni kinaweza pia kuchagua Naibu Kiongozi waKambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

(2) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni atateuaWabunge wa Chama chake au Wabunge wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni ambao watakuwa wasemaji wakuu wa Kambi yaUpinzani kwa Wizara zilizopo za Serikali.

16.-(1) Chama kinachounda Serikali na Chama chenye haki yakuchagua Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, vitateuaWanadhimu wa vyama hivyo Bungeni ambao watajulikana kwajina la Mnadhimu wa Serikali na Mnadhimu wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni. (2) Vyama hivyo vitateua pia Wanadhimu Wasaidizi ambao idadiyao itaamuliwa na vyama vyenyewe.

UteuziwaWana-dhimuwa vyama Bungeni

KambiRasmiyaUpinzaniBungeni

KiongoziwaKambiRasmiyaUpinzaniBungeni

Kiongoziwa mudawaShughulizaSerikaliBungeni

12

(3) Mnadhimu wa Serikali atakuwa kiungo cha mawasiliano kati yaKiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni na Wabunge wa Chamakinachounda Serikali na Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzaniatakuwa ni kiungo cha mawasiliano kati ya Kiongozi wa KambiRasmi ya Upinzani Bungeni na Wabunge wa Upinzani.

(4) Vyama vya Siasa vyenye uwakilishi Bungeni vinaweza kutungaKanuni za vyama kwa ajili ya uendeshaji bora wa shughuli za vyamahivyo Bungeni.

17.-(1) Katibu wa Bunge kama alivyotajwa kwenye Ibara ya 87(1)ya Katiba, atawajibika kuhakikisha utekelezaji bora wa Shughuli zaBunge na kwa madhumuni hayo:-

(a) atahudhuria au atawakilishwa katika vikao vyotevya Bunge na vya Kamati ya Bunge Zima na vikaovya Kamati nyingine yoyote ya Bunge;

(b) atawajibika kuweka kumbukumbu zinazotakiwaziwekwe kwa mujibu wa Kanuni hizi;

(c) atatayarisha Taarifa Rasmi za majadiliano yaBunge kwa mujibu wa Kanuni hizi;

(d) atatayarisha siku hadi siku, Kitabu chaShughuli za Bunge na kukihifadhi Ofisini kwake,kikiwa kinaonesha:

(i) maagizo yote yaliyotolewa na Bunge;

(ii) shughuli zote zilizopangwa kufanywasiku yoyote ya baadaye;

(iii) taarifa zote za maswali na hojazilizokubaliwa na Spika.

(2) Katibu atawajibika kutunza Kitabu cha Maamuzi ya Spika, Kitabucha Shughuli, Taarifa Rasmi, Miswada ya Sheria na Hati nyinginezilizowasilishwa Bungeni, na Mbunge au mtu yeyote anawezakukagua kumbukumbu hizo wakati wowote unaofaa kwa kufuatautaratibu utakaowekwa na Spika.

(3) Katibu ataweka kumbukumbu za maamuzi ya mara kwa maraya Spika kuhusu masuala ya utaratibu Bungeni.

MajukumuyaKatibuwaBunge

13

(4) Katibu atawajibika kuhakikisha kuwa, Ukumbi wa Mikutano yaBunge na mazingira yake, huduma kwa Wabunge na vifaa vinginevinavyohusika na Shughuli za Bunge, viko katika hali inayofaakuliwezesha Bunge kutekeleza wajibu wake ipasavyo.

18.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi kuhusuuwekaji wa nafasi na ngazi za utumishi katika Ofisi ya Bunge, Ofisihiyo itakuwa na Idara, Sehemu na Vitengo mbalimbali kwa namnana idadi ambayo itaiwezesha kutoa huduma bora na kamilifu kwaBunge, Wabunge na Kamati za Bunge.

(2) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, kutakuwana Makatibu Wasaidizi wa Bunge, kwa idadi na ngazi mbalimbalikadri itakavyoamuliwa na Tume ya Huduma za Bunge iliyoundwakwa mujibu wa Sheria ya Uendeshaji wa Bunge.

(3) Kutakuwepo na watumishi wengine wa Bunge ambao nyadhifa,kazi na idadi yao vitaamuliwa na Tume ya Huduma za Bunge.

19. Kutakuwa na Mpambe wa Bunge ambaye atatekeleza shughulimbalimbali za Bunge kwa kufuata maagizo atakayopewa na Spika,Naibu Spika, Mwenyekiti au Katibu, kwa kadri itakavyokuwa.

20.- (1) Pamoja na kutekeleza shughuli mbalimbali kwa mujibu wamasharti ya Kanuni ya 19, Mpambe wa Bunge:-

(a) atasimamia masuala yote ya ulinzi na usalama waofisi, mali, vifaa na majengo yote ya Bunge;

(b) atahakikisha utulivu na amani katika sehemuwanayokaa wageni na atawawekea utaratibumaalum wa kuingia na kutoka Bungeni; na

(c) atamtangulia Spika, akiwa amebeba Siwa, wakatiSpika anapoingia na anapotoka kwenye Ukumbiwa Mikutano ya Bunge.

(2) Kwa madhumuni ya utekelezaji bora wa majukumu yake wakatiwa vikao vya Bunge, Mpambe wa Bunge anaweza kutoa maagizoanayoona yanastahili kutolewa kwa wahudumu wa Bunge, nawahudumu hao watawajibika kutekeleza maagizo hayo.

(3) Mpambe wa Bunge atawajibika kuratibu na kushauri juu yausalama wa Ukumbi, majengo na vyumba vyote vya Bunge na pia

OfisiyaBunge

MpambewaBunge

MajukumuyaMpambewaBunge

14

sehemu zote za majengo yote yanayotumiwa na Bunge au Kamatiza Bunge au Wabunge au watumishi wa Bunge.

(4) Mpambe wa Bunge atakuwa na uwezo wa kutoa maagizo kwaaskari mwingine yeyote aliyekabidhiwa kutekeleza majukumukwenye Ukumbi wa Bunge na mazingira yake au kwenye majengo,vyumba au sehemu nyingine zinazotumiwa kwa ajili ya kutekelezashughuli za Bunge kwa mujibu wa Kanuni hizi.

21.-(1) Kutakuwa na Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheriaambaye atakuwa Msaidizi Mkuu wa Katibu wa Bunge kwa masualayote yanayohusu Sheria. Pamoja na kazi nyingine, Mshauri wa Bungewa Mambo ya Sheria atashughulikia mambo yafuatayo:-

(a) kutoa ushauri wa kisheria kuhusu Miswadayote ya Sheria inayowasilishwa Bungeni;

(b) kuchambua Miswada ya Sheria inayowasilishwaBungeni na kuwasaidia Wabunge kupatauelewa sahihi wa Miswada hiyo;

(c) kutoa ushauri kwa Bunge kupitia Kamati yaKanuni za Bunge kuhusu marekebisho yoyoteyanayohitajika kufanyika katika Kanuni zaKudumu za Bunge;

(d) kutoa huduma za ushauri wa kisheria kwa Kamatiza Bunge na Wabunge kila atakapohitajikakufanya hivyo;

(e) kuandaa Miswada ya Sheria ya Kamati, MiswadaBinafsi ya Sheria na Hoja Binafsi za Wabunge;

(f) kusaidia Wabunge kutayarisha marekebisho yaMuswada wa Sheria unaowasilishwa Bungeni;

(g) kuwa ndiye mwakilishi rasmi wa Bunge katikamasula yote ya kisheria na kwa madhumunihayo, anaweza kushirikiana na wanasheriawengine kuliwakilisha Bunge au Tume ya Hudumaza Bunge endapo Bunge au Tume ya Huduma za

Bunge itashtaki au itashtakiwa;

(h) kuhakikisha kuwa Muswada wowote wa Sheriauliopitishwa na Bunge unachapishwa kama

MshauriMkuuwaBungewaMamboyaSherianamajukumuyake

15

ulivyopitishwa na Bunge na kuwasilishwa kwaRais kwa ajili ya kupata kibali cha Rais na nakalamoja kupelekwa kwa Spika; na

(i) kushughulikia masuala yote ya Sheriayatakayopelekwa kwake na uongozi wa Bunge.

(2) Masuala ya Sheria yanayotoka kwa Mbunge mmoja mmoja auKamati yoyote ya Bunge yatapelekwa kwa Katibu wa Bungeambaye atayakabidhi kwa Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo yaSheria ili kuyafanyia kazi katika kipindi atakachoelekezwa.

(3) Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria atateuliwa naTume ya Huduma za Bunge kutoka miongoni mwa wanasheriawaandamizi.

SEHEMU YA TATU

MIKUTANO NA VIKAO VYA BUNGE

22.-(1) Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya utafanyika mahali,tarehe na saa ambayo Rais atatamka wakati akiitisha Mkutano waBunge Jipya.

(2) Bila ya kuathiri Masharti ya Kanuni hizi kuhusu kuanza na kufungwakwa vikao vya Bunge, Mkutano wa Kwanza wa Bunge utaendeleakwa muda wowote ambao utahitajika kwa ajili ya kutekeleza nakukamilisha shughuli zote za Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya.

23.-(1) Shughuli za Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya zitakuwakama ifuatavyo:-

(a) Kusomwa Tangazo la Rais la kuitisha Bunge;(b) Uchaguzi wa Spika;(c) Kiapo cha Spika;(d) Wimbo wa Taifa na Dua;(e) Kiapo cha Uaminifu kwa Wabunge wote;(f) Hoja ya kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu;

(g) Uchaguzi wa Naibu Spika; (h) Ufunguzi rasmi wa Bunge Jipya utakaofanywa na Rais; (i) Hoja ya kujadili Hotuba ya Rais; na (j) Shughuli yoyote ambayo Bunge litaona inafaa

kushughulikiwa kwa wakati huo.

MkutanowakwanzawaBunge

ShughulizaMkutanowaKwanzawaBunge

16

(2) Mwanzoni mwa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kwanza waBunge Jipya, Katibu atasoma Tangazo la Rais la kuitisha Bunge Jipya.

(3) Mara baada ya Tangazo la Rais kusomwa, Kikao kitajigeuzakuwa Mkutano wa Uchaguzi wa Spika.

(4) Katibu atamwomba Mbunge asiye mgombea wa nafasi hiyo yaSpika kutoka miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwaWabunge kwa mfululizo kwa muda mrefu awe Mwenyekiti waMkutano huo wa Uchaguzi.

(5) Katibu wa Bunge atagawa karatasi za kura kwa Wabunge, nauchaguzi wa Spika utafanywa kwa kuzingatia utaratibu na Kanunihizi.

(6) Baada ya Uchaguzi wa Spika kumalizika na mshindi kutangazwa,Mwenyekiti atasitisha Mkutano wa Uchaguzi wa Spika na kutajamuda ambao Spika Mteule ataapishwa.

(7) Baada ya Spika Mteule kuapishwa atakalia kiti chake na kutoahotuba fupi ya shukrani kwa Bunge na kisha ataliahirisha Bungehadi wakati mwingine atakaoutaja ambapo shughuli za kuapishaWabunge wote Kiapo cha Utii zitaanza.

24.-(1) Kila Mbunge ataapa Kiapo cha Utii kitakachokuwa namaneno yafuatayo:

“Mimi,…………….., naapa kwamba, nitakuwa mwaminifu kwaJamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuitumikia kwa moyo wanguwote na kwamba, nitaihifadhi, nitailinda na kuitetea Katiba yaJamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Sheriailiyowekwa. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”

(2) Wakati wa kuapa, Mbunge anayeamini kuwa kuna Mungu,atalazimika kushika Biblia au Kuran au kitabu kingine kitakatifukinachotambuliwa na imani ya dini yake.

(3) Iwapo Mbunge yeyote haamini kuwa kuna Mungu, hatashikaBiblia au Kuran au kitabu chochote kitakatifu au kutamka maneno,“Ewe Mwenyezi Mungu nisaidie,” bali atalazimika kuinua mkonowake wa kuume juu.

25.-(1) Baada ya shughuli ya kuwaapisha Wabunge kukamilika,Spika atasoma Taarifa ya Rais inayotaja j ina la Mbunge

Kiapo cha utii kwa Wabunge

Kuthibi-tishaUteuziwaWaziri Mkuu

17

anayempendekeza kuwa Waziri Mkuu ili aweze kuthibitishwa naBunge.

(2) Baada ya Spika kutaja jina la Mbunge anayependekezwa,Mwanasheria Mkuu wa Serikali atatoa hoja ya kuliomba Bungelithibitishe uteuzi wa Mbunge husika kuwa Waziri Mkuu.

(3) Baada ya kuthibitisha uteuzi wa Waziri Mkuu, Bungelitamchagua Naibu Spika.

(4) Iwapo Bunge litakataa kumthibitisha Waziri Mkuu, Spikaatamjulisha Rais kuhusu uamuzi huo wa Bunge.

26.-(1) Baada ya uchaguzi wa Naibu Spika, Spika atalitangaziaBunge mahali, siku na muda ambao Rais atalihutubia na kulifunguarasmi Bunge Jipya na baada ya Tangazo hilo, Spika anaweza:-

(a) kuahirisha Shughuli za Bunge hadi wakati huo; au(b) kuahirisha Kikao cha Bunge hadi siku na muda

atakaoutaja.

(2) Rais atakapowasili katika viwanja vya Bunge, atapokelewa naSpika akifuatana na Waziri Mkuu na kisha atakaribishwa ili alihutubiena kisha kulifungua Rasmi Bunge Jipya.

(3) Baada ya hotuba ya Rais, Waziri Mkuu atatoa hoja ya kuahirishaBunge hadi mahali, siku na muda atakaoutaja.

27.-(1) Isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo, kila Mkutano waBunge utafanyika katika ukumbi wa Bunge Dodoma.

(2) Wimbo wa Taifa utapigwa na kuimbwa katika kila kikao chakwanza na cha mwisho kwa Mikutano yote ya Bunge kufuatana nautaratibu utakaowekwa na Bunge.

(3) Bila ya kuathiri masharti yanayofuata ya Kanuni hii, kila Mkutanoisipokuwa Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, utaanza tareheitakayowekwa na Bunge.

(4) Endapo manufaa ya Taifa yatahitaji kuwa Bunge lisikutanetarehe ile iliyowekwa kwa Mkutano utakaofuata, bali likutanetarehe ya mbele zaidi au ya nyuma zaidi, basi Spika anaweza, baadaya kushauriana na Kamati ya Uongozi, kuliita Bunge likutane tarehehiyo ya mbele zaidi au nyuma zaidi.

Ufunguzi RasmiwaBungeJipya

MikutanoyakawaidayaBunge

18

(5) Iwapo Bunge litatakiwa kukutana tarehe ya mbele zaidi kulikotarehe iliyotangazwa awali, basi tarehe hiyo mpya haitakuwambele zaidi ya siku kumi na nne kutoka tarehe iliyotangazwa hapoawali.

28.-(1) Vikao vya Mikutano ya Bunge, isipokuwa Kikao cha Kwanzacha Mkutano wa Kwanza wa Bunge Jipya, vitaanza saa 3.00 asubuhi,ila tu, kama Bunge litaamua vinginevyo.

(2) Bunge litakutana hadi saa 7.00 mchana ambapo Spikaataahirisha shughuli yoyote itakayokuwa inafanyika hadi saa 11.00jioni, isipokuwa kama Spika akiona inafaa, Bunge linawezakuendelea kukutana kwa muda usiozidi dakika 30 au kusitishwawakati wowote kabla ya saa 7.00 mchana baada ya kuwahojiWabunge.

(3) Hoja ya kubadilisha nyakati za vikao itatolewa na Waziri naitaamuliwa kama hoja nyingine yoyote na haitahitaji kutolewataarifa.

(4) Bunge litaendelea kukaa hadi saa 1.45 usiku wakati ambapoSpika atasitisha shughuli na kuliahirisha hadi kesho yake au sikunyingine atakayoitaja.

(5) Iwapo shughuli zilizopangwa kwa siku hiyo zimemalizika kablaya saa 1.45, Spika ataliahirisha Bunge bila kuhoji, lakini iwapozimesalia dakika kumi kabla ya kufikia muda wa kuahirisha kikao, naBunge au Kamati ya Bunge Zima au Kamati ya Matumizi badohaijamaliza shughuli zake, Spika anaweza kuongeza muda usiozididakika thelathini, bila kulihoji Bunge au Kamati ya Bunge Zima auKamati ya Matumizi ili kukamilisha shughuli zilizobaki.

(6) Iwapo wakati wa kusitisha shughuli umefika na Spika atakuwaanalihoji au yupo karibu kulihoji Bunge, basi hatasitisha shughulimpaka hoja iwe imeamuliwa.

(7) Baada ya hoja kuamuliwa, Waziri atatoa hoja ya kuahirisha Kikaocha Bunge hadi kesho yake au siku nyingine itakayotajwa.

(8) Endapo Spika atakuwa amepokea taarifa ya Mbunge yeyoteanayetaka kutoa maelezo binafsi, basi Spika hataliahirisha Bungebali ataongeza muda usiozidi dakika thelathini bila ya kulihojiBunge ili kutoa nafasi kwa Mbunge huyo aweze kutoa maelezoyake, isipokuwa kwamba, maelezo hayo sharti yawe

Mudawa VikaovyaBunge

19

yameandikwa na kuwasilishwa kwa Spika angalau siku mojakabla hayajatolewa na Mbunge anayehusika atalazimikakuyasoma kama yalivyowasilishwa.

(9) Baada ya kusitisha Shughuli za Bunge, hakuna shughuli nyingineyoyote itakayofanywa katika kikao hicho na Spika ataliahirishaBunge hadi kesho yake au siku nyingine itakayotajwa.

(10) Endapo majadiliano yoyote katika Bunge au katika Kamati yaBunge Zima yatasitishwa na Spika kwa mujibu wa masharti ya Kanunihii, wakati yatakaporudiwa katika Bunge au katika Kamati,yataendelezwa kuanzia hapo yalipositishwa na Mbunge yeyoteambaye hotuba yake ilikatizwa na Spika atakuwa na haki yakuendelea na maelezo yake katika marudio ya mjadala huo naendapo Mbunge hakuitumia haki yake hiyo, basi atahesabiwa kuwaalikuwa amemaliza hotuba yake.

(11) Bila ya kuathiri masharti ya Kanuni hii, wakati Spika anapotakakuliahirisha Bunge, wakati huo unaweza kutumiwa kama fursa kwaMbunge yeyote kutaka ufafanuzi utolewe na Waziri juu ya jambololote lililo chini ya madaraka ya Waziri huyo au kuanzisha mjadalajuu ya jambo lolote la dharura kwa idhini ya Spika, isipokuwa kwajambo ambalo haliwezi kujadiliwa bila hoja maalumu kutolewakwanza kwa ajili hiyo.

(12) Jambo lolote haliwezi kuwasilishwa na kujadiliwa kwa mujibuwa Kanuni hii, isipokuwa tu kama Mbunge amewasilisha kwa SpikaTaarifa ya maandishi siyo chini ya saa ishirini na nne kabla yakutolewa kwa jambo hilo Bungeni akieleza kwa ufupi msingi wajambo analotaka kuzungumzia.

(13) Jumla ya dakika zisizozidi thelathini zitatumika kwa mtoa hojakuwasilisha Bungeni hoja yake pamoja na majadiliano na maamuziya Bunge kwa hoja husika.

(14) Iwapo dakika thelathini zitapita tangu Spika alipotakakuliahirisha Bunge chini ya fasili ya (7) na (10) ya Kanuni hii, basiSpika atasitisha majadiliano yanayoendelea.

(15) Iwapo shughuli zote zi l izopangwa kwa aji l i ya kikaohazijamalizika, Spika atalihoji Bunge kuhusu hoja ya kuahirisha kikaocha Bunge na baada ya hoja hiyo kuafikiwa, atakiahirisha kikaohicho hadi kikao kinachofuata ambacho, kama Bunge halikuamua

20

vinginevyo, kitakuwa ni siku itakayofuata, isipokuwa tu kamaitakuwa ni siku ya Jumamosi, Jumapili au siku ya mapumziko.

(16) Pale inapotokea dharura yoyote ndani ya Ukumbi wa Bunge,Spika anaweza kusitisha Shughuli za Bunge bila kulihoji Bunge.

29.-(1) Kila Mkutano wa Bunge utafungwa kwa kuliahirisha Bungehadi Mkutano utakaofuata.

(2) Endapo shughuli zote zilizowekwa kwenye Orodha ya Shughulikwa ajili ya Mkutano huo zimemalizika, hoja ya kuahirisha Bungeitakayotolewa na Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni itatajasiku, mahali na saa ambapo Mkutano unaofuata utaanza.

(3) Mara tu baada ya Bunge kupitisha hoja ya kuahirisha Mkutanowa Bunge, Wimbo wa Taifa utapigwa na kuimbwa kwa mujibu wautaratibu uliowekwa na Bunge.

SEHEMU YA NNE

SHUGHULI ZA BUNGE

30.-(1) Rais anaweza kulihutubia Bunge siku yoyote ambayo Bungelinakutana na wakati mwingine wowote kwa mujibu wa Ibara ya 91ya Katiba.

(2) Wakati wa kuanza Kikao cha Kwanza cha Mkutano wowote waBunge baada ya Wimbo wa Taifa kupigwa na kuimbwa na Duakusomwa au kwa vikao vinavyofuata, Dua pekee kusomwa na Spikakukalia kiti chake:-

(a) kama Spika amepata taarifa kuwa Raisanakusudia kulihutubia Bunge siku hiyo, Spikaatalitangazia Bunge ni wakati gani Rais atafanyahivyo;

(b) wakati uliopangwa kwa ajili ya Rais kulihutubiaBunge utakapofika, Spika atampokea Rais nakumkaribisha alihutubie Bunge; na

(c) baada ya hotuba ya Rais, Spika anaweza amakusitisha kikao kwa muda ili amsindikize Rais aukuliahirisha Bunge hadi siku nyingine itakayotajwa.

KuahirishaBunge

MpangiliowaShughulizaBunge

21

(3) Baada ya kushauriana na Kamati ya Uongozi, Spika atatengamuda kwa ajili ya kujadili hotuba ya Rais.

(4) Shughuli za Bunge zitaendeshwa kwa mpangilio ufuatao:-

(a) kuwaapisha Wabunge wapya Kiapocha Uaminifu;

(b) taarifa ya Rais;(c) taarifa ya Spika;(d) kuwasilisha Maombi;(e) hati za kuwasilisha Bungeni;(f) maswali kwa Waziri Mkuu;

(g) maswali ambayo taarifa zake zimetolewa;(h) hoja za kuahirisha shughuli ili kujadili mambo

muhimu ya dharura;(i) kauli za Mawaziri;(j) maelezo binafsi ya Mbunge;(k) mambo yahusuyo haki za Bunge, ikiwa ni pamoja

na kuzifanyia mabadiliko Kanuni za Bunge;(l) shughuli za Serikali;(m) hoja au taarifa za Kamati;(n) hoja binafsi za Wabunge; na(o) shughuli yoyote ambayo Bunge litaona

inafaa kushughulikiwa kwa wakati huo.

(5) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii na baada yakushauriana na Kamati ya Uongozi, katika kila Mkutano wa BungeSpika atatenga muda mahususi kwa ajili ya Bunge kushughulikiaHoja Binafsi na Miswada ya Kamati na Miswada Binafsi ya Wabungekama itakuwepo.

(6) Shughuli za Bunge katika kila kikao zitatekelezwa kwa kufuataOrodha ya Shughuli za siku hiyo au kwa kufuata utaratibu mwingineambao Spika ataagiza ufuatwe kwa ajili ya uendeshaji bora washughuli za Bunge.

31. Dua ya kuiombea nchi yetu na kuliombea Bunge itasomwa naSpika, itakuwa na maneno yafuatayo:-

“Ewe MWENYEZI MUNGU Mtukufu, Muumba Mbingu na Dunia,Umeweka katika Dunia Serikali za Wanadamu na Mabunge yaMataifa ili haki yako itendeke. Twakuomba, uibariki nchi yetuidumishe uhuru, umoja, haki na amani, Umjalie Rais wetu hekima,afya njema na maisha marefu ili pamoja na wanaomshauri,

Dua yakuio-mbeanchiyetunakulio-mbeaBunge

22

wadumishe utawala bora. Utuongezee hekima na busara, sisiWabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nautupe uwezo wa kujadili kwa dhati, mambo yatakayoletwa mbeleyetu leo, ili tufanye maamuzi sahihi yenye manufaa kwa watu wotena ustawi wa nchi yetu. Amina.”

32.-(1) Taarifa ya Rais, kama ipo, itasomwa na Spika.

(2) Kila inapowezekana, taarifa ya Rais itasomwa Bungeni kwakufuata mpangilio wa Shughuli za Bunge, lakini Spika anaweza,wakati wowote, kusitisha shughuli za Bunge kwa madhumuni yakuwezesha taarifa hiyo isomwe.

33.-(1) Spika atatoa taarifa Bungeni kuhusu Miswada yoteiliyopitishwa na Bunge katika Mkutano wake uliotangulia, yaanikama imekubaliwa na Rais au kama Rais ametoa uamuzi mwingine.

(2) Wakati wa kikao, Spika anaweza kutoa taarifa nyinginezo kadriatakavyoona inafaa.

34.-(1) Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha Bungeni maombikuhusu jambo lolote kwa niaba ya watu wanaotoa ombi hilo, naombi hilo halitawasilishwa Bungeni mpaka kwanza taarifa ya ombihilo iwe imetolewa kwa maandishi na kupokelewa na Katibu si chiniya siku mbili za kazi kabla ya Mkutano ambapo ombi hilolinakusudiwa kuwasilishwa.

(2) Ombi lolote linaweza kuwasilishwa Bungeni na Mbunge,likionesha jina la Mbunge anayeliwasilisha.

(3) Mbunge anayewasilisha ombi atatoa maelezo mafupi yakutambulisha watu wanaotoa ombi hilo, idadi yao, sainizilizoambatanishwa kwenye ombi hilo, madai ya msingi yaliyomo,na madhumuni ya ombi hilo.

(4) Baada ya kutimiza masharti ya fasili ya (3) ya Kanuni hii, Mbungeanayewasilisha ombi anaweza kutoa hoja kwamba, Bunge lijadiliombi hilo, isipokuwa kwamba hoja hiyo haitahitaji kutolewa taarifana inaweza kuamuliwa bila mjadala wowote.

(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kuwasilisha ombi linalomhusu yeyemwenyewe au ambalo yeye amelitia saini yake au ambalo linakiukamasharti yanayohusiana na utaratibu wa kutunga Sheria kuhusumambo ya fedha.

TaarifayaRais

TaarifayaSpika

Kuwasilishamaombinataarifaya ombi

23

35. Ombi lolote halitawasilishwa Bungeni isipokuwa tu kama Spikaataridhika kuwa limezingatia masharti yafuatayo:-

(a) limeandikwa katika lugha ya Kiswahili auKiingereza; na

(b) limeandikwa kwa lugha fasaha, ya heshima nalinahitimishwa kwa maelezo ya jumla kuhusumadhumuni ya ombi hilo.

36. Nakala ya kila ombi itawasilishwa kwa Katibu si chini ya sikuzisizopungua mbili za kazi kabla ya siku ya kuwasilishwa Bungeni.

37.-(1) Hati inaweza kuwasilishwa Bungeni wakati wa vikao vyaBunge na:-

(a) Waziri; au (b) Mwanasheria Mkuu wa Serikali; au(c) Kamati yoyote ya Bunge; au(d) Mbunge yeyote.

(2) Nakala za matoleo yote ya Gazeti pamoja na Nyongeza zakezilizochapishwa tangu kikao cha mwisho cha Mkutano wa Bungeuliopita, zitawasilishwa Bungeni na Waziri na kugawiwa kwaWabunge.

(3) Hati zote zitawasilishwa Bungeni bila kutolewa hoja yoyotekwa ajili hiyo.

(4) Baada ya hati kuwasilishwa Bungeni, Waziri, Mwanasheria Mkuuwa Serikali au Mbunge, anaweza kutoa hoja kwamba Bunge lijadilihati hiyo.

(5) Hoja inayotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii haitahitaji kutolewataarifa na itaamuliwa bila ya mabadiliko au mjadala wowote.

(6) Hoja ya kujadili hati iliyowasilishwa Bungeni ikikubaliwa,itashughulikiwa kwa kufuata Mpangilio wa Shughuli za Bunge.

(7) Taarifa zinazowasilishwa Bungeni na Kamati yoyote ya Kudumu,Kamati Teule, Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu zaSerikali pamoja na Mapendekezo ya Matumizi ya Nyongeza yaFedha zitatengewa muda wa kujadiliwa Bungeni bila hoja kutolewa.

(8) Taarifa ambazo Sheria inaelekeza ziwasilishwe Bungenizitajadiliwa na Kamati husika za Kudumu za Bunge.

MashartikuhusuMaombi

NakalayaMaombi

Hatizakuwasili-shaBungeni

24

(9) Mjadala unaweza kuzingatia kila jambo lililomo katika hati,isipokuwa kama Spika, kwa kuzingatia uendeshaji bora wa shughuliza Bunge, ataamua vinginevyo.

38.- (1) Waziri Mkuu anaweza kuulizwa maswali na Mbunge yeyoteambayo yatazingatia masharti kuhusu maswali ya Bunge pamojana Mwongozo uliowekwa na Nyongeza ya Sita ya Kanuni hizi.

(2) Maswali atakayoulizwa Waziri Mkuu hayatakuwa na taarifa yaawali kama maswali mengine.

(3) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kitakuwa kila siku yaAlhamisi na hakitazidi dakika thelathini.

(4) Waziri Mkuu anaweza kutumia Kipindi cha Maswali kwa WaziriMkuu kutoa taarifa au ufafanuzi kuhusu suala lolote linalohusianana shughuli za Serikali na lenye maslahi kwa umma kwa muda usiozididakika kumi, ikifuatiwa na maswali ya Wabunge kwa dakika ishirinikuhusu taarifa yake au masuala mengine yoyote ya Serikali.

(5) Iwapo siku hiyo, kwa sababu maalum, Waziri Mkuu hatakuwepoBungeni hakutakuwa na maswali kwa Waziri Mkuu.

(6) Maswali kwa Waziri Mkuu yatafuatiwa na maswali mengine kwaMawaziri kwa dakika sitini kama yatakavyokuwa yamepangwakwenye Orodha ya Shughuli ya siku hiyo.

39.-(1) Waziri anaweza kuulizwa maswali kuhusu masuala yoyoteya umma au jambo lingine lolote ambalo linasimamiwa na Ofisiyake, na vilevile Mbunge yeyote anaweza kuulizwa maswali kuhusumambo yoyote anayohusika nayo kutokana na kuteuliwa na Bungekushughulikia mambo hayo.

(2) Maswali yanayoulizwa kwa mujibu wa Kanuni hii yatakuwamafupi kwa kadri inavyowezekana na kila swali litahusu jambo mojatu mahususi.

(3) Madhumuni halali ya swali lolote yatakuwa kutekeleza Ibara ya63(2) na (3)(a) ya Katiba.

(4) Taarifa ya swali itatolewa kwa maandishi na itapelekwa na

Maswal ikwaWaziriMkuu

Maswalinat a a r i f ayaMaswali

25

kumfikia Katibu si chini ya siku ishirini na moja kabla ya tareheambayo jibu linahitajiwa kutolewa.

(5) Taarifa haitatolewa Bungeni kwa mdomo, isipokuwa kwamba,taarifa zote za maswali zitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli zaBunge kuonesha kuwa zimepokelewa na maswali yoteyaliyopangwa kujibiwa yatawekwa kwenye Orodha ya Shughuli zasiku inayohusika.

(6) Waziri aliyeulizwa swali atatoa jibu lake papohapo wakati wakipindi cha Maswali.

(7) Endapo swali halikuwahi kujibiwa siku hiyo kwa sababu ya mudawa maswali kumalizika, litapangiwa nafasi ya kujibiwa baadayekatika Mkutano huo unaoendelea. Kama siku inayohusika ndiyosiku ambapo Mkutano wa Bunge unafungwa, swali hilo litajibiwakatika Mkutano unaofuata.

(8) Bunge linapovunjwa, maswali yote ambayo hayakuwahikujibiwa yatajibiwa kwa maandishi.

(9) Kwa madhumuni ya fasili ya (1), endapo swali lililoulizwalimeelekezwa kwa Mbunge, basi kwa idhini ya Spika, Mbungeambaye swali limeelekezwa kwake atapewa fursa ya kujibu swalihilo.

(10) Maswali yatajibiwa Bungeni kwa mdomo. Lakini endapoMbunge mwenye swali hayupo Bungeni kuuliza swali lake, na Spikahakutoa ruhusa kwa swali hilo kuulizwa na Mbunge mwingine, basiWaziri aliyeulizwa swali atapeleka kwa Katibu jibu la maandishinaye Katibu ataliingiza jibu hilo kwenye Taarifa Rasmi.

(11) Katika hali ya kawaida, Mbunge haruhusiwi kuuliza zaidi yamaswali manne yanayohitaji majibu ya mdomo katika Mkutanommoja wa Bunge.

(12) Endapo kwa maoni ya Spika, swali lililoulizwa na Mbunge siyola sera na majibu yake ni marefu au linahitaji takwimu, basi swalihilo litajibiwa kwa maandishi na litaorodheshwa kwenye Orodhaya Shughuli na kuonyesha kwamba limejibiwa kwa maandishi naWabunge wote watagawiwa nakala.

26

(13) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (11) ya Kanuni hii, swalialiloulizwa Waziri mmoja laweza kujibiwa na Waziri mwingine auMwanasheria Mkuu wa Serikali.

(14) Maswali yote katika Mkutano mmoja yatapewa nambazinazofuatana kwa mfululizo na namba zilizotolewa kwa kila swalizitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli za Bunge.

(15) Maswali yote ambayo yamepangwa kujibiwa katika Kikaokimoja, yanaweza kuwekwa pamoja kwenye Orodha ya Shughulina kujibiwa kwa zamu kadri itakavyooneshwa kwenye Orodha yaShughuli.

40. Swali lolote la Bunge halitaruhusiwa kuulizwa Bungeni kama:-

(a) linakiuka Kanuni yoyote ya Bunge;

(b) linashutumu tabia au mwenendo wa mtuyeyote ambaye mwenendo wake unaweza tukujadiliwa kwa hoja maalumu;

(c) linahitaji habari ambazo zinapatikana katika hatiambazo Mbunge anaweza kujisomeamwenyewe kama vile nakala za Sheria aumaandiko ya kumbukumbu za kawaida.

(d) limekusudiwa kupata maoni ya kisheria yakinadharia au kutoa mapendekezo juu ya jambola kubahatisha tu;

(e) lina maelezo ya dhihaka, uongo, sifazisizolazimu, au linatokana na habari zakubahatisha tu;

(f) lina madhumuni ya kutoa habari, au linaulizwakwa njia inayoonesha jibu lake au kutambulishamkondo fulani wa maoni;

(g) linahusu jambo zaidi ya moja na ni refu kupitakiasi; au

(h) linamtaja mtu yeyote kwa jina au kutoa maelezomahususi juu yake ila tu kama ni lazima ilikulifanya lieleweke.

Masharti kuhusu Maswal iyaBunge

27

41. Mbunge anayeuliza swali anaweza kuliondoa swali lake wakatiwowote kabla halijajibiwa-

(a) kwa kuwasilisha barua ya kufanya hivyo kwaKatibu iwapo siku iliyopangwa kwa swali hilokujibiwa haijafika; au

(b) iwapo swali husika tayari limewekwa kwenyeOrodha ya Shughuli, kwa kusimama mahali pakejina lake linapoitwa wakati wa maswali nakutamka kuwa analiondoa swali lake nakueleza kwa kifupi sababu za kufanya hivyo.

42.-(1) Wakati swali linalohusika litakapofikiwa katika Orodha yaShughuli, Spika atamwita Mbunge mwenye swali hilo au kamahayupo, Spika atamwita Mbunge mwingine yeyote aulize swali hilokwa niaba ya Mbunge mwenye swali.

(2) Mbunge atakayeitwa atasimama na kuuliza swali, pamoja namasahihisho (kama yapo), kwa kutamka maneno yafuatayo bila yakuongeza jambo lingine lolote:-

“Naomba swali langu (atataja namba ya swali lake lililopokwenye Orodha ya Shughuli) sasa lijibiwe.”

43.-(1) Muda wa Maswali Bungeni utakuwa dakika tisini, isipokuwakatika Mkutano wa Bunge la Bajeti, ambapo muda utakuwa dakikasitini.

(2) Spika anaweza kuweka kiwango cha juu cha maswaliyatakayowekwa katika Orodha ya Shughuli ambayo anaonayanaweza kujibiwa katika muda uliowekwa.

44.-(1) Maswali ya nyongeza yanaweza kuulizwa na Mbunge yeyotekwa madhumuni ya kupata ufafanuzi zaidi juu ya jambo lolotelililotajwa katika jibu lililotolewa.

(2) Mbunge anayeuliza swali la msingi ataruhusiwa kuuliza maswaliya nyongeza yasiyozidi mawili na Mbunge mwingine yeyoteatakayepewa nafasi ataruhusiwa kuuliza swali moja tu la nyongeza.

(3) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, swali ambalo litawekwa katikavifungu vya (a) na (b) litahesabiwa kuwa ni maswali mawili.

MaswaliyaNyongeza

Kuondoa Maswali

JinsiyaKuulizaMaswal i

MudawaMaswal i

28

(4) Isipokuwa kama Spika ataelekeza vinginevyo, Wabungewatakaouliza maswali ya nyongeza hawatazidi watatu kwa swalimoja la msingi, na Mbunge hataruhusiwa kusoma swali lake.

45.-(1) Swali lolote la nyongeza ambalo linaleta mamboyasiyotokana au kuhusiana na swali la msingi au linakiuka mashartiyanayohusiana na taratibu za kuulizwa maswali litakataliwa.

(2) Endapo Spika atakataa swali la nyongeza kwa kukiuka mashartiya Kanuni hizi, swali hilo halitajibiwa wala halitaoneshwa kwenyeTaarifa Rasmi.

(3) Iwapo Spika ataridhika kuwa, swali la msingi au la nyongezahalijapata majibu ya kuridhisha, ataagiza lijibiwe kwa ufasaha zaidikatika kikao kingine cha Bunge.

46.-(1) Waziri anayeulizwa swali atakuwa na wajibu wa kulijibuswali hilo kwa ukamilifu kama lilivyoulizwa, isipokuwa kwamba, kamajibu linalohusika ni refu au lina takwimu nyingi, Waziri atampaMbunge muuliza swali nakala ya jibu mapema baada ya kikaokuanza, kabla ya muda wa kujibu swali hilo haujafikiwa.

(2) Endapo Mbunge muuliza swali atamwomba Waziri ampatienakala ya jibu la swali lake kabla ya muda wa kujibu swali hilihaujafikiwa basi Waziri anaweza kumpa Mbunge muuliza swalinakala ya jibu kama lilivyoombwa.

(3) Waziri Mkuu au Waziri mwingine yeyote au Mwanasheria Mkuuwa Serikali anaweza kutoa majibu ya nyongeza kwa majibuyaliyotolewa na Waziri.

47.-(1) Baada ya Muda wa Maswali kwisha, Mbunge yeyote anawezakutoa hoja kuwa Shughuli za Bunge kama zilivyooneshwa kwenyeOrodha ya Shughuli ziahirishwe ili Bunge lijadili jambo halisi ladharura na muhimu kwa umma.

(2) Hoja ya namna hiyo itakuwa ni maalumu na inaweza kutolewawakati wowote hata kama majadiliano yatakuwa yanaendelea.

(3) Hoja itatolewa na Mbunge kwa kusimama mahali pake nakuomba idhini ya Spika kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bungekwa madhumuni ya kujadili jambo halisi la dharura na muhimu kwaumma.

Maswali kujibiwa kikamilifu

KuahirishaShughuliza BungeiliKujadiliJambo laDharura

Maswaliyanyongezayasiyo-ruhusiwa

29

(4) Iwapo Spika ataridhika kwamba jambo hilo ni la dharura, halisina lina maslahi kwa umma, basi ataruhusu hoja hiyo itolewe kwamuda usiozidi dakika tano na mjadala juu ya hoja hiyo utaendeleakwa muda ambao Spika ataona unafaa kwa kuzingatia mazingiraya suala linalojadiliwa.

48.-(1) Masharti ya jumla yafuatayo yatatumika vilevile kuhusuhoja ya kujadili suala la dharura:-

(a) hoja hiyo haitaruhusiwa iwapo inahusu jamboambalo kwalo taarifa ya hoja imekwishakutolewa au jambo ambalo limekwishakuwekwa kwenye Orodha ya Shughuli;

(b) hoja zaidi ya moja katika kikao kimoja zenyekutaka kuahirisha Shughuli za Bunge kwakutumia Kanuni hii hazitaruhusiwa; au

(c) jambo ambalo litakuwa limejadiliwa katika hojaya kuahirisha Shughuli za Bunge iliyotolewa kwamujibu wa Kanuni hii, halitaletwa tena Bungenikatika Mkutano ule ule kwa kutumia Kanuni hii.

(2) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwa tukuwa ni jambo halisi, iwapo:-

(a) ni jambo mahususi;

(b) halikuwekwa katika lugha ya jumla mno au linamambo mengi mchanganyiko;

(c) halikutolewa kwa kutegemea habari zisizo zauhakika au habari halisi juu ya jambo hilohazipatikani; au

(d) halihusu mambo ya kinadharia.

(3) Jambo linaloletwa kwa hoja chini ya Kanuni hii litahesabiwakuwa ni jambo la dharura, iwapo:-

(a) athari zake ni dhahiri na linaweza kutokea wakatiwowote;

MashartiyajumlakuhusuJambolaDharura

30

(b) limetokea siku hiyo au siku za karibuni nalimeletwa bila kuchelewa; au

(c) hakutatokea fursa ya kulijadili siku za karibunikwa njia ya kawaida ya kushughulikia mambo yaBunge.

(4) Jambo lolote litahesabiwa kuwa ni lenye maslahi kwa ummaiwapo utatuzi wake unategemea hatua zaidi kuliko zile zautekelezaji wa kawaida wa sheria peke yake.

49.-(1) Waziri anaweza kutoa kauli Bungeni kuhusu jambo lolotelinaloihusu Serikali.

(2) Kauli za aina hiyo zinaweza kutolewa kwa idhini ya Spika katikawakati unaofaa kufuatana na mpangilio wa Shughuli za Bunge nazitahusu jambo mahususi, halisi na zisizozua mjadala na muda wakusema utakuwa ni dakika zisizozidi thelathini.

(3) Waziri mwenye kutoa kauli atawajibika kutoa nakala ya kauliyake kwa Wabunge wote wakati anapoiwasilisha Bungeni.

50.-(1) Mbunge yeyote anaweza, kwa idhini ya Spika kutoa maelezobinafsi Bungeni yanayolenga kufafanua kuhusu jambo lolotelinalomhusu na lililoifikia jamii.

(2) Mbunge anayekusudia kutoa maelezo binafsi atapaswakuwasilisha maelezo hayo mapema kwa Spika na muda wa kusemautakuwa ni dakika zisizozidi kumi na tano, na maelezo hayohayatakuwa na mjadala kuhusu jambo hilo.

51.-(1) Mbunge anayetaka kuwasilisha jambo ambalo anaaminilinahusiana na haki za Bunge atafanya hivyo wakati unaofaakufuatana na mpangilio wa Shughuli za Bunge uliowekwa na Kanunihizi na atakuwa amemwarifu Spika mapema kuhusu kusudio lakehilo na jambo ambalo anataka kuliwasilisha.

(2) Spika akimwita Mbunge anayetaka kuwasilisha jambo ambaloanaamini linahusiana na haki za Bunge, Mbunge huyo ataeleza kwakifupi sababu zinazofanya aamini kwamba jambo analoliwasilishalinahusu haki za Bunge zilizotajwa kwenye Sheria ya Kinga,Madaraka na Haki za Bunge.

Masuala yanayo- husu Haki za Bunge

Sura ya296,Toleola 2002

MaelezoBinafsiyaWabunge

KaulizaMawaziri

31

(3) Endapo Spika ataamua kwamba jambo hilo linahusu haki zaBunge, basi atampa nafasi Mbunge mhusika kutoa hoja yake kishahoja hiyo itapewa kipaumbele katika kupanga shughuli nyinginezote za kikao kinachohusika.

(4) Mambo yanayohusu haki za Bunge yatawasilishwa kwa kufuatautaratibu uliowekwa katika Kanuni hizi na endapo wakati wa kikaochochote cha Bunge jambo lolote litazuka ghafla ambalolitaonekana linahusu haki za Bunge, shughuli zitasitishwa kwamadhumuni ya kuliwezesha jambo hili kuwasilishwa na kuamuliwa,isipokuwa tu kama wakati huo kura inapigwa.

52.-(1) Shughuli za Serikali zitaanza wakati Spika atakapomwitaWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyetoa taarifa yakuwasilisha Muswada au ya kutoa hoja Bungeni baada ya Katibukusoma jambo linalohusika kwenye Orodha ya Shughuli.

(2) Baada ya Spika kutoa wito huo, Mbunge yeyote binafsihataruhusiwa kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge walakuuliza swali.

53.-(1) Isipokuwa kama Kanuni hizi zimeagiza vinginevyo, hakunamjadala wowote utakaoendeshwa Bungeni ila tu kuhusu shughuliiliyoingizwa kwenye Kitabu cha Orodha ya Shughuli za Bunge nakuwekwa kwenye Orodha ya Shughuli za kikao hicho.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba na ya Kanuni hizi, Waziri auMbunge mwingine anaweza, kwa kutoa hoja, kupendekezakwamba, suala lolote lijadiliwe Bungeni na hoja hiyo itaamuliwakwa mujibu wa masharti ya Kanuni hizi.

(3) Isipokuwa kama Spika ataamua vinginevyo, kila hoja ambayotaarifa yake imekubaliwa itapelekwa kwanza kwenye Kamatiinayohusika.

(4) Endapo hoja itapelekwa kwenye Kamati inayohusika, Kamatihiyo itaanza kuishughulikia hoja hiyo mapema iwezekanavyo, nahaitatolewa Bungeni mpaka Mwenyekiti wa Kamati hiyoatakapokuwa amemtaarifu Spika kwamba, Kamati imemalizakuishughulikia hoja hiyo.

(5) Kamati iliyopelekewa hoja kwa mujibu wa Kanuni hii inawezakufanya mabadiliko katika hoja hiyo kwa kushauriana na mtoa hojahusika.

Hojazitakazo-tolewaBungeni

Shughuli za Serikali

32

(6) Endapo hoja haikupelekwa kwenye Kamati na imewekwakwenye Orodha ya Shughuli au kama ilipelekwa kwenye Kamati naKamati hiyo imemaliza kuishughulikia na imewekwa kwenye Orodhaya Shughuli, hoja itawasilishwa na kuamuliwa Bungeni kwa kufuatamasharti yafuatayo:-

(a) baada ya hoja kutolewa na inapobidi kuungwamkono Spika ataomba hoja hiyo ijadiliwe;

(b) mara baada ya mtoa hoja kuwasilisha hojayake, Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa hojahiyo atatoa maoni ya Kamati; na

(c) kama hoja inayohusika ni hoja ya Serikali,msemaji wa Kambi ya Upinzani atapewa nafasiya kutoa maoni juu ya hoja hiyo na kama hojainayohusika siyo ya Serikali, msemaji wa Serikaliatapewa nafasi ya kutoa maoni ya Shughuli zaSerikali juu ya hoja hiyo. Isipokuwa masharti yafasili hii hayatahusu hoja za Kamati.

(7) Baada ya mjadala kumalizika, Spika atawahoji Wabunge ilikupata uamuzi wa Bunge.

(8) Mbunge yeyote hataruhusiwa kufufua jambo lolote ambaloBunge lilikwisha kuliamua ama katika Mkutano huo uliopo au uleuliotangulia, wala kuwahisha shughuli ya Mkutano huounaoendelea, isipokuwa kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi aukuwahisha shughuli ambayo itazingatiwa katika Mkutanounaoendelea.

54.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Katiba au ya Kanuni hizi, Mbungeyeyote anaweza kupendekeza jambo lolote lijadiliwe Bungeni kwakuwasilisha hoja, yaani kwa kutoa pendekezo lililokamilika ili lipateuamuzi wa Bunge.

(2) Jambo lolote litakalowasilishwa kwa mujibu wa Kanuni hiilitawekwa katika lugha ambayo italiwezesha Bunge kufanyauamuzi ambao ni bayana.

(3) Isipokuwa kama itaelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi,mfumo wa maneno ya hoja inayowasilishwa Bungeni utakuwa kamaifuatavyo:-

JinsiyaKuwasi-lishaHoja

33

“KWA KUWA, .................................................. NA KWA KUWA, ............................................ KWA HIYO BASI, Bunge linaazimia kwamba ...”

(4) Hoja ambayo, kwa maoni ya Spika ina lengo la kutaka jamboambalo lilikwisha amuliwa na Bunge katika kipindi cha miezi kumina miwili iliyopita kabla ya kikao kinachoendelea lifikiriwe tena,haitakubaliwa na Spika, isipokuwa tu kama ni hoja ya kutaka uamuziwa Bunge uliokwisha fanyika ubadilishwe.

(5) Taarifa yoyote ya hoja ambayo inakiuka masharti ya Katiba auya Kanuni hizi haitakubaliwa.

55.-(1). Isipokuwa kama Kanuni hizi zitaruhusu vinginevyo au kamaSpika atatoa idhini yake kwa kutilia maanani udharura wa jambolenyewe, hoja yoyote haitatolewa Bungeni mpaka iweimewasilishwa na kupokelewa na Katibu angalau siku moja ya kazikabla ya Mkutano ambapo hoja hiyo inakusudiwa kutolewa.

(2) Hoja yoyote itatolewa kwa maandishi na itawekwa saini naMbunge anayeitoa kabla ya kupokelewa na Katibu kufuatana namasharti ya Kanuni hizi.

(3) Hoja zifuatazo zinaweza kutolewa bila taarifa:-

(a) kutengua Kanuni yoyote kati ya Kanuni hizi;

(b) kuahirisha Bunge au kuahirisha mjadala;

(c) kutaka wageni waondoke Bungeni;

(d) kutaka ombi lililowasilishwa Bungeni lijadiliwe;

(e) kuahirisha Shughuli za Bunge zinazoendelea ilikujadili jambo la dharura;

(f) kuhusu jambo lolote linalohusiana na haki zaBunge; na

(g) kutaka Hati iliyowasilishwa Bungeni ijadiliwe.

(4) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (2) ya Kanuni hii, iwapoanayetoa taarifa ni Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali, taarifahiyo itawekwa saini na Waziri anayehusika au Mwanasheria Mkuu

TaarifayaHoja

34

wa Serikali, lakini hoja hiyo inaweza kuwasilishwa na Waziri mwingineyeyote au Naibu Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

(5) Endapo hoja ambayo kwayo taarifa iliyotolewa haitajadiliwakatika Mkutano alioutaja mtoa hoja, basi taarifa ya hoja hiyoitatenguka lakini inaweza kutolewa tena katika Mkutano mwingine.

(6) Isipokuwa tu kwa idhini maalumu ya Spika, taarifa kuhusu jambololote linalohitaji taarifa itolewe kwa mujibu wa Kanuni hizi, lazimataarifa hiyo itolewe.

(7) Hoja zitaingizwa kwenye Kitabu cha Shughuli mapema baadaya kupokelewa na Katibu, na zitawekwa kwenye Orodha ya Shughuliya kikao cha Bunge kulingana na maelekezo ya Spika.

(8) Kila hoja itawekwa kwenye Orodha ya Shughuli ikiwa kamailivyowasilishwa au kama ilivyofanyiwa marekebisho au mabadilikoambayo Spika ataagiza yafanyike.

(9) Spika hataruhusu hoja yoyote inayokiuka Katiba au Sheria auKanuni za Bunge na Katibu atairudisha hoja hiyo pamoja na vielelezovyake vyote kwa Mbunge mhusika na maelezo ya sababu zakukataliwa kwa hoja hiyo.

(10) Iwapo Mbunge anapenda kufanya mabadiliko ya manenoaliyoyatumia katika hoja anayokusudia kuitoa, anaweza kufanyahivyo kwa kutoa taarifa ya kutaka kufanya mabadiliko angalausiku moja kabla ya siku ile ambapo hoja hiyo imewekwa kwenyeOrodha ya Shughuli ili ijadiliwe.

(11) Mbunge ambaye hakutoa taarifa ya kutaka kufanyamarekebisho au mabadiliko katika hoja yake, anaweza kumwombaSpika afanye marekebisho au mabadiliko katika hoja hiyo wakatianawasilisha hoja yake bila ya kutoa taarifa.

(12) Pamoja na kuwa taarifa ya kutaka kufanya marekebisho aumabadiliko itakuwa imetolewa, marekebisho au mabadiliko yoyotehayatakubaliwa kama, kwa maoni ya Spika, mabadiliko hayoyanabadilisha mambo ya msingi yaliyomo katika hoja auyanabadilisha makusudio au upeo wa hoja hiyo.

56.-(1) Mbunge atakapoitwa na Spika kutoa hoja, atasimamamahali pake na kutoa hoja yake.

UtaratibuwakujadiliHoja

35

(2) Hoja au marekebisho au mabadiliko ya hoja yoyote, yatahitajikuungwa mkono na Wabunge wasiopungua kumi na endapohayataungwa mkono hoja au marekebisho au mabadiliko hayoyatatenguka na Katibu ataweka kumbukumbu kwenye TaarifaRasmi kwamba, kwa kuwa hoja au marekebisho au mabadiliko hayohayakuungwa mkono, basi hayakujadiliwa.

(3) Mbunge anaweza kuunga mkono hoja kwa kusimama tu mahalipake bila kusema lolote kuhusu hoja hiyo, kisha akakaa; lakiniMbunge aliyefanya hivyo bado atakuwa na haki ya kuizungumziahoja hiyo hapo baadaye.

(4) Iwapo hoja imewekwa katika Orodha ya Shughuli na Mbungemtoa hoja anapoitwa na Spika anashindwa kuitoa, hoja hiyoitatenguka, isipokuwa kama kuna Mbunge mwinginealiyeidhinishwa na mtoa hoja, anaweza kuitoa kwa niaba yake aukama mtoa hoja ametoa taarifa ya kutaka kuiahirisha, hoja hiyoitaahirishwa.

(5) Hoja inayohusu shughuli za Serikali inaweza kutolewa na Waziriau Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

(6) Hoja iliyotenguka yaweza kutolewa tena baadaye, baada yataarifa mpya kutolewa kwa mujibu wa Kanuni hizi.

(7) Endapo hakuna Mbunge zaidi anayependa kuzungumzia hojailiyotolewa, Spika atampa mtoa hoja nafasi ya kuhitimisha hojayake.

(8) Ikiwa muda uliotengwa umekwisha wakati Bunge liko kwenyeKamati ya Bunge Zima kujadili vifungu vya Muswada wa Sheria aukatika Kamati ya Matumizi kujadili Makadirio ya Matumizi ya Serikali,basi Mwenyekiti, bila kulihoji Bunge, ataongeza muda usiozidi dakikathelathini kwa ajili ya kukamilisha kazi ya kupitisha Ibara za Muswadawa Sheria au mafungu ya fedha yaliyobaki.

57.-(1) Hoja ikishatolewa ili iamuliwe inaweza kubadilishwa kwa:-(a) kuondoa maneno fulani kwa ajili ya kuingiza

maneno mengine;

(b) kuondoa maneno fulani bila kuongeza mengine;au

(c) kuingiza au kuongeza maneno mapya.

Kubadili-shaHoja

36

(2) Kabla ya kutoa hoja hiyo, mtoa hoja atamkabidhi Katibumaandishi yenye saini yake na yanayoonesha mabadilikoanayotaka yafanywe.

(3) Kila badiliko linalopendekezwa sharti l iwiane na hojainayokusudiwa kufanyiwa mabadiliko na pia liungwe mkono nalisiingize jambo lolote ambalo, kwa maoni ya Spika, linawezakuwasilishwa kwa hoja maalumu.

(4) Badiliko lolote halitaruhusiwa kama, kwa maoni ya Spika,linapingana moja kwa moja na hoja ya msingi iliyotolewa.

(5) Iwapo hoja ya mabadiliko inapendekeza kuondoa manenofulani na kuingiza maneno mengine, basi mjadala juu ya suala lakufanya mabadiliko unaweza kuangalia kwa pamoja yale manenoyanayopendekezwa yaondolewe na maneno ambayoyanapendekezwa yaingizwe.

(6) Iwapo hoja inapendekeza kuondoa au kuingiza maneno,mjadala utahusu tu uondoaji au uingizaji wa maneno mapya, kadriitakavyokuwa.

(7) Hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja nyingine ya mabadilikosharti ihusiane na hoja ya kwanza ya mabadiliko na itatolewa,itajadiliwa na kuamuliwa kabla ya ile hoja ya kwanza ya mabadilikokufanyiwa uamuzi.

58.-(1) Endapo Mbunge anapenda kupendekeza mabadilikoyafanywe katika hoja kwa kufuata masharti ya Kanuni hizi, anawezakutoa hoja yake ya kufanya mabadiliko wakati wowote baada yahoja anayotaka kuibadilisha kutolewa, lakini kabla Bungehalijahojiwa liifanyie uamuzi.

(2) Endapo kuna mapendekezo mawili au zaidi ya kubadilisha hojamoja, Spika atawaita watoa hoja hizo kwa kufuata mpangilioatakaoamua.

(3) Iwapo mapendekezo yote ya mabadiliko yameamuliwa, Spikaataitoa tena hoja ya awali ili ijadiliwe kama itakavyokuwaimebadilishwa.

(4) Hoja yoyote inaweza kuondolewa wakati wowote kabla hojahiyo haijafikishwa Bungeni iwapo Mbunge mtoa hoja atatoa kwaKatibu, taarifa ya maandishi ya kuiondoa hoja hiyo.

Mabadi-likoyaHojanaKuondoaHoja

37

(5) Endapo hoja imefikishwa Bungeni, mtoa hoja anaweza tukuiondoa hoja yake kwa kusimama mahali pake na kusema “Ninaomba ruhusa kuondoa hoja” na papo hapo Spika ataliulizaBunge kama linaafiki hoja hiyo kuondolewa na inapotokeaWabunge walio wengi watakubali, Spika atasema “Hojainaondolewa kwa idhini ya Bunge” na hoja hiyo itakuwaimeondolewa na Bunge litaendelea na shughuli inayofuata.

SEHEMU YA TANO

KANUNI ZA MAJADILIANO

59.- Kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyote anaweza kusimama nakuchangia Bungeni katika nyakati zifuatazo:-

(a) wakati wa kuchangia mjadala wa hoja yoyoteiliyowasilishwa Bungeni ambayo Kanunizinaruhusu ijadiliwe;

(b) wakati anatoa hoja ili ijadiliwe;

(c) wakati anawasilisha mabadiliko yoyote ya hoja;

(d) wakati amesimama kutaka kuzungumzia jambololote linalohusu utaratibu;

(e) wakati amesimama kuzungumzia jambo linalohusuhaki za Bunge;

(f) wakati wa kutoa hoja ya kuahirisha shughuli zaBunge kwa madhumuni ya kujadili jambo ladharura na muhimu kwa Umma;

(g) wakati wa kutoa Maelezo Binafsi;

(h) wakati wa kuuliza au kujibu swali;

(i) wakati wa kutoa taarifa baada ya kupewa idhiniya Spika kufanya hivyo.

60.-(1) Mbunge akitaka kusema anaweza:-

(a) kumpelekea Spika ombi la maandishi;(b) kusimama kimya mahali pake; au(c) kutumbukiza kadi ya elektroniki.

JinsiyakupatanafasiyakusemaBungeni

NyakatizaMbungekusemaBungeni

38

(2) Isipokuwa kwamba, Mbunge yeyote hataanza kuzungumza hadiaitwe na Spika ama kwa jina au wadhifa wake na kumruhusu kusemana wakati wa kusema ataelekeza maneno yake kwa Spika.

(3) Mbunge akimaliza kutoa maelezo yake atakaa kwenye nafasiyake na hapo Spika atamwita Mbunge mwingine aliyempelekeaombi la maandishi au kama Spika hakupata ombi lolote lamaandishi, basi Mbunge mwingine yeyote anayetaka kujadili hojaanaweza kusimama mahali pake na kusubiri Spika amwone.

(4) Iwapo Wabunge wawili au zaidi watasimama wakati mmoja,Spika atamwita Mbunge atakayemwona kwanza.

(5) Endapo maombi ya kuchangia hoja fulani yatakuwa mengi zaidiya muda uliotengwa kwa hoja hiyo, Spika atatoa nafasi ya kwanzakwa Wabunge ambao:-

(a) hawajachangia katika hoja zilizotanguliakujadiliwa katika Mkutano unaoendelea; au

(b) wamechangia mara chache.

(6) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (5) ya Kanuni hii, Spikaatahakikisha kuwa, nafasi za kuchangia zinatolewa kwa uwianounaofaa baina ya aina zote za Wabunge walioomba kuchangiahoja hiyo.

(7) Masharti yaliyotangulia katika Kanuni hii, hayatamzuia Spikakutoa nafasi ya kuchangia kwa Mbunge mwingine yeyote iwapoataona kuwa, taaluma au uzoefu fulani wa Mbunge huyoutaboresha hoja inayojadiliwa.

(8) Mbunge hatasoma maelezo, isipokuwa, kwa madhumuni yakutilia nguvu maelezo yake, anaweza kusoma dondoo kutokakwenye kumbukumbu zilizoandikwa au kuchapishwa na anawezapia kujikumbusha kwa kuangalia kwenye kumbukumbu alizoziandika.

(9) Kila Mbunge atasema akiwa amesimama na atatoa maelezoyake kwa kutumia vyombo vilivyowekwa kwa madhumuni yakutafsiri, kukuza na kurekodi sauti.

(10) Kwa ruhusa ya Spika, Mbunge yeyote aliye na ulemavu auugonjwa anaweza kuzungumza akiwa ameketi.

39

(11) Endapo Spika atasimama wakati Waziri au Mbunge anatoahotuba Bungeni au atakuwa amesimama mahali pake akisubirikuanza kuzungumza, Waziri au Mbunge huyo ataketi mahali pakena Bunge litabaki kimya ili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifayake.

(12) Mbunge hataruhusiwa kuzungumzia suala lililokuwa likijadiliwabaada ya Spika kuwahoji Wabunge na hoja hiyo kutolewa maamuzi.

(13) Mbunge yeyote anaweza pia kutoa maoni yake kwa maandishina kumpelekea Waziri au Mbunge mtoa hoja inayohusika, wakatiambapo hoja inaendelea kujadiliwa.

(14) Mtoa hoja atayakabidhi maoni hayo kwa Katibu ili yawezekuingizwa katika Taarifa Rasmi za Bunge.

(15) Katika mjadala wowote, Mawaziri watatajwa kwa majina yanyadhifa zao na Wabunge watatajwa kwa kutumia neno“Mheshimiwa” kabla ya majina yao.

61.-(1) Wakati wa majadiliano Bungeni au kwenye Kamati yoyoteya Bunge, Mbunge hataruhusiwa kuzungumzia jambo lolote ambaloyeye mwenyewe ana maslahi binafsi nalo ya kifedha, isipokuwabaada ya kusema jinsi anavyohusika nalo na kutaja kiwango chamaslahi hayo, na kwa sababu hiyo, itakuwa ni lazima kwa Mbungeyeyote anayetaka kuzungumzia jambo hilo Bungeni au kwenyeKamati yoyote ya Bunge, kusema kwanza jinsi anavyohusika najambo hilo na kutaja kiwango cha maslahi ya kifedha aliyonayokuhusiana na jambo hilo kabla ya kuanza kuzungumzia jambo hilo.

(2) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, Mbunge au mwananchi yeyoteanaweza kumwarifu Spika, kwa maandishi, akitoa na ushahidi kuwa,Mbunge amezungumzia jambo ambalo ana maslahi binafsi nalo yakifedha bila kusema jinsi anavyohusika nalo wala kutaja kiwangocha maslahi hayo.

(3) Baada ya kupokea taarifa iliyowasilishwa kwake kwa mujibu wafasili ya (2) ya Kanuni hii, Spika ataipeleka taarifa hiyo kwenyeKamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

(4) Baada ya kupokea taarifa iliyopelekewa na Spika chini ya fasiliya (3) ya Kanuni hii, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungeitaichunguza taarifa hiyo na endapo itadhihirika kwamba ni kweliMbunge amezungumzia jambo ambalo ana maslahi binafsi nalo ya

Kuto-zungumziajamboambalolinamaslahibinafsiyakifedha

40

kifedha bila kusema jinsi anavyohusika nalo wala kutaja kiwangocha maslahi hayo, Kamati hiyo ya Bunge inaweza kulishauri Bungekwamba, Mbunge huyo aadhibiwe kwa ukiukwaji wa Kanuni hiikama ifuatavyo:-

(a) ikiwa hilo ni kosa lake la kwanza, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi kumi;

(b) ikiwa hilo ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(5) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowote uliotolewana Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu adhabuanayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka masharti ya Kanuni hii.

(6) Kabla ya Bunge kupitisha Azimio la kumwadhibu Mbunge kwakuzingatia ushauri wa Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungeutakaotolewa chini ya fasili ya (4) na (5) ya Kanuni hii, Mbungemhusika atapewa nafasi ya kutoa utetezi wake mbele ya Bunge.

62.-(1) Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo kwenye Kanuni hizi:- (a) kila Mbunge anayejadili hoja, ataruhusiwa kusema kwa muda usiozidi dakika kumi na tano;

(b) Waziri anayetoa hoja ataiwasilisha hoja yakekwa muda usiozidi dakika thelathini nawakati anahitimisha hoja yake atasema kwamuda usiozidi dakika sitini;

(c) Mwenyekiti anayewasilisha maoni ya Kamatiatayawasilisha kwa muda usiozidi dakikathelathini;

(d) Msemaji wa Upinzani anayewasilisha maoni yaKambi ya Upinzani atayawasilisha maonihayo kwa muda usiozidi dakika thelathini; na

(e) Mbunge anayetoa hoja binafsi ataiwasilisha hojayake kwa muda usiozidi dakika thelathini nawakati wa kuhitimisha hoja yake atasema kwamuda usiozidi dakika sitini.

(2) Bila ya kuathiri masharti mengine ya Kanuni hii, Mbungeanayejadili hoja ataruhusiwa kusema kwa muda unaoruhusiwa naKanuni hizi.

MudawakusemaBungeni

41

63.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katibayanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katikaBunge, ni marufuku kabisa kusema uongo Bungeni na kwa sababuhiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni ana wajibu wakuhakikisha kwamba anatoa kauli au maelezo kuhusu jambo ausuala ambalo yeye mwenyewe anaamini kuwa ni la kweli na siyojambo la kubuni au la kubahatisha tu.

(2) Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni hatachukuliwakuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusujambo fulani lililotangazwa au lililoandikwa na vyombo vya habari.

(3) Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama mahali pake nakutamka “kuhusu utaratibu” na baada ya kuruhusiwa na Spika,kudai kwamba, Mbunge aliyekuwa anasema kabla yake ametoamaelezo ya uwongo kuhusu jambo au suala alilokuwa analisemaBungeni.

(4) Mbunge anayetoa madai kwa mujibu wa fasili ya (3) ya Kanunihii atakuwa na wajibu wa kutoa na kuthibitisha ukweli kuhusu jamboau suala hilo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge.

(5) Bila ya kuathiri masharti ya fasili zilizotangulia za Kanuni hii,Spika au Mbunge mwingine yeyote, baada ya kutoa maelezomafupi ya ushahidi unaotilia mashaka ya dhahiri kuhusu ukweli wakauli au usemi au maelezo juu ya jambo au suala ambalo Mbungeamelisema Bungeni, anaweza kumdai Mbunge huyo atoeuthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi au maelezo yake na kamaatashindwa kufanya hivyo, afute kauli au usemi au maelezo yakehayo.

(6) Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha ukweli wa kauli au usemi aumaelezo yake aliyoyatoa Bungeni, atawajibika kutoa uthibitishohuo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge, papo hapo au katika mudaatakaopewa na Spika kwa ajili ya kufanya hivyo.

(7) Endapo Mbunge aliyetakiwa kuthibitisha kauli au usemi aumaelezo yake aliyoyatoa Bungeni atashindwa kufanya hivyo,anaweza kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yakehayo, papo hapo au katika muda atakaokuwa amepewa na Spikakwa ajili ya kuthibitisha kauli au usemi au maelezo yake.

(8) Endapo hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa, Mbungealiyetakiwa kutoa uthibitisho wa ukweli wa kauli au usemi au

KutosemauongoBungeni

42

maelezo yake aliyoyatoa Bungeni atakataa au atashindwa kutoauthibitisho huo kwa kiwango cha kuliridhisha Bunge na kamaatakataa kujirekebisha kwa kufuta kauli au usemi au maelezo yake,basi Spika atamwadhibu kwa kumsimamisha Mbunge huyoasihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi vitano.

(9) Endapo Mbunge mwingine yeyote ataona kwamba uwongouliosemwa na Mbunge huyo Bungeni ni mkubwa kiasi cha kuathiriheshima ya Bunge, anaweza kutoa hoja kwamba, Mbunge huyo: -

(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi kumi;

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi, asihudhurievikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(c) achukuliwe hatua nyingine za kinidhamuzitakazotajwa katika hoja yake.

(10) Hoja ya aina hiyo inaweza kutolewa bila taarifa na itajadiliwana kuamuliwa kwa utaratibu ufuatao:-

(a) Mtoa hoja atatoa hoja yake;

(b) Mbunge anayetuhumiwa kusema uongo Bungenichini ya fasili ya (9) ya Kanuni hii atapewa nafasiya kujitetea;

(c) Wabunge, kwa idadi itakayoamuliwa na Spikakulingana na muda uliopo, watachangia hojahiyo kwa dakika zitakazopangwa;

(d) Mtoa hoja atahitimisha hoja yake;

(e) Mbunge anayetuhumiwa kusema uwongoBungeni au Mbunge mwingine yeyote anawezakutoa maombi ya adhabu iliyopendekezwa kwakosa la kusema uongo Bungeni ipunguzwe kwakiwango au namna atakayoipendekeza;

(f) Spika atawahoji Wabunge ili kupata uamuziwa Bunge kuhusu ombi la kupunguziwa adhabukama litatolewa na Mbunge anayetuhumiwa auMbunge mwingine yeyote.

43

(g) Iwapo pendekezo la kupunguziwa adhabulitakataliwa, basi Spika atalihoji Bunge ili kupatauamuzi kuhusu adhabu iliyopendekezwa na Mtoahoja.

64.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 ya Katibayanayolinda na kuhifadhi uhuru wa mawazo na majadiliano katikaBunge, Mbunge:-

(a) hatatoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazinaukweli;

(b) hatazungumzia jambo ambalo haliko kwenyemjadala;

(c) hatazungumzia jambo lolote ambalo linasubiriuamuzi wa Mahakama au jambo lolote ambalolilijadiliwa na kutolewa maamuzi kwenyeMkutano uliopo au uliotangulia na ambalohalikuletwa rasmi kwa njia ya hoja mahususi navilevile hatapinga uamuzi wowote uliofanywana Bunge, isipokuwa tu kwa kutoa hojamahususi inayopendekeza kuwa uamuzi huouangaliwe upya;

(d) hatatumia jina la Rais kwa dhihaka katikamjadala, au kwa madhumuni ya kutakakulishawishi Bunge kuamua jambo lolote kwanamna fulani;

(e) hatazungumzia mwenendo wa Rais, Spika,Mbunge, Jaji, Hakimu au mtu mwingine yeyoteanayeshughulikia utoaji wa haki, isipokuwa tukama kumetolewa hoja mahususi kuhusu jambohusika;

(f) hatamsema vibaya au kutoa lugha ya matusikwa Mbunge au mtu mwingine yeyote;

(g) hatatumia lugha ya kuudhi au inayodhalilishawatu wengine.

(2) Mbunge yeyote anayeamini kuwa Mbunge mwingine amevunjaau amekiuka masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, atasimama

Mamboyasiyo-ruhusiwaBungeni

44

mahala pake na kumwambia Spika wa Bunge “Kuhusu utaratibu”na atakaporuhusiwa na Spika kusema, atalazimika kutaja mashartiya Kanuni hii yaliyovunjwa au kukiukwa na Mbunge huyo mwingine,na kama Mbunge huyo mwingine atakuwa anasema wakati huo,atakaa chini kusubiri maelekezo na mwongozo wa Spika kuhusujambo hilo.

65.-(1) Isipokuwa tu kwa idhini ya Spika, Mbunge yeyotehataruhusiwa kusema zaidi ya mara moja juu ya hoja, ila tu kama:-

(a) wakati huo Bunge liko kwenye Kamati ya BungeZima au Kamati ya Matumizi;

(b) anatumia haki yake ya kujibu; au

(c) anasema kuhusu utaratibu.

(2) Mbunge ambaye amezungumza juu ya hoja anawezakuzungumza tena juu ya hoja ya kufanya mabadiliko katika hojaaliyoisemea; na Mbunge ambaye amependekeza kufanyamabadiliko katika hoja ya awali, anaweza kuzungumza tena juu yahoja ya awali baada ya mabadiliko kufanyika.

(3) Mbunge mtoa hoja ya msingi au mtoa hoja ya kutaka kufanyamabadiliko katika hoja iliyokwisha kutolewa, atakuwa na haki yakujibu kabla uamuzi juu ya hoja hiyo haujatolewa.

(4) Wakati wa kujibu, mtoa hoja atapaswa kujibu mambo yale tuyaliyozungumzwa na Wabunge waliochangia hoja yake nahataruhusiwa kutoa maelezo yoyote mapya, isipokuwa kamamaelezo hayo ni ya lazima kwa madhumuni ya kufafanua jambolililochangiwa na Wabunge.

(5) Mbunge yeyote hataruhusiwa kusema Bungeni baada ya Spikakuwahoji Wabunge na kura ya sauti ama ya elektroniki au ya siri ya“ndiyo” au “siyo” au ya “kutokukubaliana” au kura ya uamuzi yaaina nyingine yoyote kupigwa, isipokuwa pale ambapo itaonekanakuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura kwa kufuata wingi wasauti kwa mujibu wa fasili ya 5 ya Kanuni ya 79 ya Kanuni hizi.

66.-(1) Wakati wa Vikao vya Bunge, Spika anapokuwa anaingiaau kutoka katika Ukumbi wa Bunge, Wabunge na wageni wotewaliopo kwenye Ukumbi huo watasimama kwa utulivu mahali paona kubaki kimya hadi Spika atakapokuwa ameketi katika Kiti chakeau atakapokuwa ametoka kwenye Ukumbi wa Bunge.

Stahandani ya Bunge

Kuzungu-mzazaidi yamaramoja

45

(2) Wakati Bunge linaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima au katikaKamati ya Matumizi, Wabunge na wageni wote waliopo kwenyeUkumbi wa Bunge watasimama kwa utulivu mahali pao na kubakikimya ili kutoa heshima kwa mchakato wa Bunge kuingia kwenyeKamati ya Bunge Zima au kwenye Kamati ya Matumizi na baadayeBunge kurejea.

(3) Mbunge aliyepo Bungeni wakati wa mjadala atatakiwa:-

(a) kuingia au kutoka kwenye Ukumbi wa Bunge kwastaha na atainamisha kichwa kuelekea kwaSpika au kufanya mkunjo wa magoti kwaheshima, kila mara Mbunge huyo atakapokuwaakienda au kutoka mahali pake;

(b) kutulia na kukaa kwa heshima mahali pake, nahatatangatanga kwenye ukumbi wa Mikutanobila sababu;

(c) kutopita kati ya Kiti cha Spika na Mbungeanayesema;

(d) kutosoma kitabu chochote, gazeti au barua,isipokuwa kama vitu hivyo vinahusu shughuli zamjadala unaoendelea wakati huo; na

(e) kuzima simu ya mkononi na kwa namna yoyotekutotumia simu.

67.-(1) Spika anaweza kulihutubia Bunge wakati wowote na kwaajili hiyo, anaweza kumkatiza Mbunge yeyote anayezungumza.

(2) Endapo Spika atasimama wakati wa mjadala, na kuanzakuzungumza, Mbunge yeyote ambaye atakuwa anazungumzawakati huo au ambaye atakuwa amesimama mahali pake akisubirikuanza kuzungumza, ataketi mahali pake, na Bunge litabaki kimyaili Spika aweze kutoa maelekezo au taarifa yake.

68.-(1) Mbunge anaweza kusimama wakati wowote na kusemamaneno “kuhusu utaratibu”, ambapo Mbunge yeyote ambayewakati huo atakuwa anasema atanyamaza na kukaa chini na Spikaatamtaka Mbunge aliyedai utaratibu ataje Kanuni au sehemu yaKanuni iliyokiukwa.

MamlakayaSpikakukatizamajadiliano

Taarifa kuhusuutaratibunaMwongozo

46

(2) Mbunge aliyedai utaratibu atalazimika kutaja Kanuni au sehemuya Kanuni ya Bunge iliyokiukwa.

(3) Baada ya kutaja Kanuni au sehemu ya Kanuni ya Bungeiliyokiukwa Mbunge aliyesimama kuhusu utaratibu, ataketi mahalipake kusubiri maelekezo na uamuzi wa Spika.

(4) Spika anaweza, ama papo hapo kutoa uamuzi wake juu yajambo la utaratibu lililotajwa au kuahirisha uamuzi ili alifikirie zaidijambo hilo na kutoa uamuzi baadaye au kutoa uamuzi na baadayekutoa sababu za uamuzi huo, vyovyote atakavyoamua.

(5) Katika kufikia uamuzi wake, Spika anaweza kuitaka Kamati yaKudumu ya Kanuni za Bunge au Kamati nyingine yoyote ya Bungeimpe ushauri kuhusu jambo husika.

(6) Mbunge aliyekuwa anazungumza wakati jambo la utaratibulilipohojiwa anaweza kuendelea na hotuba yake baada ya Spikakutoa uamuzi juu ya jambo hilo.

(7) Hali kadhalika, Mbunge anaweza kusimama wakati wowoteambapo hakuna Mbunge mwingine anayesema na kuomba“Mwongozo wa Spika” kuhusu jambo ambalo limetokea Bungenimapema, ili Spika atoe ufafanuzi kama jambo hilo linaruhusiwa auhaliruhusiwi kwa mujibu wa Kanuni na taratibu za Bunge na majibuya Spika yatatolewa papo hapo au baadaye, kadri atakavyoonainafaa.

(8) Vilevile, Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake nakusema “taarifa” na kwa ruhusa ya Spika, atatoa taarifa auufafanuzi kwa Mbunge anayesema, ambapo Spika atamtakaMbunge anayesema aketi kusikiliza taarifa hiyo.

(9) Mtoa taarifa atakapomaliza na kuketi, Spika atamuuliza Mbungealiyekuwa akisema mwanzo kama anaikubali au haikubali taarifahiyo kabla ya kumruhusu kuendelea kuchangia hoja.

(10) Uamuzi wa Spika kuhusu suala lolote la utaratibu utakuwa niwa mwisho.

69.- (1) Mbunge anayependa mjadala unaoendelea juu ya hojayoyote uahirishwe hadi wakati wa baadaye, anaweza kutoa hoja“Kwamba mjadala sasa uahirishwe” na atataja mjadala huo

HojayakuahirishaMjadala

47

uahirishwe hadi wakati gani na pia atalazimika kutoa sababu kwanini anataka mjadala uahirishwe.

(2) Kama Spika atakuwa na maoni kwamba kuwasilishwa kwa hojahiyo ni kinyume cha uendeshaji bora wa shughuli za Bunge, atakataakuitoa ili iamuliwe; vinginevyo, papo hapo atawahoji Wabungejuu ya hoja hiyo kadri atakavyoona inafaa.

(3) Endapo hoja iliyowasilishwa haitapata kibali cha Bunge, mjadalakuhusu hoja iliyoko mbele ya Bunge utaendelea.

(4) Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa hoja ya kufanya mabadilikokatika hoja iliyotolewa kwa mujibu wa Kanuni hii.

70.-(1) Utaratibu utakaotumika kufunga mjadala ni kutoa hoja yakufunga mjadala endapo bado kuna Wabunge wanaopendakuzungumza juu ya jambo lililoko katika mjadala lakini mudauliotengwa umekwisha au endapo Bunge limewekewa kiwangocha juu cha muda wa kujadili hoja inayohusika na muda huo badohaujaisha.

(2) Hoja ya kufunga mjadala inaweza kutolewa baada ya hotubayoyote kukamilika au ikiwa Spika ataruhusu hoja ya kufanya mjadala,mara tu au muda mfupi baada ya hoja hiyo kutolewa ili iamuliwe.

(3) Mbunge anayetoa hoja ya kufunga mjadala, anawezakusimama mahali pake na kutoa hoja “Kwamba mtoa hoja sasaapewe nafasi ya kujibu”.

(4) Endapo Spika ataona kuwa hoja ya kufunga mjadala inakiukamwenendo bora wa Shughuli za Bunge au inavunja haki zaWabunge, basi ataikataa.

(5) Endapo hoja “Kwamba mtoa hoja sasa apewe nafasi ya kujibu”itakubaliwa, mtoa hoja atajibu kama akipenda na baada ya hotubaya kujibu kukamilika au kama mtoa hoja hapendi kujibu basi Spikaatawahoji Wabunge ili kuamua hoja hiyo.

71.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 100 na 101 ya Katiba,mtu yeyote asiye Mbunge ambaye atajisikia kuwa amepata atharihasi kutokana na kauli au maneno au shutuma zilizotolewa Bungenikumhusu yeye binafsi, anaweza kupeleka malalamiko pamoja namaelezo yake ya kujitetea kwa Spika:-

Hojaya KufungaMjadala

Haki yaraiakujiteteanakujisafishadhidi yakaulizinazoto-lewaBungeni

48

(a) yawe yameandikwa kwa lugha fasaha na yaheshima na yanahitimishwa kwa maelezo yajumla kuhusu madhumuni yake;

(b) yawe yamewasilishwa katika kipindi cha sikukumi na nne baada ya kauli au manenoyanayolalamikiwa kutolewa;

(c) yawe yamewasilishwa na mtu binafsi ambaye niraia wa Tanzania na hayajawasilishwa na aukwa niaba ya Kampuni, Shirika au Taasisi;

(d) yaonyeshe wazi kuwa, kwa dhahiri mhusikaaliathirika yeye binafsi kutokana na kauli aumaneno au shutuma zilizotolewa Bungeni.

(e) yaeleze kwa ufasaha ni jinsi gani mhusikaamepata athari hasi, kama vile kuchafuliwajina lake na heshima yake katika jamii aukuharibu sifa, mahusiano na ushirikiano wakena wengine au kazi yake anayoifanya katikajamii au kuingilia uhuru na maisha yake binafsina familia yake isivyo halali kutokana na kauli aushutuma zilizotolewa Bungeni.

(f) yatoe ombi kwamba, endapo kwa utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi yatakubalika, basimaelezo ya utetezi au ufafanuzi yaliyotolewa namuhusika kwa ajili ya kusafisha jina nakurejesha heshima yake yachukuliwe na Bungekuwa ndiyo majibu sahihi ya kauli au shutumazilizotolewa Bungeni.

(2) Mara baada ya kupokea malalamiko yaliyowasilishwa kwakekwa mujibu wa fasili ya (1) ya Kanuni hii na kujiridhisha kuwamalalamiko hayo yameandikwa katika lugha ya heshima na yakistaarabu na yanatoa hoja mahususi na ambayo si ya uzushi, uongo,uchochezi au chuki binafsi; na kwamba yanastahili kufikiriwa aukufanyiwa kazi na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,Spika atayapeleka malalamiko hayo kwenye Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge ili kuyatafakari na kulishauri Bunge.

(3) Katika kuyafanyia kazi malalamiko yaliyopelekwa kwake naSpika kwa mujibu wa fasili ya (3) ya Kanuni hii, Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge:-

49

(a) itakutana katika kikao cha faragha;

(b) inaweza kumhoji mtu aliyewasilisha malalamikoyake kwa Spika au Mbunge au Waziri aliyetoaBungeni kauli au shutuma zinazolalamikiwa;

(c) haitajadili wala kutoa uamuzi kuhusu ukweli wakauli au shutuma zilizotolewa Bungeni au ukweliwa maelezo yaliyotolewa kwenye malalamikohusika;

(d) haitatangaza maelezo yaliyomo kwenyemalalamiko husika wala mwenendo wamajadiliano yake kuhusiana na malalamikohusika;

(4) Baada ya kukamilisha kazi yake, Kamati ya Haki, Maadili naMadaraka ya Bunge itawasilisha Bungeni, taarifa ya uamuzi wakekuhusu malalamiko husika, pamoja na maelezo yote au sehemu yamaelezo ya malalamiko husika, kwa ajili ya kuridhiwa na Bunge.

(5) Taarifa itakayowasilishwa Bungeni na Kamati ya Haki, Maadilina Madaraka ya Bunge inaweza kupendekeza mojawapo yayafuatayo:-

(a) maelezo ya utetezi au ufafanuzi wa mlalamikaji,kama yalivyoelezwa kwenye taarifa hiyo,yaingizwe kwenye Taarifa Rasmi za Bunge; au

(b) Bunge lisichukue hatua yoyote nyingine.

SEHEMU YA SITA

AMANI NA UTULIVU BUNGENI

72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibubora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolotela utaratibu utakuwa ni wa mwisho.

(2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanuni hizianaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu na vilevileMbunge mwingine yeyote anaweza kusimama na kumfahamishaSpika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katika kufanya hivyo,atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyoweka utaratibu uliokiukwa.

MamlakayaSpikakusimamiautaratibu

50

(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa jamboau suala alilolisema Bungeni na hadi kufikia mwisho wa mudaaliopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spikaanaweza kumsimamisha Mbunge huyo kuhudhuria vikao vya Bungevisivyozidi vitano.

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahikuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spikaatalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 71 ya Kanuni hizi iliKamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu hatua za kinidhamu zinazostahilikuchukuliwa dhidi ya Mbunge huyo.

73.-(1) Mbunge au Waziri atakayezungumzia jambo au mamboambayo hayaruhusiwi na Kanuni hizi, anaweza kuamriwa na Spikaau Naibu Spika au Mwenyekiti akatishe hotuba yake na kukaa mahalipake.

(2) Endapo Mbunge au Waziri atatumia maneno au lughaisiyotakiwa Bungeni, yaani lugha ya matusi, usafihi, uchokozi aulugha ya maudhi na akitakiwa na Spika ajirekebishe kwa kufutamaneno au lugha hiyo atakataa kufanya hivyo, Spika anawezakumwamuru Mbunge huyo atoke mara moja nje ya Ukumbi waBunge na abaki huko nje kwa muda wote uliosalia wa kikao chasiku hiyo.

(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wamaneno aliyoyasema na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa,amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anawezakumsimamisha Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bungevisivyozidi vitano.

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahikuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spikaatalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge ili Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahilikutolewa kwa Mbunge mhusika.

74.-(1) Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharauMamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati yaHaki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa:-

(a) kwa maneno au vitendo, Mbunge huyoanaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au

Adhabuz i n a z o -wezakuto-lewa naSpikakwaukiukaj iwaKanuni

Adhabuzinazo-wezakutolewanaBungekwaukiukajiwaKanuni

51

(b) Mbunge huyo atafanya kitendo chochote chamakusudi cha kudharau Shughuli ya Bunge auMbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo.

(2) Ikiwa maneno au vitendo vya Mbunge vilivyoainishwa katikafasili ya (1) ya Kanuni hii vimetokea wakati Bunge likiwa katikaKamati ya Bunge Zima, basi Mwenyekiti atasimamisha shughuli zaKamati na ataagiza Bunge kurudia ili kumpatia Spika fursa ya kutoataarifa kwa Bunge kuhusu mwenendo wa Mbunge huyo nakuwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madarakaya Bunge.

(3) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itajadili sualahilo na ikithibitika kuwa Mbunge husika ametenda kosa inawezakushauri kwamba:-

(a) ikiwa ni kosa lake la kwanza Mbunge huyoasihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi; au

(b) ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi Mbunge huyoasihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;

(4) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowoteutakaotolewa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungekuhusu adhabu anayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka mashartiya Kanuni hii.

(5) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, Bunge linawezakumchukulia hatua nyinginezo za kinidhamu, ikiwa ni pamoja nakumsimamisha kazi Mbunge yeyote aliyetenda kosa chini ya Kanunihii.

(6) Adhabu yoyote itakayotolewa kwa Mbunge aliyekiuka mashartiya Kanuni hii itatolewa kupitia Azimio la Bunge ambalo litatajaadhabu hiyo pamoja na sababu zake.

75.- Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge nahataingia tena katika sehemu yoyote ya Ukumbi wa Bunge namaeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa,na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana namshahara huo.

76.-(1) Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani yaUkumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumia

MashartikwaMbungealiyesima-mishwakazi

Udhibitiwa fujoBungeni

52

nguvu, basi anaweza kuahirisha Shughuli za Bunge bila ya hojayoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujohiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge.

(2) Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamati yaHaki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababishakutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la Mbunge au majina yaWabunge waliohusika na fujo hiyo ili Kamati hiyo iweze kulishauriBunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa.

SEHEMU YA SABA

UHALALI WA SHUGHULI

77.-(1) Akidi kwa kila kikao cha Bunge wakati wa kufanya maamuziitakuwa ni nusu ya Wabunge wote, kama ilivyofafanuliwa katikaIbara ya 94 ya Katiba, isipokuwa kwamba, idadi hiyo haitahusu hojakuhusu uamuzi wa kubadilisha masharti yoyote ya Katiba kwa mujibuwa Ibara ya 98 ya Katiba.

(2) Mbunge yeyote aliyehudhuria anaweza kumjulisha Spikakwamba, Wabunge waliopo ni pungufu ya akidi inayohitajika kwaajili ya shughuli inayoendelea.

(3) Endapo Spika ataridhika kwamba ni kweli idadi ya Wabungewalio ndani ya Ukumbi wa Bunge ni pungufu ya akidi inayohitajika,basi atasimamisha Shughuli za Bunge kwa muda atakaoutaja naatamwagiza Katibu kupiga kengele.

(4) Bunge litakaporudia baada ya wakati uliotajwa kukamilika,Spika atahakikisha kama idadi ya Wabunge waliopo inafikia akidiinayohitajika ili kuruhusu uamuzi kufanyika.

(5) Endapo Spika ataridhika kwamba bado idadi ya Wabungewaliomo ndani ya Ukumbi wa Bunge haifikii akidi inayohitajika basiataahirisha Shughuli za Bunge hadi muda mwingine atakaoutaja.

78.-(1) Shughuli za Bunge hazitakuwa batili kwa sababu tu kwambanafasi yoyote ya Mbunge ipo wazi.

79.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara za 46A, 50(3), 53A na 98 zaKatiba, mambo yote yanayohitaji kuamuliwa na Bunge yataamuliwakwa kufuata maoni ya Wabunge walio wengi waliohudhuria nakupiga kura Bungeni.

Uhalali wa maamuzi ya Bunge

AkidiyaVikaovyaBunge

UamuziwaBunge

53

(2) Spika, wakati amekalia kiti cha Spika, hatakuwa na kura yakawaida bali atakuwa na kura ya uamuzi endapo kura za “Ndiyo”na “Siyo” zitalingana.

(3) Wakati mjadala juu ya hoja unapomalizika, Spika atawahojiWabunge ili kupata uamuzi juu ya hoja hiyo kama ilivyo au baadaya kufanyiwa marekebisho au mabadiliko, Spika kwanza atatakauamuzi wa wale wanaoafiki kwa kusema: “Wale wanaoafiki wasemeNdiyo” na baadaye atataka uamuzi wa Wabunge wasioafiki kwakusema: “Wale wasioafiki waseme Siyo.”

(4) Isipokuwa kama imeelekezwa vinginevyo katika Kanuni hizi,uamuzi juu ya mambo yote utapatikana kwa kufuata wingi wa sautiza Wabunge za “Ndiyo” au “Siyo” na Spika atatangaza matokeoya kura kwa kusema “Naamini Walioafiki Wameshinda” au“Naamini Wasioafiki Wameshinda.”

(5) Endapo itaonekana kuwa kuna mashaka kuhusu matokeo yakura kwa kufuata wingi wa sauti kwa mujibu wa fasili ya (4) ya Kanunihii, Spika ataruhusu muda upite ili kutoa nafasi kuhakikisha uamuziwa Bunge juu ya jambo hilo na kwa muda huo, ikiwa inaonekanakuwa kuna mashaka kuhusu matokeo ya kura, Mbunge yeyoteanaweza kusimama na kusema “Kura zihesabiwe.”

(6) Endapo hakuna Mbunge aliyeomba kura zihesabiwe, Spikaatatoa kauli ya uamuzi wa mwisho kwa kusema “WalioafikiWameshinda” au “Wasioafiki Wameshinda”, kulingana na haliitakavyokuwa.

(7) Endapo Mbunge yeyote ataomba kura zihesabiwe, basi Spikaataamuru kura zihesabiwe ikiwa Wabunge wengine kumi au zaidiwatasimama mara moja kuunga mkono maombi ya kurakuhesabiwa.

(8) Endapo Spika ataamuru kura zihesabiwe, Katibu atapigakengele ya kuwaita Wabunge kwa muda wa dakika moja na baadaya muda huo, Spika atamwagiza Katibu kumwita Mbunge mmojammoja kwa jina lake na kumuuliza anapiga kura yake upande ganina kurekodi kura hiyo.

(9) Baada ya Katibu kukamilisha shughuli ya kuhesabu kura,atamjulisha Spika kuhusu kura zote za wanaoafiki, wasioafiki nawasiokuwa na upande wowote na Spika atatangaza matokeo yahesabu hiyo ya kura.

54

(10) Orodha kamili itaandaliwa ikionyesha namna kura zilivyopigwana itarekodiwa katika Taarifa Rasmi kwa aji l i ya kuwekakumbukumbu ya uamuzi wa Bunge.

SEHEMU YA NANE

KUTUNGA SHERIA – MASHARTI YA JUMLA

80.-(1) Kila Muswada wa Sheria utatangazwa kwenye Gazeti katikamatoleo angalau mawili, kukiwa na kitambo kisichopungua sikusaba kamili kati ya toleo la kwanza na la pili.

(2) Tangazo la Kwanza la Muswada wa Sheria litatolewa na kumfikiaKatibu katika muda usiopungua siku 21 kabla ya Muswada huokusomwa Bungeni kwa Mara ya Kwanza, na litaonesha Muswadamzima, ikiwa ni pamoja na maelezo kuhusu madhumuni ya Muswadahusika yaliyotiwa saini na Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

(3) Muswada wa Serikali utahesabiwa kuwa umetangazwa maraya pili endapo itatolewa taarifa katika Gazeti inayotaja jina laMuswada, nambari na tarehe ya Gazeti ambapo Muswadaulitangazwa mara ya kwanza.

(4) Muswada wowote wa Sheria wa Serikali wa dharurahautaingizwa kwenye shughuli za Bunge bila ya kuwa na hatiiliyowekwa saini na Rais inayoeleza kuwa Muswada uliotajwa katikahati hiyo ni wa dharura.

(5) Muswada huo utawasilishwa kwanza kwenye Kamati ya Uongoziukiwa umeambatishwa na hati ya dharura ili Kamati hiyo iwezekujir idhisha iwapo Muswada husika wa sheria unastahil ikuwasilishwa kwa dharura au la.

(6) Iwapo Kamati ya Uongozi itaona kuwa Muswada wa Sheria waSerikali uliowasilishwa kwa hati ya dharura haustahili kuwasilishwakwa dharura, Kamati hiyo itaishauri Serikali ipasavyo.

(7) Haitakuwa lazima kwa Waziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikalikutoa taarifa ya Muswada wa Serikali ambao unakusudiwakuwasilishwa Bungeni iwapo Muswada huo umekwisha kutangazwakwenye Gazeti.

(8) Katibu atagawa kwa kila Mbunge nakala ya kila Muswada waSheria kama ulivyochapishwa na kutangazwa kwenye Gazeti.

Utanga-zajiwaMiswadayaSerikali

55

81.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamatiyoyote ya Kudumu ya Bunge au Mbunge yeyote anawezakuwasilisha Bungeni Muswada Binafsi wa Sheria.

(2) Taarifa ya kuwasilisha Muswada Binafsi wa Sheria na Muswadawa Sheria wa Kamati itapelekwa kwa Katibu na taarifa hiyoitaeleza jina la Muswada unaopendekezwa pamoja na madhumunina sababu zake.

(3) Baada ya taarifa kutolewa, Muswada Binafsi wa Sheria auMuswada wa Sheria wa Kamati utatangazwa katika Gazeti kamailivyo kwa Miswada ya Sheria ya Serikali, isipokuwa kwamba,madhumuni na sababu yatawekwa saini na Mwenyekiti wa Kamatiya Kudumu ya Bunge au Mbunge anayehusika.

(4) Muswada Binafsi wa Sheria utahesabiwa kuwa umetangazwamara ya pili endapo itawekwa taarifa kwenye Gazeti inayotajajina la Muswada, nambari na tarehe ya Gazeti ambapo Muswadaulitangazwa Mara ya Kwanza.

(5) Masharti kuhusu muda wa utangazaji wa Miswada ya Sheriayanaweza kuwekwa kando na kutenguliwa kwa hoja kutolewa nakuamuliwa kama kutawasilishwa Bungeni hati iliyowekwa saini natheluthi mbili ya Wajumbe wote wa Kamati kama ni Muswada waKamati na kwa Muswada wa Mbunge hati iliyowekwa saini naWabunge wasiopungua kumi inayoeleza kuwa Muswada Binafsiuliotajwa katika hati hiyo ni wa dharura.

(6) Masharti ya kujadili hoja hii yatakuwa kama yalivyo kwa upandewa Miswada ya Sheria ya Serikali.

82.-(1) Muswada wa Sheria wa Serikali utawasilishwa Bungeni naWaziri au Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

(2) Muswada Binafsi wa Sheria unaweza kuwasilishwa Bungeni naMwenyekiti wa Kamati yoyote ya Kudumu ya Bunge au Mbungeyeyote ambaye si Waziri.

83.-(1) Muswada wowote wa Sheria ambao umetangazwa kwenyeGazeti, unaweza kuwasilishwa Bungeni kufuatana na Orodha yaShughuli ili Kusomwa Mara ya Kwanza na katika hatua hiyo Katibuatasoma jina refu la Muswada wa Sheria unaohusika bila hojayoyote kutolewa kwa ajili hiyo.

Uwasi l i -shaji waMuswada

Utaratibu kuhusu Miswada Binafsi

MuswadaKusomwaMarayaKwanza

56

(2) Hakutakuwa na mjadala wowote wakati wa Muswada wa SheriaKusomwa Mara ya Kwanza.

84.-(1) Spika atapeleka Muswada wa Sheria kwenye Kamatiinayohusika na Kamati itaanza kuujadili Muswada huo mapemaiwezekanavyo

(2) Kamati iliyopelekewa Muswada itatoa matangazo au itatoabarua ya mwaliko kumwalika mtu yeyote afike kutoa maoni yakembele ya Kamati hiyo kwa lengo la kuisaidia katika uchambuzi waMuswada huo.

(3) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamatii l iyopelekewa Muswada itakuwa na uwezo wa kufanyamarekebisho katika Muswada wa Sheria kwa kumshauri Waziri auMbunge anayehusika na Muswada huo kufanya mabadiliko, vilevileSerikali itakuwa na uwezo wa kuishauri Kamati ya Kudumu ya Bungekuhusu kufanya marekebisho au mabadiliko juu ya Muswada Binafsi.

(4) Kabla Muswada wa Sheria uliofanyiwa mabadilikohaujawasilishwa Bungeni kwa ajili ya Kusomwa Mara ya Pili,utapelekwa kwenye Kamati inayohusika kwa madhumuni yakuzingatia mabadiliko hayo.

85.-(1) Kamati iliyopelekewa Muswada wa Sheria itakapokamilishakuujadili Muswada huo Mwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spikakwa maandishi kwamba, Kamati imemaliza kujadili Muswada husika.

(2) Spika ataagiza Muswada huo uwekwe kwenye Orodha yaShughuli kwa ajili ya kusomwa Mara ya Pili.

86.-(1) Siku ambayo Muswada wa Sheria uliokwisha kujadiliwa naKamati umepangwa kwenye Orodha ya Shughuli, Waziri,Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mwenyekiti wa Kamati au Mbungemwenye Muswada husika atawasilisha hoja kwamba Muswada waSheria ambao atautaja kwa jina Kusomwa Mara ya Pili.

(2) Hoja ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili itakuwakama ifuatavyo:-

“Kwamba, Muswada wa Sheria uitwao….. sasa usomwe maraya pili”. Au kadri itakavyokuwa;

Muswadakupele-kwakwenyeKamati

Taarifa ya Kamati

MuswadaKusomwaMarayaPili

57

“Kwamba, Muswada uitwao ……………… kamaulivyorekebishwa kwa mujibu wa jedwali la marekebisho au kamaulivyochapishwa upya sasa usomwe mara ya Pili.”

(3) Haitakuwa halali katika hatua hii kuleta hoja ya kufanyamabadiliko katika hoja isipokuwa tu kwamba:-

(a) mabadiliko bila kutoa sababu yanaweza kutolewakwa kusema:

“Kwamba, Muswada huu usisomwe mara ya Pilisasa na badala yake usomwe baada ya …..kuanzia …..”, na hapo muda ambao Muswadahuo unaokusudiwa kusomwa utatajwa.

(b) mabadiliko yenye kutoa sababu yanawezakutolewa kwa kusema:

“Kwamba, Bunge hili likatae Muswada huuKusomwaMara ya Pili kwa sababu zifuatazo …….”, na haposababu za kupinga Muswada Kusomwa Mara yaPili zitatajwa kwa ukamilifu.

(4) Iwapo hoja itatolewa chini ya fasili ya 3(a) na (b) ya Kanuni hii,Spika atalihoji Bunge ili kufikia uamuzi.

(5) Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa Muswada wa Sheria auMjumbe mwingine wa Kamati aliyeteuliwa kwa ajili hiyo, atatoamaoni ya Kamati kuhusu Muswada husika.

(6) Ikiwa Muswada wa Sheria unaohusika ni Muswada wa Serikali,basi Msemaji wa Kambi ya Upinzani atatoa maoni yake juu yaMuswada husika na endapo ni Muswada Binafsi au Muswada waKamati, basi msemaji wa Serikali atatoa maoni yake.

(7) Mjadala wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Piliutahusu ubora na misingi ya Muswada huo tu.

(8) Majadiliano juu ya hoja kuhusu Muswada kama yapo yatahusumaneno yanayohusiana na hoja tu.

(9) Mbunge yeyote au Waziri anaweza, wakati wa mjadala huo,kumshauri Mtoa hoja afanye mabadiliko katika Muswada, amamabadiliko ya jumla au yale atakayoyataja Mbunge.

58

(10) Katika hatua hii iwapo mtoa hoja anataka kufanyamarekebisho au mabadiliko katika Muswada wa Sheria kutokanana ushauri uliotolewa ama katika Kamati au wakati wa Muswadawa Sheria Kusomwa Mara ya Pili au kwa sababu nyingine yoyote,iwapo Muswada huo ni wa Serikali atamjulisha Mwandishi Mkuu waSheria na iwapo Muswada husika ni wa Kamati au Binafsiatamjulisha Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria iliatayarishe na kumkabidhi Katibu ambaye atagawa kwa kilaMbunge nakala ya:-

(a) Muswada wa Sheria uliochapishwa upya ukiwana marekebisho au mabadiliko yanayokusudiwakufanyika; au

(b) Jedwali la Marekebisho au mabadilikoyanayokusudiwa kufanyika.

(11) Kamati au Mbunge anaweza kuwasilisha kwa Katibu, kwamaandishi, mabadiliko anayokusudia kuyafanya katika Muswadahuo wakati wa Kamati ya Bunge Zima akionesha bayana mabadilikoyanayokusudiwa kufanyika katika kila Ibara inayohusika.

87.-(1) Endapo Muswada ulikwishasomwa mara ya Pili na haukuwana mabadiliko, lakini kuna jambo au suala jipya limetokea nalinahitaji kuzingatiwa, Mtoa hoja anaweza kumwomba Spika wakatiwowote kabla Muswada haujapelekwa katika Kamati ya BungeZima kwamba, Muswada huo urejeshwe tena kwenye Kamatiinayohusika.

(2) Endapo Muswada wa Sheria utapelekwa tena kwenye Kamatiinayohusika, Mbunge yeyote ambaye wakati wa Muswada waSheria Kusomwa Mara ya Pili alimwomba mtoa hoja kufanyamabadiliko katika Muswada huo, anaweza kuhudhuria mkutano waKamati na kushiriki katika majadiliano, isipokuwa kwamba, Mbungehuyo hatakuwa na haki ya kupiga kura kuhusu uamuzi wowote waKamati hiyo.

(3) Kamati itakutana mapema iwezekanavyo ili kujadili mabadilikoyaliyopendekezwa.

(4) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba, Kamatiinayohusika itakuwa na mamlaka ya kufanya mabadiliko katikaMuswada uliopelekwa kwake kwa mujibu wa Kanuni hii kwa:-

Kureje-shaMuswadakatika Kamati

59

(a) kumshauri Waziri, Kamati au Mbunge anayehusikana Muswada kufanya mabadiliko katika Muswadahuo; au

(b) kupitisha Azimio la kutoa Bungeni, taarifa maalumukuhusu Muswada huo.

(5) Baada ya Kamati kukamilisha kuujadili Muswada kwa mara yapili, Muswada huo utapelekwa katika Kamati ya Bunge Zima.

(6) Endapo Kamati iliyojadili Muswada kwa mara ya pili itaazimiakuwa taarifa maalumu juu ya Muswada huo itolewe Bungeni, basiMwenyekiti wa Kamati atamjulisha Spika na taarifa hiyo itatolewana Mwenyekiti au Mjumbe mwingine wa Kamati kwa niaba yaMwenyekiti, kabla Muswada huo haujawasilishwa katika Kamati yaBunge Zima.

88.-(1) Mtoa hoja au Mbunge mwingine anayekusudia kuwasilishamabadiliko katika Muswada unaojadiliwa, anaweza kumwombaSpika kwamba, hatua ya kuingia katika Kamati ya Bunge Zimaiahirishwe hadi wakati atakaoutaja katika ombi lake na Spikaatatoa uamuzi wake kadri atakavyoona inafaa.

(2) Mabadiliko yote yaliyopendekezwa kufanyika katika Muswadawa Sheria sharti yawekwe katika Jedwali la Mabadilikolitakaloandaliwa kwa ajili hiyo na kugawiwa kwa Wabunge nakatika kujadili na ama kuyapitisha au kutoyapitisha, vyovyoteitakavyokuwa, mabadiliko hayo yatashughulikiwa kwa mpangilioutakaofuata na kwa kuzingatia mtiririko wa Ibara za Muswada waSheria unaohusika.

(3) Kwa madhumuni ya Bunge kujadili na ama kupitisha aukutopitisha, mabadiliko yaliyopendekezwa, Mtoa hoja atapewafursa ya kwanza kueleza mapendekezo yake kabla ya mabadilikomengine yatakayokuwa yamependekezwa na Wabunge wengine.

(4) Mabadiliko yoyote yaliyopendekezwa kufanyika katikaMuswada wa Sheria na kuwekwa katika Jedwali la Mabadilikohayataondolewa na Mtoa hoja, isipokuwa tu kwa idhini ya Spika.

(5) Mtoa hoja anayependekeza mabadiliko kufanywa katikaMuswada wa Sheria atawasilisha hoja yake ya mabadiliko hayokwa muda wa dakika tano.

Muswadakatika KamatiyaBunge Zima

60

(6) Endapo kuna mabadiliko mengine yamependekezwa kufanyikakatika Jedwali la Mabadiliko, basi mabadiliko hayoyaliyopendekezwa awali na ambayo yamo katika Jedwali laMabadiliko hayatahesabiwa kwamba yameondolewa hadimajadiliano juu ya mabadiliko hayo yatakapokuwa yamefikiamwisho au Waziri, Kamati ya Bunge au Mbunge aliyetoamapendekezo yaliyomo katika Jedwali la Mabadilikoatakapoomba kwa Spika mapendekezo yake yaondolewe.

(7) Mtoa hoja aliyependekeza mabadiliko yoyote kufanyika katikaMuswada wa Sheria na mapendekezo hayo kuwekwa katika Jedwalila mabadiliko atapewa nafasi ya kuwasilisha na kufunga hoja yakeya mabadiliko.

(8) Baada ya Mtoa hoja kuhitimisha hoja yake ya mabadiliko, Spikaatalihoji Bunge ili kupata uamuzi kuhusu hoja hiyo ya mabadiliko.

(9) Muda wa kusema katika Kamati ya Bunge Zima kwa wachangiajimbalimbali wanaounga mkono hoja ya kufanya mabadilikoutakuwa dakika tatu.

(10) Kamati ya Bunge Zima itajadili na kupitisha au kufanyamabadiliko na kupitisha Muswada wa Sheria Ibara moja baada yaIbara nyingine, isipokuwa kwamba, Mwenyekiti, akiona inafaa,anaweza kuihoji Kamati itoe uamuzi wake kwa sehemu moja yenyeIbara kadhaa au Ibara zote zilizomo katika sehemu moja yaMuswada.

89.-(1) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi ya kupitiaMuswada wa Sheria, Bunge litarejea na Mtoa hoja atatoa taarifaBungeni kwa maneno yafuatayo:-

“Kamati ya Bunge Zima imeupitia Muswada wa Sheria, Ibarakwa Ibara na kuukubali bila mabadiliko, naomba kutoa hoja.” au kama kuna mabadiliko yaliyofanywa kwa manenoyafuatayo:-

“Kamati ya Bunge Zima imeupitia Muswada wa Sheria,Ibara kwa Ibara na imeukubali pamoja na marekebishoyaliyofanyika, naomba kutoa hoja” na kisha atatoa hoja:

“Kwamba, Muswada wa Sheria wa ……………… sasaukubaliwe”.

Taarifa baada ya Muswada KusomwaMara ya Pili

61

au kama kuna mabadiliko yaliyofanywa katika Muswada kwamaneno yafuatayo:- “Kwamba, Muswada wa Sheria wa …. Kama ulivyorekebishwaau kubadilishwa katika Kamati ya Bunge zima, sasa ukubaliwe.”

(2) Hoja ya kupitisha Muswada wa Sheria wa mabadiliko ya Katibaitaamuliwa kwa mujibu wa Ibara ya 98 ya Katiba. Kwa sababu hiyo,kura zitapigwa kwa kuita jina la Mbunge mmoja mmoja katika hatuaya Muswada huo Kusomwa Mara ya Pili.

90.- Mtoa hoja anayewasilisha Muswada wa Sheria anawezakuuondoa Muswada wakati wowote kabla ya Bunge kuhojiwakutoa uamuzi wake, baada ya kutoa taarifa kwa Spika.

91.- Baada ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Tatu,utahesabika kuwa umepitishwa na Bunge.

92.-(1) Muswada kama ulivyopitishwa na Bunge, utatayarishwachini ya uangalizi na usimamizi wa Katibu kwa kuingiza mabadilikoyote yaliyofanyika na atawasilisha nakala moja ya Muswada huokwa Rais mapema ili Rais atoe kibali chake kwa mujibu wa Ibara ya97 (1) ya Katiba na pia nakala moja kwa Spika kwa taarifa.

(2) Nakala halisi ya Sheria iliyopata kibali cha Rais itahifadhiwa naKatibu.

93.-(1) Bunge halitashughulikia hatua zaidi ya moja kwa Muswadawowote wa Sheria katika Mkutano mmoja wa Bunge.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Bungelinaweza kushughulikia Muswada wa Sheria katika hatua zaidi yamoja endapo:-

(a) hoja mahususi itatolewa kwamba Muswadahuo ushughulikiwe katika hatua zaidi ya moja;

(b) Spika ataridhika na hoja hiyo; na

(c) Bunge litaafiki hoja hiyo kwa kupiga kura.

UtaratibuwaKusomaMiswadayaSheria

KuondoaMuswadaBungeni

MuswadaKusomwaMaraya Tatunakupitishwana Bunge

Ridhaaya Rais na hifadhiyaSheria

62

(3) Masharti ya Fasili ya (1) ya Kanuni hii hayatatumika kwaMuswada wa Sheria ya Fedha, Muswada wa Matumizi ya Fedha naMuswada wowote unaowasilishwa kwa hati ya dharura.

SEHEMU YA TISA

UTARATIBU WA KUTUNGA SHERIAKUHUSU MAMBO YA FEDHA

94. Ili kutekeleza majukumu yaliyoainishwa katika Ibara ya 63(3)(c)ya Katiba, Bunge litakaa kama Kamati ya Mipango katika Mkutanowake wa mwezi wa Februari il i kujadili na kushauri kuhusumapendekezo ya mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa naSerikali katika mwaka wa fedha unaofuata.

95.- Bunge halitashughulikia Muswada, hoja au ombi lolote endapoMwanasheria Mkuu wa Serikali atathibitisha kwamba, matokeo yaMuswada, hoja au ombi hilo yatakuwa ni:-

(a) kuweka masharti yanayoanzisha au kuongezakodi yoyote au yanayoweza kuongeza kiwango chamatumizi ya fedha zitakazotolewa kutoka katikaMfuko Mkuu wa Hazina ya Jamhuri ya Muunganoau yanayofuta au kupunguza deni lolotelinalodaiwa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;au

(b) kubadilisha mishahara, marupurupu au mashartiya utumishi, ikiwa ni pamoja na likizo, usafirina kupandishwa cheo kwa mtumishi yeyote waumma au kufanya mabadiliko katika Sheria,Kanuni au taratibu zinazohusu pensheni, kiinuamgongo au marupurupu mengineyo ya mtumishiwa umma au ya mjane, watoto wanaomtegemeaau wawakilishi wake.

96.-(1) Waziri atapeleka kwa Katibu Makadirio ya Matumizi yaKawaida na ya Maendeleo ya Serikali ya Mwaka wa Fedhaunaohusika na nakala ya Makadirio hayo itapelekwa na kumfikiakila Mbunge angalau siku ishirini na moja kabla ya Mkutano ambaoutashughulikia Makadirio hayo.

(2) Makadirio ya Fedha za Matumizi ya Serikali yatawasilishwaBungeni na Waziri wa Fedha kwa Hotuba kuhusu Makadirio hayo

Mashartikuhusu Miswada,Hoja na Maombi ya Fedha

Bunge kukaa kamaKamati ya Mipango

K u w a s i -lishaMakadirioyaM a p a t onaMatumiziyaFedha za Serikali

63

itakayoitwa Hotuba ya Bajeti ambayo itatolewa kabla ya tarehe20 ya mwezi Juni kwa kila mwaka.

(3) Muda wa kusoma Hotuba ya Bajeti utaamuliwa na Spika kadriatakavyoona inafaa.

(4) Hoja ya kuwasilisha Makadirio hayo itakuwa katika manenoyafuatayo; “Kwamba Bunge likubali kupitisha Makadirio ya Mapato naMatumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha wa….”

(5) Siku ya kuwasilisha Bungeni Hotuba ya Bajeti, nafasi piaitatolewa kwa Waziri anayehusika na mipango au uchumi kutoamaelezo kuhusu hali ya uchumi kwa ujumla.

(6) Hotuba ya Bajeti na ya Waziri anayehusika na Mipangozitafuatiwa na hotuba za Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu yaBunge inayohusika na masuala ya fedha na uchumi na Msemaji waKambi ya Upinzani.

(7) Muda wa kusoma maoni ya Kamati na ya Kambi ya Upinzaniutakuwa dakika zisizozidi thelathini kwa kila hotuba.

97.-(1) Mjadala kuhusu Hotuba ya Bajeti utaendelea kwa sikuzisizozidi tano ambapo dakika zisizozidi kumi na tano zitatolewakwa kila Mbunge anayetaka kuchangia Hotuba ya Bajeti.

(2) Katika hatua hii majadiliano yatahusu mambo ya jumla kuhusianana hali ya uchumi na Mbunge yeyote hataruhusiwa kupendekezamabadiliko katika Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali.

98.-(1) Mjadala juu ya Hotuba ya Bajeti utakapomalizika, Spikaatalihoji Bunge litoe uamuzi wake wa kupitisha au kutokupitishaBajeti ya Serikali ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 90(2)(b) ya Katiba.

(2) Uamuzi wa Bunge wa kupitisha au kutokupitisha Bajeti ya Serikaliutafanywa kwa kupiga kura ya wazi kwa kuita jina la Mbunge mmojammoja.

99.-(1) Jumla ya siku zisizozidi hamsini zitatengwa kwa ajili ya Bungekujadili utekelezaji wa Wizara zote kwa mujibu wa Ibara ya 63(3)(b)ya Katiba.

MjadalakuhusuHotubayaBajeti

UtaratibuwakuidhinishaMakadirioyaMatumiziyaSerikali

Kujadiliutekele-zaji waBajeti zaWizara

64

(2) Shughuli za Bajeti ya Serikali zitapewa nafasi ya kwanza kablaya shughuli nyingine yoyote, na zitawekwa kwanza kwenye Orodhaya Shughuli za Kikao kila siku hadi pale zitakapokuwa zimemalizika,isipokuwa kama Bunge litaamua vinginevyo.

(3) Asubuhi ya siku ambayo Waziri amepangiwa kuwasilisha hojaya Makadirio ya Wizara yake, Waziri huyo, Mwenyekiti wa Kamatiinayohusika au Mjumbe yeyote atakayeteuliwa kwa niaba yake,na Msemaji wa Kambi ya Upinzani kwa Wizara husika watawasilishaMezani nakala ya taarifa zao kwa kuzingatia mpangilio wa Shughuliza Bunge.

(4) Pamoja na kuwasilisha mezani nakala ya hotuba ya hoja yaMakadirio ya Wizara yake, Waziri mhusika atawasilisha pia randamaya makadirio hayo, siku moja kabla ya siku ambayo hotuba yakeimepangwa kutolewa Bungeni.

(5) Wakati utakapofika wa kuwasil isha taarifa ya Wizarainayohusika, hoja itatolewa kwa maneno yafuatayo:- “Kwamba sasa Bunge likubali kujadili na kupitisha Makadirio yaMatumizi ya Wizara yangu.”

(6) Isipokuwa kwa Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, mudawa Waziri anayewasilisha Hotuba ya Makadirio ya Wizara yakeutakuwa ni dakika zisizozidi sitini.

(7) Waziri atafuatiwa na Mwenyekiti wa Kamati iliyopitia Makadiriohusika na Msemaji wa Kambi ya Upinzani ambao watatoa maoniyao kwa muda usiozidi dakika thelathini kila mmoja.

(8) Mbunge anayejadili Makadirio ya Matumizi ya Wizarambalimbali ataruhusiwa kusema kwa muda usiozidi dakika kumi natano.

(9) Endapo Spika ataona kuwa muda uliotengwa kwa ajili ya kujadiliBajeti ya Wizara inayohusika umekaribia kwisha, atafunga mjadalaili kumpatia Waziri mtoa hoja nafasi ya kujibu ndani ya muda wadakika sitini.

100.-(1) Mjadala wa jumla kuhusu Makadirio ya Matumizi kwaWizara utakapomalizika Bunge litaingia katika Kamati ya Matumiziili kupitisha Makadirio ya Wizara husika kifungu kwa kifungu.

Kamati ya Matumizi

65

101.-(1)Katika Kamati ya Matumizi, Mwenyekiti atawahoji Wajumbekuhusu kifungu kimoja kimoja cha Makadirio ya Matumizi ya Mwakana kila kifungu kitaafikiwa peke yake.

(2) Mbunge yeyote anaweza kuomba ufafanuzi au maelezo zaidikatika Kifungu chochote cha Fungu linalohusika, wakati Kifunguhicho kitakapofikiwa na Kamati ya Matumizi.

(3) Mbunge atakayeamua kutumia kifungu chenye mshahara waWaziri, ataruhusiwa tu iwapo ataomba ufafanuzi wa suala mahususila sera na hatazungumzia zaidi ya mambo mawili ya aina hiyo.

(4) Kwa idhini ya Mwenyekiti, Mbunge anayetaka ufafanuzi anawezakuzungumza si zaidi ya mara mbili juu ya suala hilo.

(5) Muda wa kusema katika Kamati ya Matumizi kwa ajili ya kutoaufafanuzi hautazidi dakika tano.

102.-(1) Katika Kamati ya Matumizi Mbunge yeyote anaweza kutoahoja ya kutaka kufanya mabadiliko katika Makadirio ya Matumiziya Serikali iwapo mabadiliko hayo hayatabadili madhumuni yaFungu au sehemu yoyote ya Fungu husika.

(2) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kupunguza kifungu fulanikatika Fungu lolote haijapitishwa, hoja nyingine bado inawezakutolewa kwa madhumuni ya kupunguza kifungu kingine cha Funguhilo hilo.

103.-(1) Kwa kuzingatia utaratibu wa majadiliano uliowekwa naKanuni hizi, Mbunge yeyote anaweza kuomba ufafanuzi au maelezozaidi katika Kifungu chochote cha Fungu linalohusika, wakatiKifungu hicho kitakapofikiwa na Kamati ya Matumizi.

(2) Vilevile Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja ya kuondoa shilingimoja katika kifungu chochote cha Fungu hilo.

(3) Madhumuni halisi ya hoja ya aina hiyo ni kumwezesha Mbungealiyeitoa aweze kueleza kutoridhika kwake na utekelezaji wa jambofulani mahususi ambalo dhahiri linahusika na kifungu hicho.

(4) Hoja ya aina hiyo itatolewa kwa muda wa dakika tano.

Kubadili-shaMakadirioyaMatumizikatikaKamatiyaMatumizi

MjadalakatikaKamatiyaMatumzi

HojayakuondoashilingikwenyeMakadirio

66

(5) Wabunge wanaweza kuchangia hoja ya kuondoa shilingi mojailiyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) kwa muda usiozidi dakikatatu kila mmoja.

(6) Waziri anayehusika atapewa nafasi ya kutoa majibu ya hojahiyo.

(7) Mbunge aliyetoa hoja ya kuondoa shilingi ndiye atakayefungamjadala wa hoja hiyo.

(8) Endapo Mbunge atashikilia hoja yake ya kuondoa shilingi mojakatika kifungu hicho, basi kura itapigwa.

(9) Endapo hoja ya kuondoa shilingi moja katika kifungu chochoteitakubaliwa, basi kifungu hicho kitakuwa kimepitishwa kikiwapungufu ya hiyo shilingi moja.

(10) Endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kuondoa shilingi mojakatika kifungu chochote cha Fungu linalohusika imekataliwa, hojanyingine yenye madhumuni ya kuondoa shilingi moja katika Kifungukingine cha Fungu hilo hilo bado inaweza kutolewa.

104.-(1) Iwapo zimesalia dakika kumi kabla ya kufikia muda wakuahirisha kikao cha Bunge na Kamati ya Matumizi bado haijamalizakupitisha mafungu, Mwenyekiti anaweza kuongeza muda usiozididakika thelathini bila kuihoji Kamati ili kumaliza shughuli ya kupitishamafungu yaliyobakia.

(2) Baada ya Kamati ya Matumizi kumaliza kupitisha Makadirio yaMatumizi ya Wizara inayohusika na Bunge kurudia, Waziri mtoa hojaatatoa taarifa kwamba:-

(a) “Mheshimiwa Spika, Bunge lako likikaa kamaKamati ya Matumizi limekamilisha kazi zake”; nakuomba kwamba:

(b) “taarifa ya Kamati ya Matumizi ikubaliwe naBunge”; na atamaliza kwa kusema: “naombakutoa hoja.”

(3) Spika atawahoji Wabunge kwa kuuliza, “Wanaoafiki wasemendiyo” na “Wasioafiki waseme siyo.”

KukamilikamjadalakatikaKamatiyaMatumizi

67

105.-(1) Baada ya Bunge kukamilisha kazi ya kujadili na kupitishaMakadirio ya Matumizi ya Wizara zote kwa mwaka unaohusika,Muswada wa Fedha za Matumizi utawasilishwa Bungeni nakupitishwa mfululizo katika hatua zake zote.

(2) Kwa madhumuni ya Kanuni hii, “Muswada wa Fedha za Matumizi”maana yake ni Muswada wa Sheria wenye Makadirio ya Mapatona Matumizi ya Fedha za Serikali kwa Mwaka wa Fedha unaofuatia.

(3) Muswada wa Fedha za Matumizi hautapelekwa kwenyeKamati yoyote ya Kudumu wala Kamati ya Bunge Zima, na mashartikuhusu Miswada Kusomwa Mara ya Kwanza hayatatumika.

(4) Muswada wa Fedha za Matumizi hautatangazwa kwenye Gazetikabla haujawasilishwa Bungeni.

106. Baada ya Bunge kukamilisha kazi ya kupitisha Muswada waFedha za Matumizi, Muswada wa Sheria ya Fedha utajadiliwa nakupitishwa kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na Sehemu yaNane ya Kanuni hizi.

107. Mapendekezo yoyote kwa ajili ya Matumizi ya Nyongeza yaFedha za Serikali au kwa ajili ya kutoa fedha yoyote ya nyongezazaidi ya Fedha za Matumizi ya Mwaka huo:-

(a) yataitwa Makadirio ya Nyongeza ya Matumizi;

(b) yatapelekwa kwenye Kamati ya Matumizikufuatana na masharti ya Ibara ya 99 ya Katiba;na

(c) yatafuata masharti ya Kanuni zote zinazohusuMakadirio ya Mwaka ya Matumizi ya Serikali.

SEHEMU YA KUMI

KAMATI ZA BUNGE

108.-(1) Kutakuwa na Mkutano wa Wabunge wote ambao unawezakuitishwa na Spika siku moja kabla au wakati wa Mkutano wowotewa Bunge.

(2) Mkutano wa Wabunge wote utajadili masuala yote yenyemaslahi kwa Wabunge na utaipa Serikali fursa ya kutoa taarifambalimbali kwa Wabunge kuhusu hali ya nchi kwa ujumla.

MuswadawaSheriayaFedha

MakadirioyaMatumiziyaNyongeza

MuswadawaFedhazaMatumizi

MkutanowaWabungewote

68

(3) Mwenyekiti wa Kikao cha Mkutano wa Wabunge wote atakuwaKiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni.

109.-(1) Wabunge wa kila Chama cha Siasa kinachowakilishwaBungeni wanaweza kuunda Kamati ya Wabunge wa Chama kwakuzingatia Katiba, Kanuni na Taratibu za Chama kinachohusika.

(2) Endapo makubaliano yamefikiwa baina ya Vyama viwili auzaidi vya Upinzani vyenye idadi sawa ya Wabunge ambao ni zaidiya asilimia kumi na mbili na nusu basi Wabunge wa Kambi yaUpinzani wanaweza kuunda Kamati ya Wabunge wote wa Kambihiyo.

110.-(1) Kamati za Vyama vya Siasa Bungeni zitajiwekea utaratibukwa ajili ya uendeshaji wa shughuli.

(2) Majadiliano yote kwenye mikutano ya Kamati pamoja namambo mengine yote yanayohusu Kamati hizo yatakuwa na hadhi,kinga na nafuu zote zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria kuhusumajadiliano, kumbukumbu na mambo mengineyo ya Bunge navikao vyake kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 100 (1) na (2) yaKatiba na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge.

111. Kwa kufuata yaliyomo kwenye Orodha ya Shughuli au kwamujibu wa Kanuni hizi, ukifika wakati wa Bunge au Bunge likihitajiwakuingia katika Kamati ya Bunge Zima, Spika ataondoka kwenye Kitichake bila hoja yoyote kutolewa.

112.-(1) Masharti ya Kanuni ya 77 yatatumika kuhusu Kamati yaBunge Zima, ila tu kama idadi ya Wabunge waliohudhuria itakuwabado haifikii nusu ya Wabunge wote baada ya kipindi kilichowekwana Kanuni ya 77(3), Mwenyekiti ataondoka kwenye Kiti, Bungelitarudia na Katibu atahesabu idadi ya Wabunge waliohudhuria nakama idadi yao itakuwa bado haifikii nusu ya Wabunge wote, basiSpika ataahirisha Bunge.

(2) Kanuni za Bunge zinazohusu mwenendo wa Bunge zitatumikakatika Kamati ya Bunge Zima isipokuwa kwamba katika Kamati hiyo:-

(a) hoja ikitolewa haitahitaji kuungwa mkono;

(b) Kwa idhini ya Mwenyekiti, Mjumbe anayetakaufafanuzi anaweza kuzungumza mara mbili juu yasuala hilo.

MikutanoyaKamatiza VyamavyaSiasa

KamatiyaBungeZima

KamatizaVyamavyaSiasa

Akidi naUtaratibukatikaKamatiyaBungeZima

69

(3) Mjumbe yeyote anaweza kuchangia katika hoja ya kutakaufafanuzi iliyoanzishwa kwa mujibu wa fasili ya (2) (b).

(4) Muda wa kusema katika kuchangia hoja ya ufafanuzi hautazididakika tano.

(5) Mjumbe yeyote anayetaka kutoa hoja kwamba majadiliano yaKamati ya Bunge Zima yaahirishwe mpaka wakati mwingine,anaweza kutoa hoja hiyo wakati wowote, kwa maneno yafuatayo:

“Kwamba Waziri au Mbunge atoe taarifa kwa Bunge juu yamaendeleo ya kazi ya Kamati hii na kuomba ruhusa Kamati hiiikutane tena baadae.”

(6) Bunge litakaporudia, Waziri au Mbunge aliyehusika na shughulizilizokuwa zikifanywa na Kamati atasimama mahali pake na kuliarifuBunge kwamba Kamati imeshughulikia maendeleo lakinihaikukamilisha kazi yake.

(7) Mara tu baada ya Waziri au Mbunge aliyehusika na shughulizilizokuwa zikifanywa na Kamati kuliarifu Bunge kutokamilika kwakazi yake, Spika atalitaarifu Bunge siku na wakati ambapo Kamatiitaendelea na kazi yake.

(8) Kamati ya Bunge Zima itafikiria mambo yale tu yatakayopelekwana Bunge kwenye Kamati hiyo.

(9) Kamati ya Bunge Zima, inaweza kuamua, baada ya hojakutolewa kwamba shughuli iliyo mbele yake wakati huo irudishweau ipelekwe kwenye Kamati ya Kudumu inayohusika.

(10) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha shughuli zake,Mwenyekiti ataondoka kwenye Kiti na kurejea kwenye Kiti cha Spikaambapo Bunge litarudia.

113.-(1) Mbunge yeyote ambaye si Waziri au Mwanasheria Mkuuwa Serikali anaweza kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumuya Bunge yoyote ambayo inahusika na Kanuni hii na Waziri mwenyedhamana ya jambo lolote linalopelekwa au kujadiliwa na Kamati,pamoja na Naibu Waziri aliyeteuliwa kumsaidia Waziri huyo,watakuwa wajumbe wa Kamati wakati Kamati itakapokuwainashughulikia jambo hilo.

(2) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Mbunge

MuundowaKamatizaKudumuzaBunge

70

yeyote ambaye ni Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilayahatachaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Hesabu za Serikali,Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa na Kamati ya Hesabu zaMashirika ya Umma.

(3) Wajumbe wa Kamati zote watateuliwa na Spika kwa namnaambayo itawezesha kila Mbunge kuwekwa kwenye Kamatimojawapo.

(4) Wajumbe walioteuliwa kwenye Kamati ya Kanuni za Bunge,Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Kamati yaMasuala ya Ukimwi, wanaweza pia kuteuliwa kwenye Kamatinyingine.

(5) Wakati wa kuteua Wabunge kuwa Wajumbe wa Kamatimbalimbali, Spika:-

(a) atateua idadi ya Wabunge inayolingana kwakila Kamati, isipokuwa kama imeelekezwavinginevyo katika Kanuni hizi;

(b) atazingatia aina zote za Wabunge na kuwateuaWabunge wa aina mbalimbali kwa kila Kamati,akiongozwa na kigezo cha asilimia ya kila ainaya Wabunge hao ilivyo Bungeni;

(c) kwa kadri inavyowezekana, atayapa kipaumbelematakwa ya Wabunge wenyewe, lakinihatalazimika kutosheleza kila takwa au ombi;

(d) atazingatia haja kwa kila Kamati kuwa naWabunge wenye uzoefu au ujuzi maalumu kuhusukazi za Kamati hiyo.

(6) Katibu atahakikisha kuwa Wabunge wote wanapewa orodhainayoonesha jinsi walivyoteuliwa katika Kamati mbalimbali.

(7) Ujumbe katika Kamati za Kudumu za Bunge utadumu mpakamwisho wa Mkutano wa Kumi wa Bunge ambao ni nusu ya kwanzaya maisha ya Bunge.

(8) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (7) ya Kanuni hii, Mbungeyeyote anaweza kuteuliwa tena katika Kamati aliyokuwaanaitumikia katika nusu ya kwanza ya maisha ya Bunge.

71

(9) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (7) ya Kanuni hii, Mbungeatakoma kuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge endapoatateuliwa kuwa Waziri au kuchaguliwa kuwa Spika au Naibu Spika.

(10) Wajumbe wa kila Kamati watawachagua Mwenyekiti naMakamu Mwenyekiti kutoka miongoni mwao ambao kwa mudawote watakaokuwa Wabunge, wataendelea kushika nafasi hizompaka mwisho wa kipindi kilichotajwa katika fasili ya (7) ya Kanunihii, lakini wanaweza kuchaguliwa tena.

(11) Wenyeviti wa Kamati za Bunge zinazosimamia matumizi yafedha za Umma ambazo ni Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati yaHesabu za Serikali za Mitaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika yaUmma watachaguliwa kutoka miongoni mwa Wajumbe wa Kamatihizo ambao wanatoka katika Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

114.-(1) Masharti ya Kanuni hii yatatumika kwa Kamati zote zakudumu.

(2) Mwenyekiti ataongoza vikao vyote vya Kamati na endapoMwenyekiti hayupo kwenye kikao, Makamu Mwenyekiti ataongozashughuli za kikao hicho na ikiwa Mwenyekiti na Makamu wake wotehawapo, wajumbe waliohudhuria watamchagua mmojawapomiongoni mwao kuongoza kikao hicho.

(3) Kamati ya Kudumu itakutana kila inapoitwa na Spika, NaibuSpika au na Mwenyekiti wake baada ya kupata idhini ya Spika.

(4) Mikutano ya kawaida ya Kamati za Kudumu itafanyika Dodoma,Dar es Salaam au Zanzibar.

(5) Kila Kamati itafanya vikao vyake kwa kuzingatia bajeti yaKamati husika ambayo imeidhinishwa kwa mwaka huo wa fedha.

(6) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati ya Kudumu itakuwatheluthi moja ya Wajumbe wote wa Kamati.

(7) Mambo yote yatakayojadiliwa na Kamati yataamuliwa kwakufuata maoni ya walio wengi kati ya Wajumbe wa Kamatiwaliohudhuria na kupiga kura.

(8) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, kila Kamatiitajiwekea utaratibu wake, na Kamati inaweza kuwaruhusuWabunge ambao si Wajumbe wa Kamati au watu ambao si

UtaratibukatikaKamatizakudumuzaBunge

72

Wabunge kuhudhuria na kushiriki katika shughuli za Kamati, lakinihawatakuwa na haki ya kupiga kura.

(9) Shughuli za kawaida za Kamati zitaendeshwa kwa uwaziambapo Kamati itaalika wadau ili kupata maoni na ushauri waokwa ajili ya kuboresha Muswada au jambo ambalo litakuwalinashughulikiwa na Kamati hiyo.

(10) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (9) ya Kanuni hii, shughuli zoteza Kamati zinazohusu kuandaa na kutoa mapendekezo yakuwasilishwa Bungeni zitafanywa kwa faragha.

(11) Maoni ya Kamati yatakuwa ni yale yaliyokubaliwa na wajumbewalio wengi na kuwasilishwa Bungeni na Mwenyekiti au Mjumbemwingine.

(12) Mjumbe yeyote wa Kamati hataruhusiwa kuzungumziahadharani maoni ya Kamati kuhusu Muswada au jambo lolotelitakalokuwa linashughulikiwa na Kamati kabla maoni hayohayajawasilishwa rasmi Bungeni.

(13) Mwanasheria Mkuu wa Serikali na au mwakilishi wake,atahudhuria kila mkutano wa kila Kamati ya Kudumu inapokuwainachambua Muswada wa Sheria.

(14) Kamati yoyote ambayo Spika atapeleka kwake kwanzaMuswada au jambo lingine lolote, itahesabiwa kuwa ndiyo Kamatiinayohusika kushughulikia Muswada huo au jambo hilo.

(15) Itakuwa ni lazima kwa kila Kamati ya Kudumu ya Bungekuwasilisha Bungeni taarifa ya mwaka ya shughuli zake kwamadhumuni ya kujadiliwa katika Mkutano wa mwisho kabla yaMkutano wa Bajeti.

(16) Taarifa ya Kamati inapowasilishwa Bungeni, itashughulikiwakwa kufuata mpangilio wa Shughuli za Bunge.

(17) Spika ataweka utaratibu wa kujadili taarifa za Kamati naendapo Kamati yoyote katika kutekeleza majukumu yake, itaonakuwa kuna mambo ya utekelezaji ambayo yanahitaji kurekebishwa,inaweza kutoa taarifa maalumu ya ushauri kwa Waziri mwenyedhamana juu ya mambo hayo ili Waziri aweze kuchukua hatuazinazostahili.

73

(18) Kamati yoyote inaweza kuunda Kamati Ndogo kwa ajili yautekelezaji bora wa Shughuli zake, kadri itakavyoona inafaa nakila Kamati Ndogo itapangiwa kazi zake na Kamati ya Kudumuinayohusika.

(19) Mjumbe wa Kamati yoyote hataruhusiwa kuzungumzia aukushughulikia jambo lolote lililofikishwa katika Kamati iwapo anamaslahi binafsi katika jambo hilo au idara hiyo isipokuwa anawezakufanya hivyo baada ya kutaja jinsi anavyohusika na kiwango chamaslahi hayo.

115.-(1) Kutakuwa na Kamati za Kudumu za Bunge kamazilivyoainishwa kwenye Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.

(2) Muundo na majukumu ya Kamati za Kudumu za Bungeyameainishwa kwenye Nyongeza ya Nane ya Kanuni hizi.

116. Mbali na majukumu ya msingi ambayo yameorodheshwa kwakila Kamati ya Kudumu, Kamati yoyote inaweza kupendekeza kwaSpika ipewe majukumu ya nyongeza ambayo yatatajwa katikapendekezo hilo na vilevile Spika anaweza kukabidhi jambo linginelolote kwa Kamati yoyote kadri atakavyoona inafaa, kwa ajili yakushughulikiwa na Kamati hiyo.

117.-(1) Kamati Teule inaweza kuundwa na Bunge kwa madhumunimaalumu kwa hoja mahsusi itakayotolewa na kuafikiwa.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, baada yakujadili hoja yoyote, Bunge linaweza kuunda Kamati Teule kwamadhumuni ya kushughulikia jambo lolote lililotokana na hoja hiyokwa utaratibu ufuatao:-

(a) Baada ya hoja iliyokuwa ikijadiliwa kuamuliwa,Mbunge yeyote mwenye nia ya kutoa hoja chiniya Kanuni hii anaweza kusimama mahali pake nakutoa taarifa ya mdomo kwamba anakusudiakutoa hoja ya kuunda Kamati Teule;

(b) Mbunge ambaye anakusudia kutoa hoja yakuunda Kamati Teule atawasilisha taarifa ya hoja

KamatizaKudumuzaBunge

Majukumuya jumlayaKamatizaKudumuza Bunge

UtaratibuwaKuundaKamatiTeule

74

yake kwa maandishi kwa Katibu na hoja hiyoitashughulikiwa wakati unaofaa kwa kuzingatiampangilio wa shughuli kama ulivyoainishwa chiniya Kanuni ya 30 (4).

(3) Bunge litapeleka jambo linalotokana na hoja iliyokuwaikijadiliwa Bungeni kwenye Kamati Teule.

(4) Wajumbe wa Kamati Teule watateuliwa na Spika nawatamchagua Mwenyekiti wa Kamati hiyo kutoka miongoni mwao.

118.- (1) Kila Kamati Teule itakuwa na Wajumbe wasiozidi watano.

(2) Akidi ya vikao vya Kamati Teule itakuwa ni theluthi mbili yawajumbe wake.

(3) Kamati Teule itafanya kikao chake cha kwanza mahali na saaatakayoamua Mwenyekiti na vikao vinginevyo vitafanyika kwawakati na mahali popote itakapoamua.

(4) Mwenyekiti ataongoza vikao vyote vya Kamati Teule, na iwapoMwenyekiti hayupo katika kikao chochote, Wajumbe waliohudhuriawatamteua mmoja wao kuwa Mwenyekiti wa kikao hicho.

(5) Endapo kwa sababu yoyote Mjumbe yeyote wa Kamati Teuleatashindwa kufanya kazi yake, Spika atamteua Mbunge mwinginekushika nafasi yake.

(6) Majadiliano ya Kamati Teule yatahusu tu mambo yaliyopelekwakwake na Bunge na yatakuwa ya wazi au siri kufuatana na Kamatiitakavyoamua kulingana na masuala husika.

119.-(1) Kamati Teule itatoa taarifa Bungeni kuhusu maoni nauchunguzi wake pamoja na kumbukumbu za ushahidi uliopokelewana vilevile inaweza kutoa taarifa maalumu juu ya mambo yoyoteambayo itaona yanafaa kuwasilishwa Bungeni.

(2) Taarifa ya Kamati Teule itawasilishwa Bungeni na Mwenyekiti. (3) Iwapo baada ya hoja kutolewa, Bunge litaamua kujadili taarifahiyo, hoja itakayotolewa Bungeni itakuwa ni kwa madhumuni yakuliomba Bunge likubali mapendekezo yaliyomo katika taarifa hiyo.

AkidinautaratibuwaVikaovyaKamatiTeule

TaarifayaKamatiTeule

75

(4) Bunge linaweza kuamua vinginevyo kwa kutumia utaratibu wakubadilisha hoja ambao umeelezwa katika Kanuni ya 57 ya Kanunihizi.

(5) Katibu wa Kamati Teule ataweka kumbukumbu zinazooneshamajina ya Wajumbe waliohudhuria mikutano ya Kamati na maamuziyaliyofanyika.

(6) Kumbukumbu zitakazowekwa kwa mujibu wa masharti ya fasiliya (5) ya Kanuni hii zitawekwa saini na Mwenyekiti na Wajumbe waKamati na zitaambatishwa kwenye Taarifa ya Kamati nakuwasilishwa Bungeni pamoja na taarifa hiyo.

120.- Taarifa yoyote ya Kamati inayowasilishwa Bungeni itakuwakatika muundo ufuatao:-

(a) Sehemu ya Utangulizi, ambayo itaoneshahadidu za rejea ambazo Kamati ilipewa;maelekezo yoyote yaliyotolewa kwa Kamati,njia au mbinu zilizotumika na Kamati katikakutekeleza majukumu yake, pamoja na mambomengine, kama yapo, ambayo yalijitokezawakati wa uchunguzi;

(b) Sehemu ya Katikati, ambayo itatoa maelezokamili kuhusu jambo au mambo yoteyaliyofanyiwa Uchunguzi na Kamati; na

(c) Sehemu ya Mwisho, ambayo itatoa maoni namapendekezo ya Kamati ya Bunge.

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

UTARATIBU WA KUMWONDOA RAIS MADARAKANI

121.- Mbunge yeyote anaweza kuwasilisha kwa Spika taarifa yaHoja ya kumshtaki Rais kwa madhumuni ya kumwondoa Raismadarakani kupitia Azimio la Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 46A yaKatiba ikiwa inadaiwa kwamba Rais -

(a) ametenda vitendo ambavyo kwa ujumlavinavunja Katiba au Sheria ya Maadili ya Viongoziwa Umma;

MuundowaTaarifazaKamati

Taarifa yaHoja yaKumwo-ndoaRais,

Sura ya 2,Toleo la 2002

76

(b) ametenda vitendo ambavyo vinakiuka maadiliyanayohusu uandikishwaji wa Vyama vya Siasayaliyotajwa katika Ibara ya 20(2) ya Katiba; au

(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha Kiti chaRais wa Jamhuri ya Muungano. Isipokuwakwamba, hoja ya namna hiyo haitatolewa, ndaniya miezi kumi na miwili tangu ilipotolewa nakukataliwa na Bunge.

122.-(1) Bunge halitajadili wala kushughulikia hoja ya kumshtakiRais, isipokuwa tu kama: –

(a) taarifa ya maandishi, iliyowekwa saini nakuungwa mkono na Wabunge wasiopunguaasilimia ishirini ya Wabunge wote itatolewa;

(b) taarifa hiyo itawasilishwa kwa Spika, sikuthelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyoinakusudiwa kutolewa Bungeni;

(c) taarifa hiyo pia itafafanua makosa aliyoyatendaRais; na

(d) taarifa hiyo vile vile itapendekeza kuwa, KamatiMaalumu ya Uchunguzi iundwe ili ichunguzemashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Rais.

(2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwa saini naWabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili yakuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusu mtoahoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.

(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitaka Bunge,bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ili kupatauamuzi juu ya hoja hiyo.

123.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Rais itaungwa mkono naWabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Spikaatatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi,kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 46A(4) ya Katiba.

(2) Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa na wajumbe wafuatao:-

Sura ya 398,Toleo la2002

Mashartiyahojayak u u n d aKamatiMaalumyaUchunguzi

WajumbewaKamati MaalumuyaUchunguzi,

Sura ya 2,Toleo la2002

77

(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, ambayeatakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo;

(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwa

kuzingatia uwiano wa uwakilishi baina ya Vyamavya Siasa vinavyowakilishwa Bungeni.

(3) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalumu yaUchunguzi, Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, na kwa sababuhiyo, kazi na madaraka ya Rais yatatekelezwa kwa mujibu wamasharti ya Ibara ya 37(3) ya Katiba hadi Spika atakapomfahamishaRais juu ya Azimio la Bunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewadhidi yake.

124.-(1) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalumu ya Uchunguzikuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi ya Raisna itampatia Rais fursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtakayaliyotolewa dhidi yake kwa mujibu wa masharti na utaratibuuliowekwa na Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge naKanuni hizi.

(2) Mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile katika mudausiozidi siku tisini, Kamati Maalumu ya Uchunguzi itatoa taarifa yakekwa Spika.

(3) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati Maalumu ya Uchunguziitakuwa ni Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar na Wajumbewengine wanne kutoka Bungeni.

(4) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalumu yaUchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi.

125.-(1) Endapo kwa mujibu wa Orodha ya Shughuli za Bunge utafikawakati wa Bunge kujadili taarifa ya Kamati hiyo Maalumu yaUchunguzi, basi Bunge litaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima ilikushughulikia taarifa hiyo na Bunge linaweza kumruhusu Mwenyekitina mjumbe mwingine ambaye siyo Mbunge wa Kamati Maalumuya Uchunguzi kuwasilisha na kuelezea uamuzi wa Kamati yakekwenye Kamati ya Bunge Zima.

(2) Baada ya taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuwasilishwaBungeni, Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Rais fursa yakujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.

Suraya 296, Toleola 2002

UtaratibukatikaKamatiyaBungeZimakuhusumashtakadhidi yaRais

Sura ya 2, Toleo la 2002

UtaratibuwakaziyaKamatiMaalumuyauchunguzi

78

126.-(1) Baada ya kusikiliza utetezi wa Rais, Wabunge watapigakura ya siri ili kupata uamuzi wa Bunge iwapo mashtaka dhidi yaRais yamethibitika au mashtaka hayo hayakuthibitika.

(2) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi zake na Bungekurudia, Mbunge aliyetoa hoja ya kumshtaki Rais atatoa taarifa yakukamilika kwa shughuli za Kamati ya Bunge Zima na endapomashtaka dhidi ya Rais yatakuwa yamethibitika, kwa kuungwamkono na kura za Wabunge wasiopungua theluthi mbili yaWabunge wote, papo hapo atatoa hoja kwamba, Bunge lipitisheAzimio la kumwondoa Rais madarakani, kwa mujibu wa mashartiya Ibara ya 46A(5) ya Katiba.

(3) Endapo Bunge litapitisha Azimio la kumwondoa Rais madarakani,Spika atawafahamisha Rais na Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzijuu ya Azimio hilo la Bunge na Rais atawajibika kujiuzulu katika kipindicha siku tatu tangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo.

(4) Endapo Rais ataacha kushika kiti cha Rais kutokana na mashtakadhidi yake kuthibitika na Bunge kupitisha Azimio la kumwondoamadarakani, Rais hatakuwa na haki ya kupata malipo yoyote yapensheni.

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

UTARATIBU WA KUMWONDOA MAKAMUWA RAIS MADARAKANI

127.-(1) Rais anaweza kuwasilisha Bungeni hati ya kuliomba Bungelipitishe Azimio la kumwondoa Makamu wa Rais madarakani ikiwaMakamu wa Rais ameacha au ameshindwa kutekeleza kazi zaMakamu wa Rais kwa mujibu wa Ibara ya 50(3) ya Katiba.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii, Mbungeyeyote anaweza kuwasilisha Bungeni hoja ya kutaka kumwondoaMakamu wa Rais madarakani ikiwa Makamu wa Rais:-

(a) ametenda vitendo ambavyo kwa ujumlavinavunja Katiba au Sheria ya Maadili yaViongozi wa Umma;

Sura ya 2,Toleola2002

Suraya 2,Toleola2002

Azimiolakumwo-ndoaRais

Suraya 398,Toleola 2002

Utaratibu wakumwo-ndoaMakamuwaRaisMadarakani,

79

(b) ametenda vitendo vinavyokiuka maadiliyanayohusu uandikishaji wa Vyama vya Siasavilivyotajwa kutoka Ibara ya 20 (2) ya Katiba; au

(c) amekuwa na mwenendo unaodhalilisha Kiti chaRais wa Jamhuri ya Muungano au Kiti chaMakamu wa Rais. Isipokuwa kwamba, hoja yanamna hiyo haitatolewa ndani ya miezi kumi namiwili tangu hoja ya namna hiyo ilipotolewa nakukataliwa na Bunge.

128.-(1) Bunge halitajadili wala kushughulikia hoja ya kumshtakiMakamu wa Rais isipokuwa tu kama: -

(a) taarifa ya maandishi, iliyowekwa saini nakuungwa mkono na Wabunge wasiopunguaasilimia ishirini ya Wabunge wote imetolewa;

(b) taarifa hiyo itawasilishwa kwa Spika, sikuthelathini kabla ya kikao ambapo hoja hiyoinakusudiwa kutolewa Bungeni;

(c) taarifa hiyo pia itafafanua makosa aliyoyatendaMakamu wa Rais; na

(d) taarifa hiyo pia itapendekeza kuwa, KamatiMaalumu ya Uchunguzi iundwe ili ichunguzemashtaka yaliyowasilishwa dhidi ya Makamu waRais.

(2) Wakati wowote baada ya kupokea taarifa iliyowekwa saini naWabunge na kujiridhisha kuwa masharti ya Katiba kwa ajili yakuwasilisha hoja hiyo Bungeni yametimizwa, Spika atamruhusu mtoahoja kuiwasilisha hoja hiyo Bungeni.

(3) Hoja hiyo itakapowasilishwa Bungeni, Spika atalitaka Bunge,bila ya kufanya majadiliano yoyote, lipige kura ya siri ili kupatauamuzi juu ya hoja hiyo.

129.-(1) Endapo hoja ya kumshtaki Makamu wa Rais itaungwa mkonona Wabunge wasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, Spikaatatangaza majina ya wajumbe wa Kamati Maalumu ya Uchunguzi,kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 46A(4) ya Katiba:-

Suraya 2,Toleola 2002

Mashartiyahojayakuunda KamatiMaalumuyaUchunguzi

WajumbewaKamatiMaalumuyaUchunguzi

80

(2) Kamati Maalumu ya Uchunguzi itakuwa na wajumbe wafuatao:-

(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ambayeatakuwa ndiye Mwenyekiti wa Kamati hiyo;

(b) Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar; na

(c) Wajumbe saba walioteuliwa na Spika kwakuzingatia uwiano wa Uwakilishi baina ya vyamavya siasa vinavyowakilishwa Bungeni.

(3) Endapo Bunge litapitisha hoja ya kuunda Kamati Maalumu yaUchunguzi, Makamu wa Rais atahesabiwa kuwa hayupo kazini, nakwa sababu hiyo, kazi na madaraka ya Makamu wa Raisyatatekelezwa kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 37(3) ya Katibahadi Spika atakapomfahamisha Makamu wa Rais juu ya Azimio laBunge kuhusiana na mashtaka yaliyotolewa dhidi yake.

130.-(1) Ndani ya siku saba baada ya Kamati Maalumu ya Uchunguzikuundwa, itakaa ichunguze na kuchambua mashtaka dhidi yaMakamu wa Rais na itampatia Makamu wa Rais fursa ya kujielezana kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidi yake kwa mujibuwa masharti na utaratibu uliowekwa na Sheria ya Kinga, Madarakana Haki za Bunge na Kanuni hizi.

(2) Mapema iwezekanavyo na kwa vyovyote vile katika mudausiozidi siku tisini, Kamati Maalumu ya Uchunguzi itatoa taarifa yakekwa Spika.

(3) Akidi ya mkutano wowote wa Kamati Maalumu ya Uchunguziitakuwa ni Mwenyekiti, Jaji Mkuu wa Tanzania Zanzibar na Wajumbewengine wanne kutoka Bungeni.

(4) Baada ya Spika kupokea taarifa ya Kamati Maalumu yaUchunguzi, taarifa hiyo itawasilishwa Bungeni kwa kufuata utaratibuuliowekwa na Kanuni hizi.

131.-(1) Endapo kwa mujibu wa Orodha ya Shughuli za Bunge utafikawakati wa Bunge kujadili taarifa ya Kamati hiyo Maalumu yaUchunguzi, basi Bunge litaingia kwenye Kamati ya Bunge Zima ilikushughulikia taarifa hiyo na Bunge linaweza kumruhusu Mwenyekitina mjumbe mwingine ambaye siyo Mbunge wa Kamati Maalumuya Uchunguzi kuwasilisha na kuelezea uamuzi wa Kamati yakekwenye Kamati ya Bunge Zima.

Sura ya2, Toleola 2002

Sura ya296,Toleola 2002

Sura ya 2,Toleo la2002

UtaratibuKatikaKamatiyaBungeZimakuhusumashtakadhidi yaMakamuwa Rais

Utaratibuwakaziya KamatiMaalumuyaUchunguzi,

81

(2) Baada ya taarifa ya Kamati Maalumu ya Uchunguzi kuwasilishwaBungeni, Bunge litaijadili taarifa hiyo na litampa Makamu wa Raisfursa ya kujieleza na kujitetea kuhusu mashtaka yaliyotolewa dhidiyake.

132.-(1) Baada ya kusikiliza utetezi wa Makamu wa Rais, Wabungewatapiga kura ya siri ili kupata uamuzi wa Bunge iwapo mashtakadhidi ya Makamu wa Rais yamethibitika au mashitaka hayohayakuthibitika.

(2) Baada ya Kamati ya Bunge Zima kukamilisha kazi zake na Bungekurudia, Mbunge aliyetoa hoja ya kumshtaki Makamu wa Raisatatoa taarifa ya kukamilika kwa shughuli za Kamati ya Bunge Zimana endapo mashtaka dhidi ya Makamu wa Rais yatakuwayamethibitika, kwa kuungwa mkono na kura za Wabungewasiopungua theluthi mbili ya Wabunge wote, papo hapo atatoahoja kwamba, Bunge lipitishe Azimio la kumwondoa Makamu waRais madarakani, kwa mujibu wa masharti ya Ibara ya 46A(5) yaKatiba.

(3) Endapo Bunge litapitisha Azimio la kumwondoa Makamu waRais madarakani, Spika atawafahamisha Rais, Makamu wa Rais naMwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi juu ya Azimio hilo la Bunge naMakamu wa Rais atawajibika kujiuzulu katika kipindi cha siku tatutangu Bunge lilipopitisha Azimio hilo.

(4) Endapo Makamu wa Rais ataacha kushika kiti cha Makamu waRais kutokana na mashtaka dhidi yake kuthibitika na Bunge kupitishaAzimio la kumwondoa madarakani, Makamu wa Rais, hatakuwa nahaki ya kupata malipo yoyote ya pensheni.

SEHEMU YA KUMI NA TATU

HOJA YA KUTOKUWA NA IMANI NA WAZIRI MKUU

133.-(1) Mbunge yeyote anaweza kutoa taarifa ya maandishi kwaSpika ya kutaka kuleta hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuukwa mujibu wa Ibara ya 53A ya Katiba.

(2) Hoja yoyote ya kutaka kupitisha Azimio la kura ya kutokuwa naimani na Waziri Mkuu haitatolewa Bungeni endapo:-

Sura ya 2,Toleola 2002

Azimio lakumwo-ndoaMakamu wa Raismadarakani

Taarifa yaHoja yakutokuwa na imanina WaziriMkuu

Sura ya 2,Toleo la 2002

82

(a) haina uhusiano na utekelezaji wa majukumu yaWaziri Mkuu yaliyoainishwa katika Ibara ya 52 yaKatiba;

(b) hakuna madai kwamba Waziri Mkuu amevunjaSheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma;

(c) haijapita miezi sita tangu alipoteuliwa; au

(d) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyoilipotolewa Bungeni na Bunge likakataakuipitisha.

(3) Hoja ya kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu haitajadiliwana Bunge isipokuwa tu kama:-

(a) taarifa ya maandishi iliyowekwa saini nakuungwa mkono na Wabunge wasiopunguaasilimia ishirini ya Wabunge wote itatolewakwa Spika, siku zisizopungua kumi na nnekabla ya siku inayokusudiwa kuwasilishwaBungeni;

(b) Spika ataridhika kuwa masharti ya Katiba kwaajili ya kuleta hoja hiyo yametimizwa.

(4) Hoja inayotolewa chini ya Kanuni hii na iliyotimiza masharti yaKatiba, itawasil ishwa Bungeni mapema iwezekanavyo naitaamuliwa kwa kura za siri.

(5) Hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwa tu iwapoinaungwa mkono na Wabunge walio wengi.

(6) Endapo hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu itapitishwana Bunge kwa kupigiwa kura na Wabunge walio wengi, Spikaatawasilisha Azimio hilo kwa Rais na mapema iwezekanavyo nakwa vyovyote vile ndani ya siku mbili tangu Bunge lilipopitishaAzimio hilo, Waziri mkuu atajiuzulu na Rais atamteua Mbungemwingine kuwa Waziri Mkuu.

Sura ya398,Toleola 2002

Sura ya2, Toleola 2002

83

SEHEMU YA KUMI NA NNE

KUMWONDOA SPIKA AU NAIBU SPIKA MADARAKANI

134.-(1) Mbunge yeyote anayetaka kuwasilisha hoja ya kumwondoaSpika madarakani chini ya Ibara ya 84(7)(d) ya Katiba, atawasilishataarifa ya maandishi ya kusudio hilo kwa Katibu akieleza sababukamili ya kutaka kuleta hoja hiyo.

(2) Mara tu baada ya kupokea taarifa ya maandishi ya kusudio lakumwondoa Spika kwenye madaraka, Katibu ataipeleka taarifahiyo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwaajili ya kuijadili.

(3) Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaridhikakuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Spika zinazohusu uvunjaji wamasharti ya Ibara ya 84(7)(a), (b), (e), (f), (g) na (h) ya Katiba, Sheriaau Kanuni zinazoongoza shughuli za Bunge, basi Kamati hiyoitaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe Bungeni ili iamuliwe.

(4) Naibu Spika, atakalia Kiti cha Spika wakati wa kujadili hoja yakutaka kumwondoa Spika madarakani na Spika atakuwa na hakiya kujitetea wakati wa mjadala.

(5) Spika atakuwa ameondolewa kwenye madaraka endapozitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya Wabungewote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bunge utafanywakwa kuzingatia kura za siri.

(6) Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasi yake kwa kutoamaelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzi juu ya hoja yakumwondoa madarakani.

135.-(1) Utaratibu wa kumwondoa Naibu Spika madarakani chiniya Ibara ya 85(4)(c) ya Katiba utakuwa kama ule wa kumwondoaSpika, isipokuwa tu taarifa ya kusudio la kumwondoa Naibu Spikamadarakani inayoeleza sababu kamili za kuleta hoja hiyo,itapelekwa kwa Spika ambaye ataiwasilisha kwenye Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kuijadili.

(2) Endapo Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itaridhikakuwa zipo tuhuma mahususi dhidi ya Naibu Spika zinazohusu uvunjajiwa Katiba, Sheria au Kanuni zinazoongoza Shughuli za Bunge, basi

Taarifaya HojayakumwondoaSpikamadarakani

Utaratibuwakumwo-ndoaNaibu SpikaMadarakani

Sura ya2,Toleola 2002

Sura ya 2,Toleo la2002

84

Kamati hiyo itaidhinisha kuwa hoja hiyo ipelekwe Bungeni iliiamuliwe.

(3) Spika atakalia Kiti wakati wa kujadili hoja ya kutaka kumwondoaNaibu Spika madarakani na Naibu Spika atakuwa na haki yakujitetea wakati wa mjadala.

(4) Naibu Spika atakuwa ameondolewa kwenye madaraka endapozitapigwa kura zisizopungua theluthi mbili ya idadi ya Wabungewote za kuunga mkono hoja hiyo na uamuzi wa Bunge utafanywakwa kuzingatia kura za siri.

(5) Naibu Spika anayetuhumiwa anaweza kujiuzulu nafasi yake kwakutoa maelezo ya kujiuzulu kwake Bungeni kabla ya uamuzi juu yahoja ya kumwondoa madarakani.

SEHEMU YA KUMI NA TANO

WAGENI BUNGENI

136.-(1) Wageni wanaweza kuruhusiwa kuingia kwenye Ukumbi waMikutano ya Bunge katika sehemu yoyote ya Ukumbi huo ambayoitatengwa kwa ajili hiyo.

(2) Wageni wakiwa ndani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bungewatalazimika kufuata na kuzingatia masharti yafuatayo:-

(a) Watakaa kimya na kwa heshima inayostahilihadi watakapotoka nje ya Ukumbi huo;

(b) Wanapaswa wawe wamevaa mavazi yaheshima;

(c) Wataingia na kutoka Ukumbini kwa staha;

(d) Wasisome kitabu chochote, gazeti, baruaau hati nyingineyo ambayo si Orodha yaShughuli za Bunge;

(e) Wasiandike wala kurekodi jambo lolotelinalozungumzwa, isipokuwa tu kama niwawakilishi wa vyombo vya habari;

Ruhusa kwa wageniBungeni

85

(f) Inapolazimu kuzungumza, wasizungumze kwasauti ya juu;

(g) Wasivute sigara au kiko wakati wowote wakiwandani ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge aumahali popote nje ya Ukumbi huo ambapo kunamahali pa kukaa wageni;

(h) Wazime simu zao za mikononi;

(i) Wasiingie na kamera wala kupiga picha;

(j) Wasishangilie wala kuzomea wakiwa ndani yaukumbi wa Bunge; na

(k) Wasifanye jambo au kitendo chochote ambachokinaweza kuvuruga amani na utulivu Bungeni.

(3) Spika anaweza kumwamuru mgeni yeyote aondoke kwenyeUkumbi wa Bunge endapo atavunja lolote kati ya mashartiyaliyotajwa katika fasili ya (2) ya Kanuni hii.

137.-(1) Katibu anaweza kutoa ruhusa maalumu au ya jumla kwamwakilishi wa chombo chochote cha habari kuhudhuria vikao vyaBunge katika sehemu ya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge iliyotengwakwa ajili hiyo.

(2) Ruhusa yoyote itakayotolewa na Katibu inaweza kuwekewamasharti yafuatayo:-

(a) Chombo husika kitoe maombi rasmi;

(b) Chombo husika kiteue Waandishi wenye sifa namaadili ya kuweza kuandika habari za Bunge.

(3) Katibu anaweza wakati wowote kuondoa ruhusa aliyotoa kwamwakilishi wa chombo chochote cha habari, iwapo chombo hichokitatoa taarifa yoyote kuhusu Shughuli za Bunge ambayo, kwamaoni ya Bunge, inapotosha ukweli au vinginevyo inakiuka Kanuni,taratibu au haki za Bunge.

RuhusaKwaWaandishi waHabari

86

UtaratibuwakukaakwaWabunge,WatumishinaWageni Bungeni

138.-(1) Spika anaweza kuamuru wageni watoke nje ya sehemuyoyote ya Ukumbi na maeneo yake na anaweza kuamuru milangoya Ukumbi wa Mikutano ya Bunge ifungwe.

(2) Endapo wakati wa kikao chochote Mbunge atatoa hoja kuwawageni watoke nje, Spika atalihoji Bunge papo hapo na hojaitaamuliwa bila ya mjadala au mabadiliko yoyote, wakati wowoteatakapoona inafaa kufanya hivyo.

(3) Mtumishi yeyote wa Bunge hataruhusiwa kumtoa nje mgeni aukuagiza mgeni atolewe nje ya Ukumbi wa Bunge endapo Katibuamemruhusu mgeni huyo kuwa ndani ya Ukumbi wa Bunge.

139.- (1) Spika anaweza kuwatambulisha wageni wote wa kitaifana kimataifa waliomo katika Ukumbi wa Bunge.

(2) Spika vilevile anaweza kuwatambulisha wageni wenginewaliomo katika Ukumbi wa Bunge ambao:-

(a) wanahusika moja kwa moja na shughuli zaMajimbo;

(b) wanatembelea Bunge kwa ajili ya ziara zamafunzo; na

(c) wametoa mchango wa kitaifa unaohitajikuenziwa.

SEHEMU YA KUMI NA SITA

UKAAJI NDANI YA BUNGE

140.- Spika ataweka utaratibu maalumu wa ukaaji wa Wabungendani ya Bunge, bila ya kuathiri mpangilio ufuatao:-

(a) Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni atakaakiti cha kwanza akifuatiwa na Mwanasheria Mkuuwa Serikali na Mawaziri, upande wa kulia waSpika.

(b) Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni atakaakiti cha kwanza akifuatiwa na Wasemaji Wakuuwa Upinzani upande wa kushoto wa Spika.

Mamlakayakuwao-ndoawageniBungeni

Utambu-lishowaWageni

87

(c) Endapo hakuna Kiongozi wa Upinzanialiyechaguliwa na chama chenye haki yakuchagua Kiongozi wa Upinzani Bungeni lakiniWabunge wa Upinzani wapo, basi Wabunge haowatakaa upande wa kushoto wa Spika.

(d) Wapambe wa Bunge, watumishi wa Ofisi yaBunge, wahudumu wa Bunge, Watumishi waSerikali wenye shughuli maalumu Bungeni,waandishi wa vyombo vya habari na wageniwengine watakaa sehemu ambazo zimetengwakwa ajili yao.

(e) Wageni wa Wabunge na wageni wenginewanaweza kutengewa sehemu maalumu yakukaa.

(f) Wageni mashuhuri, Mabalozi na Viongoziwengine watakaa sehemu maalumu ya Spika.

SEHEMU YA KUMI NA SABA

USALAMA WA MAENEO YA BUNGE

141.-(1) Spika ataweka utaratibu wa kutoa vitambulisho kwaWabunge, watumishi wa Bunge, watumishi wa Serikali na kwa mtumwingine yeyote anayeingia kwenye Ukumbi wa Bunge au maeneomengine ya Bunge.

(2) Katibu atatoa vitambulisho vya aina tofauti kwa ajili yaWabunge, watumishi wa Bunge, watumishi wa Serikali na wageniwanaokaribishwa katika Ukumbi wa Bunge au maeneo mengineya Bunge.

142.-(1) Kutakuwa na utaratibu wa kumkagua mtu yeyoteanayeingia katika maeneo ya Bunge kwa kuzingatia:-

(a) staha na heshima; na

(b) tofauti ya jinsia.

(2) Endapo katika kufanya ukaguzi mtu yeyote atapatikana nakifaa ambacho kwa asili yake ni cha hatari, kifaa hicho atakiachakwa walinzi waliopo mlangoni.

UtaratibuwakuingiaMaeneoyaBunge

Ukaguzi

88

LughaRasmiBungeni

TaarifaRasmizaBunge

(3) Mbunge, mtumishi au mgeni yeyote atakayekataa kukaguliwaau kukabidhi kitu chochote ambacho walinzi wataona kwamba nicha hatari, hataruhusiwa kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge aumaeneo ya Bunge.

SEHEMU YA KUMI NA NANE

MENGINEYO

143.-(1) Kuhudhuria vikao vya Bunge na Kamati zake ni wajibu wakwanza wa kila Mbunge.

(2) Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria Mikutano ya Bungemitatu mfululizo bila ruhusa ya Spika iliyotolewa kwa maandishi,atapoteza Ubunge wake kwa mujibu wa Ibara ya 71(1)(c) ya Katibana Spika ataiarifu Tume ya Uchaguzi.

(3) Mbunge atakapokosa kuhudhuria nusu ya vikao vya Mkutanommoja bila ya sababu ya msingi atapewa onyo.

(4) Mbunge yeyote atakayeshindwa kuhudhuria vikao vya Bungena Kamati zake kwa sababu maalumu atatakiwa kupata kibali chaSpika.

(5) Kwa madhumuni ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, kibali kitatolewakatika Ofisi za Bunge za Dodoma au Dar es Salaam au Zanzibar.

144.-(1) Shughuli za Bunge zitaendeshwa katika lugha ya Kiswahiliau Kiingereza, bila tafsiri ya lugha hizo kutolewa.

(2) Kwa kadri itakavyowezekana, Mbunge atajitahidikutochanganya lugha zote mbili wakati anasema Bungeni,isipokuwa tu pale anaponukuu.

145.-(1) Taarifa Rasmi ya Majadiliano Bungeni, ikiwa katika lughailiyotumiwa na msemaji, yakiwa ni maneno halisi aliyoyatamka,itatayarishwa chini ya usimamizi wa Katibu wa Bunge kwa kufuatamaagizo yatakayotolewa na Spika kwa ajili hiyo.

(2) Kila Mbunge aliyetoa hotuba Bungeni atapewa nakala yahotuba yake mapema iwezekanavyo, ili aweze kusahihisha makosaya uchapaji, kama yatakuwepo ila hataruhusiwa kubadilisha maanahalisi ya maneno aliyoyasema Bungeni.

WajibuwaMbungekuhudhuriaVikaovyaBungeSura ya 2,Toleo la 2002

89

146.-(1) Mbunge anayeingia kwenye Ukumbi wa Bunge atawajibikakuvaa mavazi ambayo ni safi na yenye kuhifadhi heshima yake,hadhi ya Bunge na utamaduni wa nchi, kama ilivyoainishwa katikaKanuni hii.

(2) Vazi Rasmi la Spika na Naibu Spika litakuwa ni joho lenyekuonesha rangi za Bendera ya Taifa, Nembo ya Taifa na baadhi yamazao makuu nchini, lililoshonwa maalumu kwa ajili hiyo, ambalolitavaliwa juu ya vazi lolote ambalo ni vazi rasmi kwa Wabunge.

(3) Vazi rasmi kwa Wabunge litakuwa lolote kati ya yafuatayo:-

(a) Kwa Wabunge wanawake:-(i) vazi lolote la heshima yaani ambalo si la

kubana mwili, lisiloonesha maungoambayo kwa mila na desturi za kitanzaniahayapaswi kuoneshwa na ni refu kuvukamagotini;

(ii) gauni la kitenge au blauzi inayovaliwana kitenge au sketi ya rangi yoyote;

(iii) kilemba cha kadri au mtandio;

(iv) suti ya kike; na

(v) vazi linalovaliwa wakati wa eda.

(b) Kwa Wabunge wanaume:-(i) suti ya Kiafrika au safari ya mikono mirefu

au mifupi yenye ukosi au shingo yamviringo na yenye fulana au bila fulanandani, ya rangi moja, isiyokuwa na nakshi,pamoja au bila baragashia;

(ii) vazi la kimwambao yaani kanzu rasmi nanadhifu, koti, baraghashia na makubadhiau viatu;

(iii) suti kamili ya kimagharibi ya rangi kadriisiyomeremeta;

(iv) koti aina ya blazer na tai, pamoja na surualiyoyote ya heshima; au

Mavazi Rasmi

90

(v) tarbushi na kilemba cha Singasinga, au kilembachochote kinachovaliwa kwa mujibu wa mashartiya imani au mila.

(4) Vazi Rasmi la Katibu na Wasaidizi wake Bungeni litakuwa kamaifuatavyo:-

(a) Kwa Makatibu wanaume:

(i) suti kamili ya kiafrika au safari, yenye ukosiau shingo ya mviringo na mikono mirefuau mifupi ya rangi nyeusi au bluu; au

(ii) suti kamili ya kimagharibi ya rangi nyeusiau bluu na shati jeupe na tai.

(b) Kwa Makatibu wanawake:

Suti ya rangi nyeusi au ya bluu na shati jeupe natai.

(c) Makatibu na Wahudumu watavaa mavazimaalumu wakati wa shughuli maalumu za Bunge.

(5) Mpambe wa Bunge na Wasaidizi wake ndani ya Ukumbi waBunge watavaa mavazi rasmi ambayo yataamuliwa na Spika.

(6) Spika anaweza kwa sababu maalumu, kumruhusu mtu mwingineanayehusika na shughuli za Bunge kuvaa viatu ambavyo sio rasmi.

(7) Mbunge yeyote anaweza kutoa taarifa Bungeni iwapo Mbungemwingine ataingia kwenye Ukumbi wa Bunge akiwa na mavaziyasiyoruhusiwa kwa mujibu wa Kanuni hii.

(8) Spika atakaporidhika kuwa Mbunge aliyetolewa taarifa kwamujibu wa fasili ya (7) ya Kanuni hii hajavaa mavazi rasmi ataamuruMbunge huyo atoke nje ya Ukumbi wa Bunge.

(9) Mbunge aliyetolewa nje kwa mujibu wa fasili ya (8) ya Kanuni hiihataingia ndani ya Ukumbi wa Bunge hadi pale atakapokuwaamevaa mavazi rasmi.

147. Kutakuwa na Bendera rasmi ya Bunge la Jamhuri ya Muunganowa Tanzania itakayoitwa Bendera ya Bunge, ambayo:-

BenderayaBunge

91

(a) itakuwa katika umbo la mstatiri na rangi ya bluuiliyoiva na pembeni itakuwa na umbo dogo labendera ya Taifa ndani yake katika pembe ya juuupande wa kushoto.

(b) itakuwa pia na Siwa ya Bunge yenye rangi yadhahabu, chini kukiwa na utepe wenye maneno“Bunge la Tanzania.”

148.-(1) Bendera ya Bunge itapepezwa kwenye maeneoyafuatayo:-

(a) Katika Ofisi za Bunge Dodoma, Dar es Salaam naZanzibar.

(b) Nje ya Ofisi za Wabunge zilizopo Makao Makuuya Mkoa, Wilaya na katika Majimbo ya Uchaguzi.

(c) Ndani ya Ofisi ya Mbunge juu ya mezaanayofanyia kazi.

(d) Katika magari binafsi ya Wabunge ambapoBendera hiyo itapepezwa ikiwa mbele upandewa kushoto wa gari la Mbunge wakati Mbungemwenyewe anapokuwa ndani ya gari hilo, naakiwa anaendeshwa na dereva mwingine, siyoanapokuwa anaendesha mwenyewe.

(2) Mbunge hatapepeza Bendera kwenye gari lake awapo katikaMiji ya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, na anapokuwaanatumia gari la kukodi au la kuazima.

(3) Bila ya kuathiri masharti yaliyotangulia ya Kanuni hii, Benderaya Bunge itapepezwa kuanzia saa 12.00 asubuhi na kuteremshwamara ifikapo saa 12.00 jioni kila siku.

(4) Bendera ya Bunge itaendelea kupepezwa katika gari la Mbungebaada ya saa 12.00 jioni endapo anayepepeza Bendera hiyoatakuwa safarini hadi pale atakapomaliza safari yake.

Utaratibuwa kupepezaBendera

92

KufanyaMabadi-likokatikaKanuni

149.- Endapo Mbunge atafariki wakati Bunge likiwa katika shughulizake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili yamaombolezo.

150.-(1) Kwa idhini ya Spika, Kanuni yoyote inaweza kutenguliwakwa madhumuni mahususi baada ya Waziri, Mwanasheria Mkuu waSerikali au Mbunge yeyote kutoa hoja kwa ajili hiyo.

(2) Hoja ya kutengua Kanuni za Bunge haitahitaji kutolewa taarifa.

(3) Maelezo ya hoja ya kutaka kutengua Kanuni yoyote itakuwa nipamoja na maelezo kuhusu madhumuni ya kutaka Kanuni hiyoitenguliwe.

(4) Kanuni hiyo itatenguliwa kwa madhumuni yaliyokusudiwa tu nasiyo kwa madhumuni mengine yoyote.

151.-(1) Endapo litatokea jambo lolote ambalo muhusika wake aumwathirika wa jambo hilo anastahili kupewa pongezi au pole naWabunge basi Spika atatoa pongezi au pole kwa mhusika aumwathirika wa jambo hilo kwa niaba ya Wabunge wote.(2) Baada ya Spika kutoa pongezi au pole kwa muhusika aumwathirika wa jambo lolote, kwa ajili ya kuokoa muda wamajadiliano, Mbunge yeyote hataruhusiwa kutoa pongezi au polekwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakati wowote wamajadiliano Bungeni.

(3) Kwa upande wa Serikali, Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeniatatoa pongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambololote kwa niaba ya Serikali.

(4) Baada ya Kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni kutoa pongeziau pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo lolote, kwa ajili yakuokoa muda wa majadiliano, Waziri yeyote hataruhusiwa kutoapongezi au pole kwa muhusika au mwathirika wa jambo hilo wakatiwowote wa majadiliano Bungeni.

152.-(1) Bunge linaweza kupitisha Azimio la kufanya mabadilikokatika Kanuni yoyote kutokana na mapendekezo ya Kamati yaKanuni za Bunge.

(2) Mabadiliko yoyote ya Kanuni za Bunge yatawasilishwa Bungenina Naibu Spika.

Salamu zaPongezi naPole

Utaratibu baada yakifo cha Mbunge

KutenguaKanuni zaBunge

93

(3) Spika, kwa kushauriana na Kamati ya Kanuni za Bunge, atakuwana madaraka ya kuzifanyia marekebisho au mabadiliko Nyongezaza Kanuni hizi, kulingana na mahitaji ya wakati, kadri atakavyoonainafaa.

153.-(1) Mabadiliko yaliyopitishwa hayataanza kutumika mpakayatakapochapishwa na kuingizwa katika Toleo la Kanuni za Bungelitakalofuata.

(2) Endapo Kanuni za Bunge zitafanyiwa mabadiliko, Spika ataagizazichapishwe upya kwenye Gazeti kwa madhumuni ya kuingizamabadiliko yaliyofanyika.

(3) Nakala za Kanuni za Bunge zilizochapishwa kwa kufuatautaratibu uliofafanuliwa katika Kanuni hii itahesabiwa kuwa nakalahalisi za Kanuni za Kudumu za Bunge zilizofanyiwa mabadiliko.

154.-(1) Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2004 zinafutwa.

(2) Bila kujali masharti ya fasili ya (1) ya Kanuni hii jambo lolote,amri yoyote, uteuzi wowote, agizo au suala jingine lolote lililofanyikakwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la 2004 halitakuwabatili na litaendelea kuwa halali hadi litakapobadilishwa, kufutwaau kuagizwa vinginevyo kwa mujibu wa Kanuni hizi.

Kanunikuanzakutumika

KufutwakwaToleola 2004nahifadhiyamamboyaliyo-fanyika

94

________

NYONGEZA_________

NYONGEZA YA KWANZA________________

KANUNI ZA UCHAGUZI WA SPIKA NA NAIBU SPIKA_________

(Chini ya Kanuni ya 9 na 10)_________

SEHEMU YA KWANZA

UTANGULIZI

1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Uchaguzi wa Spika na Naibu Spika.

2. Kanuni hizi zitatumika katika mchakato wa Uchaguzi wa Spikana Naibu Spika.

3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale maelezo yatakapohitajivinginevyo:- “Chama” ni Chama cha Siasa chenye usajili wa kudumu; “Chombo cha Uteuzi” ni Chama kinachopendekeza mgombeaau wagombea wake; “Katibu” ni Katibu wa Bunge; “ Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu waIbara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri yaMuungano; “Mgombea” ni mtu aliyejitokeza au aliyependekezwa naChama cha Siasa kuwa mgombea wa uchaguzi; “Msimamizi wa Uchaguzi” ni mtu ambaye kwa mujibu wa Kanunihizi amepewa mamlaka ya kuendesha na kusimamia Uchaguzi; “Nafasi” ni nafasi wazi ya Spika au Naibu Spika, iliyotokea amakutokana na kuvunjwa kwa Bunge au kutokana na nafasi itokeayokwa nasibu; “Nafasi ya nasibu” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabungeisiyotokana na kuvunjwa kwa Bunge; “Naibu Spika” ni Naibu Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibaraya 85 ya Katiba;

Jina

Matumizi

Tafsiri

95

“Siku ya uteuzi” ni siku ambayo imetangazwa na msimamizi wauchaguzi kwamba ndiyo siku ya mwisho ya kupokea majina yawagombea; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyetajwa katika Ibara ya 84 yaKatiba; “Uchaguzi” ni Uchaguzi wa Spika au Naibu Spika.

SEHEMU YA PILIMSIMAMIZI WA UCHAGUZI

4. Isipokuwa kama imeelezwa vinginevyo, uchaguzi wa Spika naNaibu Spika utaendeshwa na kusimamiwa na Katibu wa Bunge,kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Kanuni za Bunge pamojana Kanuni hizi.

SEHEMU YA TATUKUWASILISHA JINA LA MGOMBEA

5.-(1) Inapofika wakati wa uchaguzi wa Spika au Naibu Spika,Chama chochote cha Siasa chenye kusudio la kushiriki kwenyeuchaguzi huo kitawasilisha kwa Katibu wa Bunge jina moja tu laama Mbunge wa Chama hicho au la mtu mwingine yeyote waChama hicho mwenye sifa za kuwa Mbunge kuwa mgombea wake.

(2) Mgombea mhusika au Ofisa wa ngazi ya kitaifa wa Chamakilichompendekeza, atawasilisha jina la mgombea huyo kwa Katibuambaye ndiye Msimamizi wa Uchaguzi.

(3) Jina la mgombea huyo linatakiwa limfikie Katibu Ofisini kwakeDodoma, kabla ya saa kumi jioni ya siku ya uteuzi.

SEHEMU YA NNEMASHARTI YA MGOMBEA UCHAGUZI

6. Mtu yeyote anaweza kuteuliwa kugombea kuchaguliwa kuwaSpika au Naibu Spika iwapo tu atakuwa ametimiza masharti yoteya kuwa mgombea wa nafasi hizo, kama yalivyotajwa katikaKifungu cha 38 cha Sheria ya Uchaguzi, Sura 343, Toleo la 2002.

Uendeshaji nausimamizi wauchaguzi

Kuwasi-lishamajinayawagombea

Mashartikwamgombea

96

SEHEMU YA TANOKUCHAGULIWA BILA KUPINGWA

7. Endapo hadi kufikia saa kumi jioni ya siku ya uteuzi kutakuwa najina moja tu lililowasilishwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi, mgombeahuyo atatangazwa na Msimamizi wa Uchaguzi kuwa amechaguliwabila kupingwa kuwa Spika au Naibu Spika.

Kuchagu-liwabilakupingwa

97

_________NYONGEZA YA PILI

_________

KANUNI ZA UCHAGUZI WA WABUNGE WANAOKWENDAKWENYE VYOMBO VINGINE VYA UWAKILISHI

_________(Chini ya Kanuni ya 12)

_________

SEHEMU YA KWANZAUTANGULIZI

1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Uchaguzi wa Wabungewanaokwenda katika vyombo vingine vya uwakilishi au kuwaWajumbe wa Tume ya Bunge.

2. Kanuni hizi zitatumika kwa uchaguzi wa Wabunge wanaokwendakatika vyombo vingine kuliwakilisha Bunge na pia kwa uchaguziwa Wabunge wanaogombea kuwa wajumbe wa Tume ya Bunge.

3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale maelezo yanapohitajivinginevyo:- “Chama” ni Chama cha Siasa chenye uwakilishi Bungeni; “Chombo cha Uteuzi” ni chama kinachopendekeza mgombeaau wagombea wake; “Katibu” ni Katibu wa Bunge; “Idadi inayotakiwa” ni idadi ya kura zinazotakiwa kupatikanaau idadi ya nafasi zinazotakiwa zijazwe kwenye Uchaguzi; “Mbunge” ni mtu aliyechaguliwa au kuteuliwa kwa mujibu waIbara ya 66 ya Katiba kuwa mjumbe wa Bunge la Jamhuri yaMuungano; “Mgombea” ni mtu aliyejitokeza au aliyependekezwa na Chamacha Siasa kuwa mgombea wa uchaguzi; “Msimamizi wa Uchaguzi” ni mtu ambaye kwa mujibu wa Kanunihizi amepewa mamlaka ya kuendesha na kusimamia Uchaguzi; “Nafasi” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabunge kutokamiongoni mwa Wabunge iliyotokana na kuvunjwa kwa Bunge auna nafasi itokeayo kwa nasibu; “Nafasi ya nasibu” ni nafasi wazi ya uwakilishi wa Wabungeisiyotokana na kuvunjwa kwa Bunge;

Tafsiri

Jina

Matumizi

98

“Siku ya uteuzi” ni siku ambayo imetangazwa na Msimamizi wauchaguzi kwamba ndiyo siku ya mwisho ya kupokea majina yaWagombea; “Spika” ni Spika wa Bunge aliyechaguliwa kwa mujibu wa Ibaraya 84 ya Katiba; “Uchaguzi” ni uchaguzi wa Wabunge wanaokwenda katikavyombo vingine kuliwakilisha Bunge au kuwa Wajumbe wa Tumeya Bunge.

SEHEMU YA PILIUTEUZI WA WAGOMBEA

4. Uteuzi wa Wagombea utafuata utaratibu ufuatao:-

(a) Unapofika wakati wa Uchaguzi, kila Mbungeanayetaka kushiriki atawasilisha jina lake kwaKatibu ambaye atakuwa ndiye Msimamizi waUchaguzi huo.

(b) Majina ya Wagombea wote yatatakiwa kumfikiaKatibu Ofisini kwake Dodoma, siku moja kabla yasiku ya uteuzi.

SEHEMU YA TATUUTARATIBU WA UCHAGUZI

5.-(1) Uchaguzi wa wagombea wa nafasi za Uwakilishi utaendeshwana kusimamiwa na Katibu kwa utaratibu ufuatao:-

(a) Wakati wa Uchaguzi wa kwanza katika maisha yaBunge wa nafasi zilizotangazwa, mara tu baadaya Wagombea kuwasilisha majina yao, Spika:-

(i) Ataagiza majina ya wagombea wotewaliojitokeza yasambazwe kwa Wabunge;

(ii) Atatangaza Bungeni siku na mudaambapo kura zitapigwa;

(b) Katibu atatoa Taarifa ya maandishi kuhusu saa yakupiga kura ambayo itatolewa si chini ya saaishirini na nne kabla ya muda wa kupiga kura.

Uchaguziwawagombeawanafasizauwakilishi

UteuziwaWagombea

99

(c) Endapo itatokea nafasi miongoni mwa Wabungewaliochaguliwa kwa kufuata Kanuni hizi kutokanana sababu isiyohusiana na kuvunjwa kwa Bungeau kama nafasi ya namna hiyo haikujazwa, Spikaatatoa taarifa ya kutokea kwa nafasi hiyo kwaWabunge wote Bungeni.

(2) Utaratibu wa kujaza nafasi ambazo zimetengwa maalumu kwaajili ya ama kundi la Wabunge Wanawake au kundi la Wabungewa Kambi ya Upinzani, utakuwa kama ifuatavyo:-

(a) Katibu atatangaza siku ya uteuzi ambayoitakuwa si zaidi ya siku tano baada ya tangazola Spika kutolewa Bungeni kwa mujibu wa fasiliya (1)(c) ya Kanuni hii.

(b) Mbunge yeyote wa kundi linalohusika anayetakakuwa mgombea wa nafasi hiyo atawasilishajina lake kwa Katibu, angalau siku moja kablaya siku ya uteuzi iliyowekwa.

(c) Endapo atajitokeza mgombea mmoja wa nafasiinayohusika, Wabunge watampigia kura za“NDIYO” au “HAPANA.”

(3) Baada ya kupata majina ya wagombea wote, Katibu atatoamatangazo kuhusiana na idadi ya wagombea, siku na muda wauchaguzi.

(4) Endapo kunatokea nafasi mbili au zaidi za nasibu kwa wakatimmoja, uchaguzi na upigaji kura utaendeshwa kama uchaguzimmoja.

SEHEMU YA NNEUCHAGUZI WA KUJAZA NAFASI ZA NASIBU

6. Kwa madhumuni ya uchaguzi wa kujaza nafasi yoyote ya nasibu,kutakuwa na karatasi moja tu ya kura ambayo itakuwa na orodhaya majina ya wagombea wote waliojitokeza, inayofuata mfululizowa alfabeti pamoja na jina la Chama cha mgombea na kutakuwana nafasi tupu pembeni ya jina la kila mgombea kwa ajili ya kuwekaalama ya kupiga kura.

Uchaguziwakujazanafasizanasibu

100

SEHEMU YA TANOUTARATIBU WA KUPIGA KURA

7.-(1) Kila Mbunge atakayekuwepo ukumbini wakati wa kupigakura anaweza, katika uchaguzi wa kwanza katika maisha ya Bungeau katika uchaguzi wa kujaza nafasi ya nasibu moja au zaidi:-

(a) kupiga kura moja moja au zaidi kulingana namaelekezo yaliyomo kwenye karatasi ya kurakwa ajili ya wagombea uchaguzi wa nafasiinayoshindaniwa kutoka miongoni mwa walewaliopendekezwa; au

(b) kupiga kura moja kwa kila mgombea Uchaguzimmoja kwa kufuata idadi ya nafasi za nasibuzilizopo katika Uchaguzi huo.

(2) Mbunge atapiga kura yake kwa kuweka alama ya “V” katikanafasi wazi ya karatasi ya kura pembeni ya jina la mgombeaanayetaka kumpigia.

SEHEMU YA SITAKUPIGA KURA

8.-(1) Utakapofika wakati wa kupiga kura, Spika atasitishamajadiliano ya Bunge na kuelekeza kwamba, kura ipigwe.

(2) Wakati huo huo mambo yafuatayo yatafanyika:-

(a) Katibu atatangaza idadi au aina ya Chaguzizitakazofanyika au nafasi zitakazojazwa;

(b) Kila mgombea atapewa muda wa kujieleza nakuomba kura.

(3) Kabla ya kupiga kura, sanduku la kura litaoneshwa kwenyeukumbi kuwa ni tupu, baada ya hapo kila Mbungeatakayekuwepo ukumbini atapewa karatasi moja ya kupiga kura.

(4) Sanduku la kura litawekwa chini ya usimamizi wa Katibu pamojana Wabunge waliochaguliwa kusimamia kuhesabiwa kwa kurampaka wakati wa kuhesabiwa kwa kura, na Katibu pamoja na haoWabunge watakuwa na madaraka kuhakikisha kwamba, sandukuhilo halifunguliwi mpaka wakati wa kuanza kuhesabu kura na

Utaratibuwakupigakura

Kupigakura

101

kwamba, hakuna kitu kitakachowekwa ndani ya sanduku hilobaada ya karatasi za kura kukusanywa kwa mujibu wa fasili ya (3).

(5) Baada ya Wabunge kupiga kura, karatasi zitakusanywa nakutumbukizwa kwenye sanduku la kura.

(6) Baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika na karatasi za kurakukusanywa, Spika atachagua Wabunge wawili wasimamie kaziya kuhesabu kura na majadiliano ya Bunge yatarudia kuanzia paleyalipositishwa.

SEHEMU YA SABAKUHESABU KURA

9.-(1) Mapema itakavyowezekana baada ya kupiga kura nakabla ya kumaliza Kikao kilichopo cha Bunge, Katibu, mbele yaWabunge wawili waliochaguliwa kusimamia zoezi la kuhesabukura, atalifungua sanduku la kura, kuzihesabu na kuziandika kuraalizopata kila mgombea.

(2) Karatasi ya kura itakataliwa na kura hazitahesabiwa katikakaratasi hiyo:-

(a) ikiwa karatasi hiyo siyo rangi rasmi yakaratasi ya kupigia kura iliyotolewa na Katibu;

(b) ikiwa mpiga kura amepiga kura zaidi au pungufuya zile zinazotakiwa kupigwa;

(c) ikiwa kutaonekana kwenye karatasi hiyomaandishi yoyote au alama yoyoteiliyowekwa na mpiga kura isiyokuwa ya ile ya“V”;

(d) ikiwa haikuwekwa alama au imewekwa alamaisiyoonesha dhahiri ni mgombea yupi ambayempiga kura amempigia; isipokuwa kwamba,ikiwa baadhi ya kura kwenye karatasi ya kurani dhahiri na nyingine si dhahiri, karatasi ya kurahiyo itakataliwa kuhusu tu zile kura zisizokuwadhahiri na kura zilizo dhahiri zitahesabiwa.

(3) Uamuzi wa Spika juu ya kuwa karatasi ya kura ikataliwe yote ausehemu tu utakuwa ni wa mwisho.

Kuhesabu kura

102

SEHEMU YA NANEKUTANGAZA MATOKEO YA KURA

10.-(1) Baada ya kura kuhesabiwa, Katibu atatangaza matokeo yakura zote zilizopigwa kisha atatamka majina ya wagombeawaliochaguliwa ambao wamepata idadi kubwa zaidi ya kura nakuwatangaza kwamba wamechaguliwa.

(2) Endapo baada ya kuhesabu kura kutakuwa na sababu ya kurudiaUchaguzi kutokana na kutokupatikana mshindi katika nafasi yoyoteinayohusika katika uchaguzi huo, Spika ataeleza sababu zakutokupatikana mshindi, kisha ataagiza kura ipigwe tena ili kupatamshindi kwa nafasi hiyo.

(3) Kura ya uamuzi haitatumika kwenye uchaguzi.

(4) Iwapo imeamuliwa ipigwe kura tena kwa mujibu wa fasili ya(2), basi wagombea wanaopigiwa kura watakuwa ni wale tu ambaowalipata kura sawa.

(5) Iwapo Spika hawezi kutangaza idadi inayotakiwa yawagombea waliochaguliwa kwa sababu ya kukosekana kura, basi:-

(a) atatangaza kadri ya wingi wa wagombeawaliochaguliwaambao wamepata kura kuwawamechaguliwa; na

(b) atawaarifu Wabunge wote kuhusu nafasiiliyobakia au zilizobakia na utaratibu wa uchaguziutaanza upya kwa ajili ya nafasi hiyo au nafasi hizo.

(6) Kila tamko na agizo linalotolewa na Spika kwa mujibu wa Kanunihii litatolewa Bungeni.

Kutangazamatokeoya kura

103

SEHEMU YA TISAUTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZA KURA

11.-(1) Katibu ataandika maneno “imekataliwa” na “kurailiyokataliwa” kwenye karatasi za kura zilizokataliwa na ataziwekakaratasi hizo pamoja na zile zilizokuwa safi kwa muda wa miezi sitabaada ya kutangazwa matokeo ya uchaguzi.

(2) Baada ya hapo, isipokuwa kama Bunge litaamuru vinginevyo,Katibu ataziharibu karatasi hizo.

(3) Karatasi za kura zilizokwishatumika hazitaonyeshwa kwa mtuyeyote na Katibu, isipokuwa kwa mujibu wa azimio la Bunge baadaya hoja ya kutaka zionyeshwe kupitishwa.

SEHEMU YA KUMIKUPINGA MATOKEO YA KURA

12. Iwapo mgombea yeyote hataridhika na matokeo ya Uchaguziau jinsi uchaguzi ulivyofanywa, atakuwa na haki ya kupeleka madaiyake mahakamani na madai hayo yatashughulikiwa kwa mujibuwa Sheria il iyowekwa na Bunge kwa ajil i ya kushughulikiamalalamiko ya uchaguzi wa Wabunge.

Utunzajiwakumbu-kumbuza kura

KupingaMatokeo ya kura

104

__________

NYONGEZA YA TATU

__________

THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLYELECTION RULES

______(Made under Standing Order 12 and Article 50

of the Treaty for the Establishment ofEast African Community)

_______

ARRANGEMENT OF RULES____________

PART I

PRELIMINARY RULES

1. These Rules may be cited as the East African Legislative AssemblyElection Rules.

2. In these rules, all the parliamentary words and expressions usedshall have the same meaning assigned to them in the ParliamentaryStanding Orders and, unless the context requires otherwise:-

“Candidate” means a person who is nominated to stand forelection to the East African Legislative Assembly as provided forin rule 5 of these rules; “Election” means an election to the East African LegislativeAssembly; “Nomination” means nomination as a candidate to stand forelection to the East African Legislative Assembly; “Returning Officer” means the Clerk of the National Assembly; “Treaty” means the Treaty for the Establishment of the EastAfrican Community, 1999; “Voter” means a Member of Parliament present and votingduring the election;

Citation

Interpre-tation

105

PART IIQUALIFICATION OF CANDIDATES

3. A person shall be qualified to be a candidate for election to theEast African Legislative Assembly who he is qualified to be electedin accordance with Article 50(2) of the Treaty.

PART IIINOMINATION OF CANDIDATES

4. -(1) Where an election is to be held, the Returning Officer shallby notice published in the Gazette, appoint a nomination day forthat election.

(2) The Returning Officer shall give at least fourteen days notice ofsuch nomination day.

5.-(1) In order to be validly nominated as a candidate for the EastAfrican Legislative Assembly elections, a person must benominated in a transparent and democratic manner by the politicalparty which is sponsoring him.

(2) The nomination shall be in the prescribed form, signed by thecandidate and by the Secretary General of the party nominatinghim, and shall contain the following particulars:-

(a) The name, educational qualifications, addressand occupation of the candidate;

(b) A certificate by the candidate that he is willingand otherwise qualified to stand for election.

(3) Every nomination paper shall be accompanied by the followingdocuments:-

(a) Proof of citizenship of the United Republic ofTanzania, provided by the ImmigrationDepartment;

(b) Detailed biographical information relating tothe candidate signed by the candidate himself,

Qualifi-cationofcandidates

Nomina-tionofCandida-tes

Validity ofnomina-tion

106

which shall enable the Returning Officer todetermine whether or not the candidate hasproven experience or interest in consolidatingand furthering the aims and objectives of theCommunity in terms of Article 50(2)(e) of theTreaty; and

(c) An extract of the nomination proceedings of theparty organ which approved the finalnomination of the candidate, signed by theChairman and Secretary of that Organ whichshall enable the Returning Officer to determinewhether or not the relevant political party’sproceedings were democratic and transparent interms of the Political Parties Act.

(4) The candidate or an official of the Party nominating him, shalldeliver the nomination papers to the Returning Officer at his officein Dodoma, not later than four o’clock in the afternoon of thenomination day.

(5) Any political party which is entitled to sponsor candidates maysubmit to the Returning Officer, the names of three candidates foreach vacant seat in the following relevant groups:-

Group A: Women Candidates;Group B: Zanzibar Candidates;Group C: Opposition Parties Candidates;Group D: Mainland Candidates.

6. A candidate, or an official of the party nominating him shall, atthe time of delivering the nomination paper, deposit a non-refundable deposit of fifty thousand shillings, to cover for the costof election expenses.

7. Objections may be made by the Returning Officer to thenomination of a candidate, if it is apparent to him from the contentsof the nomination papers that the candidate is not qualified tostand for election. In which case the Returning Officer shallforthwith reject the nomination papers of that candidate.

Cap.258

Non-refunda-bledeposit

Rejectionofnomina-tionpapers

107

PART IVELECTION AND VOTING PROCEDURE

8. The Returning Officer shall by notice published in the Gazette,appoint an election day which shall be not more than seven daysafter nomination day, provided that, such election day shall be aday when the National Assembly is sitting in ordinary session.

9.-(1) A candidate may withdraw his candidature by notice inwriting, signed and delivered by him to the Returning Officer and acopy to the Secretary General of the Party sponsoring him, notlater than four o’clock in the afternoon of the day followingnomination day, thereafter no withdraws shall be accepted.

(2) Where any candidate dies after four o’clock in the afternoonof nomination day and before election day, the election processwill continue undisturbed.

10.-(1) An aspiring candidate may introduce himself to the votersand seek their support even before nomination day and maycontinue to do so after nomination day.

(2) Before the votes are cast on election day, each candidate willbe permitted to appear before the voters, duly assembled in anordinary sitting of the House and address them in English for suchlength of time and answer such number of questions, if any, as maybe determined by the Speaker for that purpose.

11.-(1) The voting shall be conducted under the general supervisionof the Returning Officer.

(2) The Returning Officer shall issue only one ballot paper to eachvoter.(3) The ballot paper shall contain the names of all candidates,arranged alphabetically in the following groups:-

Group A: Women Candidates;Group B: Zanzibar Candidates;Group C: Opposition Parties Candidates;Group D: Mainland Candidates.

Withdra-walofcandida-ture

Campaign bycandidates

Election day

Supervi-sionof theVotingprocess

108

(4) A voter shall be required to cast a specified number of votes,to be announced by the Speaker in each of the groups.

(5) On receiving a ballot paper, each voter shall secretly recordhis votes by putting a mark against the names of the ninecandidates he wishes to vote for.

(6) Each voter shall be required to cast as many votes as there arevacancies, otherwise his whole ballot paper will be regarded asspoilt.

(7) A voter who has accidentally spoiled his ballot paper whilethe voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paperto the Returning Officer and obtain a replacement thereof.

12.-(1) When all the voters have casted their votes, the Speakershall appoint two counting agents, one from the ruling party andthe other from the opposition benches, to act as counting agentsfor all the candidates.

(2) Immediately after all the ballots have votes been collected,the Returning Officer, with the assistance of Clerk Assistants andbefore the two counting agents as witnesses, shall count the votesso casted.

(3) In order to enable the National Assembly to proceed with otherbusiness, the counting of votes shall take place outside theAssembly Chamber, in a room designated by the Clerk for thatpurpose within the precincts of the Assembly.

13. When the votes have already been counted and the results ofthe election has been ascertained, the Returning Officer shall:-

(a) Report to the Assembly the election results,together with the number of votes recorded foreach candidate in each group.

(b) Announce to the Assembly the names of ninepersons receiving the majority number ofvotes in each group and shall declare thosepersons to have been elected as members ofthe East African Legislative Assembly.

VotesCount-ing agents

Announce-ment of election results

109

14.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of allballot papers and other documents relating and pertaining to theconduct of the election.

(2) The Returning Officer shall cause all documents to which thisparagraph applies to be destroyed after the expiration of sixmonths from the election day, unless otherwise directed by anorder of the High Court arising from any proceedings of a petitionrelating to the election.

PART VANNULMENT AND AVOIDANCE OF ELECTION

15. Pursuant to the provisions of Article 52(1) of the Treaty, theelection of a candidate as a member of the East African LegislativeAssembly may be declared null and void only on an Election Petition.

16. The procedure, jurisdiction and grounds for declaring theelection of such member null and void shall be the same as thoseprovided by law forelection petitions in respect of Members of the Parliament of theUnited Republic of Tanzania.

PART VIMISCELLANEOUS

17. (1) If any matter or thing arises which is not specifically providedfor in these rules, the Speaker shall make a ruling directing what isto be done in respect of that matter or thing.

(2) In making such a ruling, the Speaker shall be guided by thepractices and procedures normally followed in similar situationswith regard to Parliamentary elections.

18. These rules may be amended at any time by a resolution of theNational Assembly on a proposal submitted to it by the StandingOrders Committee.

Custodyofballotpapers

Grounds forannulmentandavaoid-anceof election

Matters notprovidedfor

Amend-mentofrules

Annulmentand avoida-nce ofelection

110

__________NYONGEZA YA NNE

__________

THE SUBMISSION OF REGULAR REPORTS TO THEPARLIAMENT OF TANZANIA BY THE TANZANIA MEMBERS

OF THE EAST AFRICAN LEGISLATIVE ASSEMBLY___________

[Made under Article 65 of the Treaty for theEstablishment of the East African Community]

_________

1. These Regulations may be cited as the Submission of RegularReports to the Parliament of the United Republic of Tanzania bythe Members of the East African Legislative Assembly Regulations.

2.-(1) These Regulations are made to provide for a procedure forthe Members of the East African Legislative Assembly hailing fromTanzania to submit regular reports to the Parliament of the UnitedRepublic of Tanzania.

(2) These Regulations shall apply to members of East AfricanLegislative Assembly hailing from the United Republic of Tanzania.

3. The Members of the East African Legislative Assembly shallpresent an annual report of the activities of the East AfricanLegislative Assembly for the relevant year, to the Parliament ofthe United Republic of Tanzania through its Standing Committeeresponsible for Foreign Affairs, Defence and Security.

4. The annual reports shall be presented at a regular meeting ofthe Standing Committee at a time to be determined by theChairman of the Committee.

5. The Tanzania members of the East African Legislative Assemblymay, if they consider it desirable to do so, present any specialreport, or make any appropriate consultations with the Committee,on any matter which is relevant to the work of the East AfricanLegislative Assembly at any other scheduled meeting of theCommittee.

Application

Presentationofannualreport

Timeofpresentation

Presenta-tionofspecialreportandconsultations

Citation

111

6.-(1) All Tanzania Members of the East African Legislative Assemblyshall be present at the time of presentation of any report.

(2) All such reports shall subsequently be laid on the Table of theHouse and shall be debated.

Attenda-nceandlayingofreportson theTable

112

__________NYONGEZA YA TANO

__________THE PAN-AFRICAN PARLIAMENTARY ELECTION RULES

[Made under Standing Order 12 and Article 2 of the Protocolto the Treaty for Establishing of the African EconomicCommunity Relating to the Pan-African Parliament]

PART IPRELIMINARY RULES

1. These Rules may be cited as the Pan-African ParliamentaryElection Rules, and shall come into operation on the day of theiradoption by resolution of the National Assembly.

2. In these Rules, unless the context requires otherwise- “Candidate” means a Member of Parliament who is dulynominated to stand for election to the Pan-African Parliament asprovided for in rule 5 of these Rules; “Election” means the election to membership of the Pan-AfricanParliament; “Election day” means the day on which the election of Membersof the Pan-African Parliament is set to be conducted; “Nomination” means nomination as a Candidate to stand forelection to the Pan-African Parliament; “Nomination day” means the day which shall by notice publishedby the Returning Officer, be set to be the last day for receivingapplication forms from Candidates; “Nominator” means a Member of Parliament of the Parliamentof the United Republic of Tanzania entitled to vote, who nominatesand supports a Candidate who aspires to stand and contest forelection to the Pan-African Parliament; “Qualification” means the qualification which entitles a personto stand and contest for election to the Pan-African Parliament; “Returning Officer” means the Clerk of the National Assembly; “Speaker” means the Speaker of the National Assembly; “Voter” means a Member of Parliament of the United Republicof Tanzania present and voting during the election.

Citation

Interpreta-tion

113

PART IIQUALIFICATION OF CANDIDATES

3. No person shall be qualified to be a Candidate for election tothe Pan-African Parliament unless he or she is a Member ofParliament of the United Republic of Tanzania, and is fluent in anyof the languages approved for use in the proceedings of the Pan-African Parliament.

PART IIINOMINATION PROCEDURE

4.-(1) Where election of Members of the Pan-African Parliament isto be held, the Returning Officer shall, by written notice circulatedto all members of the Parliament of the United Republic of Tanzania,appoint a nomination day for that election, which must be a dayduring any period when the National Assembly is in ordinary session.

(2) The Returning Officer shall give at least seven days notice ofsuch nomination day.

5. The following shall be the procedure for the nomination ofcandidates that:-

(a) in the case of a General Election of all the fivemembers of the Pan-African Parliamentrepresenting Tanzania, the candidates will benominated in accordance with thefollowing groups:-

Group A: Women Candidates;Group B: Zanzibar Candidates;Group C: Mainland Candidates;Group D: Opposition Parties Candidates;

Provided that, whereas Group A shall be reserved forWomen Candidates only, the remaining Groups shall beopen to both men and women Candidates.

(b) the number of candidates to be elected ineach group shall be as follows:-

Quqlifica-tionofCandidates

Appoint-mentofnominationday

Nomina-tionprocedure

114

Group A: One Candidate;Group B: One Candidate;Group C: Two Candidates;Group D: One Candidate;

(c) in the case of a by-election to fill a casualvacancy, candidates will be nominated only inrespect of the group in which the vacancy hasoccurred;

(d) no candidate may be nominated for more thanone specified group.

6.-(1) In order to be validly nominated to stand as a candidate forelection to Pan-African Parliament, a person shall be nominatedand supported in writing by not less than ten nominators who areentitled to vote at that election. A nominator may nominate up tofour candidates, one for each of the four groups.

(2) The nomination shall be in the prescribed form obtainable fromthe Returning Officer, and shall contain working experience of thecandidate.

(3) The time for receipt by the Returning Officer of nomination formsduly completed by the aspiring Candidates shall expire at fouro’clock in the afternoon of the nomination day and soon thereafter,the Returning Officer shall give written notification to all Membersof Parliament, of the complete list of the all Candidates who havebeen validly nominated for the election in respect of each of thefour groups.

(4) After being validly nominated, a Candidate may withdraw hiscandidature by notice in writing signed and delivered by him tothe Returning Officer, not later than four o’clock in the afternoonof the day following the nomination day, thereafter, no withdrawalsshall be accepted.

(5) Where any Candidate dies at any time after nomination dayand before election day, the election process shall continueundisturbed.

(6) After being validly nominated, a Candidate may conduct his orher election campaign.

Nomina-tionofCandi-dates

115

PART IVELECTION PROCEDURE

7. The Returning Officer shall, by written notice circulated to allMembers of Parliament, appoint an election day, which must be aday on which the National Assembly is sitting in ordinary session,and shall be not more than five days after nomination day.

8. The voting process shall be conducted under the generalsupervision of the Speaker, provided that, if the Speaker himself orherself is a Candidate, he or she shall vacate the chair before thecommencement of the election proceedings.

9. Before the voting exercise takes place on election day, eachCandidate shall be given an opportunity to appear before thevoters assembled in an ordinary sitting of the National Assemblyand address them in English for such length of time and answersuch number of questions, if any, as may be determined by theSpeaker for that purpose.

10. Immediately after address of the candidates, voting shallcommence and proceed as follows:-

(a) Only one ballot paper shall be issued to eachvoter.

(b) The ballot paper shall contain all names of theCandidates arranged in alphabetical order foreach of the groups.

(c) Each voter shall be required to cast the exactnumber of votes equal to the number ofpersons to be elected in each group. Any ballotpaper which will show a greater or smallernumber of votes than the specified number willbe treated as spoilt and will not be counted.

11.-(1) On receiving a ballot paper each voter shall secretly recordhis or her five votes by placing a tick in the space provide againstthe nameof each Candidate, and thereafter shall place the ballotpaper in the ballot box.

(2) A voter who has accidentally spoiled his or her ballot paper

Electionday

Votingprocess

Candida-testoaddressvoters

Castingofvotes

Votingprocedure

116

while voting is still in progress may surrender the spoilt ballot paperto Returning Officer and obtain a replacement thereof.

12.-(1) Immediately after all the votes have been placed in theballot boxes and before the ballot boxes are removed from theAssembly Chamber for counting the votes, the Speaker shallappoint one counting agent for the Candidates in each of thegroups.

Provided that, any candidate who wishes to appoint hisor her own counting agent may do so by submitting the name ofthat agent to the Speaker immediately after the appointments bythe Speaker have been announced.

(2) The counting of Votes shall be done by such number of Officersof the Assembly as may be appointed by the Returning Officer, andshall be witnessed by the counting agents.

13.-(1) In order to enable the National Assembly to proceed withother business scheduled for that day, the counting of votes shalltake place in a room designated by the Speaker for that purposewithin the precincts of the Assembly.

14. After the counting of votes is complete and the resultsascertained and certified by the Returning Officer and the countingagents, the Returning Officer shall immediately submit the resultsto the Speaker who shall:-

(a) Report to the Assembly the results of theelection together with the number of votesrecorded for each candidate in each of theGroups.

(b) Announce to the Assembly the names of fiveCandidates receiving the highest number of votesin each Group, and shall declare those candidatesto have been elected as Members of the Pan-African Parliament.

Appoint-mentofCountingAgentsandcountingofvotes

Decla-rationofelec-tionresults

Placeforcount-ing ofvotes

117

15.-(1) The Returning Officer shall ensure the safe custody of allballot papers and other documents pertaining to the election.

(2) The Returning Officer shall cause all documents to which thisrule applies to be destroyed after the expiration of six months fromthe election day.

PART VMISCELLANEOUS

16. Where anything arises which is not specifically provided for inthese Rules, the Speaker shall make a ruling directing what is to bedone. In making such a ruling, the Speaker shall be guided by theprocedures and practices normally followed in similar situationswith regard to Parliamentary elections.

17.-(1) These Rules may be amended at any time by a resolution ofthe National Assembly on a proposal submitted to it by the StandingOrders Committee.

Custodyofballotpapers

Mattersnotprovidedfor

Amend-ment

118

_____________NYONGEZA YA SITA

_____________

MWONGOZO KUHUSU MASWALI KWA WAZIRI MKUU______________________________

[Chini ya Kanuni ya 38(1)]____________

1. (1) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kikishaanza Bungeni,hakitakatishwa wala kusitishwa, isipokuwa kutokana na sababumaalum ya dharura.

(2) Maswali yatakayoulizwa kwa Waziri Mkuu wakati wa Kipindicha Maswali kwa Waziri Mkuu yatakuwa ni yale yanayohusu Seraza Serikali au jambo lolote lenye manufaa na maslahi kwa jamiina Taifa lililo chini ya madaraka na mamlaka ya kazi ya WaziriMkuu.

(3) Maswali kwa Waziri Mkuu yatakuwa ni ya papo kwa papo;yaani yataulizwa bila kutolewa taarifa na yatajibiwa kwa mdomopapo kwa papo.

(4) Waziri Mkuu hatalazimika kujibu swali lolote linalohitajitakwimu au majibu yanayohitaji utafiti.

2. Bila ya kuathiri masharti ya fasili ya 3(1) ya Mwongozo huu,Wabunge wanaotaka kumuuliza Waziri Mkuu swali wakati waKipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, watawasilisha majina yaokwa Katibu, kabla ya saa 2.30 Asubuhi, siku hiyo ya Maswali kwaWaziri Mkuu.

3. (1) Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu kinapoanza Bungeni,Spika atamwita Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni nakumpa fursa ya kwanza ya kumuuliza Waziri Mkuu swali.

(2) Baada ya kuuliza na kujibiwa swali lake la kwanza, Kiongozi waKambi Rasmi ya Upinzani Bungeni anaweza kumuuliza Waziri Mkuuswali moja la ziada la kudai ufafanuzi.

MaelezoyaJumla

UtaratibuwakupatafursayakumuulizaWaziriMkuuSwali

UtaratibuwakuulizamaswalikwaWaziriMkuu

119

(3) Mbunge yeyote atakayepata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuuswali na kujibiwa, anaweza kumuuliza Waziri Mkuu swali linginemoja la ufafanuzi.

(4) Endapo orodha ya majina ya wauliza maswali kwa Waziri Mkuukwa siku hiyo itafikia mwisho lakini muda wa Kipindi cha Maswalikwa Waziri Mkuu bado haujamalizika, Spika anaweza kutoa fursakwa Mbunge yeyote ambaye hakupangwa katika orodha hiyokumuuliza Waziri Mkuu swali.

(5) Mbunge anayetaka kupewa fursa na Spika kwa mujibu wa fasiliya (4), atasimama mahala pake ili Spika amwone na kumwita.

(6) Mbunge yeyote aliyepata fursa ya kumuuliza Waziri Mkuu swaliwakati wa Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, atakuwana haki pia ya kuuliza swali lake lililowekwa kwenye Orodha yaShughuli za siku hiyo, wakati wa Kipindi cha Maswali ya Bungekitakapowadia.

4. Maswali na majibu katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuuyawe mafupi.

MaswalinamajibukwamaswalikwaWaziriMkuu

120

________NYONGEZA YA SABA

________MWONGOZO WA UTARATIBU KATIKA KAMATI ZA BUNGE

_________

[Chini ya Kanuni ya 114(9) na (10)]_________

1. Mwongozo wa upatikanaji wa habari kutoka kwenye Vikao vyaKamati, ikiwa ni mojawapo ya njia za kukuza demokrasia za uwazikwa shughuli za Kamati za Bunge na kudumisha mahusiano nawananchi kupitia Vyombo vya Habari utatambua aina yamajukumu ambayo yanatekelezwa na Kamati.

2. Majukumu yatakayofanywa kwa uwazi na ambayo yanawezakutolewa kwa Waandishi wa Habari bila kuleta athari kwenyemaamuzi ya Kamati ni yafuatayo:-

(a) mambo ya kawaida ya kuisimamia na kuishauriSerikali, kama vile kutathmini utekelezaji wamiradi mbalimbali ya maendeleo;

(b) mambo yatolewayo na wadau walioalikwa naKamati ulingana na utaratibu wa ‘Public Hearing’uliowekwa na Bunge;

(c) majukumu ambayo yanalenga kuwapatiaWabunge elimu, Semina, Makongomano naziara za mafunzo;

(d) maelezo yanayotolewa na Serikali kwenyeKamati za Bunge kwa lengo la kuwaelimishaWaheshimiwa Wajumbe wa Kamati kabla yakufanya kazi ya uchambuzi wa Hoja au jambololote na ambayo Waziri ataona hayatakuwana athari kwa upande wa Serikali, mfano mmojawapo ukiwa ni pale Waziri wa Mipango,Uchumi na Uwezeshaji anapotoa taarifa ya Haliya Uchumi wa nchi.

Maelezoyajumla

Majukumuyatakayo-fanywakwauwazi

121

3.-(1) Majukumu yatakayofanywa kwa faragha yatahusu mamboyote ambayo habari zake zikitolewa kwa Waandishi wa Habarikabla ya wakati wake yanaweza kuathiri maamuzi ya Kamati napia kusababisha ukiukwaji wa Kanuni za Bunge ni yafuatayo:-

(a) kazi zote zinazopelekwa kwenye Kamati naMheshimiwa Spika ili baadaye apelekewetaarifa ya mapendekezo ya hatua zakuchukuliwa na Bunge au kuyatolea maamuzi.

(b) shughuli zote za uchambuzi wa Hoja mbalimbalizilizoko mbele ya Kamati.

(c) Shughuli zote zinazofanywa kwa utaratibu wauchunguzi.

(d) shughuli zote za kiuchunguzi zenye utaratibuuliowekewa masharti zinazofanywa na Kamati.

(e) shughuli zote zinazofanywa na Kamati Ndogozilizoundwa na Mheshimiwa Spika au Kamatihusika ili kufanya kazi maalumu.

(f) Kamati zinapofanya ziara za kiuchunguzi.

(2) Kamati zitakazofanya kazi zake kwa faragha ni Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge, Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi naUsalama, Kamati ya Hesabu za Serikali, Kamati ya Hesabu ya Serikaliza Mitaa na Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

4.-(1) Majukumu yenye uwazi wenye mipaka ni yaleyanayotekelezwa na Kamati za kiuchunguzi zifuatazo zenyeutaratibu uliowekewa masharti :-

(a) Kamati ya Hesabu za Serikali;

(b) Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa;

(c) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge; na

(d) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.

Majukumuyatakayo-fanywakwafaragha

Majukumuyenye uwaziwenyemipaka

122

(2) Mfano wa uwazi wenye mpaka ni ufuatao:-(a) taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

za Serikali inapowasilishwa Bungeni inakuwa wazikwa Vyombo vya Habari; na

(b) mchakato wa Kamati hizi kuanza kuwahojiMaafisa Masuhuli kuhusiana na taarifa ya Mdhibitina Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali utakuwawazi hadi hatua ambayo Kamati inataka kufanyamaamuzi ya kutoa mapendekezo ya hatua zakuchukuliwa na Bunge. Katika hatua hiyo ya kutoamapendekezo Kamati itafanya kazi zake kwafaragha.

(3) Iwapo mchakato wa kuhoji Maafisa Masuhuli utakuwa ni wakiuchunguzi, mchakato utafanyika kwa faragha.

(4) Kamati zinapofanya ziara kwa lengo la kujifunza au kujielimisha,shughuli zake zitafanywa kwa uwazi na Wajumbe wa Kamatiwatakuwa na uhuru wa kutoa maoni yao ya jumla kwenye vyombovya habari. (5) Maoni ya Kamati yatakuwa ni yale ambayo hayaathiri maamuziyatakayotolewa kwa faragha na Kamati baada ya ziara yake.

(6) Waandishi wa Habari katika kutoa taarifa za namna hii waelezewazi kwamba, maoni hayo ni ya Mbunge binafsi na siyo ya Bungewala Kamati ya Bunge au Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

5.-(1) Kwa kuwa Mawaziri wanapokutana na Kamati kwenye Vikaovilivyopangwa wanakuwa Wajumbe, na kwa kuwa inapotokeawamekutana na Waandishi wa Habari mara baada ya Kikaokuzungumzia suala lolote lililojadiliwa kwenye Kamati; Mwenyekitiwa Kamati au Mwakilishi wake au Msemaji wa Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni watakuwa huru kulitolea maoni jambo hilo, ilimradi maelezo yao hayatahusu maamuzi yaliyotolewa na Kamatiambayo yanatakiwa kuwasilishwa Bungeni.

(2) Wenyeviti wa Kamati zote wataandaliwa utaratibu wa kawaidawa kukutana na Waandishi wa Habari kuzungumzia shughuliitakayofanywa au iliyofanywa na Kamati na maelezo hayoyanayotolewa kwenye Vyombo vya Habari, kwa namna yoyote,yasiwe ni mapendekezo ambayo Kamati imeazimia kuyawasilishaBungeni na ambayo yanaweza kuathiri maamuzi hayo.

Mawaziriwanapo-toataarifakwawaandishiwahabaribaadayakukutananakamati

123

(3) Kama kuna jambo ambalo lina maslahi kwa umma na wananchiwanataka maelezo, Mwenyekiti wa Kamati au Mwakilishi wakeatakuwa na uhuru wa kulitolea maelezo ya jumla ili mradi maelezohayo hayatahusiana na maamuzi ya Kamati ambayo yanatakiwakuwasilishwa Bungeni.

124

_______

NYONGEZA YA NANE________

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE

[Chini ya Kanuni ya 115]

SEHEMU YA KWANZAKAMATI ZA KUDUMU ZISIZO ZA SEKTA

1.- Kamati za Kudumu zisizo za Sekta zitakuwa zifuatazo:-

(a) Kamati ya Uongozi;(b) Kamati ya Kanuni za Bunge;(c) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge;(d) Kamati ya Sheria Ndogo; na (e) Kamati ya Masuala ya Ukimwi;

2.-(1) Kamati ya Uongozi itakuwa na Wajumbe wafuatao:-

(a) Spika, ambaye atakuwa Mwenyekiti;(b) Naibu Spika;(c) Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni au

Mwakilishi wake;(d) Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni

au Mwakilishi wake;(e) Wenyeviti wa Kamati za Kudumu au Makamu

wao;(f) Mwanasheria Mkuu wa Serikali;

(2) Katibu atakuwa Katibu wa Kamati.

(3) Majukumu ya Kamati ya Uongozi yatakuwa ni:-

(a) kujadili na kumshauri Spika kuhusu mamboyote yanayohusu Shughuli za Bunge kwajumla, ikiwa ni pamoja na kuweka utaratibuutakaorahisisha maendeleo ya Shughuli za Bungeau za Kamati yoyote.

KamatizaKudumuzisizo zaSekta

Muundonamajuku-muyaKamatiyaUongozi

125

(b) kupokea hoja zenye maslahi kwa Taifazinazojitokeza kwenye Kamati za Bunge za kisektawakati wa kupitia bajeti za Wizara na kuishauriSerikali kuhusu hatua muafaka za kuchukua kablaya Hotuba ya Bajeti kusomwa Bungeni.

(4) Katika kutekeleza kazi zilizotajwa katika fasili ya 3 ya Kanuni hii,Kamati ya Uongozi itakuwa na uwezo wa kuweka muda ambaoshughuli yoyote iliyopelekwa katika Kamati inayohusika shartiikamilike, na iwapo shughuli iliyopelekwa imewekewa muda kamahuo, basi baada ya kwisha muda huo au baada ya kwisha mudawowote ulioongezwa, Kamati inayohusika itahesabiwa kuwaimemaliza shughuli hiyo na shughuli hiyo itaendelea kwenye hatuanyingine kana kwamba Mwenyekiti wa Kamati hiyo amemuarifuSpika kumalizika kwa shughuli hiyo.

3.- (1) Kamati ya Kanuni za Bunge itakuwa na Wajumbe wafuatao:-

(a) Wajumbe watakaoteuliwa na Spika;

(b) Kiongozi wa Upinzani au Mwakilishi wake; na

(c) Mwanasheria Mkuu wa Serikali au Mwakilishi wake.

(2) Spika atakuwa Mwenyekiti na Naibu Spika atakuwa MakamuMwenyekiti.

(3) Majukumu ya Kamati ya Kanuni za Bunge yatakuwa ni:-

(a) kujadili na kutoa mapendekezo juu ya kufanyamabadiliko katika Kanuni za Bunge;

(b) kuchunguza na kutoa taarifa juu ya pendekezololote linalohusu Kanuni za Kudumu za Bungeambalo limepelekwa kwa Kamati hiyo na Spikaau na Mbunge yeyote;

(c) kuchunguza na kutoa taarifa juu yamalalamiko yote kuhusu uamuzi wa Spikaambayo yamepelekwa mbele ya Kamati naMbunge yeyote.

(d) kuzifanyia marekebisho au mabadiliko Nyongezaza Kanuni hizi.

MuundonamajukumuyaKamatiyaKanuniza Bunge

126

(4) Akidi ya mikutano ya Kamati ya Kanuni za Bunge itakuwa niMwenyekiti au Makamu Mwenyekiti pamoja na nusu ya Wajumbewengine.

4.-(1) Majukumu ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bungeyatakuwa:-

(a) kuchunguza masuala yote yahusuyo haki,kinga na madaraka ya Bunge yanayopelekwakwake na Spika;

(b) kushughulikia mambo yanayohusu maadili yaWabunge; na

(c) kujadili jambo lingine lolote litakalopelekwakwake na Spika.

5. Kamati ya Sheria ndogo itakuwa na majukumu ya kuchambuaSheria Ndogo ili kujiridhisha iwapo zimekidhi matakwa na mashartiya Katiba, Sheria Mama na Sheria nyingine za nchi.

6. Kamati ya Masuala ya UKIMWI itatekeleza majukumu yafuatayo:-

(a) kuratibu masuala yanayohusu UKIMWI katikataasisi ya Bunge;

(b) kufuatilia utekelezaji wa Sera na mipango yaSerikali kuhusu UKIMWI;

(c) kujadili na kutoa mapendekezo na ushauri juuya Sera na mipango ya Serikali kuhusu UKIMWI.

SEHEMU YA PILI

KAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZA SEKTA

7.-(1) Kamati za Kudumu za Bunge za sekta zitakuwa zifuatazo:-

(a) Kamati ya Fedha na Uchumi;(b) Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala;

Majukumu yaKamati yaSheriaNdogo

MajukumuyaKamatiyamasualayaU K I M W I

K a m a t izaKudumuzaSekta

MajukumuyaKamatiya Haki, MaadilinaMadarakayaBunge

127

(c) Kamati ya Viwanda na Biashara;(d) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama;(e) Kamati ya Huduma za Jamii;(f) Kamati ya Maendeleo ya Jamii;(g) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira;(h) Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji;(i) Kamati ya Miundombinu; na(j) Kamati ya Nishati na Madini.

8.-(1) Kamati ya Fedha na Uchumi itasimamia shughuli za Wizarazifuatazo:-

(a) Wizara ya Fedha na Uchumi.

(2) Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala itasimamia shughuli zaWizara zifuatazo:-

(a) Ofisi ya Rais:

(i) Utawala Bora;(ii) Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

(b) Ofisi ya Makamu wa Rais: Muungano.

(c) Ofisi ya Waziri Mkuu:

(i) Tawala za Mikoa na Serikali zaMitaa (TAMISEMI);

(ii) Sera na Uratibu.

(d) Wizara ya Katiba na Sheria.

(3) Kamati ya Viwanda na Biashara itasimamia shughuli za Wizaraya Viwanda, Biashara na Masoko.

(4) Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama itasimamia shughuliza Wizara zifuatazo:-

(a) Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa;

(b) Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki;

(c) Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa; na

KamatinashughulizaWizara

128

(d) Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

(5) Kamati ya Huduma za Jamii itasimamia shughuli za Wizarazifuatazo:-

(a) Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii;

(b) Wizara ya Mawasiliano, Sayansi naTeknolojia; na

(c) Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

(6) Kamati ya Maendeleo ya Jamii itasimamia shughuli za Wizarazifuatazo:-

(a) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto;

(b) Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo; na

(c) Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.

(7) Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira itasimamia shughuli zaWizara zifuatazo:-

(a) Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo yaMakazi;

(b) Wizara ya Maliasili na Utalii; na

(c) Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira).

(8) Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji itasimamia shughuli za Wizarazifuatazo:-

(a) Wizara ya Maji na Umwagiliaji;

(b) Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika; na

(c) Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi.

(9) Kamati ya Miundombinu itasimamia shughuli za Wizara yaMaendeleo ya Miundombinu.

(10) Kamati ya Nishati na Madini itasimamia shughuli za Wizara yaNishati na Madini.

129

9.-(1) Majukumu ya Kamati ya Kudumu ya sekta yatakuwayafuatayo:-

(a) kushughulikia bajeti ya Wizara inazozisimamia;

(b) kushughulikia Miswada ya Sheria na Mikatabainayopendekezwa kuridhiwa na Bunge iliyo chiniya Wizara inazozisimamia;

(c) kushughulikia Taarifa za kila mwaka za utendaji zaWizara hizo;

(d) kufuatilia utekelezaji unaofanywa na Wizara hizokwa mujibu wa Ibara ya 65(3) (b) ya Katiba.

(2) Bila ya kuathiri majukumu ya jumla ya Kamati za sekta kamayalivyoainishwa katika fasili ya (1) ya Kanuni hii, Kamati ya Mamboya Nje, Ulinzi na Usalama itatekeleza pia majukumu yafuatayo:-

(a) kuimarisha ushirikiano na Mabunge ya nchinyingine;

(b) kushughulikia taarifa za wawakilishi katika Bungela Afrika Mashariki, SADC na Bunge la Afrika.

SEHEMU YA TATUKAMATI ZA KUDUMU ZA BUNGE ZINAZOSIMAMIA

FEDHA ZA UMMA

10.-(1) Kamati za Kudumu za Bunge zinazosimamia fedha za Ummazitakuwa zifuatazo:-

(a) Kamati ya Hesabu za Serikali.

(b) Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa.

(c) Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma.

11.- Majukumu ya Kamati za Hesabu za Serikali yatakuwayafuatayo:-

(a) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu yamatumizi mabaya ya fedha za Umma katika

KamatizaKudumuzaBungezinazo-simamiaFedha zaUmma

Majukumu yaKamatiyaHesabuzaSerikali

Majukumuya Kamati

130

Wizara za Serikali yaliyoainishwa katika taarifaya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali;

(b) kufuatilia utekelezaji wa mapendekezoyaliyokwishatolewa na Kamati hiyo yenye lengo lakuondoa matatizo hayo sugu ya matumizi mabayaya fedha za Umma katika Wizara za Serikali; na

(c) kutoa mapendekezo na ushauri kwa Wizara zaSerikali kuhusu matumizi mazuri ya fedha za Umma.

12.- Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa yatakuwakama ifuatavyo:-

(a) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu yamatumizi mabaya ya fedha za Serikali za Mitaayaliyoainishwa katika Taarifa ya Mkaguzi naMdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali;

(b) kufuatilia utekelezaji wa mapendekezoyaliyokwishatolewa na Kamati hiyo ili kuondoamatatizo hayo;

(c) kutoa mapendekezo na ushauri kwa Serikali zaMitaa kuhusu matumizi mazuri ya fedha ilikuhakikisha kwamba tatizo la matumizi mabayaya fedha linapungua katika Serikali za Mitaa.

13. Majukumu ya Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma yatakuwakama ifuatavyo:-

(a) kushughulikia taarifa za kila mwaka za hesabuzilizokaguliwa za Mashirika ya Umma;

(b) kushughulikia maeneo yenye matatizo sugu yamatumizi mabaya ya fedha za Mashirika ya Ummayaliyoainishwa katika taarifa za kila mwaka zahesabu zilizokaguliwa za Mashirika hayo na kutoamapendekezo na ushauri wa namna ya kuyaondoamatatizo hayo.

Majukumu yaKamatiyaHesabuzaSerikalizaMitaa

MajukumuyaKamatiyaHesabuzaMashirikayaUmma

131

(c) kufuatilia utekelezaji wa mapendekezoyaliyokwishatolewa na Kamati hiyo ili kuondoamatatizo hayo.

(d) kutathmini ufanisi wa Mashirika ya Umma.

(e) kufuatilia utekelezaji wa Sera ya Ubinafsishajiwa Mashirika ya Umma.

Zimepitishwa kwa mujibu wa Azimio la Bunge tarehe 15 Novemba,2007.

Dodoma DAMIAN S. L. FOKA Katibu wa Bunge